Monday, 11 January 2021

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARI 11,2021





























Share:

Sunday, 10 January 2021

Syrup Room and Water Treatment Team Leader at Coca-Cola Kwanza

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Title: Syrup Room and Water Treatment Team Leader   Closing Date: 2021/01/18 Reference Number: CCB210108-2 Function Manufacturing Company Coca-Cola Kwanza (Tanzania) Job Type: Permanent Location – Country Tanzania Location – Province Not Applicable Location – Town / City Mbeya Job Description Coca-Cola Kwanza Ltd has an exciting opportunity in Manufacturing Department. We are looking for […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Accountant, Call Center Interns, Debt Collection Trainees ,Sales Executives at Credit & Debt Masters Co Ltd

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

About us Credit & Debt Masters Co Ltd prides as a premier credit and debt management services provider in Tanzania, devoting our both human and capital resources into helping our clients maximize their cash flows, add value to their organizations and gain a competitive advantage. Our key services includes; Debt Management and Recovery, Credit Control […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Project Administrative Officer at Americares

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

TITLE: Project Administrative Officer – Community Partnerships for Respectful Care (CPRC) project DEPARTMENT: International Partnerships & Programs REPORTS TO: Tanzania Project Director, Community Partnerships for Respectful Care (CPRC) project ASSIGNMENT TYPE: Full-time LOCATION: Mwanza, Tanzania LENGTH:  24-months with possibility to extend based on performance and budget ABOUT AMERICARES:  Americares is a health-focused relief and development organization that […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Administration Officer at Total

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

ADMINISTRATION OFFICER   Workplace location DAR ES SALAAM-HAILE SELASSIE RD(TZA) Job Description Manage office leases and house rents for expatriates and upcountry employees. To ensure that office premises are in good state i.e. overall housekeeping is well maintained through liaison with service providers. To ensure that all services are provided on a regular basis and provide […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Information System Officers at CRDB Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Information System Officers   CRDB Bank PLC is looking for suitable candidates to fill 2 vacant positions of Information System Officers existing in the Department of Information & Communication Technology (ICT) at Head Office, Dar Es Salaam. The Business Applications Specialist (BAS) is responsible for providing operational support and maintenance of healthcare of business automation applications […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

BASI LAZUA TAHARUKI BAADA YA KUTUMBUKIA BAHARINI

Watu wawili wamenusurika kifo nchini Kenya baada ya basi la Watalii linalomilikiwa Pollman Tours na Safari Company kuanguka katika bahari ya Hindi katika feri ya Likoni.

Inaarifiwa basi hilo lilikuwa likitoka upande wa Pwani Kusini kuelekea Mombasa wakati kisa hicho kilifanyika kwenye kivukio cha Likoni. 

Walioshuhudia kisa hicho wanasema dereva wa basi hilo alipoteza mwelekeo alipokuwa akijaribu kuingia kwenye feri. 

Ni dereva na utingo wake waliokuwa kwenye basi hilo na walishauriwa kuruka nje huku basi likiendelea kuzama.

Video kwenye mitandao zilionyesha wakazi wamejawa na hofu huku wakishauri waliokuwa ndani kuruka nje. Wawili hao waliruka na kuokolewa na mashua iliyokuwa ikipiga doria baharini.

Aidha maafisa wa shirika la feri pia wamefaulu kuiokoa basi hiyo isizame.

Mtandao wa Nation , umeandika kuwa basi liliteleza kutoka kwenye feri na kuingia ndani ya majira ya saa nne asubuhi ,hatua chache kabla ya eneo la nchi kavu.

Dereva na kondakta wameokolewa wote na polisi pamoja na walinzi wa kivuko.

Basi hilo la Yutong luxury lilikuwa linatokea Diani where ambapo lilikuwa limewapeleka watalii waliowasili Mombasa hapo jana.

Ingawa kuna basi lingine kutoka kampuni hiyo hiyo lilifanikiwa kuingia kwenye feri likiwa salama.

Dereva wa basi hilo bwana Salim Omar amewaambia polisi kuwa alishindwa kulidhibiti gari kuanguka majini baada kunaza kuteleza, na kulikuwa na mvua iliyonyesha majira ya asubuhi.

"Nilikuwa karibu nafika feri lakini basi likanizidi nguvu na kuanguka,Ninamshukuru tu Mungu kuwa tuko salama," alisema bwana Omar, ambaye alikuwa bado anatetemeka.

Alisema amekuwa akivuka likoni wakati anaendesha kwa miaka 11 na hajawahi kukutana na tukio la namna hii, hii ni mara ya kwanza.

Share:

GARI LA KAMANDA WA POLISI GEITA, HIACE ZATEKETEA MOTO, CHANZO BODA MWENYE DIZELI


Na Rehema Matowo - Mwananchi
Gari ya Kamanda wa polisi mkoa wa Geita na gari ndogo ya abiria aina ya Hiace leo mchana zimewaka moto na kuteketea baada ya ajali iliyosababishwa na dereva boda boda aliyekuwa amebeba mafuta ya dizeli.

Hata hivyo, Kamanda wa polisi mkoa wa Geita, Hendry Mwaibambe hakuwemo kwenye gari hiyo na amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema imetokea leo majira ya saa 8.46 mchana katika eneo la Makurugusi wilayani Chato mkoani Geita.

Katika ajali hiyo, dereva wa boda boda ambaye inasemekana amepoteza maisha huku watu 16 wakijeruhiwa ambapo wawili kati yao ni askari polisi.

Akielezea tukio hilo, Kamanda Mwaibambe amesema dereva wa boda boda huyo alikuwa amebeba lita 100 za mafuta ya dizeli akaingia barabarani bila umakini na kugongwa na gari ya kamanda kisha kwenda kugonga hiace iliyokuwa imeegeshwa pembezoni mwa barabara na kusababisha magari yote kuwaka moto .

Amesema gari hiyo ya polisi yenye namba PT 4447 iliyokuwa ikiendeshwa na Koplo Manase Nestory imewaka moto kufuatia cheche za pikipiki baada ya ajali kuangukia mafuta yaliyomwagika.

Kwa mujibu wa kamanda, majeruhi wamekimbizwa hospitali ya wilaya ya Chato na kwamba hali ya dereva wa Hiace ni mbaya huku polisi wakitibiwa na kuruhusiwa kuondoka.



Share:

SAVE THE CHILDREN YAENDESHA MDAHALO WA BAJETI JUMUISHI NGAZI YA HALMASHAURI MANISPAA YA SHINYANGA


Mtaalam wa Haki za Watoto na Utawala Bora kutoka Save The Children Makao Makuu Jesca Ndana, akizungumza kwenye Madahalo huo.

Na Marco Maduhu  Shinyanga. 

Shirika la Save The Children linalojihusisha na utetezi wa haki za watoto katika nchi 117 duniani ikiwemo Tanzania, limeendesha mdahalo wa utekelezaji wa bajeti jumuishi katika sekta zinazomuhusu mtoto moja kwa moja katika halmashauri ya manispaa ya Shinyanga.

Mdahalo huo umefanyika leo, katika ukumbi wa Hoteli ya Empire Mjini Shinyanga, ambao umekutanisha maafisa elimu, maendeleo, wachumi, viongozi wa kisiasa, dini, wajumbe wa baraza la watoto, wadau kutoka mashirika na asasi zisizo za kiserikali, waandishi wa habari, pamoja na maofisa kutoka TAMISEMI wanaohusika na masuala ya bajeti, huku mgeni rasmi akiwa ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Geoffrey Mwangulumbi. 

Mratibu wa Mradi wa Mijadala Jumuishi katika Masuala ya Uchumi na Utawala wa Kifedha Alex Enock kutoka Shirika la Save The Children mkoani Shinyanga, amesema wameandaa na kuwezesha mdahalo huo ,ili wadau wajadili kwa pamoja namna ya kupanga bajeti bora ambayo itazingatia maslahi mapana ya watoto. 

Amesema Shirika hilo limekuwa likitekeleza miradi mbalimbali ya utetezi wa haki za watoto ikiwemo mradi huu wa mijadala jumuishi, ambao utekelezaji wake ulianza mwaka jana (2020), na umelenga zaidi masuala ya kisera ya utekelezaji wa bajeti zinazomhusu mtoto na utakoma mwaka huu (2021).

Ameongeza kuwa kupitia mradi huu Save the Children ingependa kuona ushirikishwaji wa wadau wakiwemo wanajamii wa kawaida na watoto katika mchakato wa kibajeti na kuboresha utekelezaji wa bajeti za watoto. 

"Save the Children tumeendesha mdahalo huu wa bajeti jumuishi haswa tukianzia sekta inayomgusa mtoto moja kwa moja, kwa lengo la kujadiliana namna ya kupanga bajeti ambayo itazingatia maslahi ya watoto katika sekta hizo mbazo ni afya na lishe, elimu, maendeleo ya jamii, ulinzi na usalama wa mtoto," amesema Enock. 

"Mradi huu unatekelezwa katika wilaya tano zikiwemo Unguja mjini, Magharabi “A” na “B” Visiwani Zanzibar, na wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, pamoja na manispaa ya Shinyanga, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU).

"Ni matarajio yetu kuwa wadau kwa kushirikiana na halmashauri husika zitaweza kuyapa kipaumbele masuala ya watoto kwenye bajeti zao, na hivyo kumuwezesha mtoto wa Kitanzania kupata haki zake", ameongeza. 

Kwa upande wake mgeni rasmi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Geoffrey Mwangulumbi, amelipongeza Shirika la Save the Children kwa kuendesha mdahalo huo, na kubainisha upo katika muda muafaka, ambapo wadau wanapaswa kuanza kujadili kuanzia sasa vipaumbele na malengo ya bajeti ngazi za chini. 

Amesema katika upangaji wa bajeti hizo ikiwamo ya watoto, kuwepo na vipaumbele vichache muhimu, ambavyo vitaweza kutekelezeka kulingana na bajeti ya fedha za halmashauri, kuliko kuwa na vipaumbele vingi ambavyo haviwezi kutekelezeka. 

Naye Makamu Mwenyekiti Baraza la watoto Manispaa ya Shinyanga Nancy Kasembo, amepongeza mdahalo huo, ambao umewapatia mwanga wa namna ya kushiriki kikamilifu kwenye utoaji wa mapendekezo ya bajeti zinazomhusu mtoto. 

TAZAMA PICHA HAPA CHINI
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Geofrey Mwangulumbi, akizungumza kwenye Mdahalo huo.
Mratibu wa mradi wa mijadala jumuishi katika masuala ya uchumi na utawala wa kifedha Alex Enock kutoka Shirika la Save The Children mkoani Shinyanga, akizungumza kwenye Mdahalo huo.
Mratibu wa mradi wa mijadala jumuishi katika masuala ya uchumi na utawala wa kifedha Alex Enock kutoka Shirika la Save The Children mkoani Shinyanga, akiendelea kuzungumza kwenye Mdahalo huo.
Mtaalamu wa haki za watoto na utawala Bora kutoka Save The Children Makao Makuu Jesca Ndana, akizungumza kwenye Madahalo huo.
Mtaalam wa Haki za watoto na utawala Bora kutoka Save The Children Makao Makuu Jesca Ndana, akizungumza kwenye Mdahalo huo.
Mchumi kutoka TAMISEM Allan Bendera, akizungumza kwenye Mdahalo huo.
Gerald Ng'ong'a ambaye alikuwa mwenyekiti wa Mdahalo huo akizungumza na kutoa maoni yake.
Washiriki wakiwa kwenye Mdahalo huo.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Waandishi wa Habari nao wakishiriki kwenye Mdahalo huo, wakwanza kushoto ni Fanki Mshana Mwandishi wa ITV, katika Suzy Butondo wa Mwananchi, akifuatiwa na Malaki Philipo wa RFA.
Diwani wa Kata ya Kolandoto Manispaa ya Shinyanga Mussa Elias akichangia mada kwenye Mdahalo huo.
Mchumi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Gwakisa Mwasheba, akichangia Mada kwenye Mdahalo huo.
Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Octavina Kiwone akichangia Mada kwenye Mdahalo huo
Mwenyekiti wa Shirikisho wa vyama vya watu wenye ulemavu mkoani Shinyanga (SHIVYAWATA), Richard Mpongo, akichangia mada kwenye Mdahalo huo.
John Shija kutoka Shirika la PACESH Mkoani Shinyanga akichangia mada kwenye Mdahalo huo.
John Eddy kutoka Shirika la TAWLAE, akichangia Mada kwenye Mdahalo huo.
Makamu Mwenyekiti Baraza la watoto Manispaa ya Shinyanga Nancy Kasembo, akichangia Mada kwenye Mdahalo huo.
Mchumi kutoka TAMISEM Allan Bendera, akichangia Mada kwenye Mdahalo huo.
Washiriki wa Mdahalo huo wakiwa kwenye kazi ya vikundi.
Kazi ya vikundi ikiendelea.
Kazi ya vikundi ikiendelea.
Kazi ya vikundi ikiendelea.
Uwasilishaji kazi ya vikundi ukiendelea.
Uwasilishaji kazi ya vikundi ukiendelea.
Uwasilishaji kazi ya vikundi ukiendelea.

Na Marco Maduhu- Shinyanga.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger