Thursday, 1 October 2020

Picha : KAMPUNI YA AKO GROUP LTD YATOA MSAADA WA MIFUKO 200 YA SARUJI KUSAIDIA UJENZI MADARASA SHULE YA BUGARAMA

Kushoto ni Meneja wa Kampuni ya Ako Group Limited, Athanas Kahigi akimkabidhi mifuko ya saruji Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi kwa ajili ya ujenzi wa madaras katika shule ya Msingi Bugarama.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Kampuni ya Ako Group Limited inayotoa huduma ya chakula na usafi wa mazingira katika Mgodi wa Bulyanhulu imetoa msaada wa mifuko 200 ya saruji yenye thamani ya shilingi milioni 4.2 ili kusaidia ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga.



Mifuko hiyo ya saruji imekabidhiwa Jumatano Septemba 30,2020 na Meneja wa Kampuni ya Ako Group Limited, Athanas Kahigi kwa Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ambayo imefanyika katika shule ya Msingi Bugarama.



Akizungumza katika hafla hiyo iliyohudhuriwa pia na wafanyabiashara wanaoshirikiana na Kampuni ya Ako Group Limited Kahigi alisema wao kama wafanyabiashara wanaofanya kazi na Mgodi wa Bulyanhulu ni sehemu ya jamii hivyo wanao wajibu kusaidia jamii inayozunguka mgodi huo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Sheria Mpya ya Madini.

“Tulitembelea shule hii ya Bugarama na kujionea jinsi wanafunzi wanavyosoma katika mazingira yasiyo rafiki kutokana upungufu wa madarasa na wingi wa wanafunzi nasi Ako Group Ltd tukaahidi kuchangia mifuko ya saruji 200 yenye thamani ya shilingi milioni 4.2 na leo tumekuja kuikabidhi ili ujenzi wa madarasa”,alisema Kahigi.

Aidha aliwashukuru wafanyabiashara wanaoshirikiana na Ako Group Limited kuchangia vifaa vya ujenzi na fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule hiyo huku akiwataka wajiandae kuzalisha zaidi kwani mgodi utaanza rasmi kufanya shughuli za uzalishaji rasmi hivi karibuni.

Katika hatua nyingine Ako Group Ltd inaendelea kusaidia jamii kwa kufanya shughuli mbalimbali kama vile kujenga chumba cha darasa katika shule ya sekondari Bulyanhulu pamoja na kutoa ajira katika mgodi wa Bulyanhulu ambapo wameajiri wafanyakazi 69 katika shughuli za upishi,usafi wa vyumba,ofisi na udhibiti wa taka kati yao wanawake ni 30,wanaume 39 kutoka vijiji 14 jirani na mgodi.

"Katika kutekeleza sheria Mpya ya Madini kupitia kitengo cha huduma za jamii inayozunguka eneo la Mgodi wa Bulyanhulu, Ako Group Ltd imeajiri mtu mwenye ulemavu wa ngozi 'mtu mwenye ualbino' Gaspal William kutoka kijiji cha Ilogi katika kitengo cha usafi wa ofisi na tayari kikundi kipya cha wanawake cha Mkombozi kutoka Igudija tumekipa utaratibu wa usambazaji matunda safi na mbogamboga kutoka kwenye mashamba yao",aliongeza Kahigi.

Akipokea mifuko hiyo ya saruji, Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala, Cosmas Magigi ambaye ni Afisa Elimu Shule za Msingi halmashauri hiyo,aliipongeza Kampeni ya Ako Group Limited ambao ni wakandarasi wazawa kusaidia sekta ya elimu ambapo baada ya ujenzi wa madarasa kukamilika watoto watasoma katika mazingira mazuri.

“Tunawashukuru sana Ako Group Ltd na wadau wengine waliojitokeza kuchangia vifaa kwa ajili ya ujenzi wa madarasa hali ambayo itapunguza msongamano wa wanafunzi darasani. Tunaomba wadau wengine waendelee kutusaidia ili elimu iweze kupanda katika halmashauri yetu”,alisema Magigi.

Kwa Mujibu wa Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Bugarama Kubebeka Leonard alisema shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 2324, walimu waliopo ni 23,kuna upungufu wa walimu 27, madarasa yaliyopo ni 18 na kuna upungufu wa madarasa 32.

Naye Katibu wa Chama cha Ushirika Igaka, Emmanuel Kasala ambao ni miongoni mwa wadau wanaofanya biashara na Kampuni ya Ako Group Ltd waliochangia mifuko mitano ya saruji wamesema wataendelea kushirikiana na jamii kutatua changamoto zilizopo.

Katika hafla hiyo, Kampuni ya Ako Group Ltd imetoa zawadi ya ya vyeti kwa wafanyabiashara wanaofanya kazi na Kampuni hiyo ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao,ambao ni Afrimar, Alpher Choice, Igaka, Nyakabale, Mamuu Chicken, Bufaso,Mkombozi na Juago Food Products ambapo pia walichangia vifaa vya ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Bugarama kuunga mkono juhudi za Kampuni ya Ako Group Ltd.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Kushoto ni Meneja wa Kampuni ya Ako Group Limited, Athanas Kahigi akimkabidhi mifuko ya saruji Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama Septemba 30,2020. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Meneja wa Kampuni ya Ako Group Limited, Athanas Kahigi ,Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi na viongozi wa shule na kijiji cha Bugarama wakipiga picha ya pamoja wakati wa makabidhiano ya mifuko ya saruji.
Muonekano wa sehemu ya mifuko 200 ya saruji iliyotolewa na Kampuni ya Ako Group Limited
Trekta la Ako Group Limited likiwa limebeba mifuko ya saruji.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi (kushoto) akipokea mifuko mitano ya saruji kutoka kwa viongozi wa Chama Cha Ushirika Igaka wanaofanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited.
Meneja wa Kampuni ya Ako Group Limited, Athanas Kahigi akielezea kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na Kampuni hiyo katika Mgodi wa Bulyanhulu ikiwa ni pamoja na kusaidia jamii inayozunguka mgodi huo. Alisema wamekabidhi mifuko 200 ya saruji ili kusaidia ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama. Kushoto ni Mwalimu Mkuu shule ya msingi Bugarama, Kubebeka Leonard. Wa kwanza kulia ni Meneja Mahusiano ya Jamii mgodi wa Bulyanhulu, Dk. Zumbi Musiba.
Meneja wa Kampuni ya Ako Group Limited, Athanas Kahigi akizungumza wakati wa kukabidhi mifuko 200 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Bugarama iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Msalala.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi akiishukuru Kampuni ya Ako Group Limited kuchangia mifuko ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama.
Mwalimu Mkuu shule ya Msingi Bugarama akiishukuru Kampuni ya Ako Group Limited na wadau wengine kuchangia vifaa vya ujenzi kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama.
Meneja Mahusiano ya Jamii mgodi wa Bulyanhulu, Dk. Zumbi Musiba akizungumza wakati Kampuni ya Ako Group Limited inayojishughulisha na uuzaji wa vyakula na usafi wa mazingira katika mgodi wa Bulyanhulu ikitoa msaada wa mifuko ya saruji kusaidia ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Bugarama iliyopo katika Halmashauri ya wilaya ya Msalala.
Afisa Mtendaji kata ya Bugarama Prisca Joseph akizungumza wakati Kampuni ya Ako Group Limited ikitoa msaada wa mifuko ya saruji kusaidia ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Bugarama iliyopo katika Halmashauri ya wilaya ya Msalala.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Bugarama Emmanuel Masanja Mhoja akizungumza wakati Kampuni ya Ako Group Limited ikitoa msaada wa mifuko ya saruji kusaidia ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Bugarama iliyopo katika Halmashauri ya wilaya ya Msalala.
Wafanyabiashara wanaofanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited wakiwa kwenye hafla ya kukabidhi vifaa vya ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama.
Wafanyabiashara wanaofanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited wakiwa kwenye hafla ya kukabidhi vifaa vya ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama.
Wafanyabiashara wanaofanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited wakiwa kwenye hafla ya kukabidhi vifaa vya ujenzi wa madarasa katika shule ya Msingi Bugarama.
Kulia ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi akikabidhi cheti kwa mfanyabiashara anayefanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi akikabidhi cheti kwa wafanyabiashara wanaofanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi akikabidhi cheti kwa mfanyabiashara anayefanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi akikabidhi cheti kwa mfanyabiashara anayefanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Msalala Cosmas Magigi akikabidhi cheti kwa mfanyabiashara anayefanya kazi na Kampuni ya Ako Group Limited.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog



Share:

Picha : MAGUFULI AKIWAHUTUBIA WANANCHI WA MBALIZI MBEYA LEO ASUBUHI


Baadhi ya Wananchi wakimsikiliza Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia wakazi wa eneo hilo la Mbalizi mkoani Mbeya wakati akielekea Tundumba kwa ajili ya Mikutano ya Kampeni za Urais kwa upande wa CCM leo tarehe 01 Oktoba 2020. 
Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa Mbalizi mkoani Mbeya wakati akielekea Tundumba kwa ajili ya Mikutano ya Kampeni za Urais kwa upande wa CCM leo Oktoba 01,2020. 

Share:

MWENYEKITI WA MTAA ASIMULIA JINSI MJUKUU WAKE WA MIAKA 7 ALIVYOCHINJWA NA MAMA YAKE

Picha haihusiani na habari hapa chini

Na Doreen Aloyce,TimesMajira, Online Dodoma

Mtoto wa miaka saba aitwaye Willy Wiliam mwanafunzi wa darasa la tatu Shule ya Msingi Ihumwa ameuawa kwa kuchinjwa shingo na mtu anayedaiwa kuwa ni mama yake mzazi, Grace William (45) kisha kutokomea kusikojulikana.

Tukio hilo limetokea usiku wa manane kuamkia Septemba 30,2020 katika Mtaa wa Ihumwa, nje kidogo ya Jiji la Dodoma ambako mtoto alikuwa akiishi na mama huyo.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Ihumwa ambaye pia ni baba mzazi wa Grace, William Ngilimunji, amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo na kwamba aliyekufa ni mjukuu wake. Alidai wakati mauaji hayo yanafanyika mtoto alikuwa amelala.

Amedai kwamba aliyehusika na mauaji hayo ni mama wa mtoto huyo ambaye ana matatizo ya akili na kwamba alikuwa akihudhuria kliniki Hospitali ya Wagonjwa wa Akili Mirembe, mkoani hapa.

Ngilimunji amesema mtoto wake huyo (mama wa marehemu) hana mume na amekuwa akiishi Ihumwa. 

Via TimesMajira
Share:

Financial Management Analyst – OSC at U.S. Embassy Dar es Salaam

U.S. MISSION DAR ES SALAAM VACANCY ANNOUNCEMENT The U.S. Mission in Dar es Salaam is seeking eligible and qualified applicants for the position below. Position Title: Financial Management Analyst – OSC Vacancy Number: DaresSalaam-2020-029 Duties Budget Analyst 60% Serves as the Budget Analyst for the Office of Security Cooperation (OSC), with the responsibility of performing […]

The post Financial Management Analyst – OSC at U.S. Embassy Dar es Salaam appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Nyasa District Council Jobs September, 2020. Nyasa District is a district of the Ruvuma Region of Tanzania.

The deadline for submitting the application is October 13, 2020

The post Nyasa District Council Jobs September, 2020. Nyasa District is a district of the Ruvuma Region of Tanzania. appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MAASKOFU NA WACHUNGAJI WAZINDUA KITABU CHA UONGOZI ULIOTUKUKA WA RAIS JOHN MAGUFULI


Askofu Mkuu wa Makanisa ya Naioth Gospel Assemblies of God ambaye pia ni Katibu Mkuu mstaafu wa Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste Tanzania, Dkt. David Mwasota.(kushot) akiwaongoza Maaskofu na Wachungaji kwenye maombi ya kukiombea Kitabu cha Uongozi Uliotukuka wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika hafla ya uzinduzi wa kitabu hicho iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwanzoni mwa wiki.
Maombi ya kukiombea kitabu hicho yakiendelea kufanyika.
Askofu Mkuu wa Makanisa ya Naioth Gospel Assemblies of God ambaye pia ni Katibu Mkuu mstaafu wa Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste Tanzania, Dkt. David Mwasota., akizungumza na Maaskofu na Wachungaji kwenye maombi ya kukiombea Kitabu cha Uongozi Uliotukuka wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika hafla ya uzinduzi wa kitabu hicho iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwanzoni mwa wiki.
Muonekano wa kitabu hicho.
Askofu Sedrick Ndonde wa Kanisa la Restroration Bible ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Kanisa hilo walioandika kitabu hicho.
Uzinduzi wa kitabu hicho ukifanyika.

Na Dotto Mwaibale

MUUNGANO wa Maaskofu zaidi ya 15 na Wachungaji 100 mwanzoni mwa juma walizindua kitabu kinachoelezea uongozi uliotukuka wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Kitabu hicho kimeandikwa na Mtendakazi katika shamba la Bwana, Restoration Bible Church Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Uzinduzi wa kitabu hicho kiitwacho Uongozi Uliotukuka, JPM ni Kiongozi wa Kisiasa na Kiroho, uliofanyika jijini Dar es Salaam uliongozwa na Askofu Mkuu wa Makanisa ya Naioth Gospel Assemblies of God ambaye pia ni katibu Mkuu mstaafu wa Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste Tanzania, Dkt. David Mwasota.

Mwasota alisema lengo la kuandikwa kitabu hicho ni kutazama uongozi wa Rais Magufuli kwa pande za kisiasa na kiroho.

Askofu huyo alisema katika utendaji kazi wake, Magufuli anamtegemea Mungu hivyo kumfanya aonekane anaiongoza nchi kwa upande wa kiroho.

“Imani ya Mheshimiwa Magufuli katika kushughulikia janga la Corona kiroho limefanya kuinua imani ya watu wengi kwa kulisaidia kanisa ambalo ndiyo kazi yake kubwa kuwajenga watu kiimani,” alisema askofu huyo.

Mwasota aliwaomba maaskofu, wachungaji na waumini wote kuendelea kumuombea Rais Magufuli kwani ndiyo yalikuwa maombi yao kwa miaka mingi kwa Mungu atuletee kiongozi kama yeye.

“Tunamshukuru Mungu aliyejibu maombi yetu kwa kutuletea kiongozi tuliyemuomba miaka mingi ambaye ni Magufuli anayeliongoza taifa letu kisiasa na kiroho,” alisema Mwasota.

Askofu huyo aliongeza kuwa katika nchi yetu hatukuwahi kumpata kiongozi wa juu anayemtaja Mungu wakati wote na kuwaagiza watendaji wake kila anapowaapisha wamtangulize na kumtegemea Mungu.

Naye Bishop Sedrick Ndonde wa Kanisa la Restroration Bible ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Kanisa hilo walioandika kitabu hicho, alisema lengo la kitabu hicho ni kuelezea ukweli kuhusu Rais Dkt. John Magufuli ili kufahamu zaidi nini alichobeba mbali ya wadhifa wa urais alionao na kulikumbusha kanisa na watumishi wa Mungu kuutafakari uongozi wake.

“Umuhimu wa kitabu hiki ni kuwakumbusha watumishi wa Mungu kuwa na muda wa kutafakari uongozi wa JPM kwa yote aliyoyafanya kwa upande wa kiroho,” alisema Askofu Ndonde.

Aliongeza kwa kumtegemea Mungu amefanya mambo makubwa kama kujenga miundombinu ya barabara, umeme, maji, shule, hospitali na kuwawezesha watanzania kunufaika na madini, mbuga za wanyama ambapo awali waliokuwa wakinufaika walikuwa watu kutoka nje.

 “Magufuli ni mfalme anayekiri ufalme wa Mungu kutawala taifa letu,” alisema Ndonde.

Ndonde aliongeza kuwa kuna umuhimu wa kukisambaza kitabu hicho kwa waumini wao na wananchi wengine kwa ujumla  bila kujali dini wala madhehebu wanayotoka ili waweze kuwa na mtazamo chanya. 




Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi October 1
















Share:

Wednesday, 30 September 2020

Individual National consultancy at UNICEF

The aim is to assess whether the Parenting Education Programme has been implemented effectively and whether it has brought about positive change in the knowledge and behaviour of parents and caregivers in how to protect their children from violence. UNICEF works in some of the world’s toughest places, to reach the world’s most disadvantaged in […]

The post Individual National consultancy at UNICEF appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

HESLB Yatoa Siku Tano (05) Kwa Wahitimu Mafunzo Jkt Kuomba Mikopo


Na Mwandishi Wetu, HESLB
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa muda wa siku 5 kuanzia Oktoba mosi hadi 5 mwaka huu ili kuwawezesha wanafunzi waliomaliza mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) hivi karibuni kuingia katika mfumo wa kuomba mkopo kwa njia ya mtandao na kukamilisha maombi yao.

Katika taarifa yake aliyotoa kwa vyombo vya habari leo Jumatano (Septemba 30, 2020) Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru alisema uamuzi huo unatokana na maombi ya wanafunzi, wazazi na walezi ambao hawakuweza kuomba au kukamilisha maombi yao kutokana na sababu ya kujiunga na mafunzo hayo.

Kwa mujibu wa Badru alisema katika muda huo wa siku tano, mfumo pia utakuwa wazi ili kuwawezesha waombaji ambao maombi yao yana upungufu kurekebisha kwa kuweka nyaraka sahihi ili kuiwezesha HESLB kuendelea na hatua nyingine.

“Kwa wanaorekebisha taarifa, wanapaswa kuingia katika akaunti zao walizofungua kuombea mkopo na watapata ujumbe kuhusu maeneo ya kurekebisha. Tunawasihi watumie muda huu wa siku tano kurekebisha na kukamilisha maombi yao’’ alisema Badru.

Katika mwaka wa masomo 2020/2021, Serikali imetenga TZS Bilioni 464 zitakazowanufaisha jumla ya wanafunzi 145,000. Kati yao, wanafunzi 54,000 watakuwa wa mwaka wa kwanza na wengine 91,000 ni wanafunzi wanufaika wanaoendelea na masomo. Mwaka 2019/2020 jumla ya TZS 450 bilioni zilitengwa na zimewanufaisha jumla ya wanafunzi 132,119.

MWISHO


Share:

Barabara za juu kutoka Mwenge kwenda Buguruni katika makutano za barabara ya morogoro,Nelson Mandela na Sam Nujoma zaanza kutumika rasmi leo

Barabara za juu kutoka Mwenge kwenda Buguruni katika makutano za barabara ya morogoro,Nelson Mandela na Sam Nujoma zaanza kutumika rasmi leo( Picha- MAELEZO)


 


Share:

PICHA: Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM, Dr Magufuli ahutubia wananchi wa Mbeya mjini

PICHA: Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM, Dr Magufuli ahutubia wananchi wa Mbeya mjini





 


Share:

Vijana Kagera Watakiwa Kutosubiri Ajira kutoka Serikalini.

Na Avitus Benedicto Kyaruzi,Kagera.
Vijana katika halmashauri ya Wilaya ya Missenyi Mkoani Kagera wameaswa kutosubiri ajira kutoka  serikalini bali wajikite katika kujiajili haswa katika kilimo,uvuvi na ufugaji ili kuweza kujikwamua na umasikini.


Hayo yamesemwa na bwana Agape Ishabakaki wakati akizungumza na mpekuzi blog ambaye pia ni mratibu wa shirika lisilo la kiserikali la FUAP TANZANIA linalojiusisha na masuala ya kusaidia wakulima na wafugaji ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ya watu haswa vijana ili kujenga utamaduni wa kujiajili uku wakiwa wamesubiri ajira kutoka serikalini. 


Bwana Agape amesema kuwa shirika hilo kwa sasa limetua mkoani Kagera hususani katika wilaya ya Missenyi na litazungukia kata mbalimbali ili kutoa elimu kwa vijana juu ya faida za kujiajili na kutoa elimu kwa vijana hao kujikita katika kilimo kwa manufaa yao ya badae . 


Katika hatua nyingne bwana Agape amesema kuwa  zaidi ya miti elfu kumi ya matunda itazalishwa na shirika hilo na zoezi hilo litaanza tarehe mbili mwezi wa kumi katika kata ya Bugorola ili kuwapa fursa vijana pamoja na wananchi wa Missenyi kuwa na elimu juu ya utunzaji mazingira pamoja na kuwa na utamaduni wa kupanada miti  katika maeneo yaliyowazunguka.


Kwa upande wake mkurugenzi wa shirika hilo bwana  Josephat Joseph John amesema  kuwa kwa sasa hivi shirika ilo lina mradi unaoitwa AGRI EXPERIENCE  ambapo mradi huo utawawezesha  vijana wengi kujifunza na  kujua namna ya kufuga kuku wa kisasa pamoja na kufahamu ujuzi mbalimbali wa biashara ya mayai ya kisasa, ufugaji wa nyuki nk.

Bwana Josephat amesema  kuwa vijana watumie shirika hilo vizuri kwa  kuwa elimu itatolewa bila malipo yoyote na ku ongeza kuwa kabla yakuondoka mkoani hapa vijana wawe wameisha pata maarifa na ujuzi wa kujiajili wenyewe kupitia kilimo na ufugaji wa kisasa uku akitaja kauli mbiu yao kuwa ni “Kijana wa kagera kulima kwa tija kwa maendeleo yao wenyewe na taifa kwa ujumla 2020-2025”.





Share:

Serikali Kusimamisha Mishahara Ya Maafisa Utumishi Watakaosababisha Watumishi Kutolipwa Mishahara

 Na. James Mwanamyoto-Dodoma
Maafisa Utumishi watakaozembea na kusababisha Watumishi wa Umma nchini kutolipwa mishahara yao kwa wakati, watasimamishiwa mishahara na Serikali mpaka watakapohakikisha watumishi hao wamelipwa mishahara yao.

Hayo yamesemwa jana na Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Francis Michael wakati akifungua mafunzo ya wiki mbili ya Mfumo Mpya wa Kitanzania wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara kwa kundi la pili la Maafisa Utumishi na Maafisa Tawala 140 kutoka mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Mara, Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Pwani, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Kigoma na Tabora yanayofanyika jijini Dodoma katika Ukumbi wa VETA.

DKt. Michael amesema, kuna tatizo katika baadhi ya Taasisi za Umma kwani wapo Maafisa Utumishi wanajifanya miungu watu wakati wajibu wao ni kumtengenezea mazingira mazuri ya kikazi mtumishi ili ajisikie yuko sehemu salama na aweze kutekeleza ipasavyo jukumu la kuwahudumia wananchi.

“Msiwafanye watumishi mnaowasimamia kuona sehemu ya kazi kama jehanamu, hivyo mbadilike kwani Serikali haitomvumilia yeyote atakaye kinzana na azma yake ya kuboresha huduma kwa wananchi”, Dkt. Michael alisisitiza.
Ameongeza kuwa, ni lazima Maafisa Utumishi wabadilike kwa kuwajengea mazingira Watumishi wa Umma kuipenda Serikali yao kwasababu inawajali na kuthamini mchango wao katika maendeleo ya taifa.

Dkt. Michael amefafanua kuwa, Serikali inamhakikishia mtumishi usalama wa ajira yake tofauti na sekta binafsi, hivyo hakuna Afisa Utumishi atakayevumiliwa pindi akisababisha Serikali kulaumiwa na Watumishi wa Umma au Wananchi.

Naye, Mkuu wa Idara ya Utawala na Utumishi, Halmashauri ya Wilaya ya Liwale Bw. Boniface B. Chatila kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo, ameahidi kuwa, wakirejea katika maeneo yao ya kazi watahakikisha wanatekeleza majukumu yao kikamilifu ili kuondoa kero ya Watumishi wa Umma kufuata huduma Ofisi ya Rais Utumishi Dodoma, huduma ambazo wanastahili kupewa katika maeneo yao ya kazi.

Aidha, Bw. Chatila amemhakikishia Dkt. Michael kuwa, ujuzi watakaoupata kupitia mafunzo ya Mfumo Mpya wa Kitanzania wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara watautumia ipasavyo kuongeza ufanisi kiutendaji ili kuboresha utoaji huduma kwa umma.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini, ACP Ibrahim Mahumi amesema, suala la mtumishi kukosa mshahara hivi sasa linachukuliwa kama ni kosa kubwa hivyo Afisa Utumishi atakayebainika atasimamishiwa mshahara ikiwa ni hatua ya awali na atachukuliwa hatua za kinidhamu ikizingatiwa kuwa, mfumo mpya utaonesha uzembe wa afisa huyo.

Mfumo Mpya wa Kitanzania wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara utaanza kutumika rasmi Mwezi Novemba, 2020 mara baada ya kukamilika kwa mafunzo ya makundi yote ya Maafisa Utumishi na Maafisa Tawala ambao ndio wenye jukumu la kuutumia mfumo huo kiutendaji.


Share:

Sumaye aishukia CHADEMA, asema hawawezi kuongoza nchi


Na John Walter-Hydom, Mbulu
Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Frederick Sumaye amesema vyama vya Upinzani nchini haviwezi kuongoza nchi kwa sababu hawana sera.

Ameyasema hayo Leo septemba 30,2020 akizungumza na wananchi wa Jimbo la Mbulu Vijijini katika mkutano wa Mgombea Mwenza Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia  Suluhu Hassan kunadi Sera za  Chama cha Mapinduzi katika viwanja Vya Haydom.

Sumaye amesema Chama alichotoka  CHADEMA,  ni Chama cha Uwana harakati na hakina sera  zozote za kuwasaidia wananchi.

'CHADEMA wanafikiri kuwa nchi ya Tanzania bado ipo  mikononi mwa  Wakoloni, wanapiga kelele utafikiri bado tunatawaliwa' alisema Sumaye

'Nilienda kule  lakini baada ya kugundua hawana chochote nikaamua kurejea nyumbani' alisisitiza Sumaye

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Manyara Simon Lulu amesema Chama hicho kinajiandaa kwa ushindi wa kishindo kwa sababu kimefanya maendeleo kwa wananchi.

Amemweleza Mgombea Mwenza kiti  cha Urais Tanzania Samia Suluhu Hassan kwamba katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika oktoba 28 mwaka huu, Upinzani mkoani hapo hawataambulia hata kiti  cha Udiwani.


Share:

Wahamiaji Haramu 32 Wakamatwa Wilayani Pangani

 ASKARI wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wilayani Pangani wamefanikiwa kuwakamata wahamiaji haramu 32 waliokutwa wakiwa karibu na hifadhi hiyo wakisafirishwa kupelekwa nchi za kusini mwa Afrika.
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kukamatwa kwa wahamiaji hao Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani Grace Lobora alisema kwamba wahamiaji hao walikamatwa Septemba 27 mwaka huu usiku.

Alisema ukamatwa huo waliofanya baada ya kupata taarifa kutoka wananchi wa Kijiji cha Buyuni kupitia Mwenyekiti wa Kijiji hicho Diwani Akida ambaye aliwaeleza uwepo wa mazingira yasiyoridhisha kwenye eneo lake hasa eneo la bahari baada ya boti moja kukwama.

Alisema baada ya kupata taarifa hiyo wao kama wahifadhi wana jukumu la kulinda maliasili na kuangalia usalama kwenye miji yote inayowazunguka waliandaa kikosi kazi cha kwanza waliokwenda eneo la tukio na walipofika waliwakuta wahamiaji hao eneo la bahari karibu na hifadhi hiyo katika kijiji cha Buyuni.

Alisema baadae hapo waliamua kutuma kikosi cha pili na ndipo walipofika na kufanikiwa kukaweka chini ya ulinzi wahamiaji 28 ambao ni raia wa Ethiopia lakini alfarji  wakapata taarifa nyingine ya uwepo wa wahamiaji wengine wanne ambao ni raia wa Somalia na wakatuma kikosi na kufanikiwa kuwaweka chini ya ulinzi.

“Kati yao wapo wahamiaji 32 raia wa Ethiopia 28 na raia wa Somalia wanne akiwemo mwanamke mmoja kwa hiyo baada ya kufanikisha tukio hilo tumewafikisha na kuwakabidhi kwenye mamlaka ya Polisi kwa ajili ya hatua zaidi”Alisema

Awali akizungumza kuhusiana na tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Blasius Chatanda aliwapongeza askari wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani kwa kazi nzuri kwa kushirikiana na askari wa Jeshi la Polisi wilaya ya Pangani.

Hata hivyo amesema kwamba hivi sasa wametangaza vita mpya kwa mawakala wanaojishuhulisha na usafirishaji wa wahamiaji haramu mkoani Tanga kwamba hawatasalimika watasakwa popote iwe ni nchi kavu, majini na kisha kufikishwa mahakamani.


 


Share:

Tundu Lissu adai bado hajapokea wito wa malalamiko

Mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, amesema kuwa hadi sasa bado hajapokea wito wala malalamiko yoyote kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kama taarifa ya tume hiyo ilivyoeleza hapo jana.

Lissu ametoa kauli hiyo hii leo Septemba 30, 2020, wakati akizungumza na waandishi wa habari mkoani Arusha, na na kusisitiza kuwa kwa sababu hana wito wowote yeye ataendelea na ratiba zake za kampeni kama ilivyo kwenye ratiba.

Jana Septemba 29, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC Dkt. Wilson Mahera alitoa taarifa ya kuthibitisha kumuandikia barua ya wito Tundu Lissu, kufuatia tuhuma mbalimbali anazodaiwa kuzitoa kati ya Septemba 25 na 26 mjini Musoma



Share:

Armenia yakataa upatanishi wa Urusi katika mzozo na Azerbaijan Huku Mapigano Yakizidi Kupamba Moto

Armenia Jumatano imekataa pendekezo la Urusi la kutaka kuwa mpatanishi katika mazungumzo ya amani na hasimu wake mkubwa Azerbaijan, huku mapigano yakiwa yanaendelea kupamba moto kwa siku ya nne katika jimbo linalotaka kujitenga la Nagorno Karabakh.

Waziri mkuu  wa  Armenia Nikol Pashinyan amesema haitakuwa sahihi kufanya mazungumzo ya  amani  na Azerbaijan chini ya upatanishi wa  Urusi, wakati mapigano ya kuwania udhibiti wa jimbo yakiwa yanaendelea.

"Sio sahihi kabisa kuzungumzia kuhusu mkutano kati ya  Armenia, Azerbaijan na Urusi  katika wakati wa uhasama mkubwa," amesema Pashinyan wakati akizungumza na shirika la habari la Urusi Interfax.

Ameongeza kuwa hali endelevu na mazingira yanahitajika kwa ajili ya mazungumzo hayo.

Vyombo vya habari nchini Urusi vimeripoti Jumatano kuwa waziri mkuu Pashinya amesema Armenia  haifikirii kuweka walinzi wa amani katika jimbo la Nagorno-Karabakh.

Kwa miaka kadgaa, vikosi vya Armenia na Azabajani vimekuwa vikizozania jimbo hilo la Karabakh, ambalo liliamua kutaka kujitenga na Azabajani baada ya kuanguka kwa Umoja wa Kisovieeti katika miaka ya 1990.

Mzozo huo wa muda mrefu uliibuka tena Jumapili huku pande hizo mbili zikirushiana silaha nzito za moto na kulaumiana kwa kuzuka kwa vurugu.

Karibu watu 100 wamethibitishwa kufa katika mapigano hayo ya hivi karibuni na pande zote mbili zinadai kuwa zimesababisha hasara kubwa kwa vikosi vya wapinzani.

 

DW



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger