Monday, 19 August 2019

Waziri wa Habari Dr Harrison Mwakyembe Apongeza Vyombo Vya Habari Kwa Kutangaza Vyema Mkutano Wa 39 Wa SADC

Na Shamimu Nyaki WHUSM- DODOMA
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amevipongeza Vyombo vya Habari nchini kwa kazi kubwa ya kiuzalendo na weledi wa hali ya juu katika kutangaza Mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) uliomalizika jana Jijini Dar es Salaam.

Dkt. Mwakyembe ametoa pongezi hizo jana Jijini hapo ambapo amesema kuwa uandishi wa habari wa kujenga na kukosoa ambao una lengo la kurekebisha unahitaji kupongezwa kwakua unasaidia jamii na Serikali katika kuleta maendeleo ya haraka kwa Taifa.

“Waandishi wa habari mbali na kuutangaza Mkutano wa 39 wa SADC lakini pia wametumia taaluma yao kutangaza fursa za uwekezaji zinazopatikana hapa nchini kupitia sekta mbalimbali ikiwemo Uwekezaji katika viwanda, Utalii, Uchukuzi na nyinginezo,” alisema Dkt. Mwakyembe.

Ameongeza kuwa Uwenyekiti wa Tanzania ambao unaendeshwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli umeleta ari na matumaini mapya ambayo yatasaidia nchi wanachama kuondoa vikwazo vingi vya kibiashara na mawasiliano ya karibu baina ya nchi wanachama  na kujenga ustawi wa uchumi kwa nchi hizo.

Aidha Mhe. Mwakyembe  amesema kuwa baada ya lugha adhimu ya Kiswahili kutangazwa rasmi kuwa miongoni mwa lugha nne zinazotumika ndani ya Jumuiya hiyo, amewataka Watanzania kutumia fursa hiyo kutangaza bidhaa za lugha hiyo ikwemo uandishi wa vitabu vya kiada, ufundishaji wa lugha hiyo, kuuza Sanaa zinazotokana na lugha hiyo kwa nchi wanachama wa jumuiya hiyo.

Mkutano wa Jumuiya ya Kusini mwa Afrika SADC kwa Wakuu wa nchi na Viongozi wa Serikali umefanyika kuanzia Agosti 17- 18,2019 ambapo mambo mbalimbali yanayohusu nchi hizo yalijadiliwa ikwemo namna bora ya kuimarisha biashara ndani ya nchi hizo  ambapo Tanzania imeteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia mwezi Agosti mwaka huu.


Share:

Watatu Washitakiwa Kwa Mauaji ya Mwanamke wa Miaka 55 Wakimtuhumu ni Mchawi

Jeshi la Polisi Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora limewakamata Watu watatu na kuwafikisha Mahakama ya Wilaya ya Igunga   kwa tuhuma za mauaji ya Mama wa miaka 55, Veronica Makumbi, baada ya kumtuhumu kuwa ni Mchawi

Watuhumiwa hao wanadaiwa kumuua mwanamke huyo July 28 mwaka huu saa 6:30 usiku.

Waliokamatwa ni Sung'hwa Ngasa, Willson Sunhnwa na Sunhwa Zumbi wakazi wa kitangili.

Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Elimajid Kweyamba, mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Igunga, Lydia Ilunda, alidai washtakiwa wote kwa pamoja walitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 196 kanuni ya adhabu sura ya 16 mapitio ya 2002. 

Kesi imeahirishwa hadi Agosti 29, itakapotajwa tena na washtakiwa walipelekwa mahabusu na hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza shauri hilo..


Share:

Mahakama yaamuru ushahidi wa video kesi ya Freeman Mbowe na viongozi wengine wa CHADEMA Uonyeshwe

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeamuru kuonyeshwa kwa video iliyopokelewa mahakamani hapo kama ushahidi katika kesi ya uchochezi inayowakabili viongozi tisa wa Chadema, akiwemo Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, ionyeshwe .

Uamuzi huo umetolewa  Agosti 19, 2019 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba, baada ya kupitia hoja za upande zote mbili.

Uamuzi huo unatokana na upande wa utetezi kupinga video hiyo isionyeshwe mahakamani hapo kutokana na upande wa mashtaka kushindwa kuandaa mazingira wezeshi.

Akitoa uamuzi huo, Hakimu Simba alisema sababu zilizotolewa na upande wa utetezi haina mashiko, hivyo video hiyo inatakiwa ionyeshwe katika ukumbi wa Tehama uliopo katika mahakama ya Kisutu.

Hata hivyo hakimu huyo ameiairsha  kesi hiyo kwa muda wa dakika 20 kwa ajili ya maandalizi ya kuangalia video.

Video hiyo inayosemekana ilirekodiwa wakati wa ufungaji wa kampeni za uchaguzi mdogo  wa ubunge wa Kinondoni kwa tiketi ya Chadema Februari 16 mwaka 2018, inadaiwa kubeba matukio yanayomuonyesha Mbowe na wenzake tisa wakiwa kwenye mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi huo, na kwamba ina uhusiano na kesi hiyo.


Share:

Uhusiano Kati Ya Punyeto Na Kusinyaa Kwa Maumbile Ya Kiume

Zipo sababu kuu 2 kwanini wanaume walio jihusisha na punyeto kwa muda mrefu maumbile yao husinyaa na kuwa kama ya mtoto.

SABABU YA KWANZA: Tendo la kujichua linapo fanyika kwa muda mrefu huathiri na kuharibu misuli ya uume na hivyo kusababisha kujengeka kwa mafuta na tishu zisizo vutika kwenye mishipa ya ATERI.

Kujengeka kwa mafuta na tishu zisizo vutika kwenye mishipa ya ateri husababisha mambo makuu mawili. Kwanza huzuia mishipa ya ateri kupanuka na kuongezeka.

KUPANUKA NA KUONGEZEKA KWA MISHIPA YA ATERI NI JAMBO MUHIMU SANA KATIKA UKUAJI WA MAUMBILE YA KIUME. Mishipa hii inapo shindwa kupanuka na kuongezeka huathiri ukuaji wa maumbile ya kiume na hivyo kusababisha maumbile ya mhusika kudumaa.

Lakini pili, kujengeka kwa mafuta na tishu zisizo vutika ndani ya mishipa ya ateri huzuia na kuathiri kutiririka kwa damu kwenye misuli ya uume. Mambo haya mawili yanapo tokea huathiri uzalishaji wa homoni zinazo husika na kuchochea ukuaji wa maumbile ya kiume. Homoni hizi hujulikana kitaalamu kama HGH na huzalishwa kwenye ini.

Hali hii inapo tokea basi maumbile ya kiume ya mhusika husinyaa na kudumaa kiasi cha kuyafanya yaonekane kama ya mtoto mdogo.

SABABU YA PILI: Upigaji wa punyeto huathiri utendaji wa ini. Na katika ini ndimo zinamo zalishwa homoni ziitwazo HGH ambazo hu husika na kufanya kazi ya kuchochea ukuaji wa maumbile ya kiume.

Kinacho fanya ini la mwanaume anae jihusisha na.punyeto lishindwe kuzalisha homoni za HGH ni mwili wa mhusika kukosa kiwango cha kutosha cha nishati kinacho hitajika katika uzalishaji wa homoni hizo. Nishati hii hupotea kwa wingi wakati wa tendo la upigaji punyeto.

Mwanaume anae piga punyeto hutumia nguvu, akili na nishati nyingi sana . Nishati hii ambayo inahitajika mwilini ili itumike katika kazi mbalimbali ikiwemo uzalishaji wa homoni za HGH kwenye ini inatumika kwenye tendo la upigaji punyeto na hivyo kupotea bure.

Kibaya zaidi ni kwamba waathirika wengi wa punyeto huanza kujihusisha na punyeto wakati wa balehe. Na ni katika kipindi hiki hiki cha balehe ndio kipindi ambacho homoni za HGH huzalishwa kwa wingi na huhitajika kwa wingi mwilini katika kufanya kazi ya kuchochea ukuaji wa maumbile ya kiume.

Matokeo yake ini linashindwa kufanya kazi ya kuzalisha homoni hizo kwa sababu ya kukosa kiwango cha nishati kinacho hitajika ili kuweza kuzalishwa kwa homoni hizo.

Kukosekana kwa homoni hizo hupelekea maumbile ya kiume ya mhusika kushindwa kuongezeka ambako huenda sambamba na kusinyaa, kulegea na kunywea ndani kiasi cha kuyafanya yaonekane kama ya mtoto.

NINI SULUHISHO LA MAUMBILE YA KIUME YALIYO ATHIRIKA KWA PUNYETO: Mwanaume ambae maumbile yake ya kiume yame athiriwa na upigaji punyeto wa muda mrefu anatakiwa apate tiba maalumu ya asili ambayo INATIBU na KUPONYESHA kabisa tatizo la maumbile ya kiume ambayo yameathirika kwa punyeto. Tiba hii ya asili mbali na kufanya kazi ya KUREFUSHA na KUNENEPESHA maumbile ya kiume ambayo yamesinyaa kwa ajili ya punyeto lakini pia INATIBU na KUPONYESHA kabisa tatizo la ukosefu na upungufu wa nguvu za kiume linalo tokana na kufanya punyeto kwa muda mrefu.

JINSI  YA  KUPATA  DAWA  HII
Kupata  dawa  hii  fika  katika  duka  la  kuuza  dawa  za  asili. Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

kwa  wateja  wetu  waliopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  ambao  hawana nafasi  ya  kufika  dukani  kwetu  tunayo  huduma  ya  kuwapelekea dawa  mahali  walipo  (  HOME  &  OFFICE  DELIVERY)  na  kwa  wateja  wetu  waliopo  nje  ya  mkoa  wa  Dar Es  Salaam, tunatumia  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  mbalimbali.

WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA : 0693 005 189.

Tutembelee  kwenye  site  yetu :  www.neemaherbalist.blogspot.com

Tu  follow  Instagram kupitia :  www.instagram.com/Neema Herbalist  Official.


Share:

Watu 63 wauawa kwenye mlipuko ulitokea kwenye ukumbi wa harusi

Takriban watu 63 wameuawa na wengine zaidi ya 180 kujeruhiwa jana usiku baada ya kutokea mlipuko wa kujitoa muhanga kwenye ukumbi wa harusi magharibi mwa mji mkuu wa Afghanistan, Kabul.

Ikithitbitisha tukio hilo polisi ya Afghanistan imesema mlipuko ulitokea saa 4.40 usiku ndani ya ukumbi wa harusi wa Shahr-e-Dubai huko Kabul.

Idadi ya vifo huenda ikaongezeka kwani watu kadhaa wapo kwenye hali mahututi.

Hadi sasa hakuna mtu au kundi lolote lililotangaza kuhusika na tukio hilo.


Share:

Mlipuko wa lori la mafuta waasababisha vifo vya watu wengi Uganda

Watu kadhaa wamekufa baada ya lori la mafuta kulipuka jana kwenye mtaa wa Rubirizi, magharibi mwa Uganda.

Msemaji wa polisi wa mkoa wa Great Bushenyi, Marshal Tumusiime, amesema, mlipuko huo ulitokea baada ya lori hilo kupinduka, kulipuka na kuwaka moto katika kituo cha biashara cha Kyambura, kando na Barabara kuu ya Kasese-Mbarara.

Moto huo ulienea katika nyumba na maduka kadhaa na kuteketeza vitu. Onesmus Nkesiga ambaye duka lake lilikumbwa na moto huo, alisema  amepoteza bidhaa zenye thamani ya USh 20 milioni.

Wazima moto ambao walifika katika eneo hilo saa moja baada ya tukio, wameokoa vitu kadhaa kwenye baadhi ya maduka.


Share:

Watatu Watiwa Mbaroni kwa kukutwa na vipande 10 vya madini bandia ya dhahabu

Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga linawashikilia watuhumiwa watatu kwa tuhuma za kukutwa na vipande 10 vya madini bandia aina ya dhahabu wakiwa kwenye harakati za kuyauza wilayani Kahama.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari jana, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga, Richard Abwao, alisema watuhumiwa hao walikuwa na mtambo wa kufyatua madini hayo bandia ya dhahabu ambayo huyauza wilayani Kahama, Geita pamoja na Mwanza.

Alisema katika misako ya uhalifu ambao waliufanya mwezi uliopita mkoani humo, walifanikiwa kukamata watuhumiwa 73 wa matukio mbalimbali ya uhalifu, wakiwamo wezi, wauaji, pamoja na watu watatu wa utengenezaji wa madini bandia ya dhahabu.

Alisema pia walifanikiwa kukamata watuhumiwa wanne waliohusika na matukio ya mauaji ya Kalekwa Shiku (50) mkazi wa kijiji cha Mishepo, Shinyanga vijijini, ambaye aliuawa kwa kufunikwa mfuko usoni, kufungwa mawe miguuni, na kisha kuzamishwa kwenye bwala la maji na kufariki dunia.

Alisema watuhumiwa hao walitekeleza mauaji hayo Juni 6, mwaka huu, kwa madai ya tamaa ya kutaka kujipatia ng'ombe tisa kwa mwanamke huyo na baada ya kugoma ndipo wakatekeleza mauaji hayo.


Share:

Waliofariki Ajali ya Lori la Mafuta Morogoro Wafika 97

Idadi ya waliofariki katika ajali ya Lori iliyotokea mkoani Morogoro imezidi kuongezeka na kufikia 97 baada ya majeruhi wawili kati ya 20 waliokuwa wamelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam kufarikii dunia.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano MNH, Aminiel Aligaesha amesema majeruhi waliobaki hospitalini hapo ni 18 ambao wote wapo kwenye chumba cha uangalizi maalum (ICU).

Amewataja waliofariki ni Rosijo Mollel (35) aliyefariki jana Jumapili mchana na Neema Chakachaka ambaye amefariki alfajiri ya leo Jumatatu.


Share:

Muhimbili University Selected applicants release dates announced

Muhimbili University of Health and Allied Sciences selection 2019/20 dates – MUHAS selection 2019/20- MUHAS selected applicants 2019/20 dates IMPORTANT ANNOUNCEMENT TO ALL UNDERGRADUATE DEGREE PROGRAM APPLICANTS Muhimbili University of Health and Allied Sciences informs all applicants for undergraduate degree programmes that the window for the first round of application is closed since 10th August 2019. The selection results… Read More »

The post Muhimbili University Selected applicants release dates announced appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Uchumi Wa Ukanda Wa Kusini, Wavutia Ufugaji Wa Kisasa

Na. Edward Kondela
Kutokana na watu wengi kuitikia wito wa serikali kufuga kisasa kwa kuwa na ng’ombe bora wa maziwa, Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha 2019/20 imeweka mikakati ya kuliimarisha shamba lake la kuzalisha Mifugo la Nangaramo lililopo Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara ili kusogeza zaidi huduma hiyo kwa wananchi.

Akizungumza mara baada ya kutembelea shamba la Nangaramo na kujionea mafanikio na changamoto zilizopo katika shamba hilo Mkurugenzi wa Uzalishaji na Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Felix Nandonde amesema wizara imedhamiria kuhakikisha Shamba la Nangaramo linapata ng’ombe bora wa kisasa wa maziwa, ng’ombe wazazi pamoja na kumpeleka mtaalamu katika Kituo cha Uhimilishaji (NAIC) kilichopo Mkoani Arusha kujifunza uhimilishaji ili aweze kutoa huduma katika shamba hilo.

“Shamba linatoa huduma katika mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma nia ya kuleta ng’ombe bora wa kisasa hususan kwa wafugaji ni kupata uzalishaji bora pamoja na wafugaji hao kufuga kisasa, Shamba la Nangaramo ni muhimu sana tutahakikisha mwaka huu wa fedha tunalisaidida ili liweze kutoa tija kwa wananchi kwa kuweza kununua ng’ombe bora na kisasa kutoka katika shamba hili.” Amesema Dkt. Nandonde

Akizungumzia miundombinu ya shamba hilo, Dkt. Nandonde amesema hajaridhishwa na hali ilivyo sasa kwa kuwa mifugo iliyopo shambani hapo ambayo ng’ombe ni 295 na mbuzi 64 bado ni michache na haifugwi katika maeneo yaliyo rasmi ya uchungaji ambapo amesema nia ya serikali katika kipindi cha miaka kumi idadi ya ng’ombe katika shamba hilo ifike Elfu Moja, huku Wizara ya Mifugo na Uvuvi ikiendela na mikakati ya kuboresha zaidi miundombinu ya shamba.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa Shamba la Nangaramo Bw. Salum Kamota amesema kwa sasa shamba hilo limekuwa na mafanikio makubwa kwa kuwa wananchi wengi kutoka Mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma wamekuwa wakihitaji kununua ng’ombe bora na kisasa ili kufuga kwa tija na kupata matokeo mazuri yakiwemo ya upatikanaji wa maziwa mengi kutoka katika ng’ombe hao kwa kuwa shughuli nyingi za kiuchumi zimeongezeka katika mikoa hiyo na kusababisha ongezeko la watu na mahitaji yao.

“Shamba hili ni pekee katika ukanda huu wa kusini hivyo juhudi za haraka zinahitajika kuongeza uzalishaji zaidi wa shamba hili kutokana na mahitaji ya ng’ombe bora wa kisasa katika ukanda huu kutokana na kukua kwa shughuli nyingi za uchumi kwa ukanda huu wa kusini hivyo hamasa ya ufugaji imeongezeka na soko la mazao ya mifugo limekuwa likikua siku hadi siku.” Amesema Bw. Kamota

Shamba la Kuzalisha Mifugo la Nangaramo lililopo katika Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara ni kati ya mashamba matano yanayomilikiwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ambapo yamekuwa yakizalisha ng’ombe bora wa kisasa na kuuza kwa wananchi kwa bei nafuu ili waweze kufuga kisasa na kupata mazao mazuri kutoka katika ng’ombe hao.

Mwisho.


Share:

TRA Yakanusha Habari Inayosambaa Mitandaoni Kuhusu Ajira 500 Kwa Vijana Wa Tanzania

Na Veronica Kazimoto
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekanusha habari inayosambaa katika mitandao ya kijamii ikidai kuwa TRA kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), inatangaza nafasi za kazi 500 za uelimishaji wa namna ya uchangiaji kodi pamoja na ukusanyaji wa Kodi ya Majengo vijijini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania, wananchi wameombwa kuipuuza habari hiyo.

“TRA inakanusha taarifa hiyo na inauomba umma kuipuuza kwa sababu haina ukweli wowote”. Ilifafanua taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imesisitiza kuwa, hata mawasiliano yaliyopo kwenye habari hiyo potofu siyo mawasiliano rasmi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania hivyo wananchi wanatakiwa kuwa makini ili kuepuka kutapeliwa.

Kumekuwepo na taarifa inayosambaa katika mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari "Mamlaka ya Mapato Tanzania (Tanzania Revenue Authority) kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha pamoja na Benki Kuu (BOT)", ikieleza kuhusu TRA kutangaza ajira 500 ambayo imesababisha mamlaka hiyo kukanusha na kuwatahadharisha wananchi kuhusu taarifa hiyo potofu.

TRA imewaomba wananchi kupiga simu bure Kituo cha Huduma kwa Wateja kupitia namba 0800 750 075 au 0800 780 078 au kutuma barua pepe: huduma@tra.go.tz, au kutembelea tovuti ya Mamlaka ya Mapato Tanzania:  www.tra.go.tz. Pia, wanaweza kutuma ujumbe kwa njia ya WhatsApp kwenda namba 0744-233-333 ili kupata ufafanuzi wa masuala yoyote yanayoihusu mamlaka hiyo.

Mwisho.


Share:

Mwandishi Erick Kabendera Arudishwa Rumande Hadi Agosti 30

Wakili Mwandamizi wa Serikali, Wankyo Simon ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa upelelezi wa kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Mwandishi wa Kujitegemea wa Habari za uchunguzi, Erick Kabendera bado haujakamilika.

Simon ameeleza hayo leo Jumatatu Agosti 19, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Agustina Mmbando

Mbali na upelelezi kutokamilika, Pia, hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Augustine Rwizile amepata udhuru.

Kabendera anashtakiwa kwa Makosa matatu ikiwemo kukwepa Kodi kiasi cha Tsh. Milioni 173,247,047.02, Utakatishaji Fedha na kujihusisha na genge la uhalifu Makosa ambayo  hayana dhamana
 
Kesi imeahirishwa hadi Agosti 30, 2019 itakapotajwa tena.


Share:

Gibraltar yakataa ombi la Marekani la kuizuia meli ya Iran

Gibraltar imepinga ombi la Marekani kuikamata tena meli ya mafuta ya Iran ambayo ilikuwa ikiizuia tangu mwezi Julai kwa kudhania kwamba ilikuwa ikisafirisha mafuta Syria.

Marekani iliwasilisha ombi la mwisho siku ya Ijumaa , siku moja baada ya Giraltar kuiachilia meli hiyo ya Grace 1.

Gibraltar imesema kwamba haikuweza kukubali ombi la Marekani kuikamata tena meli hiyo kwa kuwa vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran havina nguvu Ulaya.
 
Meli hiyo tayari imeondoka Gibraltar kulingana na mjumbe wa Iran nchini Uingereza.

Tehran imesema kwamba iko tayari kuyapeleka majeshi yake kuisindikiza meli hiyo ambayo jina lake lilibadilishwa kutoka Grace 1 hadi Adrian Drya 1.

Meli hiyo na wafanyakazi wake 29 kutoka India, Urusi, Latvia na Ufilipino ilikamatwa kupitia usaidizi wa wanamaji wa Uingereza tarehe 4 Julai baada ya serikali ya Gibraltar - eneo linalomilikiwa na Uingereza kusema kwamba ilikuwa ikielekea Syria hatua inayokiuka vikwazo vya Muungano wa Ulaya.

Hatua hiyo ilizua mgogoro wa kidiplomasia kati ya Uingereza na Iran , ambao umeendelea katika wiki za hivi karibuni huku Iran nayo ikiikamata meli iliokuwa ikipeperusha bendera ya Uingereza Stena Impero katika Ghuba.
 
Mamlaka ya Gibraltar iliiwachilia meli hiyo siku ya Alhamisi baada ya kupokea hakikisho kutoka Iran kwamba haitaipeleka mafuta yake nchini Syria.

Idara ya haki nchini Marekani baadaye ikawasilisha ombi mahakamani la kuizuilia meli hiyo kwa msingi kwamba ina uhusiano na jeshi la Iran ambalo imelitaja kuwa kundi la kigaidi.

Gibraltar , katika taarifa yake siku ya Jumapili ilisema kwamba haikuweza kukubali ombi hilo kwa kuwa jeshi hilo la Revolutionary Guard sio kundi la kigaidi kulingana na EU ambalo eneo hilo la Uingereza ni mshirika wake.

Pia ilisema kwamba vikwazo vya Marekani vya kuzuia uuzaji wa mafiuta wa Iran haviwezi kuidhinishwa na EU ikidai tofauti iliopo kati ya Marekani na EU kuhusu Iran.


Share:

HAYA HAPA MAJINA YA WALIOPITISHWA KUANDKISHA DAFTAR LA KUDUMU LA WAPIGA KURA MANISPAA YA SHINYANGA









Share:

UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KUFANYIKA AGOSTI 26 HADI SEPTEMBA 1 SHINYANGA


Kamishina wa Tume ya Uchaguzi ya Taifa nchini Tanzania,Mhe. Balozi Omari Ramadhani Mapuri akifungua mkutano wa Tume na Wadau wa Uchaguzi katika mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kupeana taarifa kuhusu uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura. Picha na Kadama Malunde - Malunde1 blog

 Kamishina wa Tume ya Uchaguzi ya Taifa nchini Tanzania,Mhe. Balozi Omari Ramadhani Mapuri amesema zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura mkoa wa Shinyanga litafanyika kuanzia Agosti 26,2019 hadi Septemba 1,2019.

"Tume inatarajia kuanza uboreshaji wa daftari la wapiga kura kwa awamu ya nne katika mikoa ya Mwanza (halmashauri ya wilaya Kwimba),mkoa wa Shinyanga na mkoani Geita (Halmashauri ya Mji wa Geita,Nyang'wale,Bukombe na Mbogwe) kuanzia Agosti 26 hadi Septemba 1,2019",amesema Balozi Mapuri.

Amefafanua kuwa uboreshaji wa daftari la wapiga kura unafanyika kwa kutumia teknolojia ya kielektroniki ya Biometriki (BVR) ambayo huchukua taarifa za kibaiolojia za mtu na kuzihifadhi katika Kanzidata(Database) kwa ajili ya utambuzi.

"Uboreshaji wa daftari la wapiga kura wa safari hii hautahusisha wapiga kura walioandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapiga kura mwaka 2015 ambao kadi zao hazihitaji marekebisho yoyote ya taarifa.Uboreshaji huu utawahusu wapiga kura wapya ambao wametimiza umri wa miaka 18 na wale ambao watatimiza umri wa miaka 18 siku ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.",amesema Balozi Mapuri.

Amesema uboreshaji huo pia utahusisha watu ambao wamehama kutoka maeneo yao ya awali na kuhamia maeneo mengine ya uchaguzi na wale ambao kadi zao zimeharibika au kupotea na wale ambao wanatakiwa kufutwa kwenye daftari baada ya kupoteza sifa wakiwemo waliofariki dunia.

Amewataka watu wenye sifa ya kujiandikisha wajitokeze kwa wingi ili waandikishwe na wanaohitaji kuboresha taarifa zao wakati ndiyo huu.

Share:

MBUNGE WA IKOLOMANI APATA AJALI

Mbunge wa Ikolomani,Bernard Shinali amepata  ajali ya barabarani siku ya Jumapili, Agosti 18,2019 asubuhi wakati akisafiri kutoka Kakamega akielekea jijini Nairobi baada ya kuhudhuria hafla ya mazishi ya mwanawe wa kiume iliyofanyika Jumamosi

Shinali alikuwa akisafiri jijini Nairobi pamoja na watu wengine wanne wa familia yake wakati gari lake liligongana na matatu, eneo la Lessos kwenye barabara ya Kapsabet -Mau Summit.

Gari hilo lilikuwa limewabeba watu wengine wanne ambao walinusurika na wanapania kuendelea na safari yao baada ya kuandikisha taarifa kwa polisi.

 Hata hivyo, mbunge huyo alithibitisha kuwa familia yake pamoja naye wako salama salimini kupitia njia ya simu.

 Mwanasiasa huyo alikumbana na ajali hiyo wakati alikuwa akielekea jijini Nairobi baada ya kuhudhuria mazishi ya mwanawe wa kiume Chris Masakah, ambaye alikufa maji siku ya Ijumaa, Julai 26, katika jimbo la Arizona, nchini Marekani. 

Masakah alikuwa akihudumu katika jeshi la Marekani kama mwanamaji. 
Share:

TETESI ZA SOKA LEO JUMATATU AGOSTI 19,2019

Mabingwa wa Ufaransa PSG wamefanya mazungumzo na Juventus kuhusu uhamisho wa dau la £73m kumsajili mshambuliaji wa Argentina mwenye umri wa miaka 25 Paulo Dybala. (Mail)

Kiungo wa kati wa Barcelona Philippe Coutinho amewasili nchini Ujerumani ili kukamilisha mkopo wake wa msimu huu kwa mabingwa wa ujerumani Bayern Munich. (Sun)

Paris St-Germain wamemtaka beki wa Real Madrid na Ufaransa Raphael Varane, 26, pamoja na mshambuliaji wa Brazil Vinicius Junior, 19, katika mpango wa kubadilishana wachezaji iwapo wanamuitaji mshambuliaji wa Brazil mwenye umri wa miaka 27 Neymar. (Telefoot - in French)
Barcelona inatumai kumrudisha Neymar Nou Camp , lakini kukiwa na kifungu cha kumnunua.. (Sport - in Spanish)

Aliyekuwa mshambuliaji wa Tottenham Fernando Llorente, 34, anakaribia kujiunga na klabu ya Itali Lazio. Inter Milan, Fiorentina na Napoli pia zina hamu ya kumsaini raia huyo wa Uhispania , ambaye kwa sasa hana klabu. (Corriere Dello Sport - in Italian)

Inter Milan wanataka kumtoa kwa mkopo mshambuliaji wa timu hiyo raia wa Chile Alexis Sanchez, 30, na pia wana hamu na mshambuliaji Llorente na kiungo wa kati wa Barcelona na raia wa Chile Arturo Vidal, 32. (Gazzetta dello Sport - in Italian)
Ajenti wa Sanchez yuko nchini Uingereza kuzungumzia mkopo wake kuelekea Inter Milan. (Sky Italy, via Sky Sports)

Sanchez alikua akifanya mazoezi na United siku ya Jumapili alfajiri.. (The Sun)

Inter Milan inajaribu kuafikia makubaliano ya kumnunua Sanchez lakini United imelazimika kumtoa kwa mkopo ili kutolipa mshahara wake wa £500,000 kwa wiki. (Mirror)
Manchester United wanatarajiwa kuanza mazungumzo ya kumuongezea kandarasi beki Eric Bailey mchezaji mwenye umri wa miaka 25 raia wa Ivory Coast . (Sun)

Paris St-Germain na Bayern Munich huenda zikawasilisha ombi kumnunua kiungo wa kati wa Ujerumani Emre Can, 25, baada ya kuambiwa na mkufunzi wake Maurizio Sarri anahitajiki Juventus. (Tuttosport, via Mail)

Paris St-Germain na Monaco zinafikiria kumpatia ofa kiungo wa kati wa Ufaransa Tiemoue Bakayoko, 25, kwa kuwa muda wake Chelsea unaonekana kwamba umekwisha.. (Daily Express)
Celtic imeipatia ofa Bordeaux kumnunua kiungo wa kati wa Ufaransa Olivier Ntcham . (20 Minutes via Daily Record)

Mkufunzi wa Newcastle Steve Bruce yuko tayari kumrudisha uwanjani mshambuliaji wa England Dwight Gayle, 28, haraka iwezekanavyo. (Newcastle Chronicle)
Jadon Sancho anatarajiwa kuondoka Borussia Dortmund msimu ujao huku klabu hiyo ya Ujerumani ikimtafuta mchezaji atakayechukua mahala pake. (Mail)

Mkufunzi wa Crystal Palace Roy Hodgson anasema kwamba winga wa Ivory Coast Wilfried Zaha, 26, huenda akaondoka katika klabu hiyo msimu huu . (Sun)

Mshambuliaji wa Manchester United na Chile Alexis Sanchez, 30, amekataa uhamisho wa kuelekea Roma, licha ya klabu hiyo ya Old Traford kukubali kulipa kitita kikubwa cha mshahara wake wa £560k kwa wiki.{Mirror)
Hata hivyo Sanchez huenda akaelekea katika ligi ya serie A baada ya Man United kumruhusu kufanya mazungumzo na Inter Milan, ambapo huenda akakubali kupunguza mshahara wake. (Mail)

Liverpool huenda ikafaidika na £18m iwapo mshambuliaji wa zamani wa klabu hiyo na raia wa Brazil Philippe Coutinho, 27, ataelekea Bayern Munich kwa mkopo. (Mail)
Everton imetoa ofa ya kumsaini winga wa Ufaransa Franck Ribery, 36, ambaye yupo huru baada ya kuondoka Bayern Munich baada ya kuhudumu kwa miaka 12 katika klabu hiyo ambayo ndio mabingwa wa ligi ya Bundesliga . (90Min)

Kwengineko, kiungo wa kati wa Portugal Renato Sanches, 21, anataka kuondoka Bayern kwa kukosa muda wa kucheza katika klabu hiyo. (Sport1 - in German)
Mesut Ozil, 30, huenda akaondoka Arsenal na kujiunga na klabu ya DC United iwapo klabu hiyo ya ligi ya MLS inaweza kumshawishi kiungo huyo wa Ujerumani kuhamia Washington. (Star)

Beki wa kulia wa Ivory Coast Serge Aurier, 26, huenda akaondoka Tottenham na kuelekea AC Milan iwapo beki wa timu hiyo Andrea Conti, 25, ataondoka ligi ya Serie A kabla ya kukamilika kwa dirisha la uhamisho la Ulaya. (Calciomercato)

Na mchezaji wa Everton Yannick Bolasie, 30, yuko tayari kurudi katika uwanja wa Goodison Park, huku klabu za Uturuki Besiktas na Trabzonspor zikiwa na hamu ya kumsajili mchezaji huyo wa Congo . (Sun)
Mchezaji wa zamani wa Manchester City na Liverpool Mario Balotelli, 29, anakaribia kujiunga na klabu ya Serie A Brescia. (Sun via La Gazzetta)

Mshambuliaji wa Paris St-Germain Neymar, 27, hakuorodheshwa katika kikosi cha timu hiyo kitakachocheza dhidi ya Rennes kutokana na jeraha na sio kwamba raia huyo wa Brazil anataka kurudi Barcelona. (AS - in Spanish)

Mshambuliaji wa Barcelona Kevin-Prince Boateng, 32, amefichua ni kwa nini Sir Alex Ferguson hakumsajili kujiunga na Manchester United mapema wakati wa kipindi chake cha mchezo. (Goal)
Mchezaji mpya wa Man United Hannibal Mejbri, ambaye aliwasili kutoka Monaco na hawezi kutia kandarasi ya mchezaji wa kulipwa hadi atakapofikisha umri wa miaka 17 January, anataka kuvaa jezi nambari saba Old Trafford. (Mirror)
Mchezaji wa kiungo cha kati wa Ufaransa Paul Pogba, mwenye umri wa miaka 26, bado ana hamu kubwa ya kutaka kuondoka Manchester United kuelekea Real Madrid msimu huu wa joto. (Marca)

Beki wa kati wa England Harry Maguire, mwenye miaka 26, amekataa pendekezo la thamani ya £278,000 kwa wiki kutoka Manchester City badala ya kujiunga na timu hasimu United. (Star)

Meneja wa United, Ole Gunnar Solskjaer amefanya mazungumzo na mchezaji wa kiungo cha kati wa Tottenham, Christian Eriksen kuhusu uwezekano wa uhamisho kuelekea Old Trafford, hatahivyo mchezaji huyo wa miaka 27alikuwa anataka kusubiria uhamisho kuelekea Uhispania. (Manchester Evening News)

Mchezaji wa kiungo cha mbele wa United na timu ya taifa ya Chile, Alexis Sanchez, aliye na umri wa miaka 30, yupo tayari kwa uhamisho kuelekea Italia , wakati Juventus, Napoli, AC Milan na Inter Milan zote zikiwania kumsajili. (Mirror)
Sanchez atashinikiza uhamisho kuondoka Old Trafford kabla ya kufungwa kwa dirisha la uhamisho Ulaya Septemba 2. (Times)

Kwa upande mwingine, United imeshindwa kupata mnunuzi wa Sanchez- anayepokea malipo ya £560,000 kwa wiki. (Mirror)

Juventus bado inatumai kumuondoa mchezaji wa kiungo cha mbele wa Argentina, Paulo Dybala, mwenye umri wa miaka 25, kabla ya muda wa mwisho wa uhamisho Ulaya - licha ya kwamba mabingwa hao wa Italia bado hawajapokea maombi thabiti kwa mchezaji huyo. (Independent)
Watch as Colombian U21 player Anderson Diaz scores a Maradona-like Wonder goal

Mkurugenzi wa michezo wa Paris St-Germain, Leonardo anasema mchezaji wa kiungo cha mbele wa Brazil, Neymar "amefanya makosa" lakini amesisitiza kuwa mchezaji huyo wa miaka 27 yupo Paris "kwa miaka mitatu". (RMC)

Kipa wa Stoke City na timu ya taifa ya England Jack Butland, aliye na miaka 26, ataomba uhamisho kujilazimisha kuwa katika mipango ya meneja wa England, Gareth Southgate kwa ajili ya mashindano ya Euro 2020. (Mail)

Timu ya Brazil Flamengo ilmejitoa katika uhamisho wa mshambuliaji Mario Balotelli baada ya mchezaji huyo wa miaka 29 kuitisha mkataba wa thamani ya £4m. (Mail)
Napoli imekubali kumsaini winga wa Mexico mwenye miaka 23 Hirving Lozano kutoka timu ya Uholanzi PSV Eindhoven. (Voetbal International)

Napoli imekataa ombi la thamani ya £82m kutoka kwa Manchester United kwa mchezaji wa miaka 28 raia wa Senegal Kalidou Koulibaly kabla ya kufungwa kwa dirisha la uhamisho England. (Corriere dello Sport, kupitia Calciomercato)

Winga wa Bournemouth Jordon Ibe anasakwa na mabingwa wa Uskotchi, Celtic. Timu ya Napoli Italia, tayari imemuulizia mchezaji huyo wa miaka 23. (Sun)
Manchester United imewapiga marufuku wachezaji kusaini kumbukumbu au autograph kwa mashabiki katika kiingilio cha uwanja wa mazoezi kutokana na masuala ya usalama.(Telegraph)

Meneja wa West Ham Manuel Pellegrini anasema alitaka kipa wa Liverpool Adrian, mwenye miaka 32, asalie katika klabu hiyo. (Mail)

Bora za siku ya Alhamisi:

Neymar alikuwa mazoezini mwenyewe siku ya Jumatano, ataendelea kufanya hivyo mpaka atakapouzwa.(Esporte Interactivo, via Mundo Deportivo - in Spanish)Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES

Kiungo mshambuliaji wa Brazil Philippe Coutinho, 27, anaweza bado kujiunga na PSG ikiwa hatakuwa sehemu ya ofa ya Neymar. (Goal)

Beki wa kati wa Manchester United Victor Lindelof, 25, anajiandaa kusaini mkataba mpya kwa ongezeko la mshahara mbali na pauni 75,000 alizokuwa akipata kwa wiki. (Aftonbladet - in Swedish)

Bayern Munich huenda wakafufua nia yao ya kumnasa winga wa Manchester City, Leroy Sane, ingawa mchezaji huyo, 23, ana jeraha la mguu, litakalo mfanya kuwa nje ya uwanja kwa miezi saba. (Bild - in German)


Mshambuliaji wa Marseille na Italia Mario Balotelli,29, anajiandaa kutia saini mkataba wa miaka mitatu na klabu ya Brescia baada ya kukataa ofa ya Flamengo ya Brazil. (Guardian)

Flamengo bado wana matumaini ya kubadili msimamo wa Balotelli, baada ya kukubali ombi lake la kumsajili kaka yake Enock kucheza katika moja kati ya timu zao nyingine (Gazzetta dello Sport - in Italian)

Winga wa klabu ya Everton Alex Iwobi, 23, amesema aliondoka Arsenal katika siku ya mwisho ya usajili kuthibitisha kuwa yeye si mchezaji anayechipukia tena. (Mirror)

Tottenham itazungumza na Christian Eriksen, 27,tena kuhusu mkataba mpya kabla kufungwa kwa dirisha la usajili barani Ulaya, tarehe 2 mwezi Septemba, baada ya Real Madrid na Juventus kuonesha nia ya kumnasa kiungo huyo.(Independent)

Mshambuliaji wa zamani wa Liverpool Daniel Sturridge, anaonekana kujiandaa kujiunga na timu ya Trabzonspor ya Uturuki kwa dili la pauni milioni 2.8 kwa kila msimu.(Goal)

Monaco imeingia kwenye kinyang'anyiro cha kuwasajili wachezaji kiungo Blaise Matuidi,32, na beki wa kati Daniele Rugani,25, kutoka Juventus. (Gazzetta dello Sport - in Italian)
Chanzo- BBC
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger