Tuesday 29 March 2022

Video Mpyaaa!!! NTEMI OMABALA - MAJUNGU


Hii hapa ngoma mpya ya Msanii Ntemi Omabala inaitwa Majungu..




Share:

Video : BAHATI BUGALAMA - UKOO

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE MACHI 29,2022

Magazetini leo Jumanne March 29,2022



Share:

MPIGA DEBE AMUUA MWENZAKE KWA KUMCHOMA KISU WAKIGOMBANIA ABIRIA STENDI YA MABASI MSAMVU MOROGORO

 

Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro inamshikilia mpiga debe wa Kituo cha Mabasi Msamvu,Abdallah Yassin (32) kwa tuhuma za kumchoma Kisu kifuani upande wa kushoto mpiga debe mwezake aliyetambuliwa kwa Jina la Tazani Mndeme (35) kutokana na ugomvi uliozuka baina yao kugombea Abiria na kusababisha kifo chake.


Akizungumza na Waandishi wa Habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro,Fortunatus Muslimu amesema kuwa tukio hilo limetokea Machi 28,2022 majira ya Saa 12 asubuhi katika Stendi kuu ya mabasi Msamvu.


Muslimu amesema ugomvi huo ulisababisha mpiga debe Abdallah mkazi wa Mwembesongo,Manispaa ya Morogoro kumchoma kisu kifuani upande wa kushoto mwezake Tazani mkazi wa Kihonda ambaye alikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro bahati mbaya alifariki Dunia wakati akipatiwa matibabu.


“Tayari mtuhumiwa Abdallah amekamtwa na hatua za kumfikisha mahakamani zitafuata mara upelelezi ukikamilika na Mwili wa marehemu umehifadhiwa chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro” - Kamanda Musilimu.


Chanzo - Site Digital Media

Share:

Monday 28 March 2022

TAASISI ZA KIFEDHA ZAOMBWA KUPUNGUZA RIBA ZA MIKOPO KWA WAJASIRIAMALI WADOGO

Na Ashura Jumapili, Bukoba.

Baadhi ya wajasiriamali Mkoani Kagera wameziomba taasisi za kifedha zinazotoa mikopo kwa Wafanyabiashara kupunguza riba za mikopo sanjari na kupunguza masharti kama ilivyofanya benki ya CRDB.

Wakiongea kwa nyakati tofauti katika siku ya ( Wellness Day )ya Wafanyakazi wa benki hiyo ya kukutana na kufanya vipimo vya Afya zao kwa magonjwa yasiyoambukiza wajasiriamali hao walisema wanatamani kukopa lakini masharti yanawashinda.

Martine Johansen mjasiriamali kata Kashai Manispaa ya Bukoba ,anajishughulisha na shughuli za kilimo alisema anatamani kuomba mikopo lakini anashindwa kutokana na masharti ya ukopeshaji na riba kuwa juu.

Johansen, alisema kuwa Hali ya Sasa biashara ni ngumu hivyo riba ikiwa juu wanaogopa kukopa.

"Afadhali benki ya CRDB kidogo riba yake ipo chini ukilinganisha na mabenki mengine", alisema.

Mstahiki meya wa Manispaa ya Bukoba Gypson Godson, ambaye alikuwa mgeni rasmi ameiomba benki ya CRDB kupunguza riba kwa Wajasiriamali wadogo kama walivyofanya kwa mikopo ya Kilimo na watumishi,ili na wao waweze kuchangamkia fursa ya mikopo ili waweze kukuza biashara zao na kupanua mitaji.


Godson,alitoa ombi hilo kwenye ( Wellness Day ) iliyoandaliwa na benki hiyo ya CRDB Kwaajili ya Wafanyakazi kushiriki pamoja kupima Afya zao hasa kwa magonjwa yasiyoambukiza na kushiriki michezo mbalimbali.

Alisema benki hiyo imefanya Jambo jema la kutoa mafunzo juu ya Afya kwa Wafanyakazi wake.

"Wakati naingia hapa nilienda kufanya vipimo nilikuwa najua niko salama lakini baada ya kupima urefu na uzito nimejikuta nipo sehemu mbaya kiafya hivyo nalazimika kufanya mazoezi na kupunguza baadhi ya vyakula",alisema Mstahiki Meya.

Alisema ili kufanya kazi kwa weledi ni lazima uwe na nguvu pamoja na Afya njema wakati wote.

Hata hivyo aliwaomba viongozi wa benki hiyo kushiriki katika miradi ya kimkakati ya ujenzi wa soko kuu la Bukoba na stendi kuu la mabasi ili kuiletea Manispaa hiyo maendeleo na Wafanyabiashara waweze kufanya shughuli zao katika mazingira Rafiki.

Pia aliomba kuwepo na michezo kati ya watumishi wa benki hiyo na madiwani wakishirikiana na watumishi wa Manispaa katika uwanja wa kaitaba sanjari na kupima Afya kwa magonjwa yasiyoambukiza.

Kaimu Meneja wa benki ya CRDB Kanda ya Ziwa Japhary Katura, alisema mikopo ya Kilimo imepunguzwa riba kutoka asilimia ( 20-9.9 )na kwa watumishi kutoka asilimia ( 17-13 ).

Alisema kwa Sasa benki ipo kwenye mchakato wa kupunguza riba kwa wajasiriamali wadogo na muda si mrefu watatoa taarifa .

Alisema benki ipo tayari kushirikiana na Manispaa ya Bukoba katika miradi ya kimkakati wanayoendelea kuitekeleza .

Alisema milango iko wazi kwa Manispaa ya Bukoba katika kutekeleza miradi mbalimbali.

Share:

NDEJEMBI ADHAMIRIA KUSIMAMIA SHILINGI BILIONI 7.8 ZILIZOTOLEWA NA RAIS KUTEKELEZA MIRADI YA KUPUNGUZA UMASKINI MKOANI MWANZA


 Naibu Waziri,Ofisi ya Utumishi wa Umma na utawala bora Deogratius Ndejembi wakati  akizungumza na Waratibu,wahasibu na maafisa ufuatiliaji wa mpango wa Tasaf leo Jijini Mwanza

*****



Na Mwandishi wetu,Malunde 1 blog-MWANZA


NAIBU Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Deogratius Ndejembi ameahidi kusimamia kikamilifu matumizi ya shilingi bilioni 7.8 zilizotolewa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ili kutekeleza Miradi 104 ya Kupunguza Umaskini Awamu ya Nne (TPRP IV), iliyoibuliwa mkoani Mwanza kwa lengo kuboresha maisha ya kaya maskini katika halmashauri zote mkoani humo.


Mhe. Ndejembi ameeleza dhamira yake hiyo leo wakati akizungumza na Waratibu, Wahasibu na Maafisa Ufuatiliaji wa Mpango wa TASAF mkoani Mwanza, katika kikao kazi chake na maafisa hao chenye lengo la kuhimiza usimamizi mzuri wa fedha zilizotolewa na Serikali ili kutekeleza Miradi ya Kupunguza Umaskini Awamu ya Nne mkoani humo.


Mhe. Ndejembi amesema, shilingi bilioni 7.8 ni fedha nyingi ambazo Mhe. Rais amezitafuta kwa wadau wa maendeleo ili zitumike kuboresha maisha ya kaya maskini na kuongeza kuwa, wananchi wana matarajio makubwa ya fedha hizo ziwasaidie kunyanyua maisha yao, hivyo atahakikisha anafuatilia kwa ukaribu ili zitumike kwa lengo lililokusudiwa.


Ameongeza kuwa, atahakikisha anafanya ufuatiliaji wa karibu wa utendaji kazi wa Waratibu, Wahasibu na Maafisa Ufuatiliaji wa Mpango ili fedha hizo zitumike vizuri, na kuwaasa kuwa atakayejaribu kucheza nazo zitamtokea puani hivyo ni heri acheze na mshahara wake na si fedha hizo.


“Mmemsikia Mhe. Rais mara kadhaa akisema mtu akimzingua naye anamzingua, hivyo kabla Mhe. Rais hajanizingua mimi nitawazingua kweli kweli na ndio maana nimeamua kuwaelezeni ukweli ili kila mmoja wetu atekeleze wajibu wake,” Mhe. Ndejembi amesisitiza.


Katika kutekeleza azma yake ya kufanya ufuatiliaji, Mhe. Ndejembi ameahidi kufanya ziara mara kwa mara kanda ya ziwa ili kujiridhisha na namna Miradi Miradi 104 ya Kupunguza Umaskini Awamu ya Nne inavyotekelezwa.


Aidha, amewataka waratibu wa TASAF katika Halmashauri zote za Mkoa wa Mwanza kuhakikisha wanawashirikisha Wakuu wa Wilaya na Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya ili kuwe na uwazi na ufuatiliaji mzuri wa utekelezaji wa miradi hiyo yenye manufaa kwa wananchi wanaotoka katika kaya maskini.


Naibu Waziri Ndejembi amesema kuwa, yapo maeneo ambayo yamefanya utekelezaji mzuri wa miradi ya TASAF, hivyo nikaona ni vema nije mkoani Mwanza kwa lengo la kuhimiza usimamizi mzuri wa miradi hiyo ya Kupunguza Umaskini Awamu ya Nne ili mnapoanza utekelezaji kusitokee ubabaishaji.


“Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa imejionea mkoani Njombe kituo cha afya chenye ubora na thamani kimejengwa na TASAF kwa gharama ya milioni 80 tu, hivyo natamani miradi yote ya TASAF iendelee kujengwa kwa gharama stahiki,” Mhe. Ndejembi amefafanua.


Kwa niaba ya Waratibu, Wahasibu na Maafisa Ufuatiliaji wa Mpango wa TASAF mkoani Mwanza waliohudhuria kikao kazi hicho cha Mhe. Ndejembi na Maafisa hao, Mratibu wa TASAF Sengerema Bw. Malissa Ndugha amemshukuru Mhe. Ndejembi kwa kuwakumbusha jukumu la kusimamia vizuri fedha za miradi ya TASAF ili thamani ya fedha hizo zilizotolewa na Serikali ionekane.


Bw. Ndugha amemhakikishia Mhe. Ndejembi kuwa, wamepokea maelekezo yake na watayatekeleza kikamilifu ili kutomuangusha Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ambaye amezitafuta fedha hizo kwa lengo la kuboresha maisha ya kaya maskini. 


Miradi ya Kupunguza Umaskini Awamu ya Nne (TPRP IV) ilizinduliwa tarehe 27 Oktoba,2021 jijini Mwanza. Jumla ya Miradi 104 yenye zthamani ya shilingi 7,845,316,205.24 imeibuliwa na kupitishwa kwa ajili ya utekelezaji Mkoani Mwanza katika Halmashauri zote za Kwimba, Magu, Misungwi, Ilemela, Nyamagana, Sengerema, Ukerewe na Buchosa. Kati ya miradi hiyo 104, 31 ni ya afya, 49 ya elimu na 24 ni ya kutoa ajira za muda (PWP).

 

Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza na Waratibu, Wahasibu na Maafisa Ufuatiliaji wa Mpango wa TASAF mkoani Mwanza (hawapo pichani) wakati wa kikao kazi chake na maafisa hao chenye lengo la kuhimiza usimamizi mzuri wa fedha za kutekeleza Miradi ya Kupunguza Umaskini Awamu ya Nne mkoani humo. 

 

Waratibu, Wahasibu na Maafisa Ufuatiliaji wa Mpango wa TASAF mkoani Mwanza wakimsikliliza Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deogratius Ndejembi (hayupo pichani) wakati wa kikao kazi Naibu Waziri huyo na maafisa hao chenye lengo la kuhimiza usimamizi mzuri wa fedha za kutekeleza Miradi ya Kupunguza Umaskini Awamu ya Nne mkoani humo.


Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Salum Kalli akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deogratius Ndejembi kuzungumza na Waratibu, Wahasibu na Maafisa Ufuatiliaji wa Mpango wa TASAF mkoani Mwanza wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na maafisa hao chenye lengo la kuhimiza usimamizi mzuri wa fedha za kutekeleza Miradi ya Kupunguza Umaskini Awamu ya Nne mkoani humo.

 

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bi. Sarah Mshiu akizungumza na Waratibu, Wahasibu na Maafisa Ufuatiliaji wa Mpango wa TASAF mkoani Mwanza (hawapo pichani) wakati wa kikao kazi Mhe. Deogratius Ndejembi na maafisa hao chenye lengo la kuhimiza usimamizi mzuri wa fedha za kutekeleza Miradi ya Kupunguza Umaskini Awamu ya Nne mkoani humo.

 

Mratibu wa TASAF Mkoa wa Mwanza Bi. Monica Mahundi akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ya mkoa wa Mwanza kwa Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deogratius Ndejembi wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na Waratibu, Wahasibu na Maafisa Ufuatiliaji wa Mpango wa TASAF mkoani Mwanza chenye lengo la kuhimiza usimamizi mzuri wa fedha za kutekeleza Miradi ya Kupunguza Umaskini Awamu ya Nne mkoani humo.

 

Mratibu wa TASAF Wilaya ya Ilemela Bw. Frank Ngitahoh akimueleza Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deogratius Ndejembi (hayupo pichani) namna Wilaya yake ilivyotekeleza Mpango wa TASAF wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na Waratibu, Wahasibu na Maafisa Ufuatiliaji wa Mpango wa TASAF mkoani Mwanza, chenye lengo la kuhimiza usimamizi mzuri wa fedha za kutekeleza Miradi ya Kupunguza Umaskini Awamu ya Nne mkoani humo.

 

Sehemu ya Waratibu, Wahasibu na Maafisa Ufuatiliaji wa Mpango wa TASAF mkoani Mwanza wakimsikiliza Naibu Waziri,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deogratius Ndejembi akikisisitiza jambo wakati wa kikao kazi chake na maafisa hao chenye lengo la kuhimiza usimamizi mzuri wa fedha za kutekeleza Miradi ya Kupunguza Umaskini Awamu ya Nne mkoani humo.


Mratibu wa TASAF Wilaya ya Sengerema Bw. Malissa Ndugha akitoa neno la shukrani kwa Mhe. Ndejembi kwa niaba ya Waratibu, Wahasibu na Maafisa Ufuatiliaji wa Mpango wa TASAF mkoani Mwanza waliohudhuria kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na maafisa hao chenye lengo la kuhimiza usimamizi mzuri wa fedha za kutekeleza Miradi ya Kupunguza Umaskini Awamu ya Nne mkoani humo

Share:

MBUNGE ANUSURIKA KUFA AKIENDA KUMZIKA BABAAKE..GARI LATEKETEA



Mbunge wa Masasi Mjini, Geofrey Mwambe na familia yake leo Jumapili Machi 27, 2022 wamenusurika kifo baada ya gari binafsi waliyokuwa wakisafiria kushika moto na kuteketea kabisa.

Mbunge huyo na familia yake walikuwa wakielekea Masasi kwenye msiba wa baba yake mzazi.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU MACHI 28,2022

Magazetini leo Jumatatu March 28,2022















































Share:

TARI KUTARAJIA KUZALISHA TANI ELFU 8 HADI 10 ZA SHAIRI KUANZIA MWAKA 2021/2025


Mratibu wa zao la shairi Kitaifa kutoka TARI bi Salome Munisi akitoa taarifa ya utafiti wa zao la shairi kwa Waandishi wa habari .

Na Rose Jackson - Arusha.

Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) Selian inatarajia kuzalisha Tani elfu nane Hadi elfu kumi za shairi kuanzia mwaka 2021 hadi 2025 ili kuweza kukidhi mahitaji halisi yanayohitajika hapa nchini.


Hayo yamebainishwa na mratibu wa zao la shairi kitaifa Salome Munisi wakati akizungumza na waandishi wa habari waliopatiwa mafunzo na COSTECH mara baada ya kutembelea taasisi hiyo kwa lengo la kujifunza habari za matokeo ya utafiti wa kisanyansi kwa vitendo.


Amesema agizo la serikali ni kuhakikisha kuwa uagizwaji wa zao la shairi kutoka nje unapungua hivyo wao wamepewa jukumu la kuzalisha Tani elfu nane Hadi Tani elfu kumi Hadi ifikapo mwaka 2025.

"Mwaka kesho tunatarajia kuvuna Tani elfu kumi na tano na tunategemea mpaka ifikapo mwaka 2025 mvua ikinyesha tunaweza kukidhi mahitaji ambayo tuliambiwa tuzalishe kusudi Ni kupunguza changamoto ya uagizwaji wa zao hili kutoka nje ya nchi"aliongeza bi Salome.

Amefafanua kuwa wamekuwa wakifanya utafiti wa zao la shairi ili kupata mbegu bora zinazokidhi mahitaji ya wanunuzi ikiwa ni pamoja na kuwasilisha tafiti zao kwa Wakulima ambao ni wadau wakubwa ili kuongeza tija.

Kwa upande wake Zeda Mtakimwa kutoka kitengo cha ngano TARI Selian amesema kuwa katika kufanya tafiti za ngano Wanazalisha ngano za ukanda wa juu,ngano za Ukanda wa Kati pamoja na ngano za ukanda chini ambapo wanapofanya utafiti wa mbegu wanaangalia mabadiliko ya tabia nchi ukinzani wa magonjwa na uongezaji tija kwa Wakulima .


Kwa upande wake kMratibu wa mafunzo ya sayansi na teknolojia kutoka Tume ya taifa ya sayansi na teknolojia (COSTECH ) Deusdedith Leonard amesema kuwa lengo la mafunzo hayo kwa wanahabari Ni kuhakikisha taarifa za sayansi zinaifikia jamii kwa ufasaha na kwa wakati.

Amesema kuwa wapo watafiti , ambao wametafiti vitu vikubwa lakini kutokana na kutokuwepo kwa taarifa sahihi jamii haipati taarifa hizo hivyo kupitia mafunzo hayo yatasaidia kuleta mabadiliko channya.
Share:

Sunday 27 March 2022

TBS YAWATAKA WAAGIZAJI WA BIDHAA NJE YA NCHI KUPIMA BIDHAA ZAO KABLA HAZIJAINGIA NCHINI

Maafisa wa TBS wakitoa maelezo kwa wageni waliotembelea banda la TBS kuhusu taratibu za kuingiza bidhaa nchini katika maonesho ya 23 ya ujenzi Afrika yanayofanyika Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.

************

NA Mwandishi Wetu

Waagizaji wa bidhaa nje ya nchi wameshauriwa kuhakikisha bidhaa wanazoingiza nchini zinakidhi viwango ili kuepuka kupata hasara na kuepusha Tanzania kuwa dampo la bidhaa zisizokidhi viwango.

Ushauri huo umetolewa mwishoni mwa wiki na Mkaguzi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Venance Colman wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye Maonesho ya Kimataifa ya 23 Ujenzi ya Afrika yaliyoanza Machi 24 hadi 26, mwaka huu kwenye ukumbi wa Diamond Jublee jijini Dar es Salaam.

Colman alisema TBS imeshiriki maonesho hayo kwa ajili ya kutoa elimu kuhusiana na masuala ya viwango ikiwa ni pamoja na uingizaji wa bidhaa zenye viwango nchini na kwamba hiyo imekuwa fursa muhimu hasa ikizingatiwa kwamba washiriki wengi wa maonesho hayo walitoka nje ya nchi.

''Washiriki wengi wa maonesho haya wametoka nje ya nchi, hivyo elimu kubwa iliyotolewa ilikuwa ni kuhusiana na taratibu za uingizaji wa bidhaa nchini, sisi kama Shirika tumetumia fursa hiyo kutoa elimu na kuwahimiza washiriki hao kuhakikisha bidhaa zinazoingizwa nchini zimepimwa na kukidhi viwango,''alisema.

Kwenye Maonesho hayo washiriki walikuwa wanauliza sana kuhusiana na uingizaji wa bidhaa nchini, hivyo walihimizwa wahakikishe wanapima ubora wa bidhaa kabla hazijaingizwa nchini.

Alitaja faida za kupima ubora wa bidhaa kabla ya kuingizwa nchini kuwa ni pamoja na kuepuka kupata hasara pindi zikifika nchini na zikabainika hazikidhi viwango pamoja na kuepusha Tanzania kuwa dampo la bidhaa zisizokidhi viwango.

Hasara hizo ni pamoja bidhaa zao kuteketezwa iwapo zitabainika hazikidhi viwango ikiwa ni pamoja na kutozwa faini. Aidha, washiriki hao walipewa elimu kuhusiana na umuhimu wa uthibitishaji ubora wa bidhaa.

Wakizungumza kwenye maonesho hayo baadhi ya washiriki walipongeza uwepo wa TBS kwenye maonesho hayo, kwani wameweza kupata elimu kuhusiana na faida za kuingiza nchini bidhaa zilizopimwa, hatua ambayo inawahakikishia usalama wa mitaji yao.

''Kwa washiriki wa maonesho haya ambao tumepata elimu hiyo tunaahidi kuwa mabalozi wa viwango hatua ambayo italinda mitaji yetu, hivyo kuongeza mchango wetu katika ukuzaji uchumi wa nchi tunazotoka,'' alisema mmoja wa washiriki aliyejitambuisha kwa jina Yasini.

Share:

MWENYEKITI WA CCM MKOA WA KAGERA ARIDHISHWA NA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI

Wa pili kushoto ni msimamizi wa mradi wa shule hiyo Raymond Mutakyahwa
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Bi. Konstansia Buhiye

Na Mbuke Shilagi Kagera.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kagera Bi. Constansia Buhiye ameridhishwa na utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari inayojengwa katika mtaa wa Mafumbo kata ya Kashai Manispaa ya Bukoba.


Akizungumza baada ya kutembelea mradi huo akiwa ameambatana na kamati ya siasa ya mkoa, mwenyekiti huyo amesema kuwa kata ya Kashai ilistahili kuwa na shule nyingine ya sekondari kutokana na kuwa na idadi kubwa ya watu, wakiwamo wenye uhitaji wa kuendelea na elimu ya sekondari.


Akitoa taarifa ya ujenzi wa shule hiyo mpya msimamizi wa mradi wa ujenzi Raymond Mutakyahwa amesema kuwa tayari wamekwishapokea shilingi milion 600 kwa ajili ya ujenzi huo ulioanza Februari 12, 2022.


Mutakyahwa ameongeza kuwa ujenzi huo ni wa madarasa nane, Maabara ya Kemia, Baiolojia, Fizikia, chumba cha Kompyuta, Maktaba, pamoja na matundu 20 ya vyoo, na kwamba wamefikia hatua ya kuezeka.


Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kashai Ramadhan Kambuga amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Moses Machali kwa kushirikiana naye na kuhakikisha linapatikana eneo kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo ambayo uwepo wake utawezesha kuwepo kwa ongezeko la idadi ya watoto wanaoendelea na elimu ya sekondari.


"Kulikuwepo na changamoto ya upatikanaji wa eneo, lakini namshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kusimama kidete na kuhakikisha eneo linapatikana, na napendekeza shule hii iitwe kwa jina la Samia Suluhu Hassan, ikiwa ni hatua moja wapo ya kuenzi jitihaza za Rais wa awamu ya sita, za kuwaletea wananchi maendeleo" amesema Kambunga.
Diwani wa Kata ya Kashai Ramadhani Kambuga akizungumza
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger