Thursday, 8 September 2016

Mahakimu 11 Wafukuzwa Kazi,Wengine 30 Kikaangoni

Watumishi 34 wa mahakama wakiwemo mahakimu 11, wamefukuzwa kazi kutokana na makosa mbalimbali ya kinidhamu.

Aidha, Tume ya Utumishi wa Mahakama inaendelea kujadili hatma ya mahakimu 30, waliokuwa wanatuhumiwa kuhusika na rushwa na kushinda zao mahakamani ili kuangalia kama walifanya makosa ya kinidhamu.

Jaji Mkuu, Mohammed Chande Othman alisema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kupokea taarifa za ukaguzi wa mahakama pamoja na uendeshwaji wa mashauri.

Othman alisema watumishi hao, wamefukuzwa kutokana na uamuzi wa kikao cha Tume ya Mahakama, kilichofanyika Agosti 18, mwaka huu baada ya kushughulikia masuala mbalimbali ya kinidhamu.

“Tumewafukuza mahakimu wakazi wafawidhi, mahakimu wa mahakama za Mwanzo za Rombo, Temeke, Bahi na Chamwino na watumishi wengine 23. Hii ni idadi ndogo ambayo ni sawa na asilimia 0.005 ya wafanyakazi wote lakini kwa mahakama ni doa kubwa,” alisema Jaji Mkuu.

Alisema mahakimu hao wamefukuzwa kwa makosa mbalimbali ya kinidhamu, ikiwemo kutumia muhuri wa mahakama kinyume cha taratibu, kuathiri utendaji wa haki kwa kumsaidia mtu kufungua kesi moja katika mahakama mbili pamoja na kufungua kesi ya mirathi bila kuwa na hati ya kifo.

Aliongeza kuwa kuna makosa ya kisheria ambayo jaji au hakimu akikosea kutumia kifungu cha sheria hawajibishwi, lakini kuna makosa ya kinidhamu ambayo yanaondoa sifa ya kuwa hakimu au jaji.

Kuhusu mahakimu walioshinda kesi za rushwa mahakamani, Jaji Chande alisema mahakama inaweza isiwakute na hatia, lakini Tume itaangalia kama walifanya vitendo vya ukosefu wa nidhamu na kuwawajibisha.

Aidha, alisema mahakimu wengine 32 waliokuwa wanakabiliwa na kesi za jinai na kushinda kesi mahakamani, wanafunguliwa mashitaka ya kinidhamu katika Kamati ya Maadili ya Maofisa wa Mahakama kwa sababu inawezekana hawajapatikana na hatia ya kosa la jinai, lakini kama kuna vitendo vya ukosefu wa maadili watawawajibisha kimaadili.

Mahakama Maalumu ya Ufisadi
Katika hatua nyingine, Mahakama Maalumu ya Ufisadi na Uhujumu Uchumi imeanza rasmi na wiki ijayo Kanuni za Uendeshaji wa mahakama hiyo, zinatarajiwa kuchapishwa. 
Jaji Mkuu Othman alisema mahakama hiyo, imeanza rasmi Julai 18 mwaka huu baada ya Rais John Magufuli kusaini sheria ya uanzishwaji wa mahakama hiyo.

“Wiki ijayo tutachapisha kanuni mbalimbali za uendeshwaji wa mahakama hiyo, ikiwemo jinsi ya kulinda mashahidi pamoja na taratibu za ufunguaji wa kesi,” alisema Othman.

Alisema mahakama hiyo itakuwa na majaji wa kutosha ili kufanya kazi kwa uadilifu na kumaliza kesi kwa wakati, pia haitakuwa ikiahirisha kesi mara kwa mara.

Kuhusu utendaji kazi wa mahakama, Jaji Mkuu alisema mahakama haiwezi kutoa haki kama itakuwa inajificha au kuendeshwa kwa siri, ndiyo maana kwenye maboresho ya mahakama, wameamua kuwapa fursa wananchi kutoa mapendekezo au kero zao kupitia namba za simu pamoja na barua pepe.

Kesi za uchaguzi 
Awali akiwasilisha taarifa za utendaji wa Mahakama Kuu, Mahakama za Hakimu Mkazi, Wilaya na za Mwanzo, Msajili wa Mahakama Kuu, Ilvin Mugeta alisema baada ya uchaguzi, walipokea kesi 247 za uchaguzi, 53 za kupinga matokeo ya ubunge na 194 za udiwani.

Mugeta alisema tayari wameshamaliza kesi 234, zimebaki 13, lakini hadi kufikia Desemba mwaka huu kesi zote zitakuwa zimemalizika.

Aidha, alisema tathmini waliyoifanya inaonesha kesi zilizopo zinawiana na mahakimu, na kama watawezeshwa kwa vifaa vya kutendea kazi hadi Desemba mwaka huu watamaliza kesi zote zilizofunguliwa mwaka huu.

Mahakama ya Rufaa 
Kwa upande wake, Msajili wa Mahakama ya Rufaa, John Kahyoza alisema kiwango cha kumaliza mashauri katika Mahakama ya Rufaa kimeongezeka, pia wana lengo la kuhakikisha nakala za hukumu zinapatikana siku hukumu na ndani ya siku tatu zitapatikana kwenye tovuti ya Mahakama ya Tanzania.

Aidha, aliwaomba wananchi watoe ushirikiano ili rufaa zisikilizwe na kuisha mapema, kwa sababu kuna watu wanashindwa kufika mahakamani bila sababu za msingi au kutoa visingizio jambo linalosababisha rufaa zao kuchelewa.

Umuhimu wa mahakama
Katika hotuba yake kwenye Maadhimisho ya Siku ya Sheria Februari 4, mwaka huu, Rais Magufuli alisema anaitegemea sana Mahakama na aliwaambia majaji na mahakimu nchini kuwa:

“Nawaomba waheshimiwa majaji na waheshimiwa mahakimu, muitangulize Tanzania kwanza. Mkiitanguliza Tanzania kwanza tutaweza kufika mbali na tutaweza kuwasaidia watanzania wengi. 
"Nimeamua nchi iende, na itaenda. Anayefikiri ataikwamisha, atakwama yeye kwa sababu Mungu yuko pamoja na mimi. Na watu ninaowategemea sana ni Mahakama. Mahakama unafunga kila mmoja. Hata Rais nikitaka kufungwa na Mahakama, nafungwa. Mbunge anafungwa, nani anafungwa, nyinyi ndio wenyewe”.
Share:

magazeti ya leo alhamisi september tarehe 8.9.2016

Share:

Wednesday, 7 September 2016

MPYA:SERIKALI IMEANZA KUTANGAZA AJIRA KWA SEKTA ZA UMMA,IMETANGAZA NAFASI MPYA LEO SEP 7 2016

Share:

MPYA:ANGALIA MAJINA ,ADA NA JOINING INSTRUCTIONS ZA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA BUGANDO DIPLOMA,DIGRII NA MASTER 2016/2017

 CUHAS - Bugando

Financial Information    

Diploma in Pharmaceutical Sciences (DPS)    

Diploma in Radiography (DDR)    

Diploma in Medical Laboratory Sciences (DMLS)    

Bachelor of Pharmacy (BPHARM)    

Bachelor of Science in Nursing (BSN)    

Bachelor of Science in Nursing Education (BSNE)    

Bachelor of Medical Laboratory Sciences (BMLS)    

Doctor of Medicine (MD)    

Clinical Postgraduate (M.MED)    

Master in Public Health (MPH)-Morning and Evening Sessions  

Masters of Science in Paediatrics Nursing - (MScPN Programme)  

Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA CHUO CHA CBE-CAMPUS ZOTE 2016/2017

Share:

Kampuni ya Sukari Kilombero yatangaza nafasi za kazi

[​IMG]
Share:

MPYA:TANGAZO LA MUHIMU KWA WANAFUNZI WOTE WA DODOMA UNIVERSITY 2016

 Logo
ALL STUDENTS ARE REQUIRED TO PAY TUITION FEES AND DIRECT COSTS FOR THE ACADEMIC YEAR 2016/2017 BY 28TH OCTOBER 2016.  STUDENTS WHO WILL FAIL TO COMPLY WITH THIS NOTICE WILL NOT BE ALLOWED TO CONTINUE WITH THEIR
Share:

MPYA:TANGAZO LA TENDER WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI LEO SEP 7 2016

 Ministry of Education, Science and Technology

TENDER NO. ME-O24/2016-2017/HQ/C/19 FOR PROVISION OF CONSULTANCY FOR DEVELOPMENT OF EDUCATION SUB-SECTOR QUALITY ASSURANCE FRAMEWORK SYSTEM


 The Government of United Republic of Tanzania received a Grant from the Global Partnership for Education (GPE) Fund towards the cost of Literacy & Numeracy Education Support (LANES) Program that aims to improve the teaching and learning of
basic literacy and numeracy skills. The Ministry of Education,Science and Technology (MoEST) in collaboration with Presindent Office – Regional Administration and Local Government (PO’s – RALG) and the Ministry of Community Development, Gender and Children (MoCDGC) are implementing the three years of this of the said Program.
 Rationale
In order to improve the quality of education at all levels, there is a need to periodically revisit the Basic Education Sub-Sector Quality Assurance System (BESQAS) with the aim of ensuring that education quality aspects are clearly taken into consideration in planning, implementation, monitoring and Evaluation of education provision.
Objective of the assignment
Is to develop a Basic Education Sub-Sector School Quality Assurance Framework (BESQAF) that clearly underpins and defines the Education Sector Quality Assurance System.
 Scope of Assignment
The scope of work includes the following activities:
  1. Background to the Assignment;
  2. Objectives of the exercise and Expected Outputs;
  3. Tasks to be undertaken along with a Detailed Work Plan and Schedule of activities;
  4. Methodology for undertaking the SITAN, key tools/Instruments and outline of the report;
  5. Methodology for development of the Basic Education Sub-Sector School Quality Assurance Framework
  6. The process for Monitoring and approval at different levels of the exercise;
  7. Major documents to be reviewed; and
  8. List of Key Stakeholders expected to provide inputs;
  9. A Situational Analysis (SITAN) report on the current Basic Education Sub-Sector School Quality Assurance Framework (BESQAF ;)
  10. Submission of the Basic Education Sub-Sector School Quality Assurance Framework
The Consultancy will be selected in accordance with procedures set out in Public Procurement Act 2011, Regulations 2013 employment and selection of Consultants Guidelines.
A short list on PASS or FAIL basis will be prepared by assessing the submissions in a competence of the applicant, based on the criteria mentioned in the Document.
Required Education and other qualifications
The Consultant should have:
  1. A minimum of a Master’s Degree in fields/areas that are directly relevant to this assignment;
  2. Direct knowledge and experience on development of Education Quality Assurance Frameworks in East Africa or in any one of the Sub-Saharan Countries;
  3. A minimum work experience of 5 years directly relevant to the assignment;
  4. A track record of quality outputs in implementation of similar tasks;
  5. Experience and/or knowledge of the Tanzania Education Structure;
  6. Proven experience in undertaking similar task for a variety of clients such as Governments, NGOs, Private Sector and Civil Society;
  7. Excellent command of English and
  8. Excellent interpersonal and communication skills and report writing skills.
You may obtain further information at the address below from 0900 – 1500 hours local time (Monday to Friday) exclusive of public holidays: Secretary Ministerial Tender Board, Ministry of Education, Science and Technology, 7Magogoni Street, P.O. Box 9121, 11479 Dar es Salaam, Tanzania Old UTS Building, Room No. 7,
Place, Date and Time of Opening           
The Documents for Expression of Interest submitted to the above address shall be opened publicly in the 1st Floor, Conference Room, Ministry of Education, Science and Technology Headquarters Building located at 7 Magogoni Street, 11479,Dar es Salaam, Tanzania.at 1130 hours local time on Wednesday 21st September, 2016 Submission shall be strictly be one original plus three copies.
Late submitted documents, portion of Tenders, electronic Tenders, Tenders not opened and not read out in public at the date of opening ceremony shall not be accepted for evaluation irrespective of the circumstances.

PERMANENT SECRETARY
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY
Share:

SUA:List of applicants who do not have certificates in their applications 2016/2017

Image result for SUANET.AC
The following applicants for the 2016/2017 academic year are required to submit missing certificates before 13/09/2016. The mode of submission is online but one may submit in Room No. 223 and 224 in the administration building on the 2nd floor.

>>List of applicants who do not have certificates in their applications<<



Share:

MPYA:HII HAPA JOINING INSTRUCTION YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA MUM UNIVERSITY -MOROGORO DIPLOMA 2016/2017

Share:

Joining instruction for diploma and certificate in health Programmes 2016/17

                                                               
Share:

MPYA:HIZI HAPA JOINING INSTRUCTION ZA CHUO CHA AFYA SENGEREMA KWA WANAFUNZI WOTE WALIOCHAGULIWA 2016/2017

Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUSOMEA MISITU CHETI NA DIPLOMA-OLMOTONYI ARUSHA AMBAO WAMEPATA SCHORALSHIP YA KUDHAMINIWA MASOMO YAO 2016/2017

Share:

MPYA:HIZI HAPA JOINING INSTRUCTIONS ZA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA CHUO CHA AFYA NA UALIMU(DIPLOMA&CHETI) SEKOMU BUMBULI 2016/2017

JOINING INSTRUCTIONS:PRIMARY TEACHERS EDUCATION[DIPLOMA||CERTIFICATE] 

 BUMBULI DOCUMENTS--> 1.JOINING INSTRUCTIONS [DIPLOMA & CERTIFICATE  IN CLINICAL MEDICINE] | | [ BASIC TECHN. CERTIFICATE IN COMMUNITY HEALTH]    2. MEDICAL FORM   
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger