Thursday, 29 December 2016

Wassira akimbilia Mahakama ya Rufaa kumpinga Bulaya

WAZIRI mwandamizi wa serikali ya Tanzania kwa awamu nne za uongozi, Stephen Masato Wassira, kupitia kwa wafuasi wake watatu, amekata rufaa Mahakama ya Rufaa, akipinga uamuzi wa Mahakama Kuu kwa kuhalalisha ushindi wa Mbunge wa Bunda Mjini, Esther Bulaya (Chadema).

Wassira (71 ) alikuwa waziri kwa mara ya kwanza tangu Desemba 07, 1973 akiwa naibu waziri wa Kilimo na ameendelea kuwa kiongozi mwandamizi wakati wa serikali ya Mwalimu Julius Nyerere, akarithiwa wakati wa Rais Ali Hassan Mwinyi, baadaye Rais Benjamin Mkapa na hatimaye uongozi wa awamu ya nne wa Rais Jakaya Kikwete.

Tayari wafuasi hao wa Wassira; Magambo Masato, Matwiga Matwiga na Ascetic Malagaila, wamefungua kesi hiyo na imesajiliwa katika ofisi za mahakama ya rufaa jijini Mwanza tarehe 16 Desemba, 2016 na itakuwa ni kesi ya rufaa namba 199 ya mwaka 2016.

Katika rufaa hiyo iliyoandikwa na wakili wao, Constatine Mutalemwa, wametoa sababu kadhaa kama hoja zao za kukata rufaa.

Kwanza, wanadai kwamba jaji hakuzingatia makosa yaliyofanyika baada ya zoezi la kupiga kura.

Pili, Wassira au wakala wake wanadai hakuitwa kwenye majumuisho kujulishwa siku, mahali wanafanyia majumuisho.

Tatu, wanadai kuwa jaji hakutilia maanani kesi zinazofanana na hii zilizotolewa kama mfano mahakamani.

Nne, Jaji alikosea kutoa uamuzi kwa misingi ya maoni binafsi badala ya kuzingatia mambo ya maana.

Wanadai kuwa jaji alisema wananchi wa Bunda ni maskini waachwe wafanye shughuli za maendeleo kwa sasa.

Tano, wanadai jaji alikosea kuamua kuhusu sheria ya viapo na matamko iliyotajwa katika kanuni za kuendesha kesi za uchaguzi.

Novemba 18, mwaka huu, Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza ilitoa uamuzi wa kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa ubunge uliompa ushindi Mbunge wa Bunda Mjini, Esther Bulaya (Chadema) dhidi ya Stephen Wassira (CCM).

Kesi hiyo ya kupinga matokeo ya uchaguzi ilifunguliwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, lakini ilikuwa inasikilizwa mjini Musoma, mkoani Mara.

Mahakama hiyo ilieleza kutoridhishwa na ushahidi wa kupinga matokeo hayo uliowasilishwa na upande wa walalamikaji, hivyo ikamthibitisha Bulaya kuwa mbunge halali wa jimbo hilo.

Kesi ya kupinga matokeo hayo ilifunguliwa na wafuasi wa Wassira ambaye alikuwa mbunge wa jimbo hilo kabla ya kuondolewa kupitia uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka jana.

Katika kesi ya msingi, walalamikaji ambao ni wakazi wa Bunda walidai kuwa uchaguzi haukuwa huru na haki kwakuwa uligubikwa na vitendo vya rushwa, mgombea wanaemuunga mkono kunyimwa fursa ya kuhakiki matokeo pamoja na kuongezeka kwa idadi ya vituo vya kupigia kura visivyo halali.

Katika kesi hiyo, Bulaya alitetewa na mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu.
Credit: FikraPevu
Share:

Bodi ya Mikopo yawatosa Watanzania wanaosoma China

Watanzania waliopata ufadhili wa kusoma nchini China, hawatapata mikopo baada ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kuwaondoa kwenye orodha ya wanufaika. 
Taarifa iliyotolewa na HESLB, ikijibu Ubalozi wa Tanzania nchini China, kuhusu madai ya kuchelewa kwa fedha za mikopo kwa wanafunzi wanaosoma nchini humo imeeleza kuwa hatua hiyo inatokana na maelekezo ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwamba wanafunzi wote wanaopata ufadhili kutoka nchi rafiki watajitegemea ikiwamo gharama za tiketi za ndege.

Barua hiyo ya Desemba 20, 2016 iliyomnukuu Mkurugenzi Mtendaji wa bodi hiyo, Abdul Razaq Badru inaeleza kuwa mwaka huu wanafunzi hao hawatanufaika na mikopo kama ilivyokuwa ikitolewa miaka ya nyuma.

Jana, akizungumza na waandishi wa habari, Badru aliitambua barua hiyo huku akisita kutolea ufafanuzi wake kwa madai ilikuwa ni majibu kwa wanafunzi hao wa China.

Hata hivyo, alisema endapo kutakuwa na madai kutoka kwa wanafunzi hao watalazimika kutolea ufafanuzi.

Akizungumzia suala hilo Naibu Waziri Elimu, Stella Manyanya alisema ni hekima zaidi kuangalia au kusaidia wanafunzi wa ndani wasiokuwa nacho kuliko wanaopata ufadhili wa nje ya nchi.
Share:

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI DEC TAREHE 29.12.2016


Share:

Wednesday, 28 December 2016

SEKRETARIETI YA AJIRA DAR IMEFAFANUA TAARIFA KUHUSU KUFUTWA KWA AJIRA SERIKALINI WALIOFAULU USAILI

 Image result for SERIKALI YA TANZANIA

TAARIFA KWA UMMA



Mnamo tarehe 26 na 27 Desemba, 2016 baadhi ya mitandao ya kijamii imeandika taarifa zenye nia ya kupotosha Umma ambazo Sekretarieti ya Ajira inapenda kuzitolea ufafanuzi kama ifuatavyo;-
1. Sekretarieti ya Ajira inapenda kutoa ufafanuzi kufuatia hoja iliyoandikwa katika baadhi ya mitandao ya kijamii ya tarehe 27 Desemba, 2016 zenye vichwa vya habari vinavyosomeka “Waliofaulu usaili ajira serikalini kufutwa” na “Taarifa kwa waliokuwa wakisubiri kupangiwa vituo vya kazi kabla ya ajira kusitishwa serikalini” zikidaiwa kutolewa na Taasisi hii katika majibu ya hoja za mwezi Novemba, 2016 katika utaratibu wake wa kujibu hoja za kila mwezi kama ifuatavyo;- 
Kwa mujibu wa kumbukumbu za Sekretarieti ya Ajira tangu mwezi Juni, 2016 Serikali  ilipositisha  Ajira  hapakuwa na orodha ya waombaji kazi waliokuwa wakisubiri matokeo ya usaili, kwa kuwa usaili wa mwisho ulioendeshwa na Sekretarieti ya Ajira ulifanyika mwezi Mei, 2016 na waombaji waliofaulu walipangiwa vituo vya kazi kwa idaidi ya nafasi zilizokuwepo.
Aidha, kwa wale ambao walifaulu na hawakuweza kupangiwa vituo vya kazi  kutokana na kukosekana kwa nafasi zilizokuwepo walihifadhiwa katika kanzidata (Database) ambayo hudumu kwa  muda cha miezi sita (6) baada ya matokeo ya usaili husika kutolewa.
Baada ya ufafanuzi huo hususani aya ya tatu Sekretarieti ya Ajira ingependa kufafanua zaidi namna kanzidata ya waliofaulu usaili inavyotumika ili kuweza kuwa na uelewa wa pamoja kwa wadau na jamii kwa ujumla ili kuepusha kupokea ama kusikia taarifa  zisizo rasmi zenye nia ya kupotosha Umma zinazojitokeza mara kwa mara hususani katika baadhi ya mitandao ya kijamii.
Kanzidata ya waliofaulu  usaili:
Kwa mujibu wa Kanuni za Uendeshaji wa shughuli za Sekretarieti ya Ajira za mwaka 2016, Kanuni ya 21. (1) - (5) imefafanua juu ya kanzidata kama ifuatavyo;-
(1) Baada ya waombaji waliofaulu usaili kuwapangia vituo vya kazi, orodha itakayobaki itatunzwa na Katibu katika kanzidata ili pale itakapotokea fursa ya ajira orodha hiyo iweze kutumika.
(2) Orodha ya waombaji walioko kwenye kanzidata itatumika kujaza nafasi wazi kulingana na mahitaji ya Waajiri. Hata hivyo, wakati wa upangaji, Katibu atazingatia mpangilio wa matokeo ya alama za ufaulu wa mwombaji kwa aliyepata alama za juu zaidi ya wengine kufikiriwa kwanza.
(3) Sekretarieti itatangaza nafasi wazi za ajira na kufanya usaili endapo orodha iliyotunzwa katika kanzidata itakuwa imekwisha au haina mtumishi mwenye utaalam au sifa zinazohitajika na Mwajiri.
(4) Endapo katika orodha iliyotajwa kwenye Ibara ya 21(2) kutakuwa na waombaji waliopata alama zinazolingana, utaratibu ulioainishwa katika Ibara ya 14(1) utazingatiwa.
(5) Orodha ya kanzidata itadumu kwa kipindi cha miezi sita (6) tangu kuidhinishwa kwa matokeo na Wajumbe wa Sekretarieti.
2.       Sekretarieti ya Ajira pia inapenda kutoa ufafanuzi kwa taarifa nyingine iliyoandikwa katika mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari kinachosema “Mhe Rais Magufuli nakuomba Sekretarieti ya Ajira uifute maana haina majukumu sasa hivi lengo la Sekretarieti ya Ajira ni kutangaza kazi na ........”. kama ifuatavyo;-
Ni vyema wadau wa Sekretarieti ya Ajira na Jamii kwa ujumla ikafahamu kuwa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma ilianzishwa kupitia Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 18 ya mwaka 2007 kifungu cha 29 (1). Kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa na Sheria Na. 18 ya mwaka 2007 kifungu cha 29 (6) (a-f) na Sera ya Menejimenti ya Ajira toleo Na. 2 la mwaka 2008 Sekretarieti ya Ajira ina majukumu yafuatayo;-
i.        Kutafuta wataalam wenye ujuzi maalum na kuandaa mfumo wa kuhifadhi taarifa (kanzidata) za wataalam hao ili kurahisisha utaratibu wa kuwaajiri pindi wanapohitajika,
ii.       Kuandaa orodha ya wahitimu wa Vyuo Vikuu na Wataalam Weledi (Professionals) kwa madhumuni ya kurahisisha rejea na ujazaji wa nafasi wazi za ajira katika Utumishi wa Umma,
iii.      Kutangaza nafasi wazi za kazi zinazotokea katika Utumishi wa Umma.
iv.      Kuhusisha wataalam maalum (Appropriate experts) kwa ajili ya kufanya usaili kulingana na mahitaji,
v.       Kutoa ushauri kwa Waajiri kuhusu masuala mbalimbali yanayohusiana na ajira,
vi.      Kufanya kazi nyingine yoyote inayoendana na majukumu yake kadri itakavyoelekezwa na Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma.
Kutokana na ufafanuzi huo Sekretarieti ya Ajira ingependa jamii ifahamu mbali na jukumu la kuendesha mchakato wa Ajira ina majukumu mengine inayoyatekeza kama yalivyoainishwa hapo juu kwa mujibu wa Sheria.

Riziki V. Abraham
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, Sekretarieti ya Ajira.
27 Desemba, 2016.
Share:

MWALIMU ASHUSHIWA KIPIGO KWA KUMCHARANGA MAPANGA MWANAFUNZI WAKE SIKU YA KRISMASI



Kijana Limbe akipata matibabu
Mwalimu Pendo akipata matibabu
*****

MWANAFUNZI Marco Limbe(14) aliyemaliza darasa la saba mwaka huu katika shule ya msingi Yitwimila iliyoko kata ya Kiloleli wilaya ya Busega mkoani Simiyu amelazwa katika kituo cha afya Busega mara baada ya kuchalangwa mapanga kichwani na mdomoni na mwalimu wake.



Tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 11.30 jioni wakati mwanafunzi huyo alipokuwa akirejea nyumbani kwao akitokea katika malisho ya mifugo,alipokaribia katika shamba la mwalimu Pendo Gabriel ndipo mwalimu huyo alimkamata kijana huyo na kuanza kumcharanga kwa panga na kusababisha kijana Limbe kupoteza fahamu kwa muda wa masaa 6.

“Shuhuda wa tulio hilo aliyejitambulisha kwa jina moja la Manoga anasema ilikuwa kama mchezo lakini kumbe ni kweli kwani niliona mifugo ya Limbe iliyokuwa ikielekea nyumbani na huku Limbe akiwa nyuma ya mifugo hiyo katika barabara ambayo iko karibu na maeneo ya shule, ghafla nilimuona mwalimu Pendo wakishikana na kijana huyo na ndipo nikamuona akiwa na panga na kuanza kumcharanga”,alieleza.
"Nilikimbia katika tukio na kutoa msaada kwa wote lakini, watu walijaa na kuanza kumshambulia mwalimu Pendo kwa kumpiga ingawa jaribio hilo lilikwama baada ya mwenyekiti wa kijiji hicho Mshemas Bahai.
Mwandishi wa habari hizi alikwenda katika kituo cha afya cha Nyashimo na kujionea hali mbaya kwa kijana Limbe ambaye alikuwa amepoteza fahamu kwa muda wa masaa 6 bila kujitambua na huku akiwa anaongezewa drip na kwa pembeni mwalimu Pendo Gabriel naye akipata matibabu ya jeraha lake kichwani ambAlo alishambuliwa na wananchi na huku akiwa chini ya ulinzi wa jeshi la polisi.
Mwenyekiti wa Sogesca Bahai Mshemas alisema sikukuu Krismasi imekuwa ni mbaya katika kijiji chake baada ya wananchi wenye hasira kali kufanya shambulio la kumshambulia mwalimu Pendo kwa kosa la kumcharanga na panga mwanafunzi wake aliyekuwa akitokea kwenye malisho na kupita karibu na shamba lake la mahindi akitokea katika malisho.
Hata hivyo alisema alifanikiwa kuwatuliza wananchi wa kijiji chake na kuanza kufanya mikakati ya kuwapeleka kituo cha afya ili wapate huduma za matibabu.
Aliongeza kuwa walifika polisi na kuandikiwa barua ya kwenda kutibiwa wote wawili mwalimu pamoja na mwanafunzi.
Kwa upande wake kaimu mganga mfawidhi wa kituo hicho cha afya Dk. Ayubu Ismail alithibitisha kuwapokea kwa majeruhi hao na kudai kuwa kijana Limbe ndiye aliyekuwa na hali mbaya zaidi kuliko mwalimu Pendo.
Aliongeza kuwa kijana ameshonwa nyuzi 9 katika sehemu zake zote alizopatwa na majeraha na huku mwalimu  akishonwa nyuzi 6.
“Ni kweli Limbe alikuwa ametokwa na damu nyingi sana na hivyo kumpelekea kupoteza fahamu kwa muda wa masaa 6 lakini hali yake inaendelea vizuri alisema Dk. Ismail”.
Na Shushu Joel- Busega
Share:

NYOKA WA MAAJABU AFA NA MTU WAKE,ALIKUWA AMEMBEBA KWENYE NGUO YAKE



DUNIANI kuna mambo, ndivyo unaweza kusema kutokana na mkazi wa Mtaa wa Mateka, Manispaa ya Songea, Denis Komba (26) kufa baada ya nyoka wake aliyekuwa amembeba kwenye mfuko wa jaketi kuuawa na wananchi.
Komba alifariki dunia katika hospitali ya Rufaa Songea mkoa wa Ruvuma (Homso) ambako alilazwa baada ya watu wenye hasira kumuua kwa mawe na fimbo nyoka wake huyo.
Mashuhuda wanaeleza kuwa kabla ya wananchi kumuua nyoka huyo, Komba aliwasihi wasifanye hivyo kwa kuwa wakimuua na yeye angekufa, lakini ombi lake hilo halikusikilizwa.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, siku ya tukio Komba alikodi pikipiki ya Kassian Haule (24) ambaye ni mkazi wa Mpitimbi, yenye namba za usajili MC 724 AKB ili apelekwe nyumbani kwake mtaa wa Mateka.
Akisimulia tukio hilo, alisema alipofika katika eneo la Benki ya Posta ya zamani barabara kuu ya Sokoine, dereva wa pikipiki alihisi kuna kitu kinamtekenya na kumgonga gonga kwa nyuma, ndipo alipogeuka nyuma na kumwona abiria wake amebeba nyoka mkubwa huku amesimamisha kichwa.
Haule alisema, baada ya kumuona nyoka huyo aliruka kutoka kwenye pikipiki na kuanguka pembeni mwa barabara na abiria wake alimwachia yule nyoka ambaye alikimbilia kwenye kalavati la maji.
Aliongeza kuwa ndipo alipopiga kelele za kuomba msaada na kundi la vijana waendesha pikipiki wenzake walifika eneo hilo la tukio kwa lengo la kumsaidia mwenzao juu ya maswahiba yaliyompata hadi kumfanya apige kelele.
Alisema kabla ya vijana hao hawajafanya jambo lolote, Komba aliwaomba vijana hao na watu wengine waliofika katika eneo hilo wasimpige nyoka wake kwani iwapo watampiga na kufa yeye pia atapoteza maisha. Kutokana na maneno hayo, Haule alimtoa nyoka huyo ndani ya kalavati na kwa kushirikiana na vijana wenzake walianza kumpiga nyoka huyo hadi kufa.
Alisema wakati wanampiga nyoka huyo, Komba ambaye ndiye mmiliki wa nyoka huyo naye alianza kulegea kisha akaanguka chini huku akitokwa na mapovu mdomoni na puani.
Habari zinasema kuwa,baada ya Komba kuanguka alikimbizwa hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu; hata hivyo juhudi za madaktari na wauguzi wa hospitali za kuokoa maisha yake zilishindikana kwani Komba alifariki.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Zuberi Mwombeji, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa mwili wa marehemu haukuwa na jeraha lolote na umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya rufaa Songea.
Alisema nyoka aliyeuawa na wananchi amechukuliwa na idara ya maliasili na uchunguzi zaidi ya tukio hilo unaendelea ili kubaini kiini cha tukio hilo la kuuawa kwa nyoka na kisha mmiliki wake naye kufa. Kamanda Mwombeji alisema, kwa upande wa dereva wa pikipiki yeye anaendelea vizuri na anapatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Ruvuma.
Aidha Kamanda Mwombeji, ametoa rai kwa wananchi kuacha mara moja kumiliki nyara za serikali zinazoweza kuwaletea madhara kama vile majeraha au vifo.
Aidha katika tukio lingine, mkazi wa kijiji cha Mdunduwalo Joseph Charles (27) amefariki dunia kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali tumboni na Oddo Komba (34) mkazi wa Mhepai Peramiho baada ya kuhitilafiana wakati wakitoka kunywa pombe.
Kamanda huyo wa polisi alisema, tukio hilo limetokea tarehe 26 mwezi huu saa 1 usiku katika kijiji cha Mtyangimbole kata ya Gumbiro katika halmashauri ya wilaya ya Madaba wilayani Songea ambapo chanzo cha mauaji hayo ni ugomvi uliotokea njiani kati yao wakati wakirudi nyumbani kutoka kwenye klabu za pombe ya kienyeji.
IMEANDIKWA NA MUHIDIN AMRI- habarileo SONGEA
Share:

MWANAFUNZI APIGWA RISASI KWENYE MGOGORO WA NYUMBA


Mwanafunzi wa kidato cha pili wa shule ya sekondari Mringa, Vanessa Josephat [16] mkazi wa Sakina jijini Arusha amejeruhiwa vibaya kwa kupigwa risasi kichwani na walinzi wa kampuni ya ulinzi ya kifaru waliokuwa wakiwatoa kwa nguvu kwenye nyumba yao yenye mgogoro .
Tukio hilo limethibitishwa na kamanda wa jeshi la polisi mkoani Arusha Charles Mkumbo ambaye alisema kuwa polisi inamshikilia Fabian Charles mlinzi wa kampuni ya kifaru pamoja na silaha aina ya shoot gun iliyo tumika katika tukio hilo huku majeruhi amelazwa katika hospitali ya KCMC kutokana na hali yake kuwa mbaya .
Kamanda mkumbo alisema kuwa tukio hilo limetokea jana majira ya saa tatu asubuhi katika eneo la sakina jijini hapa, ambapo alisema walinzi watatu wa kampuni hiyo waliokuwa wakilinda nyumba hiyo inayomilikiwa na Josephat Nehemia walitumia silaha hiyo kuwafyatulia familia inayoishi hapo ili waondoke na ndipo silaha hiyo ilipomjeruhi mwanafunzi huyo .
Taarifa zinaeleza kuwa December 21 mwaka huu kampuni ya udalali ya Marc Recorders Limited wakiwa na mabaunsa na watu wengine walivamia nyumba hiyo na kuwatoa nje wamiliki wa nyumba hiyo na kuondoka na vyombo vyao vya ndani wakidai nyumba hiyo imeshauzwa kwa , Thobias Ludovick Senya baada ya mmiliki kushindwa kulipa deni la shilingi million 3.7 alilokuwa akidaiwa na taasiai ya fedha Heritage.
Baada ya tukio hilo familia hiyo yenye watu wapatao kumi wakiwemo watoto na kichanga walianza kulala nje kando ya geti la nyumba hiyo wakipigwa na baridi kali pasipo kuwa na msaada wowote
Mmiliki wa nyumba hiyo Josephat Nehemia Ogaga alisema baada ya familia yake kutolewa nje wakati yeye akiwa safarini walikuja walinzi hao wa kampuni ya kifaru na kuanza kulinda na baada ya yeye kurejea alifanikiwa kuwaondoa walinzi hao na kuirejesha ndani familia yake akidai taratibu za kuuza nyumba yake hazikufuatwa ila kilichofanyika ni uhuni .
“Nikweli nilikuwa nadaiwa na Heritage financial shilingi milioni 3 .7 na nililipa deni na kubaki shilingi million 1.8 hivyo hatua ya kuja kuuza nyumba yangu yenye thamani shilingi million 200 kwa deni hilo ni uhuni mtupu umefanyika” alisema Nehemia
Hata hivyo siku moja baadae walinzi hao walirejea tena wakiwa na silaha za moto na kuanza kufyatua risasi ovyo ndani ya nyumba hiyo kwa lengo la kuwatisha familia hiyo ili waondoke ndani ya nyumba hiyo ambapo moja ya risasi ilimjeruhi mwanafunzi huyo kichwani ambaye amelazwa katika hospitali ya rufaa ya KCMC Mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya matibabu
Kamanda Mkumbo amezitaka kampuni za ulinzi kutoingilia migogoro bila kufuata utaratibu kwani vyombo vyenye mamlaka ya kushughulikia migogoro kama hiyo vipo na hivyo amezitaka kampuni za ulinzi kufuata taratibu zao za utendaji wa kazi na kuacha kukimbilia maslahi yao ya kupata fedha haraka,
Mkumbo alisema mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu shitaka linalomkabili.
Share:

Waziri Mkuu: Waliofaulu Ni Lazima Waende Sekondari

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali haitavumilia kuona mamia ya vijana waliofaulu mitihani ya darasa la saba na kuchaguliwa kuingia kidato cha kwanza wanabaki nyumbani eti kwa kuwa hakuna madarasa ya kutosha.

“Serikali haitaridhika kuona vijana waliofaulu vizuri wanashindwa kwenda kidato cha kwanza. Halmashauri zilijua tangu mapema ni wanafunzi wanaenda shule za msingi kwa hiyo inataka kuona wote waliofaulu wanakwenda sekondari kwa asilimia 100,” amesema.

Ametoa kauli hiyo jana  mchana wakati akizungumza na viongozi na watendaji wa mkoa wa Lndi mara baada ya kupokea taarifa ya mkoa huo kwenye Ikulu ndogo wilayani Nachingwea. Waziri Mkuu amewasili wilayani Nachingwea akiwa njiani kuelekea Ruangwa kwa mapunziko ya mwisho wa mwaka.

Alisema Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kutoa elimu ya bure kwa kila mtoto sasa iweje watoto wengine wanafaulu na wanashindwa kujiunga na elimu ya sekondari. 
“Tumesema elimu ni bure hakuna sababu ya kufanya wengine wasiende shule wakati azma ya Serikali ni kutoa elimu ya bure. Hakikisheni wote wanaingia katika chaguo la kwanza,” alisema.

Aliwataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri ambazo zimefaulisha wanafunzi lakini hazina madarasa na madawati ya kutosha warudi mezani na kujipanga upya ili kuhakikisha wanafunzi wote waliofaulu wanapangwa na kuanza na wenzao katika chaguo la kwanza kwani wakisubiri chaguo la pili wanakuwa wamechelewa.

“Kama tumepokea vijana wengi kwenye udahili wa kidato cha kwanza, ni dhahiri kuwa ,tutapata Vijana wengi watakaomaliza kidato cha nne. Sote tunajua kuna agizo la kila tarafa kuwa na sekondari moja ya kidato cha tano na sita, nataka utekelezaji wa agizo hili usimamiwe kuanzia sasa.”

“Tafuteni moja kati ya shule kwenye tarafa zenu na ipandishwe hadhi kwa kuwekewa miundombinu inayotakiwa ya bwalo, jiko, mabweni, mifumo ya maji, madarasa na vyoo vya kutosha,” alisema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alisema atafuatilia ili abaini ni kwa nini taasisi ya maghala ya Serikali inadai tozo kwa wakulima wanaohifadhi mazao kwenye maghala hayo.

Waziri Mkuu alisema atapitia sheria ya kuanzishwa kwa taasisi hiyo ili kuona kama inaruhusu tozo hizo na kuangalia sheria gani inawaruhusu kutoza kodi. Alihoji inakuwaje taasisi ya Serikali inatoza tozo kwenye maghala ambayo yamejengwa na wananchi.

Akitoa mfano kuhusu ghala la Liwale, Waziri Mkuu alisema: “Kuna viagency vimeanzishwa kazi yao ni kutoza mapato tu. Inakuwaje kunakuwa na taasisi imekaa tu na kuanza kutoza tozo kwa wananchi wanaotumia facility za Serikali. Sheria ya kutoza tozo imetokana na nini na hizo zinakwenda kwa nani, je srikali imeanza kufanya biashara?,” alihoji.

“Nimepata taarifa kuwa walikuja kuzuia mazao yasitoke hadi wao walipwe, hapana huu siyo utaratibu. Ni kwa nini tuwanyang’anye fedha wale waliojenga ghala? Wao walijenga ghala kutokana na ubunifu halafu unasema unawapa sh. 7/- kwa kilo wakati wewe umetoza sh.25/- kwa kilo moja. Hapana hilo halikubaliki,” alisisitiza.

Waziri Mkuu alisema kama Serikali inaruhusu kuwepo kwa tozo hizo kwa jambo ambalo wananchi wamelibuni wenyewe, basi ilipaswa kudai kodi na hiyo kodi ilitakiwa kukusanywa na Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) na siyo vinginevyo.

Waziri Mkuu alisema atafuatilia wakala mbalimbali walioanzishwa kwenye wizara kwani kuna nyingine zinafanya kazi ambazo zilistathili kufanywa na idara kwenye wizara mama.
    
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
Share:

Malipo ya Korosho: Waziri Mkuu Awasha Moto,Ataka Majibu Kucheleweshwa kwa Malipo ya Wakulima

Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATANO DECEMBER TEREHE 28.12.2016

Share:

Tuesday, 27 December 2016

SERIKALI IMESITISHA KUWAPA UFADHILI WANAFUNZI WANAOSOMA NCHINI CHINA

http://www.jamiiforums.com/mobile-gallery/34b9f1fcb30783d19882a9d6410b364d.jpg
Share:

NAFASI ZA KAZI 191 NIROD CONSULTANTS, TUMA MAOMBI KABLA YA TAREHE 2 JANUARY 2017

Function: DISTRICT LOCAL GOVERNMENT OFFICERS 72 vacancies)

Employer: International NGO
Job Location: Agricultural Zones in Tanzania ( 17 regions )
Commitment: Permanent Career Position
Organization Description

Source: MKaguzi Blog
Our client is an agricultural NGO in Tanzania,Kenya, Rwanda,Uganda and Burundi that is innovating a new way of helping farm families to achieve their full potential. Our client invests in farmers to generate a permanent gain in farm income.
They provide farmers with a “market bundle” that includes education, finance, seed and fertilizer, and market access. Their program is proven impactful – every year, they weigh thousands of harvests and measure more than 100% average gain in farm income per acre.
Thgey are growing quickly. In five years, they have grown to serve 89,000 farm families with more than 500 full-time field staff.
Job Title – DISTRICT LOCAL GOVERNEMENT OFFICERS
Number of positions- 72 openings
Our client is a rapidly growing organization; increasing the number of sub-locations, districts, and members they serve in each year.
Our client is seeking 72 District local government officers to serve as:
-a first point of contact for local officials;
-an administrator for reports and meetings;
– a resource for risks and issues involving local officials.
-They would begin engaging with local government officials through district meetings and forums (DAC, DDC, and DSHF) in their respective Districts

REPORTING LINE :
-This role would report to the government relations analyst and demonstrate a strong understanding of local government structures,
-have an interest in agriculture,
-be prepared to travel regularly in Agricultural Zones of Tanzania and
-be an effective communicator.
-The role requires someone with IT skills, and at least diploma or undergraduate degree.
Duties of the Local Government Officers

    Draft reports for new district introductions and quarterly operations updates, in consultation with FDs
    Arrange new district introduction meetings and track operations meetings
    Gather information on the activities of government and other non-state actors at the local level
    Track risks and issues emanating from local officials that affect 1AF’s operations, and coordinate resolutions
    Report back to operations staff on local government relations, including risk/issue reporting
    Draft responses to local officials, in consultation with FDs, following reports on risks/issues
    Maintain key local government official contacts database and track interactions
    Provide 1AF field staff training on building relations with local officials
    Provide updates on local government relations at FD meetings
    Coordinate 1AF involvement in district shows and arrange field days and DAO functions
    Manage local government engagement budget

Career Growth and Development
Our client invests in building management and leadership skills. They provide constant, actionable feedback delivered through weekly mentorship and through regular career reviews. They also have regular one-on-one meetings, where They listen to and discuss career goals, and work collaboratively to craft roles that each person can be passionate about.
Qualifications
We are seeking exceptional professionals with a six months of work experience, and a demonstrated long-term passion for sustainable agricultural development in Tanzania.
We are looking for extraordinary candidates that are proactive; please only apply if you fit these criteria:.

    Leadership experience at work, or outside of work: Demonstrated experience leading a team and managing other people.
    Proven ability to set and meet targets on the job
    Clear communicator/mentor
    Proactively solve problems
    Top-performing Certificate / diploma or degree in social sciences, administration, finance, accounting, agriculture or other relevant fields, from a recognized college or university
    Integrity and a positive attitude
    Demonstrated computer skills in email, internet usage, Microsoft Office
    High quality work with a strong attention to detail
    A willingness to commit to living in remote places for a long time
    Languages: Fluent in Kiswahili and English required
    Passionate about serving smallholder farmers

Timeline: Resumes should be submitted by 02/01/2017.
We will begin interviews in early January and plan to have new officers begin by the second week of January, 2017
Compensation: Competitive Salary
Benefits: NSSF and NHIF, airtime, hardship and transportation allowances
Career development: Twice annual career reviews and constant feedback. Your manager will invest significant time in your career development.
NOTE: CERTIFICATE HOLDERS SHOULD ONLY APPLY FOR WARD LOCAL GOVERNMENT OFICERS AND NOT OTHERWISE
Industry: Nonprofit / International Development / Agriculture / Microfinance


Function: WARD LOCAL GOVERNMENT OFFICERS 106 vacancies)
Employer: International NGO
Job Location: Agricultural Zones in Tanzania ( 17 regions )
Commitment: Permanent Career Position
Organization Description
Our client is an agricultural NGO in Tanzania,Kenya, Rwanda,Uganda and Burundi that is innovating a new way of helping farm families to achieve their full potential. Our client invests in farmers to generate a permanent gain in farm income.
They provide farmers with a “market bundle” that includes education, finance, seed and fertilizer, and market access. Their program is proven impactful – every year, they weigh thousands of harvests and measure more than 100% average gain in farm income per acre.
Thgey are growing quickly. In five years, they have grown to serve 89,000 farm families with more than 500 full-time field staff.
Job Title – WARD LOCAL GOVERNEMENT OFFICERS
Number of positions- 106 openings
Our client is a rapidly growing organization; increasing the number of sub-locations, districts, and members they serve in each year.
Our client is seeking 106 Ward local government officers to serve as:

    a first point of contact for local officials;
    an administrator for reports and meetings;
    a resource for risks and issues involving local officials.
    They would begin engaging with local government officials through district meetings and forums (DAC, DDC, and DSHF) in their respective Districts

REPORTING LINE :
-This role would report to the government relations analyst and demonstrate a strong understanding of local government structures,
-have an interest in agriculture,
-be prepared to travel regularly in Agricultural Zones of Tanzania and
-be an effective communicator.
-The role requires someone with IT skills, and at least diploma or undergraduate degree.
Duties of the Local Government Officers

    Draft reports for new district introductions and quarterly operations updates, in consultation with FDs
    Arrange new district introduction meetings and track operations meetings
    Gather information on the activities of government and other non-state actors at the local level
    Track risks and issues emanating from local officials that affect 1AF’s operations, and coordinate resolutions
    Report back to operations staff on local government relations, including risk/issue reporting
    Draft responses to local officials, in consultation with FDs, following reports on risks/issues
    Maintain key local government official contacts database and track interactions
    Provide 1AF field staff training on building relations with local officials
    Provide updates on local government relations at FD meetings
    Coordinate 1AF involvement in district shows and arrange field days and DAO functions
    Manage local government engagement budget

Career Growth and Development
Our client invests in building management and leadership skills. They provide constant, actionable feedback delivered through weekly mentorship and through regular career reviews. They also have regular one-on-one meetings, where They listen to and discuss career goals, and work collaboratively to craft roles that each person can be passionate about.
Qualifications
We are seeking exceptional professionals with a six months of work experience, and a demonstrated long-term passion for sustainable agricultural development in Tanzania.
We are looking for extraordinary candidates that are proactive; please only apply if you fit these criteria:.

    Leadership experience at work, or outside of work: Demonstrated experience leading a team and managing other people.
    Proven ability to set and meet targets on the job
    Clear communicator/mentor
    Proactively solve problems
    Top-performing Certificate / diploma or degree in social sciences, administration, finance, accounting, agriculture or other relevant fields, from a recognized college or university
    Integrity and a positive attitude
    Demonstrated computer skills in email, internet usage, Microsoft Office
    High quality work with a strong attention to detail
    A willingness to commit to living in remote places for a long time
    Languages: Fluent in Kiswahili and English required
    Passionate about serving smallholder farmers

Timeline: Resumes should be submitted by 02/01/2017
We will begin interviews in early January and plan to have new officers begin by the second week of January, 2017
Compensation: Competitive Salary
Benefits: NSSF and NHIF, airtime, hardship and transportation allowances
Career development: Twice annual career reviews and constant feedback. Your manager will invest significant time in your career development.
NOTE: -CERTIFICATE HOLDERS SHOULD ONLY APPLY FOR WARD LOCAL GOVERNMENT OFICERS AND NOT OTHERWISE
-APPLICANTS FROM LOCAL GOVERNMENT TRAINING INSTITUTES ( HOMBOLO ) ARE HIGHLY ENCOURAGED TO APPLY AND WILL BE GIVEN FIRST PRIORITY
APPLY ONLINE THROUGH
-SEND YOUR FULL RESUME HERE : nirodconsultants@gmail.com  or before 02/01/2017
-include your referees plus contacts
-WRITE YOUR NUMBER IN THE SUBJECT LINE PLUS THE POST YOU ARE APPLYIMNG FOR ( EXAMPLE – RE: ‘ 0777 999 999 – WARD LOCAL
Share:

NAFASI MBALI MBALI ZA KAZI REGEN CONSULTANTS CO. LTD TUMA MAOMBI KABLA YA TAREHE 1 JANUARY 2017


COMPANY: REGEN CONSULTANTS CO. LTD
HEAD OFFICE: ILALA - TABATA - TANZANIA
Email:  regencorporateopenings@gmail.com

CLERICAL OFFICERS – 14 POSITIONS

 Responsibilities and duties:

The officer will carry out the following duties:
•    Assisting on clerical works in the various sections in the sector.
•    Assisting in maintaining registry and circulation of files in various sections.
•    Assisting in filling and maintaining of mailing records in the sector.
•    Assisting in ensuring that proper recording and Safety, health and environmental standards are maintained in the sector.
•    Assisting in other computer related works in the sector.
•    Assisting in procurement, accounting and administrative offices.
•    Any other duties assigned by the senior officers in various sections of the sector.
Qualifications:
•    At least a Certificate in office management or secretarial course or any clerical related field.
•    Certificate in Computer applications
•    Good communication skills.

REGISTERED NURSES – 22 POSITIONS
Duties and Responsibilities
•    Assessing, planning, implementing nursing interventions and evaluating patients outcomes.
•    Providing appropriate healthcare services including integrated management of Childhood Illnesses (IMCI), immunization, PMTCT, ante-natal care and delivery , providing health education and counseling to patients and clients appropriately.
•    Referring patients and clients appropriately.
•    Facilitating patients admission and initiating discharge plans.
•    Ensure a tidy and safe clinical environment
•    Collecting and compiling data
Requirements
•    Diploma in any of the following disciplines: Community Health Nursing,  Nursing, Midwifery, Nursing/Midwifery or Nursing/Mental Health and Psychiatry from a recognized institution.
•    Certificate in computer application skills from a recognized insitution.


WATER SURVEYORS -  48 POSITIONS

Responsibilities and duties
The officers will carry out the following duties:
•    Field Surveys of projects
•    Responsible for working drawings for water and sanitation development projects
•    Responsible for setting out and checking of levels during constructions
•    Responsible for preparation supervision, monitoring and evaluation of water and sanitation infrastructural projects.
•    Responsible for Baseline Survey and feasibility studies for proposed projects
•    Resource mapping in the Sector
•    Responsible for collecting and collating data for preparation of BQs for development projects.
Requirements
•    BSc in Survey and Photogrammetry or diploma in Hydrological survey with required experience or equivalent qualification from recognized institution.
•    Years’ experience in a similar field

ADVISORY MANAGERS - 14 POSITIONS
Advisory Deals-Transactions Manager Job
 Our client is a  network of firms in 157 countries with more than 702,,000 people who are committed to delivering quality in Assurance, Tax and Advisory services. The client’s purpose is to build trust in society and solve important problems. The client’s in-depth knowledge and understanding of operating environments in East Africa and West Africa  regions enables them to put themselves  in their clients’ shoes and offer truly tailored Tax, Assurance and Advisory solutions to unique business challenges.
In Advisory, they help organisations to work smarter and grow faster. They consult with their clients to build effective organisations, innovate, grow, reduce costs, manage risk and regulation and leverage talent.
Advisory Manager Job Purpose
•    We are seeking to strengthen our Advisory services by recruiting and developing highly motivated individuals for the position of Managers  in our Deals Transactions – Sub Line of Service.
•    The position holders will lead and manage consulting assignments in delivery of client strategic projects in Valuations/Pricing, Due Diligence, Structuring deals and transactions and / or Merger and Acquisitions (M&A).
•    These positions are based in Tanzania  to lead such projects in the East Market Area (EMA).
Responsibilities
•    The job holders will be expected play an important role in the business development and delivery of client assignments through active pursuit and conversion of leads, preparation of Proposals in response to Requests for proposals (RFPs) issued at the bidding phase and leading The Company’s  teams on putting together proposals from the network
•    Constantly develop and demonstrate subject matter expertise in our service offerings and act as trusted advisor to our clients
•    Working with the PCS and Private Sector Mergers & Acquisitions deal cycle
•    Understanding of the basics of Valuations/Pricing, Due Diligence, Structuring deals and transactions in complex Sales & Purchase Agreements
•    Undertaking buy side, sell side and contingent fee based lead advisory roles
•    Enhancing good relationship base and experience in EMA countries in this and wider Corporate Finance areas
•    Manage delivery of client assignments based on the Company’s  service offerings and methodologies Manage project economics through delivery within budget, timely billing and collection
•    Maintain excellent relationships with our clients
•    Lead and coach less experience team members
Qualifications For Advisory Manager Job
•    Master in Business Administration, Financial or Economics
•    A Bachelor’s Degree in Finance, Accounting or Economics
•    Experience of 3 and above  Years of experience in the professional services firms, investment Banks, and or private Business
Required Skills & Competencies
•    Related professional certifications and qualifications
•    Excellent team leadership, interpersonal and collaboration skills
•    The ideal candidate needs to have been playing a major role in running transaction deals from a sell side, buy side, and or finance raising. Knowledge of the local PCS market, the Private Equity houses, and the overall
•    Transactions dynamics that drive these opportunities.
•    Ability to build long term relationships, with PCS clients, and work across borders on international or inter Africa transactions
•    In depth knowledge of the full cycle of the deals process, from pitching to deal closure, including the ability to deal with the financial institutions on financing propositions
•    Experience in relationship building and ability to deliver projects and close deals.


YARD SUPERVISORS – 12 POSITIONS

Our client  is a global integrated energy producer and provider, a leading international oil and gas company, and the world’s second-ranked solar energy operator with SunPower. Their 100,000 employees around the world are committed to better energy that is safer, cleaner, more efficient, more innovative and accessible to as many people as possible.  As a responsible corporate citizen, they focus on ensuring that their operations in more than 130 countries worldwide consistently deliver economic, social and environmental benefits.  In Tanzania, they are  a major player in the Oil and Gas sector with 125 service stations across the country.


Job Summary: The Yard Supervisor will carry out safety checks on trucks and wagons entering the depot as well as calibration charts, dipsticks.


Key Duties and Responsibilities:
•         The incumbent will observe and implement the company HSE programs in the depot
•         Supervise tank dipping on a daily basis as per the required standards
•         Carry out safety checks on trucks and wagons entering the depot as well as calibration charts, dipsticks
•         Regularly analyse the safe to load data and ensure that all trucks are effectively assessed using this tool
•         Deploy and supervise Operatives to maximise full productivity and efficiency
•         Maintain the cleanliness of the depot to the required standards
•         Manage safe transition of the depot maintenance to the night guards after the day’s operations


Qualifications, Skills and Experience:
•         The applicants  should hold at least a good diploma in  Engineering
•         A minimum of two years working experience in a petroleum-related role
•         Broad knowledge of the Petroleum industry operations with an appreciation of Operational Health and Safety
•         Highly flexible, quick to adapt, self motivated and able to supervise others
•         Proven ability to work under pressure with minimum supervision
•         Excellent computer and numeric skills
•         Excellent interpersonal and communication skills.


A MINING ( PETROLEUM / OIL / GAS ) COMPANY ( SEVERAL POSITIONS )
Our Client  is a subsidiary of Sinopec Group, the Number 5 of Fortune Global 500 companies and the world’s third largest petrochemical group. The company has recently embarked on an ambitious growth programme and as a result there are numerous openings within its subsurface, drilling and facilities teams for seasoned and performance driven employees and consultants.

It was founded in 1994 upon leading petroleum industry expertise and a deep-rooted understanding and respect for African cultures. Over the years, Our cleint  has evolved from a young pioneer into an established international oil and gas, exploration and production company focused on Africa and the Middle East.

Its assets are located in Nigeria, the Joint Development Zone of Sao Tome & Principe, Gabon, Cameroon and the Kurdistan Region of Iraq, comprising an excellent combination of oil and gas reserves and exploration opportunities.

The Company now holds a total of 32 licensed blocks undergoing exploration, development or production, with 26 offshore and 6 onshore. The Company’s approximate average oil production is in excess of 160,000 bbl/d.

It has over 1000 employees worldwide with a service office in Geneva (Switzerland) and operating offices in Lagos and Abuja (Nigeria), Port-Gentil (Gabon) and Douala (Cameroon).
Get recognition for your talent!.

With its current presence in East Africa and Tanzania in particular, our client is now  recruiting to fill the following positions with immediate effect;

•    Controls and Instrumentation Engineer ( several openings )
•    Pipeline Engineer ( several openings )
•    Piping Engineer ( several openings )
•    Structural Engineer ( several openings )
•    Structural Autocad Operator ( several openings )
•    Project Engineers (Platform and FPSO) ( several openings )
•    Project Services Lead ( several openings )
•    Cost and Controls Engineer ( several openings )
•    Planning Engineer ( several openings )
•    Electrical Engineers ( several openings )
•    Project Controls Engineers ( several openings )
•    Principal Drilling Engineers ( several openings )
•    Drilling Engineers ( several openings )
•    Day Drilling Supervisor ( several openings )
•    Asset Managers ( several openings )
•    Geologists ( several openings )
•    Geophysicists ( several openings )
•    Reservoir Engineers ( several openings )
•    Production Technologist ( several openings )
•    Petroleum Engineers ( several openings )

QUALIFICATIONS:

-At least A degree in any related field
- At least 1 year experience in the field
- Must be fluent in English ( written and spoken )
- Must be A Tanzanian Citizen
- Must be able to drive and use a computer easily


GENERAL APPLICATION INSTRUCTIONS
SEND YOUR FULL RESUME WITH THREE PROFESSIONAL REFEREES
INCLUDE YOUR DAY TIME NUMBER IN THE SUBJECT LINE PLUS THE POST YOU ARE APPLYING FOR e.g RE: 0768 000 000 - MINING ENGINEER
APPLY ONLY ONCE IN YOUR AREA OF INTEREST ( NEVER APPLY TWICE- this will lead to an automatic disqualification  )
SEND YOUR APPLICATIONS HERE :  ( regencorporateopenings@gmail.com ) on or before January, 01/01/2017
Share:

NAFASI YA KAZI DRIVER TANROADS – SIMIYU TUMA MAOMBI KABLA YA TAREHE 17 JANUARY 2017

NAFASI YA KAZI DRIVER TANROADS – SIMIYU
The regional manager’s office TANROADS- SIMITU on behalf of the Executive TANROADS intends to recruit qualified and competent Tanzanians to fill the post on specific duty short-term contract within the Region
QUALIFICATIONS
·         Age not below 25 and not above 35 years of age
·         educational minimum qualification holder of ordinary secondary educations
·         driving certificates from recognized institutions is an advantage preferable from  national institute of transport
·         must have genuine and valid driving license Class D
·         must be fluent I Kiswahili and English language
·         must have a clean track record
·         must be a Tanzania citizen
DUTIES AND RESPONSIBILITIES
o   drive Agency motor vehicle
o   maintains vehicle logbook
o   check and report the maintenance requirements
o   maintain safety and cleanliness of the motor vehicle delivers and collect mail goods etc
o   perform other duties as may be assigned from the time to time supervisor
MODE OF APPLICATIONS
All interested are invited to apply and submit their handwriting applications letters to the mentioned address not later than 17th Januarys with  their CV, and copies of all academic certificates and birthdates and names of 3 referees address of previous employers applicant applications letter should be in English language
Applications letter should be posted /emailed to the following address  hand delivery is acceptable
REGIONAL MANAGER,
TANROADS,
NYAKABID AREAS,
P.O. BOX 389,
SIMIYU.
Fax no 028 2986334
Telephone 028 2986332
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger