Sunday, 24 January 2021

FULL POWER, ZATI 50 NI KIBOKO YA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA UUME MDOGO



Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume:


⇒Ngiri,

⇒Henia

⇒Kisukari

⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri

⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu

⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi

⇒Msongo wa mawazo 



⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.



FULL POWER



⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.



⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa

⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.

Zati 50


⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4


⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.



Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama



Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

Video Mpya Kali Balaa: BHUDAGALA, YOBAT & SHIJA KADOKE - KELELE


Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii  Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wimbo unaitwa Kelele.Video hii imetengenezwa Makula Studios..Ni ngoma yenye ujumbe safi unaozungumzia kiujumla maisha ya jamii inayotuzunguka. Tazama hapa chini
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 24,2021











Share:

Saturday, 23 January 2021

Nurse Midwifes at Medical Teams International Tanzania

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Nurse Midwifes (3)   Job Description Medical Teams International Tanzania Department Programs Reports to Direct: Medical Officer Technical: NA Location Nyarugusu and Mtendeli Work Days & Hours Monday-Sunday, 40- 45/week as per duty roster. May include weekends, night shifts and public holidays. MTI Calling Daring to love like Jesus, we boldly break barriers to health and […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Driver at Medical Teams International Tanzania

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Driver  Medical Teams International – Tanzania Department: Operations Reports to (position): Logistic Assistant Location(s): Kasulu Work Days & Hours: Monday-Sunday, 40-45 hours/week as per duty roster. May include weekends, night shifts and public holidays Medical Teams International Calling: Daring to love like Jesus, we boldly break barriers to health and restore wholeness in a hurting world. JOB SUMMARY  […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

53 Job Opportunities at Tanzania Red Cross Society ,Kigoma Region

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

The Tanzania Red Cross Society (TRCS) is a voluntary humanitarian organization established as an independent National Society (NS) by the Act of Parliament No. 71 of December 1962 and amended by the Parliament of Tanzania in 2019. Tanzania Red Cross Society was recognised and admitted to the membership of the International Federation of the Red […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Lecturers at University of Arusha

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Lecturer     UNIVERSITY OF ARUSIIA POSITIONS: One Lecturer in each of the following: Kiswahili and Geography. QUALIFICATIONS: For Assistant Lecturers, BA in the specified area (GPA 3.5/5 or equivalent), and MA in the same area (GPA 4/5 or equivalent); and For Lectures, BA in the specified area (GPA 3.5/5 or equivalent), MA in the same area […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Assistant Lecturers at University of Arusha

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Assistant Lecturers    University Of Arusha POSITIONS: One Assistant Lecturer in each of the following: Theology (Biblical Languages)/Kiswahili, and/ Geography. QUALIFICATIONS: For Assistant Lecturers, BA in the specified area (GPA 3.5/5 or equivalent), and MA in the same area (GPA 4/5 or equivalent); and For Lectures, BA in the specified area (GPA 3.5/5 or equivalent), MA […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Finance Manager at Celebi Aviation Holding

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Finance Manager   Celebi Aviation Holding Dar es Salaam, Tanzania   We are looking for a Finance Manager to take over all the responsibilities of Finance Activities in Celebi Tanzania. Group Profile   First privately founded Independent Ground Handling Company in the world established in 1958 in Turkey. Global provider of Airport Services Present in […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Principal Insurance Officer at TIB Rasilimali Ltd

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Principal Insurance Officer     TIB Rasilimali Ltd (formerly known as RASIUMAU LIMITED) is a wholly owned subsidiary of TIB Development Bank Limited. It is a Securities Brokerage and Advisory firm licensed by the Capital Markets and Securities Authority of Tanzania and a licensed member of the Dar es Salaam Stock exchange. TIB Rasilimali Ltd is […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Chief of Party at PATH

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Title: Chief of Party Location: Dar es Salaam, Tanzania Division: Global Health Programs PATH is a global organization that works to accelerate health equity by bringing together public institutions, businesses, social enterprises, and investors to solve the world’s most pressing health challenges. With expertise in science, health, economics, technology, advocacy, and dozens of other specialties, PATH develops and […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Senior Monitoring, Evaluation, and Learning Manager at PATH

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Title: Senior Monitoring, Evaluation, and Learning Manager Location: Arusha, Tanzania Division: Global Health Programs PATH is a global organization that works to accelerate health equity by bringing together public institutions, businesses, social enterprises, and investors to solve the world’s most pressing health challenges. With expertise in science, health, economics, technology, advocacy, and dozens of other specialties, PATH develops […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

BENKI YA ABSA YAKABIDHI VIFAA VYA USAFI KWA SHULE 54

Na Fred Alfred - Dodoma
BENKI ya ABSA imetoa vifaa vya usafi kwa shule 54 za halmashauli ya jiji la Dodoma vyenye thamani ya Sh. milioni 10 vitakavyotumiwa na wanafunzi kujiweka safi wanapokuwa shuleni.

Akizindua vifaa hivyo mwakilishi wa mkurugenzi wa jiji la Dodoma Elias Mazengo alisema vifaa  vilivyotolewa na benki hiyo  ni pamoja na ndoo 304 na sabuni ambazo zitaanza kugawiwa hivi karibuni kwa shule zote lengwa.

Alisema vifaa hivyo vitasaidia wanafunzi kunawia mikono baada na kabla ya kula chakula chochote itasaidia kupunguza magonjwa mlipuko.

“Tunashukuru wadau wetu Benki ya ABSA  kwa kutuletea msaada huu, utasaidia kupunguza magonjwa ya mlipuko kwa wanafunzi na kuwajengea utamaduni wa kunawa mikono mara kwa mara”,alisema.

Kwa upande wake Muwakilishi wa Benki ya ABSA Elizabeth Kiwale alisema lengo la kutoa msaada huo ni kuhakikisha wanafunzi wanalindwa afya zao wanapokuwa shuleni.

Alisema Benki ya ABSA  inashirikiana na serikali kuhakikisha wanaisaidia jamii katika masuala mbalimbali na hiyo ni kama shukrani kwasababu wateja wake wakubwa wanatoka katika jamii.

“Tunatambua mchango wa jamii kwenye benki yetu na leo tumeamua kutoa misaada hii ilivijana wetu wanapokuwa shule afya zao zikawe stimilifu, na vifaa hivi vitawasaidia kunawa mikono mara kwa mara ilikujiepusha na magonjwa ya mlipuko”,alisema.

Akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya wakuu wa shule Mkuu wa Shule ya Ipagala B Praxeda Fundisha alisema vifaa hivyo vitasaidia kupunguza magonjwa ya mlipuko kwa wanafunzi ambayo yanasababishwa na uchafu.

Alisema  kwa upandew wa wanafunzi hasa wa shule za msingi ni haki ya mzazi na mwalimu kumlinda afya yake kuhakikisha anakuwa katika mazingira bora sambamba na kuipongeza Benki ya ABSA kwa kutambua afya za watoto.

“Tunawashukuru sana absa kwa kutambua mchango wa afya za watoto kupitia misaada hii itasaidia kupunguza magonjwa ya mlipuko ambayo kipindi cha nyuma yalikuwa ni tishio hasa kwa watoto wa shule za misingi ambao kwa kiasi kikubwa inabidi tuwalinde”alieleza

Share:

NYAMA YA NG'OMBE WANAODAIWA KUCHINJWA WAKIWA WAMEKUFA YAZUA JAMBO SHINYANGA MJINI

 

Nyama ikiwa imening'inizwa kwenye machinjio ya Manispaa ya Shinyanga kata ya Kambarage

Na Shinyanga Press Club Blog
Mkaguzi Mkuu wa nyama wa Manispaa ya Shinyanga, Verani Mwaluko amemsimamisha kazi mchinja Ng'ombe mkuu wa machinjio ya manispaa ya Shinyanga, Rashid Masanja kwa tuhuma ya kuruhusu kuingizwa ndani ya eneo la machinjio nyama ya ng'ombe wawili wanaodhaniwa wamekufa (Kibudu).

Amesema mchinja ng'ombe huyo alihalalisha nyama hiyo ikauzwe kwenye mabucha ya nyama mitaani hali ambayo inadaiwa kuwa ingeweza kuleta madhara ya magonjwa kwa wananchi wa manispaa hiyo.

"Nilipata taarifa kwamba kuna ng'ombe wameingizwa machinjio wakiwa wameshakufa, nikafuatilia kwa wakaguzi na madaktari wa eneo hili wakakanusha kuhusika na jambo hilo, ndipo nikafuatilia kwa Bakwata (Rashid) ambaye alienda huko porini. Kisheria mnyama aliyekufa bila kuchinjwa kwa sababu za aina yoyote lazima ataketezwe kwa sababu kuna magonjwa mnyama akishachinjwa hayawezi kuonekana.

"Hatua zitakazochukuliwa sasa ni kumsimamisha mchinjaji wa Bakwata na kumkabidhi kwao kwa ajili ya taratibu za kimaadili, pia hii nyama lazima iteketezwe na hatua za kisheria zitafuata ikiwemo kwenda polisi na mahakamani," amesema Mwalukwa.

Mmoja wa madaktari katika machinjio hiyo ya Ernest Nigo akizungumzia suala hilo, amesema alipigiwa simu na Rashid (mchinjaji) kujulishwa kuwa kuna ng'ombe wameshawachinja na akawaelekeza wawatafute madaktari.

"Nikawaambia cha kufanya wakiwa wanakuja wamtafute mhusika, sasa hadi usiku napigiwa simu ng'ombe wakawa wameshafika bila mimi kujulishwa wakati niliwaambia wamtafute mhusika na wakimkosa wanijulishe tujue tunafanya nini, sasa nakuta nyama iko hapa tayari," amesema.

Kwa upande wake Rashid Masanja ambaye ni mchinjaji wa Bakwata Mkoa wa Shinyanga ameeleza "ninapopigiwa simu nakuwa najua kwamba mawasiliano yote ya wahusika na taratibu zote zinakuwa zimekamilishwa.
Mazoea tuliyonayo ni kwamba mfanyabiashara anapopata ng'ombe wa bei rahisi humtafuta daktari na mchinjaji, kwahiyo mimi niliambiwa kuchinja na mwenye ng'ombe siwezi kuwa na utaalam wa kujua kama kitaalam wana shida ama la,".

Kwa upande Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa nyama, Abdi Kidodo ameeleza kuwa ng'ombe siyo kwamba walikuwa wamekufa bali wamechinjwa nje ya tukio (machinjio) na kuletwa machinjioni bila kufuata utaratibu wa kuchinjwa kwenye machinjio, ambapo amewataka wafanyabiashara kufuata taratibu na watakaokiuka watasimamishwa. 

"Kwahiyo, itabidi tuanze kuwaelimisha wachinjaji na wenye mabucha kufuata sheria na utaratibu...kwahiyo wito kwa wafanyabiashara wafuate sheria ng'ombe wote ziletwe kwenye machinjio zichinjwe pale na watakaokiuka ni kuwasimamisha kufanya biashara," amefafanua.

Mkaguzi Mkuu wa nyama wa Manispaa ya Shinyanga, Verani Mwaluko
Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Nyama, Abdi Kidodo
Rashid Masanja ambaye ni mchinjaji wa Bakwata Mkoa wa Shinyanga
Share:

Video Mpya : MAMA USHAURI - GUKUMYA

Msanii Mama Ushauri kutoka Tinde mkoani Shinyanga ameachia wimbo mpya unaitwa Gukumya.... Tazama Video hapa chini
Share:

DC MBONEKO ATINGA HOSPITALI YA MKOA WA SHINYANGA SAKATA LA MLINZI KUPIGA MTU..AITAKA KAMPUNI YA ULINZI SUMA JKT KUCHUKUA HATUA

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akiondoka katika Wodi ya Wanawake katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga baada ya kumaliza kuendesha kikao cha kujadili tukio la Mlinzi wa Kampuni ya Suma JKT Guard, Geofrey Paul anayetuhumiwa kumpiga Daudi Lefi aliyekuwa akifuatilia dawa za mama yake aliyelazwa hospitalini hapo.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza katika kikao kuhusu tukio la mlinzi kupiga mwananchi aliyekuwa anahudumia mgonjwa wake katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mlinzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Gofrey Paul akimshambulia Daudi Lefi kama inavyoonekana kwenye video ya tukio hilo iliyosambaa mtandaoni 

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko ameiagiza Kampuni ya Ulinzi ya Suma JKT Guard kumuondoa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Mlinzi wake Geofrey Paul anayetuhumiwa kumpiga Daudi Lefi aliyekuwa akifuatilia dawa za mama yake aliyelazwa hospitalini hapo. 

Mbali na kuagiza kuchukulia hatua za kinidhamu kwa mlinzi huyo, Mboneko pia ameitaka Kampuni hiyo kuwaondoa hospitalini hapo walinzi wanaolalamikiwa 

Mboneko amechukua uamuzi huo leo Jumamosi Januari 23,2021 wakati akiongoza kikao cha kujadili kuhusu tukio hilo lililotokea katika hospitali hiyo Januari 22,2021 kilichodumu takribani saa tatu kilichohudhuriwa na wajumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya ya Shinyanga, Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga pamoja na Viongozi wa Kampuni ya Ulinzi ya Suma JKT Guard. 

Mboneko amesema viongozi wa serikali waliona taarifa ya tukio kupitia mitandao ya kijamii na kuanza kuchukua hatua mara moja ili kubaini ukweli kuhusu tukio hilo ambapo amevipongeza na kuvishukuru vyombo vya habari vilivyoripoti kuhusu tukio hilo. 

“Tumeona tukio hili kupitia mitandao ya kijamii, kama uongozi wa serikali hatukufurahishwa na jambo hili,baada ya kuona tukio hili tulianza kupata ufafanuzi kutoka hospitalini lakini pia nilimuagiza Mkuu wa Polisi wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kufuatilia tukio hili ambapo tayari hospitali walikuwa wameshaanza kuchukua hatua. Kwa hiyo ikapendeza kuwa leo Jumamosi tufanye kikao kujadili tukio hili, pia tuwaita wahusika kwa maana ya Yule kijana aliyepigwa bwana Daudi Lefi na Mlinzi Geodfrey Paul aliyekuwa akimpiga,tumepata ufafanuzi kutoka pande zote mbili,uongozi wa hospitali na kiongozi wa Suma JKT Guard kanda ya Ziwa kwamba ni hatua gani wamechukua”,ameeleza Mboneko. 

"Kwa sababu tuko na mkataba na Suma JKT Guard na tukio hili limetokea kwa mara ya kwanza kutokea,tumewapa nafasi ya kutafuta walinzi wazuri na tumewaambia kwamba hatutaki kusikia tukio jingine likihusisha walinzi kuharibu taswira ya hospitali yetu. Kwa hiyo kuanzia sasa nimewaambia warekebishe", amesema. 

Amesema serikali inakemea jambo hilo na isingependa kuona linaendelea mahali popote penye hospitali zetu, zahanati na vituo vya afya na sehemu zingine na kwamba serikali inataka watu wapate huduma nzuri hospitalini. 

“Jambo hili limetokea baada ya watu hawa kupishana lugha lakini nimewaelekeza SUMA JKT Guard na Idara ya afya wahakikishe wanatoa elimu kwa watoa huduma hospitalini na walinzi wanaolinda hospitali kuhusu namna ya kuhudumia watu,namna ya kuzungumza na watu kama huyu changamoto yake ilikuwa ni kumhudumia mama yake zaidi alitakiwa kuelimishwa kuliko kupigwa”,amesema Mboneko. 

Amesema wamelikemea jambo hilo na kumwelekeza kiongozi wa SUMA JKT Guard Kanda kuchukua za kinidhamu mara moja juu ya mtumishi wao na watuletee maandishi ofisini kwangu kuhusu hatua za kinidhamu walizochukua. 

“Lakini SUMA JKT Guard wamesema wameshachukua hatua ya kumuondoa hospitalini mtumishi wao, na sisi tunasema sawa sawa. Lakini nataka na wale wote walinzi wote wanaolalamikiwa kuwa na kauli mbaya kwenye Geti letu,kwenye mapokezi pale lakini pia kwenye kuondoa watu wanaokuja kuona wagonjwa. Nimewaelekeza wawaelimishe kuliko kufukuza watu utadhani wamekuja kuiba. 

“Waliopo hapa hospitalini wanahitaji faraja zaidi, wanahitaji upendo,wamekuja kuhudumia ndugu zao lakini pia wanatoka maeneo tofauti tofauti,pengine hawana ndugu hapa Shinyanga kwa hiyo muda anaopata yeye anakuja kuhudumia mgonjwa,akija pale mtu akajieleza,asikilizwe,apewe fursa ili apate kuhudumia mgonjwa wake kwani wengine wanakuja mbio mbio baada ya hali ya wagonjwa wao kubadilika”,ameongeza Mboneko. 

Mkuu huyo wa wilaya pia amesisitiza watoa huduma na Walinzi wa hospitali kudhibiti kauli mbaya na kuepuka vijembe wa wagonjwa na watu wanaohudumia au kuona wagonjwa huku akiwataka viongozi wa hospitali kuhakikisha wanachukua hatua dhidi ya malalamiko yanayotolewa. 

“Lakini pia nimewaelekeza kutoa namba za viongozi wa hospitali na nimeelekeza pia namba zangu ziwekwe ili wananchi waweze kutoa maoni na malalamiko yao,zionekane sehemu za kuingilia, kutoka na hata kwenye wodi wanazolala wagonjwa”,amesema. 

Amewataka walinzi kutumia muda mwingi kusaidia wananchi kuwaelimisha badala ya kuwapiga na kuwatolea lugha chafu ili watoa huduma nao wapate muda mzuri wa kuhudumia wateja wao na wanaotembelea wagonjwa wapate muda wa kufariji wagonjwa. 

Amesema lengo la serikali ni kuona kila mwananchi anafurahishwa na huduma zinazotolewa kwenye vituo vya afya kwani serikali inataka kuona wananchi wanapata huduma nzuri,bora na wanakuja salama na kuondoka salama wasipate taharuki yoyote. 

“Hatutaki taharuki hospitali, hatutaki misongamano hospitali. Tunataka watu waje kuhudumiwa na sisi tutaendelea kusimamia maboresho ya hospitali yetu. 

"Tulikuwa tumepokea pia malalamiko ya watu wanakaa muda mrefu bila kuhudumiwa kutokana na foleni kwenye eneo la Control number,Mapokezi kote huko nataka waboreshe,waweke walau watu wawili wawili ili kurahisisha huduma, mtu akija atumie muda mfupi aondoke akafanye shughuli zingine za kiuchumi na kijamii”,amesema Mboneko. 

Aidha amesema hataki kuona wala kusikia watumishi wa hospitali,zahanati na vituo vya afya wanafanya kazi huku wakichati nyakati za kazi badala yake watumie muda wao kuhudumia wagonjwa na kwamba hataki kusikia mgonjwa anatoka hospitali bila kupata dawa akiambia akanunue kwenye maduka ya dawa. 

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Nuru Mpuya amesema tukio hilo lilizua taharuki hospitalini na kwamba tayari hatua zimeshachukulia na kuahidi kuwa tukio kama hilo lililofanywa na mlinzi wa Kampuni ya walinzi waliyoingia nayo mkataba halitatokea na kwamba wataboresha huduma ikiwa ni pamoja na kuwapa elimu walinzi hao. 

Naye Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Shinyanga, Dkt. Luzila John Boshi amesema uongozi wa hospitali umesikitishwa na tukio hilo na kwamba kinachofuata ni kutekeleza maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga, Jasinta Mboneko. 

Meneja wa Kampuni ya Ulinzi ya Suma JKT Guard Kanda ya Ziwa, Captain Manika Kihiri amesema mara baada ya kutokea kwa tukio hilo,hatua za awali walizochukua ni kumuondoa mlinzi huyo eneo la hospitali na kwamba watatekeleza maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga na ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua za kinidhamu kwani Suma JKT haipo kwa ajili ya kuzua taharuki katika jamii bali ni kuleta amani katika jamii. 

Tukio hilo limetokea Ijumaa Januari 22,2020 majira ya saa 11 na dakika 45 jioni wakati Daudi Lefi (45) akiwa katika wodi ya wanawake namba 1 ambako mama yake mzazi Victoria Lugano Mwakagari amelazwa hospitalini hapo alishambuliwa kwa kupigwa mkanda sehemu mbalimbali za mwili wake na mlinzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga kutoka Kampuni ya Ulinzi ya Suma JKT Guard Geofrey Paul akimtaka aondoke wodini kwamba muda wa kusalimia wagonjwa umeisha. 

Akisimulia kuhusu tukio hilo, ndugu wa kijana huyo Lydia Lefi aliiambia Malunde 1 blog kuwa kaka yake alikutwa na mkasa huo wakati akiwa katika harakati za kulipia dawa za mama yao ambaye amelazwa katika hospitali hiyo Januari 21,2021 lakini jina lilikuwa halionekani kwenye Computer. 

“Kaka alikuwa alipie dawa, alipewa karatasi ya kwenda kulipia dawa, alipoenda kufuata Control number ili alipie, jina likawa halionekani kwenye Computer, ikabidi aende wodini kwa mgonjwa kuangalia/kuulizia amesajiliwa kwa jina gani,akiwa wodini hao walinzi ndipo walipoingia wodini na kumtaka aondoke kwamba muda umekwisha. 

"Walivyomtaka aondoke wodini akawaambia amekuja kuangalia jina gani mgonjwa ameandikishwa, wale walinzi wakamwambia aondoke muda huo huo, akawaomba lakini wakamwambia Huwezi kutupangia kazi. Kaka akasema nitaondokaje mama hajapata huduma ,wale walinzi wakaanza kumsukuma, ndipo mlinzi mmoja akachomoa mkanda wa suruali na kuanza kumshambulia huku mwingine akimsukuma, wakati purukushani zikiendelea baadae akaja mlinzi wa kike akasogea na kuwaachanisha”,ameeleza Lydia. 

Naye Daudi Lefi alisema mlinzi huyo alidhani amefika muda huo huo hospitalini wakati yeye alikuwa amefika hospitalini hapo muda mrefu lakini Computer za Hospitali zikawa hazisomi jina la mgonjwa wake wakati anataka kununua dawa. 

"Sikurusha ngumi kupigana kwa sababu ni eneo la hospitali, wangesema nimeenda kufanya vurugu. Walionishambulia walikuwa wawili lakini mmoja ndiyo aliyeanza kwa kunichapa na mkanda akisema nitamtambua kuwa yeye ni nani huku akinitukana,nami nikamsihi aache kutumia lugha chafu eneo la kazi",alisema Daudi. 

"Hayo yote yametokea wakati nikimweleza kuwa nimefika wodini kuulizia ndugu zangu na mgonjwa kuwa wameandikisha jina gani mapokezi kwani jina halionekani mapokezi ili nilipie dawa,wakati naendelea kushambuliwa nikamuona mama yangu mgonjwa akitoka wodini huku akihema presha imepanda akifuatilia nini kinaendelea ndipo nikaanza tena kumrudisha wodini kumhudumia nikaulizia jina aliloandikisha nikaenda kuchukua dawa nikamletea wodini", alieleza Daudi. 

Daudi alisema kutokana na kipigo hicho ameumia mkono wa kushoto ambao umevimba na kuchanika kwenye kiwiko.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza katika kikao kuhusu tukio la mlinzi kupiga mwananchi aliyekuwa anahudumia mgonjwa wake katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza katika kikao kuhusu tukio la mlinzi kupiga mwananchi aliyekuwa anahudumia mgonjwa wake katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Wajumbe wakiwa kwenye kikao hicho.
Meneja wa Kampuni ya Ulinzi ya Suma JKT Guard Kanda ya Ziwa, Captain Manika Kihiri akizungumza katika kikao hicho na kueleza hatua za kinidhamu zilizochukuliwa na kampuni hiyo juu ya mlinzi aliyepiga mwananchi katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akiingia katika wodi ya wanawake katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya kumjulia hali mama ambaye mwanaye alipigwa na mlinzi hospitalini hapo.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akiwa ndani ya wodi ya wanawake katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Daudi Lefi akiwaelezea waandishi wa habari namna alivyoshambuliwa na Mlinzi wa hospitali
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akiondoka katika wodi ya wanawake katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akiondoka katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

TAZAMA VIDEO HAPA CHINI
Share:

Video Mpya : MAMA USHAURI - ABEL REMIX

 Msanii wa Nyimbo za Asili Mama Ushauri kutoka Tinde Shinyanga anakualika kutazama Video yake Mpya ya Wimbo wa Abel Remix..Tazama hapa chini
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger