Monday, 19 August 2019

TETESI ZA SOKA LEO JUMATATU AGOSTI 19,2019

Mabingwa wa Ufaransa PSG wamefanya mazungumzo na Juventus kuhusu uhamisho wa dau la £73m kumsajili mshambuliaji wa Argentina mwenye umri wa miaka 25 Paulo Dybala. (Mail)

Kiungo wa kati wa Barcelona Philippe Coutinho amewasili nchini Ujerumani ili kukamilisha mkopo wake wa msimu huu kwa mabingwa wa ujerumani Bayern Munich. (Sun)

Paris St-Germain wamemtaka beki wa Real Madrid na Ufaransa Raphael Varane, 26, pamoja na mshambuliaji wa Brazil Vinicius Junior, 19, katika mpango wa kubadilishana wachezaji iwapo wanamuitaji mshambuliaji wa Brazil mwenye umri wa miaka 27 Neymar. (Telefoot - in French)
Barcelona inatumai kumrudisha Neymar Nou Camp , lakini kukiwa na kifungu cha kumnunua.. (Sport - in Spanish)

Aliyekuwa mshambuliaji wa Tottenham Fernando Llorente, 34, anakaribia kujiunga na klabu ya Itali Lazio. Inter Milan, Fiorentina na Napoli pia zina hamu ya kumsaini raia huyo wa Uhispania , ambaye kwa sasa hana klabu. (Corriere Dello Sport - in Italian)

Inter Milan wanataka kumtoa kwa mkopo mshambuliaji wa timu hiyo raia wa Chile Alexis Sanchez, 30, na pia wana hamu na mshambuliaji Llorente na kiungo wa kati wa Barcelona na raia wa Chile Arturo Vidal, 32. (Gazzetta dello Sport - in Italian)
Ajenti wa Sanchez yuko nchini Uingereza kuzungumzia mkopo wake kuelekea Inter Milan. (Sky Italy, via Sky Sports)

Sanchez alikua akifanya mazoezi na United siku ya Jumapili alfajiri.. (The Sun)

Inter Milan inajaribu kuafikia makubaliano ya kumnunua Sanchez lakini United imelazimika kumtoa kwa mkopo ili kutolipa mshahara wake wa £500,000 kwa wiki. (Mirror)
Manchester United wanatarajiwa kuanza mazungumzo ya kumuongezea kandarasi beki Eric Bailey mchezaji mwenye umri wa miaka 25 raia wa Ivory Coast . (Sun)

Paris St-Germain na Bayern Munich huenda zikawasilisha ombi kumnunua kiungo wa kati wa Ujerumani Emre Can, 25, baada ya kuambiwa na mkufunzi wake Maurizio Sarri anahitajiki Juventus. (Tuttosport, via Mail)

Paris St-Germain na Monaco zinafikiria kumpatia ofa kiungo wa kati wa Ufaransa Tiemoue Bakayoko, 25, kwa kuwa muda wake Chelsea unaonekana kwamba umekwisha.. (Daily Express)
Celtic imeipatia ofa Bordeaux kumnunua kiungo wa kati wa Ufaransa Olivier Ntcham . (20 Minutes via Daily Record)

Mkufunzi wa Newcastle Steve Bruce yuko tayari kumrudisha uwanjani mshambuliaji wa England Dwight Gayle, 28, haraka iwezekanavyo. (Newcastle Chronicle)
Jadon Sancho anatarajiwa kuondoka Borussia Dortmund msimu ujao huku klabu hiyo ya Ujerumani ikimtafuta mchezaji atakayechukua mahala pake. (Mail)

Mkufunzi wa Crystal Palace Roy Hodgson anasema kwamba winga wa Ivory Coast Wilfried Zaha, 26, huenda akaondoka katika klabu hiyo msimu huu . (Sun)

Mshambuliaji wa Manchester United na Chile Alexis Sanchez, 30, amekataa uhamisho wa kuelekea Roma, licha ya klabu hiyo ya Old Traford kukubali kulipa kitita kikubwa cha mshahara wake wa £560k kwa wiki.{Mirror)
Hata hivyo Sanchez huenda akaelekea katika ligi ya serie A baada ya Man United kumruhusu kufanya mazungumzo na Inter Milan, ambapo huenda akakubali kupunguza mshahara wake. (Mail)

Liverpool huenda ikafaidika na £18m iwapo mshambuliaji wa zamani wa klabu hiyo na raia wa Brazil Philippe Coutinho, 27, ataelekea Bayern Munich kwa mkopo. (Mail)
Everton imetoa ofa ya kumsaini winga wa Ufaransa Franck Ribery, 36, ambaye yupo huru baada ya kuondoka Bayern Munich baada ya kuhudumu kwa miaka 12 katika klabu hiyo ambayo ndio mabingwa wa ligi ya Bundesliga . (90Min)

Kwengineko, kiungo wa kati wa Portugal Renato Sanches, 21, anataka kuondoka Bayern kwa kukosa muda wa kucheza katika klabu hiyo. (Sport1 - in German)
Mesut Ozil, 30, huenda akaondoka Arsenal na kujiunga na klabu ya DC United iwapo klabu hiyo ya ligi ya MLS inaweza kumshawishi kiungo huyo wa Ujerumani kuhamia Washington. (Star)

Beki wa kulia wa Ivory Coast Serge Aurier, 26, huenda akaondoka Tottenham na kuelekea AC Milan iwapo beki wa timu hiyo Andrea Conti, 25, ataondoka ligi ya Serie A kabla ya kukamilika kwa dirisha la uhamisho la Ulaya. (Calciomercato)

Na mchezaji wa Everton Yannick Bolasie, 30, yuko tayari kurudi katika uwanja wa Goodison Park, huku klabu za Uturuki Besiktas na Trabzonspor zikiwa na hamu ya kumsajili mchezaji huyo wa Congo . (Sun)
Mchezaji wa zamani wa Manchester City na Liverpool Mario Balotelli, 29, anakaribia kujiunga na klabu ya Serie A Brescia. (Sun via La Gazzetta)

Mshambuliaji wa Paris St-Germain Neymar, 27, hakuorodheshwa katika kikosi cha timu hiyo kitakachocheza dhidi ya Rennes kutokana na jeraha na sio kwamba raia huyo wa Brazil anataka kurudi Barcelona. (AS - in Spanish)

Mshambuliaji wa Barcelona Kevin-Prince Boateng, 32, amefichua ni kwa nini Sir Alex Ferguson hakumsajili kujiunga na Manchester United mapema wakati wa kipindi chake cha mchezo. (Goal)
Mchezaji mpya wa Man United Hannibal Mejbri, ambaye aliwasili kutoka Monaco na hawezi kutia kandarasi ya mchezaji wa kulipwa hadi atakapofikisha umri wa miaka 17 January, anataka kuvaa jezi nambari saba Old Trafford. (Mirror)
Mchezaji wa kiungo cha kati wa Ufaransa Paul Pogba, mwenye umri wa miaka 26, bado ana hamu kubwa ya kutaka kuondoka Manchester United kuelekea Real Madrid msimu huu wa joto. (Marca)

Beki wa kati wa England Harry Maguire, mwenye miaka 26, amekataa pendekezo la thamani ya £278,000 kwa wiki kutoka Manchester City badala ya kujiunga na timu hasimu United. (Star)

Meneja wa United, Ole Gunnar Solskjaer amefanya mazungumzo na mchezaji wa kiungo cha kati wa Tottenham, Christian Eriksen kuhusu uwezekano wa uhamisho kuelekea Old Trafford, hatahivyo mchezaji huyo wa miaka 27alikuwa anataka kusubiria uhamisho kuelekea Uhispania. (Manchester Evening News)

Mchezaji wa kiungo cha mbele wa United na timu ya taifa ya Chile, Alexis Sanchez, aliye na umri wa miaka 30, yupo tayari kwa uhamisho kuelekea Italia , wakati Juventus, Napoli, AC Milan na Inter Milan zote zikiwania kumsajili. (Mirror)
Sanchez atashinikiza uhamisho kuondoka Old Trafford kabla ya kufungwa kwa dirisha la uhamisho Ulaya Septemba 2. (Times)

Kwa upande mwingine, United imeshindwa kupata mnunuzi wa Sanchez- anayepokea malipo ya £560,000 kwa wiki. (Mirror)

Juventus bado inatumai kumuondoa mchezaji wa kiungo cha mbele wa Argentina, Paulo Dybala, mwenye umri wa miaka 25, kabla ya muda wa mwisho wa uhamisho Ulaya - licha ya kwamba mabingwa hao wa Italia bado hawajapokea maombi thabiti kwa mchezaji huyo. (Independent)
Watch as Colombian U21 player Anderson Diaz scores a Maradona-like Wonder goal

Mkurugenzi wa michezo wa Paris St-Germain, Leonardo anasema mchezaji wa kiungo cha mbele wa Brazil, Neymar "amefanya makosa" lakini amesisitiza kuwa mchezaji huyo wa miaka 27 yupo Paris "kwa miaka mitatu". (RMC)

Kipa wa Stoke City na timu ya taifa ya England Jack Butland, aliye na miaka 26, ataomba uhamisho kujilazimisha kuwa katika mipango ya meneja wa England, Gareth Southgate kwa ajili ya mashindano ya Euro 2020. (Mail)

Timu ya Brazil Flamengo ilmejitoa katika uhamisho wa mshambuliaji Mario Balotelli baada ya mchezaji huyo wa miaka 29 kuitisha mkataba wa thamani ya £4m. (Mail)
Napoli imekubali kumsaini winga wa Mexico mwenye miaka 23 Hirving Lozano kutoka timu ya Uholanzi PSV Eindhoven. (Voetbal International)

Napoli imekataa ombi la thamani ya £82m kutoka kwa Manchester United kwa mchezaji wa miaka 28 raia wa Senegal Kalidou Koulibaly kabla ya kufungwa kwa dirisha la uhamisho England. (Corriere dello Sport, kupitia Calciomercato)

Winga wa Bournemouth Jordon Ibe anasakwa na mabingwa wa Uskotchi, Celtic. Timu ya Napoli Italia, tayari imemuulizia mchezaji huyo wa miaka 23. (Sun)
Manchester United imewapiga marufuku wachezaji kusaini kumbukumbu au autograph kwa mashabiki katika kiingilio cha uwanja wa mazoezi kutokana na masuala ya usalama.(Telegraph)

Meneja wa West Ham Manuel Pellegrini anasema alitaka kipa wa Liverpool Adrian, mwenye miaka 32, asalie katika klabu hiyo. (Mail)

Bora za siku ya Alhamisi:

Neymar alikuwa mazoezini mwenyewe siku ya Jumatano, ataendelea kufanya hivyo mpaka atakapouzwa.(Esporte Interactivo, via Mundo Deportivo - in Spanish)Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES

Kiungo mshambuliaji wa Brazil Philippe Coutinho, 27, anaweza bado kujiunga na PSG ikiwa hatakuwa sehemu ya ofa ya Neymar. (Goal)

Beki wa kati wa Manchester United Victor Lindelof, 25, anajiandaa kusaini mkataba mpya kwa ongezeko la mshahara mbali na pauni 75,000 alizokuwa akipata kwa wiki. (Aftonbladet - in Swedish)

Bayern Munich huenda wakafufua nia yao ya kumnasa winga wa Manchester City, Leroy Sane, ingawa mchezaji huyo, 23, ana jeraha la mguu, litakalo mfanya kuwa nje ya uwanja kwa miezi saba. (Bild - in German)


Mshambuliaji wa Marseille na Italia Mario Balotelli,29, anajiandaa kutia saini mkataba wa miaka mitatu na klabu ya Brescia baada ya kukataa ofa ya Flamengo ya Brazil. (Guardian)

Flamengo bado wana matumaini ya kubadili msimamo wa Balotelli, baada ya kukubali ombi lake la kumsajili kaka yake Enock kucheza katika moja kati ya timu zao nyingine (Gazzetta dello Sport - in Italian)

Winga wa klabu ya Everton Alex Iwobi, 23, amesema aliondoka Arsenal katika siku ya mwisho ya usajili kuthibitisha kuwa yeye si mchezaji anayechipukia tena. (Mirror)

Tottenham itazungumza na Christian Eriksen, 27,tena kuhusu mkataba mpya kabla kufungwa kwa dirisha la usajili barani Ulaya, tarehe 2 mwezi Septemba, baada ya Real Madrid na Juventus kuonesha nia ya kumnasa kiungo huyo.(Independent)

Mshambuliaji wa zamani wa Liverpool Daniel Sturridge, anaonekana kujiandaa kujiunga na timu ya Trabzonspor ya Uturuki kwa dili la pauni milioni 2.8 kwa kila msimu.(Goal)

Monaco imeingia kwenye kinyang'anyiro cha kuwasajili wachezaji kiungo Blaise Matuidi,32, na beki wa kati Daniele Rugani,25, kutoka Juventus. (Gazzetta dello Sport - in Italian)
Chanzo- BBC
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu 19 August





















Share:

Sunday, 18 August 2019

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714006521


Share:

Picha : PIKIPIKI YA CCM YAIBIWA SHINYANGA.....POLISI WAKAMATA WAHALIFU 73


Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao akionesha pikipiki ya CCM iliyoibiwa na kukamatwa na polisi.

Na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limefanikiwa kuikamata pikipiki yenye namba za usajili MC 276 BBM aina ya SUNLG Mali ya Chama Cha Mapinduzi ' Umoja wa Wazazi CCM) mkoa wa Shinyanga iliyoibiwa katika ofisi za chama hicho Mjini Shinyanga.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumapili Agosti 18,2019 ,Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao amesema pikipiki hiyo iliibiwa mahali inapohifadhiwa Mjini Shinyanga na jeshi la polisi limefanikiwa kuikamata pikipiki hiyo katika wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu.

"Tumeikamata pikipiki hiyo wilayani Bariadi ikiwa imetengenezewa kadi ya kufoji.Tumemkata mtuhumiwa mmoja na tunaendelea kufuatilia kubaini mtandao wa watu wanaotengeneza kadi za kufoji",ameeleza.

Kamanda Abwao amesema pikipiki hiyo ni sehemu ya pikipiki tano ambazo zimekamatwa na polisi kufuatia misako iliyofanywa na jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga kwa kipindi cha kuanzia tarehe 23.07.2019 hadi tarehe 18.8.2019 katika kukabiliana na uhalifu na wahalifu.

"Pikipiki hizi zingine tulizozikamata zimetumika katika vitendo vya mauaji ya mwanamke aitwaye Kalekwa Shiku (50) mkazi wa kijiji cha Mishepo,wilaya ya Shinyanga na mauaji ya mwendesha bodaboda Juma Nedadi (28) kisha kuporwa pikipiki yenye namba za usajili MC.841 CCG aina ya Honlg na pikipiki zingine ni zile zilizokuwa zinatumika kusafirishia dawa za kulevya aina ya bangi",alisema Kamanda Abwao.

Alizitaja pikipiki zingine zilizopatikana zinazodhaniwa kuwa ni za wizi kuwa ni zenye namba za usajili T.609 CZE,MC 159 BWQ na MC 881 aina ya SANYA na SANLG.

Alifafanua kuwa katika misako hiyo,Jeshi la polisi limefanikiwa kukamata watuhumiwa 73 wa uhalifu wakiwemo wa matukio ya mauaji,dawa za kulevya kama vile bangi,wezi,heroine,cocaine na mirungi.

Alisema mbali na kukamata wahalifu pia wamefanikiwa kupata mali zidhaniwazo kuwa ni za wizi ambazo ni pamoja na radio aina ya subwofer,simu tablet,laptop,TV,pikipiki,gari 1(chakavu),betri za gari,solar panel,ng'ombe,booster,baiskeli na madini yyadhaniwayo kuwa ni ya bandia aina ya dhahabu.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao  akielezea kuhusu misako mbalimbali iliyofanywa na jeshi la polisi katika kukabiliana na uhalifu na wahalifu leo katika mkutano wake na waandishi wa habari. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Pikipiki ya Umoja wa Wazazi iliyoibiwa.
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao akionesha pikipiki ya Umoja wa Wazazi CCM iliyoibiwa na kukamatwa na polisi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao akielezea namna pikipiki ya Umoja wa Wazazi CCM ilivyoibiwa na kukamatwa.
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao akionesha pikipiki zilizoibiwa katika matukio ya mauaji na usafirishaji wa dawa za kulevya aina ya bangi.
Pikipiki zilizoibiwa katika matukio ya mauaji na usafirishaji wa dawa za kulevya aina ya bangi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao panga lililokuwa linatumiwa na watuhumiwa wa mauaji.

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao akionesha TV Flat inayodhaniwa kuwa ni ya wizi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao akionesha laptop aina ya Sumsung inayodhaniwa kuwa ni ya wizi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao akionesha kifaa cha kukabia roba kilichokuwa kinatumiwa na wahalifu kuibia watu mali zao.

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao akionesha mifuko iliyobeba bangi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao akiangalia bangi iliyowekewa karanga juu ili mtu akiangalia aone ni mifuko iliyobeba karanga kumbe kuna bangi kwa ndani.

Laptop na vifaa vinavyotumiwa na wahalifu kufanya uhalifu vilivyokamatwa. 

Mali za wizi zilizokamatwa na polisi.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Share:

Wakuu Wa Nchi za SADC Wasaini Itifaki Ya Kubadilishana Wafungwa

Na John Bukuku/FullShangweblog
Wakuu wa nchi 16 zinazounda Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika SADC wamesaini  itifaki na makubaliano mbalimbali kwa ajili ya kuanza utekelezaji. 

Itifaki iliyosainiwa na wakuu hao wa nchi ni Itifaki ya viwanda yenye lengo la kuboresha mazingira ya kukuza viwanda viweze kuzalisha vya kutosha na katika ubora unaoweza kushindana  duniani.

Wakuu hao pia wamesaini Itifaki ya kubadilishana wafungwa miongoni mwa nchi wanachama itakayowezesha wafungwa waliohukumiwa nje ya nchi zao kwenda kutumikia kifungo ndani ya nchi zao.

Aidha walisaini pia makubaliano ya kurekebisha sheria za nchi zao ili kuendana na Itifaki zilizosainiwa pamoja na makubaliano ya kusaidiana katika mambo ya uhalifu.

Itifaki hizo zimesainiwa wakati wa kufunga mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Kiuchumi Kusini  mwa Afrika SADC uliofanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam  ambapo pamoja na mambo mengine wakuu wa nchi 16 zinazounda jumuiya hiyo wamesaini itifaki na makubaliano mbalimbali kwa ajili ya kuanza utekelezaji.

Akizungumza katika wakati akifunga mkutano huo Mwenyekiti  wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Rais Dk John Magufuli ameisisistiza  Sekretarieti ya SADC kutumia fedha wanazopata vizuri badala ya kuishia kuzitumia katika warsha, semina na mikutano.

Rais alipendekeza Sekretarieti hiyo ione umuhimu wa kuanza kutumia fedha hizo katika masuala ya maendeleo kama vile ya elimu, afya na miundombinu.

“Bajeti ya Jumuiya yetu inafikia Dola milioni 74 lakini kituo cha afya kinagharimu Sh  milioni 400 hadi 500 sawa na dola 200,000 ambazo zipo ndani ya uwezo wa sekretarieti, ” alisema Rais Magufuli.

Rais Magufuli pia amesema katika mkutano huo wamepitisha kauli mbiu itakayotumika mwaka mzima ambayo inasisitiza ujenzi wa viwanda endelevu vitakavyoongeza ufanyaji biashara na kukuza ajira.

Kauli mbiu hiyo inasema, “Maendeleo endelevu ya viwanda kuongeza ufanyaji biashara na kukuza ajira,”

Rais Magufuli amesema katika mambo waliyoazimia wamehimizana nchi wanachama kuahkikisha zinajenga miundombinu wezeshi ili kuweza kusaidia kukuza uchumi wa nchi hizo pamoja kuboresha sera za uchumi na fedha.

Aidha amesema mambo mengine waliojadili katika mkutano huo ni ombi la nchi ya Burundi kutaka kuingia SADC ambapo walijiridhisha kuwa bado kuna mambo ambayo hayajafanyiwa kazi na kuagiza sekretatieti kuwapa taarifa hiyo na baadae kwenye kuchunguza kama mambo hayo yamefanyiwa kazi.

Akizungumza kuhusu suala la vikwazo vya kiuchumi kwa nchi ya Zimbabwe Rais Magufuli amesema wamekubaliana waendelee na mazungumzo na jumuiya za kimataifa ili kuangalia namna ya kuondoa vikwazo hivyo.

 Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Sekretaieti ya SADC, Dk Stergomena Tax mkutano huo umekubaliana kuwa Oktoba 25 mwaka huu itakuwa siku ya kutoa wito kwa jumuiya za kimataifa kuondoa vikwazo dhidi ya Zimbabwe.


Share:

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598


Share:

Ardhi University second round application starts on 21st to 29th August 2019.

Ardhi University second round application starts on 21st to 29th August 2019. Dear Applicants to ARDHI UNIVERSITY (ARU) undergraduate programmes; Window for the first round applications is closed from 10th August 2019; and results will be announced from 20th August 2019. Window for second round applications for unsuccessful and new applicants will be opened from 21st to 29th… Read More »

The post Ardhi University second round application starts on 21st to 29th August 2019. appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Tigo Yaing'arisha Tanzania Katika Mkutano Wa Sadc Jijini Dar Es Salaam

Rosemary Mroso kutoka kitengo cha huduma kwa wateja Kampuni ya simu za mkononi Tigo Tanzania akimhudumia mteja wa kampuni hiyo Emmanuel Liwimbi Ofisa Huduma za Mikutano Mwandamizi kutoka Sekretarieti ya SADC alipotembelea banda hilo kwenye mkutano wa SADC unaoendelea katika ukumbi wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam. Tigo ni mdhamini wa huduma za intaneti katika Mkutano huo.
Mtaalam wa Mifumo ya Mtandao Kampuni ya Tigo Bw. Kundasen Simon akiwasikiliza wateja wa kampuni hiyo waliotembelea banda la kampuni ya Tigo lililopo kwenye ukumbi wa mikutano wa Julius Nyerere JNICC   jijini Dar es salaam ambako Mkutano wa Wakuu  wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaoendelea , Tigo ni miongoni mwa wadhamini wa intaneti ya bure katika mkutano huo.
Mtaalam wa Mifumo ya Mtandao Kampuni ya Tigo Bw. Kundasen Simon akimsikiliza mteja wa kampuni hiyo Bw. Selemani Kifyoga aliyefika kwenye banda hilo kwa ajili ya kusajili laini yake ya simu kwa mfumo wa kutumia vidole. Tigo ni miongoni mwa wadhamini katika mkutano unaondelea wa SADC

Mfanyakazi wa  Tigo akitoa huduma kwa wateja waliofika katika banda lake lililopo ndani ya Ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam ambapo Mkutano Mkuu wa 39 wa marais wa Jumuiya ya Maendeleo kwa Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) unafanyika. Tigo ni  mdhamini mkuu wa Huduma ya intaneti katika mkutano huo.  



Share:

Okoa Ndoa Yako Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Kisukari

Ni dawa zilizopimwa na mkemia na kupewa no 341/VOL,XV/36 na TFDA no 0127/F/F/1819/ MTINJETINJE ni dawa ya kisukari .....Hurudisha kongosho katika hali ya kawaidi hata kama limefeli haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin, itaifanya sukari kuwa normal

SUPER MAJINJA ni dawa inayotibu nguvu za kiume yani matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka (2)kuwai kufika kabla ya  mwenzi wako (3)maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa (4)maumbile ya kiume  kuingia ndani na kuwa mafupi kwa wale walio jichua (5)miuungurumo ya tumbo,ngiri,kukosa choo,kiuno kuuma

ACHA KUONGOPEWA SASA DAWA HIZI NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA

NJOO OFISINI KWANGU MBAGALA KARIBU NA BENK YA KCB NA mwanza yupo wakala piga simu ya DR AGU whatsapp 0783185060. 0620113431


Share:

Mkutano wa SADC wahitimishwa, Rais Magufuli ataja Mambo waliyokubaliana

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa SADC, Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa wamekubaliana mambo kadhaa katika kikao cha wakuu wa nchi 16 kilichofanyika jana jioni Ikulu jijini Dar es salaam yakiwamo suala la kuondolewa kwa vikwazo kwa Zimbabwe, kufuatilia hali ya usalama nchini Congo na ombi la Burundi kujiunga na jumuiya hiyo.

Mengine ni kuwekeza kwenye miundombinu itakayowezesha kukua kwa uchumi katika ukanda wa nchi wanachama wa jumuiya hiyo, kuwa na chombo cha kukabiliana na majnga na suala la upatikanaji wa mapato.

Makubaliano hayo yamefikiwa katika mkutano huo wa SADC wa siku mbili uliomalizika leo Jumapili Agosti 18, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa hotuba ya kuhitimisha mkutano huo, Rais Dk. John Magufuli amesema wakuu wa nchi wamekubaliana kuendelea kufuatilia hali ya usalama nchini Congo lakini pia wameiagiza sekretarieti kuharakisha chombo cha kukabiliana na majanga kitakachosaidia nchi wanachama kukabiliana na majanga kama vile njaa, mafuriko, vimbunga, magonjwa ya mlipuko na mengineyo.

Amesema katika mkutano huo pia, wakuu wa nchi walipitia hali ya uchumi katika ukanda wao ambapo uchumi wa nchi hizo ulishindwa kukua kama ulivyotarajiwa kwa asilimia saba na kushuka hadi asilimia 3.1, hivyo wamekubaliana kuwekeza kwenye miundombinu kwa kuwa ni mojawapo ya kikwazo cha kukua kwa uchumi kwenye bara la Afrika ikiwamo nchi za SADC.

Pamoja na mambo mengine, amesema mkutano huo pia umepitisha mpango wa kuongeza mapato kwa SADC ambapo nchi wanachama zitakuwa na hiyari ya kuchagua njia bora ya kuchangia.


Share:

Rais Magufuli: Tuimarishe Umoja Na Mshikamano Kuijenga Sadc Kuleta Maendeleo Kwa Wananchi

Na Mwandishi Wetu, MAELEZO
RAIS Dkt. John Magufuli amewataka Wakuu Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuendelea kuimarisha Umoja na Mshikamano na kuwa na sauti moja katika kusimamia maslahi mapana ya Jumuiya hiyo katika kuleta maendeleo kwa wananchi wake.

Akifunga Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya hiyo, leo Jumapili (Agosti 18, 2019), Jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo alisema Tanzania ipo tayari kutoa ushirikiano unaohitaji ili kuharakisha jitihada za kuleta maendeleo katika jumuiya hiyo.

Aliongeza kuwa Umoja ni kiungo muhimu cha maendeleo katika ushirikiano wa Jumuiya yoyote, hivyo ili kuleta kasi ya mabadiliko ndani ya Jumuiya hiyo ni wajibu wa Nchi wanachama kuhakikisha inatumia vyema rasilimali zake pamoja na kuweka mkazo wa maazimio na agenda za Mkutano wa 39 kwa kutafakari masuala muhimu ya maendeleo.

Rais Magufuli alisema chini ya Uongozi wake, jumuiya hiyo itaendelea kusimama imara na kuwa na nguvu ya pamoja katika kutetea maslahi ya Nchi wanachama ikiwemo vikwazo ilivyowekewa Nchi ya Zimbabwe na kusema Viongozi wa Jumuiya hiyo kwa kauli moja wameungana katika kuitaka jumuiya ya kimataifa kuondoa vikwazo dhidi ya nchi hiyo.

“Tutahakikisha kuwa jumuiya yetu inaondoa changamoto mbalimbali zinazozuia ukuaji wa uchumi ukiwemo vitendo vya rushwa na ukiritimba vinavyokwamisha sekta ya sekta ya biashara baina ya nchi zetu” alisema Rais Magufuli.

Akifafanua zaidi, Rais Magufuli alisema katika mkutano huo wa 39, Wakuu wa Jumuiya hiyo kwa pamoja wameweza kuwa na mjadala wa pamoja uliowawezesha Viongozi hao kutoa maoni, ushauri na michango yao na pamoja kusaini itifaki mbalimbali zilizoridhia agenda na mikakati mbalimbali kwa ajili ya kuharakisha maendeleo ya Jumuiya hiyo.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli alisema kutokana na kasi ndogo ya ukuaji uchumi iliyopo kwa sasa ndani ya jumuiya hiyo, aliwataka Viongozi hao kuhakikisha wanaweka mkazo katika kukuza na kuimarisha sekta ya miundombinu pamoja na kuboresha sera za kifedha na kiuchumi ili kukuza kiwango cha ukuaji wa Pato la Taifa kwa kila Nchi mwanachama.

Rais Magufuli pia aliitaka Sekretarieti ya Jumuiya kutumia fedha kwa malengo yaliyokusudiwa badala ya fedha hizo kutumika katika kuandaa makongamano, warsha na semina mbalimbali na sasa zielekezwe katika utekelezaji wa miradi inayoweza kuleta manufaa kwa nchi wanachama ndani ya jumuiya hiyo.

“Katika Bajeti yetu ya mwaka 2019/2020 tumepanga kutumia Dola Milioni 74, mchango wa Dola Milioni 43 zinazotolewa nan chi wahisani tunaweza kujenga vituo 17, nitafurahi kuona siku moja Sekretarieti ya jumuiya yetu ikiwaalika wanachama katika uzinduzi wa vituo hivyo” alisema Rais Magufuli.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli aliwakaribisha wawekazaji waliopo ndani ya SADC kuja kuwekeza katika miradi ya sekta mbalimbali iliyopo nchini ikiwemo nishati, madini, utalii, mifugo, kilimo pamoja na utalii kwani Tanzania imeweka mazingira bora na wezeshi kwa kwa ajili ya wawekezaji na wafanyabiashara.

Akizungumzia kuhusu maombi ya Nchi ya Burundi kujiunga na Jumuiya hiyo, Rais Magufulli alisema Sekretarieti ya jumuiya hiyo imepanga kutuma timu ya uchunguzi katika nchi hiyo kwa ajili ya kujiridhisha na masuala muhimu ya kimsingi yanayopaswa kuzingatiwa kabla ya kukubaliwa kwake kujiunga na Jumuya hiyo.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo, Dkt. Stegomena Tax alisema Mkutano huo wa 39 wa SADC umekuwa wa mafanikio makubwa kutokana na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Nchi wanachama ambapo wameweza kuweka mikakati ya pamoja itakayosaidia kuongeza kasi ya ukuaji uchumi na maendeleo ya Nchi hizo.

Dkt. Tax alisema kuwa katika mkutano huo pia, Viongozi wa Jumuiya hiyo waliweza kufanya maamuzi ya kuchagua viongozi wa ndani katika Jumuiya hiyo ikiwemo Nafasi ya Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama ndani ya Jumuiya hiyo (TROIKA) aliyokwenda kwa Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa.

MWISHO.


Share:

IT support assistant at the World Bank Tanzania- Jobs in Tanzania

IT support assistant at the World Bank Tanzania- Jobs in Tanzania The World Bank Group works in every major area of development.  We provide a wide array of financial products and technical assistance, and we help countries share and apply innovative knowledge and solutions to the challenges they face  

The post IT support assistant at the World Bank Tanzania- Jobs in Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

NGOs 158 Zaondolewa kwenye Rejista ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.

Na Mwandishi Wetu Mbeya
Msajili   wa   Mashirika   Yasiyo   ya   Kiserikali   nchini   (NGOs)   Bi.   Vickness   Mayao ameyaondoa Mashirika zaidi  ya 158  kwenye  Rejista ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.

Hayo yamesema jijini Mbeya na Mkurugenzi Msaidizi Uratibu wa NGOs kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi Grace Mbwilo kwa niaba ya Mkurugenzi na Msajili wa NGOs nchini.

Bi. Grace amesema kuwa katika Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Namba 24 ya Mwaka 2002  kama ilivyofanyiwa Mabadiliko  na Sheria  Namba 3 ya Mwaka  2019, imefafanua bayana kuwa jukumu  la kusajili mashirika yanayoendesha shughuli za kijamii, kiutamaduni, kiuchumi, utawala bora, haki  za  kibinadamu na  mazingira   katika  ngazi  ya  jamii  kwa  lengo  la kutogawana faida  na  ambazo hazina mrengo wa  wa  kukuza  biashara, zimeelekezwa kusajililiwa na Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGOs).

“Mashirika   yaliyoondolewa   kwenye   daftari    la   Msajili   wa   NGOs   ni   yale   ambayo yalisajiliwa chini  ya Sheria  ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na.  24   ya mwaka 2002 ambayo yanafanya kazi kwa   lengo  la kunufaisha wanachama wake, kugawana faida, yenye   mlengo  wa   dini,  yenye   lengo   la  kukuza   biashara  na   Bodi  za   wadhamini”, alisema Bi. Grace.

Bi. Grace ameongeza kuwa, hatua ya kuyaondoa mashirika haya  kwenye  daftari  la msajili wa NGOs imefikiwa kwa mujibu wa Sheria ya Marekebisho Na. 3 ya mwaka 2019 iliyoanza  kutekelezwa  kuanzia  tarehe 1 Julai  2019.  Kwa mujibu  wa  Sheria,  Mashirika hayo yanatakiwa kwenda kujisajili chini ya Sheria  husika ikiwemo  Sheria  ya Jumuiya za Kijamii(Sura  ya 337), Sheria  ya Munganisho wa Wadhamini(Sura ya 318)  na  Sheria  ya Makampuni (Sura  ya 212), na kwamba inatakiwa kukamilisha zoezi  hili kabla  ya tarehe 01 Septemba,2019.

Ameeleza kuwa wa  kuzingatia ufafanuzi wa  mipaka ya  usajili ulioainishwa na  Sheria  Namba 3  ya Mwaka   2019,  Msajili  wa   Mashirika  Yasiyo  ya   Kiserikali  (NGOs)  anayakumbusha Mashirika yanaofanya shughuli kwa lengo  la kugawana faida, yenye mrengo wa dini na ambayo yana  malengo wa kukuza  biashara, kwamba  mashirika ya aina  hiyo yatafutwa kwenye  daftari  la Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali baada ya kipindi cha  miezi miwili  kuanzia  tarehe  01.07.2019 na  yatahamishiwa  chini  ya  Mamlaka  nyingine  za Usajili kutokana na kukosa sifakuwa NGO.

Katika kuhitimisha zoezi  la usajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali liliofanyika Mkoani Mbeya, Ofisi ya Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali imewaagiza wadau wa mashirika yote  yaliyosajiliwa kwa  lengo  la kuzalisha faida  na  kugawana faida  kuhakikisha kuwa wanahamisha usajili ili kuhuisha taarifa zao kwa Msajili stahiki.

Hatua  hii imechukuliwa na  Msajili wa  Mashirika Yasiyo ya  Kiserikali katika  hatua ya mwisho   ya   Usajili   wa   Mashirika   hayo   kwa   Kanda   ya   Nyanda    za   Juu  Kusini inayohitimishwa mwisho wiki katika ukumbi wa Mkapa Jijini Mbeya na orodha ya Mashirika 158 yaliyoondolewa kwenye  daftari inapatikana katika tovuti ya Wizara www.mcdgc.go.tz na ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali. www.tnnc.go.tz


Share:

Accountability Assistant at Save the Children- Jobs in Tanzania

Accountability Assistant at Save the Children- Jobs in Tanzania Accountability Assistant   TEAM/PROGRAM: Programme Development and Quality LOCATION: Kibondo, Kigoma GRADE: TBC POST TYPE: National Child Safeguarding: Level 3 – the responsibilities of the post may require the post holder to have regular contact with or access to children or young people ROLE PURPOSE: The Accountability Assistant will be… Read More »

The post Accountability Assistant at Save the Children- Jobs in Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger