Wednesday, 29 October 2025

WANANCHI WAJITOKEZA KWA UTULIVU KUPIGA KURA BUYUNI, DAR ES SALAAM

...




Na Mwandishi wetu, Dar

Zoezi la kupiga kura linaendelea kwa utulivu katika kituo cha Buyuni, kilichopo Changanyikeni, Wilaya ya Ubungo, jijini Dar es Salaam, likianza mapema saa 1.00 asubuhi. Wananchi wameendelea kujitokeza kwa utaratibu kutekeleza haki yao ya kikatiba katika mazingira ya amani na usalama.

Maafisa wa tume ya uchaguzi wanaendelea kusimamia mchakato huo kwa weledi, wakitoa huduma kwa wapiga kura kwa namna inayoonesha maandalizi mazuri ya uchaguzi huu.

Wananchi wametakiwa kuendelea kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa amani, wakizingatia maelekezo yanayotolewa na wasimamizi wa vituo, ili zoezi hilo muhimu kwa demokrasia ya nchi liwe na mafanikio makubwa.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger