Monday 14 April 2014

Dk.Bilal,Waziri Magufuli wanusurika ajali ya chopa

Dk.Bilal,Waziri Magufuli wanusurika ajali ya chopa

Baadhi ya watu wakiangalia helikopta iliyokuwa imembeba Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, muda mfupi baada ya ndege hiyo kuanguka eneo la Uwanja wa Ndege Terminal One jijini Dar es Salaam jana.Picha: Mpigapicha Wetu
Makamu wa Rais, Dk. Ghalib Bilal , Waziri wa Ujenzi, Dk.John Magufuli na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick, wamenusurika kifo baada ya Helkopita ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliyokuwa wakisafiria kupata hitilafu angani na kuanguka.

 Wengine walionusurika katika ajali ya helikopta hiyo  iliyokuwa imebeba watu 11 ni Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, waandishi wa habari wawili, walinzi wawili na maofisa wengine wa serikali.

Kamanda wa Polisi wa Viwanja vya Ndege, Kamishna Khamis Suleiman,akizungumza na NIPASHE alisema kuwa ajali hiyo ilitokea  jana majira ya saa 3:15 asubuhi katika eneo la uwanja wa ndege wa Air Wing unaotumiwa na jeshi.

 Suleiman alisema viongozi hao baada ya kupata ajali hiyo walikimbizwa hospitali ambayo hakuitaja jina kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Hata hivyo, taarifa ambazo NIPASHE ilizipata zilieleza kuwa viongozi hao baada ya kupata ajali hiyo walipelekwa katika hospitali ya usalama wa Taifa iliyopo Makumbusho jijini Dar es Salaam.

Kamanda Suleiman alisema viongozi hao walipata ajali hiyo wakati wanakwenda kukagua maeneo yaliyoathirika na mafuriko ya mvua zilizonyesha tangu juzi  jijini Dar es Salaam.

Alisema helkopita hiyo muda mfupi baada ya kuruka katika uwanja huo wa Air Wing, ilipata hitilafu ikiwa angani na kuanguka.

Aliongeza kuwa hali za viongozi hao zinaendelea vizuri, na wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali hiyo.

Waziri wa Uchukuzi, Dk.Harrison Mwakyembe, alipoulizwa na NIPASHE alisema taarifa za tukio hilo amezipata na kwamba ajali hiyo haijatokea upande wa uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa  Mwl.Julius Nyerere (JNIA)  kama ambavyo baadhi ya watu wanaeleza.

“Kimsingi taarifa za tukio hili unaweza kuzipata zaidi kutoka kwa watu wa jeshi maana ajali imetokea upande wa air wing,”alisema Dk.Mwakyembe.

Wakati huo huo, Kurugenzi ya Habari ya JWTZ, imesema helikopta hiyo ilipata ajali katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwl Julius Nyerere (JNIA) kwa upande wa Jeshi wakati ilipokuwa katika hatua ya kuanza kuruka.

 Katika taarifa hiyo iliyotumwa kwa vyombo vya habari na Msemaji wa JWTZ, Kanali Erick Komba imeeleza kuwa mbali na viongozi hao, wengine waliokuwemo ni Dk. Mnzava ambaye ni msaidizi wa Makamu wa Rais, Msaidizi wa Kamanda Kova na waandishi wa habari watatu.  

 Alisema ujumbe wa Makamu wa Rais ulikuwa  katika safari ya kuzungukia maeneo yaliyoathirika na mafuriko  katika jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani kufuatia mvua hizo zilizoanza kunyesha kuanzia Aprili 11, mwaka huu.

Komba alisema Makamu wa Rais pamoja na ujumbe wake hawakupata majeraha katika ajali hiyo. Aidha, rubani na wasaidizi wake pia wametoka salama.
Aliongeza kuwa uchunguzi wa ajali hiyo umeanza mara moja kwa ajili ya kubaini chanzo cha ajali hiyo.
 
Share:

Thursday 10 April 2014

JK: Gas, oil policy in place in October


President Jakaya Kikwete opens 19th Annual Research Workshop organised by Research and Poverty Allevation (REPOA) in Dar es Salaam yesterday. (Photo: Tryphone Mweji)
President Jakaya Kikwete yesterday reassured Tanzanians that the government will finalise the policy and legislation for oil and gas extraction in October, this year.

Speaking at the 19th REPOA Annual Research Workshop held in Dar es Salaam yesterday, President Kikwete said there have been extensive discussions on the role natural resources should play in the country’s economy.

“This is particularly relevant today, considering the recent discoveries of large volumes of natural gas, now approximated at 46 trillion cubic feet, and the vast reserves of forests, minerals, diverse wildlife and land that Tanzania has,” he said.

The President also said that the challenge facing the country is how to link these resources with the aspirations of the 2025 Development Vision and the socio-economic transformation the nation desires.

“The strategies and policies are meant to ensure that our people participate productively in the utilisation of the natural resources we are blessed with.

We are also in the process of putting in place a local content policy that will provide a framework for ensuring adequate participation of Micro, Small and Medium Enterprises and local communities in exploiting and utilising our
natural resources,” he said.

He added: “We hope that the private sector, working closely with the government, will proactively engage in the efforts to build the capacity of Tanzanians in different disciplines that are relevant to the various segments of our natural resources’ value chain”.

He underscored that the oil and gas sector is a priority subsector, given the volume of the resources, the intensity of capital investments, and flow of revenues expected from their commercialisation.

“I hope that this workshop will dwell on these issues too, drawing from the experience of other countries as well, on how the enterprise sector including the MSMEs can be leveraged to participate more meaningfully in the desired socio-economic transformation,” the President said.

The president noted that a sound business environment and regulatory landscape have allowed enterprises, both large and MSMEs to thrive and effectively address the problem of unemployment, especially among the youths.
He added that the quest for inclusive development requires dramatic transformation of mind-sets and attitudes as well.

For his part, REPOA Executive Director Prof Samwel Wangwe said that reviews of trends in growth, employment and poverty in Tanzania have highlighted challenges and risks of achieving high growth which is not accompanied with the requisite transformation of the economy and widespread job creation.

“This signifies the challenge of low productivity and low returns to labour in agriculture and micro and small enterprises is predominantly in the informal economy where majority of Tanzanians derive their livelihoods from,” he said.

He added: “The low returns to labour in agriculture push people out of the sector in search of alternative sources of employment, but most of this migrating labour ends up in the lowest end of the non-farm sectors, mainly trade, other services and a few in manufacturing activities.”

He also said that the resulting kind of urbanisation where the informal economic activities provide low returns to labour carries with it the risk of turning rural poverty into urban poverty.

He insisted that there is a quest for deeper understanding of what it would take to transition from rural and urban poverty to prosperity in both the rural and urban economy.

The main objective of the two-day workshop is to achieve deeper understanding of the dynamics of micro and small scale economic activities and identify options for managing the enterprise transformation process with a view to realising more inclusive growth. 

Share:

Bunge Maalum laanza kusikiliza taarifa za Kamati


Bunge Maalum laanza kusikiliza taarifa za Kamati

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta amesema mjadala kuhusu  taarifa za Sura ya Kwanza na ya Sita za Rasimu  ya  Katiba  ya Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania unatarajia kuanza wiki ijayo katika Bunge hilo mara baada ya kumaliza kupokea taarifa za Kamati.
 Sitta  alisema hayo  katika ukumbi wa Bunge hilo mjini Dodoma baada  baadhi ya wajumbe kumwomba  kuchangia mjadala wakati ripoti hizo zikiendelea kuwasilishwa.
 Alisema mdajala wa kuchangia sura hizo utaanza mara baada  ya   Kamati 12 za Bunge Maalum la Katiba  kuwasilisha  taarifa zao  za Sura ya Kwanza na ya Sita  kuhusu  Rasimu ya  Katiba  ya Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania katika Bunge hilo.
 Aliongeza kuwa  kwa kujibu wa Kanuni ya namba 33(6) ambayo inasema baada ya  hoja za taarifa za Kamati  Namba Moja  hadi Namba Kumi na Mbili kutolewa katika Bunge Maalum na Mwenyekiti kuelekeza hoja hizo zijadiliwe , mjadala kuhusu taarifa hizo utaanza.
 Mwenyekiti huyo aliwataka baadhi ya wajumbe hao kusubiri mpaka uwasilishaji wa taarifa hizo utakapokamilika ndio watapata nafasi  ya kuchangia kwa muda mrefu  na kuwezesha wajumbe wengi kupata nafasi hiyo.
Share:

Wednesday 9 April 2014

VIDEO:UOZO MTUPU ANGALIA WANAFUNZI HAWA MAMBO WANAYOYAFANYA


Share:

VIDEO:AFUMANIWA NA MME WA MTU CHUMBANI KWAKE AKUTWA NA HIRIZI ZA KUTOSHA


Share:

VIDEO:KANGA MOJA WAKIWA NDANI YA TANGA-LAKI SI PESA MILIONI MATUMIZI


Share:

Tuesday 8 April 2014

VIDEO:JAMAA AFUMANIWA NA MKE WA MTU


Share:

VIDEO:JINSI YA KUSOMA SMS ONLINE BILA YA MWENYE SIMU KUJUA

SOMA KUPITIA HAPA...........BONYEZA

Share:

VIDEO: LOOK HERE THE WONDERS OF GAUCHO


Share:

SOMA HABARI HIZI KUHUSU MASTAA WA BONGO

MASTAA MATAJIRI WACHUNGUZWA



KIMENUKA! Jeshi la Polisi Tanzania kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali za serikali zimeanza kuwachunguza watu wenye majina makubwa ‘mastaa’ Bongo ambao wameibuka na utajiri wa ghafla, Uwazi limeambiwa.
Masanja Mkandamizaji.
Kwa mujibu wa chanzo nyeti ambacho kiko ‘jikoni’ kwenye jeshi hilo, mbali na mastaa, wengine ambao tayari orodha yao ipo ni wafanyabiashara, wafanyakazi wa serikali na viongozi wa dini ambao wameibuka kuwa mamilionea kwa muda mfupi huku shughuli zao za…

ANAYEISHI KWENYE HANDAKI BALAA JIPYA!


CHACHA Makenge (38) aliyeripotiwa awali kuishi ndani ya handaki katika eneo la pori la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani, amepatwa na balaa jipya baada ya makazi yake kuvamiwa na askari, kukamatwa na mwishowe kupelekwa Muhimbili kitengo cha wagonjwa wa akili kwa ajili ya matibabu.
Chacha Makenge (38) akiota moto nje ya handaki lake katika eneo la pori la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani.
Kana kwamba haitoshi, Makenge ambaye aliwahi kuishi…

MAAJABU YA MUNGU!


KATIKA hali ya kushangaza, wagonjwa wa mtindio wa ubongo, Paul Ngido na Asha Yahya wanaolelewa kwenye kituo cha watoto wenye matatizo mbalimbali wakiwemo yatima cha Ngido kilichopo Mazimbu FK mkoani hapa wamejikuta wakizaa watoto wawili, Keisha na Glory ndani ya kituo hicho.
Paul Ngido na Asha Yahya  wanaolelewa kwenye kituo cha watoto wenye matatizo mbalimbali waliowazaa watoto Keisha na Glory.
Mkurugenzi mkuu wa kituo hicho, Linda Cyprian Ngido amethibitisha kutokea…

NJEMBA YAMBAKA MTOTO WA MIAKA MINNE


NI AIBU!Jamaa mmoja anayejulikana kwa jina la Iddi Mgosi anashikiliwa na Polisi wa Kituo cha Wazo jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka minne (jina linahifadhiwa) huko Mivumoni, Madale Machi 18, mwaka huu.
Mtoto wa miaka minne aliyefanyiwa unyama huo.
Mgosi, ambaye umri wake haukuweza kupatikana mara moja, anadaiwa kumrubuni mtoto huyo kutoka nyumbani kwao na kumpeleka kwake, ambako alimuingilia kwa nguvu na baadaye kumtisha…

TATIZO LA MACHINGA LINATAKA BUSARA

NINAWASALIMU kwa jina la Bwana Mungu, mwingi wa rehema na muweza wa kila jambo. Siku zote nimekuwa nikiwasihi kumuweka mbele muumba wa nchi na mbingu, kwani kwake hakuna lisilowezekana.
Wagambo wakiwa kazini katika operesheni bomobomoa maeneo ya Posta mpya.
Hivi sasa kuna kampeni kubwa ya kusafisha jiji kwa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Temeke na Kinondoni kubomoa vibanda vya biashara vilivyojengwa kinyume na taratibu katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Jambo hilo limesababisha usumbufu mkubwa kwa wakazi wa jiji…

UNAKUBALIKA KWENYE JAMII-2

BADO tunaendelea na somo letu ambalo safari hii nagusia upande wa maisha. Ndugu zangu, kukubalika kwenye jamii kuna manufaa makubwa kama nilivyosema wiki iliyopita.

Niliishia pale nilipofafanua hasara za kutokubalika kwenye jamii. Sasa leo tuendelee.
KWA NINI HUKUBALIKI?

Wakati naanza kabisa kuandika mada hii, nimeeleza kwamba kila kinachotokea duniani huwa na sababu zake. Haiwezekani ukawa hukubaliki kwa chuki za watu au watu kukuonea wivu.

Lazima kuna sababu zinazosababisha usikubalike. Najua kila mmoja anaujua ukweli wa maisha yake ndani ya moyo wake.
Hapa nitakuandikia sababu muhimu…

MBWA WALIOMLA MTOTO NUSURA WAMLE BABA MTU

Mtoto Christian Alex aliyeliwa na mbwa enzi za uhai wake.


ZIMEKATIKA wiki mbili tangu kuzikwa kwa mtoto Christian Alex (6)  aliyeuawa kwa kushambuliwa na mbwa watatu waliodaiwa ni wa Ubalozi wa Qatar nchini, mbwa hao wamemkosakosa baba mtu.

Tukio la kuuawa kwa mtoto huyo lilijiri Kunduchi  Jangwani Beach jijini Dar Machi  26, mwaka huu.
Kwa mujibu wa chanzo, mara baada ya kumaliza shughuli ya kumzika marehemu katika Makaburi ya Mburahati jijini Dar, baba mzazi Alex Augustino alikaa kikao na ndugu ili kuangalia uwezekano wa kufika kwenye makazi hayo ya ubalozi na kuzungumza nao kujua hatima ya sakata hilo.
Baada ya makubaliano,…

TUZO YA MWANAMKE BORA, HESHIMA YA KWELI YA MWANAMKE, PINDA NI MSOMI WA UWAZI


Mgeni rasmi, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akihutubia kabla ya kukabidhi tuzo.

Mwanamke wa…

TUUCHOKONOE, TUUPINDUE ILI TUUBORESHE

WAJUMBE wa Bunge Maalum la Katiba wanaendelea na mchakato wa kupitia vifungu vya Rasimu katika ngazi ya kamati, kabla ya keshokutwa kuanza rasmi mjadala wa namna gani Tanzania inaweza kupata katiba mpya, miaka 50 baada ya kuungana kwa nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar.
Katika hatua za awali ngazi ya kamati, tumeshuhudia mambo mengi hasa yanayohusu hatima ya Muungano, ambao umekuwa ndiyo simulizi kuu katika mchakato mzima.
Kwa miaka mingi Watanzania tumeishi tukiaminishwa kuwa Muungano huu uko safi na yeyote aliyeonekana kuuzungumzia kwa namna ya kuukosoa, alichukuliwa kama msaliti, mhaini na mtu asiye na nia njema na nchi yetu.
Mambo mengi yanayohusu uhusiano wa nchi hizi mbili umekuwa siri kubwa, baadhi ya mambo yameharibika au kwenda mrama kwa kuwa kila mmoja alikuwa hataki kuonekana…

Share:

ANGALIA MAJINA HAPA YA WALIOPANGIWA VITUO VYA AFYA (AJIRA) 2013/2014

Share:

SOMA MAGAZETI YA LEO 08/04/2014

1_df6c1.jpg
2_60742.jpg
3_abfda.jpg
4_146e8.jpg
5_46469.jpg
6_6457f.jpg
66854_688389021225559_7905396027206939490_n_b7655.jpg
984038_688393924558402_8227931919131465226_n_48ad2.jpg
1012133_688388851225576_7974244423289239200_n_15ad8.jpg
1511914_688393854558409_4524716445678454352_n_6ca0e.jpg
1618432_688389154558879_4227702238964895763_n_49548.jpg
10150701_688389124558882_2727082128162427829_n_1_968cf.jpg
10151186_688392871225174_6366814600379550084_n_ab357.jpg
10154011_688392311225230_3505961519200983127_n_a0890.jpg
10155426_688398157891312_7651917783195626200_n_35ea1.jpg
10171238_688389074558887_9140776556010772895_n_46b35.jpg
Share:

Monday 7 April 2014

VIDEO:ANGALIA FUMANIZI HILI HATARI SANA MKE WA MTU SUMU


Share:

MATOKEO YA AWALI UCHAGUZI CHALINZE

Share:

VIDEO:ANGALIA LIVE SHOW YA KHANGA MOJA ILIVYOFANA


Share:

Thursday 3 April 2014

VIDEO:MTOTO ALIEZALIWA AKIWA HANA UBONGO


Share:

Tangazo la kazi:JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA RAIS
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA
UMMA
Kumb. Na EA.7/96/01/G/09
01 Aprili, 2014
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Sekretariati ya Ajira katika Utumishi wa Umma ni chombo ambacho kimeundwa kwa
mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa
na Sheria Na. 18 ya mwaka 2007 kifungu 29(1). Kwa mujibu wa Sheria hiyo, chombo hiki,
pamoja na kazi zingine kimepewa jukumu la kutangaza nafasi wazi za kazi zinazotokea
katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Waajiri (Taasisi za Umma).
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma anakaribisha maombi kwa
Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi 482 za kazi kwa waajiri mbalimbali
kama ifuatavyo:
MASHARTI YA JUMLA KWA KAZI ZOTE.
i. Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania.
ii. Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa.
iii. Waombaji ambao tayari ni Watumishi wa Umma na wamejipatia sifa za kuingilia
katika kada tofauti na walizonazo, wapitishe barua zao za maombi ya nafasi za
kazi kwa Waajiri wao na Waajiri wajiridhishe ipasavyo.
iv.
Nafasi ya kazi inayoombwa iandikwe katika kichwa cha habari cha barua na juu
ya bahasha, kutozingatiwa hili kutasababisha maombi ya kazi kuwa batili.
v.
Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye
anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (referees)
watatu wa kuaminika.
1
vi.
Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, nakala za vyeti vya kidato cha nne
na kidato cha sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo
mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika. Viambatanisho hivyo vibanwe sawa
sawa kuondoa uwezekano wa kudondoka au kupotea.
- - Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VI
- Cheti cha Kompyuta
- Vyeti vya kitaaluma (Professional certificates from respective boards)
-
vii.
Shahada ya juu/Shahada/Stashahada ya juu/Stashahada/Astashahada.
Picha moja “Passport size” ya hivi karibuni iandikwe jina kwa nyuma.
“Transcripts”, “Testmonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hati
matokeo za kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS)
HAVITAKUBALIWA.
viii.
ix.
Waombaji wawe na umri usiozidi miaka 45.
Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa
kama wanakibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
x.
Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika
utumishi wa umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika
Waraka Na CAC. 45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba, 2010.
xi.
Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kugushi wahusika watachukuliwa hatua za
kisheria.
xii. Mwisho wa kupokea barua za maombi ni tarehe 15 Aprili, 2014
xiii. Aidha, uwasilishaji wa barua kwa mkono katika ofisi za Sekretarieti ya Ajira
HAURUHUSIWI.
xiv.
Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na
kuidhinishwa na Mamlaka husika (TCU na NECTA).
xv.
Maombi yanaweza kuandikwa kwa Lugha ya Kiswahili au Kiingereza na yatumwe
kupitia posta kwa anuani ifuatayo;-
Katibu,
Sekretarieti ya Ajira katika
Utumishi wa Umma,
SLP.63100,
Dar es Salaam.
AU
2
Secretary,
Public Service Recruitment
Secretariat,
P.O.Box 63100
Dar es Salaam.
1.0 AFISA TAWALA DARAJA LA II (ADMINISTRATIVE OFFICER GRADE II) –
(NAFASI 1)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Afrika Mashariki.
1.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kusajili vizazi, vifo na ndoa na kutoa hati za viapo.
 Kuweka kumbukumbu za matukio muhimu,
 Kuwapokea na kuwahoji wakimbizi wanaowasili,
 Kuweka kumbukumbu za Wakimbizi
 Kutunza na kugawa vifaa vya wakimbizi katika makazi.
 Kuainisha, kuchambua na kushauri kuhusu matatizo ya wakimbizi.
 Kusimamia nidhamu ya wakimbizi.
 Kusimamia utekelezaji wa Sheria, Sera, Kanuni na Taratibu mbalimbali Serikalini
kutegemeana mahali alipo.
 Kusimamia kazi za utawala na uendeshaji katika ofisi za Serikali.
 Kutoa vitambulisho kwa wakimbizi.
1.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Shahada ya kwanza kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na
Serikali katika fani zifuatazo:- Utawala, Sheria (baada ya internship), na
Menejimenti ya Umma
 Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta
1.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
2.0 MCHUMI DARAJA LA II (ECONOMIST GRADE II) – (NAFASI 23)
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Afrika Mashariki, Katibu Mkuu Wizara
ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Katibu Mtendaji Ofisi ya Rais Tume ya
Mipango na Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia .
2.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kuhudumia kamati mbalimbali za Bunge (Kamati za mahesabu ya Serikali, Kamati
ya mahesabu ya mashirika ya Umma)
 Kukusanya takwimu na taarifa mbalimbali za kiuchumi kwa ajili ya uchambuzi na
uandaaji wa sera na mipango ya kiuchumi na kijamii
 Kufanya utafiti na uchambuzi wa sera na vigezo vya kiuchumi jumla
 Kufanya utafiti na kubainisha fursa zilizopo katika sekta husika
3


Kukusanya taarifa na takwimu zinazohitajika katika kubainisha vipaumbele vya
ustawi namaendeleo ya jamii.
Kutayarisha na kusambaza takwimu na taarifa za kiuchumi kwa wadau
2.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye shahada ya kwanza ambao wamejiimarisha (major) katika mojawapo ya
fani zifuatazo;
 Uchumi (Economics)
 Takwimu (Statistics )
 Sayansi ya Uchumi Kilimo (BSc Agriculture Economics & Agribusness) kutoka
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Sokoine au Chuo kingine
chochote kinachotambuliwa na Serikali na wenye ujuzi wa kutumia kompyuta
2.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
3.0 MCHUMI DARAJA LA II (ECONOMIST GRADE II) – (NAFASI 1)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha
3.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kuhudumia kamati mbalimbali za Bunge (Kamati za mahesabu ya Serikali, Kamati
ya mahesabu ya mashirika ya Umma)
 Kukusanya takwimu na taarifa mbalimbali za kiuchumi kwa ajili ya uchambuzi na
uandaaji wa sera na mipango ya kiuchumi na kijamii
 Kufanya utafiti na uchambuzi wa sera na vigezo vya kiuchumi jumla
 Kufanya utafiti na kubainisha fursa zilizopo katika sekta husika
 Kukusanya taarifa na takwimu zinazohitajika katika kubainisha vipaumbele vya
ustawi namaendeleo ya jamii.
 Kutayarisha na kusambaza takwimu na taarifa za kiuchumi kwa wadau
3.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye shahada ya Uzamili ambao wamejiimarisha (major) katika mojawapo ya
fani ya Uchumi (Economics) au Fedha (Finance) kutoka Chuo chochote
kinachotambuliwa na Serikali na wenye ujuzi wa kutumia kompyuta
4
3.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
4.0 AFISA MAENDELEO YA JAMII DARAJA II (COMMUNITY DEVELOPMENT
OFFICER GRADE II) – (NAFASI 2)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Afrika Mashariki na Katibu Mtendaji Ofisi
ya Rais Tume ya Mipango.
4.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kuandaa na kupendekeza mipango na mikakakati ya kubadili fikra za watu ili
waweze kuwa na mawazo ya maendeleo sawia na Sera za Serikali na wakati
uliopo
 Kupitia mbinu shirikishi kuwezesha jamii kuanzisha miradi ya kijamii kama vile:-
- Usafi wa mazingira
- Ujenzi wa nyumba bora
- Ujenzi wa shule
- Ujenzi wa zahanati
- Kuchimba au kuzifanyia matengenezo barabara hasa za vijijini
- Ujenzi wa majosho
- Uchimbaji wa visima vifupi
- Utengenezaji wa malambo
 Kuhamasisha matumizi endelevu ya mazingira
 Kusambaza na kuhamasisha matumizi ya teknolojia sahihi kama vile uvunaji wa
maji ya mvua, majiko sanifu, matumizi ya mikokoteni
 Kuhamasisha watu kutumia huduma za mafunzo ya Vyuo vya Maendeleo ya
Wananchi
 Kuwasadia wanachi vijijini kuandaa maandiko (Project Write ups) ya kuombea
fedha za kuendesha miradi yao
 Kuhamasisha, kuandaa na kutoa elimu kwa umma kuhusu uraia na Utawala bora
 Kukusanya, kutunza, kutafsiri na kusambaza takwimu na kumbukumbu muhimu
kwa ajili ya matumizi ya jamii
 Kuwezesha wananchi kupambana na mila zenye madhara kwa afya za wanchi
hasa wanawake na watoto wa kike, kuenea kwa virusi vya UKIMWI na magonjwa
ya mlipuko.
 Kuelimisha viongozi wa Serikali za Vijiji, Dini na Mashirika yasiyo ya Kiserikali
kuhusu Sera mbalimbali za Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na
kutumia Sera hizo
 Kutoa taarifa za hali ya jamii kwa ngazi mbalimbali
5
4.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa Shahada au Stashahada ya Juu ya Maendeleo ya Jamii
kutoka Vyuo vinavyotambuliwa na Serikali katika fani zifuatazo:-
 Maendeleo ya Jamii (Community Development)
 Elimu ya Jamii (Sociology)
 Masomo ya Maendeleo (Development Studies)
 Mipango na Usimamizi wa Miradi (Project Planning and Management)
 Maendeleo na Jinsia (Gender and Development)
4.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
5.0 AFISA HABARI II – (NAFASI 3)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Afrika Mashariki na Katibu Mtendaji Ofisi
ya Rais Tume ya Mipango.
5.1







MAJUKUMU YA KAZI
Kukusanya na kuandika habari.
Kupiga picha.
Kuandaa picha za maonyesho.
Kuandaa majarida na mabango (Posters).
Kukusanya takwimu mbalimbali.
Kuandaa majarida na vipeperushi.
Kuhifadhi picha na kuhudumia maktaba na marejeo.
5.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Awe na Shahada ya Kwanza au Stashahada ya Juu ya Uandishi wa Habari au sifa
inayolingana nayo kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali.
5.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
6.0 MKAGUZI HESABU WA NDANI II (INTERNAL AUDITOR II) – (NAFASI 3)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Afrika Mashariki na Katibu Mtendaji Ofisi
ya Rais Tume ya Mipango.
6.1 MAJUKUMU YA KAZI
6




Kufanya Ukaguzi wa hesabu katika Idara
Kusahihisha na kuidhinisha ripoti za ukaguzi
Kusahihisha na kuidhinisha hoja za Ukaguzi wa ndani
Kufanya kazi zingine atakazopangiwa.
6.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiri wahitimu wa kidato cha sita (VI) wenye cheti cha kati cha uhasibu
(intermediate stage) kinachotolewa na NBAA au sifa zinazolingana na hizo.
 AU
 Wenye shahada/Stashahada ya juu ya uhasibu kutoka vyuo vinavyotambuliwa na
serikali.
6.3 MSHAHARA
 Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
7.0 MHASIBU DARAJA LA II (ACCOUNTANT GRADE II) – (NAFASI 2)
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Afrika Mashariki na Katibu Mkuu Wizara
ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
7.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kuidhinisha hati za malipo.
 Kuandika taarifa ya mapato na matumizi ya mwezi.
 Kusimamia Wahasibu Wasaidizi katika kazi zao za kila siku.
 Kusimamia shughuli za uhasibu kwenye Kitengo cha Idara.
 Kuandika taarifa ya maduhuli.
7.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiri wahitimu wa kidato cha sita (VI) wenye cheti cha kati cha uhasibu
(intermediate stage) kinachotolewa na NBAA au sifa zinazolingana na hizo.
AU
 Wenye shahada/Stashahada ya juu ya uhasibu kutoka vyuo vinavyotambuliwa na
serikali.
7.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
8.0 MHIFADHI WANYAMAPORI DARAJA LA III – (NAFASI 100)
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii.
7
8.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufanya doria ndani na nje ya maeneo ya hifadhi
 Kudhibiti vitendo vya ujangili nje na ndani ya hifadhi
 Kusimamia shughuli za uwindaji wa kitalii na utalii wa picha
 Kulinda binadamu na mali zake dhidi ya Wanyamapori
 Kukusanya na kulinda Nyara za Serikali
 Kufanya usafi na ulinzi wa kambi
 Kusimamia uingiaji na utokaji wa watu na mali zao kwenye hifadhi
 Kukusanya na kutunza vielelezo vya ushahidi na kutoa ushahidi Mahakamani
 Kukagua wanyamapori kwenye mashamba na mazizi ya wanyamapori na
kukusanya takwimu zao
 Kusimamia taratibu za kusafirisha wanyamapori hai na nyara nje na ndani ya Nchi
 Kudhibiti wanyamapori waharibifu
 Kudhibiti moto kwenye hifadhi
 Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa zinazoendana na taaluma yake
8.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha IV au kidato cha VI wenye Astashahada ya
Uhifadhi Wanyamapori (Technician Certificate in Wildlife Management) kutoka
Chuo cha Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi au chuo kingine kinachotambuliwa
na Serikali.
8.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS B2 kwa mwezi.
9.0 MHIFADHI WANYAMAPORI DARAJA LA III – (NAFASI 327)
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii.
9.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kufanya doria ndani na nje ya maeneo ya hifadhi
 Kudhibiti vitendo vya ujangili nje na ndani ya hifadhi
 Kusimamia shughuli za uwindaji wa kitalii na utalii wa picha
 Kulinda binadamu na mali zake dhidi ya Wanyamapori
 Kukusanya na kulinda Nyara za Serikali
 Kufanya usafi na ulinzi wa kambi
 Kusimamia uingiaji na utokaji wa watu na mali zao kwenye hifadhi
 Kukusanya na kutunza vielelezo vya ushahidi na kutoa ushahidi Mahakamani
 Kukagua wanyamapori kwenye mashamba na mazizi ya wanyamapori na
kukusanya takwimu zao
8




Kusimamia taratibu za kusafirisha wanyamapori hai na nyara nje na ndani ya Nchi
Kudhibiti wanyamapori waharibifu
Kudhibiti moto kwenye hifadhi
Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa zinazoendana na taaluma yake
9.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha IV au kidato cha VI wenye Astashahada ya Awali
ya Uhifadhi wa Wanyamapori (Basic Technician Certificate in Wildlife
Management) kutoka Chuo cha Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi au chuo
kingine kinachotambuliwa na Serikali.
9.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS B1 kwa mwezi.
10.0 MHIFADHI WANYAMAPORI DARAJA LA II – (NAFASI 10)
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii.
10.1












MAJUKUMU YA KAZI
Kufanya doria ndani na nje ya maeneo ya hifadhi
Kudhibiti vitendo vya ujangili nje na ndani ya hifadhi
kusimamia uwindaji wa kitalii na utalii wa picha
kulinda Nyara za Serikali
Kusimamia usafirishaji wa wanyamapori na nyara nje na ndani ya Nchi
Kusimamia matumizi ya magari ya doria
Kukagua wanyamapori kwenye mashamba na mazizi ya wanyamapori na kutunza
takwimu zao
Kuratibu uingiaji wa wageni katika Mapori ya Akiba
Kudhibiti moto katika hifadhi
Kukusanya na kutunza vielelezo vya ushahidi na kutoa ushahidi Mahakamani
Kukusanya takwimu za wanyama na mimea kwenye hifadhi
Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa zinazoendana na taaluma yake
10.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha IV au kidato cha VI wenye Stashahada ya
Uhifadhi Wanyamapori (Diploma in Wildlife Management) kutoka Chuo cha
Usimamizi Wanyamapori Mweka au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.
10.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.
9
11.0 DEREVA DARAJA LA II (DRIVER II) – (NAFASI 2)
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mtendaji Ofisi ya Rais Tume ya Mipango.
11.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kuendesha magari ya abiria, magari madogo na malori
 Kuhakikisha gari na vyombo vyake vipo katika hali nzuri wakati wote, na kufanya
uchunguzi wa gari kabla na baada ya safari ili kugundua ubovu unaohitaji
matengenezo,
 Kufanya matengenezo madogo madogo katika gari,
 Kutunza na kuandika daftari la safari “Log-book” kwa safari zote.
11.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Cheti cha Mtihani wa Kidato cha IV, Wenye Leseni daraja la “C”
ya uendeshaji pamoja na uzoefu wa kuendesha magari kwa muda usiopungua
miaka mitatu bila kusababisha ajali na wenye Cheti cha Majaribio ya ufundi Daraja
la II (Trade test II).
11.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGOS.A kwa mwezi.
12.0 AFISA USAFIRISHAJI DARAJA LA II (TRANSPORT OFFICER GRADE II ) –
(NAFASI 1)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mtendaji Ofisi ya Rais Tume ya Mipango.
12.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kutayarisha gharama za uendeshaji wa usafiri kwa ajili ya kusaidia kutoa
maamuzi.
 Kuhakikisha kuwa takwimu na kumbukumbu zinazohusu vyombo vya usafiri
pamoja na mitandao yake zinatunzwa vyema na kwa usahihi. Kuandaa takwimu
zinazohusu maendeleo ya ukuaji wa sekta ya usafirishaji, na kuwasilisha kwa
watumiaji ndani na nje ya nchi.
 Kukusanya takwimu za usafirishaji nchini.
 Kukadiria na kushauri juu ya utendaji wa miradi mbalimnbali ya sekta ya
usafirishaji.
 Kutekeleza majukumu mengine yanayohusu sekta ya usafirishaji
12.2 SIFA ZA MWOMBAJI
 Kuajiriwa wenye Stashahada ya kawaida ya Usafirishaji kutoka Vyuo
vinavyotambuliwa na Serikali.
10
12.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi
13.0 AFISA MAZINGIRA DARAJA LA II – (NAFASI 1)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Katibu Mtendaji Ofisi ya Rais Tume ya Mipango.
13.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kukusanya Takwimu na Taarifa mbalimbali zinazohusu Usimamizi na Hifadhi ya
Mazingira.
 Kutoa (disseminate) elimu ya Hifadhi ya Mazingira kwa Wadau mbalimbali.
 Kushiriki katika kuandaa Mpango wa kazi na bajeti.
 Kushiriki katika tafiti zinazohusu Usimamizi na Hifadhi ya Mazingira.
 Kufuatilia utekelezaji wa Sera na Sheria zinazohusiana na Usimamizi wa
Mazingira.
 Kufuatilia na Kuainisha Maeneo yanayopaswa kuhifadhiwa.
 Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa kulingana na uwezo na taaluma yake.
13.2 SIFA ZA MWOMBAJI.
 Kuajiriwa wahitimu wenye Shahada ya kwanza ya Sayansi/Sanaa yenye
mwelekeo wa Usimamizi na Hifadhi ya Mazingira katika moja ya fani zifuatazo,
‘Geography and Environmental Studies, Aquatic Environmental Science and
Conservation, Environmental Science and Management, Environmental
Laboratory Science Technology, Environmental Planning and Management’ au
sifa zinazolingana na hizo kutoka Vyuo vinavyotambulika na Serikali.
13.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.
14.0 MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU (REGISTRY ASSISTANT) – (NAFASI 1)
Nafasi hii ni kwa ajili ya Mkurugenzi Mtendaji Mfuko wa Pembejeo za Kilimo na Mifugo.
14.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kusimamia usahihi (accuracy) wa kumbukumbu.
 Kugawa kazi na kusimamia kazi zote za masjala.
 Kuangalia barua zote zinazoingia, kutoka na kuweka kwenye majalada husika.
 Kutunza diary za (Bring up) na kuhakikisha zinafanyiwa kazi kwa wakati muafaka.
 Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa kulingana na uwezo na taaluma yake.
11
14.2 SIFA ZA MWOMBAJI.
 Kuajiriwa wahitimu wenye Stashahada ya Kumbukumbu (Diploma in Records
Management) kutoka Vyuo vinavyotambulika na Serikali.
 Awe na uzoefu wa miaka Sita (6) katika fani hii.
14.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Taasisi yaani GSS 5 kwa mwezi.
15.0 AFISA MTENDAJI WA KATA DARAJA LA II (WARD EXECUTIVE OFFICER
GRADE II) – (NAFASI 5)
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Halmashauri.
MAJUKUMU YA KAZI
 Atakuwa Mtendaji Mkuu wa Kata na kiungo cha Uongozi kwa Idara zote katika
kata na atashughulikia masuala yote ya kata
 Atakuwa Mhamasishaji mkuu wa Umma katika mikakati mbalimbal.i ya uzalishaji,
mali, kuondoa njaa na Umasikini.
 Atakuwa ni Katibu wa kamati ya maendeleo ya kata.
 Ataratibu na kusimamia upangaji wa shughuli za maendeleo ya kata, vijiji na Mtaa.
 Atatafsiri sera na kusimamia utekelezaji wa sheria ndogondogo katika Kata
yake.Atamsaidia Mkurugenzi Kuratibu na kusimamia shughuli za Uchaguzi katika
Kata.
 Kumsaidia na kumwakilisha Mkurugenzi katika kusimamia maendeleo ya eneo
lake.
 Kusimamia utendaji kazi wa wataalamu na watendaji wengine katikangazi ya Kata.
 Kuratibu na kuandaa taarifa za utekelezaji na kuziwasilisha kwa mkurugenzi na
nakala kwa Katibu Tarafa.
 Atakuwa mwenyekiti katika vikao vinavyowahusisha wataalamu na watendaji wa
vjiji, na NGO’S katika kata yake.
 Atakuwa Msimamizi na mratibu wa takwimu zote zinazokusanywa katika vijiji,
vitongoji, na kata yake.
15.1 SIFA ZA MWOMBAJI.
 Kuajiriwa wenye Shahada ya Sanaa yenye mwelekeo wa Sayansi ya Jamii (Social
Sciences) Utawala, (Public Administration and Local Gorvernment), Sheria au Sifa
nyingine inayolingana na hizo kutoka Chuo chochote kinachotambuliwa na
Serikali.
12
15.2 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS D. kwa mwezi.
X.M. DAUDI
Katibu
Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.
13
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger