Saturday 28 October 2023

MAPEPELE AWAONGOZA WANAHABARI KUTEMBELEA MIRADI YA REGROW, HIFADHI YA NYERERE.


Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. John Mapepele, leo amewaongoza wanahabari kutembelea miradi inayofanywa na Mradi wa Kuboresha Usimamizi wa Maliasili na Kukuza Utalii Nyanda za Juu Kusini (REGROW) katika Hifadhi ya Taifa Nyerere.

Akiwa hapo Bw. Mapepele amepongeza kazi nzuri inayofanywa na REGROW ndani ya Hifadhi ya Taifa Nyerere, huku akitoa wito kwa vyombo vya habari nchini kuiunga mkono Serikali kwa kutangaza vivutio vya Utalii vilivyopo nchini.

Wanahabari hao wamejionea kasi ya ujenzi wa Kambi ya Askari wa Uhifadhi, Mtemere, geti la kuingilia na kutokea Hifadhini Kwa upande wa Wilaya ya Rufiji, Kambi ya kulala Watali/ public campsite, Nyumba za kulala Watalii na ujenzi wa Kiwanja cha ndege cha Mtemere.

Aidha, Mapepele amesema dhamira ya Serikali kwa sasa kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii ni kufungua hazina kubwa ya utalii wa Tanzania ulio katika ukanda wa kusini kwa kutumia mradi huo.

" Tanzania imebarikiwa kuwa na hazina kubwa wa Utalii katika maeneo takribani yote nchini, kazi inayofanywa Sasa ni kuboresha miundombinu ili wageni waweze kufika kirahisi kwa kuwa kwa upande wa kaskazini wageni tayari ni wengi hivyo ni muhimu pia kugeukia upande wa kusimi amefafanua Mapepele

Amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa maono yake na kazi kubwa aliyofanya ya kuutangaza Utalii duniani kwa mafanikio makubwa kupitia filamu ya The Royal Tour.

Amesema kwa sasa Tanzania inapokea mafuriko ya wageni kutoka sehemu mbalimbali duniani na kuliingizia taifa mapato makubwa kupitia sekta hiyo ambapo ametoa wito kwa vyombo vya habari nchini kusaidia kuutangaza utalii.

Ameongeza kuwa vyombo vya habari vina mchango mkubwa wa kuutangaza vivutio vya Utalii.
Share:

Friday 27 October 2023

RC SIMIYU ATEMBELEA VIKUNDI VYA WAJASIRIAMALI 'VIJANA WAPAMBANAJI' BARIADI,...... AHIMIZA MAREJESHO KWA WAKATI KUJENGA UAMINIFU




Bariadi,

Vijana wajasiriamali  Mkoani Simiyu wamehimizwa  kufanya  marejesho ya mikopo inayotolewa na Serikali kwa wakati ili kujenga uaminifu jambo litakalowawezesha kuaminika na kukopeshwa fedha nyingi zaidi jambo  litakayosaidia kukuza mitaji yao na hivyo kujikwamua na umaskini.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Dkt Yahaya Nawanda alipotembelea kikundi Cha Vijana Wajasiriamali almaarufu "Vijana wapambanaji" kilichopo eneo la Stendi kuu ya Mabasi Somanda Wilayani Bariadi wanaojihusisha na shughuli za uchapaji mabango kwa lengo la kutatua Kero zao.

"Kwa uzoefu nilionao nikiwa DC  kwa miaka zaidi ya saba ni kuwa  vikundi vingi vya Vijana vina changamoto ya kutofanya marejesho kwa wakati tofauti na vikundi vya walemavu na wakina mama."Alisema mkuu wa Mkoa Dkt Nawanda. 

Aidha Mkuu wa Mkoa Dkt Nawanda amewapongeza Vijana wapambanaji kwa kuwa mfano mzuri katika kufanya marejesho ya mikopo waliyowezeshwa na Serikali kwa wakati na kuwataka Vijana wengine kuiga mfano.

Kikundi cha Wajasiriamali cha vijana wapambanaji ni moja kati ya Vikundi vya Wajasiriamali Wilayani Bariadi  vilivyonufaika na Mkopo wa Asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya kuwawezesha Vijana,akina Mama na wenye ulemavu.

www.simiyu.go.tz



Share:

RC TANGA- ACHENI KUTUMIA MIFUMO YA KIZAMANI KUHIFADHI FEDHA ZENU


Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungusha mfano wa kadi ya NMB leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata –Halipoi uzinduzi uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir


Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Waziri Kindamba akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabara –Halipoi iliyofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Mjini Tanga kulia ni Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus,


Mkuu wa Idara ya Kadi ya Benki ya NMB Philbert Casmir akizungumzia wakati akielezea kampeni ya Mastabata –Halipoi leo kwenye viwanja vya Mkwakwani Mjini Tanga wakati wa uzinduzi wake kulia Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus

Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Mastabata –Halipoi leo kwenye viwanja vya Mkwakwani Mjini Tanga


Watumishi wa Benki ya NMB Mkoa wa Tanga wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Mastabata –Halipoi leo kwenye viwanja vya Mkwakwani Mjini Tanga.


Na Oscar Assenga,TANGA.

WANANCHI wa Mkoa wa Tanga wametakiwa kuacha kutumia mifumo ya kizamani ikiwemo ya kutembea na fedha mifukoni badala yake watumie mifumo ya kibenki ya Master Card Qr kwani ndio njia salama na ya uhakika wa kuhifadhi fedha zao

Hatua hiyo inaeleza kwambaa itakuwa ni salama kwani itawaepusha wananchi hao na changamoto mbalimbali ambazo wanaweza kukutana nazo ikiwemo wizi

Wito huo ulitolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Mastabata-Halipoi inayoendeshwa na Benki ya NMB kwenye Halfa iliyofanyika kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mjini Tanga.

Ambapo alisema wakitumia mifumo ya kibenki ya Master Card QR itawawezesha kuwa na usalama wa fedha zao ikiwemo kutokuchakaa haraka.

Alisema kwamba wananchi wakiwa na mwamko wa kufanya hivyo itawaepusha na kuharibika kwa fedha lakini pia kama nchi itasaidia kuondokana na kuingia gharama na ndio maana wanasistiza umuhimu wa kadi.

“Ndugu zangu leo tupo hapa kwenye uzinduzi wa kampeni hii ya Mastabata –Haipoi niwaambie huu ni mfumo salama na makini hivyo niwaase wana Tanga na watanzania tuuchangamkie”Alisema

Aidha aliwaeleza wakazi wa mkoa huo kutumia njia mbadala kwa ajili ya kufanya malipo kuna kuwa na faida nyingi hivyo niwapongeze benki ya NMB kwa kuja na ubunifu huu.
Hata hivyo aliwataka wananchi wa mkoa huo kuacha kutumia mifumo ya kizamani kutembea na fedha mfukoni ili kuepukana na changamoto mbalimbali ambazo wanaweza kukumbana nazo ikiwemo wizi.

Alisema kwa sababu unapotumia kadi kwa kufanya malipo Benki ya NMB haikuachi hivihivi bali inakupa na zawadi mbalimbali hivyo wananchi changamkieni fursa hiyo muhimu.

Awali akizungumza katika uzinduzi huo,Mkuu wa Idara ya Kadi wa Benki ya NMB Philbert Casmir alisema kampeni hiyo ni kusisitiza matumizi ya kadi wanaoita mastabata haipoi.

Alisema ili kurudisha faida ya benki ya NMB kwa jamii kila mwaka mwishoni wanafanya kampeni hiyo kwa kushirikiana na wadau wao wa mastakadi kwa kufanya kampeni kubwa kutoa zawadi kemukemu.

Aidha alisema utoaji wa zawadi hizo unakwenda sambamba na kuhamasisha wateja wao kuachana na matumizi ya pesa taslimu badala yake watumie kadi kufanya miamala,manunuzi.

Alisema pia watumie simu zao kufanya manunuzi ambapo kampeni hiyo leo wameizinduliwa Tanga na ilianza mwaka 2018 na 2022 waliita mastabata kivyakovyako na leo wanaita mastabata haipo.

Philbert alisema kwamba kupitia kampeni hiyo benki ya NMB inaendelea kuhamasisha malipo ya njia kidigitali na kuachana na pesa taslimu kupitia hiyo watakuwa na droo ya kila wiki,mwezi na hatimaye fainali droo sasa hapa mnisikilize kwa umakin.

Hata hivyo alisema kwamba benki ya NMB wakishirikiana wenzao wa mastakadi wameandaa milioni 350 zawadi ambazo zitakuwa zikishindaniwa na wateja wao huku akieleza vigezo kwanza zawadi za kila wiki.

Ambapo alisema watakuwa na washindi 100,kila mmoja atashinda pesa taslimu 100,000 lakini watafanya zoezi akikuta mtu afanaya manujnuzi kwa kutuimia kadi palepele anapewa 50,000.
Share:

SHERIA YA LOCAL CONTENT INAVYONUFAISHA WAWEKEZAJI WAZAWA GGML


Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Terry Strong (kushoto) na Makamu Rais wa AngloGold Ashanti- GGML anayeshughulikia miradi endelevu Ghana na Tanzania, Simon Shayo (kulia) wakipokea zawadi kutoka kwa mmoja wa wafanyakazi wa Blue Coast.
Mabasi ya kampuni ya Blue Coast yanayotumika kusafirisha wafanyakazi na wakandarasi wa GGML.
Mmiliki wa kampuni AKO Group, Silvestry Koka akizungumza katika kongamano la wachimbaji madini mkoani Geita.
Mmoja wa wafanyakazi wa AKO Group akimhudumia mmoja wa wateja waliofika katika banda la kampuni hiyo kwenye maonesho ya teknolojia ya madini Geita.


NA MWANDISHI WETU
Miaka mitano baada ya kuanza kutekelezwa kwa Sheria ya Uwezeshaji Wazawa (Local Content) mafanikio yameanza kuonekana kuwa lulu kwa Watanzania huku fursa za ajira zikizidi kufunguliwa.

Sheria hiyo ya mwaka 2018 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2019 inalenga kutoa fursa kwa Watanzania kushiriki kikamilifu katika uchumi wa madini.

Mafanikio hayo yameelezwa katika Maonesho ya Sita ya Teknolojia ya Madini Geita wakati wa kongamano la wadau wa sekta ya madini kujadili fursa za uwekezaji kupitia sheria hiyo lililofanyika katika Maonesho ya Sita ya Kimataifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika kuanzia Septemba 20 hadi Oktoba 1, 2023 katika viwanja vya EPZA Bombambili mkoani Geita.

Kamishna wa ‘Local Content’, Janeth Lukeshingo anasema ajira zimeongezeka, manunuzi ya bidhaa na huduma kwa Watanzania, ushirikishwaji na uhaulishaji wa teknolojia na utafiti, maendeleo na kuongezeka kwa uelewa kuhusu ushirikishwaji wa Watanzania katika seta ya madini.
Mratibu wa Local Content katika Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) Riwald Tenga, anasema wanatekeleza sheria hiyo kwa asilimia 90.

“Tunafuata masharti yote katika manunuzi na katika utoaji ajira, yote tunayofanya kwenye Local Content tuko kati ya asilimia 60 mpaka 90,” anasema Tenga.

AngloGold Ashanti ambayo ni kampuni mama ya GGML, hivi karibu ilitoa kandarasi ya usafirishaji wa mafuta, yenye thamani ya takriban Sh bilioni 25 kwa mwaka kwa wakandarasi wawili wa Tanzania.
Miongoni mwa makampuni ya ndani yaliyonufaika ni pamoja na Blue Coast Investment Limited, kampuni ya Geita inayojishughulisha na usafiri na usafirishaji.

WAWEKEZAJI WAZAWA

Mkurugenzi Mtendaji wa Blue Coast, Ndahilo Athanas anasema wameanza kufanya biashara na GGML tangu mwaka 2021.

“Tunaishukuru Serikali kwa kuona umuhimu wa sheria hii na kuipitisha, lakini tunamshukuru zaidi Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kusimamia utekelezaji wa sheria hii.

“GGML wana mchango mkubwa wa kutufikisha hapa tulipo, wamekuwa chachu ya sisi kufikia viwango vya ubora. Wametupatia elimu ya kutosha juu ya umuhimu wa ubora na namna ya kuendelea kufanya biashara endelevu,” anasema Athanas.

Anasema wanaendesha shughuli zao kupitia viwango vya kitaifa na kimataifa ambapo wana cheti cha usalama kazini, cheti cha ubora wa kazi na sasa wanaendelea na usajili wa ubora katika usimamizi wa mazingira.

Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, kampuni hiyo imeajiri zaidi ya wafanyakazi 400 kwenye ajira rasmi na zisizo rasmi kwa wakazi wa Geita na maeneo mengine yanayozunguka mkoa huo na kufanya idadi kufikia 580 kutoka 220 wa mwaka 2021.

Aidha, anasema wamejikita kutoa elimu kazini ili kuwajengea uwezo vijana kabla ya kuwapa ajira rasmi hasa wahitimu wa vyuo vikuu.

“Mpaka sasa vijana 50 wameajiriwa kupitia utaratibu huu katika nyanja mbalimbali kama uhasibu, maofisa ugavi, mafundi magari, maofisa uendeshaji na nyingine,” anasema.

Mkurugenzi huyo anasema pia wamepata tuzo ya mlipakodi bora kwa Mkoa wa Geita na kwamba kupitia fursa ya Local Content kampuni hiyo imekua na sasa imehamishiwa kwenye kundi la walipakodi wakubwa.

AKO

Ako ni kampuni iliyoanzishwa kutoa huduma ya chakula. Ni moja ya kampuni ya wazawa ambayo ilianza mahusiano GGML mwaka 2010.

Mmiliki wa kampuni hiyo, Silvestry Koka anasema walianza kwa kutoa huduma za chakula kwa GGML ambapo wakati huo walikuwa wanachukua bidhaa za kupika na mahitaji mengine kutoka Dar es salaam.

“Lakini wakati huo tulikuwa tunaendelea kuwajengea uwezo wananchi wanaozunguka maeneo yote yanayokaliwa na mgodi,” anasema.

Anasema sasa AKO inajivunia kwa kuwapa mnyororo wa uchumi wananchi wanaozunguka eneo la mgodi.
Kwamba wamewasaidia kuwa soko kubwa la bidhaa zao za mbogamboga, matunda na bidhaa zingine pia.

“Kwahiyo tumekuwa tukinunua kwa asilimia kubwa, japo kuna bidhaa tunazitoa nje ya hapa Geita. Lakini lengo letu tufikie hatua bidhaa zote kwa asilimia 100 zitoke katika maeneo yanayozunguka mgodi.

“Tunatumia nyama, mchele, matunda na mbogamboga, kwa mfano kuna kikundi kinaitwa NYAKABALE Commercial group ambacho wao wanatusambazia nyama, matunda pamoja na mbogamboga lakini pia tunaye mzabuni wetu anaitwa Masuka, MASUKA ambaye amekuwa ana supply mchele kwetu kwa zaidi ya miaka nane mpaka sasa,” anasema.

Aidha, Koka anatoa wito kwa watoa huduma wazawa kufanya kazi kwa kusimamia kampuni zao na kuzipa Zaidi uwezo poamoja na kuzingatiwa viwango.

Anasema kinachoangusha kampuni nyingi za wazawa ni kuangushana wao wenyewe kwa wenyewe jambo ambalo si afya kwa uchumi wa Taifa.

DHANA YA LOCAL CONTENT

Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula, anasema dhana ya Local Content ilikuwa mpya wakati tume hiyo inaanzishwa lakini hivi sasa imeanza kueleweka.

“Watu waliturushia matusi kuhusu Local Content lakini kwa sababu kuna watu walikuwa hawajaielewa lakini tumefikia mahali ambapo panastahili,” anasema Profesa Kikula.

Mbunge wa Geita Mjini, Costantine Kanyasu, amesema baada ya marekebisho ya sheria hiyo wameanza kuona manufaa na kuipongeza Serikali kwa kuisimamia.

“Baada ya kuanza kutekelezwa kwa Local Content hasira ya wananchi imepungua, wengi wanashiriki, wanajishughulisha na uuzaji na usambazaji wa bidhaa wenye migodi mbalimbali,” anasema Kanyasu.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela anashauri uzoefu uliopatikana katika sekta ya madini uendelezwe katika sekta nyingine.

“Tukifanya hivi itatusaidia kuendeleza ujuzi na uelewa kwa Watanzania ili wengi zaidi washiriki katika sekta nyingine,” anasema Shigela.

Waziri wa Madini, Anthony Mavunde ambaye alikuwa mgeni rasmi katika kongamano hilo anasema ndani ya muda mfupi ushiriki wa Watanzania umeongezeka katika sekta ya madini.

“Tumejifunza kuna mambo lazima twende tukayafanyie kazi kwa haraka, Local Content inagusa maisha na uchumi wa Watanzania.

“Profesa Kikula moja ya alama ambayo utaiacha tena katika mioyo ya Watanzania na hasa wadau wa sekta ya madini ni namna ulivyosimamia Sheria ya Local Content…matokeo tumeanza kuyaona,” anasema Mavunde.

Share:

MAKONDA, RABIA ‘WARIPOTI’ KWA CHONGOLO, AWAPATIA RUNGU KUANZA KAZI


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Komredi Daniel Godfrey Chongolo amesema CCM iko salama na imara katika kusimamia misingi, shabaha na malengo yake, ikiwemo kuendelea kuwa daraja la kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi.

Amesema kuwa hali hiyo inatokana na jinsi ambavyo CCM kinaendelea kuwatumikia wananchi kwa kuzisimamia Serikali zote mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya Rais Dokta Samia Suluhu Hassan na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, chini ya Rais Dokta Hussein Ali Mwinyi, ambazo zimeendelea kutafsiri maelekezo ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025, kwa vitendo.

Ndugu Chongolo amesema hayo Alhamis, Oktoba 26, 2023, alipokutana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi, Ndugu Paul Christian Makonda na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Ndugu Rabia Abdallah Hamid, walipofika ofisini kwake, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba, jijini Dar Es Salaam, kwa ajili ya kuonana naye, kujitambulisha na kuanza kazi, baada ya kukabidhiwa ofisi zao rasmi na watangulizi wao.

Ndugu Chongolo aliwaelekeza Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi Ndugu Paul Makonda na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Rabia Abdallah Hamid, kuanza majukumu yao, wakitambua imani kubwa waliyopewa na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, chini ya Mwenyekiti wa CCM, Ndugu Dokta Samia Suluhu Hassan, kutumikia Chama kupitia nafasi hizo walizoteuliwa.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Chongolo amesema kuwa nafasi hizo mbili, Idara ya Itikadi na Uenezi na Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, ni mojawapo ya maeneo ya kimkakati ya CCM, hivyo wanapaswa kujua kuteuliwa kwao ni sehemu ya kuongeza chachu na kasi ya idara hizo kutekeleza malengo yaliyokusudiwa na CCM, katika kutumikia wananchi na kuzisimamia Serikali zote mbili za CCM.

“Karibuni sana. Hongereni sana kwa kuaminiwa na kuteuliwa. Ujio wenu utakuwa sehemu ya kuongeza kasi ya yale ambayo Chama tumekusudia. Uenezi na siasa ndiyo kila kitu. Mmeaminiwa na kuteuliwa kushika maeneo muhimu.

“Siasa (na Uhusiano wa Kimataifa) ni mojawapo ya core activities za Chama chetu. Kwa upande wa Itikadi na Uenezi ni core activity ya siasa yetu na imani ya Chama chetu. Hatuna mashaka na ninyi. Tunatarajia mtafanya makubwa kufikia malengo. Tuna maandalizi ya uchaguzi hapa, 2024 na 2025 (Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu). Tuko kwenye reli…tuko kwenye track sahihi. Karibuni sana.”

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Chongolo, pia alitumia nafasi hiyo kuwatakia kila la heri katika majukumu yao na kuwaelekeza kuwa, baada ya kukabidhiwa ofisi zao na majukumu yao rasmi na watangulizi wao, waanze kazi mara moja, kwa kuwa hakuna muda wa kusubiria.

“Najua watu wetu wa Dar Es Salaam wamewaandalia mapokezi. Nawatakia mapokezi mema na kila la heri mnapoenda kuanza majukumu yenu rasmi. Na Gavu (Mkuu wa Idara ya Oganaizesheni, Issa Haji Usi Gavu) atawasindikiza,” amesema Katibu Mkuu Chongolo.

Ndugu Makonda na Ndugu Hamid, waliteuliwa kushika nafasi hizo, hivi karibuni na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), iliyoketi katika kikao chake maalum chini ya Mwenyekiti wa CCM, Ndugu Dokta Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Oktoba 22, 2023, jijini Dodoma.

Ndugu Paul Makonda aliteuliwa kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi, akichukua nafasi ya Ndugu Sophia Edward Mjema aliyeteuliwa kuwa Mshauri Ofisi ya Rais, Masuala ya Wanawake na Makundi Maalum, ambapo Ndugu Rabia Abdallah Hamid aliteuliwa kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), akichukua nafasi ya Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Share:

Thursday 26 October 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 27,2023

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger