Sunday 28 May 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MEI 28,2023



















Share:

Saturday 27 May 2023

TANZANIA YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA UGAIDI,UTAKATISHAJI FEDHA HARAMU




Katika kupambana na vitendo vya ugaidi na utakatishaji fedha haramu, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Katiba na Sheria imezindua mwongozo wa ushirikiano wa wadau katika upelelezi, uratibu na kupambana na makosa hayo.

Akizungumza mara baada ya uzinduzia wa mwongozo huo uliofanyika Jijini Dodoma, Waziri wa Katiba na Sheria amesema kuwa mwongozo huo utasaidia kuleta pamoja wadau wanaopambana na makosa hayo na hivyo kukomesha uhalifu huo.

“Kila mmoja amekuwa akifanya kivyake vyake, lakini kwa mwongozo huu unawaleta pamoja wadau wote ili juhudi zao za kudhibiti makosa haya matatu ya utakatishaji wa fedha, ufadhili wa ugaidi na ugaidi wenyewe uweze kufanyika kwa pamoja maana tunafahamu umoja ni nguvu,” amesema Waziri Ndumbaro.

Dk. Ndumbaro ameongeza pia kuwa mwongozo huo hautaunganisha wadau wa ndani ya nchi pekee bali pia unatoa mwongozo wa namna ya kushirikiana na nchi nyingine Duniani kukabiliana na makosa hayo.

“Mtu anaweza akafanya uhalifu wa ugaidi au utakatishaji fedha akajipatia fedha na kuwekeza kwenye nchi nyingine,” amesema Waziri Ndumbaro huku akitoa wito kwa jamii kuwafichua wanaoshiriki vitendo hivyo katika jamii.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini, Sylvester Mwakitalu amesema mwongozo huo ni muhimu na utasaidia taasisi za uchunguzi kukusanya taarifa za uhalifu kwa kushirkiana na kuwasaidia kuendesha mashtaka ya makosa hayo.

Uzinduzi huo pia ulihudhuriwa na Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupamba na Dawa za Kulevya (DCEA), Aretas Lyimo,Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi, Camillus Wambura, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), CP. Salum Hamduni na wadau wengine kutoka ndani na nje ya nchi.
Share:

RUWASA SHINYANGA YAENDESHA MKUTANO WA WADAU WA MAJI, DC SAMIZI AZINDUA KAMATI ZA MALALAMIKO


Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi akizungumza wakati wa mkutano wa wadau wa maji wilayani Shinyanga.

Na Mwandishi wetu - Shinyanga
Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini RUWASA wilaya ya Shinyanga wameendesha mkutano mkuu wa nusu mwaka wa wadau wa maji ulioambatana na uundaji wa kamati za malalamiko.

Mkutano huo umefanyika leo Mei 26, 2023 kwenye ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.


Mkutano huo uliowakutanisha wadau wa maji kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ikiwemo uwasilishaji wa takwimu za CDMT na taarifa za fedha, usimamizi wa fedha na upangaji bei, ubora wa maji na utiaji dawa ya Chlorine, usajili wa CBWSO na utaratibu wa kutatua malalamiko katika wilaya pamoja na majadiliano.


Akitoa taarifa ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini RUWASA wilaya ya Shinyanga meneja wa RUWASA wilayani humo Mhandisi Emael Nkopi amesema miongoni mwa majukumu makubwa ya RUWASA ni kupanga, kusanifu, kujenga miundombinu ya maji, kusimamia na kufanya matengenezo kwa kushirikiana na vyombo ya watumia maji ambapo kwa sasa hali ya upatikanaji wa maji kwenye wilaya ya Shinyanga sawa na asilimia 72.3.


“Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa sasa imefikia takribani watu 338,962 kati ya watu 468,611 sawa na asilimia 72.3 ya watu wote waishio vijijini idadi hii ya watu ni kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 na hii imechangiwa na uwepo wa miundo mbinu ya maji ya bomba pamoja na visima vinavyutumia pampu ya mikono kwenye maeneo ambayo bado haijafikiwa na miundombinu ya bomba”, amesema Mhandisi Nkopi.


Awali akifungua mkutano huo Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Ngassa Mboji amewapongeza Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini RUWASA wilaya ya Shinyanga kwa kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi wa vijijini kwani kwa sasa hali ya upatikanaji wa huduma ya maji vijijini imezidi kuimarika.


Akizindua kamati za malalamiko mkuu wa wilaya ya Shinyanga Johari Samizi amesema serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo kwa lengo la kuhakikisha wananchi waishio maeneo ya vijijini wanafikiwa na huduma hiyo ya maji na kuwataka viongozi kushirikiana kwa pamoja katika kufanikisha miradi ya maendeleo.


“Kwanza niwapongeze RUWASA wilaya ya Shinyanga kwa kuona umuhimu wa kuandaa mkutano huu wa kukutana na wadau wa maji ili kujadili mustakabali wa maendeleo ya huduma ya maji vijijini, nitumie fursa hii kuwasihi viongozi wote katika maeneo yetu kushirikiana kwa pamoja na si kukwamisha shughuri za kimaendeleo”,amesema.


“Ni matarajio yetu ifikapo 2025 vijiji vyote vitakuwa vimefikiwa na maji, niwaelekeze kila mmoja kwa nafasi zenu kwenda kutekeleza yale yote ambayo tumekumbushwa kupitia mkutano huu ili yaweze kuleta tija ya utekelezaji wa huduma ya maji vijijini”, ameongeza Dc Johari Samizi.
Mhandisi Emael Nkopi Meneja wa RUWASA akisoma taarifa ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini RUWASA wilaya ya Shinyanga
Ngassa Mboje Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga akifungua mkutano wa wadau wa maji.
Joseph Buyugu Diwani wa Kata ya Salawe akichangia wakati wa mkutano wa wadau wa maji.
Mhandisi Clement Bundala akitoa taarifa ya Hali ya Bwawa la Maji.
Mhandisi Charles Chambila kutoka LifeWater International akizungumza wakati wa mkutano wa wadau wa maji wilaya ya Shinyanga.
John Singolile akitoa taarifa ya uendeshaji na matengenezo (OPM) wakati wa mkutano wa wadau wa maji wilaya ya Shinyanga.

Baadhi ya madiwani wakati wa mkutano wa wadau wa maji wilaya ya Shinyanga.
Julieth Payovela Meneja wa RUWASA Mkoa wa Shinyanga akizungumza wakati wa mkutano na wadau wa maji.
Wadau wa maji wilayani Shinyanga wakati wa mkutano.
Wadau wa maji wakisikiliza wakati wa mkutano wa wadau wa maji wilaya ya Shinyanga..
Wadau wa maji wilayani Shinyanga wakati wa mkutano.
Baadhi ya madiwani wakati wa mkutano wa wadau wa maji wilaya ya Shinyanga.
Baadhi ya madiwani wakati wa mkutano wa wadau wa maji wilaya ya Shinyanga.
Baadhi ya madiwani wakati wa mkutano wa wadau wa maji wilaya ya Shinyanga.
Share:

KLABU ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA MSALALA ZARUDISHA SHULE WANAFUNZI WALIOACHA SHULE NA KUKIMBILIA MACHIMBONI.



Jackson Malangalila mwezeshaji katoka Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) akizungumza na Musa Juma mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya Msingi Shilela
Mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya Sekondari Nyikoboko Jackson Amosi ambaye aliacha shule na kurejea tena baada ya kushawishiwa na klabu ya kupinga ukatili akizungumza kwenye mdahalo wa kupinga ukatili uliondaliwa na mtandoa wa jinsia Tanzania (TGNP)
Juma Mohammed kiongozi wa Klabu ya kupinga ukatili Nyikoboko sekondari ambaye pia ni Mwanafunzi wa kidato cha nne akichangia mada kwenye mdahalo wa kupinga ukatili uliandaliwa na mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP)
Mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya sekondari Nyikoboko Kurumna Nicholaus ambaye aliacha shule na kwenda Machimboni akungumza kwenye mdahalo wa kupinga ukatili wa kijinsia ulioandaliwa na mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP)
Joseph Samweli katibu wa kituo cha taarifa na maarifa cha kata ya Shilela akizungumza na wanafunzi katika mdahalo ulioandaliwa na mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP)
Mwezeshaji kutoka Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) Jackson Malangalila akizungumza na wanafunzi wa Shule Msingi Shilela na Sekondari ya Nyikoboko kuhusiana na masuala ya ukatili

Na Salvatory Ntandu - Msalala

Wanafunzi wawili katika Shule ya Sekondari Nyikoboko Halmashauri ya Msalala mkoani Shinyanga waliokuwa wamesitisha masomo kwa sababu mbalimbali na kisha kukimbilia Machimboni hatimaye wamerejea shuleni baada ya kupatiwa ushauri juu ya faida za elimu na klabu ya kupinga ukatili wa kijinsia.

Hayo yamebainishwa jana na Juma Mohamed Mwanafunzi wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Nyikoboko ambaye ni kiongozi wa Klabu hiyo,wakati akitoa ushuhuda kwenye Mdahalo wa kupinga ukatili wa Kijinsia uliondaliwa na Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) katika viwanja vya shule ya Msingi Shilela.

Amesema kuwa walifanikiwa kuwarejesha shule kwa kuwashawishi wanafunzi wenzao ambao walikuwa wamesitisha masomo kwa kipindi ncha miezi minne na kukimbilia Machimboni kutokana na elimu waliyoipata kupitia Midahalo mbalimbali iliwawezesha kujitambua na kujua haki zao.

Wanafunzi hao ni pamoja na Jackson Amosi (19) na Kurumna Nicholaus (18) wawili hao wakiwa ni wanafunzi wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Nyikoboko ambao waliacha masomo kwa sababu mbalimbali ikiwemo mwamko mdogo wa elimu wa wazazi ambao wengi wao ni wakulima na wafugaji.

“Klabu yetu baada ya kuundwa tuliweka maazimio ya kuhakikisha tunawarejesha wanafunzi walioacha shule na kuwenda kwenye shughuli za uchumbaji wa madini ya dhahabu katika mgodi mdogo wa Madini ya dhahabu wa Nyamishiga ,tulizungumza nao na kisha wazazi wao na kisha wakakubali rudisha shule ,”amesema Mohamedi.

Kurumna Nicholaus ambaye aliacha shule na kwenda Machimboni alisema kuwa baada ya wanafunzi wenzake kumfuata na kumweleza faida za elimu alikubali kurejea darasa ili kutimiza ndoto zake za kulitumikia taifa katika kada ya Uhandisi katika sekta ya Madini.

“Wazazi wangu hawana mwamko wa elimu,ukikaa nyumbani utalazimika kuchunga mifugo au kuozeshwa mimi niliona nitoroke nyumbani ili nikatafute maisha kama mchimbaji lakini kwa umri wangu nilishindwa ndio maana walipokuja wenzangu nikubali kurudi shule,”amesema Nicholaus.

Kwa upande wake John Banda Mwalimu wa Malezi katika Shule hiyo ya Sekondari alisema wameanzisha dawati la Malezi,unasihi, ulinzi na usalama kwa wanafunzi,litakalokuwa na dhima ya kusikiliza kero mbalimbali zinazowakabili ndani ya eneo la shule na kwenye jamii.

Naye Afisa Mtendaji wa kata ya Shilela Mwanaidi Mzee aliwataka wazazi kuwafichua watu wanaofanya ukatili kwa watoto kwenye ngazi za familia ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa sambamba na kuacha tabia ya kutokubaliana watu wanaobainika kuwapa mimba wanafunzi.

Awali akizungumza na wanafunzi hao Jackson Malangalila Mwezeshaji kutoka Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) amesema midahalo hiyo imeanza kuleta matokeo chanya baada ya makundi mbalimbali kwenye jamii kutambua, athari za ukatili wa kijinsia na kuanza kutafuta suluhisho ya kuzitatua.

“Wanafunzi wamehamasika na kuanzisha klabu za kupinga ukatili,wanatambua haki zao za msingi ikiwemo kupatiwa elimu kutokana uwepo wa mwamko mdogo wa jamii na kutotoa kipaumbe cha elimu kwa wanafunzi wa kiume na kike,”amesema Malangalila.

Amefafanua kuwa mradi huo Ushirikishwaji wa jamii kupitia midahalo ya una lengo la kutokomeza Ukatili wa Kijinsia na mila na desturi hasi kwa kuyahusisha makundi mbalimbali wakiwemo wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ili kuondoa ukatili wa kijinsia kwa wasichana shuleni na kwenye jamii.


“Mradi huu unatekelezwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa ufadhili wa Shirika la Kimataifa la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu (UNFPA) na Shirika la Misaada la Korea Kusini (KOICA),”amesema Malangalila.
Share:

WADAU WA UTALII WAMPA TANO MHE.RAIS, WASIFU KASI YA WIZARA



Na John Mapepele

Wadau wa Sekta ya Utalii nchini wametumia mkutano wao na Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta mabadiliko chanya katika kipindi kifupi cha uongozi wake, huku wakisifu kasi ya sasa ya utendaji wa Wizara.

Wadau hao wa utalii takribani mia sita kutoka katika vyama vyote vya wadau wa utalii nchini wameyasema hao usiku wa kuamkia leo mei 27, 2023 katika mkutano maalum na Wizara ya Maliasili na Utalii uliochukua zaidi ya masaa nane na kumalizika saa sita usiku, ulioratibiwa na Wizara ya Maliasili ambapo Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mohamed Mchengerwa akiambatana na Katibu Mkuu Dkt Hassan Abbasi na Naibu wake Anderson Mutatembwa ameongoza menejimenti ya Wizara na taasisi zote zilizochini ya wizara hiyo kufanya kikao maalum na wadau hao.

Kikao hicho ambacho Mhe. Mchengerwa ndiye Mwenyekiti kimekuwa na lengo mahususi moja tu la kujadili changamoto mbalimbali za kisekta na kuzipatia ufumbuzi wa kudumu ili kuboresha sekta huku watendaji wakitakiwa kujibu hoja zote za wadau.




Akichangia hoja katika mkutano huo, Mwenyekiti wa waongoza utalii kanda ya kaskazini (NTSGS) Qorro Englebert amempongeza Rais Samia kwa kutumia kipindi cha mlipuko wa ugonjwa wa uviko 19 kuwapatia mafunzo maalum wadau wa utalii zaidi ya 1000 katika vyuo vya Serikali ambayo amedai yamesaidia kuwaongezea ujuzi maalum katika kazi zao za kila siku.

Ameiomba Serikali kuwapa upendeleo maalum wanafunzi wanaomaliza mafunzo maalum ya uaskari wa uhifadhi katika vyuo vya Serikali ili waweze kutumia taaluma hiyo waliyoisomea badala ya kuajiri askari wasiyokuwa na elimu ya uhifadhi.

Pia amempongeza Mhe. Rais kwa kupunguza kodi za kutua ndege na kufafanua kuwa baada ya punguzo hilo kumekuwa na matokeo chanya ya wimbi kubwa la ndege kuwaleta watalii.

Aidha wadau hao wamepongeza uongozi mpya kwa kuonesha kasi mpya ya ufanyaji kazi huku wakisifu namna Waziri Mchengerwa anavyoshirikiana na watendaji wake katika shughuli mbalimbali huku wakifafanua kuwa ushirikishwaji baina ya watendaji wa Wizara na wadau ni nguzo muhimu katika kuleta mafanikio ya haraka kwenye sekta.

“Naomba niwe mkweli Timu ya sasa hivi haijawahi kutokea. Katika kipindi kifupi tangu kuteuliwa kwenu tumeshuhudia Mhe. Waziri na Katibu Mkuu mmekuwa pamoja katika utendaji wenu wa kazi jambo ambalo limetupatia moyo, kwa kasi na ushirikishwaji huu na jinsi ambayo mmeanza vizuri tunatarajia mtatufikisha mbali.” Amesisitiza Mwenyeki Wile Chambulo ambaye ni Mwenyekiti wa TATO nchini.

Awali akifungua mkutano huo, Waziri Mchengerwa amesisitiza kuwa katika kipindi hiki Serikali itakuwa karibu na wadau kwenye kila hatua ili kuhakikisha sekta inasonga mbele kwa maslahi ya wadau na taifa kwa ujumla.

“Kwa kushikiana na wadau na Serikali mtegemee maboresho makubwa yanakuja, na kamati yetu nataka ifanye kazi na ije na mapendekezo ili marekebisho haya yaweze kufanyika haraka.” Amesisitiza Mhe. Mchengerwa

Pia amesema katika kipindi hiki Serikali itaboresha miundo mbinu ikiwa ni pamoja na kuweka barabara za kiwango cha lami itakayokuwa inapitika mwaka mzima pamoja, pia kuimarisha ulinzi kwa mgeni.


Akifafanua mchango wa sekta ya utalii amesema Sekta hii ni miongoni mwa sekta muhimu na yenye mchango mkubwa katika kuchangia ukuaji wa uchumi wetu, kutoa fursa za ajira na kuchochea ukuaji wa sekta nyingine muhimu.

“Mathalan, katika kipindi cha kuanzia mwaka 2021 hadi mwaka 2022 mchango wa sekta hii ulikuwa takribani asilimia 17 ya pato la Taifa, ambapo idadi ya watalii iliendelea kuongezeka kutoka watalii 922,692 mwaka 2021 hadi kufikia watalii 1,454,920 kwa mwaka 2022. Mapato yatokanayo na utalii yaliongezeka kutoka kutoka Dola za Marekani Bilioni 1.3 mwaka 2021 hadi kufikia Dola za Marekani Bilioni 2.5 mwaka 2022. Kadhalika, sekta hii ilitoa fursa za ajira takribani milioni 1.5 za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja." Ameongeza Mhe Mchengerwa

Amesema mafanikio hayo yanatokana na jitihada kubwa zinazofanywa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuipa kipaumbele sekta hii kupitia uwekezaji wa aina mbalimbali alioufanya pamoja na ushirikiano imara uliopo baina ya sekta za umma na Sekta Binafsi.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger