Friday, 22 January 2021

Picha : RPC MAGILIGIMBA AZINDUA MRADI WA KUTOKOMEZA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO....SPC, RAFIKI SDO, YWL, TAI NA HALMASHAURI YA SHINYANGA WAUNGANA.


Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba akionesha Mpango Mkakati wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto Mkoa wa Shinyanga wakati akizindua rasmi Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog 
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba amezindua rasmi Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT). 

Uzinduzi huo umefanyika leo Januari 22,2021 katika kata ya Iselamagazi halmashauri ya wilaya ya Shinyanga na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa mkoa, halmashauri, maafisa maendeleo ya jamii,maafisa watendaji wa kata, waandishi wa habari na wawakilishi wa mashirika yanayotetea haki za wanawake na watoto. 

Kamanda Magiligimba amesema suala la ulinzi wa mtoto ni la kila mtu katika jamii na kusisitiza kuwa ni wajibu wa kila kiongozi kuanzia ngazi ya mkoa,halmashauri,kata na kijiji kuhakikisha wanakuwa na mipango mikakati ya kuzuia unyanyasaji wa mwanamke na mtoto katika himaya zao. 

Aidha amempongeza Mkuu wa mkoa wa Shinyanga kwa kuweka Mpango Mkakati wa Mkoa katika kukomesha vitendo vya ukatili wa kijinsia ifikapo mwaka 2025 ambao umekuwa chachu ya mabadiliko katika mkoa wa Shinyanga. 

“Nimtake Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kutengeneza Sheria ndogo ambazo zitasaidia kila Mtendaji wa Kata au Kijiji kuhakikisha kwenye himaya yake hakuna mimba kwa wanafunzi wala ndoa za utotoni na kama zitatokea basi tujitahidi kumpata mtuhumiwa ili kupata hukumu ambayo itakuwa fundisho kwa jamii ili iachane na vitendo vya ukatili”,amesema Kamanda Magiligimba. 

Amelishukuru Shirika la Women Fund Tanzania kwa kufadhili mradi wa Ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ambao utadumu kwa muda wa miezi mitatu kuanzia Januari 2021 hadi Machi 2021. 

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Hoja Mahiba amesema mradi huo utakuwa chachu ya mabadiliko katika jamii ili kuondokana na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto. 

Hata hivyo amesema halmashauri hiyo inaendelea na utaratibu wa kuwa na Sheria ndogo katika kila kijiji ili kuchukua hatua dhidi ya matukio ya ukatili wa kijinsia katika jamii. 

Kwa upande wake, Afisa Mradi wa Shirika la Women Fund Tanzania mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia amewasihi wadau waliopata ruzuku kutekeleza mradi huo ikiwemo halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Rafiki Social Development Organization, Thubutu Africa Initiatives (TAI), Young Women Leadership ( YWL) na Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club –SPC) kuzingatia taratibu za utekelezaji miradi pamoja miongozo ya serikali. 

Amesema WFT inaendelea kupokea mawazo mazuri kutoka kwa wadau yatakayoleta matokeo chanya kwani shirika hilo lipo kwa ajili ya kuhudumia jamii na kuhakikisha wananchi wanaishi kwa amani na kufurahia nchi yao. 

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga, Alphonce Kasanyi amewataka watekelezaji wa mradi huo kutoa taarifa za fedha za mradi kwa wakati bila kuchelewa hata kidogo na kuepuka kutoa takwimu za uongo huku akiwasisitiza kufanya kazi kwa ushirikiano. 

Kwa upande wao, watekelezaji wa Mradi huo,wamesema wamejipanga kikamilifu katika kuhakikisha wanatekeleza mradi wa kutokomeza ukatili wa dhidi ya wanawake na watoto katika kata 13 ambazo ni Solwa, Lyabukande, Lyamidati, Nyamalogo, Mwalukwa, Pandagichiza, Ilola, Puni, Nyida, Usule, Mwamala, Itwangi na Masengwa. 

Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Shinyanga Lydia Kwesigabo aliwakumbusha watekelezaji wa mradi huo wasisahau kuyafikia makundi maalumu wakiwemo watu wenye ulemavu kwani wapo wanaofanyiwa matukio ya ukatili lakini hawapati nafasi ya kusemewa. 

Nao wadau walioshiriki uzinduzi huo wameshauri ushirikishwaji wa wazee maarufu, wa kimila wanaume wanaopendelea kwenye vijiwe vya kahawa, viongozi wa sungusungu,watoto,wasanii wa nyimbo za asili ‘marenga’ ili jamii ione kuwa huo ni mkakati halisi wa kuhamasisha kuachana na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto. 

Naye Mkaguzi Msaidizi wa Polisi kutoka ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga Analyse Kaika ameshauri jamii kutoa ushahidi kwenye kesi zinazohusu matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto huku Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto wilaya ya Shinyanga Victoria Maro akiwaomba wadau kulifikia pia kundi la wanawake wanaofanya biashara ya ngono na kuangalia vyanzo vya mimba kwa wanafunzi.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba akizungumza leo Januari 22,2021 wakati akizindua rasmi Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT). Kulia ni Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Hoja Mahiba, Kushoto ni Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga, Alphonce Kasanyi. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba akizungumza leo Januari 22,2021 wakati akizindua rasmi Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT). Wa kwanza kulia ni  Afisa Mradi Shirika la Women Fund Tanzania mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia akifuatiwa na Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Hoja Mahiba.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba akizungumza leo Januari 22,2021 wakati akizindua rasmi Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga 
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba akizungumza leo Januari 22,2021 wakati akizindua rasmi Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga 
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga, Alphonce Kasanyi akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na halmashauri hiyo pamoja na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT).
Afisa Mradi wa Shirika la Women Fund Tanzania mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na halmashauri hiyo pamoja na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT).
Afisa Mradi wa Shirika la Women Fund Tanzania mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na halmashauri hiyo pamoja na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT).
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Hoja Mahiba akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na halmashauri hiyo pamoja na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT).
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Hoja Mahiba akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na halmashauri hiyo pamoja na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT).
Mratibu wa MTAKUWWA halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Aisha Omary akielezea kuhusu utekelezaji wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na halmashauri hiyo pamoja na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT).
Mratibu wa MTAKUWWA Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga , Aisha Omary akiwasilisha Mpango Kazi wa Halmashauri hiyo kuhusu namna watakavyotekeleza mradi wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini wakifuatilia uwasilishwaji wa mipango kazi ya utekelezaji wa mradi wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Afisa Miradi wa shirika la Young Women Leadership (YWL), Veronica Massawe akiwasilisha mpango kazi namna watakavyotekeleza Mradi wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga
Mratibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club -SPC), Estomine Henry akiwasilisha mpango kazi wa utekelezaji wa mradi wa Nafasi ya Vyombo vya Habari katika kumaliza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Mratibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club -SPC), Estomine Henry akiwasilisha mpango kazi wa utekelezaji wa mradi wa Nafasi ya Vyombo vya Habari katika kumaliza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

Mratibu wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto kutoka Shirika la Rafiki SDO, George Nyanda akiwasilisha mpango wa utekelezaji wa mradi wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto walioupa jina la "Tuwalee".
Meneja Miradi kutoka Shirika la Thubutu Africa Initiatives ,Paschalia Mbugani akiwasilisha mpango kazi wao katika kutekeleza mradi wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto  wilaya ya Shinyanga, Victoria Maro akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa mradi wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya wanawake na watoto
Afisa Mradi wa Shirika la Women Fund Tanzania mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga 
Mwanasheria wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Salehe Hassan akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Mkaguzi Msaidizi wa Polisi kutoka ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga Analyse Kaika akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga 
Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wilaya ya Shinyanga Faustine Sengerema akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga
Mtoto Stephen Kiyenze akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Mtoto Irene Laurent akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini.
Meneja Miradi wa Shirika la ICS ,Sabrina Majikata akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Kuruthum Mlolwa kutoka shirika la PWWCO akichangia hoja ukumbini.
Mdau akichangia hoja ukumbini.
Mdau kutoka Shirika la TIDO akichangia hoja ukumbini
Afisa Ustawi wa Jamii halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Agnes Ginethon akichangia hoja ukumbini.
Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Deus Muhoja akizungumza ukumbini.
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba akipiga picha ya pamoja na wadau wa haki za wanawake na watoto baada ya kuzindua Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT).

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

Tutegemee Makubwa Kutoka Kampuni Ya Simu ya Infinix.


Kampuni ya simu Infinix Mobile LTD inasema tukae mkao wa kula. Je ni nini tutegemee kutoka Infinix?


Na kama ni simu mpya je nisimu kutoka series gani na kama ni valentine campaign basi watujuze tuanze kujichanga mapema ...nimewazatu.


Nikiwa bado najiuliza ni nini hasa Infinix kutuletea mapema mwaka huu? lakini pia tufahamu Infinix imekuwa kampuni imara na iliweza kuthibitisha hilo mwaka jana ambapo COVID-19 iliweza kusimamisha biashara nyingi lakini kwa Infinix bado walisimama imara nakuendelea kutupa simu zilizo bora kama vile Infinix NOTE 8 inayoendelea kutamba sokoni kutokana na ubora wake wa MP16 za camera ya mbele na MP64 za camera ya nyuma.


Uimara wa kampuni hii kunazidi kunipasha shauku ya kutaka kujua ni nini kipo njiani,lakini kwa taarifa zilizopo chini ya pazia ni kwamba Infinix itakuja na moja ya simu kabambe na huenda ikawa tishio kwa simu zote zenye kupatikana sokoni kwa bei isiyozidi sh. 350,000 huku baadhi ya sifa zikitajwa kupitia tovuti mbalimbali kwa kuusifu zaidi uwezo wa battery yenye mAh6000 kudumu na chaji kwa muda mrefu pamoja na ubora wa resolution yenye kukifanya kioo cha HOT 10 play kioo6.82 HD kuwa ang’avu wakati wote. 


Tembelea https://www.infinixmobility.com/tz/ ili kufahamu mengi zaidi.




Share:

AMUUA MDOGO WAKE KISA KUKU KUINGIA KWENYE SHAMBA LAKE

Na Amiri Kilagalila, Njombe
RAINARY Lugome mkazi wa wilaya ya Ludewa mkoani Njombe ameuawa na ndugu yake aliyefahamika kwa jina la Claus Samweli Lugome (46) kwa tuhuma za kuku wake kuingia katika shamba la kaka yake.

Akizungumza na vyombo vya habari kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Hamis Issa amesema wanawashikilia wanafamilia wawili akiwemo baba wa watoto hao, Ado Samweli Lugome pamoja na kijana aliyehusika na mauaji kwa ajili ya upelelezi.

“Haya mauaji ni ya hovyo,yaani kaka kamuua mdogo wake kisa na mkasa kuku wa mdogo mtu wameenda kwenye shamba la kaka mtu.”Alisema Kamanda Issa

Hata hivyo ameongeza kuwa katika upelelezi uliokuwa unaendelea wamebaini familia hizo zimekuwa zikituhumiana na maswala ya ushirikina.

“Katika ufuatiliaji wa swala hili tumeona wanatuhumiana kuwa mmoja anatembea na mke wake na mwingine anamtuhumu mwenzie kuwa alikuwa anamloga.”Alisema kamanda Issa

Ametoa rai kwa jamii kuacha kuamini ushirikina badala yake kutoa taarifa sehemu husika ili kusaidiwa kuliko kuchukua hatua mkononi.

Share:

SIMBA YATANGAZA MICHUANO YAKE....KOCHA MPYA KUTANGAZWA KESHO


Simba Sport Club leo January 22, 2021 , imetangaza michuano ya Kimataifa ‘Simba Super CUP’ ikihusisha timu tatu Simba, TP Mazembe ya Congo na Al Hilal ya Sudan.


Pia, timu hiyo imesema, kesho Jumamosi, itamtangaza kocha mpya atakayechukua mikoba ya Sven Vanderbroeck aliyeondoka. Kocha mpya atasaidiwa na kocha msaidizi, Suleiman Matola.

Akitangaza michuano hiyo leo Ijumaa tarehe 22 Januari 2021, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba (CEO), Barbara Gonzalez amesema, michuano hiyo, itaanza Jumatano ijayo tarehe 27- 31 Januari 2021.

Amesema, mechi ya kwanza itakuwa Simba dhidi ya Al Hilal saa 11 jioni.

Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema, michuano hiyo “ni maalum kwa mabingwa wa nchi, kama timu yako siyo bingwa, huhusiki na michuano hii.”


Share:

WALIMU WAWILI MKOANI NJOMBE WATIWA MBARONI KWA KUMTOA MIMBA MWANAFUNZI


Na Amiri Kilagalila, Njombe
JESHI la Polisi mkoani Njombe linawashikilia walimu wawili wa shule ya sekondari Mang’oto wilayani Makete mkoani Njombe kwa tuhuma za kumsababishia ujauzito na kumtoa mwanafunzi wa shule hiyo mwenye umri wa miaka 17.

Akizungumza na vyombo vya habari, kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa Njombe,  Hamis Issa amesema wanamshikilia mwalimu Ezekiel Thomas (36) maarufu kwa jina la Dokole kwa kuwa na mahusiano na mwananfunzi na kumsababishia ujauzito.

“Huyu mwalimu amekuwa na mahusiano na mtoto wa sekondari mwenye umri wa miaka 17 na binti huyo amepimwa amegundulika ni mjamzito.” Alisema kamanda Issa

Aidha amesema wanamshikilia mwalimu, Ben Liamdilo (35) kwa kushirikiana katika tukio la utoaji wa mimba na kumsababishia maumivu mwanafunzi huyo.

“Mwalimu Thomas alifanya juhudi akamtuma huyu mwalimu mwenzake akambeba na boda boda kwenda kumtoa mimba mpaka sasa hivi walimu wote wawili tunawashikilia na wanatuhumiwa na makosa haya.”Alisema kamanda Issa

Vile vile ameitaka jamii kushirikiana kwa kutoa taarifa kwa jeshi la Polisi ili kukabiliana na vitendo kama hivyo.


Share:

WAZIRI MKUU ACHANGISHA SH. MILIONI 18.9 KUMSAIDIA MTOTO MIRIAM


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameendesha harambee ya papo kwa papo na kuchangisha sh. milioni 18.9 ambapo kati ya hizo, sh. milioni 10 zimetolewa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

“Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli anafuatilia tukio hili na amesema anamchangia Miriam shilingi milioni 10 ili ziweze kumsaidia katika mtaji wa biashara na umaliziaji wa ujenzi wa vyumba vya kupangisha”

Fedha hiyo ilichangishwa kwa ajili ya Miriam Msagati, binti mwenye ulemavu wa mwili ili ziweze kumsaidia kama mtaji wa biashara na uendelezaji wa ujenzi wa vyumba vya kupangisha katika nyumba ambayo amekabidhiwa leo (Ijumaa, Januari 22, 2021) na Waziri Mkuu. Gharama ya ujenzi wa nyumba na samani zilizomo ndani ni sh. milioni 47.32.

Waziri Mkuu ameendesha harambee hiyo kwenye kitongoji cha Fune, kata ya Mombo wilayani Korogwe baada ya kumkabidhi binti huyo nyumba aliyojengewa na wadau mbalimbali kutokana na mchango ulioasisiwa na Waziri Mkuu Machi 5, 2020 alipomtembelea Miriam na kumpatia mchango wa sh. milioni 5 za kuanza ujenzi wa nyumba hiyo.

Waziri Mkuu alimsaidia Miriam baada ya kumsikia binti akimuomba amsaide kupata makazi yeye na bibi yake kupitia kipindi cha Wape Nafasi kinachoongozwa na Tuma Dandi, mtangazaji wa Shirika la Utangazi Tanzania (TBC1).

Baada ya Waziri Mkuu kukabidhi nyumba hiyo, aliwaomba wadau wamchangie Miriam fedha ili apate mtaji pamoja na umaliziaji wa vyumba vya kupangisha ili aweze kujitegemea.

Akiwa bado anaendesha harambee hiyo, Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan alizungumza na wananchi hao kupitia simu aliyompigia Waziri Mkuu, ambapo alimpongeza kwa kuhakikisha Miriam anapata makazi bora. “Nimeona kazi kubwa iliyofanyika hapo, hongereni sana Waziri Mkuu pamoja na uongozi wa mkoa wa Tanga nami namuongezea shilingi milioni tano afanye mtaji.”

Kwa upande wake, Miriam baada ya kukabidhiwa nyumba hiyo alimshukuru Rais Dkt. Magufuli, Makamu wa Rais Mama Samia, Waziri Mkuu kwa uongozi wao wenye kujali wanyonge.

Alisema Tanzania imepata kiongozi mzuri anayewajali wanyonge, hivyo ameahidi kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu awazidishie baraka ili wapate mafanikio mazuri zaidi.

“Siwezi kusahau kitu kama hiki, Mwenyezi Mungu ameniona, Mwenyezi Mungu awabariki watu wote walioshiki katika kufanikisha jambo hili kwani mmeweka hazina yenu kwa Mungu.”

Kwa upande wake, Muandaaji wa Kipindi cah Wape Nafasi, Tuma Dandi alitumia fursa hiyo kuishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa namna inavyoshughulikia masuala mbalimbali ya watu wenye mahitaji maalumu.

“Nimeishiwa maneno, leo ni siku nyingine ambayo itaingia katika historia ya maisha yangu. Ninamshukuru Mwenyezi Mungu na Serikali kwa kufanikisha jambo hili kwani watu wenye ulemavu ni sehemu ya Watanzania ambao wanapaswa kuishi kama wengine.”

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


 


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger