Tuesday, 16 February 2016

BREAKING NEWS:TAARIFA KAMILI KUHUSU MATOKEO KIDATO CHA NNE 2015/16,HII HAPA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

Official VIDEO | Mirror Ft. Baraka Da Prince - Naogopa | Watch/Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
https://www.youtube.com/watch?v=W9MkMJ9Hr6s
Share:

New AUDIO | JamboSquad - DigiDigi | Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
https://mkito.com/song/digi-digi/18840/bwi-1-36787
Share:

New AUDIO | Dudu Baya#MAMBA - Kokoriko | Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
http://old.hulkshare.com/dl/mjp0w5dk0q2o/Kokoriko-_Dudu_Baya%23MAMBA.mp3?d=1
Share:

Majambazi Yaua Polisi Tanga

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Askari wa jeshi la polisi Koplo George Braiton aliyepigwa risasi na majambazi wakati akikabiliana nao katika tukio la ujambazi lililotokea barabara ya sita na saba jijini Tanga amefariki dunia.

Koplo Braiton amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Mkoa wa Tanga,Bombo, akiwa na watu wengine wawili waliopigwa risasi katika tukio hilo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga ACP.Mihayo Msikhela amesema kuwa bastola ilitumika kupoteza uhai wa Koplo George Braiton wa kituo cha polisi Chumbageni na kujeruhi raia wengine wawili ambao bado wanaendelea na matibabu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tanga.

Polisi wamesema walifanikiwa kuwakamata majambazi hao wakiwa na bastola waliyoitumia kwenye tukio hilo pamoja na visu wanavyovitumia kwenye matukio ya kihalifu.

Majirani waliokuwa wakiishi na Koplo Braitoni wamesema tukio hilo limewagusa,lakini wakaiomba jamii kuwafichua wahalifu kwa lengo la kukabiliana na vitendo hivyo.

Kolpo Braitoni anatarajiwa kusafirishwa kupelekwa mkoani Mara Februari 16 kwa ajili ya mazishi.
Share:

ANGALIA RATIBA YA UEFA:MECHI ZITAKAZOCHEZWA LEO JUMANNE FEBRUARY 16 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

MPYA:BODI YA MIKOPO WATUMBULIWA MAJIPU MKURUGENZI WA BODI YA MIKOPO ASIMAMISHWA KAZI

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako amewasitishia mikataba ya kazi Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mikopo (HESLB), George Nyatega na Wakurugenzi wengine watatu kutokana na utendaji mbovu katika kuendesha bodi hiyo.

Wengine ni Mkurugenzi Mkuu wa Mikopo ya wanafunzi asimamishwa kazi, wengine ni Mkurugenzi wa Urejeshaji wa Mikopo, Mkurugenzi Upangaji na Utoaji wa Mikopo.

Mkataba wa Mkurugenzi Mtendaji HESLB umesitishwa. Ilikua uishe mwezi August 2016. Mhasibu Mkuu (Bw. Kisare), Mkurugenzi wa Utoaji Mikopo (Bw. Laizer) na Mkurugenzi wa Urejeshaji Mikopo (Bw. Chagonja) wamesimamishwa kupisha uchunguzi.

Amewateua wafuatao ku Kaimu nafasi; Kaimu Mkurugenzi Mtendaji mteule ni Bw. Jerry Sabi kutoka Mzumbe University na Kaimu Mhasibu Mkuu mteule ni Bw. Daniel Mafie kutoka NECTA
Share:

SEKRETARIETI YA AJIRA:MATOKEO YA USAILI ULIOFANYIKA TAREHE 13-02-2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


TANGAZO LA KAZI DEC 29, 2015 Wasailiwa waliochaguliwa kuendelea na usaili wanatakiwa kufika, tarehe na muda kama ilivyo oneshwa kwenye ratiba ya usaili.
Wasailiwa wanakumbushwa kufika na vyeti halisi (Original certificates)
KADA: ICT OFFICER GRADE II (APPLICATION DEVELOPMENT ICT MANAGEMENT)               
MWAJIRI: (e-Government Agency)               
               
SN    EXAM NUMBER                          SCORES  REMARKS
1    eGA ICT APPL DEV MGT - 0081        53    SELECTED
2    eGA ICT APPL DEV MGT - 0069        52    SELECTED
3    eGA ICT APPL DEV MGT - 0140        52    SELECTED
4    eGA ICT APPL DEV MGT - 0035        51    SELECTED

Read more...
 
Share:

breaking news:haya hapa matokeo kidato cha nne 2015

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
bonyeza hapa kuyatazama
Share:

Serikali kutangaza ajira 40,000 za walimu

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
jaffo
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jaffo

Ili kupunguza ukosefu wa walimu katika shule za msingi na sekondari nchini, serikali inatarajia kutoa ajira 40,000 kwa walimu mwaka huu ili kuendana na kasi ya uandikishaji wa wanafunzi na utoaji wa elimu bure.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jaffo, amewaeleza wanahabari kuwa idadi hiyo inalenga kupunguza changamoto ya upungufu wa walimu shuleni na utoaji wa elimu bora zaidi.
Jaffo alisema ajira hizo zitatangazwa mapema mwaka huu na zitaongeza nguvu kwenye shule zenye uhitaji wa walimu hasa mpya na zile zilizoandikisha wanafunzi wengi wa darasa la kwanza na kidato cha kwanza.
Sambamba na hilo, ameahidi kushirikiana na shule za msingi zilizoandikisha wanafunzi wengi zaidi wa darasa la kwanza ili shule hizo zipate miundombinu ya kutosha kuwahifadhi wanafunzi hao.
Amesema kwa kuanza, serikali imejipanga kuongeza majengo katika shule ya msingi Mbagala Majimatitu ambayo imeandikisha wanafunzi wa darasa la kwanza 1,022, idadi ambayo ni sawa na wanafunzi wa shule moja kuanzia darasa la kwanza hadi la saba.
Share:

Rais Magufuli Amteua Dr. Asha Rose Migiro Na Mathias Chikawe Kuwa Mabalozi Wapya....Dr. Kipilimba Kateuliwa Kuwa Bosi Mpya Wa NIDA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa mabalozi watatu katika Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa.

Rais Magufuli pia amefanya uteuzi wa makamishna wanne wa Jeshi la Polisi na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, imewataja mabalozi walioteuliwa kuwa ni Dkt. Asha-Rose Mtengeti Migiro, Mheshimiwa Mathias Meinrad Chikawe na Dkt. Ramadhan Dau.

Vituo vya uwakilishi kwa mabalozi hawa vitajulikana baada ya taratibu husika za kidiplomasia kukamilika.

Kwa upande wa Makamishna wa Polisi, Balozi Sefue amewataja walioteuliwa kuwa ni:

Naibu Kamishna wa Polisi Simon Nyakoro Sirro ambaye amepandishwa cheo kuwa Kamishna wa Polisi, na ameteuliwa kuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam. Kamishna Sirro anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Kamishna Mstaafu Suleiman Kova.

Naibu Kamishna wa Polisi Albert Nyamuhanga ambaye amepandishwa cheo kuwa Kamishna wa Polisi na ameteuliwa kuongoza Idara ya Fedha, Utawala na Lojistiki. Kamishna Nyamuhanga anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Kamishna wa Polisi Clodwing Mathew Mtweve aliyeteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza.

Naibu Kamishna wa Polisi Robert Boaz Mikomangwa ambaye amepandishwa cheo kuwa Kamishna wa Polisi na ameteuliwa kuongoza Idara ya Intelijensia. 
Kamishna Mikomangwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Kamishna Valentino Mlowola aliyeteuliwa kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Nsato Marijani Mssanzya ambaye amepandishwa cheo kuwa Kamishna wa Polisi na ameteuliwa kuongoza Idara ya Mafunzo na Operesheni. 
Kamishna Mssanzya anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Kamishna wa Polisi Paul Moses Chagonja aliyeteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi.

Aidha, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Modestus Francis Kipilimba kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA). 
Kabla ya Uteuzi huu Dkt. Kipilimba alikuwa Mkurugenzi wa Menejimenti ya Udhibiti (Director of Risk Management) katika Benki Kuu ya Tanzania. Dkt. Kipilimba anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Dikson Maimu ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Teuzi zote zinaanzia leo tarehe 15 Februari, 2016

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
15 Februari, 2016
Share:

Mchakato Wa Kura Ya Maoni Ya Katiba Mpya Waanza

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva, amesema mchakato wa Kura ya Maoni ya Katiba mpya umeanza baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana.

Kauli hiyo ya Jaji Lubuva imekuja wakati wadau wa siasa nchini wakimtaka Rais Dk. John Magufuli, kutoendelea na Kura ya maoni badala yake mchakato wa Katiba mpya urudi nyuma baadhi ya mambo yaliyo kwenye Katiba iliyopendekezwa yarekebishwe.

Itakumbukwa kuwa mchakato wa Katiba mpya uliingia dosari baada ya baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kupinga mfumo wa Serikali Tatu uliokuwa umependekezwa na Tume ya Jaji mstaafu Joseph Warioba, iliyokusanya maoni nchi nzima na matokeo yake kuzaa kundi lililojiita Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

“Tulikuwa tunangoja tumalize uchaguzi, kama vile ambavyo Mnyamwezi anavyobeba mzigo, unamaliza mmoja unakwenda kwa mwingine. Sasa tumemaliza (uchaguzi mkuu), tunakwenda kwa lingine (Kura ya Maoni),” alisema Jaji Lubuva.

Aliongeza: “Tunaliangalia na kama Tume tutakuja kuwajulisha wananchi hali ikoje, tuliahirisha (Kura ya Maoni) ili tumalize hili (uchaguzi mkuu).” alisema Jaji Lubuva na kuongeza.

“Hili ni suala linalohitaji mambo ya bajeti kubwa na ndiyo tumetoka kwenye uchaguzi na serikali ndiyo inaanza, kwa hiyo ni suala ambalo tunaliangalia na baadaye wananchi watajulishwa,” alisema Jaji mstaafu Lubuva.

Alipoulizwa kuhusu makadirio ya bajeti ya kuendesha kura hiyo ya maoni, Lubuva alisema: “Hilo niulize siku nyingine, sina zaidi ya hapo kwa leo.”

Rais Magufuli alipokuwa akihutubia Bunge la 11 siku ya kulizindua Novemba 20, mwaka jana, alisema serikali yake imepokea kiporo cha mchakato wa Katiba ambao haukukamilika katika awamu iliyomtangulia kutokana na kutokukamilika kwa wakati kwa uandikishaji wapiga kura.

“Napenda kuwahakikishia kuwa tunatambua na kuthamini kazi kubwa ya kizalendo iliyofanywa na wananchi walioshiriki hatua ya awali ya ukusanyaji wa maoni kuhusu Katiba mpya, Tume ya Marekebisho ya Katiba na Bunge la Katiba lililotupatia Katiba Inayopendekezwa. Tutatekeleza wajibu wetu kama ulivyoainishwa katika Sheria ya Marekebisho ya Katiba,” alisema Rais Magufuli. 

Mbali na muundo wa serikali tatu, baadhi ya mambo ambayo Ukawa walitaka yawe kwenye Katiba mpya ni mamlaka ya Rais kupunguzwa, ushindi wa Rais uwe zaidi ya asilimia 50, Tume huru ya Uchaguzi, matokeo ya Rais kupingwa mahakamani, kuwe na mgombea binafsi, mawaziri wasitokane na wabunge, na muundo mpya wa Bunge la Muungano.
Share:

Waziri Kairuki : "TAKUKURU Kuna Majipu Yanayohitaji Kutumbuliwa "

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

WAFANYAKAZI wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), wametakiwa kuanza kujisafisha huku wakiambiwa kwamba taasisi hiyo haitaepuka kutumbuliwa majipu.

Aidha, wameagizwa kuwasilisha upya taarifa za mali zao kwa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, zifanyiwe uhakiki wa mali; moja baada ya nyingine kubaini waliofanya udanganyifu wa umiliki wa mali zao.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angela Kairuki alisema hayo jana Dar es Salaam kwenye ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa viongozi wa taasisi hiyo.

Alisisitiza kuwa tayari anazo taarifa zinazohitaji baadhi ya viongozi wa taasisi hiyo kutumbuliwa majipu muda muafaka utakapowadia. 
Kairuki aliagiza taasisi hiyo kufanyia tathmini kesi zake zote, ilizowahi kushindwa na kuja na majibu ya sababu za kushindwa na endapo itabainika hazikushinda kutokana na mchezo mchafu wa wachunguzi, wahusika wachukuliwe hatua haraka iwezekanavyo.

“Niliposikia mnataja majina yenu wakati wa kujitambulisha, nilikuwa nafurahi sana kwani wengi wenu nawajua na nina taarifa zenu. Haiwezekani wewe mtu mmoja watu wengi wawe wanakuongelea vibaya. Msifikiri majipu humu (Takukuru) hakuna, yapo na nawahakikishia tutayatumbua tu,” alisisitiza Waziri huyo.

Alisema iwapo yupo mtumishi hasa viongozi wa taasisi hiyo, anayejitambua kuwa ni ‘jipu’, ajisalimishe kwani akiendelea kusubiri na kutumbuliwa, mwisho wake utakuwa mbaya. 
“Tukiwatumbua hali itakuwa mbaya kwani nyie mko chini ya Ofisi ya Rais, hata Rais (Dk John Magufuli) hatasita kuwachukulia hatua si tu za kinidhamu bali hata za kisheria,” alibainisha.

Alisema katika taasisi hiyo, yapo maeneo mengi yanayohitaji kutumbuliwa majipu kuanzia Uhasibu, Ukaguzi na Manunuzi zikiwemo ofisi za mikoani akitolea mfano Mkoa wa Kilimanjaro na makao makuu, Upanga, Dar es Salaam.

“Tutasafisha nawahakikishia hata ikibidi kuanza upya, ikitulazimu pia kufukuza wote ikithibitika mnakwenda kinyume na maadili yenu tutawafukuza ila hatutamwonea mtu, kwani wako watu wengi wenye sifa wanaotaka kufanya kazi,” alisisitiza Kairuki.

Alisema kuanzia sasa, ofisi hiyo itawekewa malengo ya utendaji wake na kufanyiwa tathmini hasa kwa kesi zilizoshindwa ifahamike aliyezifanya, sababu za kushindwa, iwapo imetokana na uzembe au kama upo mkono wa mtu. 
Alisema imefikia wakati sasa watumishi wa taasisi hiyo wanapaswa sasa wale kiapo cha ahadi ya uadilifu na kukisaini ili watakaoshindwa wachukuliwe hatua za kinidhamu.

Taarifa za mali
Aliwataka watumishi wote wa taasisi hiyo, kurejea upya kuwasilisha taarifa za mali zao kwa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma.
 Alisema taarifa hizo zitapewa kipaumbele cha kuhakikiwa mali moja baada ya nyingine na endapo mtumishi atabainika kufanya udanganyifu wa mali anazomiliki, atachukuliwa hatua.

Alihadharisha kuwa chombo hicho cha kupambana na rushwa hakipaswi kutuhumiwa kwa rushwa. Alisema kikituhumiwa kwa sifa hiyo, ni sawa na kuigeuza Takukuru kuwa jipu badala ya vidole vya kutumbulia majipu.

Takukuru mpya
Alisema Serikali ya Awamu ya Tano, imejipanga kuhakikisha inazalisha chombo kipya cha kuzuia na kupambana na rushwa chenye maadili. 
Aliwataka wanaoona hawawezi kwenda na kasi hiyo, wawasilisha barua zao za kujiuzulu kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, Kamishna wa Polisi Valentino Mlowola.

Hata hivyo, alisema Serikali inatambua kuwa kazi ya upelelezi na uchunguzi ni ngumu kutokana na kukabiliwa na vishawishi vingi, jambo ambalo wanahitaji ujasiri. Alisisitiza watumishi hao kutunza heshima yao na chombo hicho.

“Faraja ya uchunguzi ni kufanikisha majalada kwenda kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) na baadaye watuhumiwa kufikishwa mahakamani. Sasa ili kufanikisha faraja hii ni vyema kufanya kazi kwa weledi na tusiwe na pupa ili mradi tupeleke kesi nyingi kwa DPP na kuziwasilisha mahakamani,” alisema Kairuki.

Aliendelea, “Nasema haya kwa sababu nafahamu bado kwenye uchunguzi hapa Takukuru kuna upungufu. Nafikiri mmemuona Mheshimiwa Rais anavyoshughulikia suala la rushwa na ufisadi, ni wajibu wenu Takukuru kufanikisha azma hii kwa kuja na matokeo ya utendaji chanya.”

Aidha, waziri huyo aliitaka taasisi hiyo kutumia weledi, sifa yaa ukachero wa kiupelelezi na kiuchunguzi kufuatilia matukio yenye shaka yanayoendelea mitaani na si kusubiri taasisi kubwa kuyavumbua.

“Nyie ndio makachero tumieni ukachero wenu kuibua ufisadi, kuna mtu mmoja amebainishwa na Rais lakini jina lake kwa umaarufu na utajiri wake linatumika kama kituo, alishajiuliza sababu na kuchunguza?” alihoji.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mlowola aliwataka wafanyakazi wa taasisi hiyo kubadilika na kuacha kufanya kazi kwa mazoea. 
Kasi ya Magufuli 
Aliwataka wahakikishe wanaendana na kasi ya Dk Magufuli na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya utendaji na utumbuaji wa majipu katika maeneo yenye ubadhirifu wa fedha, rushwa, ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.

“Natarajia tutafanya kazi kwa weledi na si nguvu, kwa mfano taarifa zilizotolewa katika maeneo ya bandarini na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), siye ndio tulitakiwa tuziwasilishe juu (ngazi ya Rais). Naomba tusisubiri kuletewa,” alisisitiza.

Aliwataka watumishi hao kujiepusha kuwa watuhumiwa wa rushwa. “Jamani hii ni mbaya kwetu Polisi akituhumiwa ujambazi ni mbaya sana, lakini ofisa wa Takukuru akituhumiwa rushwa ni dhambi kubwa. Sisi tuwe watu wa mwisho kutuhumiwa kwa rushwa."

Aliwataka watumishi hao kuelekeza nguvu zao katika kuhakikisha wanaisaidia Serikali kwenye eneo la upotevu wa fedha kwa kufuatilia matumizi na miradi ya maendeleo na fedha zinazopelekwa kwenye halmashauri na kwenye manunuzi ya umma.

Alisema katika utekelezaji wa jukumu la kuzuia na kupambana na rushwa nchini kwa mwaka 2014/15 taasisi hiyo ilipokea malalamiko 4,675. Ilifanyia uchunguzi na kukamilisha majalada 667, kupeleka kwa DPP majalada 278, walirejeshewa majalada 172 yenye vibali vya kufungua mashtaka na kufungua kesi mpya 314 nchini kote.

Aidha alisema taasisi hiyo ilishinda kesi 132 mahakamani na washitakiwa walihukumiwa vifungo mbalimbali ikiwemo faini. Ziliokolewa Sh bilioni saba zilizokuwa ziingie kwenye mifuko ya wabadhirifu wachache.

Ndani ya siku 100 za Rais Magufuli madarakani taasisi hiyo ilipokea malalamiko 411 kutoka kwa wananchi, imefungua mafaili 146 ya uchunguzi. Imepeleka kwa DPP mafaili 103, mafaili 65 yenye kibali cha DPP yamerejeshwa kwa ajili ya kufunguliwa mashtaka, jumla ya kesi 72 mpya zimefunguliwa mahakamani na imeshinda kesi 40 na kushindwa kesi 52.

“Ndani ya siku 100 tumefanikiwa kuwafikisha mahakamani watuhumiwa 11 akiwemo Mtendaji Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRL) Kipallo Kisamfu,” alisisitiza.
Share:

Tanzia: Msanii Wa Bongo Fleva John Woka Afariki Dunia

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye alijipatia umaarufu mkubwa kwa staili yake ya kuimba kama mlevi, Joni Woka amefariki dunia alfajiri ya leo.

Woka amefariki baada ya juzi kupata ajali ya kulipukiwa na mtungi wa gesi. Alikuwa amelazwa kwenye hospitali ya taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.
 
Hii ni taarifa iliyotolewa na mtu wa karibu na rapper huyo kuelezea ajali hiyo:
 
"Walikuwa wanahangaika kurekebisha usafiri kwenye garage hapo Sinza, sasa katika kuhangaikia upande wa AC mtungi wa gas ukalipuka,moja ya vipande vya chuma chenye ncha kali kikamchoma kichwani. Madaktari wanahofia imefika mbali kiasi kwamba damu inamwagikia kwenye ubongo."

Msanii John Woka ambaye alikuwa kwenye kundi la Watukutu Family, alijipatia umaarufu kwa nyimbo zake za Sophia, baby gal na nyinginezo, ambazo aliziimba kwa mtindo wa ulevi.
 
Kwa yeyote aliyeguswa na angependa kutoa rambi rambi anaweza kuwasiliana na kaka yake kwa namba +255767007005.
 
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger