Saturday, 28 June 2025

FRED ROMANUS AJITOSA KUWANIA UBUNGE JIMBO JIPYA LA ITWANGI

...

Kijana na mwanazuoni Fred Romanus kutoka Kijiji cha Mendo, Kata ya Ilola, ametangaza nia ya kugombea Ubunge katika Jimbo jipya la Itwangi, mkoani Shinyanga.

Fred Romanus amesema amekuwa na ndoto ya muda mrefu ya kuwatumikia wananchi kupitia nafasi ya Ubunge, akilenga kuwaletea maendeleo jumuishi na endelevu kwa makundi yote katika jamii.

“Ndoto yangu ni kuona kila mwananchi ananufaika na matunda ya uongozi bora. Naamini kupitia nafasi hii ya Ubunge, nitaweza kusukuma gurudumu la maendeleo kwa vitendo,” amesema Fred Romanus.

Kwa sasa, amesema sera na mikakati yake ya maendeleo itawasilishwa kwa wananchi katika siku zijazo wakati wa kampeni rasmi endapo chama kitampa ridhaa ya kugombea Ubunge.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger