Saturday, 26 October 2019

TIMU YA TASSY FC MABINGWA WA MASHINDANO YA IDARA TANGA CEMENT MPIRA WA MIGUU

 Mkuu wa kitengo cha Rasilimali watu wa Tanga Cement Diana Malambugi na mgeni rasmi wakati wa Fainali ya mashindano ya Idara ya Kiwanda cha Uzalishaji wa Saruji cha Simba Cement ambaye ni Meneja Uzalishaji wa kiwanda  hicho Godwin Kamando katikati akikabidhi kombe kwa Nahodha wa timu ya Tassy Hassani Macho ambao walikuwa mabingwa wa mashindano ya mpira wa miguu  
 Mkuu wa kitengo cha Rasilimali watu wa Kiwanda cha Kuzalisha Saruji cha Tanga Simba Cement Diana Malambugi kulia akimkabidhi kombe Nahodha wa timu ya Tassy ambao ni mabingwa kwa upande wa mpira wa miguu Hassani Macho baada ya kuifunga Quary FC mamabo 2-0 mchezo huo ulifanyika kwenye uwanja wa shule ya Msingi Saruji mabao yalifungwa na Mustapha Bakari na Nassoro Chande
 Mkuu wa kitengo cha Rasilimali watu wa Kiwanda cha Kuzalisha Saruji cha Tanga Simba Cement Diana Malambugi kulia akikabidhi zawadi ya mbuzi kwa nahodha wa timu ya Tassy ambao ni mabingwa kwa upande wa mpira wa miguu baada ya kuifunga Quary FC mamabo 2-0 mchezo huo ulifanyika kwenye uwanja wa shule ya Msingi Saruji
 Mkuu wa kitengo cha Rasilimali watu wa Kiwanda cha Kuzalisha Saruji cha Tanga Simba Cement Diana Malambugi kulia akikabidhi zawadi ya mbuzi kwa nahodha wa timu ya Tassy ambao ni mabingwa kwa upande wa mpira wa miguu baada ya kuifunga Quary FC mamabo 2-0 mchezo huo ulifanyika kwenye uwanja wa shule ya Msingi Saruji katikati ni Meneja Uzalishaji wa kiwanda  hicho Godwin Kamando ambaye alikuwa mgeni rasmi

 Mkuu wa kitengo cha Rasilimali watu wa Kiwanda cha Kuzalisha Saruji cha Tanga Simba Cement Diana Malambugi kulia akikabidhi zawadi kwa washindi wa mashindano mbalimbali
 Mkuu wa kitengo cha Rasilimali watu wa Kiwanda cha Kuzalisha Saruji cha Tanga Simba Cement Diana Malambugi kulia akisalimiana na wachezaji wa timu ya Quary kabla ya kuanza kwa mchezo huo
 Mkuu wa kitengo cha Rasilimali watu wa Kiwanda cha Kuzalisha Saruji cha Tanga Simba Cement Diana Malambugi kulia akisalimiana na wachezaji wa timu ya Tassy FC ambao ni mabingwa wa mashindano ya Idara kwa upande wa mpira wa miguu
 Wachezaji wa timu ya Quary FC wakijadiliana jambo kabla ya kuanza mchezo huo
 TIMU ya Quary wakiwa kwenye picha ya pamoja 
 TIMU ya Tassy ambao ni mabingwa kwa upande wa mpira wa miguuwakiwa kwenye picha ya pamoja kabla ya mchezo huo kuanza

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya October 26




Share:

Friday, 25 October 2019

AERONAUTICAL INFORMATION OFFICER – 7 POST – TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY

AERONAUTICAL INFORMATION OFFICER – 7 POST Employer: TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY Date Published: 2019-10-25 Application Deadline: 2019-11-07 JOB SUMMARY: NA DUTIES AND RESPONSIBILITIES: i.To assist in accepting, processing and disseminating Flight Plans to all Air Traffic Management units designated Authorities, Search and Rescue units, including those along aircraft flight routes to destination, and alternate aerodromes according to ICAO Flight plan format;… Read More »

The post AERONAUTICAL INFORMATION OFFICER – 7 POST – TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Tanzania yaitaka dunia kuiondolea vikwazo vya kuichumi Zimbabwe bila masharti

Na Mwandishi wetu,
Tanzania imelaani vikali vikwazo ilivyowekewa nchi ya Zimbabwe na kuitaka dunia kuiondolea nchi hiyo vikwazo hivyo bila masharti kwani haviaathiri tu Zimbabwe bali huathiri pia nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).
 
Kauli ya kulaani vikwazo hivyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) wakati alipokuwa akiwasilisha mada katika kongamano maalum kuhusu "vikwazo vya kiuchumi na hatma ya Afrika: Uzoefu wa Zimbabwe" leo Jijini Dar es Salaam.
 
Prof. Kabudi alisema kuwa kitendo cha dunia kuiwekea vikwazo nchi ya Zimbabwe, hakuiathiri tu Zimbabwe bali hata nchi wanachama wa SADC. 

"Tulikubaliana katika mkutano wetu wa mwezi Augosti kuwa leo tarehe 25/10/2019 kuiambia dunia kuiondolea Zimbabwe vikwazo vya kiuchumi ilivyoviwekea bila masharti..…leo siyo siku ya kuomba wala kukumbushana bali leo ni siku ya kuiambia dunia rasmi iiondolea Zimbabwe vikwazo vya kuichumi" Alisema Prof. Kabudi
 
Waziri Kabudi aliongeza kuwa "vikwazo ilivyowekewa Zimbabwe ni batili na kama Marekani na Umoja wa Ulaya wana hoja ya msingi wapeleke azimio katika baraza kuu la umoja wa mataifa na ndiyo maana katika mkutano wa SADC tuliazimia kulaani vikali Zimbabwe kuwekewa vikwazo vya kiuchumi na kuitaka dunia kuiondelea Zimbabwe vikwazo hivyo bila masharti,".
 
Pia tunasahau sababu ya msingi iliyoifikisha Zimbabwe ktk maamuzi iliyoyachukua, maamuzi hayo kiini chake kikubwa na suala la ardhi ambapo suala la ardhi ni miongozni mwa masuala ambaya hadi Zimbabwe inapata uhuru lilikuwa halijapatiwa ufunguzi. 
 
Kwa mujibu wa Prof. Kabudi, mzizi wa mambo yote haya ni sheria ya kibaguzi iliyopitishwa na waingereza kwa kusingizia kuwa wameipa Zimbabwe utawala wa ndani mwaka 1923 lakini wao walibaki na mamlaka yote juu ya ardhi. Sheria ile ilikuwa ya kibaguzi kwani ilichukua zaidi ya nusu ya ardhi yote ya Zimbabwe.
 
"Ni wajibu wetu sisi kama Tanzania kuendelea kusimama na Zimbabwe katika kuhakikisha kuwa ni jukumu letu sote kuhakikisha kuwa Zimbabwe inaondolewa vikwazo vya kiuchumi ilivyowekewa" Alisema Waziri Kabudi na kuongeza kuwa vikwazo hivyo haviiathiri tu Zimbabwe kiuchumi bala hata nchi wanachama wa SADC wanaathirika hivyo tunaitaka dunia kuindolea Zimbabwe vikwazo hivyo.
 
Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamiii, Jinsia na Wazee, Prof. Jingu alisema kuwa diplomasia ya uchumi imeiwezesha Tanzania kuingia katika uwekezaji, kusaini mkataba, msaada au masoko hivyo tunapaswa kuhakikisha kuwa masuala ya kiuchumi yanapewa uzito wa hali ya juu.
 
"Vita ya kiuchumi imekuwa na athari mbalimbali kwa wananchi kijamii, kisiasa na kiuchumi kwa ujumla….vita hii ya Zimbabwe kuwekewa vita ya kiuchumi imeleta athari nyingi baadhi ni kukusekana kwa maji safi na salama, kukosekana kwa nishati ya uhakika na ongezeko la mfumuko wa bei ambao umeathiri si tu Zimbabwe, bali hata nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC). 
 
Nae Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango alisema kuwa vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Zimbabwe vimesababisha anguko kubwa na adha kwa wanachi masikini tena wasio na hatia hivyo ni vyema Afrika itambue kuwa vikwazo hivi vinaweza kutumika kama fursa ya kukuza biashara na uwekezaji miongoni mwa nchi za Afrika. 
 
"Ni muhimu nchi zetu za Afrika zifanye uchambuzi mapema ili kubaini maeneo ambayo ya kimkakati ambayo ni dhaifu na yanaweza kuwekewa vikwazo, na moja ya eneo hilo ni umiliki wa hisa katika makampuni hasa yale makubwa ya kimkakati ili tuweze kuchukua hatua stahiki za kujihami kwa kushirikisha sekta binafsi," Alisema Dkt. Mpango
 
Aliongeza kuwa, vikwazo dhidi ya Zimbawe vimewekwa kimabavu kwani havikufuata taratibu, hivyo ni wajibu wetu sisi kama nchi za SADC kusimama na Zimbabwe kuhakikisha kwamba Wazimbabwe wanarudishiwa ardhi yao na kuondolewa vikwazo vya uchumi.
 
Awali, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. William Anangisye alisema kuwa Zimbabwe inakabiliwa na vikwazo vya kiuchumi kutokana na maazimio yaliyochukuliwa na nchi za Uingereza, Marekani na Umoja wa Ulaya mwaka 2001. 
 
"Vikwazo hivi vimeathiri sana uwezo wa Serikali ya Zimbabwe kiuchumi hususani fursa za mikopo, kupata nafuu ya madeni, na zaidi kupata uwezo wa kutoa huduma kwa jamiii. Zimbabwe inapita katika kipindi kigumu cha msukosuko wa kiuchumi uliogubikwa na mfumuko wa bei, upungufu mkubwa wa bidhaa, chakula na huduma muhimu katika jamii" Alisema Prof. Anangisye
 
Kwa mujibu wa Prof. Anangisye vikwazo vya kiuchumi vipo katika makundi ambayo ni vikwazo vya biashara ambavyo vinalenga mauzo ya nje na manunuzi ya bidhaa za nchi kama ambavyo vilivyowahi kuwekwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, vikwazo vya kifedha ambavyo vinalenga sekta, taasisi na mfumo mzima wa kifedha ikiwemo misaada, mikopo na mfumo mzima wa fedha za kigeni, na vikwazo vyenye malengo maalum yaani " Targerted Sanctions".
 
Kongamano hilo lilihudhuriwa na vongozi mbalimbali waandamizi wa Serikali, vyma vya siasa na ujumbe wa balozi za nchi mbalimbali hapa nchini. 
 
Katika kongamano hili, Serikali ya Chini Ikongozwa na Balozi wake nchini Tanzania, Balozi Wang Ke alisema kuwa serikali ya China inasimama pamoja na nchi za SADC katika kuhakikisha kuwa Zimbabwe inaondolewa vikwazo vya kiuchumi.
Mwisho….




Share:

ELECTRICAL ENGINEER II – 1 POST – TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY

ELECTRICAL ENGINEER II – 1 POST Employer: TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY Date Published: 2019-10-25 Application Deadline: 2019-11-07 JOB SUMMARY: NA DUTIES AND RESPONSIBILITIES: i.To assist in carrying out minor electrical works repairs and other facilities; ii.To assist in preparing requirements of maintenance and repairs; iii.To assist in preparing sketches and cost estimates for materials and services; iv.To provide assistance during emergencies… Read More »

The post ELECTRICAL ENGINEER II – 1 POST – TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

RECORDS MANAGEMENT ASSISTANT II AT TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY – 1 POST

RECORDS MANAGEMENT ASSISTANT II.. – 1 POST Employer: TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY Date Published: 2019-10-25 Application Deadline: 2019-11-07 JOB SUMMARY: NA DUTIES AND RESPONSIBILITIES: i.To prepare file Index; ii.To maintain records/ documents in the registry; iii.To file, dispatch and cross check correspondences; iv.To maintain diary and records for files movements; v.To check and cross check mails, claims and returns; vi.To receive… Read More »

The post RECORDS MANAGEMENT ASSISTANT II AT TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY – 1 POST appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Tangazo la Nafasi 16 za Kazi toka Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)

On behalf of Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA), Public Service Recruitment Secretariat invites qualified Tanzanians to fill 16 vacant posts mentioned below.

1.0 THE TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY, (TCAA)
The Tanzania Civil Aviation Authority, (TCAA) was established by the enactment of the Tanzania Civil Aviation Authority Act 2003 Cap 80 (R.E 2006) to regulate the civil aviation industry in the United Republic of Tanzania in order to ensure effective implementation of Standards and Recommended Practices (SARPs) as provided in the Annexes of the International Civil Aviation Organization (ICAO). The Authority is also responsible for economic regulation of the activities of persons and institutions providing air transport services and aeronautical airport services. In addition the Authority provides air navigation services in Tanzania.

1.1 AIRWORTHINESS DEVELOPMENTAL INSPECTOR - 1 POST
1.1.1 DUTIES AND RESPONSIBILITIES
i. To assist in enforcement of regulatory requirements and report deficiencies to the Supervisor;
ii. To assist in accident/incident and complaint investigations;
iii. To assist in recertification of air operators and Approved Maintenance Organizations;
iv. To assist in the review of manuals (maintenance, flight) and other documents associated with certification requirements of air operators for accuracy and compliance with Civil Aviation Regulations;
v. To assist in conducting inspections and evaluation of Approved Maintenance Organizations under supervision of a qualified inspector;
vi. To assist in evaluation of applications for issue/renewal of certificates of airworthiness;
vii. To assist in evaluation of applications for AME license issue/extension applications in accordance with procedures in Airworthiness Orders as specified in the Civil Aviation (Personnel Licensing) Regulations and Annex 1 to ICAO convention;
viii. To assist in carrying out continuous programmed surveillance to aircraft operations, air operators and approved maintenance organizations and make appropriate recommendations to the supervisor; and
ix. To assist in carrying out accident and incident investigations in accordance with procedures.

1.1.2 QUALIFICATIONS AND EXPERIENCE
i. Bachelor Degree either in Aeronautical, Mechanical, Electrical, Electronic or Telecommunication. Must have (3) three years working experience in an Aircraft Maintenance Organization as Aircraft Maintenance Engineer.
ii. For graduates, except for Aeronautical Engineers, they should have attended or be provided with a basic training in Aircraft Maintenance Engineering;
iii. For equivalent professional qualifications they should possess Aircraft Maintenance Engineer’s Licenses with ratings or appropriate approvals, commensurate with their job responsibilities, i.e., Category A or C (Mechanical) Licences with airframe and power plant ratings, category X or R (Avionics) Licence with ratings in Electrical, Instrument or Radio.

1.1.3 REMUNERATION
Attractive remuneration package in accordance with the institutions salary TCAA.SS 10

1.2 AERODROME AND GROUND AIDS DEVELOPMENTAL INSPECTOR - 2 POSTS
1.2.1 DUTIES AND RESPONSIBILITIES
i. To conduct guided safety oversight of aerodromes including certification and licensing of aerodromes;
ii. To assist assessment of applications for the initial and renewal of Aerodrome certificates and licences; and
iii. To perform any other related duties as may be assigned by immediate supervisor.

==>>Endelea Nalo kwa Kubofya Hapa


Share:

Assistant Lecturers at Job SJUT ( 8 positions )

St John’s University of Tanzania (SJUT) is owned by the Anglican Church of Tanzania (ACT). SJUT is a relatively young but dynamic university aspiring to become a global player in the provision of higher education. SJUT is committed to a culture of quality, excellence and absolute integrity in the context of Biblical values. The University is seeking to… Read More »

The post Assistant Lecturers at Job SJUT ( 8 positions ) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

WATOTO 1000 WANAOZALIWA NCHINI, WATATU HUZALIWA NA ULEMAVU WA KICHWA KIKUBWA NA MGONGO WAZI

Share:

DAKTARI MATATANI BAADA MTOTO KUZALIWA BILA USO,PUA WALA MACHO

Daktari mmoja amesimamishwa kazi nchini Portugal baada ya mtoto kuzaliwa bila pua, macho na sehemu ya fuvu la kichwa.

Wazazi wa mtoto Rodrigo hawakuwa na ufahamu kuhusu maumbile hayo ya mtoto wao hadi alipozaliwa mapema mwezi huu.
Maafisa wa baraza la matibabu waliamua kumsimamisha kazi daktari Artur Carvalho kufuatia madai ya uzembe.

Imebainika kwamba malalamishi mengine zaidi yanayohusu watoto wengine, yaliyofanyika zaidi ya muongo mmoja iliyopita pia yamewasilishwa mbele ya baraza hilo.

Ripoti ya visa hivyo , zilizoelezewa na vyombo vya habari vya Ureno vimezua hisia kali.

Daktari Carvalho alikua hajatoa tamko lolote hadharani kuhusu madai yoyote na BBC imeshindwa kuwasiliana naye moja kwa moja

Ni nini kilichomkumba Rodrigo?

Rodrigo alizaliwa tarehe 7 mwezi Oktoba katika hospitali ya Sao Bernardo mjini Setubal , takriban kilomita 40 kusini mwa Lisbon.

Mamake alikuwa chini ya uangalizi wa daktari Carvalho akipigwa picha mara tatu katika kipindi chake cha uja uzito katika kliniki moja ya kibinafsi na wazazi hao wanasema kwamba daktari huyo hakuonesha wasiwasi wowote kuhusu afya ya mtoto huyo akiwa tumboni.

Mama huyo baadaye alifanyiwa uchunguzi wa skani yenye maelezo zaidi kwa kutumia mfumo wa 5D katika kliniki tofauti akiwa na ujauzito wa miezi sita.

Wakati wa skani hiyo uwezekano wa mtoto huyo kuwa na umbo lisilo la kawaida uliwasilishwa , lakini daktari Carvalho anadaiwa kupuuza hofu iliyojitokeza kufuatia uchunguzi huo mpya wa kina

Amenukuliwa na akielezea kwamba mara nyengine wakati wa utafiti baadhi ya sehemu za uso wa mtoto wao akiwa tumboni zilikuwa hazionekani , hasa wakati uso wa mtoto umeshikana na tumbo la mama, shangazi lake Rodrogo , alikielezea chombo cha habari cha AFP.

Baada ya kuzaliwa kwa Rodrigo na umbo lake lisilo la kawaida kubainika, wazazi wake waliambiwa ataishi kwa saa chache.

Hata hivyo baada ya wiki mbili , mtoto huyo bado yuko hai chini ya usimamizi wa hospitali.

Wazazi wake wamewasilisha malalamishi kuhusu Daktari Carvalho kwa afisi ya mwendesha mashtaka wa Ureno.

Je malalamishi mengine ni yapi?

Kufuatia hisia kali zilizotokana na kisa cha mtoto Rodrigo, malalamishi mengine dhidi ya Daktari Carvalho yamefichuka.

Takriban malalamishi sita ya kiafya ,tokea mwaka 2013 kulingana na maafisa wa afya ,yamewasilishwa dhidi yake.Wazazi wengine wamekuwa wakitoa hadithi zao kuhusu visanga walivyopitia

Wazazi wengine wamejitokeza kusimulia visa vyao kwa vyombo vya habari vya Ureno kufuatia hatua ya daktari huyo kushindwa kubaini maswala ya kiafya ya mtoto huyo

Katika kisa kimoja mtoto alizaliwa 2011 akiwa na uso usio wa kawaida, mbali na miguu na uharibifu mkubwa wa ubongo.

Mama huyo kwa jina Laura Afonso, aliambia gazeti la Publico kwamba aliwasilisha malalamishi ya uhalifu dhidi ya daktari huyo kabla ya mwemdesha mashtaka kufutilia mbali kesi hiyo.

Sasa akiwa na umri wa miaka minane, hata baada ya mtoto wao kufanyiwa operesheni kadhaa lakini hawezi kuzungumza wala kutembea, alisema.

Kesi nyengine ya kihalifu ambapo mtoto alifariki miezi baada ya kuzaliwa 2007 pia ilitupiliwa mbali kabla ya kufika awamu ya kuamuliwa, hii nikulingana na gazeti hilo la Publico.
Je kisa hicho kimevutia hisia gani?

Kashfa hiyo inayozidi kuwa kubwa imezua hisia kali nchini Ureno.

Imezua maswali kuhusu jinsi mfumo wa afya nchini humo unavyofanya kazi mbali na uwasilishaji wa malalamishi.
Chanzo- BBC
Share:

SERIKALI, SIDA, UNESCO WAANZA MAANDALIZI YA RIPOTI YA KITAIFA UANUAI WA KITAMADUNI

 Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo (katikati) akisalimiana na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos mara baada ya kuwasili kwenye warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Balozi wa Sweden nchini Mh. Andres Sjoberg.
 Afisa Mtendaji Mkuu COSOTA ambaye pia ni Mtaalamu wa Taifa wa mradi unaolenga kutekeleza makubaliano ya UNESCO ya mwaka  2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Tamaduni Anuwai, Bi. Doreen Sinare akitambulisha meza kuu (hawapo hewani) wakati wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo akitoa hotuba kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe wakati wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos akitoa salamu za UNESCO wakati wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa Sweden nchini Mh. Andres Sjoberg akitoa salamu za SIDA wakati wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo (katikati) akimkabidhi Afisa Mtendaji Mkuu COSOTA na Mtaalamu wa Taifa wa mradi unaolenga kutekeleza makubaliano ya UNESCO ya mwaka  2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Tamaduni Anuwai, Bi. Doreen Sinare cheti cha ushiriki wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Balozi wa Sweden nchini Mh. Andres Sjoberg (kushoto) pamoja na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos (kulia).
 Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo (katikati) akimkabidhi  Bw. Maximilian Chami kutoka Tume ya Taifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (NATCOM-Unesco) cheti cha ushiriki wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Balozi wa Sweden nchini Mh. Andres Sjoberg (kushoto) pamoja na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos (kulia).
 Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo (katikati) akimkabidhi Meneja wa Programu wa Taasisi ya Culture and Development East Africa (CDEA), Bw. Mandolin Kahindi cheti cha ushiriki wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Balozi wa Sweden nchini Mh. Andres Sjoberg (kushoto) pamoja na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos (kulia).
 Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo (katikati) akimkabidhi Mwakilishi kutoka COSOTA Bw. Zephania Lyamula cheti cha ushiriki wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Balozi wa Sweden nchini Mh. Andres Sjoberg (kushoto) pamoja na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos (kulia).
 Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo (katikati) akimkabidhi Afisa Uhusiano wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Bi. Mwamini Mohamed cheti cha ushiriki wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Balozi wa Sweden nchini Mh. Andres Sjoberg (kushoto) pamoja na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos (kulia).
Baadhi ya washiriki wakiwasilisha kazi za vikundi wakati wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya washiriki waliohudhuria warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo katika picha ya pamoja na washiriki wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam.


Na Mwandishi Wetu
SERIKALI ya Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Utamaduni, Elimu, Utamaduni na Sayansi la Umoja wa Mataifa (UNESCO) wamezindua mafunzo ya kuandaa ripoti ya kitaifa ya Mkataba wa UNESCO wa mwaka 2005.

Mkataba huo ambao serikali ya Tanzania umetia saini mwaka 2011 unazungumzia kulinda na kuendeleza uanuai wa kujieleza kiutamaduni.

Kwa mujibu wa matakwa ya mkataba huo kila baada ya miaka mine mataifa yanayotakiwa kuandika taarifa kuelezea utekelezaji wa mkataba huo. Mengi ya mataifa ikiwamo Tanzania haijawahi kuandika  taarifa hiyo.

Kwa kawaida taarifa hiyo ni mchanganyiko wa taarifa za serikali na wadau wengine wakiwemo wa taasisi zisizo za kiserikali (AZAKI).

Fedha za kufanyia mafunzo hayo na kuandika taarifa zimetolewa na Sweden kupitia Mfuko wake wa Maendeleo (SIDA) chini ya uratibu wa UNESCO.

Taarifa hiyo ikishakamilika inatarajiwa kujadiliwa na wadau na kupelekwa serikalini ambako nako itapitiwa na kufikishwa UNESCO.

Akisoma hotuba ya ufunguzi wa mafunzo hayo kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu nchini Dk. Kiagho Kilonzo, alisema kwa sasa Tanzania ipo tayari kwa taarifa hiyo ndio maana imeunda kamati na kuanza mafunzo.

Kamati hiyo ya kuandika Ripoti inaongozwa na Robert Mwampembwa ambaye ikisimamiwa na Doreen Sinare, Ofisa mtendaji Mkuu wa COSATA ambaye ndiye mtaalamu wa mradi.

Kwa mujibu wa Balozi wa Sweden nchini Andres Sjoberg, ufadhili wa taifa hilo kwa nchi 16 zinazotakiwa kuandika utekelezaji wa mkataba huo umelenga kuhakikisha kuwa kuna uhuru wa wasanii kujieleza kiutamaduni na hasa wanawake.

Alisema kwa sasa dunia sio kijiji bali kutokana na mifumo ya upashanaji wa habari kuzidi kuimarika dunia imekuwa ni moja na hivyo masuala ua kujieleza yanabaki kuwa wazi kila mahali.

Naye Dk. Harrison Mwakyembe alisema kwa sasa Tanzania iko vizuri kutokana na kuridhia mkataba huo wa 2005 ambao lengo lake kubwa ni kutengeneza fursa kwa wasanii kuwa karibu na soko la dunia.

Aidha alisema kwamba nia kubwa ya makubaliano hayo ni kulinda uanuai wa kujieleza kiutamaduni na hivyo kutengeneza mazingira ya kukua kwa utamaduni kwa manufaa ya watu wote.

Kwa mujibu wa Dk. Mwakyembe ni matarajio yake kwamba ifikapo Aprili mwakani taarifa hiyo itakuwa imekamilika na tayari kutumika na tasnia ya utamaduni na ubunifu na dunia pia.

Naye Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO Dar es Salaam, Tirso Dos Santos,  alisema kwamba taarifa ya Tanzania itaunganishwa na mataifa mengine ili kuelezea dunia inavyoendelea katika kutekeleza matakwa ya mkataba.

"Sote tunajua kwamba Tanzania ni kitovu cha ubunifu na hasa kwa kuwa na matamasha mbalimbali hali inayodhirisha umuhimu wa mradi huu kwa ajili ya maendeleo maendelevu ", alisema mwakilishi huyo wa UNESCO ambapo aliyataja matamasha makubwa ya filamu nchini ikiwamo ya ZIFF na Azam kama moja ya uanuai wa utamaduni.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger