Wednesday, 22 April 2026

RAIS SAMIA ASHIRIKI KONGAMANO LA KITAIFA LA MAMA NA BABA LISHE JNICC



Na mwandishi Maalum, Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan,ameshiriki kongamano la kitaifa la Babalishe na Mamalishe na kugua mabanda ya maonesho ya mapishi ya mama na baba lishe mara baada ya kuwasili katika Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), jijini Dar es Salaam, leo Aprili 21, 2026.

Rais Samia pia amepata fursa ya kutembelea mabanda mbalimbali yaliyoandaliwa na wajasiriamali hao, ambapo alijionea aina tofauti za vyakula vya asili na vya kisasa vinavyotayarishwa na mama lishe na baba lishe kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Akizungumza kwa ufupi na washiriki wa maonesho hayo, Rais Samia amewapongeza kwa ubunifu wao katika mapishi na mchango wao mkubwa katika kukuza ajira pamoja na uchumi wa taifa. Alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuboresha viwango vya usafi, ubora wa huduma na ubunifu ili kuvutia wateja zaidi na kuongeza thamani ya biashara zao.

Maonesho hayo ni sehemu ya kongamano linalowakutanisha mama lishe na baba lishe nchini, likiwa na lengo la kubadilishana uzoefu, kujifunza mbinu bora za biashara na kuimarisha sekta ya chakula ambayo imeendelea kuwa mhimili muhimu wa uchumi wa wananchi wa kipato cha chini na cha kati.

Ujio wa Rais Samia katika tukio hilo umeongeza hamasa kwa washiriki, wengi wao wakieleza kufurahishwa na kitendo hicho cha kutambua na kuthamini juhudi zao katika kujipatia kipato na kuchangia maendeleo ya taifa.




Share:

MASHAHIDI 553 WAMELETA USHAHIDI KWA KIAPO NA MAANDISHI, 1323 ANA KWA ANA - PROF. IBRAHIM JUMA














Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRILI 22,2026

Magazeti
 
Share:

Tuesday, 21 April 2026

UVCCM BUKOBA YATOA VIFAA VYA MICHEZO KUELEKEA MASHINDANO YA “BUKOBA CUP 2026”


Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi UVCCM Bukoba Bw. James MichaelNyamanza (kulia) akimkabidhi zawadi za washindi wa mashindano ya UVCCM BUKOBA CUP 2026 Katibu wa Chama cha Mpira Wilaya ya Bukoba Bw. Mwinyi Mohamed Mwinyi (kushoto) na katikati ni Katibu wa chama cha mpira Mkoa wa Kagera Bw. Ali Amini Abdul

**

Na Mbuke Shilagi Kagera. 

Mwenyekiti wa UVCCM Manispaa ya Bukoba, James Michael Nyamanza, amekabidhi jezi na mipira kwa wawakilishi wa Kata zote 14 za manispaa hiyo ikiwa ni maandalizi ya mashindano ya UVCCM Bukoba Cup 2026 yanayotarajiwa kuanza rasmi Ijumaa, tarehe 24 Aprili 2026.

Katika hafla hiyo, mwenyekiti huyo pia amekabidhi zawadi zitakazotolewa kwa washindi kwa Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Bukoba, akisisitiza kuwa lengo la mashindano hayo ni kuwakutanisha vijana, kujenga mahusiano, kuibua na kuendeleza vipaji pamoja na kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia michezo.

Ameeleza kuwa kupitia mashindano hayo, vijana watapata fursa ya kuonesha uwezo wao huku wakijenga nidhamu na mshikamano, mambo ambayo ni muhimu katika maendeleo ya jamii.

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Bukoba, Mwinyi Mohamed Mwinyi, amesisitiza umuhimu wa kufuata taratibu zote za michezo, akieleza kuwa shughuli yoyote ya michezo katika ngazi ya wilaya lazima ipitie kwa viongozi husika na kupata kibali kinachotolewa hadi ngazi ya Mkoa kwa kuzingatia kanuni na sheria za michezo.

Amefafanua kuwa mashindano hayo yataendeshwa kwa kuzingatia Sheria 17 za mpira wa miguu, huku kila Kata ikicheza mechi za nyumbani na ugenini, pamoja na kuzingatia mfumo wa bao la ugenini.

Naye Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Kagera, Ali Amin Abdul, amempongeza Mwenyekiti wa UVCCM Bukoba kwa kuanzisha mashindano hayo pamoja na kudhamini vifaa na zawadi kwa washindi. 

Huku akibainisha kuwa kuanzia hatua ya robo fainali na nusu fainali, mechi zitachezwa kwa dakika 90 na endapo sare itatokea, mshindi atapatikana kwa njia ya mikwaju ya penalti, huku fainali ikichezwa kwa dakika 90 pamoja na dakika 30 za nyongeza kabla ya penalti iwapo sare itaendelea.

Ikumbukwe kuwa, mashindano ya UVCCM Bukoba Cup 2026 yanatarajiwa kuanza rasmi Ijumaa, tarehe 24 Aprili 2026, ambapo mchezo wa ufunguzi utazikutanisha timu za Kashai na Bilele katika Uwanja wa Kaitaba stadium.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger