Thursday, 9 January 2020

Iran Yagoma Kuipa Marekani "Black Box" Ya Ndege ya Ukraine Iliyoanguka Jana

Iran imesema kuwa haitakabidhi kisanduku cha kunakili safari ya ndege ama ''Black box'' ya ndege ya Ukraine iliyopata ajali na kuua watu 176, kwa kiwanda kilichotengeneza ndege hiyo au kwa Marekani.

Ndege hiyo ya Ukraine aina ya Boeing 737-800 ilianguka muda mfupi baada ya kuanza safari yake kutokea uwanja wa ndege wa Tehran, na hakuna mtu aliyenusurika katika ajali hiyo.

Kwa mujibu wa sheria za anga za kimataifa , Iran ina haki ya kufanya uchunguzi kuhusu ajali hiyo.

Lakini watengenezaji wa ndege hiyo kwa ushirikiano na wataalamu kutoka nchi kadhaa wanaweza kuchunguza kisanduku hicho.

Ajali hiyo imetokea wakati ambapo kuna mvutano mkubwa kati ya Marekani na Iran, muda mfupi baada ya Iran kushambulia kwa makombora kambi mbili za kijeshi za Marekani zilizopo Iraq.

Aidha hakuna ushahidi kuwa matukio haya mawili yanahusiana na kuanguka kwa ndege hiyo.

Kwa kawaida, bodi ya Marekani ya usafirishaji salama ina jukumu la kuchunguza masuala yeyote ya kimataifa yanayohusisha ndege aina ya Boeing iliyotengenezwa Marekani kwa idhini ya sheria za nchi husika.

Kiongozi wa shirika la anga Iran Ali Abedzadeh alinukuliwa katika vyombo vya habari nchini humo akisema:"Hatutawapa kisanduku cheusi kampuni iliyotengeneza ndege hiyo au Wamarekani"

"Tukio hilo litachunguzwa na shirika la anga la Iran lakini Ukraine itaruhusiwa kuwepo katika uchunguzi huo" 


Share:

Taarifa Kwa Umma: Uwepo Wa Matapeli Katika Utoaji Wa Huduma Za Fedha.




Share:

Marekani Yasema Iko Tayari Kufanya Mazungumzo na Iran Bila Masharti Yoyote

Serikali ya Marekani imetangaza kuwa, iko tayari kufanya mazungumzo na Iran bila masharti yoyote.

Shirika la Habari la Reuters limeripoti kuwa,  balozi na mwakilishi wa kudumu wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Kelly Craft  ametangaza katika umoja huo kwamba, nchi yake ipo tayari kuanza mazungumzo na Iran bila masharti yoyote.

Hayo yanajiri katika hali ambayo, Rais wa Marekani Donald akizungumza jana katika hotuba yake kuhusiana na mashambulio ya makombora ya Iran dhidi ya kambi za kijeshi za nchi hiyo nchini Iraq alidai kuwa, hakuna raia wa Iraq au Marekani aliyeuawa katika shambulio hilo japo kambi hizo ziliharibiwa kidogo. 

Trump alidai kwamba, Iran inaonekana kurudi nyuma, hatua ambayo ni nzuri kwa pande zote husika. Hata hivyo alisema kuwa, ataongeza vikwazo dhidi ya Iran.

Wakati Rais Trump akidai kwamba, hakuna mwanajeshi wa Marekani aliyejeruhiwa au kuuawa katika shambulio hilo, vyombo vya Iran jana vilisema kuwa Wanajeshi 80 wa Marekani  waliuawa japo havikutoa uthibitisho wowote


Share:

MVULANA WA MIAKA 10 AJITAHIRI KWA KISU AKIOGOPA KUCHEKWA NA WENZIE


Mvulana wa miaka 10 mkazi wa kijiji ya Itare nchini Kenya amejitahiri kwa kutumia kisu cha jikoni baada ya wazazi wake kushindwa kulipia gharama ya Ksh 1000/- ya kupewa huduma hiyo hospitali.

Mtoto huyo wa darasa la pili ameeleza chombo cha habari kimoja nchini humo kuwa alilazimika kufanya hivyo kwa kuhofia unyanyapaa atakaofanyiwa na wenzake ambao wao walifanyiwa toraha kipindi cha likizo ya mwezi Desemba.

Inaelezwa kuwa hali ya mtoto huyo kiafya sio nzuri tangu alipojifanyia kitendo hicho mwezi mmoja uliopita na awali alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Kisii lakini wazazi wake walimrudisha nyumbani kwa kushindwa kumudu gharama za matibabu.

Mwanaharakati wilayani Kisii, Samwel Momanyi ameomba serikali iingilie kati na kumsaidia mtoto huyo kupata matibabu kwani anapata maumivu makali sana hususani akijisaidia haja ndogo.

Mvulana huyo ameshindwa kuanza masomo shule zilivyofunguliwa  siku ya Jumatatu Januari 6,2020 kutokana na afya yake kutoimarika.
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi January 9





















Share:

Wednesday, 8 January 2020

Israel Yatoa Onyo Kama Itashambuliwa na Iran

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ameonya kwamba nchi yake italipiza kisasi kwa yoyote atakayewashambulia, huku akirejelea matamshi yake ya kuiunga mkono hatua ya Marekani ya kumuua mkuu wa kikosi maalumu cha Iran Jenerali Qassemi Soleimani wiki iliyopita. 

Amesema mjini Jerusalem kwamba yoyote atakayewashambulia atakabiliwa na hatua kali ya kulipiza kisasi na kuongeza kuwa Israel inasimama kikamilifu na uamuzi wa rais wa Marekani Donald Trump na kuongeza kuwa anahitaji kupongezwa kwa kuchukua hatua hiyo kwa utaratibu, ujasiri na umadhubuti.


Share:

Iran Yasema Mashambulizi Ya Leo Dhidi Ya Marekani Ni Kama Makofi ya Uso Tu

Kiongozi mkuu wa  Iran, Ayatollah Ali Khamenei amesema hii leo kwamba shambulizi la makombora kwenye kambi za kijeshi zinazotumiwa na Marekani nchini Iraq ni kofi la uso kwa taifa hilo na  amesisitiza hatua hiyo ya kijeshi haitoshi. 

Ayatollah amelihutubia taifa masaa kadhaa baada ya kushambulia kambi hizo za kijeshi.

Shambulizi hili ni la kisasi dhidi ya mauaji ya jenerali wa kikosi maalumu cha Quds cha Iran, Qassemi Soleimani aliyeuliwa na Marekani mjini Baghdad Ijumaa iliyopita. 

Khamenei amesema uwepo usio halali wa Marekani kwenye ukanda huo unatakiwa kumalizwa akisema umesababisha vita, mgawanyiko na uharibifu. 

Waziri wa mambo ya nje wa Iran Mohamad Zarif amesema shambulizi hilo ni sawa na hatua za kujilinda huku rais wa halmashauri ya Ulaya Ursula von der Leyen akitoa mwito wa kufanyika makubaliano ya kidiplomasia.


Share:

Watoto 404 Wafanyiwa Ukatili Wa Kingono Iringa

Na Mwandishi Wetu Iringa
Mkoa wa Iringa kwa kipindi cha Januari mpaka Novemba 2019 umekuwa na matukio takribani 404 ya vitendo ya ukatili wa kingono kwa watoto ikiwa ni tatizo kubwa linalowakabili watoto katika malezi na makuzi yao nchini.

Hayo yamebainika mkoani Iringa wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Afya, Mendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipotembelea vikundi vya malezi kwa watoto katika kijiji cha Kising’a kilichopo Wilaya ya iirnga mkoani Iringa.

Akitoa taarifa hiyo Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Saida Mgeni amesema kuwa mkoa wa Iringa unakabiliwa na matatizo mbalimbali na umekuwa ukiongoza katika masuala mabalimbali yasiyofaaa katika jamii ikiwemo vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Ameongeza kuwa Serikali ya mkoa wa Iringa imejipanga katika kuhakikisha inapambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto mkoani humo kwa kuhakikisha inaratibu utoaji wa elimu kwa wananchi juu ya madhara ya vitendo hivyo kwa wanawake na watoto.

Akizungumza katika ziara hiyo Naibu Waziri wa Afya, Mendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa Serikali haijalala wala kufumbia macho suala la vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto bali inachukua hatua kali kwa wahusika wa vitendo hivyo wanaobainika.

Dkt. Ndugulile amezitaka Kamati za malezi ya mtoto mkoani Iringa na nchi nzima kuhakikisha wanatoa taarifa za vitendo vya kikatili dhidi ya wanawake na watoto kwa kuhakikisha hawawafichi watuhumiwa na hawamalizani kifamilia kesi za ukatil wa kijinsia.

Ameongeza kuwa ni jambo la aibu kwa Tanzania ya viwanda kuwa na vitendo vya kikatili kutokea katika jamii zetu kwani ni kikwazo kikubwa katika kuhakikisha jamii inajiletea maendeleo yao na taifa kwa ujumla.

“Mkiona wanajamii miongoni mwenu wanataka kumalizana katika kesi za vitendo vya ukatili wa kijinsia toeni taarifa ili tukomehse vitendo hivi visiendelee nchini” alisema Dkt. Ndugulile

Dkt. Ndugulile amewataka wazazi na walezi nchini kuhakikisha wanakaa na kuzungumza na watoto wao na sio kuwapiga na kuwapa adhabu zinatazosababisha kupata ukatili wa kisaikilojia ambao ni hatari kwa malezi na makuzi yao na kuhakikisha watoto hao wanapata haki zao za msingi zilizopo kisheria.


Share:

Nafasi 100 za Kazi CRDB Bank | Direct Sales Executive (DSE)

CRDB Bank PLC is looking for suitable people to fill vacant positions of Direct Sales Executive (DSE) – (1 year contract- 100 positions) in the Department of Retail Banking in different zones.

Job Purpose:

Translation and execution of retail sales agenda to ensure all set goals are met within agreed time. This is a sales target role based; in which the DSE is required to ensure door-to-door sales activities to meet the set sales target. The main agenda is to open new accounts, attract more deposits and promote usage.

==> BOFYA HAPA KUJUA ZAIDI


Share:

ELIMU JUU SEKTA YA MADINI INATAKIWA MOROGORO


 Waziri wa Madini Doto Biteko kushoto akizungumza kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga  Loata Sanare



Waziri wa Madini Doto Biteko katikati akizungumza, kushoto ni Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Sanare wakiwa kwenye kikao.


 Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo akizungumza




Na Tito Mselem Dodoma


Waziri Biteko ameagiza uongozi wa Mkoawa Morogoro kwa kushirikiana na Wizara ya Madini kuandaa maonesho ya madini kwalengo la kuelimisha Umma kwa watu wa Morogoro na mikoa jirani juu yaSheria, Kanuni na fursa zilizopo katika Sekta ya Madini.

Hayo yamebainishwa leo January 08, 2020 na Waziri wa Madini Doto Biteko alipofanya kikao na MkuuwaMkoawa Morogoro, LoataSanare, kilichofanyika katika ukumbi wa WizarayaMadini, Mtumba Jijini Dodoma.

“Nichukue fursa hii kuwaelekeza wataalamu wote wa Wizara ya Madini na Taasisi zake kuhakikisha wanashirikiana naMkoa wa Morogoro kuzitangaza fursa zinazopatikana katika Sekta ya Madini Mkoani Morogoro kwa kutumia njia mbalimbali ikiwemo kuandaa maonesho yatakayopelekea kuelimika kwa wananchi wa Mkoa huo,” alisema Waziri Biteko.

Aidha, Waziri Biteko amesisitiza ushirikiano katika kusimamia Sekta ya Madini kati yaWizara na Mkoa wa Morogoro na kumpongeza Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Morogoro Emmanuel Shija kwa kazi nzuri anazozifanya katika ukusanyaji wa mapato ya serikali.

Waziri Biteko amesema maendeleo ya Sekta ya Madini katika Mkoa wa Morogoro yatatokana na wachimbaji wenyewe, hivyo Wizara na Mkoa inapaswa kuwalinda nakuwalea wachimbaji na wadau wote wa madini mkoanihumo.

Akizungumzia changamoto inayowakabili wananchi wa Morogoro Biteko alisema ni pamoja na uelewa mdogo walionao juu ya masuala yanayohusiana na Sekta ya Madini kuwa ni kikwazo katika kupelekea maendeleo Mkoani humo.

Kwa upande wake,Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo, ameonesha kufurahishwa na kitendo cha Mkoa wa Morogoro kuonesha mafanikio makubwa katika makusanyo ya mapato ya serikali kutoka shilingi 811,714,294.12 kwa mwaka 2017/2018 mpaka kufikia 1,031,865,068.41 kwamwaka 2018/2019.

“Madini ya Ujenzi, Vito na Dhahabu tukiyasimamia vizuri hakika yatatuingizia fedha nyingi watu wa Morogoro, hivyo nikuombe Mkuu wa Mkoa ukalifanyie kazi hilo, pia sisi kama Wizara ya Madini tutashirikana na Mkoawa Morogoro kuhakikisha wawekezaji wanakuja kuwekeza katika Sekta ya Madini Mkoani Morogoro,”alisemaNyongo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Loata Sanare, amemuomba Waziri kupatiwa ushirikiano katika kuitangaza Morogoro kuwani Mkoa wa Madini na sio kilimo peke yake.

Pia Sanare, amesema, Mkoawa Morogoro una mpango wakufufua viwanda vya Ceramics vilivyokuwepo ili kuongeza matumizi ya madini ya viwandani yanayopatikana katika Mkoa huo kwa wingi na kuendeleza uhamasishaji wa uanzishwaji wa viwanda vipya vya Ceramics.

Wakatihuohuo, AfisaMadiniMkaziwaMkoawa Morogoro, Emmanuel Shija,amesema Mkoawa Morogoro una Jumlaya leseni 3082 za wachimbaji wa dogo kati yake ni leseni 250 tu ndizo zinafanya kazi ya uzalishaji, hivyo Ofisi ya Madini inaendelea na zoezi la kufuta leseni zote zenye makosa.

“Mwaka 2019 jumlayaleseni 223 zilifutwa na jumla ya hati za makosa kwa leseni 836 zimetolewa, leseni hizo ziko kwenye utaratibu wa kufutwa ndani ya mwaka huu wa fedha endapo wamiliki wa leseni hizo hawatarekebisha makosa yao kama Sheria inavyoelekeza,” alisemaShija.

Kikao hicho kilicho lenga kujadili changamoto na maendeleo ya Sekta ya Madini kwaMkoa wa Morogoro ikiwa ni pamoja na kuangalia fursa zilizopo katika Sekta ya Madini katika kuharakisha maendeleo ya mkoa huo.

Ambacho kilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wizara ya Madini na Taasisi zilizo chini ya Wizara akiwepo Naibu Waziri waMadini, StanslausNyongo, Mtendaji Mkuu wa Tume ya Madini Prof. ShukraniManya, Mkurugenzi Taasisi ya Jiolojia na Utafiti Tanzania Dkt Musa Budeba, Kamishna wa Madini Mhandisi David Mulabwa, Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Wizara ya Madini Edwin Egenge, Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Madini Augustine Ollal na wengine.
Share:

Nafasi za Kazi Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka-DART

Mtendaji  Mkuu  wa  Wakala  wa  Mabasi  Yaendayo  Haraka,  anakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa watanzania wenye sifa na uwezo kujaza nafasi wazi mbili (2)kwa kazi ya Derevakama zilivyobainishwa katika tangazo hili.

1.0.DEREVA (2)
1.1.SIFA ZA MUOMBAJI.
I.Cheti cha Mtihani wa Kidatocha IV, 
II.Leseni ya daraja ”C1’’au “E” ya uendeshaji magari ambayo amefanyia kazi kwa muda wa mwaka mmoja bila kusababisha ajali,
III.mafunzo  ya  msingi  ya  uendeshaji  magari  (Basic  Driving  Course) yanayotolewa na Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) au chuo cha Usafirishaji (NIT). IV.Waombaji   wenye   Cheti   cha   Majaribio   ya   Ufundi   Daraja   la   II watafikiriwa kwanza.
 
1.2.MAJUKUMU YA KAZI.
II.Kukagua gari kabla na baada ya safari ili kubaini hali ya usalama wa gari,
III.Kuwapeleka watumishi maeneo mbalimbali kwenyesafari za kikazi,
IV.Kufanya matengenezo madogo madogo ya gari,
V.Kukusanya na kusambaza nyaraka mbalimbali,
VI.Kujaza na kutunza taarifa za safari zote katika daftari la safari,
VII.Kufanya usafi wa gari, na
VIII.Kufanya kazi nyingine kadri anavyoelekeza na Msimamizi wake

Kutuma Maombi <<BOFYA HAPA>>


Share:

USAFIRISHAJI WA MIZIGO KWA NJIA YA RELI WAREJEA MKOANI TANGA

 Meneja wa Shirika la Reli Kanda ya Kaskazini (TRC) Ramadhani Ebrahim Gombo akizungumza na waandishi wa habari Jijini Tanga kuhusu kurejea kwa treni ya mizigo
 MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajab akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea eneo la reli ambalo liliathirika kwa kusombwa na maji Muheza ambalo kwa sasa limekarabatiwa na kuanza kupitisha treni
 MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajab akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea eneo la reli ambalo liliathirika kwa kusombwa na maji Muheza ambalo kwa sasa limekarabatiwa na kuanza kupitisha treni

 MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajab katikati aliyevaa tisheti ya mistari nyeupe akiangalia ukarabati huo ukiwa unamalizika kuendelea eneo la Muheza ambapo kwa sasa Reli zimeanza kupita
 Mafundi wa shirika la Reli mkoa wa Tanga wakiendelea na ukarabati huo
  Greda likiendea na kazi eneo la reli Muheza kama lilivyokutwa
 Greda likiendea na kazi eneo la reli Muheza kama lilivyokutwa

HATIMAYE usafirishaji wa mizigo kwa njia ya reli kutoka mkoa wa Tanga kwenye mikoa ya Kanda ya Kaskazini umerejea kwenye hali yake ya kawaida baada ya kukwama kwa kipindi cha miezi mitatu


Hatua hiyo inatokana na daraja kubwa lililopo eneo la Muheza kusombwa na maji mwishoni mwa mwaka jana wakati wa mvua kubwa zilizokuwa zikinyesha hapa nchini na hivyo kuleta athari kubwa.

Hayo yalisemwa jana na Meneja wa Shirika la Reli Kanda ya Kaskazini (TRC) Ramadhani Ebrahim Gombo wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo alisema usafiri huo umerejea baada ya kufanyia matengenezo makubwa kwenye eneo hilo.

Alisema kwamba baada ya daraja kubwa la reli lililopo eneo la Muheza kukatika lilishindwa kutumika na hivyo wafanyabiashara kushindwa kuitumia kwa ajili ya kusafirishia bidhaa zao na hivyo kusimama kwa muda.

“Daraja la Muheza lilisombwa na Maji Octoba 10 mwaka jana na ulazimika kuanza kunyia ukarabati kuanzia mwezi wa 11 tulianza kurekebisha kwa kuondoa maji eneo hilo kuwawezesha wananchi kuendelea na shughuli zao”Alisema

“Lakini baada ya hapo tulihamia maeneo mengine Korogwe,Mnyuzi, Gendagenda kwani maeneo mengi yaliathirika na tulivyomaliza maeneo hayo 23 Novemba 2019 ndipo tuliporudi hapa muheza mpaka Januari mwaka huu tulipomaliza daraja hilo na kwa sasa treni zinatembea na usafirishaji mizigo umerudi kwenye hali yake ya kawaida”Alisema

Alisema kwa sasa treni inaendelea vizuri na usafirishaji wa mizigo umerudi kwenye hali yake ya kawaida huku akielezwa kwamba wamepata hasara kubwa kwani treni za mizigo hazikufanya kazi ya kusafirisha mizigo na mzigo wa mingi wanategemea kutoka Bohari ya Mafuta mkoani Tanga (GBP) na Saruji kwenda mikoa ya Kilimanjaro, Dar na mikoa mingine Kanda ya Ziwa wamepata hasara kubwa kwa kusombwa daraja la muheza.

Hata hivyo Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu ambaye alitembelea eneo la reli wilayani Muheza ambalo lililikuwa limeathirika na mvua kubwa na kupelekea usafiri huo kusitishwa.

Alisema kwamba athari ambazo zimetokea kutokana na kusitishwa usafiri huo ni kubwa kwa sababu daraja hilo la reli na maeneo yote yalijaa maji na mawasiliana ya reli dar kwenda Tanga kukatika.

Aidha alisema lakini sasa shirika la reli wamefanya kazi nzuri sana kwa kipindi kifupi wamekuwa wakifanya kazi kwa usiku na mchana kuhakikisha inafanya kazi.

Mbunge huyo alisema kwamba kuanzia juzi wananchi wa Muheza wamejisikia furaha kubwa baada ya kuanza kuona reli inapita licha ya kupatikana kwa hasara kutokana na huduma hiyo kusitizwa kutokana na mvua kubwa zilizokuwa zikinyesha mwaka jana na kuleta athari hiyo.

“Kama juzi juzi mmesikia reli inapita kwenda Moshi lakini pia ilikuwa ipite na hapo Muheza kwenda Tanga lakini kutokana na tatizo hilo imeshindwa kufika huku lakini naamini serikali itaanzisha usafiri wa kuelekea mkoani Tanga kwa sasa baada ya matengenezo “Alisema
Share:

Syrup Room And Water Treatment Team Leader at Coca-Cola Kwanza

Closing Date  2020/01/22
Reference Number CCB190528-4
Job Title Syrup Room and Water Treatment Team Leader
Function Manufacturing
Company Coca-Cola Kwanza (Tanzania)
Job Type Permanent
Location – Country Tanzania
Location – Province Not Applicable
Location – Town / City Mbeya

Job Description
Coca-Cola Kwanza Ltd has an exciting opportunity in Manufacturing Department. We are looking for a talented individual with the relevant skills and experience for a Syrup Room and Water Treatment Team Leader position, to be based in Mbeya. The successful candidate will report directly to the Manufacturing Manager.

Key Duties & Responsibilities
The Syrup Room and Water Treatment Team Leader will be responsible in monitoring the syrup and water treatment plant; Ensure good operational control and equipment maintenance in his/her process area (syrup and water treatment plant) in order to supply syrup and treated water to customers as per daily operational plan. Provide leadership to the Syrup Room and Water Treatment team, communicating the business direction and implementing organisational improvement initiatives. Ensure compliance with all internal and related legal/regulatory requirements with respect to safety, water quality and environmental management. Where necessary assist with the development of operational quality system procedures/guidelines for Syrup Room and Water Treatment. Ensure optimization of resources in daily operations as per budget.

Skills, Experience & Education
The incumbent should have at least a Bachelor’s degree in Food Science and Technology; Chemistry; Micro-Biology or Environment Science. Three (3) years of manufacturing experience which include experience in a leadership or managerial role and 2 years water treatment experience preferably with FMCG; Should also be a good communicator, physically flexible and demonstrate high level of integrity and leadership.



Share:

Customer Sales Agent 3 post at Sokowatch Arusha

Sokowatch is transforming communities across Africa by revolutionizing access to essential goods and services. By connecting small shops to the digital economy, we fix inefficient supply chains and provide services previously unavailable to informal businesses. Sokowatch aims to provide everything a retailer needs, no wholesalers or banks necessary. Thousands of retailers across Kenya, Tanzania, and Rwanda use Sokowatch’s… Read More »

The post Customer Sales Agent 3 post at Sokowatch Arusha appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Officer Reconciliation Job at National Bank of Commerce (NBC)

National Bank of Commerce (NBC) Job Title: Officer Reconciliation Head Office NBC NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Job Description​ EXECUTION OF MAIN ROLE Prepare reconciliations of reconcilable accounts of Head office Finance Identify,… Read More »

The post Officer Reconciliation Job at National Bank of Commerce (NBC) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

RC TELACK AMTAKA MWENYEKITI WA KIJIJI KUMTOA MTOTO MACHUNGANI


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack (kushoto) na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Jasinta Mboneko wakimhoji mtoto Majebele Masanja baada ya kumkuta akichunga ng'ombe muda wa masomo hapo jana tarehe 07/01/2020 eneo la shule ya Sekondari Ilindi, kata ya Zongomela Wilaya ya Kahama.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack (kushoto) na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Jasinta Mboneko wakimhoji mtoto Majebele Masanja baada ya kumkuta akichunga ng'ombe muda wa masomo hapo jana tarehe 07/01/2020 eneo la shule ya Sekondari Ilindi, kata ya Zongomela Wilaya ya Kahama.

***
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amemtaka Mwenyekiti wa kijiji cha Ilindi, kata ya Zongomela kuhakikisha mtoto Majebele Masanja anaacha mara moja kazi ya kuchunga ng’ombe na anapelekwa shule.

Mhe. Telack ametoa agizo hilo jana tarehe 07/01/2020 baada ya kumkuta mtoto huyo maeneo ya shule ya Sekondari Ilindi akiwa anachunga ng’ombe badala ya kuwa shuleni ambapo alihojiwa na kusema kuwa anafanya kazi kwa ujira wa sh. 20,000 kwa mwezi na kuwa hasomi kwa sababu mzazi wake hana uwezo.
Akizungumza na Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji wa Halmashauri ya Mji Kahama katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo ambapo ametoa agizo hilo kwa Mwenyekiti huyo, Telack amesema wenyeviti wote wakahakikishe wazazi wanaelekezwa kusimamia mahudhurio ya wanafunzi shuleni.
“Mkazungumze na wananchi, wazazi na walezi kuhusu wanafunzi wasiofika shuleni, mkafanye mikutano ya hadhara na muazimie kusimamia mahudhurio shuleni” amewaambia.
“Haiwezekani wazazi kuacha watoto wanachunga badala ya kusoma, mtoto yule apelekwe shuleni na nitafuatilia” amesema Mhe. Telack.
Aidha, Telack amewasisitiza Wenyeviti wote wa Mitaa na Vijiji kushirikisha wananchi katika shughuli za maendeleo ikiwa ni pamoja na kujenga maboma ya madarasa, kusaidia kukomesha matumizi ya madawa ya kulevya na kuwaongoza wananchi bila kuendekeza migogoro isiyokuwa na sababu.
Share:

WANANCHI WA KAHAMA WAMSHUKURU RAIS MAGUFULI KWA KUWACHANGIA UJENZI WA SHULE


 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack (Mwenye ushungi wa njano), Katibu Tawala Mkoa Bw. Albert Msovela (mwenye suti nyeusi), Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Jasinta Mboneko na Viongozi wengine wakiwa kwenye moja ya vyumba vya madarasa ya shule ya msingi Mayila ambapo wanafunzi wa darasa la kwanza wameanza masomo yao hapo tarehe 06 Januari, 2020. 
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akizungumza na wananchi wakiwemo wazazi na walezi (hawamo pichani) waliokuwa shuleni Mayila kuwachukua watoto wao baada ya muda wa masomo
Shule ya msingi Mayila iliyopo Mtaa wa Mayila, kata ya Nyihogo Wilaya ya Kahama imefunguliwa rasmi huku wananchi wa kata hiyo wakimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli kwa kuwachangia shilingi mil. 5 ili kuhakikisha shule hiyo inakamilika.
Wazazi hao wametoa shukrani hizo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack alipokwenda kukagua utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais la kuhakikisha shule hiyo inafunguliwa mapema jana tarehe 07 Januari, 2020.
Wamesema kuwa, kukamilika kwa shule hiyo kutawapunguzia adha ya umbali wa zaidi ya kilomita 3 watoto wa kata hiyo waliokuwa wanalazimika kuvuka barabara kubwa kufuata shule kata za jirani hali iliyopelekea kuwa katika hatari ya kugongwa na magari.
“Nashukuru sana kwa shule hii, watoto wetu mwanzo walikuwa wanakwenda mbali na sisi kama wazazi tupo tayari kuendelea kushirikiana na Serikali kujenga maboma” amesema Bw. Richard Joseph.
Diwani wa kata ya Nyihogo Mhe. Shadrack Mguami amesema, “kuna wakati naamka usiku kumuombea Mhe. Rais, sikutegemea kupata fedha kutoka kwake kwani angeweza kufanya shughuli nyingine lakini akaona atoe hapa, tunaahidi tutaendelea kumuunga mkono kwa kujenga maboma”
Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kahama Mji Bw. Anderson Msumba amesema watoto zaidi ya 200 wameandikishwa kuanza darasa la kwanza hivyo uhitaji ni mkubwa, hata hivyo Halmashauri inaendelea kukamilisha maboma 108 na kufunga shule mpya 8.
“Tunamshukuru Mhe. Rais ametupa mori kuhakikisha shule hii inafunguliwa” amesema Msumba.
Mhe. Rais alichangia shilingi milioni 5 ili kuongeza nguvu ya kukamilisha shule hiyo alipopita Wilayani Kahama akielekea Wilayani Chato mwezi Novemba, mwaka jana 2019 na kuagiza ifunguliwe mwezi Januari mwaka huu 2020.
Shule hiyo iliyokuwa na vyumba viwili vya madarasa, hivi sasa ina vyumba 8 na matundu ya vyoo 12.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger