Tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa tareh 25 Oktoba 2015, usalama wa raia wa Zanzibar na mali zao umekuwa katika hali tete.
Hali
hii inatokana na kushuhudiwa kushamiri kwa matukio ya kuogopesha
wananchi na kufurutu ada ukiukwaji wa HAKI ZA BINAADAMU miongoni mwa
wananchi kunakofanywa na vyombo vilivyopewa dhamana ya kuhakikisha
ulinzi na usalama wa nchi yetu raia wake na mali zao.
Katika
siku za hivi kadribuni, hususan baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi
ya Zanzibar (ZEC), Jecha Sali Jecha, kutangaza kinyume na katiba ya
nchi, kufuta uchaguzi wa 25 Oktoba 2015 na matokeo yake, Zanzibar
imeshuhudia uingizwaji na uingiaji mkubwa wa askari, vifaa na zana nzito
za kivita katika visiwa vya Unguja na Pemba.
Sambamba
na hayo kumekuwepo kwa askari wengi wa JWTZ wanaorandaranda mitaani
wakiwa na silaha nzito za kivita na operasheni isiyo rasmi ya kuwakamata
na kuwabambikizia kesi wananchi wasio na hatia na hatimaye kuwaweka
katika vituo mbali mbali vya polisi na kuwanyima dhamana hata kwa makosa
ambayo kisheria yanapaswa kudhaminiwa.
Katika
mwezi wa February 2016 huko kengeja wafuasi wa CUF walikamatwa na
polisi na kuwekwa ndani kwa tuhuma ya kuchoma tawi la CCM la eneo hilo.
Polisi walichukuwa hatua hiyo mara tu tukio hilo liliporipotiwa kwao.
Aidha katika mwezi huu wa Machi baadhi ya matawi ya CUF na Baraza za CUF
zilichomwa moto na kuteketea tikitiki.
Taarifa
ya uhalifu huu zlipripotiwa katika vituo vya polisi na RB kuandikwa,
hata hivyo hadi hii leo hakuna yoyote aliyekamatwa kwa tuhuma ya uhalifu
huo. Matukio ya uchomwaji moto na uharibifu wa mali za CUF umetokea
mahala mwingi Unguja na Pemba kama vile Kisauni ambapo ofisi mpya ya CUF
jimbo la Dimani zilizogharimu zaidi ya sh 90m zilichomwa moto tarehe
24/03/2015 na kuteketea. Kwa makusudi kabisa, hata baada ya polisi
kupata taarifa hiyo na kulikagua eneo husika hakuna yeyote aliyetuhumiwa
na kukamatwa.
Mtakumbuka
kwamba tabia hii ya wananchi ambao kwa asilimia kubwa huwa ni CCM au
vyombo vya serikali vilikuwa vikihujumu kwa makusudi mali ya CUF na hata
mali ya serikali kama vile shule, zahanati, visima vya maji nk. Tukio
la Shengajuu la 1996 ambapo watu waliofanya tukio la kcuhoma moto shule,
kutia kinyesi visima walikamatwa wakiwa na petrol, bunduki, mapanga,
madoo ya kinyesi vyote vikiwa usoni ya gari la idara ya usalama wa Taifa
lenye namba za usajili ZNZ 1296).
Baada
ya tukio hilo la kufedhehesha serikali na mapambamo yaliyofuata baina
ya wafuasi wa CUF na wahalifu (usalama wa Taifa), serikali iliwaadhibu
kwa kuwapiga, kuwaibia mali zao, kuwafanyia vitendo vya kinyama na
kuwaweka ndani kwa zaidi ya miezi 9 wananchi wasio na hatia. Hivyo haya
yanayoendelea hivi sasa huko Pemba si mambo mageni hasa katika kipindi
hiki ambapo SMZ imechukia sana kwanini CUF wamegomea kushiriki uchaguzi
batili wa madrudio wa 20/03/2016.
Sisi
CUF tunaamini pasipo na shaka yeyote kwamba matukio ya kuchomwa moto
kwa masikani na matawi ya CCM huko Pemba ama baadhi ya nyumba za watu
binafsi na mali za serikali ni mwendelezo tu wa siasa chafu za chuki
zinazoendelezwa na serikali dhidi ya wananchi wasio na hatia. CUF
imesikitishwa sana na vitendo hivi vya kihuni na visivyoonyesha siasa za
kistaarabu na inalaani vikali na kwa nguvu zote uhalifu huu ambao
unarejesha nyuma ‘spirit’ ya kushindana bila kupigana.
Kwa
upande mwengine, CUF imepokea taarifa kwamba zaidi ya wananchi 30 wengi
wakiwa wafuasi, viongozi na wanachama wa CUF wamekamatwa na polisi na
wameshikiliwa katika vituo mbali mbali vya polisi huko pemba. Utendaji
huu wa Jeshi la polisi umeipelekea Zanzibar kugawika vipande vipande na
kuwa chanzo cha siasa za chuki, uhasama na kusababisha nchi yetu
kushindwa kutekeleza shughuli zake za kimaendeleo.
Kwa
mfano amri ya Mkuu wa Mkoa kaskazini Pemba kupiga marufuku watu
wasitembee baada ya saa mbili za usiku na kwamba atakayevunja amri hiyo
atakamatwa na kushtakiwa kwa kosa la uzembe na uzururaji ni hatua
nyengine ya SMZ ya kuwahalalilisha na kuwaweka wananchi wa mkoa wa
Kaskazini Pemba katika hali ngumu ya maisha. Amri hii inazuwia hata sala
za Isha na Alfajiri jambo ambalo waumini wa Kiislamu hawatakubaliana
nalo.
CUF
inamtaka Mkuu wa Mkoa uliotajwa hapo juu awache ukereketwa na aendeshe
mkoa kwa hekima, busara, na weledi. Kuongoza watu kwa amri za kidikteta
kumepitwa na wakati. Asome alama za nyakati, aache kutoa amri
zinazopingana na hata haki za binaadamu.
Chama
Cha Wananchi CUF kinaamini kuwa kutokea kwa matukio haya ni mwendelezo
wa njama za CCM zinazoratibiwa na kutekelezwa kimkakati kwa malengo
mahususi ya kuamsha hamasa na kupandisha joto la jazba miongoni mwa
wananchi ili kuhalalisha mpango maalum na kutoa fursa kwa vyombo vya
ulinzi na usalama kutumika kutisha, kukamata, kupiga na kufungulia
mashtaka wananchi wasio na hatia.
Kutokana
na unyeti wake matukio ya uvunjifu wa amani na hatua za ukiukwaji wa
HAKI ZA BINAADAMU, hayapaswi kupuuzwa kwani yanaweza kupelekea
kufanikiwa kwa dhamira mbaya waliyonayo baadhi ya watu katika nchi yetu
wasioitakia mema Zanzibar na kwa hivyo kuathiri umoja wa kimataifa
uliopo uliopatikana kwa gharama kubwa ya jasho la viongozi wazalendo,
Mheshimiwa Rais mstaafu wa Zanzibar Dr. Amani Karume na Katibu Mkuu wa
CUF Maalim Seif Sharif Hamad na uhai wa wananchi wanyonge. Kwa hivyo
sisi katika CUF:
•
Tunavinasihi vyombo vya ulinzi na usalama wa nchi yetu kukataa katakata
kuingia katika mtego wa mipango miovu ya wanasiasa waliofilisika wenye
lengo la kuleta taharuki miongoni mwa wananchi na kuamsha hamasa na
kupandisha jazba na ghamidha zitakazopelekea kuchafuka kwa hali ya amani
ya nchi yetu. CUF inatoa wito kwa kwa vyombo vyote vya Ulinzi na
Usalama hapa nchini kusimamia amani na utulivu pasi na kuegemea upande
wowote wa kisiasa.
Ni
muhimu vyombo hivyo vikajipambanua na kujijengea heshima na kulinda
imani ya wananchi waliyonayo kwao. Kinyume na haya, vyombo vyetu vya
ulinzi na usalama hasa jeshi la polisi na jeshi la wananchi wa Tanzania
JWTZ, ambalo katika siku za hivi karibuni limeonekana kutumika vibaya,
kufahamu kuwa mustakbali wa utu wa raia, mali zao na amani ya nchi yetu
imo mikononi mwao na watakuwa wa mwanzo kuwajibika endapo jahazi la
amani yetu litakwenda mrama.
•
Tunaziomba Taasisi za kiraia za ndani kuacha woga na badala yake kupaza
sauti zao masikioni mwa viongozi madhalimu kukemea unyanyasaji na
ukandamizaji wa haki za binadamu. Aidha, CUF inaziomba jumuiya za
kimataifa kuendelea kuitazama Zanzibar kwa umakini wa hali ya juu
kufuatilia mwenendo na matukio na kuweka kumbukumbu kwa hatua za baadae
kwa kila anaeonekana kushtadi kuonea wananchi wanyonge kutokana na
nafasi yake katika utumishi wa umma.
•
Tunatoa wito kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa,
John Magufuli, kuchukua dhamana ya uongozi kukataa kuhadaiwa na
wasaidizi wake na kukomesha matumizi mabaya ya vyombo vya ulinzi na
usalama vilivyo chini ya amri yake na kudhibiti uhuni wa kisiasa wa
baadhi ya watendaji wa vikosi vya Idara Maalum ya Zanzibar kama Amiri
Jeshi Mkuu wa Tanzania. Kwa la zanzibar, Rais Magufuli hana pa kupenyea
na kwamba atawajibika kutokana na mfumo wa Katiba, sheria na utaratibu
wa kuongoza nchi tuliojiwekea.
•
Tunatambua usumbufu, idhilali na mateso makubwa yanayowapata wananchi
wa visiwa vyote vya zanzibar kufuatla maamuzi yao ya tarehe 25 Oktoba
2015 ya kuikataa CCM na kuamua kufanya mabadiliko katika uongfozi wa
nchi. CUF inawaomba wananchi wote kuendelea na kujipamba na mavazi ya
subira na kuamini kuwa hizi ni hatua za mwisho za CCM kuelekea kufutika
katika nyoyo za wazanzibari na kwamba wananchi wote wausiane katika
kuvumilia na kukataa kuchokozeka kwa lengo la kutunza amani ya nchi yetu
na kufikia malengo yetu ya muda mrefu ya kukamata hatamu za dola ya
zanzibar bila kuathiri wanachi wetu.
•
CUF inawahakikishia wananchi wote kuwa haitarudi nyuma katika mapambano
ya kudai haki ya wananchi na kwamba maamuzi yao ya tarehe 25 Oktoba
2015 yatazingatiwa, kuheshimiwa na hatimaye haki kutamalaki katika
visiwa vya zanzibar. Ni wajibu kwa wazanzibari wote kutambua kuwa giza
nene hufuatiwa na miale ya nuru inayotoa faraja kwa kila mwanandamu.
Mamia
ya wafuasi wa CHADEMA wakiongozwa na Mwenyekiti wao Freeman Mbowe
leo wamefurika mahakama kuu jijini Mwanza katika kesi ya mbunge wa
zamani wa Nyamagana, Ezekiel Wenje (CHADEMA) anayepinga matokeo ya
Stanslaus Mabula (CCM).
Polisi wametumia nguvu ya ziada kuhakikisha ulinzi unaimarika mahakamani hapo
Ezekia Wenje akiwa Mahakamani
Mbunge wa Nyamagana Stanslaus Mabula akiwa mahakamani
Baada ya kimya cha muda mrefu Dogo Janja kutoka Tip Top
Connection 2016 aliachia hit single yake ya ‘My Life’, ngoma hiyo Dogo
Janja amebadili ni tofauti na tulivyomzoea katika ngoma zake za nyuma.
March 14 Dogo Janja kaachia rasmi video ya hit Single ya ‘My Life’ enjoy
mtu wangu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
amefanya uteuzi wa wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara, ambapo kati yao
13 ni wapya, 7 wamebakizwa katika vituo vyao vya kazi, 5 wamehamishwa
vituo vya kazi na 1 amepangiwa Mkoa Mpya wa Songwe.
Uteuzi huo umetangazwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Mussa
Ibrahim Iyombe leo tarehe 13 Machi, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam.
Wakuu wa Mikoa walioteuliwa ni kama ifuatavyo;
Mh. Paul Makonda - Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam.
Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga - Mkuu wa Mkoa wa Geita.
Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu - Mkuu wa Mkoa wa Kagera.
Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga - Mkuu wa Mkoa wa Katavi.
Brigedia Jeneral Mstaafu Emmanuel Maganga - Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.
Mh. Godfrey Zambi - Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
Dkt. Steven Kebwe - Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
Kamishna Mstaafu wa Polisi Zerote Steven - Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.
Mh. Anna Malecela Kilango - Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
Mhandisi Methew Mtigumwe - Mkuu wa Mkoa wa Singida.
Mh. Antony Mataka - Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.
Mh. Aggrey Mwanri - Mkuu wa Mkoa wa Tabora.
Mh. Martine Shigela - Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
Mh. Jordan Mungire Rugimbana - Mkuu wa Mkoa Dodoma.
Mh. Said Meck Sadick - Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.
Mh. Magesa Mulongo - Mkuu wa Mkoa Mara.
Mh. Amos Gabriel Makalla - Mkuu wa Mkoa Mbeya.
Mh. John Vianey Mongella - Mkuu wa Mkoa Mwanza.
Mh. Daudi Felix Ntibenda - Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Mh. Amina Juma Masenza - Mkuu wa Mkoa wa Iringa.
Mh. Joel Nkaya Bendera - Mkuu wa Mkoa wa Manyara.
Mh. Halima Omary Dendegu - Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.
Dkt. Rehema Nchimbi - Mkuu wa Mkoa wa Njombe.
Mhandisi Evarist Ndikilo - Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
Mh. Said Thabit Mwambungu - Mkuu wa Mkoa Ruvuma.
Luteni Mstaafu Chiku Galawa - Mkuu wa Mkoa wa Songwe (Mkoa mpya).
Wakuu wote wa Mikoa walioteuliwa, wataapishwa Jumanne tarehe 15 Machi, 2016 saa 3:30 Asubuhi Ikulu, Jijini Dar es salaam.
Wasifi (CV) ya Katibu Mkuu wa Chadema Tanzania kamanda Dr. Vincent B. Mashinji
Professional experience
Clinical Advisor & TB/HIV lead
UMSOM-IHV
July 2008 - Present
ART Program Doctor/IMA team lead
IMA Worldhealth
August 2006 - June 2008 (1 year 10 months)
Medical Officer/Anaesthesiology
Regency Medical Centre
October 2005 - August 2006 (10 months)
Medical Officer
Muhimbili National Hospital
August 2003 - October 2005 (2 years 2 months)
Research Assistant
Freelance
November 2002 - August 2003 (9 months)
Intern Docor
Muhimbili National Hospital
September 2001 - October 2002 (1 year 1 month)
Education history
Open University of Tanzania
PhD
August 2010 - Present
AMREF/UCLA Anderson School
MDI Certificate
April 2010 - April 2010
Blekinge Institute of Technology
MBA
September 2007 - March 2010 (2 years 6 months)
UMSOM-IHV
IPEP Certificate
May 2008 - May 2008
Evin School of Management
Certificate in CSR
October 2005 - October 2005
Muhimbili University College of Health Sciences
MMed/Anaesthesiology
September 2003 - April 2005 (1 year 7 months)
Muhimbili University College of Health Sciences
Certificate in Research Methodology
September 2004 - September 2004
Makerere University
MBChB
October 1995 - July 2001 (5 years 9 months)
Mzumbe High School
ACSEE
July 1992 - June 1994 (1 year 11 months)
St. Pius X Seminary, Makoko
GCSEE
January 1988 - October 1991 (3 years 9 months)
Iligamba Primary School
Leaving Certificate/Primary School
January 1981 - October 1987 (6 years 9 months)
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimemteua Dr Vicent Mashinji usiku
huu kuwa katibu mkuu mpya wa chama hicho kuchukua nafasi iliyoachwa
wazi na Dr Slaa ambaye alijiuzulu wadhifa huo mwaka jana.
Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi inautangazaia umma kuwa
wahitimu mahiri 10,629 waliofuzu Vyuo vya Kilimo vya Inyala, Mtwara,
Horti Tengeru, Igurusi, Katrin, Ukiriguru, Maruku, Uyole, KTC Moshi,
Mlingano, Tumbi, Ilonga, NSI Kidatu na Mubondo, wanaweza wakatumiwa
kwa lengo la kuongeza uzalishaji na tija katika kilimo.
Jumla ya wahitimu 7,525 wamefaulu katika ngazi ya Astashaada
kati ya hao, wanawake ni 2,557 na wanaume ni 4,968. Wahitimu 3,104
wameafaulu katika ngazi ya Stashahada (Diploma) ambapo wanawake ni
774 na wanaume 2,370.
Wahitimu hawa ni mahiri katika michepuo ya Stashahada ya fani
ya kilimo cha mboga matunda na maua (Horticultural Crops), Zana za
Kilimo, Uzalishaji wa Mazao, Umwagiliaji na Huduma za Kiufundi,
Mipango na Matumizi Bora ya Ardhi ya Kilimo na Chakula na Lishe.
Aidha, Wahitimu hao wanauwezo wa kiutendaji katika kuanzisha
na kutunza bustani za mimea, mboga na matunda, kushauri wakulima kwa
kutumia teknolojia mbalimbali ikiwemo TEHAMA, kusimamia kazi zote
zinazohusu matumizi ya Zana za Kilimo na kuzifanyia matengenezo kila
itapohitajika, kujenga miundombinu ya shamba ikiwemo maghala, vihenge
na mabanda ya wanyama mbalimbali.
Pia wanauwezo wa kuzalisha mazao makuu ya chakula na biashara
yanayolimwa nchini, kusaidia tafiti na kukusanya takwimu za utafiti wa
mazao, kusimamia ujenzi wa miradi midogo ya umwagiliaji na kuandaa
michoro ya miradi hiyo.
Wahitimu hao pia wanao uwezo wa kuandaa mazao baada ya
kuvunwa, kuchakata na kufungasha, kufanya tathmini ya lishe na mahitaji
ya chakula katika jamii, kuandaa mipango na kutoa ushauri kwa jamii
kuhusu masuala ya lishe.
Serikali inawafahamisha Wadau wa maendeleo ya kilimo na
mifugo, Wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi na yeyote mwenye
mahitaji yanayoweza kutekelezwa na wataalam hawa kuwa wanayo fursa ya
kuwaajiri, wahitimu hao ili kupata ufanisi katika shughuli zao za
kilimo. Imetolewa na; Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
WIZARA YA KILIMO MIFUGO NA UVUVI