Saturday, 19 January 2019

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 196 na 197 )

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA     
  
Swali la Jojo likanifanya niyanyanyue macho yangu taratibu hadi kwenye kioo kidogo kilichopo mbele yangu na kumtazama Magreti kwa nyuma.
“Unaogopa kujibu kisa Magreti, usimfiche bwana. Magreti mimi baba yangu ni malaya, sasa kama unampenda jiandae kuumia tu”
Nikajikuta nikikausha kimya, hata kufungua kinywa changu ninashindwa.
“Yaani kama baba angekupata leo, wewe ungekuwa msichana wa mia moja”
“Mungu wangu”
Magreti alizungumza huku akinitazama vizuri kwa kunichukungulia usoni.
“Hivi Dany huna ukimwi kweli wewe?”
Swali la Magreti likazidi kuninyong’onyeza kiasi kwamba nikashindwa kujibu chochote na kuendelea kukaa kimya

ENDELEA   
“Huwezi kuamini nikikuambia baba yangu hana Ukimwi kabisa, japo amekuwa na wanawake wengi sana”
“Mmmmm”
 
“Kweli vile hata ukisema umpime hapo sasa hivi hana, japo alitembea na wanawake ambao wana maambukizi ya magonjwa hayo”
“Munanitania nyinyi”   
“Kweli vile, damu ya baba yangu ni toafuti sana na damu za watu wenginene, haipokei maradhi kabisa”
“Mmmmmmm”
“Hembu hizo mada zife”
Nilizungumza kwa sauti nzito na kuwafanya Magret na Jojo kutabasamu. Tukasimamishwa kwenye moja ya kwenye moja ya kituo cha ukaguzi. Nikataka kutoa bastola yangu ila Jojo akatingisha kichwa.
“Musiogope najua nini cha kufanya”
Tukatulia tu kwenye siti zetu, Jojo akafungua kioo chake.
“Habari yako binti”
Askari huyu alizungumza huku akimtazama Jojo.
“Salama tu kaka, shikamoo”
“Marahaba, una umri  gani binti?”
“Miaka ishirini”
“Ninaomba leseni yako”
Jojo akatoa leseni yake, askari huyu akaitazama kwa muda, kisha akamrudishia Jojo.
“Unaelekea wapi?”
“Ninakwenda Dar”
“Kuwa makini barabarani, kwa maana kwa msichana mdogo kama wewe kuendesha masafa marefu ni hatari kidogo”
“Sawa kaka afande nitajitahidi kuwa makini”
“Sawa binti, je ninaweza kuipata namba yako ya simu”
“Hahahaa hapana”
 
“Basi chukua ya kwangu ili hata huko mbele usisumbuliwe sumbuliwe na askari wengine”
“Mmmmm sawa naomba uniandikie kwenye karatasi”
“Huna simu nikaiandika namba yangu haraka haraka”
Polisi huyu alizungumza huku akitazama tazama humu ndani ya gari kitu nilicho kigundua kwa uharaka ni kwamba askari huyu hajagundua uwepo wetu ndani ya hili gari. Jojo akampatia askari huyu simu yake, askari huyu akaiandika kwa haraka huku akitazama wezake kama wanao tukio hili kishaa kamrudishia Jojo.
“Niaitwa afande Mweta, utanipigia mtoto mzuri”
“Asante Afande Mweta”
 
“Karibu sana, wewe wakikusimamisha tu nipigie”
“Sawa afanye”
“Una pesa ya mafuta?”
“Mmmm ninayo”
“Ok nilijua huna nikupatie japo kidogo mtoto mzuri”
“Unaweza kunipatia?”
Askari huyu akarudi kutazama tazama wezake kisha akafungua mfuko wake wa shati na kutoa dola mia na kumpatia Jojo.
“Hiyo utabadilisha, mtoto mzuri, hakikisha unanipigia basi sawa Jojo”
“Sawa afande”
“Safari njema mrembo”
Afande Mweta alizungumza huku meno yote thelathini yakionekana. Jojo akafunga kioo cha gari na tukaondoka eneo hili.
“Hivi unataka kusema kwamba huyo afande hajatuona?”
Nilimuuliza Jojo huku nikimtazama usoni mwake.
“Nimewapoteza ndio maana akawa anajishebedua”
“Yaani wanaume nyinyi, utakuta yule mbaba ana mke na watoto, ila kamuona Jojo hapa kashoboka laiti ungemuonyeshea kama ulivyo nionyeshea mimi vituko ninahisi angekufa kwa presha”
 
“Weee sio kufa tu angeacha hata hiyo kazi yenyewe”
“Hahaaa”
Nilijikuta nikicheka tu, huku nikimtazama Jojo na Magret ambao tayari wamesha onekana kuzoeana. Tukafika jijini Dar es Salaam majira ya usiku, hatakuona haja ya kusimama sehemu yoyote na tukaelekea Kigamboni kwenye fukwe ambayo ndipo yalipo maficho yetu, tukakuta boti ikitusubiria huku wasichna wawili wa Livna ndio wanao linda hili eneo.
Safari ikaanza huku wasichana hawa wawili wakimtazama Jojo, simu yangu ikaita, nikaitoa mfukoni na kukuta Livna akinipigia, nikamtazama Jojo kisha nikaosogea pembeni na kuipokea.
 
“Niambie”
“Huyo aliye ongezeka ni nani?”
“Tutakuja kuzungumza?
“Dady usijiokotee okotee watu tu ukawaleta huku ikiwezekana muue”
“Livna nimekuambia kwamba tutakuja kuzungumza nikifika, mimi sio kichaa wakusema sielewi kile kitu ninacho kifanya, wewe tulio utajua kila kitu nikifika”
Livna akaka kimya kwa sekunde kadhaa akionekana kujifikiria.
 
“Dany kumbuka kwamba haya ni maficho muhimu sana, huyo msichana utamuamini vipi au umemjulia wapi?”
“Livna hivi hunielewi ninavyokuambia  kwamba nitakuamia kila kitu nikifika huko au huniamini?”
Ilinibidi kuzungumza kwa ukali kidogo ili kusisitizia msimamo wangu kwa Livna ambaye tayari nimesha ziteka hisia zake za mapenzi.
“Ninakuamini”
“Sasa maswali mengi ya nini, unahisi kwamba mimi ni mjinga niokote okote watu?
“Naomba unisamehe mpenzi wangu”
“Poa”
 
Nikakata simu, Jojo akanisogelea huku akinitazama usoni mwangu.
“Kumbe baba yangu na wewe unakoromea watu”
“Kwa nini?”
“Ninaona jinsi unavyo mkoromea Livna hapo kisa mimi?”
“Usujali mwangu ni mambo ya kawaida tu”
“Ila kama hawato nihitaji tunaondoka kwenye meli yao kwa manaa siwezi kuishi mbali na wewe baba yangu, nilikusubiria kwa muda mrefu japo nilifahamu ni  sehemu gani upo ila nilishindwa kukufwata”
“Kwa nini ulishindwa kunifwata?”
“Mama aliniambia kwamba nitakutana na wewe siku fulani, katika eneo fulani na katika hali fulani na ndivyo ilivyo tokea”
“Sawa”
 
“Ni kweli mama alikuwa na maana yake kwa maana ningekufwata kwa njia ya kawaida tu hivi na kukuambia kwamba mimi ni mwanao ungenikubali?”
“Ningealia na maelezo yako kisha ningekupima kwa maswali kadhaa kama usinge nijubu kama ninavyo hitaji ningekukataa”
“Ila kwa nini ulinikubali haraka?”
“Kwa sababu mama yako aliniambia kwamba mwanangu atakuja kunisaidia nikiwa na matatizo”
“Ahaaa sawa”
 
“Baba na mwana munazungumza nini?”
“Ahaaa stori za kawaida tu”
“Ila Dany umejitahidi kumpata Jojo ni mzuri sana”
“Hahaaaa, unajua ni nini Magreti”
“Eheee”
“Unaonaje kuaolewa na baba yangu?”
“Weee ongea taratibu nisije nikasikiwa nikauwawa bure”
“Nani akuue?”
“Huyo ni mume wa mkuu wangu Livna”
“Mmmmm mbona baba Livna amekupita umri, hembu mchukue Magreti anaendana na wee”
“Sasa nitamchukuaje ikiwa ana ujauzito wangu?”
“Mmmm hana mimba, kizazi chake hakina uwezo wa kushika ujauzito?”
 
“Acha kunitani?”
“Kweli kabisa baba yangu, yule mwanamke anakupotezea muda, na yeye anajijua kabisa kwamba hana uwezo wa kubeba ujauzito”
“Hayo makubwa, ila jamani zungumzeni taratibu hawa wapambe watatusikia?”
“Hapana hawatusikii, niwewaziba masikio yao na wakizungumza wao kwa wao wanasikiana”
“Hivi unawezaje kufanya hayo yote?”
“Hahaaaa, ninaweza ila tukienda nyumbani nitaweza kukufundisha”
“Sawa”
“Jamani na mimi ninataka kwenda, kusema kweli kwa siku hizi kadhaa nilizo kuwa nje ya ile meli nimefurahia sana maisha. Sikuwahi kukumbatiwa na mwanaume ila baba yako ameweza kufanya hivyo”
“Hahaa masikini weee kumba ndio umekumbatiwa leo?”
“Ndio”
 
“Mkumbatie sasa hivi?”
“Nyie hembu acheni ujinga”
“Hahaaa baba ujinga gani, unamridhisha kidogo tu”
“Hayo mambo yataendelea muda mwengine sio sasa”
Tukafanikiwa kufika katika meli salama Salim, tukamkuta Livna na Logate wakitusubiria katika eneo hili. Tukasalimana na wakamsalimia Jojo, tukaongozana moja kwa moja hadi katika chumba cha mapumziko na Magreti akaelekea katika chumba chake.
“Livna huyu anaitwa Jojo ni mwanangu”
Nilizungumza huku nikimtazama Livna usoni mwake, akaonekana kujawa na mshangao mkubwa sana bada ya kusikia kwamba jojo ni mwanangu.
 
“Lini Dany umekuwa na mtoto mkubwa kama Jojo sijui Jojo gani huko?”
Livna alizungumza kwa sauti iliyo jaa dharau kidogo, nikamtazama Jojo, nikamuona anavyo benua midomo yake naye akimtazama Livna.
“Mimi si mwanaume na lazima niwe na mtoto”
“Dany nimekukubalia Hawa azae hapa, nimekukubalia Yemi azalie hapa, leo hii unaniletea mtoto ambaye ni mkubwa kabisa anaye weza kujitafutia, yaani kusema kweli sipo tayari kabisa kumlea huyo mwanao, kumbuka kwamba mimi umesha nipa ujauzito na mimi”
Jojo akaachia msunyo mkali sana hadi Livna akamtolea macho ya hasira.
 
“Mwaharamu mkubwa wewe, unakazi ya kumuongopea hapa baba yangu kwamba una ujauzito, yaani huna chochote wala huna uwezo wa kubeba ujauzito. Umesahau miaka kumi nyuma kizazi chako kilifanywaje kule Urusi?”
Jojo alizungumza huku akiwa amemkazia macho Livna aliye nitazama kwa macho yaliyo jaa wasiwasi.
“Hivi unahisi hiyo roho yako mbaya unaweza kuibadilisha na kuwa nzuri, eheee?”
Jojo alizungumza kwa suati ya ukali na kumfanya Livna kutulia kwa muda kidogo huku macho yakiwa yamemtoka sana.
“Baba yangu alikuthamini sana na kukuamini ila sio hicho kitu ambacho unahitaji kukifanya kwa watu wake.”
 
“Ulipanga kumuwekea sumu, Yemi na Hawa, ili wafe na mimba zao na wewe ubaki na mimba hewa ni uongo?”
“Livna ni kweli anacho kizungumza Jojo?”
Livna akaka kimya huku macho yake akiwa ameyaelekezea chini.
“Unahisi unaweza kummiliki baba yangu, baba yangu moja ni mzuri, pili anajiweza na kujitambua. Kwa nini unataka kumrudisha nyuma ikiwa ninajua nina wadogo zangu wawili wanao kuja?”
“Livna nimekuiliza ni kweli?”
Nilizungumza kwa hasira huku nikipiga meza hii hadi Livna akastuka macho yakamtoka mwili mzima ukamtatetemeka. Waswahili wanasema kwamba ukimya nao pia ni jibu. Nikanyanyuka kwa haraka na nikamshika Livna mabega yake na kumnyanyua juu, nikamsogeza hadi ukutani huku nikiwa nimekasiria sana na macho yamenitoka.
 
“Kwa nini Livna unakuwa na roho za Kiswahili, kwa nini usingeniambia mapema kwamba nisiwalete hapa hao wasichana wa watu eheeee?”
Nilizidi kuzungumza kwa uchungu sana huku machozi ya hasira yakinimwagika usoni mwangu.
“Da……d….”
Livna alishindwa kabisa kuliita jina langu, kinywa chake kimejawa na uzito ambao hakuutarajia kuupata kwa muda huu.
 
“Unahitaji niondoke hili eneo si ndio?”
“Hapana Dany, ninakupenda, ninakuhitaji mume wangu”
“Unahitaji kwa upuuzi huo wa kuhitaji kuwaua wezako eheeee. Wamekukosea nini viumbe wa watu  ambao wapo matumboni mwa hao wasichana. Kumbuka zile ni damu zangu, ni damu zangu kama ilivyo kwa Jojo pale, bora nife mimi kuliko zife damu zangu kwa nini lakini Livna”
“Dany na mimi nina wivu, na mimi nina wasiwasi wa kuachwa na wewe ukigundua kwamba sina mimba na wezangu wana mimba”
“So umeona njia ya kuwaua wao ndio sahihi si ndio eheheeee?”
Nilizunguma kwa ukali huku mwili mzima ukinitetemeka kwa wasiwasi.
“Sasa na Magreti eti pia unamuonea wivu ukapanga ukirudi umkamate na umtese ili akujibu ni kitu gani ambacho amekifanya huko na baba yangu”
 
Mameno ya Jojo yakazidi kunipatandisha hasira laiti kama ningekuwa na wezo wa kama Joho ningeuchomoa moyo wa Livna ambao kumbe umejaa uhasama mkubwa sana juu ya watu wenye ukaribu wangu.
“Magreti naye anatatizo gani, amekufanya nini binti wa watu ambaye hata swala la mapenzi halijuia. Hivi unahisi wezako hawana hisia, hawana miooyo hawana roho za kupenda kama unavyo penda wewe eheeee?”
Livna machozi yakazidi kumwagika usoni mwake, maneno ya kujitetea yakamtoweka kabisa akilini mwake.
“Si unaogopa mimi kukuacha, basi nitakuacha kuanzia hivi sasa mimi na wewe basi. Na kama kunisiaidia, mwisho uwe leo na nitajua nitafanya nini, nikifungwa, nikikikamatwa nikiuwawa yote ni kwa ajili ya dhambi zangu nilizo zifanya na nipo tayari kuzitumikia kwa namna yoyote na muda wowote. Nitaondoja na kila nilite kuja naye hapa, pia nitaondoka na Magret kwani ndio mwanamke ambaye ameziteka hisia za moyo wangu na ndio aliye kubaliwa na mwanangu awe mke wangu. Kwaheri”
Baada ya kumaliza kuzungumza maneno hayo nikamuachia Livna aliye toa ukunga mkali wa kulia kwani alicho kisikia ninaimani ni sawa na mkuki ulio uchoma moyo wake na kuutoboa tundu ambalo halito pona kabisa kwenye maisha yake.
 
AISIIIII……….U KILL ME 197

“Bye”   
Jojo alizungumza huku akinikimbili kwa nyuma, tukatoka katika chumba hichi. Tukaelekea katika chumba anacho ishi Hawa na Babyanka. Nikawakuta wakiwa wamekaa vitandani.
“Jiandaeni tunaondoka, Winy yupo wapi?”
“Jamani Dany hiyo ndio salamu?”
Hawa alizungumza huku akinitazama usoni mwnagu.
“Salamu ya kazi gani hembu chukueni kila kilicho chenu ninahitaji tuondoke hapa sasa hivi sawa?”
Nilizungumza kwa ukali sana.
 
“Hawa jifunze kusoma alama za nyakati”
Babyanka alizungumza huku akishuka kitandani mwake.
“Hata kama huo sio ustarabu, kukerwa akerwe na wengine hasira aje kutumalizia sisi, na unataka twende wapi?”
Hawa alizungumza kwa kujiamini huku akisimama, nikamtazama kuanzia juu hadi chini, kisha nikayarudisha macho yangu tumboni mwake na kuona ukubwa wa tumbo  umeongezeka.
“Tunaondoka katika hii meli, sihitaji nilio kuna nao humu kuendelea kuishi humu”
“Kwa sababu gani?”
“Livna alihitaji kuwau wewe na Yemi ili musiweze kuzaa watoto wenu”
Jojo aliniwahi kunijibu na kunifanya nimgeukie na kumtazama.
“Wewe ni nani unaye ingilia vitu visivyo kuhusu?”
“Nimwanangu”
“Mwanao…..!!!?”
 
“Unanitumbulia nini macho, ndio ni mwanangu”
“Hahahaaa Dany sasa unakuwa mwenda wazimu. Mtoto wa watu umemchukua humu humu ndani unajidanganya ni mwanao au ni wahiyari”
“Mwanangu wa kumzaa”
“Hhaaaa uwiiiiii, jamani hahaaa kumbe kuna siku ambazo unachangayikiwa. Sasa kama umechanganyikiwa siwezi kuondoka humu, nitmzaa mwanangu humu na atakulia humu sawa?”
Maneno ya Hawa yakazidi kunikera na kunipandisha hasira, nikatamani kumzaba kofi ila nikajikuta nikiuzuia mkono wangu kwa kukunja ngumi kwani ninafahamu kwamba nikimtandika ngumi itanigrimu sana kwenye maisha yangu na yake.
“Sijasingiziwa, huyu ni baba yangu wa damu, hata ukitupima DNA, basi tupo sawa”
 
“Heee makubwa haya”
“Babyanka hakikisheni kwamba munakusanya kila kilicho chenu tunaondoka hapa?”
“Siwezi kuondoka hapa, ninakuomba unisamehe”
“Unasemaje?”
“Nimesema kwamba siwezi kuondoka hapa ninakuomba unisamehe, sina sehemu ambayo nitakwenda na kuishi kwa amani kama ilivyo hapa kama Livna anahitaji kuwaua hawa basi ni acha na mimi nife tu”
“Mimi pia siondoki, una sehemu gani ya wewe kwenda kutuweka na kuwa salama?”
Hawa alizungumza kwa dharau sana.
“Baba tuondoke zetu”
Jojo alizungumza huku akinishika mkono.
“Baba huwezi kuwabadilisha hao, tayari wamesha kuwa wana ndoa, wanamahusiano ya jinsia moja”
Nikawaona Babyanka na Hawa wakistuka sana, wakatazamana na nikaona sura zao jinsi zinavyo poteza furaha. 
 
“Ni kweli anacho kisema Jojo?”
Hawa na Babyanka wakashindwa hata kunijibu na macho yao hayakuwa na ujasiri kabisa kunitazama usoni mwangu, nikakumbuka siku nilipo wakuta wakiwa wamekumbatiana na wamelala uchi kabisa.
“Tuondoke baba”
Jojo alizingumza huku akinishika mkono tukatoka chumbani humu na kukutana na Ester kwenye kordo akiwa ameongozana na wasichana wengine wanne wakiwa wameshika bunduki mikononi mwao.
 
“Dany samahani, ninafwata amri ya mkuu. Tumeambiwa tumkamate mwanao”
“Kwa kosa gani?”
“Sijajua kwa kweli, ila nimeambiwa nimemkamata”
“Ester natambua kwamba wewe ni mtendaji mzuri kwa Livna na hata kwangu ulifanya kila kitu kunisaidia kwa chochote ambacho nilikuomba kukifanya. Ninahitaji kukuomba hichi kitu cha mwisho tu na sinto kuomba tena”
Nikamuona Ester akishusha pumzi nyingi sana huku akiwa amejawa na huzuni kubwa sana kwani amelazimishwa kufanya kitu ambacho hajui hata sababu.
“Ninakuomba niondoke eneo hili, ninakuomba utuachie mimi na mwanangu tuweze kuondoka hapa”
Nilizungumza kwa sauti ya upole sana huku nikimtazama Ester usoni mwake.
“Muacheni apite”
Ester alizungumza huku akiwatazama vijana  wake alio ongozana nao, wasichana hawa wakatupisha taratibu na tukaanza kupita katikati yao huku nikiwa nimemshika mkokono Jojo. 
 
“Livna anajiingiaza kwenye tatizo ambalo litamshinda kulimaliza”
Jojo alizungumza huku akitazama nyuma.
“Tuachane naye”
“No lazima atawau hawa wasichana kwa kushindwa kutii amri yake.”
“Sasa tunafanyaje?”
“Hapo mbele atawatuma wasichana wengine waniangamize”
Jojo alizungumza huku tukizidi kutembea kwa mwendo wa haraka kwenye hii kordo ndefu.
“Simama”
Jojo alizungumza huku akijibaza kwenye ukuta kwa haraka na mimi nikajibanza kwenye ukuta, hazikupita hata sekunde kumi wakatokea wasichan zaidi ya sita wakiwa na silaha, kwa haraka Jojo akaanza kupambana nao, hazikupita hata dakika mbili wasichana wote wakawa wamelala chini huku wakiwa wamezimia.
 
“Siwaui kwa maana ninahitaji kumuonyesha Livna uwezo wangu”
Jojo alizungumza huku tukizidi kusonga mbele. Kadri jinsi tunavyo zidi kusonga mbele ndivyo jinsi tunavyo kutana na vikwazo za wasichana walio agizwa kumkamata Jojo ambaye hakuwa na haja ya kumuua zaidi ya kuhakikisha kwamba anawazimisha.
“Unaelekea wapi?”
Nilimuuliza Jojo huku tukimwafwata kwa nyuma. Jojo hakunijibu kitu chochote zaidi ya kuufungua mlango wa kuingia ndani ya chumba kimoja.
Tukamkuta Livna akiwa amekaa kwenye moja ya meza huku amezungukwa na wasichana zaidi ya kumi.
“Livna hivi unahisi kwamba una uwezo wa kupambana na mimi?”
 
Jojo alizungumza kwa sauti ya hasira kidogo huku akimtazama Livna.
“Siwezi kukuacha ukiwa hai, ni lazima nikuue”
“Hahaaa, unajiamini nini wewe, unanijua mimi ni nani?”
“Hei Livna najua una hasira ila ninakuomba mimi na mwanangu tuondoke hapa, sihitaji mafarakano mimi na wewe, au wewe na mwanangu”
“Mwanao wapi, umechukua malaya tu huko nje anaye jifanya anajua kuzungumza mambo ya watu ya nyuma ambayo hayamuhusu”
 
“Mimi ni malaya?”
Jojo alizungumza huku  akipiga hatua moja mbele kwa haraka nikamuwahi kumshika mkono wake na kumsimamisha.
“Ndio malaya”
“Livna hembu acha majibizano ya ajabu, tazama watoto wengine wa watu wamesha jeruhiwa elewa kwamba huwezi kumdhuru Jojo”
“Hembu niachie upuuzi na wewe, unaniletea malaya ndani kwangu leo hii unaniambia kwamba ni mwanao.”
Kwa kasi ya ajabu, Jojo akatoa mkono wake kwangu, kufumba na kumbua akawa amemfikia Livna aliye hisi kwamba wasichana wake wanaweza kumsaidia, nikastukia Livna akinyanyuliwa kwa mkono mmoja huku akiwa ameshikwa koo lake.
 
“Hivi unahisi kwamba ninashindwa kukua eheee”
Jojo alizungumza huku akizidi kumkaba Livna aliye anza kulitoa jicho lake akionekana kuanza kupoteza pumzi yake.
“Jojo Jojo”
Nilizungumza huku nikimftwa Jojo kwa ukaribu kabisa, nikamshika mkono alio mshika Livna, kusema kweli Jojo ana nguvu kubwa sana.
“Tafadhali  mwanangu ninakuomba umuachie”
Nilizungumza kwa upole sana huku nikumsisitizia Jojo kumuachia Livna kwa maana akiendelea kumshikilia hivi anavyo mshikilia ni lazima atakufa.
“Ukirudia na ukiendelea na mawazo ya  kuhitaji kumua yoyote kati ya wasichana wako au watu alio kuna nao baba yangu, nitahakikisha ninakurudia na nikirudi nitakigawanyisha kiuongo chako kimoja baada ya kingine.”
Jojo baada ya kumaliza kuzungumza hivyo akamuachia Livna aliye anza kuvuta pumzi nyingi huku akiwa amekaa chini.
“Tuondoke”
Jojo alizungumza huku akitangulia kutoka nje, hapakuwa na msichana hata mmoja aliye jaribu kumshika wala kumsogelea Jojo. Tukapandisha juu kabisa ya meli hii.
“Ninahitaji twende nyumbani sasa baba”
Jojo baada ya kuzungumza hivyo akanikumbatia kwa nguvu kisha tukajitosa kwenye bahari na nikajikuta nikianza kupiga kelele kwani kasi tunayo kwenda nayo chini kusema kweli inatisha na kuogopesa na ukitegema ni usiku  basi ujasiri ukaniisha kabisa.
 
ITAENDELEA
‘Haya sasa safatri ya kuelekea nyumbani kwa kina Jojo imeanza, je ina mafanikio yoyote kwa Dany? Usikose sehemu inayo fwata ya hadi hii ya kusisimua kutoka kwa muandishi mahiri Eddazaria G.Msulwa”


from MPEKUZI http://bit.ly/2T4KXFu
via Malunde
Share:

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 56

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA
Nikagonga kidogo na ukafunguliwa. Biyanka akanipokea kwa sura iliyo jaa hasira sana, sikuhitaji kusemeshea kitu cha aina yoyote zaidi ya kuingia ndani. Nikavua koti langu na kulirusha kwenye kiti.
“Umetoka wapi na ulikuwa wapi na ulikuwa na unafanyaje na kwa nini ulinikatia simu kisha ukazima eheeee?”
Biyanka alizungumza kwa ukali sana ambao sikuujali, nikaka kwenye sofa na kuweka nne, nikailegeze vizuri tai yangu kisha nikapitia meseji za afande Kimaro. Nikajikuta nikinyanyuka huku nikiwa nimejawa na mshangao mkubwa sana mara baada ya kusoma meseji ya Afande Kimaro akidai kwamba Clara haonekani hospitalini na askari wake wawili alio kuwa amewaacha waimarishe ulinzi wameuwawa usiku wa kuamkia leo.

ENDELEA
Sikutaka kuendelea kujishauri kichwani mwangu kwa muda mrefu, nikaitafuta namba ya afande Kimaro na kumpigia, ikaanza kuita kwa muda kisha ikapokelewa.
“Ndio, afande”   
“Nimejaribu kukupigia simu yako kwa muda kidogo nikaona kimya”
“Ni kweli afande nilizima ili watu wale walio panga kuniaua wasiweze kunitafuta kwa kupitia simu yangu”
Biyanka akastuka macho yakamtoka, kwa haraka akanisogelea sehehemu nilipo simama. Uso wa hasira ambao ulikuwa umumtawala nikaushuhudia taratibu ukianza kumuondoka na kuwa mpole huku akinisikiliza kwa umakini kile nilicho kizungumza.
 
“Ahaa sawa sawa nina imani kwamba meseji zangu umewezeza kuziona?”
“Ndio nimeweza kuzioana kwa sasa mupo wapi?”
“Nipo kituaoni, unaweza kufika”
“Sawa ninakuja sasa hivi”
Nikakata simu na kuirudisha mfukoni.
“Ethan nitakuwa nimesikia vibaya, umesema kwamba kuna watu walihitaji kukuaa?”
“Ndio”
 
Nikaitafuta meseji ya vitisho niliyo tumiwa na nikamkabidhi Biyanka simu yangu kisha mimi nikaelekea bafuni kuweza kunawa ili niweze kutoa harufu harufu ya pafyumu za Qeen na Latifa. Nikatoka bafuni na kumkuta Biyakna akizungumza na simu.
“Ehee baba wanamtishia mume wangu anahitaji kumuua”
Nikataka kumzuia Biyanka asizungumze na baba yake juu ya hili swala ila nikajikuta nikiwa nimesha chelewa kumzuia.
“Ndio nimekutumia, tayari hiyo namba. Hembu  baba nakuomba basi watu wako wa usalama wamtuafute muhisika wa hili tukioa basi”
“Mume wangu anaogopa amekuwa ni mtu wa kuzima zima simu kila mara jamani”
 
Biyanka alizungumza kwa masikitiko makubwa akionekana ameguswa sana na hili swala.
“Ndio yupo hapa”
“Eheee”
Biyanka akanikabidhi simu yake nikaiweka sikioni.
“Shikamoo baba”
“Marahaba. Ethan una ugomvi na mtu wa aina yoyote?”
“Hapana baba yangu, Tanzania mimi sina hata rafiki kabisa, na nimeshangaa mtu huyo ni wapi  ameipatia namba yangu na kwa nini ananitisha ikiwa sijafanya jambo lolote baya”
“Punguza wasiwasi, swala lako  nitalihushulikia mwanagu sawa”
“Sawa baba yaani nimejikuta ninanunua gari jipya ili wasiweze kunikremisha kwamba ni mimi”
“Hahaaa, hivi huna mlinzi”
“Ndio kwa sasa sina mlinzi”
“Basi nitaagiza vijana wangu wawili wawe wanakulinda kila unapo kwenda. Nina imani wana ujuzi mkubwa sana wa kukufanya uwe salama kila muda”
“Nashukuru sana baba yangu”
 
“Sawa sawa, niwatakie mchana mwema na nitawajulisha mara baada ya kuweza kumkamata muhusika wa hili tukio”
“Sawa baba”
Nilijikaza kumuita tu baba, ila laiti kama angefahamu kwamba yeye ndio adui yangu namba moja basi asinge weza kujipendekeza sana kwangu. Simu ikakatwa, Biyanka kwa haraka akanikumbatia huku akilia.
“Jamani pole mume wangu, nilihisi kwamba unanisaliti jamani”
“Siwezi kukusaliti mke wangu, kwa nini nifanye hivyo ikiwa nina kupenda kuliko kitu chochote.”
“Nisamehe kwa kuweza kukufikiria vibaya mpenzi wangu. Nisamehe kwa kweli”
“Usijali mpenzi wangu. Nahitaji kuelekea polisi kwa sasa, tunaweza kuongozana?”
“Ndio”
 
“Nitolee nguo hapo kabatini”
Biyanka akaniachia na kufanya nilicho muagiza. Nikavaa nguo hizi huku nikijaribu na mimi kuweza kuumiza kichwa juu ya baba mdogo wa Clara tuliye mkamata ana kundi kubwa kiasi gani la kuweza kufanya mauaji ya kiasi hichi kisa kikubwa ni Clara.
“Usiwe na mawazo sana mume wangu, kila jambo litakuwa sawa”
Biyanka alizungumza kwa sauti ya upole huku akinitazama usoni mwangu. Tulipa maliza kujiandaa tukatoka ndani humu na kuelekea eneo la maegesho. Tukaingia kwenye gari langu hili jipya.
“Gari nzuri”
Biyanka alizungumza huku akilichunguza gari langu kwa ndani.
 
“Nashukuru, walinzi wako wapo wapi?”
“Gari zao zile pale”
Tukaanza kuondoka eneo hili taratibu huku gari za walinzi wa Biyanka zikitufwata kwa nyuma. Tukafika kituo kikuu cha polisi na moja kwa moja tukaelekea ofisini kwa afande Kimaro. Akatukaribisha kwa furaha kiasi huku wakionekana kufahamiana sana Biyanka.
“Ila baba anaendelea vizuri”
“Ndio anaendelea vizuri na nilisha mdokezea juu ya lile ombi lako la kuwa IGP”
“Akasemaje?”
“Kama kawaida yake, subiri nipate Ikulu mwanangu kila jambo litakwenda sawa”
 
Biyanka alizungumza huku akiwa ameiigiza sauti ya baba yake jambo lililo tufanya sote tucheke.
“Kumbe muna fahamiana na Ethan?”
“Ndio ni mume wangu mtarajiwa”
“Weee kumbe ningemkoromea mwanzoni nahisi hata hii nafasi ningepokonywa”
“Haaaa ndio”
“Nashukuru Mungu damu zetu mimi na Ethan zimeendana”
“Nanyi mumejuana vipi?”
“Ni swala la binti mdogo aliye muokoata nina imani kwamba atakuwa amekusimulia?”
“Binti gani mume wangu?”
 
“Yule niliye kuambia kwamba nimemuokota kule kwenye maegesho ya magari pale ofisini”
“Ahaaa…ehee amefikia wapi?”
Afande Kimaro akafungua faili moja na kulisogeza karibu yetu. Tukaona picha za askari walio uwawa katika mlango wa chumba ambacho alilazwa Clara.
“Muuaji ni mwanamke, sura bado hatujaweza kuifahamu na alivalia mavazi ya kidaktari na aliweza kuifumba sura yake kwa kutumia vile vitambaa vyoa wakiwa katika chumba cha upasuaji”
Afande Kimaro alizungumza huku akituonyesha picha za msichana huyo ambazo imerekodiwa na CCTV kamera. 
 
“Baada ya kufanya mauaji ya vijana wetu wawili, akaingia ndani na kumchukua mtoto nahisi alimchoma sindano ya usingizi, alimpakiza kwenye kiti kile cha magurudumu nakuanza kumsukuma kumpeleka nje na aliweza kuzi vunja kamera za nje ambazo hatukuweza kujua aliondoka pale hospitalini kwa gari gani”
 
“Ila pale hospitalini niliweza kumuona mlinzi naye hakuona jambo lolote?”
“Mlinzi hadi sasa hivi hajulikani ni wapi alipo. Ila vijana wangu wanaendelea na msako mkali sana na watahakikisha kwamba wanamtia nguvuni msichana huyo”
Nikashusha pumzi nyingi huku nikionekana kuchoka sana.
“Je muhusika wa namba ambaye amenipa vitisho vipi?”
“Yule muhisika bado tunaendelea kuitafuta namba yake kwenye mitandao ila bado hatujampata”
“Basi utanifahamisha kile ambacho kitaendelea”
“Sawa Ethan”
 
“Kimaro, jitahidini basi, mume wangu mumemfanya aishi maisha ya woga ikiwa yupo Tanzania nchi yenye amani kuliko nchi zote Afrika bwana”
“Usijali nitahakikisha hili swala linakwenda kuwa sawa hivi karibuni”
“Sawa tunashukuru”
Tukaagana na afande Kimaro na kutoka ofisini humu. Tukaingia kwenye gari letu huku kichwa changu kikiwa na msongamano wa mawazo.
“Utaweza kuendesha kweli mume wangu?”
Nikamjibu Biyanka kwa kutingisha kichwa nikimaanisha kwamba sinto weza kuendesha gari hili. Nikampisha Biyanka kwenye siti ya dereva na tukaondoka eneo hili la kituo kikuu cha polisi cha kati.
 
“Kichwa chako mume wangu hakipo sawa, unahitaji tuelekee wapi kupata mapumziko”
“Nahitaji kwenda kulala sasa hivi”
“Huitaji kukaa labda kwenye sehemu ukapunga upepo wa bahari hivi”
“Nahitaji kulala, watu wananiwinda. Unataka wakaniulie huko baharini ehee?”
Nilizungumza kwa ukali kidogo huku machozi yakinilenga lenga usoni mwangu. Biyanka akajawa na unyonge ulio mfanya ajikute akiomba msamaha pasipo kunifanyia jambo lolote baya. Tukafika hotelini na kuingia chumbani kwetu.
“Ethan naona ni vyema nikakuacha peke yako upumzike, ninaelekea nyumbani nitarudi usiku”
 
“Sawa”
Biyanka akanitazama kwa muda kidogo kisha akanisogelea na kunibusu mdomoni mwangu.
“Ninakupenda sana mume wangu”
“Ninakupenda pia mke wangu”
“Kweli?”
“Ndio au unahisi kwamba nina kudanganya?”
“Hapana mume wangu, nashukuru kwa kunipenda”
“Poa”
Nikajitupa kitandani, Biyanka akanitazama kwa unonge sana kisha akanivua viatu, akaviweka sehemu yake, akataka kunivua suruali ila nikamzuia kwa ishara.
“Nenda tu nyumbani”
“Sawa mume wangu”
Biyanka akanibusu shavuni kisha akatoka ndani humu. Nikanyanyuka kwa haraka hadi mlangoni, nikaufunga vizuri kwa komeo, kisha nikaitoa simu yangu mfukoni na kumtafuta Camila nina imani kwamba atakuwa amenitafuta. Simu ya Camila ikaanza kuita, kisha aikapokelewa.
“Niambie mume wangu”
“Poa baby vipi?”
“Safi, leo nimehitimu mafunzo yangu ya juto, kung fu na taikondo”
 
“Umeyasomea wapi hayo mafunzo”
“Si Dany amenifundisha, yaani hapa nipo vizuri sana. Mtu anizingui kabisa”
“Hahaa kama ninakuona vile”
“Weee yaani, siku nikikufuamania na mwanamke, yaani nitampiga hadi ajute kuzaliwa”
Tabasamu nililo kuwa nalo usoni mwangu, likapotea gafla kwani hiyo ni si taarifa nzuri kwani huku nilipo nimesha tambulishwa kabisa.
“Sawa mama”
“Mbona unanijibu kwa unyonge”
“Hamna, mwenzangu sasa hivi upo vizuri, mimi bado”
“Nitakufundisha. Uzuri wa mke wako kichwa changu kina shika mambo kwa haraka na ninaweza kumsaidia hata mtu mwengine katika swala zima la kumfundisha”
 
“Sawa, ehee niambie”
“Kesho ninaanza mazoezi mawili ya mwisho, moja ni kutumia upanga na na jengine kutumia silaha”
“Mmm angalia asije kufundisha ugaidi bure”
“Hahaaa hii ni kwaajili ya kujilinda na familia yetu. Natambua baba wewe una mambo mengi kwa namna moja ama nyingine mimi mama nitasimama kama mlinzi wako”
“Hahaa, haya bwana mama watoto”
“Nikimaliza, tunarudi Ujerumani, ume umemaliza, hujamaliza tunarudi Ujerumani. Mama yangu amenimiss sana”
“Sawa mpenzi wangu, wanaendeleaje lakini?
 
“Wanaendelea vizuri”
“Nashukuru kusikia hivyo”
“Fanya uwasiliane nao”
“Poa mpenzi wangu”
“Haya baadae, tambua nina kupenda na kukuhitaji. Mtu akijichanganya kwako nami ninamchanganya kisawa sawa”
“Hahaa haya bwana mama”
Nikakata simu, nikaitafuta namba ya mtu ambaye amenitumia meseji ya vitisho, nikampigia ila kwa bahati mbaya nikakuta kwamba hapatikani hewani. Gafla nikamuona Ethan akiwa amekaa kwenye moja ya sofa huku akiwa amevalia suti nyeupe na inayo ng’ara vizuri.
 
“Naona unaumiza kichwa sana kwa mtu aliye kukoromea?”
“Wewe unahisi nitakuwa na furaha jaaa yangu”
“Hhaaa….hawawezi kukuua”
“Wewe umesha mfahamu mtu ambaye amenitishia?”
“Ninaweza kumfahamu”
“Ni nani”
“Vaa viatu twende”
Nikavaa viatu na tukatoka katika chumba hichi na Ethan, watu ninao kutana nao njiani hawawezi kumuona Ethana zaidi ya mimi pekee, nikakabidhi kadi ya chumba changu mapokezi na tukaingia kwenye gari. Ethan akaanza kunielekeza hadi kwenye moja ya gorofa moja linalo jenge na halijamaliziwa.
 
“Simamisha gari hapa, tukifika pale mambo yanaweza kuwa mabaya”
“Kwani ni kina nani?”
“Wewe twende”
Nikasimamisha gari kwenye mitimiti kadhaa, tukashuka kwenye gari na Ethan akanisogogelea na kunishika mkono wangu wa kulia na kuniambia kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kuniona nikitembea katika eneo hili. Tukapandisha hadi gorofa ya tano, nikaanza kusikia vilio vya mtu akigugumia kulia kwa kipigo anacho kipokea kutoka kwa mtu anaye mpiga. Tukaingia kwenye chumba hicho, sikuamini macho yangu mara baada ya kumkuta baba mkwe, Biyanka pamoja na walinzi wapatao kumi huku Biyanka akimpiga kijana huyo kwa rungu kubwa.
 
“Niliwakanya mucheze na kote ila si kucheza na mume wangu. Kama muna fanya kazi chini ya baba yangu mufanye tu ila si kumgusa mume wangu sawa wewe mwana haramu”
Biyanka alizungumza  huku akihema, akafuta jasho linalo mtiririka usoni mwake, kisha akaandelea kumshushia marungu kijana huyu huku baba yake akitabasamu kwa binti yake kuifanya kazi hiyo ya kikatili sana.

==>>ITAENDELEA KESHO


from MPEKUZI http://bit.ly/2FCqTrb
via Malunde
Share:

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,


from MPEKUZI http://bit.ly/2ASUqZo
via Malunde
Share:

Tiba Asilia ya Tatizo la Nguvu za Kiume

Kifaru vidonge asilia hurefusha maumbile ya kiume nchi 6-8 dk 60 garantii mika 30- 40 .itakupa nahamu ya kufanya tendo la ndoa mara 4- 5 bila kuchoka au hamu kuisha, ina imalisha misuri  ya uume  na haina madhara kwa mtuaji

Malelemba; inatibu presha kisukari, ngili, busha bila uperesheni, kiuno, kutopata choo vizuri, vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto, kisosono

Jirumba; kumvuta mume mke mpenzi mchumba kwa masaa 3 yoyote unae mtaka  uta mpata ..acha kuumiza roho bure hatakama una fanya nae kazi sehemu moja ila unaogopa kumuanza au muone mzee jirumba atakusaidia

Fika mbagara kwa wa mikoani shinyanga kahama mwanza kwa mawasiano piga 0713560943 /0762540447 dr jirumba


from MPEKUZI http://bit.ly/2W3JkKh
via Malunde
Share:

Bunge la Ujerumani Lapiga Kura.....Laukataa Mradi wa Stiegler's Gorge Tanzania

Bunge la Ujerumani limepitisha muswada wa kuitaka serikali ya Ujerumani itafute njia mbadala ya mradi wa Tanzania wa kuzalisha nishati ya umeme katika Bonde la Stiegler kwenye Mto Rufiji, kusini mwa Tanzania ili kulinda turathi na asili.

Wabunge wa vyama vilivyomo katika serikali ya mseto ya Ujerumani; CDU/CSU, Kijani na AFD walishiriki katika kupiga kura hiyo lakini chama cha mrengo mkali wa kulia cha AfD, hakikushiriki. Azimio la vyama vya CDU,CSU na SPD pia linatokana na mapendekezo ya Kamati ya Serikali ya Ujerumani ya Ushirikiano wa Kiuchumi.

Azimio lililopitishwa bungeni na vyama hivyo vilivyomo katika serikali ya mseto ya Ujerumani linaitaka serikali kuu isaidie katika masuluhisho ya kukidhi mahitaji ya nishati ya Tanzania bila ya kuathiri mazingira. Katika azimio lao, vyama hivyo vimesema mradi huo mkubwa wa kuzalisha nishati ya umeme utavuruga mfumo wa mto mmojawapo mkubwa barani Afrika.

Tanzania inakusudia kujenga bwawa kubwa la kuzalisha nishati ya umeme kwa kutumia nguvu ya maji kutoka kwenye Mto Rufiji. Sehemu hiyo ni muhimu kwa shughuli za kilimo za wakazi wake. Ikiwa mradi huo utaendelea,  Bonde la Stiegler ambalo ni miongoni  mwa turathi za Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), litapoteza hadhi yake na huenda likasababisha athari kubwa katika raslimali zilizopo kwenye sehemu hiyo.

Katika ombi lao kwa serikali ya Ujerumani, wabunge wa vyama vya CDU, CSU na SPD wamesema sehemu hiyo ya mbuga ya wanyama ya Selous nchini Tanzania ni eneo kubwa na kongwe la hifadhi ya wanyamapori barani Afrika.

Wabunge hao wamesema mradi huo wa bwawa la nishati utahitaji sehemu kubwa itakayotokana na kukatwa kwa miti na hivyo kusababisha athari kubwa katika mazingira, tabianchi na katika uchumi.

Wabunge wa chama cha upinzani cha FDP wameshauri kujengwa kinu cha nishati kutokana na gesi kwa sababu Tanzania inayo gesi ya kutosha iliyogunduliwa hivi karibuni.   Chama hicho kilichopinga azimio hilo,  kimeitaka serikali ya Ujerumani ifanye mazungumzo na serikali ya Tanzania.

CREDIT: DW


from MPEKUZI http://bit.ly/2QZVfFk
via Malunde
Share:

CHADEMA Wapinga na Kulaani Madai ya DC Sabaya Kumnyang'anya Freeman Mbowe Ofisi ya Ubunge

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Hai kimesema mkuu wa wilaya hiyo, Lengai ole Sabaya amepotosha umma kueleza kuwa amemnyang’anya ofisi mbunge wa jimbo hilo, Freeman Mbowe ilhali hajawahi kuwa na ofisi katika jengo la halmashauri hiyo.

Januari 14, Sabaya alitangaza kumnyang’anya ofisi ya ubunge Mbowe baada ya kueleza hajaitumia tangu mwaka 2010 hivyo itatumiwa na idara ya uhamiaji.

Wakizungumza katika ofisi ya mbunge huyo jana, mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Helga Mchomvu ambaye pia diwani wa Muungano alisema wanalaani kauli ya Sabaya kwa kuwa amepotosha umma.

Mchomvu alisema ofisi ya mbunge huyo ipo mji mdogo wa Bomang’ombe.

“Wananchi ondoeni hofu huduma katika ofisi ya mbunge zinaendelea kama kawaida, katibu wake yupo na ofisi haijawahi kufungwa, muda wowote wananchi njooni,” alisema.

Hata hivyo, Sabaya alipoulizwa kwa simu jana kuhusu madai hayo ya Chadema, alisema ameshafunga suala hilo hivyo wamwache aendelee na kazi za wananchi.

Mbowe yupo gerezani baada ya kufutiwa dhamana na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa madai kuwa alikiuka masharti ya dhamana yeye na mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko.


from MPEKUZI http://bit.ly/2W5IQn4
via Malunde
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger