Wednesday, 19 October 2016

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU IRINGA THIRD BATCH 2016/2017

 Image result for UNIVERSIT OF IRINGA.AC.TZ
THIRD SELECTION FOR DEGREE PROGRAMMES 2016 - 2017
Congratulations! The following students have been admitted to join various first degree programmes for 2016-2017 Academic year for the third selection batch
Bachelor of Arts in Journalism
S/N LASTNAME FIRSTNAME MIDDLE SEX
1 MOHAMMED AHMED ABDI M
2 WAZIRI MWANAIDI T F
Bachelor of Laws
1 OMARY HABIBA SAID F
2 MAKWAIA CLARA A F
3 YUSUPH JANE M F
Bachelor of Education (Mathematics)
1 KALINGA MICHAEL JANUALY M
2 DEUS ELIZABETH DAUD F
Bachelor of Arts in Community Development
1 URIO CHRISTABELLA E F
2 NGANYILA MATANGA M M
3 STANSLAUS SUNDAY SYLVANUS M
4 MAKWABE ROBIN J M
5 DANIEL PIUS   M
6 NOVATH AIDAN   M
7 MTEI CATHERINE ALBERT F
Bachelor of Accounting  and Finance 
1 BENJAMIN WAKILI MUGAMBI M
2 ATHUMANI JUMA MIRAJI M
Bachelor of Education (Arts)
1 KAMONONGO ELIPHAS WILLIAM M
2 SAMWELI STELA M F
3 JILALA JUMA   M
4 SAID JAFARI   M
5 REDSON LUCY   F
6 JOHN LIMBU   M
Bachelor of Human Resource Management
1 AUGUSTINO AUGUSTINO FESTUS M
Bachelor of Business in Procurement and Supply Chain Management
1 BUNYANYA EMILIANA JOHN F
2 ISACK DANIEL   M
Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU AJUCO SONGEA 2016/2017 THIRD BATCH

Image result for AJUCO.AC.TZ  

KUONA MAJINA 

Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA HOSTEL CHUO KIKUU IFM 2016/2017

KUONA MAJINA 
Share:

Zitto Atoa Neno Ugomvi wa RC Arusha na Godbless Lema

lema
Kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameamua kutoa ya moyoni kufuatia hali iliyojitokeza jana mkoani Arusha wakati wa uzinduzi wa Hospitali ya Mama na Mtoto. Katika uzinduzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo alisema kuwa eneo la hospitali hiyo lilitolewa na familia ya Nyaga Mawalla,
Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA CHUO HURBERT KAIRUKI 1ST,2ND AND 3RD BATCHES 2016/2017

KUONA MAJINA HAYO 

Share:

MH.ANTONY MTAKA ATEKELEZA AHADI YA MH.MAGUFULI YA VIWANDA KWA VITENDO MKOANI SIMIYU




File Photo
Baada ya Mkoa wa Simiyu kukamilisha uanzishwaji wa viwanda vidogovidogo kwenye wilaya za Meatu na Maswa, hivi sasa umeanza kazi hiyo  kwa Itilima, Bariadi na Busega ili kwenda sambamba na uamuzi wa Rais John Magufuli.
Share:

Mikopo bilioni 80/- elimu ya juu yapelekwa vyuoni kwa ajili ya first years 2016/2017

[​IMG]
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Mafunzo ya Ufund, Stella Manyanya.​

SERIKALI imetoa Sh bilioni 80 kwa ajili ya malipo ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu wanaoanza na wanaoendelea na masomo na wameanza kulipwa jana.

Aidha, imewataka wakuu wa vyuo ambao hawajawasilisha matokeo ya wanafunzi wao wanaoendelea na masomo kufanya hivyo haraka ili wakamilishe uchakataji wa mgawo wa mikopo. Katika mwaka huu wa fedha, serikali imetenga Sh bilioni 427 kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Stella Manyanya alisema hayo Dar es Salaam jana wakati akielezea mchakato wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu na kueleza kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya wanaoanza na wanaoendelea katika robo mwaka.

Manyanya alisema serikali imetoa fedha zinazotakiwa kukamilisha mchakato wa malipo unaofanyika kuanzia jana baada ya kumalizika kwa uchambuzi kulingana na vigezo.
Alisema kwa mujibu wa ulipaji mikopo, inazingatiwa vigezo vya kisheria vya kutoa mikopo kulingana na uhitaji kwa kuangalia anayepewa, kweli ana uhitaji na siyo kwa kila mtu kwani lengo la serikali kusaidia na siyo kuondoa majukumu ya mzazi.

Alisema pia wanaangalia bajeti iliyopo kwa wakati huo, kwani kwa mujibu wa Sera ya Elimu ya Mwaka 2014 na matamko ya Rais John Magufuli amedhamiria kuendelea kutoa mikopo kwa wahitaji wote pamoja na kuboresha elimu kwa namna mbalimbali.
Alitaja baadhi ya miradi iliyotekelezwa sambamba na kutoa mikopo ni ukamilishaji wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Mloganzila kwa Sh bilioni 100 pamoja na kukamilisha ukarabati wa vyuo vya ualimu ambapo tayari vyuo 10 vimekamilika.

Alisema pia baada ya Rais kutembelea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na kuona adha ya wanafunzi kukabiliwa na kukaa mbali na chuo, Sh bilioni 10 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa mabweni 20 katika ghorofa tatu zitakazochukua wanafunzi 3,800.

Manyanya alisema pia serikali imelipia ada moja kwa moja vyuoni kwa wanufaika wa mikopo ya Sh bilioni 40 katika vyuo vya serikali na binafsi nchini.

Aliwataka wanafunzi wanaolalamika kutopata mikopo kukamilisha kupeleka viambatanisho vyote stahili huku wakihakikisha wanakuwa na vigezo vya ufaulu kwani sasa ufaulu umepanda wengi wamepata daraja la kwanza na pili, hivyo kuchukua hao kwanza na wale wa daraja la tatu wachache.

Naibu Waziri alisema kwa yatima wapo wasiopewa mikopo baada ya uchambuzi kubaini kuwa na uwezo wa kujilipia kutoka kwa ndugu au mali zilizoachwa na wazazi hivyo kuna utofauti wa yatima, kwani wapo wahitaji na wasio wahitaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Abdul Razaq Badru alisema bodi hiyo hutoa mikopo kwa kuzingatia kozi za vipaumbele kama udaktari au uhandisi kwa ajili ya ujenzi wa wataalamu katika Tanzania ya viwanda.

Alisema pia mikopo hutolewa kwa ulinganifu wa uhitaji kwa asilimia huku wakifanya uchambuzi wa kina ili kuwafikia wahitaji wengi na wanufaika kuongezeka kama anavyotaka rais.

Katika hatua nyingine, Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu (Tahliso) imesema kuwa muongozo mpya wa utoaji mikopo uliotolewa kwa mwaka huu wa masomo 2016/17 utawahusu wadahiliwa wapya tu wanaoanza masomo.

Taarifa iliyotolewa jana na Tahliso kwenda kwa wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu, ilieleza kuwa wanafunzi wanaonufaika na mikopo ambao wanaendelea na masomo, wao wataendelea na utaratibu kama ulivyokuwa tangu awali walivyoingia makubaliano na utaratibu mpya hautawaathiri.

Mwenyekiti wa Tahliso, Stanslaus Kadugalize ambaye amesaini taarifa hiyo, alifafanua kuwa msimamo huo umetolewa baada ya jumuiya hiyo kuingilia kati baada ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi kutoa mwongozo wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.

Kadugalize alisema baada ya kutolewa kwa mwongozo huo walienda kufanya majadiliano na Waziri, Profesa Joyce Ndalichako ili kumwomba wabadili msimamo wa mwongozo huo kwa kuwa utawaathiri wanafunzi wengi ambao ni watoto wa maskini.

Hivi karibuni Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia walitangaza vigezo vya utoaji mikopo kuwa kuanzia mwaka huu wa masomo, wanufaika wote wa mikopo wapya na wanaoendelea na masomo watakopeshwa kulingana na uwezo wao (means tested) katika vipengele vyote vya mikopo.

Tahliso ilieleza kuwa kutokana na maelezo hayo ni dhahiri mikopo kwa wanafunzi wanaoendelea hasa kwa wale wenye wazazi bila kujali ana uwezo ama hana uwezo, mikopo yao ingepungua kutoka kwenye asilimia walizopangiwa awali.

Taarifa hiyo ilisisitiza kuwa muongozo huo ungepelekea fedha inayotolewa kwa ajili ya chakula na malazi kupungua, jambo ambalo lingesababisha wanafunzi wengi kushindwa kuendelea na masomo, kutokana na uwezo wa wafamilia wanazotoka hasa watoto wa maskini ambao hutegemea fedha hizo hizo za boom kulipia sehemu ya ada iliyobakia na huku wakiendelea kuishi maisha ya shida vyuoni.

Katika vigezo hivyo, Serikali ilisema itatoa kipaumbele kwanza kwa wanafunzi wanaoenda kusomea fani za Sayansi za Tiba na Afya, Ualimu wa Sayansi na Hisabati, Uhandisi wa Viwanda, Kilimo, Mifugo, Mafuta na Gesi Asilia, Sayansi Asilia na Mabadiliko ya Tabianchi na wale watakaosomea Sayansi za Ardhi, Usanifu Majengo na Miundombinu.

Kwenye vigezo hivyo pia serikali ilisisitiza kuwa kipaumbele kingine kitakuwa ni kwa waombaji hususani wenye mahitaji maalumu kama vile ulemavu na yatima.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATANO OCTOBER 19 2016

Share:

Rais Magufuli Atuma Salamu za Rambirambi Kufuatia vifo vya Watu 11 Ajali ya basi la Barcelona


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bw. Godfrey Zambi kufuatia vifo vya watu 11 vilivyosababishwa na ajali ya basi la kampuni ya Barcelona iliyotokea jana tarehe 17 Oktoba, 2016 katika eneo la Miteja Wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi.
Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI MWAKA WA KWANZA WALIOPANGIWA VYUMBA CHUO KIKUU MUHIMBILI 2016/2017

  MUHIMBILI UNIVERSITY OF HEALTH AND ALLIED SCIENCES

Rooms Allocations at MUHAS Hostels

Kindly informed that rooms have been allocated to both Undergraduate and Postgraduate Students  for Academic Year 2016/2017. For more details, download the Rooms Allocation and Important Notice Regarding Room Allocation.
Share:

Mwanafunzi apigwa Dar, ‘afa, afufuka’ mochwari



File Photo

Dar es Salaam. Mwanafunzi wa shule ya Sekondari Lumo wilayani Temeke, Isack Ernest alionja mauti baada ya kupigwa na wananchi kiasi cha kufikiriwa kwamba amekufa, akapelekwa chumba cha maiti ambako alizinduka.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Gilles Muroto alisema jana kwamba kijana huyo alipigwa hadi kupoteza fahamu na alipofikishwa katika Hospitali ya Rufaa ya Temeke aliwekwa kwenye chumba cha maiti pamoja na kijana mwingine aliyeuawa katika tukio hilo.
“Mwanafunzi huyo hali akiwa amelazwa pamoja na maiti nyingine zinazosubiri kuwekwa katika majokofu, alitikisika kutokana na baridi ya chumba cha maiti, wahudumu wakamwona na kumtoa, wakamvalisha nguo za maiti nyingine, akarudishwa hospitalini kwa ajili ya huduma,” alifafanua Kamanda Muroto.
Share:

Tuesday, 18 October 2016

MPYA:TAARIFA KWA UMMA: KUHUSU UHAKIKI WA VYUO NA WANAFUNZI WANAOENDELEA NA MASOMO YA SHAHADA

 Image result for SERIKALI YA TANZANIA

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inawatangazia Viongozi wa vyuo vyote vinavyotoa shahada nchini vya umma na vya binafsi kuwa kutakuwa na uhakiki wa ubora wa vyuo hivyo.
 
Uhakiki huo utaanza siku ya Jumatano Oktoba 19, 2016, hivyo, vyuo vyote vinatakiwa kutoa ushirikiano kwa timu za wataalamu zitakazofika kwa ajili ya kufanya uhakiki huo. 

Aidha, katika ukaguzi wa sifa za wanafunzi wanaoendelea na masomo vyuo vyote, Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), itatoa majina ya wanafunzi wanaotambuliwa na kwamba walidahiliwa kupitia TCU katika Programu zao za Shahada katika vyuo mbalimbali vinavyotoa shahada nchini siku ya Jumanne Oktoba 18, 2016.

Hivyo, wanafunzi wote wanatakiwa kuangalia majina yao katika Tovuti ya TCU na kwa yeyote ambaye hataona jina lake awasiliane na Uongozi wa TCU haraka iwezekanyo ili kupata maelezo Zaidi. Mwanafunzi ambaye hatazingatia haya ndani ya wiki mbili atapoteza sifa za kuendelea na masomo.

Imetolewa na:
Katibu Mkuu
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
Share:

BREAKING NEWS:RAIS MAGUFULI KAMFUKUZA KAZI MRUGENZI WILAYA YA MKINGA-TANGA

Image result for RAIS MAGUFULI ATENGUA
Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA CHUO KIKUU MZUMBE SECOND ROUND 2016/2017

KUONA MAJINA

Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA CHUO KIKUU NIT 2016/2017-1ST,2ND AND 3RD BATCH

Image result for NIT.AC.TZ
Share:

MPYA:SERIKALI KUTANGAZA ORODHA YA PILI(BATCH 2) YA WANAFUNZI WATAKAOPATA MKOPO 2016/2017

Image may contain: 9 people
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger