Sunday, 18 December 2016

Msanii Darasa akiwa na Hanscana wapata ajali ya gari huko Kahama

Mwanamuziki Darasa amepata ajali maeneo ya Ntobo barabara yakuelekea mgodi wa Bullyanhulu wilaya ya Kahama mkoa wa Shinyanga. Waliokuwa garini wote wamenusurika.

Katika gari hiyo pamoja na watu wengine alikuwa na mtayarishaji wa video aliye kwenye chart Hanscana.




15492537_10206378362818256_6093491712623732141_n.jpg 15492570_10206378362218241_7745684630275410784_n.jpg
 
Share:

Ma-DC hatarini kutumbuliwa

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa

WAKUU wa Wilaya (Ma-DC) na Wakurugenzi nchini, ambao hawajakamilisha kutengeneza madawati, yanayokidhi idadi ya wanafunzi katika shule za maeneo yao, wamepewa siku 14 kukamilisha kazi hiyo.
Imeelezwa kuwa wanafunzi watakapofungua shule, lazima wakae kwenye madawati hayo.
Wakuu wa wilaya na wakurugenzi, watakaoshindwa kutimiza agizo hilo hadi ifikapo Desemba 30, mwaka huu, watakuwa wamejifukuzisha kazi wenyewe.
Aidha, wametakiwa kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kwenda kidato kwanza mwakani, wanaanza masomo yao kwa awamu moja, badala ya awamu mbili tofauti.
Agizo hilo lilitolewa jijini hapa jana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati akizungumza na watumishi wa wilaya ya Arumeru katika ziara yake ya kikazi mkoani hapa.
Aliagiza wakuu wa wilaya na wakurugenzi wote nchini kuwa hadi Desemba 30, mwaka huu wilaya zote zenye upungufu wa madawati ziwe zimekamilisha.
“Wale ambao watashindwa kufanya hivyo, watakuwa wamejifukuzisha kazi wenyewe” alisema. Akizungumzia ukusanyaji wa mapato katika wilaya hiyo, Majaliwa alisema kuwa hadi Desemba 30, mwaka huu, wawe wamefikia asilimia 50, tofauti na hali ya sasa ambapo wamekusanya asimilia 30 tu. “Ongezeni kasi ya ukusanyaji wa mapato katika halmashauri zenu na mhakikishe kila mtu anafanya kazi zake kwa kumheshimu mwenzie,” alisema Waziri Mkuu.
Serikali inahitaji haraka madawati ili kuondoa uhaba unaozikabili shule za sekondari na msingi wa madawati. Hali halisi ikoje? Hadi sasa, zaidi ya madawati milioni moja, sawa na asilimia 88 ya madawati yanayohitajika katika shule za msingi na asilimia 95 kwa shule za sekondari, yamepatikana. Kwa shule za msingi, imebaki asilimia asilimia 12 kumaliza tatizo la madawati, huku shule za sekondari imebaki asilimia 5.
Mikoa sita ambayo ina hali mbaya na haijatekeleza kikamilifu agizo hilo la madawati ni Mwanza, Kigoma, Mara, Rukwa, Simiyu, Dodoma na Geita, ambapo Geita inadaiwa madawati zaidi ya 80,000 ya shule za msingi na sekondari.
Mwanza inadaiwa madawati 41, 438, Kigoma madawati 31,171, Mara madawati 16,978, Dodoma madawati 14,873, Rukwa madawati 10,978 pamoja na Mkoa wa Simiyu.
Mkoa wa Mwanza unaundwa na wilaya za Nyamagana, Ilemela, Misungwi, Kwimba, Ukerewe, Magu na Sengerema, wakati wilaya za mkoa wa Kigoma ni Buhigwe, Uvinza, Kakonko, Kasulu, Kibondo na Kigoma.
Wilaya za mkoa wa Mara ni Tarime, Bunda, Butiama, Musoma, Serengeti na Rorya na Mkoa wa Rukwa una wilaya za Sumbawanga, Kalambo na Nkasi.
Mkoa wa Simiyu wilaya zake ni Bariadi, Maswa, Busega, Meatu, Itilima na Mkoa wa Dodoma wilaya zake ni Kondoa, Bahi, Mpwapwa, Kongwa, Dodoma, Chamwino na Chemba, wakati mkoa wa Geita wilaya zake ni Geita, Chato, Bukombe, Mbogwe na Nyang’hwale.
Mikoa ambayo imemaliza tatizo hilo la madawati kwenye shule za msingi na sekondari ni 14 ambayo ni Mtwara, Lindi, Dar es Salaam, Arusha, Iringa, Kilimanjaro, Mbeya, Ruvuma, Njombe, Manyara, Pwani, Shinyanga, Singida na Tabora.
Mikoa mingine iliyosalia, imebakiza idadi ndogo ya madawati ambayo inakaribia kukamilika. Tanzania Bara ina mikoa 26.
Share:

Marufuku matajiri kuwatumia polisi kupiga mabomu wananchi



WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amepiga marufuku watu binafsi wenye uwezo kifedha kutumia Jeshi la Polisi kuwapiga mabomu na kuwanyanyasa wananchi kwa kuwapiga mabomu wanachi wasio na silaha.
Ameagiza nguvu hizo wazitumie kwenye maeneo ambayo yanahatarisha usalama wa nchi na wananchi.
Aidha amewaambia wananchi wa Kata ya Bwawani Kitongoji cha Omapinu kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi atafika kijijini hapo wiki ijayo, kuzungumza nao namna ya kutatua mgogoro wa shamba la Tanzania Plantation na wananchi hao.
Waziri Mkuu Majaliwa aliyasema hayo baada ya kusimamishwa na wananchi wa kitongoji hicho, wakati alipokuwa akiendelea na ziara yake mkoani hapa jana.
“Kuanzia sasa ni marufuku kwa watu binafsi wenye uwezo wa fedha kutumia Jeshi la Polisi kuwapiga mabomu na kuwanyanyasa wananchi kwa kuwapiga mabomu wakati hawana silaha. “Polisi wanaruhusiwa kutumia nguvu hizo kwenye maeneo ambayo yanahatarisha usalama wa nchi na wananchi na si vinginevyo,” alisema Waziri Mkuu.
Kuhusu mgogoro wa shamba la Tanzania Plantation, Waziri Mkuu alihoji; “Ni kwanini polisi wawapige mabomu wananchi wanaozuiwa kulima au kuchota maji katika eneo hilo la shamba hadi kufikia hatua ya wanawake kuharibu mimba? “Nyie polisi kwanini mnawapiga mabomu hawa watu, nani anatoa amri ya kupigwa mabomu wananchi hawa. Nasema kuanzia leo msiwapige mabomu watu hawa na pia nawasihi nyie wananchi msifanye fujo, subirini Waziri Lukuvi anakuja wiki ijayo kwa ajili ya kutatua mgogoro huu wa shamba.”
Alisema polisi wanaruhusiwa kutumia nguvu, pale tu panapotokea jambo linaloweza kuhatarisha maisha au vurugu, ila si kuwanyanyasa wananchi wanaodai ardhi yao kwa kuwapiga mabomu.
Alisema Lukuvi atafika mkoani humo kwa ajili ya kushughulikia migogoro ya ardhi, ambayo ipo zaidi wilayani Arumeru, na atakaa muda mwingi kwa ajili ya kutatua kero za wananchi.
Alisema kuanzia sasa mwekezaji ambaye ana mashamba wilayani humo na hayaendelezi, mashamba hayo yatachukuliwa na serikali ili kugawanywa kwa wananchi.
Alisema Waziri Lukuvi akiwa wilayani humo pamoja na kushughulikia migogoro mingine, pia atatatua mgogoro huo baina ya shamba la Tanzania Plantation na wanachi hao.
Awali, Ofisa Ardhi Wilaya ya Arumeru, Rehema Jato alikiri kuwepo kwa mgogoro wa ardhi kati ya mwekezaji wa wa Shamba la Tanzana Plantation, Pradeep Lodhia na wananchi.
Alisema kuna kesi mahakamani na wanachosubiri sasa ni uamuzi wa Mahakama ndipo hatua zingine zichukuliwe. Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti alisema wilaya hiyo ni moja ya wilaya nchini zenye migogoro mingi ya ardhi na wakati mwingine watu wanauana.
Share:

CCM washinda Meya, Naibu Meya Kigamboni

UCHAGUZI wa kumpata Meya wa Manispaa ya Kigamboni jijini Dar es Salaam, umefanyika na hatimaye Diwani wa Kata ya Pemba Mnazi kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM), Maabadi Hoja amechaguliwa kuwa Meya wa kwanza.
Uchaguzi huo ulifanyika jana kwenye ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigamboni, Rahel Mhando, ambaye alikuwa msimamizi wa uchaguzi, alisema mgombea huyo wa CCM ndiye aliyeshinda.
Washiriki wengine walitoka vyama vya CCM, Chama cha Wananchi (CUF) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Mhando alisema Hoja alipata kura tisa dhidi ya Celestine Maufi (CUF) aliyepata kura tano na kura moja iliharibika.
Pia, Mhando alisema katika uchaguzi huo, Amini Sambo ambaye ni Diwani wa Kata ya Kibada, pia kutoka CCM, alishinda nafasi ya Naibu Meya, akipata kura 10 dhidi ya Ernest Mafimbo wa CUF, aliyepata kura tano. “Tunashukuru uchaguzi umefanyika vizuri Kigamboni, sasa tumepata Meya na Naibu Meya,” alisema Mhando.
Uchaguzi wa Meya na Naibu wake kwa upande wa Kigamboni, umefanywa baada ya Wilaya ya Temeke kugawanywa na kuwa wilaya mbili za Temeke na Kigamboni.
Mhando alieleza kuwa uchaguzi huo ambao ni wa mara ya kwanza kwa halmashauri hiyo, ulifanyika kwa amani bila kuwapo na malalamiko.
Mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndungulile, baada ya kumalizika kwa uchaguzi huo, alisema uchaguzi ulifanyika bila tatizo lolote na kwamba baada ya uchaguzi kuisha, kinachofuata ni kazi.
Alisema kwa muda mrefu mambo mengi katika halmashauri hiyo, yalisimama kwa kukosa Baraza la Madiwani. Akizungumza na gazeti hili, meya huyo, Hoja alisema anajipanga kuiweka Halmashauri hiyo mpya kimji. Aliahidi kuanza na kusimamia mipangomiji na miundombinu.
“Manispaa yetu ni mpya na haijapangwa, tunataka kuiweka kimji zaidi na tutaanza na mipangomiji kwani kuna ujenzi holela na pia tutasimamia miundombinu,” alisema Hoja.
Hii si mara ya kwanza kuchaguliwa kushika nafasi hiyo. Alichaguliwa kuwa Meya wa Manispaa ya Temeke mwaka 2010 baada ya kushinda udiwani wa kata hiyo kwa mara ya kwanza.
Baada ya kufanyika uchaguzi mkuu mwaka jana, Hoja alipata tena udiwani katika kata hiyo, lakini aliposhindania nafasi ya meya, hakushinda nafasi hiyo. Lakini, baada ya Temeke kugawanywa kuwa wilaya mbili za Temeke na Kigamboni, Hoja amegombea tena na kushinda.
Kwa upande wake, akihojiwa, Naibu Meya mpya, Sambo, anasema hii ni mara ya kwanza kushika nafasi ya udiwani. Alichaguliwa mwaka jana.
Sambo alisema anaishukuru Serikali kwa kusogeza huduma karibu, kwa kuifanya Kigamboni kujitegemea kama halmashauri.
Alisema yeye na viongozi wenzake watashirikiana na serikali, kuifanya halmashauri hiyo mpya kuwa ya mfano. Halmashauri ya Kigamboni inaundwa na kata tisa za Pembamnazi, Kimbiji, Somangila, Kisarawe, Kibada, Vijibweni, Kigamboni, Mjimwema na Tungi.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI DEC TAREHE 18.12.2016

Share:

Saturday, 17 December 2016

Tangaza Biashara Yako Au Bidhaa Yako Kwenye Mtandao huu Kwa BEI NZURI Kabisa


Tunakaribisha  matangazo  ya  aina  zote.Bei  zetu  ni  nzuri  sana  na  kamwe  hutajuta  kutangaza  biashara  yako  kupitia  mtandao  huu.
Kwa Siku tunafunga na Pageviews zaidi  ya  laki tatu kama graph  inavyoonyesha  hapo  chini
Share:

Dr Mwele Malechela(Aliyetumbuliwa) : Safari itasonga kwa msaada wa Mungu

Share:

Mahakama yatupa pingamizi la serikali katika kesi ya mbunge Godbless Lema.

Share:

Baada ya Dkt. Mwele Malecela kutumbuliwa, Prof. Yunus Mgaya ateuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu NIMR

Share:

Waziri Simbachawene atoa agizo jipya kwa machinga

Share:

Waziri Mkuu Amsimamisha Kazi Mwekahazina Wa Wilaya Ya Bahi,Aagiza arudishwe Longido kujibu tuhuma zinazomkabili

Share:

Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR)


Taarifa kutoka IKULU inasema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, tarehe 16 Desemba, 2016 ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Dkt. Mwele Malecela.
Share:

Waziri Mkuu: Waliouza Kiwanja Cha Shule Wachukuliwe Hatua

Share:

Taarifa ya Bodi ya Mikopo kwa wadaiwa sugu kuhusu mwisho wa kulipa kwa hiari

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu imeongeza muda kwa wadaiwa sugu kulipa madeni yao hadi Desemba 30, 2016.
Share:

Wafanyabiashara Morogoro watelekeza masoko yao na kuhamia katikati ya mji.





Siku chache baada ya Rais Dokta John Pombe Magufuli kuwataka wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya zote nchini kuacha kuwabughudhi wamachinga na badala yake wawatafutie maeneo maalumu ya kufanyia biashara zao hali imekuwa tofauti kwa Manispaa ya Morogoro baada ya wafanyabiashara mbalimbali kuyatelekeza masoko na kupeleka bidhaa zao katikati ya mji huku wafanyabiashara wa madu
Share:

Sungusungu wavamia kijiji na kutembeza viboko.


Kwa hali isiyo ya kawaida sungusungu zaidi ya mia nane wamevamia kijiji cha Welezo katika kata ya Tinde wilayani Shinyanga na kutembeza kichapo kwa wakazi wa kijiji hicho hali ambayo imezua taharuki na kusababisha kamati ya ulinzi na usalama ikiongozwa na mkuu wa wilaya hiyo kuingilia kati na kumsimamisha kazi mwenyekiti wa kijiji hicho kwa kosa la kufanya uzembe uliosababisha vurugu.
Share:

Magazeti Ya Leo Jumamosi ya Disemba 17 2016

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger