Tuesday, 7 January 2020
Monday, 6 January 2020
Raia Watatu wa Marekani Wauawa Kenya....Pentagon Yasema Tukio Hilo Halina Uhusiano na Mzozo wa Iran
Wafanyakazi watatu wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani wameuawa kwenye shambulizi la kigaidi katika kambi ya kijeshi ya Manda ilioko mjini Lamu
Wafanyakazi 2 pamoja na makandarasi wawili wameripotiwa kuachwa na majeraha mabaya kufuatia shambulizi hilo la Jumapili, Januari 5.
" Wakati wa shambulizi hilo la kigaidi katika kambi ya kijeshi ya Manda, wafanyakazi wa wizara ya ulinzi ya Marekani waliuawa, huku wengine wawili wakijeruhiwa vibaya ila hawako katika hali mbaya,"Sehemu ya taarifa ya ubalozi wa Marekani ilisoma.
Aidha, Marekani imeapa kupambana vilivyo na magaidi wa al- Shabaab hasa wale waliotekeleza shambulizi la Manda.
Kivuko kipya MV.Ilemela chashushwa kwenye maji Ziwa Victoria Mwanza
Wakazi wa Ilemela mkoa wa Mwanza leo wameshuhudia kwa mara ya kwanza kivuko kipya cha Kayenze Bezi, MV.Ilemela ambacho kimegharimu kiasi cha shilingi bilioni 2.7 kikishushwa kwenye maji baada ya kukamilika kwa ujenzi wake. Tukio hilo limefanyika katika yadi ya Songoro iliyopo Wilaya ya Ilemela ambapo mgeni rasmi alikua Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi na Mawasiliano) Mhe. Atashasta J. Nditiye (MB)
Akizungumza katika tukio hilo Mhe. Nditiye alimshukuru Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na serikali ya awamu ya tano kwa kuendelea kutimiza ahadi ya miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini.
‘’Hadi sasa Mheshimiwa Rais tayari ameshatoa fedha zote kiasi cha shilingi za Kitanzania bilioni 9,953,916,200 iliyokuwa imepangwa kwenye bajeti ya miradi ya maendeleo ya vivuko kwa mwaka wa fedha wa 2019/2020’’, alisema Mhe. Naibu Waziri ambapo aliongeza kuwa kivuko cha MV.Ilemela kitakapoanza kutoa huduma kitaondoa changamoto ya usafiri kwa wananchi kati ya Kayenze na kisiwa cha Bezi.
‘’Kivuko hiki kitakapoanza kutoa huduma ni dhahiri kuwa kitaondoa changamoto ya usafiri kwa wananchi kati ya Kayenze na kisiwa cha Bezi hivyo kitainua maisha ya wananchi wa maeneo hayo kibiashara, kiuchumi na kijamii, mara tu mtakapokamilisha majaribio anzeni kutoa huduma ’’. Aliongeza Naibu Waziri ambapo pia alitoa wito kwa watumishi wa TEMESA kufanya kazi kwa weledi na kuhakikisha kivuko hicho pamoja na vivuko vingine vinatunzwa vizuri na vinadumu kwa muda mrefu huku wakizingatia usalama wa abiria na mali zao.
Awali, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle, akisoma taarifa kwa mgeni rasmi katika tukio hilo alisema serikali kupitia TEMESA inaendelea na ujenzi wa vivuko vingine vipya kwa ajili ya Mafia Nyamisati kwa gharama ya shilingi bilioni 5.3, Bugorola Ukara kwa gharama ya shilingi bilioni 4.2 pamoja na Chato Nkome kwa gharama ya shilingi bilioni 3.1.
‘’Vivuko hivi vyote vinagharimu jumla ya shilingi za Kitanzania bilioni 15.3 na fedha zote hizi zinatolewa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania’’, alisema Mhandisi Maselle ambapo aliishukuru serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutoa fedha zote zilizotengwa kwa ajili ya kutekeleza miradi ya ununuzi wa vivuko, ukarabati na ujenzi wa maegesho ya vivuko, ambapo alisema Fedha hizo zimewezesha miradi hiyo kuanza na mingine kuwepo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.
Naye Mbunge wa Ilemela Mhe. Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angelina Mabula akizungumza katika tukio hilo aliishukuru serikali kwa kuweza kutimiza ahadi iliyoitoa. ‘’Nimshukuru Mhe. Rais niwashukuru TEMESA kwa kazi kubwa na nzuri ambayo imefanyika, tunao uhakika sasa kwamba adha ya usafiri katika eneo la visiwa vya Kayenze Bezi sasa litakua ni historia’’, alisema Dkt. Mabula.
Aidha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella alimuomba Mhe. Nditiye kufikisha salamu za shukrani kwa Rais kwa mambo makubwa anayoufanyia mkoa wa Mwanza hasa kwenye sekta ya usafiri wa majini ambapo alisema watu wa mkoa huo wanategemea mwezi wa pili kuona vivuko vingine vikiingia ziwani tayari kuanza kutoa huduma kwa wananchi.
Kivuko cha MV.Ilemela kina uwezo wa kubeba abiria 200 na magari 10 sawa na tani 100. Hadi sasa Wakala unaendesha na kusimamia vivuko 30 katika vituo (Ferry stations) 20 Tanzania Bara na hivyo kukamilika kwa kivuko cha MV. Ilemela kutafanya idadi ya vivuko kufikia 31 na vituo kuwa 21.
NATO kuangazia upya mpango wa majeshi yake Iraq
MUUNGANO wa kujihami wa NATO unakutana leo kujadili mustakabali wa ujumbe wake wa kutoa mafunzo nchini Iraq wakati ambapo mivutano Mashariki ya Kati inaongezeka baada ya Marekani kumuua jenerali wa ngazi ya juu wa Iran.
Mabalozi kutoka nchi ishirini na tisa wanachama wa NATO wanatarajiwa kukutana katika makao makuu muungano huo mjini Brussels
Hali imezidi kuwa mbaya nchini Iraq ambapo wabunge wametaka kuondolewa kwa wanajeshi 5,200 wa Marekani walioko nchini humo
Waziri Ndalichako aamuru kuwekwa ndani mhandisi na mshauri elekezi ujenzi wa VETA Sumbawanga
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako ameagiza kukamatwa kwa mhandisi wa ujenzi Ding Fubing pamoja na mshauri elekezi wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Rukwa Swalehe Kyabega kutokana na kushindwa kukamilisha mradi huo kwa wakati huku wakiendelea kusuasua juu ya ukamilifu wa ujenzi huo ambao ulitakiwa kukamilika 30.12.2019 baada ya kuongezewa siku 100 na hatimae hadi sasa wamefikia asilimia 52 ya ujenzi.
Prof. Ndalichako alisema kuwa kimkataba mkandarasi huyo alitakiwa kuthibitisha kwa risiti matumizi ya shilingi bilioni 1.5 malipo ya awali ya ujenzi kupitia kwa Mshauri elekezi ambae alishindwa kutoa vielelezo vinavyoonesha utekelezaji wa takwa hilo la kisheria na kuongeza kuwa mshauri huyo ameshindwa kusimamia matumizi ya fedha za serikali katika utekelezaji wa mradi huo.
“Mkandarasi aende akakae ndani mpaka vile vifaa mlivyoruhusu viondoke hapa, mpaka vitakaporudi ndio muwaachie, wasababu naona sasa hii inakuwa ni kuchezeana, majibu hamna kitu ambacho kinachoeleweka, utakwenda kukaa sero hadi utakapotoa maelezo ya ufasaha juu ya jambo hili, kwasababu huwezi kucheza na serikali namna hii, mara ya mwisho nilipokja hapa mlikuwa na vifaa kama vyuma chakavu, mmeleta vifaa ahalafu mmeviondoa kuvuipeleka sehemu nyingine, utakaa ndani hadi vifaa hivyo vitakaporudi na uwe na watu wa kutosha kufanya kazi, kwasababu tumechoka tunataka huu ujenzi uishe, wachukue wakae ndani,” Alisisitiza.
Halikadhalika mhandisi huyo alionekana kuwafanyika kazi wafanyakazi wa mradi huo kwa malipo ambayo yapo kinyume na mkataba wa serikali huku baadhi ya watendaji wengine wa sekata ya umeme wakilalamika kufanyishwa kazi bila ya mkataba maalum.
Prof. Ndalichako aliyasema alipotembelea ujenzi wa chuo cha ufundi Stadi VETA katika eneo hilo la Kashai lililopo Manispaa ya Sumbawanga huku akiongozana na watumishi idara ya elimu kutoka halmashauri mbili za wilaya ya Sumbawanga, Mkuu wa Wilaya hiyo, kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya pamoja na uongozi wa VETA taifa.
Awali akisoma taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa chuo hicho Mkurugenzi Mkuu wa VETA nchini Dkt.Pancras Bujuru alisema kuwa mkandarasi huyo tayari amelipwa shilingi 3,507,174,603 ambayo ni sawa na asilimi 35 ya thamani ya mradi huo na malipo ya mwisho yalikuwa shilingi 330,521,213.79 ambapo alilipwa tarehe 20.12.2019 na kutegemea kuwa baada ya malipo hayo kasi ya ujenzi ingeongezeka lakini haikuwa kama walivyotaraji.
Mh. Waziri kwa hali hii mkandarasi amethibitisha uwezo mdogo kutekeleza mradi huu na hatuna imani kama utatekelezwa kwa wakati kwasababu muda aliopewa na kuongezewa siku 100 vyote vimekwisha nab ado kazi hazijaweza kuisha kwa muda, kwahiyo tunadhani kwamba uwezo wake wa kutekeleza mradi hauturidhishi hata sisi, mshauri elekezi anajukumu la kumsimamia mkandarasi kwa niaba yetu kwasababu tumemuajiri kwa kazi hiyo, tunajua kwamba amekuwa akitoa maelekezo lakini kumekuwa na udhaifu wa kuyasimamia kwa kuchukua hatua zinazostahili na kwa muda muafaka naye tunadhani ana mapungufu,” alisema.
Tarehe 31/8/2019 mkandarasi Tender International alikabidhiwa kiwanja kwaajili ya kuanza ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) katika Manispaa ya Sumbawanga pamoja mshauri Elekezi wa Mradi huo Sky Architect Consultancy Ltd, ambapo mradi huo ulitegemewa kukamillika mwezi Septemba 2019 huku gharama za mradi huo ikiwa shilingi 10,700,488,940.05.
Mpango:wahasibu Mafisadi Kukiona Cha Moto
Ramadhani Kissimba na Josephine Majura, Dar es Salaam
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, ameiagiza Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Mipango kuwachukulia hatua kali za kinidhamu wahasibu wote wanaofanya vitendo vinavyokinzana na maadili ya kitaaluma ya uhasibu kama wizi, ubadhirifu wa mali za umma, ufisadi na rushwa.
Dkt. Mpango alitoa maagizo hayo wakati akifungua Kikako Kazi cha kuandaa Hesabu za Majumuisho za Serikali za mwaka 2018/19 pamoja na kuzindua Mfumo mpya wa uandaaji wa taarifa za fedha za Majumuisho (Government Accounting Consolidation System (GACS), Jijini Dar es Salaam
Dkt. Mpango aliwataka wahasibu wote nchini kuwa wazalendo na kusimamia ipasavyo matumizi ya rasimali za Umma na kuwataka kuhakikisha kuwa usalama katika Mifumo ya Fedha unakuwa madhubuti ili kuondoa uwezekano wa mifumo hiyo kudukuliwa na kuleta hasara kubwa kwa Serikali na Wananchi.
Aidha Dk. Mpango alimpongeza Mhasibu Mkuu wa Serikali CPA Francis Mwakapalila, pamoja na Mkurugenzi wa Mifumo ya Fedha Bw. John Sausi kwa kuonesha dhamira na nia ya kweli ya kuhakikisha wanatengeneza Mifumo bora ya kifedha ili kuleta ufanisi mkubwa katika kukusanya na kuhasibu mapato na matumizi ya Serikali.
Aliongeza kuwa dhamira hiyo imedhihirika kwa kuanzisha Mifumo ya Kifedha ya kimtandao kama Government e-payment Gateway (GePG), Government Salary Payment Platform (GSPP), na sasa Government Accounting Consolidation System (GACS).
‘’Nimefurahi sana kuona kwamba ndani ya kipindi kifupi cha miaka minne tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani, mmeanzisha Mifumo mingi na madhubuti ya kukusanya Mapato na Maduhuli ya Serikali, pamoja na Mifumo ya kuhasibu rasilimali za umma yenye kukidhi viwango vya kimataifa” alisema Dkt. Mpango.
Aliongeza kuwa ni ushahidi bayana kuwa, watendaji hao wanatafsiri kwa vitendo dhamira na dira ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Uongozi shupavu wa Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ya kusimamia rasilimali za nchi kwa manufaa ya Wananchi hasa Wanyonge.
Pia alieleza kuwa matarajio ya Serikali ni kwamba mfumo huu ulioanzishwa pamoja na Mifumo iliyokwisha kuanzishwa itaitumika vizuri kwa weledi na uadilifu mkubwa katika kutoa huduma bora kwa Wananchi na ikizingatiwa hilo matarajio ya wananchi na rasimali za umma zitatumika ipasavyo kuboresha Maisha yao.
Awali Mhasibu Mkuu wa Serikali CPA. Fransis Mwakapalila alisema hatua ya kuandaa Hesabu za Majumuisho kwa kutumia Mfumo wa Kielektroniki unaifanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza Barani Afrika kutayarisha Hesabu za Majumuisho kwa kutumia mfumo uliandaliwa na wataalamu wake wa ndani kutoka Wizara ya Fedha na Mipango.
CPA. Mwakapalila alisema kwa sasa Tanzania ni nchi inayoongoza kwa ubora wa Taarifa za FeFha za Majumuisho (CFS) zenye kukidhi viwango vya Kimataifa katika sekta ya Umma (IPSAS) Barani Afrika.
Akizungumza katika kikao kazi hicho Mkurugenzi wa Idara ya Mifumo ya Usimamizi wa fedha kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. John Sausi, amesema Idara yake itaendelea kujenga mifumo ya kielektroniki ya fedha ili kuhakikisha makusanyo ya pesa za Serikali yanapita katika mifumo sahihi.
“Mafanikio yanayopatikana katika uandaaji wa mifumo hii yanatokana na watalaamu kutoka Wizara ya Fedha na Mipango kuwa na uzalendo wa kuitumikia nchi yao, na wataalamu hao wamekuwa wakiandaa mifumo mbalimbali ukiwemo mfumo wa kukusanya maduhuli ya Serikali kwa njia ya Mtandao (GePG) ambapo Taasisi zaidi 616 zimeshaunganishwa kwenye mfumo huo.
Bw.Sausi alisema kuwa mfumo mpya wa uandaaji wa taarifa za fedha za majumuisho (GACS) ambao umezinduliwa na Mhe.Dkt. Philip Isdor Mpango utasaidia kupunguza utiriri wa kuwa na mifumo mingi ya uandaaji wa taarifa za fedha.
Mwisho
Taarifa Kwa Umma Kuhusu Tuhuma Zinazosambaa Mitandaoni Kwamba Wagonjwa Wengi Wanapoteza Maisha Katika Hospitali Ya Taifa Muhimbili-mloganzila.
Kumekuwa na taarifa kwenye mitandao ya kijamii ambazo bila kuchanganua zinatuhumu kwamba Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila inasababisha vifo kwa wagonjwa.
Uongozi wa hospitali unapenda kuwahakikishia Umma wa Watanzania kwamba habari hizi si za kweli na hazitoi picha halisi ya huduma ambazo zinazotolewa hospitalini hapa.
Uongozi wa hospitali unapenda kuwahakikishia Umma wa Watanzania kwamba habari hizi si za kweli na hazitoi picha halisi ya huduma ambazo zinazotolewa hospitalini hapa.
Takwimu tulizonazo zinaonyesha kwamba wagonjwa wanaotibiwa MNH- Mloganzila wameongezeka katika makundi yote. Wagonjwa wa nje wameongezeka kutoka 17,115 katika kipindi cha robo mwaka cha Julai hadi Septemba, 2018 kufikia wagonjwa 25,493 katika kipindi cha Julai hadi Septemba, 2019 ambalo ni ongezeko la asilimia 48.8.
Aidha, wagonjwa wanaotibiwa na kulazwa wameongezeka kutoka 1,459 katika kipindi cha robo mwaka cha Julai hadi Septemba, 2018 na kufikia wagonjwa 2,795 katika kipindi cha Julai hadi Septemba, 2019 ambalo ni ongezeko la asilimia 91.6.
Aidha, wagonjwa wanaotibiwa na kulazwa wameongezeka kutoka 1,459 katika kipindi cha robo mwaka cha Julai hadi Septemba, 2018 na kufikia wagonjwa 2,795 katika kipindi cha Julai hadi Septemba, 2019 ambalo ni ongezeko la asilimia 91.6.
Wakati huo huo idadi ya vifo (mortality rate) ikipungua kutoka asilimia 14.9 iliyokuwepo katika kipindi cha robo mwaka cha Julai hadi Septemba, 2018 na kufikia asilimia 10.4 katika kipindi cha Julai-Septemba 2019.
Aidha, takwimu za MNH-Upanga zinaonyesha kwamba katika kipindi cha robo mwaka cha Julai hadi Septemba 2018 wagonjwa waliolazwa walikua ni 12,375 ambapo kulitokea vifo 1,000 (mortality rate) ambayo ni asilimia 8.1.
Vilevile katika kipindi cha Julai hadi Septemba 2019 MNH Upanga ililaza wagonjwa 17,230 na kati ya hao vifo vilikua 1,673 ambayo ni asilimia 9.7(mortality rate).
Vilevile katika kipindi cha Julai hadi Septemba 2019 MNH Upanga ililaza wagonjwa 17,230 na kati ya hao vifo vilikua 1,673 ambayo ni asilimia 9.7(mortality rate).
Hivyo basi takwimu kati ya MNH-Mloganzila na MNH-Upanga za asilimia ya wagonjwa waliofariki hazitofautiani sana ambapo MNH-Upanga ni asilimia 9.7 wakati MNH-Mloganzila ni asilimia 10.4 katika robo ya Julai – Septemba, 2019.
Hatua hii inaonyesha juhudi ambazo zinafanyika za kuboresha utoaji wa huduma katika MNH- Mloganzila zinazaa matunda.
Moja ya sababu ambazo imeelezwa na mtoa taarifa kwamba Madaktari wanaotoa huduma MNH-Mloganzila ni wanafunzi waliopo katika majaribio si za kweli, hivyo tungependa kufafanua kwamba Hospitali ya MNH-Mloganzila ina Madaktari Bingwa 52, Madaktari wa kawaida 50 na kwa sasa ina Madaktari tarajali 53.
Licha ya Madaktari Bingwa hawa walioajiriwa MNH-Mloganzila kutoa huduma lakini pia wanashirikiana na Madaktari Bingwa kutoka MNH-Upanga katika kutoa huduma hapa MNH-Mloganzila, vilevile hospitali hii ina madaktari wawili waliobobea wenye hadhi ya Profesa kutoka Korea nao wapo wanatoa huduma.
Hivyo sio kweli kwamba madaktari ambao wapo mafunzoni wanafanyakazi bila usimamizi kwani hospitali imeweka utaratibu wa kila mgonjwa anayefika kupata huduma anaonwa na Daktari Bingwa kwa ajili ya maamuzi.
Wakati uongozi wa hospitali ukifanyia kazi tuhuma na malalamiko yaliyotolewa juu ya utoaji huduma katika taarifa hii, tunapenda kuutarifu Umma kwamba tangu MNH ipewe dhamana ya kusimamia hospitali hii, tumejielekeza katika kutatua changamoto zilizokuwepo katika utoaji huduma na kwa kiasi kikubwa imeonyesha mafanikio ambayo yanaonyesha kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa na pia kuna ushuhuda wa wagonjwa ambao wametibiwa na kuridhika na utoaji wa huduma zetu.
Tunawahakikishia Watanzania kwamba huduma zinazotolewa katika Hospitali ya MNH-Mloganzila zimeboreshwa na tunawakaribisha Watanzania wenye jukumu la kuelimisha jamii waje kuzungumza na wataalam na waone jinsi huduma zinavyotolewa ili waweze kutoa taarifa sahihi kwa jamii.
Imetolewa na
Prof. Lawrence M. Museru
Mkurugenzi Mtendaji,
MNH-Mloganzila.
Uganda: Bob Wine Akamatwa Tena
Mbunge wa Kyadondo nchini Uganda, Robert Kyagulani, maarufu Bobi Wine, leo Januari 6, 2020, Jeshi la Polisi nchini humo limemkamata na kisha kurusha mabomu ya machozi kwa lengo la kuzuia mkutano wake, uliokuwa umepangwa kufanyika eneo la Gayaza, Kyadondo Mashariki
Bobi Wine alikamatwa pamoja na wabunge wengine Asuman Basalirwa, Latif Ssebagala,Waiswa Mufumbira na mwenyekiti wa baraza la Kasangati na kwa sasa wanashikiliwa katika kituo cha polisi cha Kasangati.
Gazeti la The Observer limemnukuu Basalirwa akisema walikuwa wakiendesha gari la Kyagulanyi kabla ya polisi kuwazuia katika eneo la Kasangati na kuwapeleka katika kituo cha polisi. Kyagulanyi alikuwa akitarajiwa kuzindua mikutano ya mashauriano kuhusu malengo ya urais kwa uchaguzi mkuu ujao.
Polisi wamedai kuwa ilibidi kuuzuia mkutano huo kwa sababu ulipangwa kufanyika kwenye eneo la wazi, wakati mikutano ya namna hiyo hufanyika ndani ili kutoingilia shughuli za watu wengine.
Pia polisi wamedai kuwa hakukuwa na vyoo vya kutosha kwa ajili ya wageni waliokuwa wakitarajiwa.
Mbunge huyo aliiandikia tume ya uchaguzi kabla ya krisimasi akieleza nia yake ya kufanya mkutano kitaifa kuhusu nia ya kuwania urais. Ingawa alitoa taarifa kwa tume hiyo, ambayo ilimruhusu, imesema hakutimiza vigezo vingine kama vinavyoelezwa kwenye sheria.
Bobi Wine ameeleza nia yake ya kuwanida urais dhidi ya rais Yoweri Museveni ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 1986.
Gazeti la The Observer limemnukuu Basalirwa akisema walikuwa wakiendesha gari la Kyagulanyi kabla ya polisi kuwazuia katika eneo la Kasangati na kuwapeleka katika kituo cha polisi. Kyagulanyi alikuwa akitarajiwa kuzindua mikutano ya mashauriano kuhusu malengo ya urais kwa uchaguzi mkuu ujao.
Polisi wamedai kuwa ilibidi kuuzuia mkutano huo kwa sababu ulipangwa kufanyika kwenye eneo la wazi, wakati mikutano ya namna hiyo hufanyika ndani ili kutoingilia shughuli za watu wengine.
Pia polisi wamedai kuwa hakukuwa na vyoo vya kutosha kwa ajili ya wageni waliokuwa wakitarajiwa.
Mbunge huyo aliiandikia tume ya uchaguzi kabla ya krisimasi akieleza nia yake ya kufanya mkutano kitaifa kuhusu nia ya kuwania urais. Ingawa alitoa taarifa kwa tume hiyo, ambayo ilimruhusu, imesema hakutimiza vigezo vingine kama vinavyoelezwa kwenye sheria.
Bobi Wine ameeleza nia yake ya kuwanida urais dhidi ya rais Yoweri Museveni ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 1986.
Tanasha Donna avunja kimya kuhusiana na madai ya Diamond Kuwa na Mpenzi Mwingine
Mpenzi Mkenya wa msanii Diamond Platinumz, Tanasha Donna hatimaye amevunja kimya chake baada ya kuibuka kwa maneno kuwa mwanamuziki huyo ana uhusiano wa pembeni.
Diamond anadaiwa kuwa katika uhusiano mwingine na mrembo wa Tanzania yapata miezi sita tu baada ya kumkaribisha mwanawe wa kiume Naseeb Junior.
Mama huyo wa mtoto mmoja kupitia ukurasa wake wa Instagram, aliwaomba watu kukoma kueneza habari ambazo macho yao hayajashuhudia kwa kutumia mdomo.
Ni bayana kuwa mrembo huyo alikuwa anajibu madai kuwa mpenziwe ana uhusiano na mwanadada kwa jina Rose.
Katika hali ya kuzima fununu kuhusu uhusiano wake, mtangazaji huyo wa radio ya NRG alisema mapenzi yake na Diamond hayawezi kuvunjika.
Donna alichapisha picha yake na Diamond katika hali ya mahaba na kuonyesha kuwa hawawezi kutengana hivi karibuni.
Watu wasiojulikana waiba vifaa vya NIDA Arusha
Watu wasiojulikana wameiba mashine zote za Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa(NIDA) zilizokuwa katika kituo kidogo cha NIDA katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha, Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha usiku wa kuamkia leo, kituo hicho kimefungwa kwa leo na Polisi wameanza mchakato wa kuwasaka waliohusika na wizi huo.
Mkuu wa wilaya Arumeru, Jerry Muro amesema wizi huo umetokea usiku wa kuamkia leo Jumatatu Januari 6, 2020 katika ofisi za Nida zilizopo jengo la halmashauri ya Wilaya ya Arusha (DC).
Muro amesema vifaa vilivyoibwa ni kamera mbili, stendi mbili, kompyuta mpakato mbili, kompyuta moja (Desk top), stendi mbili, Extation mbili, keyboad moja na Damalog moja.
Mkuu wa wilaya Arumeru, Jerry Muro amesema wizi huo umetokea usiku wa kuamkia leo Jumatatu Januari 6, 2020 katika ofisi za Nida zilizopo jengo la halmashauri ya Wilaya ya Arusha (DC).
Muro amesema vifaa vilivyoibwa ni kamera mbili, stendi mbili, kompyuta mpakato mbili, kompyuta moja (Desk top), stendi mbili, Extation mbili, keyboad moja na Damalog moja.
"Vifaa vyote vimeibiwa, tumepata mshtuko, milango haikuvunjwa inaonekana ni wizi wa kimkakati umefanywa ndani, vifaa vya NIDA ni mali za Taifa sasa hawa wanapata wapi ujasiri wa kuiba!"- Jerry Muro, Mkuu wa Wilaya Arumeru
Trump atishia kuiwekea Iraq vikwazo Kama Itawafukuza Wanajeshi wa Marekani Nchini Humo
Rais wa Marekani, Donald Trump, ametishia kuiwekea Iraq vikwazo baada ya bunge la nchi hiyo kupiga kura kupitisha azimio linalovitaka vikosi vya Marekani viondoke nchini humo.
Trump amesema iwapo wanajeshi hao wataondoka, Iraq itapaswa kuilipa Marekani gharama za kambi ya jeshi la anga iliyoko Iraq.
Trump amebainisha kuwa hawatoondoka hadi hapo Iraq itakapoilipa Marekani gharama za kambi hiyo ambayo amesema iko muda mrefu hata kabla ya wakati wake na iligharimu mabilioni ya dola kuijenga.
Trump amesema kama Iraq itavitaka vikosi vya Marekani kuondoka na suala hilo kufanyika katika njia isiyokuwa na misingi ya kirafiki, basi nchi yake itaweka vikwazo vikali kwa Iraq ambavyo haijawahi kushuhudia.
Wakati huo huo, Ikulu ya Marekani imesema kuwa Trump amezungumza na Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson kuhusu hali inayoendelea nchini Iraq na Iran.
Soma hii: Ajira Mpya 250+ zilizotangazwa wiki hii
Mvutano bado ni mkubwa baada ya Marekani kuusika kumuua kiongozi wa jeshi wa Marekani jenerali Qasem Soleimani huko Baghdad wiki iliyopita.
Soleimani ambaye alifariki akiwa na umri wa miaka 62, alikuwa akiongoza operesheni za vita katika nchi za mashariki ya kati
Soleimani ambaye alifariki akiwa na umri wa miaka 62, alikuwa akiongoza operesheni za vita katika nchi za mashariki ya kati
Kiongozi mpya wa kikosi cha jeshi la Iran la Quds - ambacho Soleimani aliongoza - ameapa kuwaondoa Wamarekani katika mataifa ya mashariki ya kati.
Iran yasitisha utekelezaji wa makubaliano wa Nyuklia ya Mwaka 2015
Serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran usiku wa kuamkia leo Jumatatu imetoa taarifa ikitangaza kuwa imechukua hatua ya tano na ya mwisho ya kupunguza utekelezaji wa ahadi zake katika makubaliano ya nyuklia maarufu kwa kifupi kama JCPOA.
Taarifa hiyo imesema kuwa, kuanzia sasa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitakuwa na kizuizi chochote katika shughuli zake za nyuklia ikiwa ni pamoja na kurutubisha madini ya urani, asilimia ya urutubishaji wa madini hayo, kiwango kinachorutubishwa na katika masuala ya utafiti na uchunguzi.
Kwa msingi huo katika hatua hii ya tano, Iran imetupilia mbali kizuizi muhimu zaidi cha shughuli zake kwa mujibu wa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA ambacho kinahusiana na idadi ya mashinepewa zinazoruhusiwa kufanya kazi.
Iran imesema katika taarifa hiyo kwamba, tokea sasa miradi yake ya kuzalisha nishati ya nyuklia itafanya kazi kwa mujibu wa mahitaji yake ya kiufundi.
Imesisitiza kuwa, Iran itaendelea kushirikiana na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) na kwamba iwapo vikwazo vyote vitaondolewa na Tehran ikafaidika na maslahi ya JCPOA, iko tayari kutekeleza tena vipengee vya makubaliano hayo.
Imesisitiza kuwa, Iran itaendelea kushirikiana na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) na kwamba iwapo vikwazo vyote vitaondolewa na Tehran ikafaidika na maslahi ya JCPOA, iko tayari kutekeleza tena vipengee vya makubaliano hayo.
Serikali Kufuta Vyama 3,436 Vya Ushirika
Serikali inakusudia kuvifuta vyama vya ushirika vipatavyo 3,436 ambavyo vimeshindwa kutekeleza majukumu yake ya msingi na havipatikani huku vingine vikiwa havijulikani vilipo.
Kwa kuzingatia matakwa ya sheria no 6 ya mwaka 2013 ya vyama vya ushirika kifungu 100 na kanuni ya 26, Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga amemuagiza Mrajisi wa vyama hivyo kutoa notisi ya siku 90 kwenye gazeti la serikali ya kusudio la kuvifuta.
Akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake jijini Dodoma jana, Mhe Hasunga amesema asilimia kubwa ya vyama vilivyokusudiwa kufutwa ni vyama vya ushirika wa akiba na mikopo ambavyo ni asilimia 73.8.
Amesema vyama hivyo vingi ni matokeo ya mfumo wa uwezeshaji wa wananchi kiuchumi ujulikanao kama Jakaya Kikwete Fund ambao ulilenga kuwawezesha wananchi kiuchumi.
" Katika mpango huu wa JK Fund wananchi wengi walianzisha SACCOS kwa lengo la kupata mikopo kutoka kwenye mfuko huo, Aidha vyama ambavyo havikupata mkopo havikuendelea na majukumu yake na hata vilivyopata mikopo baada ya kupata walitelekeza vyama hivyo jambo linalopelekea kuwa na SACCOS nyingi hewa," Amesema Mhe Hasunga.
Amevitaka vyama ambavyo orodha yake itapatikana kwenye tangazo la mrajisi litakalotolewa kwenye gazeti la serikali, mtandao wa wizara ya kilimo na mtandao wa Tume ya Ushirika kujitokeza na kutoa sababu za kwanini wasifutwe kwenye orodha ya vyama vya ushirika.
" Tunavitaka vyama vyote vya ushirika nchini kuendesha shughuli zao kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizopo. Vyama vyote vinatakiwa kuwahudumia wanachama wake na siyo vinginevyo," Amesema Mhe Hasunga.
Mhe Waziri amesema mpaka sasa daftari la mrajisi wa vyama vya ushirika lina jumla ya vyama 11,149 vilivyoandikishwa kati ya vyama hivyo, 3,436 havijulikani vilipo, vyama 1,250 vimesinzia na vyama 6,463 vipo hai.
Amesema sababu zinazopelekea kufutwa kwa vyama hivyo ni kushindwa kuwa na ofisi huku viongozi wake wakiwa hawajulikani, Chama kushindwa kufanya shughuli zake ndani ya miezi sita tangu kiandikishwe pamoja na idadi ya wanachama kupungua kwa mujibu wa mahitaji ya kisheria.
Sababu nyingine ni vyama hivyo kushindwa kutekeleza takwa la kisheria la kutayarisha makisio ya mapato na matumizi na kuyapeleka kwa mrajisi kuyapitisha, kutayarisha taarifa ya mwaka, kufunga mahesabu na kuyapeleka COASCO kwa ukaguzi, kutofanya mikutano ya mwaka ya wanachama na bodi zao.
Katika orodha ya vyama vya ushirika kimkoa vinavyokusudiwa kufutwa kwenye daftari la mrajisi wa vyama, Mkoa wa Mwanza unaongoza ukiwa na jumla ya vyama 393, Pwani ya pili yenye vyama 335 huku Kagera ikishika nafasi ya tatu kwa vyama 301.
Kwa upande wake Kaimu Mrajisi wa Vyama vya Ushirika, Dk Benson Ndiegi amesema serikali haitowavumilia viongozi wa vyama ambavyo vitakaidi maagizo hayo yaliyotolewa na Mhe Waziri.
" Baada ya agizo hili la Mhe Waziri na baada ya kutoa notisi hizo kwenye gazeti la serikali tutakua tayari kupokea maelezo na taarifa kutoka kwenye vyama na wale ambao watakua wanafutwa waje na wanaamini wana nafasi ya kuendelea kuwepo inabidi waje na vielelezo vyao," Amesema Dk Ndiegi
Sunday, 5 January 2020
Mmiliki Mabasi ya Sahara Akutwa Amekufa Gesti
Mfanyabiashara na mmiliki wa mabasi ya Sahara, Abdalah Msangi (47) mkazi wa Usangi Mkoani Kilimanjaro, leo Jumapili Januari 5, 2020 amekutwa amekufa kwenye moja ya nyumba ya wageni iliyopo Mtaa Dar es Salaam Mjini Moshi.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Kilimanjaro, Tanzania, James Manyama amethibitisha kutokea kwa kifo hicho.
Amesema mfanyabiashara huyo alikuwa na rafiki yake wa kike chumbani, lakini baada ya kuona mwenzake anaishiwa nguvu na kuanza kutokwa na povu puani na mdomoni akakimbia.
“Huyu Mfanyabiashara alikuwa na rafiki yake wa kike kwenye chumba cha wageni huko Dar es Salaam street, baada ya kuona ameishiwa nguvu na kuanza kutokwa na povu mdomoni alitoroka, amedai Kamanda Manyama.
Aidha, amesema baada ya kupata taarifa na kufika eneo la tukio na kulipekua gari la Msangi kulikutwa dawa ya kienyeji ambayo imechukuliwa kwa uchunguzi.
Amesema Mwili wa marehemu umepelekwa Hospitali ya Mkoa Mawenzi kwa uchunguzi zaidi.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Kilimanjaro, Tanzania, James Manyama amethibitisha kutokea kwa kifo hicho.
Amesema mfanyabiashara huyo alikuwa na rafiki yake wa kike chumbani, lakini baada ya kuona mwenzake anaishiwa nguvu na kuanza kutokwa na povu puani na mdomoni akakimbia.
“Huyu Mfanyabiashara alikuwa na rafiki yake wa kike kwenye chumba cha wageni huko Dar es Salaam street, baada ya kuona ameishiwa nguvu na kuanza kutokwa na povu mdomoni alitoroka, amedai Kamanda Manyama.
Aidha, amesema baada ya kupata taarifa na kufika eneo la tukio na kulipekua gari la Msangi kulikutwa dawa ya kienyeji ambayo imechukuliwa kwa uchunguzi.
Amesema Mwili wa marehemu umepelekwa Hospitali ya Mkoa Mawenzi kwa uchunguzi zaidi.
WAVUTA BANGI TISHIO KITANGILI , VIBAKA NGOKOLO.... "TUNAKOMBWA MCHANA", MBUNGE ATAKA VITUO VYA POLISI KILA KATA
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza katika kata ya Ngokolo wakati akifanya ziara yake kusikiliza kero za wananchi na kuzungumza na wajumbe wa kamati ya siasa CCM ngazi ya matawi na kata ya Ngokolo leo Januari 5,2020. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkazi wa Ngokolo Rehema Mkono akimweleza Mbunge wake Stephen Masele kero ya vibaka wanaotishia amani katika mitaa ya Ngokolo.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza katika kata ya Ngokolo na kuahidi kuzungumza na mamlaka mbalimbali ili kuhakikisha changamoto ya vitendo vya uhalifu katika Jimbo lake vinakomeshwa.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Songambele katika kata ya Kitangili Madeha Khamis akitoa kero ya wahalifu wanaotishia amani kwa Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele aliyetembelea kata hiyo Januari 4,2019.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza na wajumbe wa kamati ya siasa CCM ngazi ya matawi na kata ya Kitangiri na kupokea kero mbalimbali za wananchi Januari 4,2020.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza na wajumbe wa kamati ya siasa CCM ngazi ya matawi na kata ya Kitangili Januari 4,2020.
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Vijana wanaovuta bangi na kunywa pombe aina ya gongo katika kata ya Kitangili Manispaa ya Shinyanga wametajwa kuwa tishio na kuchochea vitendo vya ubakaji wa wanawake na watoto,kuvamia watu na kupora mali za wananchi huku vibaka Kata ya Ngokolo wakiwakosesha amani wananchi kwani sasa wanaiba mchana kweupe.
Hayo yamebainika wakati wananchi wakitoa kero zao kwa Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Masele alipofanya ziara katika kata 17 za Jimbo la Shinyanga kusikiliza kero za wananchi na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Kata zilizolalamikiwa kuongoza kwa vitendo vya uhalifu ni Ndala, Ngokolo na Kitangili katika mitaa ya Songambele,Busulwa na Kitangiri.
Wananchi hao walimweleza Mbunge wao Stephen Masele kuwa katika maeneo hayo wananchi wamekuwa wakiuawa,kuvamiwa na kuibiwa mali zao majumbani huku Jeshi la Polisi likidaiwa kutochukua hatua stahiki kwa wahalifu wanaosumbua mitaani.
Wakazi wa Kitangili walisema licha ya vijana wanaojihusisha na uvutaji bangi na kunywa pombe aina ya gongo kuwa tishio lakini kila wanapotoa taarifa jeshi la polisi limekuwa likichelewa kufika eneo la tukio na kushindwa kuchukua hatua kwa wahalifu hao.
"Ukubwa wa tatizo la uhalifu Kitangili ni pale tunapowaita polisi pindi panapotokea tukio huwa wanachelewa kufika kwenye matukio. Lakini pia huwezi amini kama kuna polisi wanawajua hao wavuta bangi na wanajua bangi zinakonunuliwa,wakikutana na wavuta bangi mtaani wanaishi vizuri na wavuta bangi ",walisema wananchi hao.
"Mhe. Mbunge hapa Kitangiri kuna tatizo la hawa vijana wanaovuta bangi,vijana hawa wanaovuta bangi hawalimi bangi wapo wanaolima na kuuza bangi na hatujui wanakonunulia bangi. Tunaomba wanaouza bangi wadhibitiwe kwani bangi na gongo ni kichocheo cha masuala ya ubakaji,kuvamia watu na wizi",alieleza Mwenyekiti wa Mtaa wa Songambele Madeha Khamis.
Naye Rehema Mkono mkazi wa kata ya Ngokolo alisema Ngokolo inakabiliwa na changamoto ya vibaka akisema hivi Sasa Ngokolo inazalisha kundi la 'Panya Road' bila kujua ambapo vijana wenye umri chini ya miaka 20 wamekuwa wakifanya vitendo vya uhalifu mchana kweupe kwa kuvizia nyumba za watu na kuiba mali.
"Ngokolo tunaibiwa mchana na usiku. Mimi mwenyewe nimeibiwa vitu ndani ya nyumba mchana kweupe 'Tunakombewa mchana kweupe' tunaomba tujengewe kituo cha polisi hapa Ngokolo ili kukomesha tatizo hili",alisema Mkono.
Kwa Upande wake,Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Masele alieleza kusikitishwa na vitendo vya uhalifu vinavyoendelea katika baadhi ya maeneo katika Jimbo la Shinyanga akisema upo umuhimu wa kujenga vituo vya polisi katika kila kata.
"Katika ziara yangu kutembelea kata 17 za Jimbo la Shinyanga nimepewa taarifa ya vitendo vya uhalifu nitazungumza na mamlaka mbalimbali ili kuhakikisha tunamaliza changamoto hii ili wananchi wetu wawe salama na mali zao",alisema Masele.
Masele ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika alianza ziara yake kukagua miradi ya maendeleo,kusikiliza kero za wananchi na kuzungumza na wajumbe wa kamati za siasa CCM ngazi ya matawi na kata zote 17 za Jimbo la Shinyanga Mjini kuanzia Desemba 27,2019 na kuhitimisha ziara yake Januari 5,2020.





















































