Tuesday, 21 January 2020

Aston Villa Yatangaza Rasmi Kumsajili Mbwana Samatta.

Klabu ya Aston Villa ya England, imetangaza kumsajili mshambuliaji wa kimataifa kutoka Tanzania Mbwana Samatta. 

Usajili wa Mbwana Samatta unatarajiwa kuimarisha safu ya mashambulizi ya timu ya Aston Villa ambayo imekuwa ikilegalega katika ligi ya Premier.

Aston Villa imecheza mechi zake tatu zilizopita bila mshambuliaji wa kutambuliwa baada ya mshambuliaji wao raia wa Brazil Wesley Moraes kujeruhiwa hivyo kutoweza kucheza tena msimu huu. 

Samatta aliyekuwa akiichezea klabu ya Genk nchini Ubelgiji, amefunga mabao kumi katika mechi zote likiwemo bao alofunga dhidi ya Liverpoool katika ligi ya Mabingwa uwanjani Anfield

Yeye ndiye mchezaji wa kwanza kutoka Tanzania kuwahi kusajiliwa na timu katika ligi ya Premier.


Share:

Naibu Waziri Mabula Azitaka Halmashauri Kupanga Miji Kuepuka Migogoro

Na Munir Shemweta, WANMM KIGOMA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amezitaka Halmashauri nchini kuhakikisha zinapanga, kupima na kumilikisha ardhi ili kuepuka migogoro ya ardhi pamoja na kuongeza mapato ya serikali kupitia kodi ya pango la ardhi.

Dkt Mabula alitoa agizo hilo jana mkoani Kigoma wakati akizungumza na watumishi wa sekta ya ardhi wa halmashauri nane za mkoa huo akiwa katika ziara yake ya kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi. Halmashauri hizo ni Buhigwe, Kasulu DC, Kasulu TC, Kakonko, Kibondo, Kigoma DC, Kigoma MC, na Uvinza DC.

Alisema, wakurugenzi wa halmashauri wanapaswa kutambua kuwa wana jukumu la kusimsmia halmashauri zao ili ziwe na miji yenye mpangilio mzuri ambapo alibainisha kuwa kama maeneo ya miji hiyo yataachwa bila kupangwa, kupimwa na kumilikishwa basi yatakuwa hovyo na maeneo mengi kuingia kwenye zoezi la urasimishaji.

‘’ Halmashauri zote nchini jukumu la kupanga miji ni la kwenu Wizara itasimamia nidhamu na ajira na mkizubaa katika hili miji itaendelea kuwa mibaya na serikali haitaki kuona ujenzi holela ukiendelea’’ alisema Naibu Waziri Mabula.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, urasimishaji unaofanyika sasa katika maeneo mbalimbali umesababishwa na kasi ndogo ya upangaji miji unaofanywa na halmashauri na kinachofanyika katika zoezi hilo ni huruma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa wananchi na kubainisha kuwa mwisho wa zoezi la urasimishaji ni mwaka 2023.

Alisema, hata idadi ndogo ya hati zilizotolewa katika halmashauri za mkoa wa Kigoma ni ishara ya kasi ndogo ya upangaji na upimaji katika mkoa wa Kigoma ambapo Naibu Waziri Mabula alishangazwa na halmashauri za Kigoma DC na Kasulu DC kwa kushindwa kutoa hata hati moja katika kipindi cha nusu mwaka huku halmashauri ya Buhigwe ikitoa hati sita tu na hivyo kuutaka mkoa kuhakikisha unazisimamia halmashauri hizo ili ziweze kupanga, kupima na kumilikisha maeneo mengi zaidi.

Kuhusu suala la mapato ya kodi yataokanayo na ardhi, Naibu Waziri Mabula ameoneshwa kutofurahishwa na kasi ya ukusanyaji mapato katika mkoa wa Kigoma ambapo kwa kipindi cha nusu mwaka 2019/2020 halmashauri za mkoa huo zimekusanya shilingi milioni 312,233,500.9 sawa na asilimia 13 tu huku Kigoma DC na Kasulu DC zikiwa zimekusanya mapato ya ardhi chini ya asilimia 1.2 na halmashauri pekee iliyofanya vizuri ni Kakonko iliyokusanya milioni 17,281,142.59 sawa na aslimia 28.

‘’Kama taasisi nyingine za serikali kama TRA zingekuwa hazikusanyi kodi kama ulivyo mkoa wa Kigoma katika suala la ardhi ambapo mna asilimia 13 tu basi miradi mikubwa inayofanywa kwa kutumia kodi za ndani ingekwama’’ alisema Dkt Mabula.

Awali Afisa Ardhi wa mkoa wa Kigoma Jairo Pilla katika taarifa yake ya nusu mwaka 2019/2020 ya utendaji kazi wa sekta ya ardhi katika mkoa wa Kigoma alisema, kiwango kidogo cha kodi ya ardhi kilichokusanywa kwenye mkoa wake kimesababishwa na sehemu kubwa ya ardhi kwenye mkoa huo kutopimwa na kumilikishwa.

Aidha, alisema suala lingine lilichongia mapato kidogo ya ardhi ni idara ya ardhi kutopewa kipaumbele na halmashauri za mkoa huo ambapo hakuna bajeti inayotengwa kwa ajili ya kupanga na kupima maeneo na kitu pekee kinachofanyika ni zoezi la urasimishaji na kusisitiza michoro mingi inayowasilishwa ni ya urasimishaji tu.


Share:

NHC Yakusanya Milioni 618.2 Kigoma

Na Munir Shemweta, WANMM KIGOMA
Shirika la Nyumba la Taifa mkoa wa Kigoma limekusanya kiasi cha shilingi 618,246,592 sawa na asilimia 70 ya makusanyo ya mwaka ambapo matarajio ya shirika hilo ilikuwa kukusanya asilimia 50 kufikia Desemba 2019.

Akitoa taarifa ya makusanyo ya kodi kwa miradi ya Shirika lake kwa Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula kwa mwaka 2019/2020 wakati wa ziara ya kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi kwenye mkoa wa Kigoma jana, Kaimu Meneja wa NHC mkoa wa Kigoma Ramadhani Sadick alisema Shirika hilo ilipangiwa kukusanya 886,732,105 na kubainisha kuwa ziada iliyopatikana ilitokana na mahusiano mazuri na wateja wake pamoja na huduma bora zinazotolewa.

Kwa mujibu wa Sadick, Shirika la NHC limekuwa likifanya jitihada za dhati kuhakikisha linaboresha mahusiano na wapangaji ili kuhakikisha panakuwepo maridhiano kati ya shirika na wateja wake jambo alilolieleza linasaidia kupunguza migogoro baina ya pande hizo hasa kipindi ambacho ilipaji kodi ulikuwa ukisuasua.

‘’Shirika limekuwa lifanya  mazungumzo na wateja ili kuona namna bora ya kuwasaidia kutekeleza majukumu ya kiupangaji ilhali wakiendelea na biashara zao na tunatoa fursa ya kulipa kodi kwa awamu tofauti na utaratibu uliozoeleka wa kulipa kodi kwa mara moja’’ alisema Sadick.

Akielezea hali ya soko, Kaimu Meneja wa NHC mkoa wa Kigoma, alisema Shirika lake limekuwa likifanya tafiti mara kwa mara ili kuhakikisha bei inazotoza kwenye nyumba za kupanga zinaendana na hali ya soko pamoja na mazingira halisi ya soko la nyumba.

Akigeukia nyumba za kuuza katika mradi wa Mlole, Kaimu Meneja huyo wa NHC mkoa wa Kigoma alisema, Shirika lilijenga nyumba 36 za makazi na nyumba 26 kati ya hizo ziliuzwa huku nyumba 13 zikipangishwa kwa wateja ambao walipewa fursa ya kununua nyumba hizo pale watakapohitaji.

Aidha, alibainisha kuwa, fursa hiyo inatolewa pia kwa mwananchi yeyote anayetaka kununua nyumba zilizopangishwa ambapo mkataba wa upangishaji unatoa fursa kwa mnunuzi asiye mpangaji kununua nyumba yoyote aitakaye.

Kwa upande wale Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amelitaka shirika la nyumba la taifa mkoa wa kigoma kuangalia namna bora ya kushirikiana na halmashauri zilizopo nje ya miji katika kujenga nyumba za watimishi badala ya kuangalia halnashauri za mjini pekee.

Alisema, katika kuhakikisha Shirika la Nyumba linajenga nyumba za bei nafuu kwa watumishi katika halmashauri mbalimbali nchini Naibu Waziri Mabula alitaka shirika hilo kukabidhiwa viwanja huku kazi ya kuweka miundombinu na gharama nyingine ikibaki halmashauri husika.

Aidha, amelitaka shirika la nyumba la Taifa kujenga nyumba kwa kuingia makubaliano na halmashauri kulingana na mahitaji au aina ya nyumba inazohitaji ili kuepuka ujenzi wa nyumba zitakazokosa wanunuzi.


Share:

Business Development Advisor (Tanzania Milk Processing Project) at HEIFER International, Tanzania

Business Development Advisor (Tanzania Milk Processing Project), Tanzania Description Heifer International is an equal opportunity employer. All qualified applicants will receive consideration for employment without regard to race, religion, color, national origin, gender, gender identify, sexual orientation, age, status as a protected veteran, among other things, or status as a qualified individual with disability. Tanzania Milk Processing Project… Read More »

The post Business Development Advisor (Tanzania Milk Processing Project) at HEIFER International, Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Business Development Assistant- TMPP at Heifer International

Business Development Assistant- TMPP, Tanzania Description Heifer International is an equal opportunity employer. All qualified applicants will receive consideration for employment without regard to race, religion, color, national origin, gender, gender identity, sexual orientation, age, status as a protected veteran, among other things, or status as a qualified individual with disability. Tanzania Milk Processing Project (TMPP) is an… Read More »

The post Business Development Assistant- TMPP at Heifer International appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Finance Officer Jobs at Save the children Tanzania

Finance Officer – (2000004V) TITLE: Finance Officer – Rukwa TEAM/PROGRAMME: Finance Team Lishe Endelevu project LOCATION: Rukwa GRADE: 4 POST TYPE: National CHILD SAFEGUARDING: Level 3 – the responsibilities of the post may require the post holder to have regular contact with or access to children or young people. As part of these responsibilities the post holder will… Read More »

The post Finance Officer Jobs at Save the children Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Monitoring Learning and Evaluation Officer at Heifer International -Tanzania Jobs

Monitoring Learning and Evaluation Officer at Heifer International Description Heifer International is an equal opportunity employer. All qualified applicants will receive consideration for employment without regard to race, religion, color, national origin, gender, gender identity, sexual orientation, age, status as a protected veteran, among other things, or status as a qualified individual with disability. FUNCTION Tanzania Milk Processing… Read More »

The post Monitoring Learning and Evaluation Officer at Heifer International -Tanzania Jobs appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Driver Jobs at Save the Children Tanzania- Kibondo

Driver – Kibondo – (200000C2) TITLE: Driver TEAM/PROGRAMME: Supply Chain LOCATION: Kibondo – Kigoma region – Tanzania GRADE: 6 CONTRACT LENGTH: 1 year, renewable CHILD SAFEGUARDING: Level 3: √ the post holder will have contact with children and/or young people either frequently (e.g. once a week or more) or intensively (e.g. four days in one month or more… Read More »

The post Driver Jobs at Save the Children Tanzania- Kibondo appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Child Protection Officer Jobs at Save the children Kigoma-Tanzania

Child Protection Officer Jobs at Save the children Kigoma-Tanzania Child Protection Officer – (200000DQ) JOB TITLE: Child Protection officer TEAM/PROGRAMME: Humanitarian emergency response for Burundi refugee LOCATION: Kigoma region – Tanzania GRADE: 4 CONTRACT LENGTH: 1 year, renewable CHILD SAFEGUARDING: Level 3: √ the post holder will have contact with children and/or young people either frequently (e.g. once… Read More »

The post Child Protection Officer Jobs at Save the children Kigoma-Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne January 21
























Share:

Monday, 20 January 2020

Senior Supply Chain Officer at The International Rescue Committee (IRC)

Requisition ID: req7798 Job Title: Senior Supply Chain Officer Sector: Supply Chain Employment Category: Fixed Term Employment Type: Full-Time Open to Expatriates: No Location: Kibondo, Tanzania Job Description The International Rescue Committee (IRC) is an International Non-Governmental Organization working in 40 countries, responding to the world’s worst humanitarian crises and helps people to survive and rebuild their lives.… Read More »

The post Senior Supply Chain Officer at The International Rescue Committee (IRC) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Consultant Obstetrician/Gynecologist at VSO, Mtwara, Tanzania

Consultant Obstetrician/Gynecologist, Mtwara, Tanzania Organization: Voluntary Service Overseas (VSO) Country: Tanzania Field location: Mtwara, Tanzania Office: VSO in Mtwara Closing date: Friday, 31 January 2020 Consultant Obstetrician/Gynecologist Type of role: Healthcare Location: Mtwara, Tanzania Salary: Competitive Contract type: Consultant Agreement Contract length: 1 Month Full Time: 35 hours per week Application Closing Date: 1 Feb 2020 Interview date:… Read More »

The post Consultant Obstetrician/Gynecologist at VSO, Mtwara, Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

International Consultant for Development of Media Training Manual, Media Guide and a Media Monitoring Framework on Women’s Leadership and Political Participation

International Consultant for Development of Media Training Manual, Media Guide and a Media Monitoring Framework on Women’s Leadership and Political Participation Background Grounded in the vision of equality enshrined in the Charter of the United Nations, UN Women works for the elimination of discrimination against women and girls; the empowerment of women; and the achievement of equality between… Read More »

The post International Consultant for Development of Media Training Manual, Media Guide and a Media Monitoring Framework on Women’s Leadership and Political Participation appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Sr. Health Information Systems Expert – Tanzania, USAID Global Health Technical Assistance Mission Support

Sr. Health Information Systems Expert – Tanzania, USAID Global Health Technical Assistance Mission Support   About Us Are you passionate about driving programs focused on foreign assistance? Do you want to be part of an organization that offers meaningful assignments and opportunities to expand your skills and expertise? At Dexis, you will experience a corporate culture of inclusiveness,… Read More »

The post Sr. Health Information Systems Expert – Tanzania, USAID Global Health Technical Assistance Mission Support appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Program Officer at PATH- Tools for Integrated Management of Childhood Illness

Program Officer, Tools for Integrated Management of Childhood Illness Tracking Code 9817 Job Description PATH is a global organization that works to accelerate health equity by bringing together public institutions, businesses, social enterprises, and investors to solve the world’s most pressing health challenges. With expertise in science, health, economics, technology, advocacy, and dozens of other specialties, PATH develops… Read More »

The post Program Officer at PATH- Tools for Integrated Management of Childhood Illness appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Project Operation/Procurement and Logistic Assistant at The Elizabeth Glaser Pediatric AIDS Foundation

VACANCY ANNOUNCEMENT “Sometimes in life there is that moment when it’s possible to make a change for the better. This is one of those moments.” -Elizabeth Glaser The Elizabeth Glaser Pediatric AIDS Foundation is a global leader in the fight against pediatric HIV and AIDS, working in 19 countries and supporting close to 6,000 sites around the world… Read More »

The post Project Operation/Procurement and Logistic Assistant at The Elizabeth Glaser Pediatric AIDS Foundation appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Kilichoendelea Mahakamani Leo Kesi Ya Tundu Lissu

Mdhamini wa aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, Robert Katula ameiambia mahakama kuwa wakati anamdhamini mshtakiwa huyo hakujua kama atapigwa risasi.

Katula ametoa madai hayo leo Jumatatu Januari 20, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakati kesi hiyo ilipokuwa ikitajwa.

Amesema Desemba 19 mwaka jana, mahakama iliamuru Lissu afike leo mahakamani lakini amefanya juhudi za kuwasiliana naye akawafahamisha kwamba atawasiliana na wakili wa chama lakini hadi leo kimya.

Mdhamini huyo ameomba apewe muda zaidi wa kuhakikisha anamfikisha mshtakiwa huyo mahakamani.

“Mheshimiwa wakati natoa ahadi kwamba nitahakikisha anafika mahakamani sikujua kama atapigwa risasi, tumemuandikia Mwenyekiti Freeman Mbowe barua atusaidie kumfikisha mshtakiwa nchini,” amedai Katula.

Hakimu Simba ameahirisha kesi hadi Februari 20 mwaka huu na kuamuru kwamba mshtakiwa ni lazima afike mahakamani tarehe hiyo kabla mahakama haijatoa amri nyingine zenye nguvu zaidi dhidi ya wadhamini.

Mdhamini wa mwingine wa Lissu ni Ibrahim Ahmed.

Kesi hiyo ilifunguliwa Juni 14 mwaka 2016 baada ya muda mshtakiwa wa nne, Lissu akapata matatizo yaliyomfanya ashindwe kufika mahakamani.

Mbali na Lissu, washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Mhariri wa gazeti la Mawio, Simon Mkina, Jabir Idrisa na Mchapishaji wa Kampuni ya Jamana, Ismail Mehboob.

Lissu na wenzake wanakabiliwa na mashtaka matano ikiwamo la kuandika habari za uchochezi kinyume na Sheria ya Magazeti ya Mwaka 2002.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger