Friday, 16 December 2016

Kafulila ahama NCCR, ahamia Chadema


Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kigoma Kusini kwa tiketi ya Chama cha NCCR-Mageuzi, David Kafulila leo ametangaza kukihama chama hicho na kusema kuwa atajiunga na Chama cha Demokrasia na Manendeleo (CHADEMA).
Share:

Ndalichako Asitisha Ajira za Walimu Wa Masomo ya Sanaa

WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, ametoa masharti mapya ya ajira za ualimu nchini, huku akisema Serikali haitaajiri walimu wa masomo ya sanaa (arts) kwa kuwa wapo wa kutosha.

Akizungumza mjini Dodoma jana wakati akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA), Profesa Ndalichako, alisema Serikali kwa sasa haiwezi kuajiri walimu wa masomo hayo kwa kuwa inataka kuajiri walimu wa masomo ya sayansi na hisabati ambao idadi yao ni ndogo.

“Pamoja na uamuzi huo mpya, ajira za walimu wapya wa masomo ya sayansi nazo zimebadilika kwani wale wote waliohitimu ualimu wa sayansi na hisabati, wanatakiwa watume vyeti vyao kabla ya kupangiwa kituo cha kazi.

“Kuhusu wale walimu wa ‘arts’, kule tuna walimu wa ziada ambao tutajaribu kuwapanga kutokana na shule, kwani wengi walikuwa wamepangwa shule moja. Kwahiyo, tutaangalia utaratibu wa kuwapanga kulingana na mahitaji,’’ alisema Profesa Ndalichako.

Akizungumzia suala la ubora wa elimu nchini, Profesa Ndalichako aliwataka walimu wakuu hao kuhakikisha wanasimamia ubora wa elimu kwa kuwa wao ndio wanaowaandaa wanafunzi kabla hawajaenda vyuoni.

“Vilevile pelekeni takwimu sahihi za wanafunzi waliopo katika shule zenu kuisaidia Serikali katika kupanga bajeti ili iweze kutoa fedha sahihi.

“Hapa kuna kimbembe, yaani wakati mwingine huwa najifanya nimepoteza takwimu ya shule fulani, nikiziomba na kutumiwa, zinakuwa ni tofauti na zile za mwanzo.

“Hili nawaomba mkalisimamie ili iwe rahisi kwetu kupanga bajeti yenye tija,’’ alisema.

Kuhusu ujenzi wa maabara katika shule za sekondari, waziri huyo alisema kwamba kutokana na nyingi kukamilika, Serikali itatoa vifaa vya maabara kuanzia Januari mwakani baada ya kuwa vimeingia nchini kutoka vilikoagizwa.

Awali, akisoma risala ya walimu hao, Rais wa TAHOSSA, Bonus Nyimbo, aliiomba Serikali itoe waraka wa kupiga marufuku matumizi ya simu kwa wanafunzi shuleni kwa kuwa zimekuwa zikichangia kushuka kwa ufaulu kwa baadhi ya wanafunzi.

“Ili kuboresha elimu, tunaiomba Serikali itoe waraka wa kupiga marufuku matumizi ya simu kwa wanafunzi kwani simu nyingi tunazozikamata tunakuta mule hakuna taaluma,’’ alisema Nyimbo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Global Education Link, Abdulmalik Molel, ambaye pia kampuni yake ilipewa tuzo ya heshima katika kuendeleza elimu nchini, alisema ni jukumu la kila mmoja kutimiza wajibu wake ili kuiendeleza elimu ya Tanzania.

“Kila mmoja anapaswa kutimiza wajibu, wazazi, walezi na walimu, waambieni wanafunzi wasiwe na ‘expectation’ (matarajio) makubwa kwani wanapokuwa na matarajio hayo, wakienda vyuo vikuu wanakuwa wasumbufu,” alisema.

Wakati hayo yakiendelea, juzi taarifa ilitolewa jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Maimuna Tarishi, ikisema kwamba, walimu wahitimu wa masomo ya sayansi na hisabati waliohitimu shahada na astashahada mwaka 2015, wanatakiwa kuwasilisha nakala za vyeti vya elimu ya sekondari vya kidato cha nne na sita na taaluma ya ualimu kwa uhakiki.

Pamoja na hayo, hivi karibuni Serikali ilitangaza kusitisha ajira zote nchini ili kukabiliana na wimbi la watumishi hewa.

Sambamba na uamuzi huo, nyongeza za mishahara kwa watumishi wa Serikali nazo zilisimamishwa ili kukabiliana na watumishi hao hewa ambao walikuwa wakiingizia hasara Serikali.
Share:

Mwanzilishi wa JamiiForums afikishwa mahakamani,Ashindwa Kutimiza Masharti ya Dhamana

Share:

MAGAZETI YA LEO IJUMAA DEC 16 2016

Share:

Humphrey Polepole aeleza mikakati yake baada ya kukabidhiwa ofisi na Nape Nnauye

Share:

Nape awaaomba msamaha wapinzani.

Alikuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amewaomba radhi viongozi na wafuasi wa vyama vya upinzani nchini kwa lolote ambalo aliwakwaza wakati akitekeleza majukumu yake katika nafasi hiyo.

Nape amewaangukia wapinzani pamoja na makundi mengine ya watanzania ikiwemo viongozi wenzake ndani ya chama leo wakati akikabidhi rasmi ofisi kwa kiongozi mpya anayechukua nafasi hiyo, ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Dar es Salaam, Humphrey Polepole katika ofisi ndogo za makao makuu ya chama hicho, Lumumba Jijini Dar es Salaam.

"Nawaomba msamaha viongozi wenzangu, wanachama, waandishi na hata wapinzani pale ambapo nimewaumiza katika kufanya kazi yangu, samahani sana. Nategemea ushirikiano niliopatiwa mimi na wanahabari utaendelea kwa ndugu yangu Humphrey Polepole, ni mtu mwenye weledi mpana" amesema Nape

Nape pia amekiri kuwa chama hicho kimemsaidia zaidi kwenye maisha yake kuliko yeye alivyokisaidia wakati akiitumikia nafasi hiyo.

"Nakiri mbele yenu kuwa chama kimenisaidia zaidi kuliko mimi nilivyokisaidia Chama, nashukuru Mungu kuwa nimemaliza kazi hii salama, nilipata wosia wa Mzee Kinana kuwa nishukuru nikimaliza salama"
Share:

Daladala Dodoma zagoma kupinga manyanyaso

Share:

Walimu wapya wa Sayansi, Hisabati wabanwa


WALIMU wa Sayansi watakaoajiriwa na serikali, watalazimika kutuma vyeti vyao kabla ya kupangiwa kituo cha kazi.
Hiyo ni sehemu ya mabadiliko katika utaratibu wa ajira wenye lengo la kuimarisha ufundishaji kwa waliohitimu Ualimu wa Sayansi na Hisabati.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (Tahossa).
Pamoja na kuzungumzia mabadiliko hayo katika mfumo wa ajira, alisema ni nia ya serikali kuimarisha elimu ya sekondari, ikiwa ni pamoja na kuimarisha ufundishaji wa masomo hayo ya Sayansi.
Aidha, Profesa Ndalichako aliwataka Walimu wakuu nchini, kusimamia ubora wa elimu kutokana na wao kuwa karibu na wanafunzi.
Akifafanua, alisema walimu wakuu wanawajibu wa kuwa wasimamizi na wakaguzi wa kwanza wa wanafunzi ili kuiboresha elimu ya Tanzania, wakizingatia kuwa elimu ya Sekondari ni kiungo muhimu katika kuendeleza elimu nchini.
Vile vile, aliwataka wakuu hao kupeleka takwimu sahihi za wanafunzi waliopo katika shule zao ili kuisaidia serikali katika kupanga bajeti ili iweze kutoa fedha sahihi.
“Hapa kuna kimbembe wakati mwingine huwa najifanyisha nimepoteza takwimu ya shule fulani nikitumiwa inakuwa tofauti na ile ya mwanzo, niwaombe walimu mkalisimamie hili ili iwe rahisi kwetu kupanga bajeti yenye tija,’’ alisema.
Prof. Ndalichako alisema kutokana na maabara nyingi kukamilika, serikali itatoa vifaa vya maabara kuanzia Januari mwaka mwakani. Katika mkutano huo, Waziri pia aliwaomba Makatibu Tawala na Wakurugenzi, kuwalinda walimu wanaofuata kanuni, taratibu na sheria katika utendaji kazi wao na kudhibiti wanasiasa kuingilia masuala ya elimu.
Pia aliwataka walimu wakuu kuwa na mahusiano mazuri na jamii inayowazunguka pamoja na kufanya usafi katika shule zao.
Akisoma risala, Rais wa Tahossa, Bonus Nyimbo aliiomba serikali itoe waraka wa kupiga marufuku matumizi ya simu kwa wanafunzi shuleni, kwani imekuwa ikichangia kushusha ufaulu wa baadhi ya wanafunzi.
Nyimbo ambaye ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwenge ya mkoani Singida, aliiomba serikali iajiri pia walinzi, watumishi na madereva ili waweze kufanya kazi kwa ufasaha. Alisema changamoto nyingine, wanayokabiliwa nayo ni baadhi ya wanachama kutoelewa vizuri katiba pamoja na kutokulipa ada kwa wakati.
“Kwa upande wake Mkurugenzi wa Global Education Link, AbdulMalik Molel ambaye kampuni yake ilipewa tuzo ya heshima katika kuendeleza elimu nchini”, alisema ni jukumu la kila mmoja kutimiza wajibu wake ili kuiendeleza elimu ya Tanzania.
Share:

MAJALIWA CAHARUKA



WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ametoa miezi sita ya kujitathimini mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) yanayofanya kazi zake wilayani Ngorongoro mkoani Arusha, kama yanafanya kazi kwa misingi ya sheria na maadili.
Baadaye, yatahakikiwa na kama yatabainika yanachochea migogoro, yatafutwa.
Pia, Majaliwa amezicharukia NGOs nyingine zinazoitangaza vibaya Tanzania kimataifa kwa kupiga picha za kudhalilisha watoto wakiwa wanatembea kwenye mawe huku wamevaa kandambili kubwa, kuonesha nchi ni masikini. Ametaka NGOs hizo kuondoka nchini, la sivyo serikali itazishughulikia.
“Hizi NGOs zingine si muondoke, nendeni kwingine mkafanye kazi. Halafu nyie mnaotuma picha za kudhalilisha watoto wakiwa wamevaa kandambili kubwa, kudai nchi za nje eti Tanzania ni masikini, tutawashughulikia,” alisema Majaliwa alipozungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro jana.
Aidha alisema Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) atakuja wilayani hapo kukagua kazi walizozifanya, wanazozifanya na miradi wanaosaidia jamii.
Majaliwa aliwaambia watumishi hao wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro pamoja na wadau mbalimbali wakiwemo wakurugenzi wa mashirika yasiyo ya serikali, yanayofanya shughuli zake wilayani hapo, kuwa serikali haitaki mashirika chochezi wa migogoro na itayafuta.
Alisema serikali haitasita kuyafuta mashirika yanayofanya kazi wilayani humo, ambayo yapo kwa nia ya uchochezi na kuacha kufanya kazi katika malengo yaliyokusudiwa.
Waziri Mkuu alisema wilaya hiyo, ina mashirika yasiyo ya serikali 30 ambayo yamesajiliwa, lakini yanayofanya kazi ni 19 tu.
Alisisitiza kuwa haiwezekani serikali isajili mashirika hayo, lakini utendaji kazi wake uwe hafifu.
Alisema ukifuatilia, mashirika hayo utagundua kuwa yanapokea fedha nyingi, lakini hakuna cha maana wanachokifanya kwa wananchi. Alisema serikali ina taarifa ya NGOs hizo zinazopewa fedha na wafadhili.
“Najua taarifa zenu mnapokea kiasi gani cha fedha na mnazifanyia nini, lakini namleta Mkaguzi wa serikali ili akague mnatumiaje fedha zenu, nawapa miezi sita tu halafu ukaguzi utaanza, maana kuna mashirika mengi lakini kazi mnazofanya hazionekani,” alisema Majaliwa.
Alisema baadhi ya mashirika, yana akaunti nchi jirani ya Kenya na mengine kama PWC anapewa Sh bilioni 2.5 kwa mwaka na shirika la UCRT linapokea Sh bilioni 1.5 kwa mwaka, lakini hajui yanafanya nini.
“Nina taarifa zenu mnapata hela nyingi, lakini mnahudumia vipi jamii hakuna, sasa ngojeni ukaguzi ufanyike halafu nitachukua maamuzi maana kila siku Loliondo kuna nini hapa mnasajiliwa halafu hakuna cha maana,” alisema.
“Kuna nini Loliondo, kwani kila mara Loliondo nina taarifa za kila NGOs zinazofanya kazi hapa, najua mnachokifanya, sasa nawaambia serikali haitawafumbia macho kuona hiki ninachokifanya hapa na ikigundulika mnafanya kinyume na matakwa ya usajili tutazifuta”.
Alisema serikali itazifuta NGOs zote, ambazo zitabainika ni kiini cha migogoro Loliondo. Alitoa hadhari kwa kampuni zinazofanya kazi zake bila usajili, kuwa zikigundulika, zitachukuliwa hatua.
Aliwageukia watumishi wa umma na kuwatahadharisha wale wanaotoa taarifa za migogoro ya ndani kwa wahusika wa NGOs na kisha kuzituma nje ya nchi kwenye mitandao ya kijamii na barua pepe.
Alisema kuwa nao watashugulikiwa, kwa kuwa wanapaswa kuwa majibu ya migogoro na si wasambazaji wa habari mbaya za nchi.
Alisisitiza watekeleze kikamilifu kauli ya ‘Hapa Kazi Tu’ ; na si kutumia NGOs kwa ajili ya kudai kuwasaidia wananchi, huku wakijua kuwa wananchi hawanufaiki na fedha hizo wanazopewa na wafadhili Awali akizungumza na watumishi wa halmashauri ya Wilaya hiyo, Majaliwa alitoa tahadhari kwa madiwani kuacha kushirikiana na watu wa Uhasibu wanaotoa hela kwaajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo.
Alisema baadhi ya madiwani, wanakwamisha miradi ya maendeleo kwa kula fedha kwa sababu ya ukaribu walionao.
Akizungumzia nidhamu ya fedha, Majaliwa alisisitiza kila mtumishi lazima afanye kazi kwa bidii, ikiwemo kutoa huduma bila kuwabagua wananchi kwa itikadi zao za vyama.
Share:

MWANAFUNZI ALIYEFUKUZWA CHUO CHA UDOM KWA KUONGOZA MGOMO ARUDISHWA CHUO AMALIZIE MASOMO



MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dodoma imetengua uamuzi wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) ya kumfukuza mwanachuo Phillip Mwakibinga na kuamuru arudishwe ili kumalizia masomo yake.
Uamuzi huo ulitolewa jana na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, John Chaba kwa niaba ya Jaji Awadhi Mohamed aliyekuwa akisikiliza shauri hilo.
Mwakibinga alikuwa akisoma Shahada ya Kiswahili mwaka wa tatu wakati akisimamishwa na alikuwa Waziri Mkuu wa Kitivo cha Sayansi ya Jamii. Katika uamuzi huo, mahakama ilisema mlalamikaji hakupewa nafasi ya kusikilizwa na hivyo kukiuka haki ya asili ya mlalamikaji. Pia mlalamikaji hakupewa haki ya kusikilizwa na hakuandikiwa mashtaka rasmi.
“Baraza liliegemea upande moja bila kumhoji wala nafasi ya kusikilizwa na kujitetea,” alisema. 
Mwakibinga alifukuzwa Udom Januari 14, mwaka jana, kwa madai ya kuongoza mgomo ambapo siku hiyo baraza la chuo lilikaa na kumfukuza bila kupewa nafasi ya kusikilizwa.
Alifungua kesi Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma kutaka mahakama kutengua uamuzi huo. Kwa mujibu wa wakili wa Mwakibinga, Elias Machibya alisema awali waliomba ruhusa ya kufungua kesi na wakapewa Februari 5, mwaka jana wakiomba kutengua maombi ya baraza la Chuo Kikuu cha Dodoma.
“Tulipata kibali cha kufungua kuomba kutengua maamuzi ya Chuo Kikuu cha Dodoma kwa kumfukuza,” alisema.
Alizitaja sababu kuu tatu za kupinga mwanafunzi huyo kufukuzwa chuo kuwa ni pamoja na kutopewa nafasi ya kusikilizwa, hakuna hatua za nidhamu zilizochukuliwa, walimfukuza wakidai aliwahi kuhusika na migomo ya nyuma.
Alidai barua ya kumfukuza ilisainiwa na Profesa Shaban Mlacha.
Januari 14, mwaka jana uongozi wa Udom ulimfukuza Mwakibinga ambaye wakati huo alikuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya wanafunzi, Kitivo cha Sayansi ya Elimu ya Jamii, na kupewa barua ya kusimamishwa kutokana na kosa la kuhamasisha mgomo.
Uongozi huo ulisema Mwakibinga amefukuzwa kabisa kwa kuwa alishawahi kujihusisha na mgomo wa mwaka 2010/2011 akafukuzwa lakini akakata rufaa na kuomba msamaha kwenye Kamati nidhamu.
“Baada ya kukata rufaa Kamati ikamuonea huruma ikamrudisha kabla ya kurudi alitakiwa aje na kiapo kutoka kwa mwanasheria kwamba hatajihusisha na mgomo tena lakini akarudia tena kosa hilo."

Mwakibinga amesema amefurahia uamuzi huo kwani ndio sababu ya msingi ya kufungua kesi na mahakama imetenda haki. Alisema anasubiri barua ya hukumu ambayo itatoka kesho ndipo taratibu zake za kurudi chuo zitakapoanza.
Share:

Thursday, 15 December 2016

HAYA HAPA MAJINA KIDATO CHA SITA WALIOCHAGULIWA JKT AWAMU YA PILI 2016

 BOFYA JINA LA KIKOSI HAPO CHINI  KUANGALIA MAJINA JA VIJANA WA MUJIBU WA SHERIA AWAMU YA PILI  2016  

BULOMBORA JKT-KIGOMA                           RWAMKOMA JKT -MARA                  MSANGE JKT-TABORA

KANEMBWA JKT-KIGOMA                                         MTABILA-KIGOMA                      RUVU JKT-PWANI

MAKUTUPORA JKT- DODOMA                           MGAMBO JKT-TANGA              MARAMBA JKT- TANGA

MAFINGA JKT- IRINGA                                                                                MLALE JKT -RUVUMA


Share:

New AUDIO | Mwasiti - Kaa Nao | Download

Share:

New AUDIO | Mwasiti - Kaa Nao | Download

Share:

New AUDIO | P Square Ft Akon - Bedroom | Download


Share:

New AUDIO | QChief - Sungura | Download


Share:

Official VIDEO | Mr Nay - Sijiwezi | Watch/Download


Share:

New AUDIO[Official] | Diamond Platnumz Ft. Neyo - Marry You | Download

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger