Tuesday, 14 July 2020

Godbless Lema 'Atamba' Kushinda Ubunge Arusha Mjini....."Natamani Wawe 30 ili Nishindane Nao"

Mbunge wa Arusha Mjini anayemaliza muda wake,  Godbless Lema amesema sheria ingeruhusu, angetaka wagombea wote wa CCM Arusha ashindane nao.

 
“Nime sikia sikia majina ya wagombea Ubunge Arusha Mjini kupitia ccm.Kama sheria ingeruhusu wote 30 kushindana nami na picha zao wote kutokea kwenye karatasi ya kura dhidi yangu,bado wangeimba wimbo walio imba 2010/2015.Twendeni mpaka mwanzo wa bahari,wepesi sana hawa.” ameandika Lema kwenye ukurasa wake wa twitter.

Leo, CCM imefungua pazia kwa wanachama wake kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea nafasi hiyo, zoezi hilo linatarajiwa kusitishwa tarehe 17 Julai 2020.


Share:

Mtoto wa Lowassa Achukua Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Monduli

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Monduli, Langael Akyoo, leo Jumanne July 14,2020 amemkabidhi Fredrick Lowassa fomu ya kuomba ridhaa ya Chama hicho ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Monduli. Fredrick ni Mtoto wa Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa.


Share:

Angela Kairuki Achukua Fomu Ya Ubunge Same Magharibi

Waziri wa Uwekezaji, Angellah Jasmine KAIRUKI akichukua Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Same Magharibi kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi leo Julai 14 , 2020. 

Anayemkabidhi fomu hiyo ni Katibu wa CCM Wilaya ya Same Victoria Mahembe.


Share:

MTOTO WA MUUZA KAHAWA 'HASSAN FATIU' ACHUKUA FOMU KUNYAKUA UBUNGE SHINYANGA MJINI

Wakili  Hassan Athuman Fatiu maarufu 'Mtoto wa Muuza Kahawa' akionesha fomu ya Kuomba Kugombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo Jumanne Julai 14,2020 katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini. 

Akizungumza baada ya kuchukua fomu, Hassan Athuman Fatiu ambaye ni Wakili na Mkulima wa mpunga, mkazi wa kata ya Kitangili amesema endapo chama chake kitampa ridhaa ya kugombea ubunge jimbo la Shinyanga kipaumbele chake kikubwa ni Ilani ya Uchaguzi ya CCM na vipaumbele binafsi vitakavyofikishwa katika ofisi ya mbunge. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

PICHA: Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Yahamia Dodoma

Murugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Dk. Wilson Mahera (kushoto) akizungumza na watumishi wa NEC ambao wamehamia Ofisi mpya za Makao Makuu ya Ofisi hiyo yaliyopo Njedengwa Jijini Dodoma jana. Awamu ya kwanza ya watumishi wa NEC wamehamia Dodoma wiki hii. (Picha na NEC).



Share:

Naibu Waziri wa Ardhi Dkt.Angelina Mabula naye ajitosa rasmi kugombea ubunge tena

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ilemela Dkt.Angelina Mabula leo amechukua fomu ya kutetea kiti chake cha ubunge katika ofisi ya Chama cha CCM wilaya ya Ilemela


Share:

Naibu Spika Tulia achukua fomu kuwania ubunge Mbeya Mjini Kupitia CCM

Naibu Spika Dkt.Tulia Ackson amechukua fomu ya kuwania nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Mbeya mjini kupitia tiketi ya CCM


Dkt.Tulia amechukua fomu hiyo katika ofisi za CCM Wilaya akisindikizwa na Mume wake James Andilile Mwainyekule.


Share:

Askofu Gwajima Achukua Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Kawe Kupitia CCM

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea ubunge Jimbo la Kawe kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi. Jimbo hilo lilikuwa linaongozwa na Halima Mdee (Chadema).

“Kwa sasa itoshe tu kwamba nimechukua fomu,” amesema Askofu Gwajima muda mfupi baada ya kuchukua fomu.

Kwenye foleni hiyo, alikuwemo Abbas Tarimba, aliyekuwa kiongozi katika Timu ya Mpira ya Yanga na Diwani wa Kata ya Hananasifu ambaye anaomba ridhaa ya kugombea Jimbo la Kinondoni.

Mbunge anayemaliza muda wake kwenye jimbo hilo ni, Maulid Mtulia wa CCM. 



Share:

Mrisho Gambo Achukua fomu za kugombea ubunge katika jimbo la Arusha Mjini

Aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, leo amechukua fomu za kugombea ubunge katika jimbo la Arusha Mjini, kupitia chama cha Mapinduzi


Share:

BANDORA MILAMBO AJITOSA KINYANG'ANYIRO CHA UBUNGE JIMBO LA SHINYANGA MJINI


Mfanyabiashara Bandora Salum Milambo mkazi wa Ngokolo Manispaa ya Shinyanga akionesha fomu ya kuomba kugombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kuchukua katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini leo Jumanne Julai 14,2020. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

GRACE ANTHONY LYON ACHUKUA FOMU KUGOMBEA UBUNGE SHINYANGA MJINI

Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Grace Anthony Lyon mkazi wa Majengo Mapya Manispaa ya Shinyanga akionesha fomu ya kuomba kugombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kuchukua katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini leo Jumanne Julai 14,2020. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

Associate Reporting Officer Job vacancy at UNV

Eligibility criteriaMinimum age: 25 years old. Nationals of the country of assignment are not eligible, except the assignments in Headquarters duty stations. Description of taskWithin the delegated authority and under the supervision of the Senior Programme Officer or his/her designated mandated representative(s), the UNV Associate Reporting Officer will: Keep abreast of all developments in the […]

The post Associate Reporting Officer Job vacancy at UNV appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MUSA NGANGALA AJITOSA KUWANIA UBUNGE SHINYANGA MJINI

Musa Jonas Ngangala akionesha fomu ya kuomba kugombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
*****
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Musa Jonas Ngangala amechukua fomu ya kuomba kugombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Musa Jonas amewasili katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Mjini leo Jumanne Julai 14,2020 majira ya saa tatu na kuchukua fomu ya kuomba  kugombea ubunge katika Jimbo la Shinyanga.

Akizungumza baada ya kuchukua fomu, Musa Jonas Ngangala ambaye ni mkazi wa Mtaa wa Imalilo kata ya Kitangili katika Manispaa ya Shinyanga mwenye Elimu ya Shahada ya Mipango Miji na Maendeleo amesema endapo chama chake kitampa ridhaa ya kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini atahakikisha anasimamia na kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM kikamilifu ikiwa ni pamoja na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi.

"Nimechukua fomu ili kuomba ridhaa chama changu kinipatie nafasi ya kwenda kuwatumikia wananchi,naamini chama changu kikinipitisha kugombea Ubunge nitakuwa mwakilishi mzuri wa wananchi katika kutatua kero za wananchi na kutekeleza miradi mbalimbali kwa ajili ya maendeleo ya wananchi",amesema Ngangala.
Musa Jonas Ngangala akinawa mikono baada ya kuwasili katika ofisi cha CCM wilaya ya Shinyanga Mjini kuchukua fomu ya kuomba kugombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Share:

Maswali 15 Yanayoulizwa Mara kwa Mara Kwenye Usaili ( Interviews ) na Namna ya Kuyajibu

Usaili wa ajira (interviews) husababisha hofu na msongo wa mawazo kwa vijana wengi kabla au baada ya kutoka chumba cha usaili.

Tatizo hilo hutokana na hofu inayojenga wakati wa kujibu maswali unayoulizwa  na watu ambao wamekuzunguka wakati wa kufanyiwa usaili.

Njia moja ya kuzuia hii kutokea ni kufuatilia mfumo wa kujibu maswali.

Ifuatayo ni orodha yetu ya maswali 15 yanayoulizwa mara kwa mara kwenye interviews( Usaili) na namna ya kuyajibu;

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬ 

1.Jitambulishe(Wewe ni Nani?)
Mara nyingi hili ni swali ambalo mtahiniwa huulizwa mara tu aingiapo kwenye chumba cha usaili. Kwa bahati mbaya watahiniwa wengi hudhani kuwa waajiri hutamani kujua majina yao. Hapana, majina yako wanayafahamu na pengine hata taarifa za ziada. Katika swali hili waajiri uhitaji kujua sifa zako zihusianazo na ajira zitakazo dhihirisha kuwa wewe ni mtu sahihi.

Mfano mtu anaweza kujibu hivi, “Jina langu ni Mti Mkavu, ni Mhitimu wa Shahada ya Masoko ya Chuo Kikuu Dodoma. Ni mtu makini, mbunifu, mchapa kazi na ninayependa watu. Pamoja na hayo ninao ujuzi usio na shaka kwenye masuala ya mawasiliano. Uwezo wangu unadhihirishwa na mrejesho ambao huwa na upata kwa kila mtu ninaye fanya naye kazi”.

Katika swali hili ni muhimu kujua kuwa halihitaji wewe kuzungumzia mambo yasiyo husiana na kazi na ajira. Kwenu mpo wa ngapi,jina la mama yako, mkoa unaotoka, kabila, kazi ya baba au mama yako havihitajiki katika taarifa unazotakiwa. 


2.Kwanini upewe ajira kwetu? | au unaweza ukaulizwa Kwa nini unahisi wewe ni mtu sahihi kwa kazi hii na siyo mwingine?

Kumbuka kuwa usaili wa kazi unahusisha ushindani hivyo swali hili linataka uoneshe utofauti ulionao. Katika kujibu swali hili zingatia mahitaji ya kazi husika kujenga hoja kwani hata kama una utofauti wa aina gani kama hautasaidia katika kufikia  malengo ya taasisi bado itakuwa ni kazi bure.

Mfano, “ Siyo kwamba mimi ni mchapakazi na mbobezi katika uhasibu pekee lakini pia ni mtu ambaye ninaweza kufanya shughuli zangu bila kusimamiwa. Mimi ni mtu wa matokeo hivyo kwa kila ambacho hufanya hulenga kutimiza malengo kwa wakati na kufikia viwango stahiki. 


"Ubora wangu unathibitishwa na tuzo kadhaa nilizowahi kupata ikiwemo mfanyakazi bora wa mwezi mara nne nilipokuwa nikifanya kazi na na Magogo Media. Hii inathibitisha kuwa mkinipa fursa hii hamtakuwa mnajaribu bali mtakuwa mnafanya maamuzi sahihi”.

3.Unajua nini kuhusu sisi?
Siku zote maandalizi ya usaili yanaenda sambamba na kutafuta taarifa sahihi za taasisi husika. Hivyo ni vyema kuhakikisha kuwa taarifa unazotoa hapa ni sahihi na muhimu katika kudhirisha kuwa ulishafanya utafiti wa kutosha kuhusu taasisi husika.

Mfano, “ Benki yenu ilianzishwa mwaka 1987 ina maono ya kuwa benki bora kuliko zote nchini kwa kutoa huduma za kifedha zinazo aminika na kufikia maeneo mengi nchini. Kwa sasa benki yenu ina matawi 700 na ATMs 500 huku ikiwa na mpango wa kufungua matawi mengine Kigoma hivi karibuni. 


Endapo mtanipa fursa ya kufanya kazi na nyinyi nitahakikisha natumia vyema uwezo wangu katika masuala ya masoko ili kuongeza wateja na kuhaikisha huduma bora mnayotoa inafahamika kwa watu wengi.”

4. Ni vitu gani unavyojivunia?
Katika swali hili waajiri huhitaji kujua mambo kadhaa ambayo unayaona kama mtaji mkubwa katika utendaji kazi. Ni vyema kukumbuka kuwa mambo utakayo yataja hapa ni yale yenye umuhimu katika kuongeza ufanisi au ubora katika kazi husika kwani kila kazi inamahitaji yake ya tofauti na kazi nyingine.

Kwa mfano, “mambo makuu mawili ninayojivunia ni ujuzi na uwezo katika huduma kwa wateja na kujisimamia katika majukumu yangu. Kila ninapowahudumia wateja huwa napokea mrejesho chanya juu ya namna wanavyoridhishwa na huduma yangu hivyo kutamani kuhudumiwa nami tena.


Hii hunifanya nijione kuwa mtu muhimu sana katika taasisi yoyote ninayofanya nayo kazi. Pia, uwezo wangu katika kufanya shughuli bila kusimamiwa au chini ya usimamizi mdogo unanifanya niwe mtu wa kuaminiwa na kutegemewa katika kufanya shughuli zangu.Haya ni baadhi ya mambo mengi yanayonifanya mimi kuwa mtu wa tofauti. Nina amini hamtaacha fursa ya kufanya kazi nami”
 

5.Udhaifu wako ni upi?
Hili ni moja ya maswali ambayo watainiwa wengi huyachukia na kuyaona kama yana lengo la kuwatafutia sababu za kuwanyima kazi. Wengine kwa lengo la kuonesha ukamilifu huthubu kusema kuwa hawana udhaifu wowote-usithubutu kusema hivyo. Kila mtu ana udhaifu wake kwani hakuna aliye mkamilifu.

Suala la msingi ni kujua namna ya kujibu suali hili. Mambo ya kuzingatia ni pamoja na kuchagua udhaifu ambao hauta athiri utendaji wako na pili hakikisha udhaifu huo unahusiana na ujuzi na sio tabia. 


Ujuzi ni rahisi kuutafuata lakini kubadilisha tabia ni ngumu zaidi hivyo usiseme kuwa wewe ni mvivu,mdokozi, na mengineyo ya kitabia. Na unapotaja udhaifu wowote kumbuka kuonesha jitihada ambazo umeshazifanya ili kudhibiti udhaifu huo.

Kwa mfano, kwa kazi ya uhasibu mtu anaweza sema, “Udhaifu nilio nao ni masuala ya ‘graphic designing’ niligundua hili nilipohitaji kuandaa tangazo kwa ajili ya ofisi niliyokuwa nikifanya nayo kazi. Hata hivyo, nimeanza kujifunza mwenyewe kupitia mtandao wa internet na naona napata mabadiliko chanya kila leo”.

Kwa jibu hili ni dhahiri kabisa graphic designing siyo mahitaji muhimu ya kazi ya uhasibu hivyo haita athiti utendaji wa kazi.


6. Kwa nini uliacha kazi yako ya mwanzo?
Hapa unahitajikua makini sana, kumbuka na epuka kuzungumza vibaya kuhusu muajiri yeyote kabla au sasa au uwezo wa muajiri. 


Hapa unaweza ukawajibu tu kwamba;" Kwa sababu ya kuboresha na kuongeza ujuzi, pia natafuta fursa bora zaidi."

7.Unatarajia kupata nini kutokana na kufanya kazi hapa? au unaweza ukaulizwa | Baada ya miaka mitatu wewe mwenyewe utakua wapi?
Ongelea unachotumaini kutimiza ila kuwa mkweli. Pia usiongee kwa ujumla. Chagua kitu maalum ambalo ni muhimu kwa kampuni alafu ilenge. Ila, uwe wazi kwa kusema itachukua muda kujifunza zaidi kuhusu kampuni ili kufanikiwa zaidi.

Kwa mfano; “Nikiwa mwalimu wa kiingereza, lengo langu ni kuongeza asilimia ya wanafunzi wanaofaulu mtihani wa taifa kuwa 85% ya darasa yangu. Najua itachukua muda kujua vizuri changamoto za wanafunzi ila, naamini nitafanikiwa”


Ni vizuri kusema kwamba unatumaini kuona uwajibikaji zaidi  katika kampuni hiyo na kuongeza thamani katika kampuni kwa mchango wako. 

8.Kwanini umekaa muda mrefu bila kupata ajira?

Wajibu kwamba; "Nilikuwa najiendeleza katika taaluma yangu "


9. Eleza namna unavyoweza kujisimamia mwenyewe
Wajibu kwamba: Nitakuwa nafanya kazi niliyopewa nikishirkiana na wasimamizi wangu na viongozi juu ya namna ya kumaliza kazi kabla ya muda uliopangwa.


10. Kitu gani kinakukera miongoni mwa wafanyakazi wenzako?

Wajibu kwamba; "Naamini katika kufanya kazi kwa pamoja. Hata kama nikikerwa na kitu chochote, huwa najaribu kuepuka isipokuwa kama ni kitu cha binafsi."

11.Unategemea kufanya kazi kwa muda gani kama ukipewa ajira?

Wajibu:Kwa muda mrefu kama nitaendelea kuongeza kitu katika taaluma yangu.

12:Je, mwenyewe unajiona kufanikiwa?

Wajibu: Ndio, ukiachana na uwezo wa taaluma yangu, nadhani nimepata watu sahihi wa kufanya nao kazi.

13. Uwezo wako ni upi katika kazi?
Wajibu: Mimi huwa naelewa na kufundishika kwa haraka na ni mchapakazi wa kweli.

14,Unapenda nafasi au cheo gani katika timu unayofanya nayo kazi?
Wajibu: Haijalishi hadi nitakapojifunza kitu kipya kwa kila mradi au kazi.

15.Je, unaswali lolote kwetu? 

Mwishoni wa interview, ni kawaida kwa mwajiri kuuliza kama una maswali kwao. Ukipewa nafasi hii, usiulizie mshaara na faida zingine. Badala yake, uliza:
  1.     Maadili ya kampuni
  2.     Aina ya uongozi
  3.     Wafanyakazi wenzako
  4.     Chochote ambacho hukuelewa kuhusu kazi hiyo.
  5.     Watakupa jibu baada ya muda gani?
==>>USIFANYE HAYA MAKOSA KATIKA SWALI HILO:
- Je, kuna fursa ya kukua / kupandishwa ngazi?
- Nitapata siku ngapi za likizo?

- waajiliwa wanafaidika vipi na kampuni hii. 

==>Tiba bora ya msongo wa interview ni kujiandaa
Ingawa interview inaweza ikakupa misongo mingi, ukijiandaa vizuri Utashangazwa na mafanikio yako.

Interview ni nafasi yako ya mwisho kumvutia mwajiri, na vidokezo vilivyoelezwa hapo juu vitakusaidia na hilo.

Kumbuka, hamna haja ya kuwa na wasiwasi ukiwa umejiandaa. 


Nakutakia Mafanikio mema kwenye Interview
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

👉Sasa, kwa kuwa umeshajua jinsi ya kujibu vizuri maswali ya Interview, anza kutafuta kazi unayoitaka kwa kubofya hapo chini. 


Hilo ni Jukwaa Maalumu la Ajira zote za Serikali, Makampuni Binafsi n.k. Kuna Nafasi za Kazi zaidi ya 7000 kwa ajili yako.

👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
http://ajirazote.com/jobs


▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬


Share:

Evaluation and Learning Specialist – S/A & Participation Job vacancy at VSO Tanzania

At VSO we believe progress is only possible by working together. Whether you want to join us as an employee, or as a volunteer working in your own country, overseas or online, our selection process includes an assessment based on these core competencies: * Ability to be open minded and respectful * Ability to be […]

The post Evaluation and Learning Specialist – S/A & Participation Job vacancy at VSO Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 14,2020





\














Share:

WCF YATWAA TUZO YA MSHINDI WAKWANZA KUNDI LA TAASISI ZA BIMA NA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII MAONESHO YA 44 YA SABASABA



Waziri wa Viwanda na Biashara, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Balozi Amina Sa;lum Ali (kushoto), akimkabidhi tuzo Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Masha Mshomba, baada ya kuibuka mshindi wa muoneshaji bora kundi la Taasisi za bima na hifadhi ya jamii, katika maonesho ya 44 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam yaliyofikia kilele leo Julai 13, 2020 katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Bw. Mshomba akionyesha tuzo hiyo mbele ya banda la WCF viwanja vya Julius Nyerere, maarufu Sabasaba mara baada ya kukabidhiwa.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Masha Mshomba akiungana na wafanyakazi wa Mfuko waliokuwa wakihudumia wananachi waliotembeela banda hilo wakati wakisherehekea ushindi huo.
Bw. Mshomba katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Mfuko, wakiwa na tuzo hiyo.
Bw. Mshomba akiwashukuru wafanyakazi wake waliokuwa wakihudumia wananchi katika banda hilo kwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo na kwa weledi.
***

MFUKO wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) umetwaa tuzo ya mshindi wa kwanza ya muoneshaji bora kundi la Taasisi za Bima na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwenye maonesho ya 44 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba amepokea tuzo hiyo kutoka kwa Waziri wa Viwanda na Biashara wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Amina Salum Ali wakati wa kilele cha maonesho hayo yaliyofanyika kwenye viwanja vya Julius Nyerere maarufu Sabasaba jijini Dar es Salaam leo Julai 13, 2020.

“Kusema kweli siku ya leo tunayo furaha sana mimi mwenyewe na wafanyakazi wenzangu wote, kwa mara ya kwanza tumeweza kushika nafasi ya kwanza katika sekta ya bima na mifuko ya hifadhi ya jamii, hii inadhihirisha kwamba penye nia pana njia, mwaka jana tulikuwa washindi wapili tukaweka azma kwamba walau siku moja tuwe washindi wakwanza na leo imefika tunashukuru sana.” Alisema Bw. Mshomba na kuongeza….

Ushindi huu unaendana na vision ya Mfuko, tumejiwekea malengo ya kuwa taasisi ya kuigwa sio tu hapa Tanzania lakini Afrika hususan katika taasisi za hifadhi ya jamii na haswa katika Mifuko ya Fiadia na tunapokuwa wakwanza katika maonesho haya makubwa hapa nchini hiyo inaonyesha kwamba tumko katika njia sahihi na lengo letu ni kuendelea kushika nafasi kama hizi katika maonesho na shughuli mbalimbali tunazoshiriki.

“Huduma zetu ni bora tumeboresha sana huduma zetu na kwa sasa zinapatikana kupitia mtandao (online portal) na waliofika katika banda hili wameelezea jinsi walivyovutiwa na huduma zetu zote zinapatikana kupitia mtandao na ule usumbufu kwa wateja haupo kabisa kwa sababu Mafao yanalipwa kupitia mtandao, lakini hata taarifa za kutokea ajali au kuumia kazini zinawasilishwa kupitia mtandao, usajili wa waajiri na wanachama wenyewe ni kupitia mtandaoni, , kitu kwa sasa tunafanya kupitia mtandao, usajili wa waajiri ni kupitia mtandao, ukusanyaji wa michango ni kupitia mtandaoni kwahivyo kila kitu tunafanya kwa kutumia mtandao na hilo kwakweli limewezesha kuboreshwa kwa shughuli zetu na nia yetu kwakweli ni kuwa kileleni.” Alifafanua Bw. Mshomba.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger