Sunday 25 July 2021

PROF. MANYA AFUNGUA MAONESHO YA PILI YA BIASHARA NA TEKNOLOJIA YA MADINI SHINYANGA...AFICHUA SIRI WANAOUZIWA MADINI FEKI

Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya akizungumza leo Jumapili Julai 25,2021 wakati akifungua Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Na Asteria Muhozya, Shinyanga

Wanunuzi wa Madini wametahadharishwa kununua Madini nje ya Mfumo wa Masoko  ili kuepuka  madini bandia tofauti na wanapofanya biashara  ndani ya masoko kwani hakuna kificho.

 Tahadhari hiyo imetolewa Julai 25, 2021 na Naibu  Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya wakati akifungua Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia kwa Mkoa wa Shinyanga kwa  niaba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa .

Prof. Manya amesisitiza kuwa, mfumo wa biashara ya madini uliopo kwenye masoko yote 39 na Vituo vya Ununuzi wa Madini 50 yaliyoanzishwa mikoa yote nchini ni ya uwazi na hauruhusu madini bandia kuuzwa kwenye masoko hayo.

"Mnaotaka kununua madini ya Tanzania msinunue nje ya mfumo wa masoko, nje ya masoko mnauziwa madini feki,’’ amesisitiza Prof. Manya.

 Ameongeza kuwa kutokana na Tanzania kuonesha mageuzi makubwa kufuatia kuanzishwa kwa masoko ya madini, ndiyo nchi pekee duniani ambayo inaendesha biashara ya madini kwa uwazi kupitia masoko hayo jambo ambalo limeyafanya mataifa mengine duniani kutaka kujifunza.

"Wasiotaka kufuata taratibu ndiyo wanaokosoa mfumo wa masoko kwa kudhani Serikali imeyaanzisha ili kukusanya mapato. Wasiojua umuhimu wa masoko hayo waulizeni FEMATA na vyama vya wachimbaji kwenye mikoa watawaeleza", amesema Prof. Manya.

Ameongeza kuwa, Serikali itaendelea kuimarisha mifumo, sheria ili wananchi waendelee kunufaika na rasilimali madini na kuongeza kwamba, itaendelea kuimarisha masoko ya madini na kuyaongeza pale itakapohitajika.

Akizungumzia suala la uzalishaji wa katika Mgodi Almasi Mwadui, Prof. Manya amesema uzalishaji katika mgodi huo uliathiriwa na janga la ugonjwa wa korona na hivyo kupelekea kusitishwa kwa uzalishaji lakini unatarajiwa kuanza tena uzalishaji wake mwezi Agosti, 2021.

Katika hatua nyingine, Prof. Manya amesema kuwa, Mkoa wa Shinyanga uko mbioni kuanzisha kiwanda cha kusafisha dhahabu kama ilivyo kwa mikoa ya Mwanza, Geita na Dodoma ili kuhamasisha shughuli za uongezaji thamani madini kufanyika nchini badala ya madini ghafi kusafirishwa katika nchi nyingine jambo ambalo litasaidia kuchochea ajira ikiwemo kuyapatia thamani halisi madini yanayozalishwa nchini.

Aidha, Prof. Manya ametumia fursa hiyo kuwaasa viongozi kuacha alama ya uongozi iliyotukuka kwa kufuata kanuni na misingi ya utawala bora ikiwemo kutoa kipaumbele katika usimamizi wa fedha za maendeleo kwa ajili ya manufaa ya wananchi na taifa kwa ujumla.

Akizungumzia kuhusu kuwaendeleza wachimbaji wadogo amesema kuwa serikali itaendelea kutenga maeneo kwa ajili ya wachimbaji   yenye taarifa za msingi za kijiolojia ili kuwawezesha wachimbe kwa tija.

Kuhusu ruzuku kwa wachimbaji wadogo Prof. Manya amesema awali, ruzuku iliyotolewa na Serikali kwa wachimbaji wadogo haikuleta tija iliyokusudiwa na kueleza kuwa, hivi sasa Serikali inaangalia namna bora ambayo itawezesha ruzuku hizo kuwa na tija. Ufafanuzi huo unafuatia ombi lililowasilishwa  na viongozi mbalimbali akiwemo Rais wa Chama Cha Wachimbaji wa Madini Tanzania (FEMATA) la kuwawezesha wachimbaji kupatiwa ruzuku.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati amesema kuwa, katika Mwaka wa Fedha 2021/22 kuna uwezekano wa mkoa huo kukusanya mapato zaidi yanayotokana na rasilimali madini kutokana na kupatikana kwa maeneo mengine matatu kwa ajili ya shughuli za uchimbaji madini.

Ameyataja manufaa ya maonesho hayo kuwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu, kuwakutanisha wazalishaji, wauzaji na walaji na kutoa mafunzo kwa wachimbaji wadogo , kuongeza mbinu  bora za kukuza sekta ya madini mkoani humo pamoja na  kutangaza fursa mbalimbali zilizopo katika mkoa huo.

Kwa upande wa wakuu wa Mikoa walioshiriki katika maonesho hayo wameleeza kuhusu kuunga juhudi za  mkoa huo,  kujifunza kuhusu namna mkoa unavyosimamia sekta ya madini na kubadilisha uzoefu.

Kwa upande wake, Rais FEMATA John Bina akizungumza katika ufunguzi huo, ameiomba Serikali ione namna ya kuwawezesha mafundi mchundo kupata mafunzo nje ya nchi ili kuwawezesha kujifunza kuhusu teknolojia bora ambazo zitawasaidia wachimbaji wadogo nchini kupata teknolojia rahisi kuendeleza shughuli zao.

Maonesho hayo yamehudhuriwa pia na wakuu wa mikoa kutoka mikoa jirani ikiwemo ya Mara, Tabora, Geita na Simiyu. Aidha, washiriki katika maonesho hayo ni kutoka sekta za umma, sekta binafsi, kampuni za madini, taasisi za kifedha, watoa huduma na wajasiliamali.

Maonesho ya Pili ya Biashara na teknolojia kwa Mkoa wa Shinyanga yanaongozwa na kaulimbiu Uwekezaji wa Madini na Viwanda Shinyanga kwa Uchumi Endelevu. Maonesho hayo yaliyoanza tarehe 23 Julai, yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 1 Agosti, 2021.



Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya akizungumza leo Jumapili Julai 25,2021 wakati akifungua Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya akizungumza leo Jumapili Julai 25,2021 wakati akifungua Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizungumza kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
Mbunge wa Jimbo la Solwa Mhe. Ahmed Salum akizungumza kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
Rais wa Chama Cha Wachimbaji wa Madini Tanzania (FEMATA) , John Bina akizungumza kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Ally Hapi akizungumza kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
 Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga , Zuwena Omary akizungumza kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
 Katibu wa CCM mkoa wa Shinyanga, Donald Magesa akizungumza kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
 Mkuu wa wilaya ya Kahama Mhe. Festo Kiswaga akizungumza kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
 Mkuu wa wilaya ya Kishapu, Mhe. Joseph Modest akizungumza kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko akizungumza kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Maonesho, Dkt. Meshack Kulwa ambaye ni Mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Shinyanga akizungumza kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.

Burudani ikiendelea kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.

Burudani ikiendelea kwenye ufunguzi wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akitambulisha viongozi mbalimbali wa mkoa wa Shinyanga kwa Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya (wa pili kushoto).
Picha za kumbukumbu baada ya ufunguzi wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Soma pia:



Share:

WAZALISHAJI WA POMBE KALI MAARUFU 'SHUJAA NA ZHIMWA' WASHIRIKI MAONESHO YA BIASHARA NA TEKNOLOJIA YA MADINI SHINYANGA

Wafanyakazi wa Kampuni ya Canon General Supply iliyopo Mjini Shinyanga inayozalisha pombe kali maarufu kwa jina la Shujaa na Zhimwa, Clementina Mkongwa (kulia) na Amina Shamte wakionesha pombe kali wanazozalisha katika kiwanda hicho leo Jumapili Julai 25,2021 kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mfanyakazi wa Kampuni ya Canon General Supply iliyopo Mjini Shinyanga inayozalisha pombe kali maarufu kwa jina la Shujaa na Zhimwa, Clementina Mkongwa akionesha pombe kali ya Zhimwa
Wafanyakazi wa Kampuni ya Canon General Supply iliyopo Mjini Shinyanga inayozalisha pombe kali maarufu kwa jina la Shujaa na Zhimwa, Clementina Mkongwa (kulia) na Amina Shamte wakiwa kwenye banda la Kampuni ya Canon General Supply kwenye kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
Muonekano wa pombe kali za Shujaa na Zhimwa
Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya akizungumza leo Jumapili Julai 25,2021 wakati akifungua Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya akizungumza leo Jumapili Julai 25,2021 wakati akifungua Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya akizungumza leo Jumapili Julai 25,2021 wakati akifungua Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

STAMIGOLD YANOGESHA MAONESHO YA BIASHARA NA TEKNOLOJIA YA MADINI SHINYANGA....YASHUKURU SERIKALI KUWAPA UMEME


Afisa Utumishi wa Kampuni ya STAMIGOLD, Mhunda Nyakiroto (kulia) akimwelezea Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya (wa pili kushoto) shughuli wanazofanya kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kampuni ya STAMIGOLD ambayo ni kampuni tanzu ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kupitia mgodi wake wa Stamigold Biharamulo (Stamigold Biharamulo Mine - SBM) uliopo wilayani Biharamulo mkoa wa Kagera umeishukuru serikali kwa kupeleka huduma ya umeme wa TANESCO hali ambayo itapunguza gharama za uendeshaji kutoka shilingi Bilioni 1.2 hadi shilingi milioni 400 au 300 kwa mwezi.

Shukrani hizo zimetolewa na Afisa Utumishi wa Kampuni ya STAMIGOLD, Mhunda Nyakiroto leo Jumapili wakati Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya akitembelea banda la Kampuni ya STAMIGOLD kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yanayofanyika Uwanja wa Zainab Telack katika kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.

Afisa Utumishi wa Kampuni ya STAMIGOLD, Mhunda Nyakiroto amesema wanaishukuru serikali kwa kuwapelekea huduma ya umeme wa TANESCO kutoka Geita hali ambayo itasaidia gharama kubwa ya uzalishaji wa madini ya dhahabu ambapo wamekuwa wakitumia genereta za dizeli.

"Tangu mgodi huu uwe chini ya Serikali mwaka (2014), na kuanza uzalishaji rasmi 2015, umekuwa ukiingia kwenye gharama kubwa ya kutumia Genereta na mafuta ya Diesel yenye gharama za Shilingi Bilioni 1.2 kwa mwezi na baada ya kupata huduma ya umeme gharama itapungua na tutatumia shilingi Milioni 300 au 400",amesema Nyakiroto.

Katika hatua nyingine, Nyakiroto amesema wanashiriki maonesho ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya kuonesha jinsi wanavyofanya shughuli za uchimbaji madini ya dhahabu pamoja kueleza manufaa ya mgodi wao kwa wananchi.

“Miongoni mwa manufaa wanayopata wananchi kupitia mgodi wa Stamigold chini ya Meneja Mkuu wa mgodi Mhandisi Gilay Shamika ni pamoja na ajira. Tumeajiri Watanzania 610. Pia tumesaidia ujenzi wa miundo mbinu na miradi kwa jamii ikiwemo zahanati ya Nampalahala, barabara za vijiji vya Mavota, Mkunkwa na Msalabani vilivyopo katika kata ya Kaniha wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera”,ameeleza Nyakiroto.

“Hali kadhalika tunatumia maonesho haya kuonesha zao jipya la mkaa mbadala unaotumia makaa ya mawe ‘Rafiki Briquate’ ili kutunza mazingira. Bei ya mkaa huu mbadala ni rafiki lakini pia mkaa huu hautoi moshi. Tutaanza uzalishaji kamili wa mkaa huu mwishoni mwa mwezi Julai,2021”,amesema.

Amesema mgodi wa STAMIGOLD pia unaendelea kusaidia wajasirimali kwa kununua bidhaa zao kama vile ng’ombe, mboga mboga, matunda na samaki katika masoko ya Runzewe na Chato

Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya ameupongeza mgodi wa STAMIGOLD hatua inayoendelea nazo katika uzalishaji wa madini akieleza kuwa faida imekuwa ikipanda kila Mwaka na kusaidia STAMICO kulipa gawio Serikalini.
Afisa Utumishi wa Kampuni ya STAMIGOLD, Mhunda Nyakiroto (kulia) akimwelezea Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya (wa pili kushoto) shughuli wanazofanya kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yanayofanyika Uwanja wa Zainab Telack katika kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Afisa Utumishi wa Kampuni ya STAMIGOLD, Mhunda Nyakiroto (kulia) akimwelezea Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya (wa pili kushoto) shughuli wanazofanya kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga
Afisa Utumishi wa Kampuni ya STAMIGOLD, Mhunda Nyakiroto (kulia) akimwelezea Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya (katikati) shughuli zinazofanywa na kampuni hiyo kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga
Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya(katikati) akiangalia vipeperushi na bidhaa mbalimbali kwenye banda la Kampuni ya STAMIGOLD katika Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya(katikati) akiondoka kwenye banda la Kampuni ya STAMIGOLD katika Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya(kushoto) akiondoka kwenye banda la Kampuni ya STAMIGOLD katika Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

SIMBA SC YAIZIMA YANGA SC KIGOMA, YATWAA TENA TAJI LA ASFC



SIMBA SC wamefanikiwa kutetea Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya watani wa jadi, Yanga SC jioni ya leo Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma.

Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, kiungo wa kimafaifa wa Uganda, Thadeo Lwanga dakika ya 80 kwa kichwa akimalizia mpira wa kona uliopigwa na kiungo wa kimafaifa wa Msumbiji, Jose Luis Miquissone.

Yanga ililazimika kucheza pungufu tangu dakika ya 45 na ushei baada ya kiungo Mkongo, Tonombe Mukoko kutolewa kwa kadi nyekundu kufuatia kumchezea rafu Nahodha wa Simba SC, John Raphael Bocco.

Ni taji la pili mfululizo la ASFC kwa Simba SC na taji la tatu la msimu, baada ya kubeba Ngao ya Jamii na ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara mapema mwezi huu.

Via Binzubeiry blog
Share:

SHINYANGA BEST IRON YASHIRIKI MAONESHO YA PILI YA BIASHARA NA TEKNOLOJIA YA MADINI SHINYANGA...KASHI ATAKA TAASISI ZA FEDHA ZIKOPESHE WACHIMBAJI MADINI


Mkurugenzi wa Kampuni ya Uundaji wa Vifaa vya Uchimbaji na Uchenjuaji Madini ya Shinyanga Best Iron, Kashi Salula (kulia) akimuonesha Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya, Miundo michundo  alipotembelea banda la Shinyanga Best Iron kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga. 

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkurugenzi wa Kampuni ya Uundaji wa Vifaa vya Uchimbaji na Uchenjuaji Madini ya Shinyanga Best Iron, Kashi Salula ameziomba Taasisi za Fedha zikiwemo Benki ziwakopeshe Wachimbaji Wadogo wa Madini ili wanunue Miundo Michundo ‘Pembejeo za uchimbaji’ kutokana na wengi wao kutokuwa na mitaji ya kununua mitambo hiyo ya kuchimba na kuchenjua madini.

Kashi Salula ameyasema hayo leo Jumapili Julai 25,2021 wakati Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya akitembelea banda la Shinyanga Best Iron kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yanayofanyika Uwanja wa Zainab Telack katika kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.

Mkurugenzi huyo wa Kampuni ya Shinyanga Best Iron, Kashi Salula amesema ni vyema taasisi za kifedha zikawapa mikopo wachimbaji wadogo wa madini ili waweze kununua vifaa kwa ajili ya uchimbaji na uchenjuaji madini ili uchimbaji wao uwe na tija.

“Kampuni yetu inajihusisha na uchimbaji na uchenjuaji wa madini lakini pia tunajihusisha na utengenezaji wa miundo michundo na kuuza nchi nzima. Tunaomba taasisi za kifedha zikiwemo Benki ziangalie namna ya kuwawezesha wachimbaji wadogo ili wanunue mitambo kwa ajili ya kuchimba na kuchenjua madini”,amesema Gacha.

Katika hatua nyingine amesema wametumia fursa ya maonesho kuonesha namna wanavyofanya kazi.

Salula amesema pia kampuni yao inajihusisha na masuala ya uchomaji na ubunifu,uundaji wa mashine za nafaka ‘vinu’,ufundi wa mitambo ya viwandani,zana za mgodini na matengenezo mbalimbali.

Kwa upande wake, Rais wa Shirikisho la Wachimbaji Wadogo Tanzania (FEMATA), John Bina amempongeza Mkurugenzi wa Kampuni ya Uundaji wa Vifaa vya Uchimbaji na Uchenjuaji Madini ya Shinyanga Best Iron, Kashi Salula kwa kazi nzuri anayofanya ya kutengeneza na kuuza Miundo Michundo nchi nzima huku akipendekeza mafundi michundo akiwemo Salula Gacha kupewa mafunzo zaidi ya kuboresha kazi yao ikiwa ni pamoja na kuwapeleka nje ya nchi kwa ajili ya kupata ujuzi zaidi.

Naye Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amesema Serikali itaendelea kuwezesha wachimbaji madogo na kutenga maeneo ya msingi yenye taarifa ya Jiolojia na utafiti.

“Mpaka sasa kuna Masoko 39 na vituo 50 vya kuuzia madini.Serikali inaendelea kusimamia vituo hivi vya ununuzi wa madini na kufanya jitihada za kuongeza vingine.Tunawasihi watu wote wanaojihusisha na mnyororo wa madini waache kutorosha madini kwani bado kuna utoroshaji wa madini, hasara watakayopata wakikamatwa wakitorosha madini ni kubwa sana”,amesema Prof. Manya.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Uundaji wa Vifaa vya Uchimbaji na Uchenjuaji Madini ya Shinyanga Best Iron, Kashi Salula (kulia) akimwelezea Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya (wa nne kushoto)  namna wanafanya kazi alipotembelea banda la Shinyanga Best Iron kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yanayofanyika Uwanja wa Zainab Telack katika kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga leo Jumapili Julai 25,2021. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkurugenzi wa Kampuni ya Uundaji wa Vifaa vya Uchimbaji na Uchenjuaji Madini ya Shinyanga Best Iron, Kashi Salula (kulia) akimuonesha Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya, Miundo michundo  alipotembelea banda la Shinyanga Best Iron kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga. 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Uundaji wa Vifaa vya Uchimbaji na Uchenjuaji Madini ya Shinyanga Best Iron, Kashi Salula (kulia) akizungumza wakati Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya, alipotembelea banda la Shinyanga Best Iron kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Uundaji wa Vifaa vya Uchimbaji na Uchenjuaji Madini ya Shinyanga Best Iron, Kashi Salula (kulia) akimuonesha Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya, Miundo michundo  alipotembelea banda la Shinyanga Best Iron kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.  
Mkurugenzi wa Kampuni ya Uundaji wa Vifaa vya Uchimbaji na Uchenjuaji Madini ya Shinyanga Best Iron, Kashi Salula akiziomba Taasisi za Fedha zikiwemo Benki ziwakopeshe Wachimbaji Wadogo wa Madini ili wanunue Miundo Michundo ‘Pembejeo za uchimbaji’  wakati Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya  alipotembelea banda la Shinyanga Best Iron kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
 Naibu Waziri wa Madini Prof. Shukrani Manya (katikati) akizungumza kwenye banda la Shinyanga Best Iron katika Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.








Muonekano wa Miundo Michundo ‘Pembejeo za uchimbaji’ katika banda la Kampuni ya Uundaji wa Vifaa vya Uchimbaji na Uchenjuaji Madini ya Shinyanga Best Iron.

Picha zote na  Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

Senior Treasury Sales Dealer at CRDB

Senior Treasury Sales Dealer    Job Summary Responsible for developing new treasury revenue growth strategies for Large Corporate and Institutional customer segments. This involves driving profitability and increasing business volume while maintaining a strong risk/income ratio and a high-quality treasury portfolio. significant cross-functional interaction with other teams, a strong understanding of the Bank’s products, sales […]

This post Senior Treasury Sales Dealer at CRDB has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

23 Job Opportunities at BRELA

Government Transfer Vacancies At BRELA, July 2021. BRELA is a Government Executive Agency which was established under the Executive Agencies Act No. 30 of 1997 and published on the 8th October, 1999 through Government Notice No. 294. The Agency was officially inaugurated on the 3rd December 1999 to facilitate orderly conduct of business and provision […]

This post 23 Job Opportunities at BRELA has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Engineers at TARURA

Tanzania Rural and Urban Roads Agency (TARURA) is an Executive Agency of the President’s Office, Regional Administration and Local Government, (PO-RALG), established under Section 3 (1) of the Executive Agencies Act. (Cap. 245) by Order published in Government Notice No.211 dated May 12, 2017; and was inaugurated on July 02, 2017. Tanzania Rural and Urban […]

This post Engineers at TARURA has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Procurement and Supplies Officers at TARURA

Procurement and Supplies Officers    Tanzania Rural and Urban Roads Agency (TARURA) is an Executive Agency of the President’s Office, Regional Administration and Local Government, (PO-RALG), established under Section 3 (1) of the Executive Agencies Act. (Cap. 245) by Order published in Government Notice No.211 dated May 12, 2017; and was inaugurated on July 02, […]

This post Procurement and Supplies Officers at TARURA has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

73 Job Opportunities At Rural and Urban Roads Agency (TARURA)

TARURA  The Rural and Urban Roads Agency (TARURA) was officially opened by Prime Minister Kassim Majaliwa Kassim on 2 July 2017. The launch of TARURA was followed by the announcement in Government Gazette No. GN 211 of 12 May 2017. The Prime Minister directed TARURA to reject the massive corruption that is involved in tender […]

This post 73 Job Opportunities At Rural and Urban Roads Agency (TARURA) has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Traffic Liaison -Intern at ATCL

Traffic Liaison (4 Positions) -Intern   OPPORTUNITIES FOR INTERNSHIP AT ATCL Air Tanzania Company Limited (ATCL) is a legal entity owned by the Government of the United Republic of Tanzania and established under section 4 (1) of the Air Tanzania Corporation (Re-Organization and Vesting of Assets and Liabilities) Act, Cap. 205 R.E of 2002 and incorporated […]

This post Traffic Liaison -Intern at ATCL has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Aviation Quality and Safety – Intern at ATCL

Aviation Quality and Safety (4 Positions) -Intern (   OPPORTUNITIES FOR INTERNSHIP AT ATCL Air Tanzania Company Limited (ATCL) is a legal entity owned by the Government of the United Republic of Tanzania and established under section 4 (1) of the Air Tanzania Corporation (Re-Organization and Vesting of Assets and Liabilities) Act, Cap. 205 R.E of […]

This post Aviation Quality and Safety – Intern at ATCL has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Customer Service and Reservation -Intern at ATCL

Customer Service and Reservation (4 Positions) -Intern   OPPORTUNITIES FOR INTERNSHIP AT ATCL Air Tanzania Company Limited (ATCL) is a legal entity owned by the Government of the United Republic of Tanzania and established under section 4 (1) of the Air Tanzania Corporation (Re-Organization and Vesting of Assets and Liabilities) Act, Cap. 205 R.E of 2002 […]

This post Customer Service and Reservation -Intern at ATCL has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Cargo Sales -Intern at ATCL

 Cargo Sales (5 Position) -Intern   OPPORTUNITIES FOR INTERNSHIP AT ATCL Air Tanzania Company Limited (ATCL) is a legal entity owned by the Government of the United Republic of Tanzania and established under section 4 (1) of the Air Tanzania Corporation (Re-Organization and Vesting of Assets and Liabilities) Act, Cap. 205 R.E of 2002 and incorporated […]

This post Cargo Sales -Intern at ATCL has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Aircraft Maintenance -Intern at ATCL

Aircraft Maintenance (4 Positions) -Intern   OPPORTUNITIES FOR INTERNSHIP AT ATCL Air Tanzania Company Limited (ATCL) is a legal entity owned by the Government of the United Republic of Tanzania and established under section 4 (1) of the Air Tanzania Corporation (Re-Organization and Vesting of Assets and Liabilities) Act, Cap. 205 R.E of 2002 and incorporated […]

This post Aircraft Maintenance -Intern at ATCL has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger