Thursday, 16 January 2020

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi January 16



















Share:

Download & Install Udahiliportal app

Udahiliportal is a free, data-saving, and convenient app for reading the most education news, new Job adverts, Scholarships opportunities in Tanzania With Udahiliportal app you can Get : Admission and Education News : Stay updated on the current education news and information in Tanzania such as Examination results updates, College and University selection results, students Loans and bursaries… Read More »

The post Download & Install Udahiliportal app appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Wednesday, 15 January 2020

KAGERA SUGAR WAICHAPA YANGA 3 -0


Yusuph Mhilu mshambuliaji wa Kagera Sugar leo amekiongoza kikosi chake kuingamiza Yanga kwa mabao 3-0 kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa leo, Januari,15, Uwanja wa Uhuru.

Mhilu alifungua akaunti ya mabao dakika ya 13 kwa kuachia shuti kali lililomshinda mlinda mlango Farouk Shikalo.

Yanga ikiwa chini ya nahodha wao Haruna Niyonzima kwenye mchezo wa leo ilimshuhudia kiungo wao Mohamed Issa 'Mo Banka' akiwapunguzia kasi dakika ya 44 baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu kutokana na kuonyeshwa kadi mbili za njano kwa kucheza faulo kwa wachezaji wa Kagera Sugar.

Kipindi cha kwanza Yanga walikwenda mapumziko wakiwa nyuma kwa bao 1-0 walijipanga kurejea kupindua meza kipindi cha pili mambo yakazidi kuwa magumu kwani Kagera Sugar iliyo chini ya Mecky Maxime ilimzidi ujanja Luc Eymael ambaye ni mara yake ya kwanza kukaa kwenye benchi la ufundi akipokea kijiti cha Mwinyi Zahera.

Bao la pili kwa Kagera Sugar lilifungwa dakika ya 66 kupitia kwa Ally Ramadhan aliyemalizia pasi ya Abdallah Siseme na msumari wa mwisho ulipachikwa kwa kichwa dakika ya 89 na kuifanya Yanga kushindwa kutumia dakika nne za nyongeza kupata bao la kufutia machozi.

Kagera Sugar imecheza jumla ya mechi 17 inafikisha jumla ya pointi 27 inapanda mpaka nafasi ya nn, Yanga inakuwa nafasi ya nane ikiwa imecheza jumla ya mechi 13 na ina pointi 25 kibindoni.
Share:

AFARIKI DUNIA KWA KULA WALI NA PILIPILI

Wu Huayan alikuwa akila wali na pilipili ili aweze kuweka akiba ya kumwezesha kumtunza ndugu yake mgonjwa.

Mwanafunzi wa China ambaye amekula wali na pilipili kwa miaka mitano ili aweze kuweka akiba ya kumwezesha kumtunza ndugu yake mgonjwa amefariki, vyombo vya habari vya China vimeeleza.

Magumu yaliyokuwa yakimkabili Wu Huayan yaliishitua China baada ya picha za binti huyo, ambaye alikuwa na uzito wa karibu kilo 20, kuibuka mwaka jana.

Alilazwa hospitalini mwezi Oktoba mwaka 2019 alipokuwa na tatizo la kupumua.

Michango ilifurika kwa ajili ya kumsaidia kurudi katika afya njema, lakini kaka yake aliwaambia wanahabari kuwa alifariki siku ya Jumatatu.

Bi Wu aliliambia gazeti la Chongqing kuwa alivigeukia vyombo vya habari kwa ajili ya kuomba msaada baada ya kushuhudia baba na bibi yake wakifariki kwa kuwa hawakuwa na pesa za kulipa matibabu.

''Sitaki kushuhudia hayo tena -kusubiri kifo kwa sababu ya umasikini,'' alisema.

Kaka yake, ambaye hakutajwa jina lake, aliliambia gazeti la vijana la Beijing kuwa amefariki akiwa na miaka 24.

Madaktari walisema mwaka jana kuwa mwanafunzi huyo wa mwaka wa tatu alikuwa na maradhi ya moyo na figo kutokana na miaka mitano aliyokuwa akila chakula kidogo sana.

Maisha ya Wu Huayan yalikuwaje?

Wu Huayan na kaka yake waliishi katika mazingira magumu kwa miaka mingi baada ya kufiwa na wazazi wao wakiwa wadogo.

Yeye na ndugu yake walilelelwa na nyanya na baadaye mjomba na shangazi ambao waliweza kuwapatia yeni 300 kila mwezi.

Sehemu kubwa ya fedha hizo zilitumika kulipa malipo ya matibabu ya ndugu yake mdogo ambaye alikuwa anakabiliwa na changamoto za kiafya.

Hii ilimaanisha Bi Wu alitumia yeni mbili kwa siku ambayo ilimwezesha kununua mchele na pilipili kwa miaka mitano.

Alipowasili hospitali alikuwa na na urefu wa futi nne na nusu (4ft 5in).

Madaktari walisema alikuwa katika hali mbaya kutokana na ukosefu wa lishe kiasi cha kupoteza 50% ya nywele zake kichwani.

Kisa hicho kimepokelewaje?

Ndugu hao ambao wanatokea mkoa wa Guizhou, moja ya mikoa maskini zaidi nchini China na kisa hiki kimeeangazia hali mbaya ya umasikini nchini China.

Japo uchumi wa China umekuwa kwa miongo kadhaa iliyopita viwango vya umaskini havijapungua, huku takwimu ya kitaifa ya mwaka 2017 zikionyesha kuwa takribani watu milioni 30.46 wanaoishi katika maeneo ya mashambani wanaishi chini ya dola $1.90 kwa siku.

Viwango vya ukosefu wa usawa pia viliongezeka huku ripoti ya mwaka 2018 ya shirika la fedha duniani, IMF, ikisema kuwa China ni ''moja ya mataifa yasiyokuwa na usawa duniani''

Kisa cha Wu Huayan kilizua ghadhabu kwa umma dhidi ya mamlaka katika mitandao ya kijamii huku baadhi ya watu katika mitandao ya kijamiii wakisema ndugu hao walitelekezwa.

Wengine walisifia upendo wake kwa kaka yake kiasi cha kujinyima vitu muhimu maishani mwake.

Kando na michango ya umma ilianzishwa kupitia mitandao ya kijamii walimu na wanafunzi wenzake walimchangia yeni 40,000, huku wanakijiji wakichanga yeni 30,000 kumsaidia.

Kabla ya kifo chake , maafisa walitoa taarifa kusema kuwa Bi Wu amekuwa akipokea msaada wa serikali kwa jamii - ambayo inasadikiwa kuwa kati ya yeni 300, 700 kwa mwezi - na kwamba sasa anapokea usaidizi wakati wa dharura ya yeni 20,000.
Chanzo- BBC
Share:

MBUNGE WA CCM AFARIKI DUNIA

 
Mbunge wa Newala Vijijini (CCM), Rashid Akbar amefariki dunia leo Jumatano Januari 15, 2020 mkoani Lindi.

Taarifa iliyotolewa leo na ofisi ya Bunge la Tanzania inamnukuu Spika Job Ndugai akieleza kuhusu kifo cha mbunge huyo, kutoa pole kwa wafiwa.

Inaeleza kuwa mipango ya mazishi inaendelea kuratibiwa na ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na familia ya mbunge huyo.

“Natoa pole kwa wafiwa wote wakiwemo familia ya marehemu, wabunge, ndugu, jamaa na marafiki. Mungu awape uvumilivu katika kipindi hiki kigumu,” amesema Ndugai.

Awali taarifa ya katibu wa siasa na uenezi wa CCM mkoani Mtwara, Seleman Sankwa ilieleza kifo cha mbunge huyo.

“CCM inathamini na kutambua mchango mkubwa wa marehemu enzi ya uhai wake akiwa mbunge katika kuwatumikia wananchi wa Newala vijijini,” amesema Sankwa.

Share:

Picha : WADAU WA MAJI KUTOKA TABORA WATEMBELEA SHUWASA KUJIFUNZA MBINU ZA KUENDESHA MRADI WA MAJI YA ZIWA VICTORIA


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Wadau wa Maji zaidi ya 80 kutoka mkoani Tabora leo Januari 15,2020 wametembelea Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) kwa ajili ya kujifunza mbinu za kuendesha mamlaka za maji na kuendesha Mradi wa Maji ya Ziwa Victoria ambao hivi karibuni utaanza kuwanufaisha wananchi wa Tabora.

Wadau hao wametembelea chanzo cha Maji cha Bwawa la Ning’hwa kilichopo katika kata ya Chibe Manispaa ya Shinyanga na namna wanavyotibu maji hayo sambamba na kujionea Tenki la maji lililopo kata ya Old Shinyanga lenye ujazo wa mita za ujazo 18,000 linalopokea maji kutoka kwenye Tenki la Mabale ambalo lina maji ya Ziwa Victoria.

Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira katika mji wa Kahama na Shinyanga (Kahama Shinyanga Water Supply and Sanitation Authority (KASHWASA)ndiyo inatekeleza mradi wa Maji ya Ziwa Victoria na kuyasambaza kwenye maeneo mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na kuuza maji hayo kwenye mamlaka za maji ikiwemo SHUWASA na sasa inapeleka mradi wa maji mkoani Tabora.

Mkurugenzi Mtendaji wa SHUWASA,Flaviana Kifizi alisema wanategemea maji kutoka vyanzo vikuu viwili ambavyo ni Bwawa la Ning’hwa na Maji ya Ziwa Victoria kupitia KASHWASA.

“Kutokana na changamoto za upatikanaji na uzalishaji wa majisafi kutoka Bwawa la Ning’hwa na kwa kuzingatia uwekezaji wa serikali katika mradi unaosimamiwa na KASHWASA. Mwaka 2009 SHUWASA iliamua kuanza kutumia maji kutoka KASHWASA ili kutatua changamoto za upatikanaji na uzalishaji wa maji katika Manispaa ya Shinyanga na kutufanya kuwa na chanzo cha uhakika cha maji”,alifafanua Kifizi.

Alisema licha ya kufanikiwa kuwafikishia wananchi wa Manispaa ya Shinyanga huduma ya maji safi kwa asilimia 80.3 kutokana na maji ya KASHWASA,wanakabiliwa na changamoto ya gharama kubwa ya uzalishaji,mgandamizo mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria unaosababisha miundombinu kupasuka mara kwa mara na kusababisha gharama za uendeshaji kuongezeka.

“Changamoto nyingine ni umbali mkubwa baina ya vifaa vya kudhibiti maji ‘control valves’ katika mabomba makubwa hali inayosababisha kupotea kwa maji mengi wakati wa matangazo”,alieleza Kifizi.

Aidha alisema uhaba wa vitendea kazi bado ni tatizo pamoja na uhaba wa mabomba na viungio vyake kwa ajili ya matengenezo ‘spare pipes and fittings’.

Kifizi alizikumbusha Mamlaka za Maji na Usafi wa Mazingira Tabora,Nzega na Igunga (TUWASA,NZUWASA na IGUWASA) kutambua kuwa mradi wa Maji ya Ziwa Victoria ni mkubwa hivyo kujipanga vizuri ili kukabiliana na changamoto za uendeshaji wa mradi huo.

Naye Kaimu Tawala Msaidizi mkoa wa Tabora,Rukia Manduta alisema pindi maji yatakapofika mkoani Tabora watajitahidi kupanga bei za maji zinazoendana na kipato cha wananchi.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Leopard alisema ziara hiyo imewasaidia kupata elimu ya kutosha kuhusu namna ya kuendesha mamlaka za maji lakini pia jinsi ya kutekeleza kwa ufanisi mradi wa maji ya Ziwa Victoria.

Nao Mkuu wa wilaya ya Nzega, Godfrey Ngupula na wilaya ya Igunga,John Mwaipopo walisema wapo tayari kupokea mradi wa maji ya Ziwa Victoria mkoani Tabora ambapo tayari Maji yamefika katika Tenki la Ushirika lililopo Nzega kwa ajili ya majaribio.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mkurugenzi Mtendaji wa SHUWASA,Flaviana Kifizi akielezea namna Bwawa la Ning'wa linavyosaidia wananchi wa Manispaa ya Shinyanga kupata huduma ya maji safi wakati Wadau wa Maji kutoka Mkoa wa Tabora walipotembelea Bwawa la Ning'wa lililopo katika kata ya Chibe ili kujionea namna uzalishaji na usambazaji wa maji unavyofanyika. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Muonekano wa sehemu ya bwawa la Ning'wa.
Meneja Ufundi wa SHUWASA,Mhandisi Yusuph Katopola akielezea kuhusu bwawa la Ning'hwa lililojengwa mwaka 1972 na kufanyiwa ukarabati mwaka 1984 na lilipokauka mwaka 2000 wakaanzisha mradi wa Visima ili kuwapatia huduma ya maji wakazi wa Shinyanga.
Wadau wa maji kutoka mkoa wa Tabora wakiondoka katika bwawa la Ning'hwa ambalo ni chanzo cha maji kwa SHUWASA.
Mkuu wa wilaya ya Igunga,John Mwaipopo (mbele) na Mkuu wa wilaya ya Nzega, Godfrey Ngupula wakiwa na wadau wa maji mkoa wa Tabora wakitembelea eneo la kutibu maji ya bwawa la Ning'hwa na kuangalia namna maji hayo yanavyochujwa kabla ya kusafirishwa kwenda kwa wananchi.
Wadau wa maji mkoa wa Tabora wakitembelea eneo la kutibu maji ya bwawa la Ning'hwa. Mbele ni Katibu Tawala Msaidizi mkoa wa Tabora,Rukia Manduta.
Wadau wa maji wa mkoa wa Tabora wakitembelea eneo la kutibu maji ya bwawa la Ning'hwa.
Wadau wa maji mkoa wa Tabora wakitembelea eneo la kutibu maji ya bwawa la Ning'hwa.
Wadau wa maji mkoa wa Tabora wakitembelea eneo la kutibu maji ya bwawa la Ning'hwa.
Katibu Tawala Msaidizi mkoa wa Tabora,Rukia Manduta (katikati) akiwa na Mkuu wa wilaya ya Igunga,John Mwaipopo (kushoto) na Mkuu wa wilaya ya Nzega, Godfrey Ngupula (kulia) katika eneo la kutibu maji ya bwawa la Ning'hwa.
Wadau wa maji kutoka mkoa wa Tabora wakiwa katika eneo la kutibu maji ya bwawa la Ning'hwa.
Muonekano wa mitambo inayotumika kusukuma maji ya Bwawa la Ning'hwa kwenda kwenye matenki tayari kwa ajili ya kuwafikia wananchi.
Mkurugenzi Mtendaji wa SHUWASA,Flaviana Kifizi akionesha Tenki la Maji ya Ziwa Victoria lililopo katika kata ya Old Shinyanga.Tenki hilo linalomilikiwa na SHUWASA ndiyo linapokea maji kutoka KASHWASA.
Mkurugenzi Mtendaji wa SHUWASA,Flaviana Kifizi akiwaelezea wadau wa maji kutoka Tabora jinsi wanavyonunua maji kutoka KASHWASA na kuyauza kwa wananchi wa Manispaa ya Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa SHUWASA,Flaviana Kifizi akiwaelezea wadau wa maji kutoka Tabora jinsi wanavyonunua maji kutoka KASHWASA na kuyauza kwa wananchi wa Manispaa ya Shinyanga.
Mjumbe wa Bodi ya SHUWASA, Ziporah Pangani akifafanua jambo kwa wadau wa maji kutoka mkoa wa Tabora.
Muonekano wa tenki la SHUWASA linalopokea maji kutoka KASHWASA.
Wadau wa maji kutoka mkoa wa Tabora wakiondoka katika tenki la SHUWASA.
Wadau wa maji kutoka mkoa wa Tabora wakiangalia tenki dogo la maji linalotumika kusambaza Maji katika Manispaa ya Shinyanga.
Afisa Mahusiano wa SHUWASA,Nsianel Gelard akisoma taarifa ya SHUWASA kwa wadau wa maji kutoka mkoa wa Tabora wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara ya wadau hao wa maji kutoka mkoa Tabora leo Januari 15,2020 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga.
Afisa Mahusiano wa SHUWASA,Nsianel Gelard akisoma taarifa ya SHUWASA kwa wadau wa maji kutoka mkoa wa Tabora.
Mkurugenzi Mtendaji wa SHUWASA,Flaviana Kifizi akizungumza wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara ya wadau wa maji kutoka mkoa Tabora leo Januari 15,2020 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa SHUWASA,Flaviana Kifizi akizungumza wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara ya wadau wa maji kutoka mkoa Tabora leo Januari 15,2020 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga.
Katibu Tawala Msaidizi mkoa wa Tabora,Rukia Manduta akizungumza wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara ya wadau wa maji kutoka mkoa Tabora leo Januari 15,2020 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga.
Wadau wa maji kutoka Tabora wakiwa ukumbini.
Wadau wa maji kutoka Tabora wakiwa ukumbini.
Wadau wa maji kutoka Tabora wakiwa ukumbini.
Wadau wa maji kutoka Tabora wakiwa ukumbini.
Mkurugenzi wa KASHWASA,Mhandisi Joshua Mgeyekwa akizungumza wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara ya wadau wa maji kutoka mkoa Tabora leo Januari 15,2020 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Igunga, John Mwaipopo akizungumza wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara ya wadau wa maji kutoka mkoa Tabora leo Januari 15,2020 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Nzega Godfrey Ngupula akizungumza wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara ya wadau wa maji kutoka mkoa Tabora leo Januari 15,2020 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Leopard  akizungumza wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara ya wadau wa maji kutoka mkoa Tabora leo Januari 15,2020 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Shinyanga.
Wadau wa maji wakiwa ukumbini.
Wadau wa maji wakiwa ukumbini.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger