Wednesday 12 May 2021

Waziri Mkenda Awataka Wakala Wa Mbegu Za Kilimo Kufufua Mashamba Yake Yote


 Waziri wa Kilimo Prof. Aldof Mkenda ameitaka Menejimenti ya Wakala wa Mbegu (ASA ) pamoja na Bodi mpya inayotarajiwa kupatikana hivi karibuni kufufua mashamba 13 ya kuzalisha mbegu bora na kuweka miundombinu ya umwagiliaji ili kuahakikisha yanazalisha kwa tija ili kuwasaidia Wakulima kupata mbegu bora; Kwa wakati na kwa bei nafuu.

Waziri Mkenda amesema jana Mei 11, 2021 Ofisi za Wizara ya Kilimo, Jijini Dodoma wakati akizungumza na Bodi ya Wakurugenzi ya (ASA) iliyomaliza muda wake pamoja na Menejimenti ya kuwa uzalishaji wa mbegu bora ni lazima uende sambamba na matumizi ya maji ili kuhakikisha mbegu zinazalishwa kwa bei nafuu.

Prof. Mkenda amesema uzalishaji wa mbegu bora kwa mwaka ujao wa fedha ni kipaumbele cha Wizara hiyo ni katika uzalishaji wa mbegu bora kupitia mashamba hayo ndio maana Wizara imeamua kuanzisha Mfuko Maalum wa Kilimo ambao unataraji kugharamia shughuli mbalimbali za maendeleo ya Sekta ya Kilimo, mbegu ni eneo moja wapo.

Waziri Mkenda amesema ili kuongeza tija Wakala wa Mbegu Bora za Kilimo (ASA) inatakiwa kufunga miundombinu hiyo ya umwagiliaji ili kuongeza tija kwenye upatikanaji wa mbegu bora.

“Tuyafufue mashamba yote 13 ya ASA na yafungiwe miundombinu ya umwagiliaji na kwa sababu Tume ya Maendeleo ya Umwagiliaji ipo chini ya Wizara ya Kilimo; Na tumeelekeza hakuna kuanzisha Mradi mpya wa umwagiliaji mpaka tuwe tumemaliza kujenga miundombinu ya umwagiliaji kwenya mashamba yote ya ASA.” Amesisitiza Waziri Mkenda.

Waziri Mkenda ameongeza kuwa njia pekee ya kuhakikisha maisha ya Watanzania yanakuwa bora ni kuongeza tija kwenye kilimo kwa kuhakikisha mbegu bora zinapatikana kwa bei nafuu ili Wakulima wazitumie kuzalisha kwa tija na kwa kufanya hivyo mazao ya chakula yatapatikana kwa wingi na kwa bei nafuu. Jambo hilo litachangia kupunguza gharama za maisha na kwa ajili hiyo. Wananchi wengi watanunua chakula kwa bei nafuu.

Waziri Mkenda amesema uzalishaji wa tija kwenye mbegu za mafuta utasaidia kupunguza matumizi ya fedha za kigeni kutokana na kuagiza mafuta ya kula kutoka nje ya nchi ambapo Serikali imekuwa ikitumia zaidi ya nusu tilioni kuagiza mafuta kutoka nje.

Pia Prof.Mkenda amesema kuwa ipo haja kwa Serikali kuwa msimamo unaoakisi kauli mbiu ya kilimo ni uti wa mgongo ili Wakulima walime kwa tija na kuondokana na umaskini miongoni mwao.

“Tunaweza kuwa kwenye uchumi wa kati na hata kufikia uchumi wa juu lakini wimbi la umaskini likaendelea kwa Wananchi na tukawa tegemezi wa chakula; Lakini pia hatuwezi kuwa na mageuzi ya viwanda bila kufanya mageuzi ya kilimo hususani katika suala la uzalishaji wa mbegu.” Amesisitiza Waziri Mkenda.

Hata hivyo amesema kuwa ni lazima mashamba yote ya ASA yafufuliwe kwa kuwa utegemezi wa mbegu kutoka nje ya nchi wakati mwingine hausaidii kilimo cha hapa nchini.

Awali Mwenyekiti wa Bodi ya ASA, Dkt. Ashura Kihupi amesema kuwa zipo kero kubwa kwenye Sekta ndogo ya Mbegu ni uwekezaji mdogo uliofanywa pamoja na mtaji mdogo kwa ajili ya kuzalisha mbegu.

Dkt. Kihupi ametoa mfano wa shamba la mbegu la Msimba lililopo Kilosa mkoani Morogoro; Kuwa uzalishaji umekuwa mdogo kwa sababu hakuna miundombinu ya umwagiliaji maji.


Share:

Majaliwa: Watendaji Sekta Ya Maji Fanyeni Kazi Wa Uzalendo

 


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka viongozi na watendaji wote wa sekta ya maji nchini kufanya kazi kwa uzalendo, bidii na weledi na kwa kutanguliza maslahi mapana ya nchi.

Amesema lengo ni kuhakikisha kuwa kiwango cha upatikanaji wa huduma ya maji nchini kinaongezeka ili kufikia malengo ya kufikisha maji kwa kiwango cha asilimia 85 Vijijini na asilimia 95 Mijini ifikapo mwaka 2025.

Ametoa kauli hiyo jana (Jumanne, Mei 11, 2021) wakati wa mkutano wa watendaji wa sekta ya maji uliofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango Jijini Dodoma.

Kadhalika, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwataka watendaji wa sekta maji nchini kushirikiana na wanajiosayansi kufanya tafiti za mara kwa mara zitakazotuwezesha kuwa na takwimu za uhakika kuhusu kiwango cha maji, mahali yalipo na ujazo wake.

“Kama nilivyotangulia kueleza kuwa maji ni chachu katika maendeleo ya viwanda nchini. Kwa mantiki hiyo, uwepo wa takwimu sahihi kuhusu upatikanaji wa maji ni muhimu katika kurahisisha na kuvutia uwekezaji wa viwanda kote nchini”

Aidha, Waziri Mkuu ameigiza Wizara ya Maji ishirikiane na Mamlaka za Serikali za Mitaa katika kusimamia vema na kwa uadilifu rasilimali fedha zinazotolewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji ili miradi iweze kukamilika kwa wakati na uwepo wa thamani ya fedha za walipa kodi.

Akizungumzia kuhusu uboreshwaji wa huduma ya upatikanaji wa majisafi na salama kwa wananchi waishio vijijini na mijini, Waziri Mkuu amesema “kufikia Machi 2021, jumla ya miradi 177 ya maji imeendelea kutekelezwa katika Miji Mikuu ya Mikoa, Miji Mikuu ya Wilaya, Miji midogo na Miradi ya Kitaifa. Tayari, miradi 67 imekamilika kwa gharama ya shilingi bilioni 759.211 na utekelezaji wa miradi 110 upo katika hatua mbalimbali”

Waziri Mkuu pia alikabidhi pikipiki 147 kwa ajili ya mameneja wa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Viijini, malori matatu ya kunyonya majitaka kwa halmashauri za miji ya Kahama, Tanga na Lindi.

Awali akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza, Waziri wa Maji Jumaa Aweso amesema kuwa hatakuwa na huruma na mtendaji yeyote atakayegundulika anahujumu miradi ya maji, lengo ni kuhakikisha watanzania wanapata huduma ya maji safi na salama wakati wote.

Amesema “Hatuwezi kukubali wakandarasi wasio na uwezo wa kufanya kazi, tutawapa kazi wakandarasi wenye uwezo wa kuwasaidia wananchi kupata huduma ya maji”

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Ummy Mwalimu amesema kuwa ataweka mazingira rafiki kwa RUWASA kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi ili kuhakikisha miradi yote maji inakamilika.


Share:

Rais Mwinyi Aishukuru Ofisi Ya Rais Utumishi Na Utawala Bora Kwa Ushirikiano Mzuri Na SMZ Katika Masuala Ya TASAF, MKURABITA Na Ajira

 Na. James K. Mwanamyoto-Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi ameishukuru Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuboresha maisha ya kaya maskini, urasimishaji ardhi, biashara na utoaji wa fursa za ajira kwa uwiano uliokubalika kwenye vikao vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na vikao vya mashirikiano vya Mawaziri kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzaia na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Mhe. Rais Mwinyi ameyasema hayo leo Ikulu ya Zanzibar alipokuwa akizungumza na ujumbe kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ulioongozwa na Waziri mwenye dhamana ya Ofisi hiyo, Mhe. Mohamed Mchengerwa.

Mhe. Rais Mwinyi amesema ni matarajio yake kuona ushirikiano huo ukiendelezwa na kuondoa changamoto za kiutendaji zilizopo ili wananchi wa Tanzania Bara na Zanzibar wanufaike na masuala yote yanayohusu MKURABITA, fursa za ajira na ruzuku inayotolewa na TASAF.

Kuhusiana na fursa za ajira kwa Wazanzibari, Rais Mwinyi amempongeza Mhe. Mchengerwa kwa utashi wake katika kusisitiza uzingatiaji wa makubaliano ya uwiano wa Ajira kwa taasisi za Muungano ambapo katika vikao vya Bunge ilikubalika kuwa Tanzania Bara iwe na asilimia 79% na Tanzania Zanzibar asilimia 21% ya nafasi za Ajira kila zinapotangazwa.

Akizungumzia suala la kujengeana uwezo kwenye mchakato wa ajira, Mhe. Rais amesema ni muhimu Zanzibar ikajifunza kutoka Bara kwa kuwa na kanzidata ya waombaji wa ajira ili fursa za ajira zinapotolewa iwe rahisi kuwapata watu sahihi wanaohitajika.

Akizungumiza melekezo ya Mhe. Rais Mwinyi, Mhe. Mchengerwa amesema, Ofisi yake imejipanga kuhakikisha suala la kubadilishana uzoefu kwa Watumishi wa Umma wa pande zote mbili litafanyiwa kazi.

Mhe. Mchengerwa ameongeza kuwa, atashirikiana na Waziri mwenye dhamana ya masuala ya Utumishi wa Umma Zanzibar kuhakikisha Watumishi wa Umma wanapata mafunzo ya kuwajengea uwezo kiutendaji ili waweze kutoa huduma bora kwa wananchi.

Tutajipanga vizuri kuhakikisha wataalam wa vyuo vya Utumishi wa Umma Tanzania Bara na Zanzibar wanakutana na kupanga namna bora ya kuwawezesha Watumishi wa Umma kupata mafunzo yenye tija katika utumishi wao.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Ladislaus Mwamanga amemueleza Rais Mwinyi kuwa, Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 112.87 kwa upande wa Zanzibar kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika Kipindi cha Pili cha Awamu ya Tatu.

Amefafanua kuwa, kiasi hicho kitatumika katika kutekeleza miradi ya kutoa ajira za muda, ikiwa ni pamoja na kuondoa mapungufu yaliyopo katika sekta ya elimu, afya na maji na kuongeza kuwa wazee wataendelea kupata ruzuku kama kawaida kwani hawana uwezo wa kushiriki katika miradi ya kutoa ajira za muda.

Naye Mratibu wa MKURABITA, Dkt. Seraphia Mgembe amesema urasimishaji wa biashara kwa upande wa Zanzibar umefanyika katika maeneo 8 ambapo wameweza kuwafikia wananchi kwa kutoa mafunzo na kusajili biashara zao ambapo watu 2926 wamepata leseni za biashara na utambulisho wa mlipa kodi ambao umewawezesha kuchangia pato la taifa kwa kulipa kodi.

Kwa upande wake Katibu wa Sekretarieti ya Ajira, Bw. Xavier Daudi amesema Ofisi yake iliyoko Zanzibar itahakikisha inatoa elimu kwa wahitimu ili waweze kupata taarifa sahihi zitakazowawezesha kuomba ajira zinazotangazwa.

Ameongeza kuwa, Ofisi yake hivi sasa imeanzisha dirisha litakalowawezesha waombaji wa fursa za ajira kupata taarifa za ajira, kuwasilisha maombi popote walipo na kupata mrejesho wa maombi yao.

Rais Mwinyi amekutana na ujumbe kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora uliolenga kutoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa upande wa Zanzibar.




Share:

Roketi zapiga mji wa Tel Aviv - Israel baada ya ghorofa kuharibiwa Gaza


Wanamgambo wa Kipalestina wanasema wamerusha makombora 130 katika mji wa Israeli wa Tel Aviv baada ya shambulio la anga la Israeli kuangusha ghorofa katika eneo la ukanda wa Gaza.

Jumba hilo la ghorofa 13- lilishambuliwa saa moja unusu baada ya wakazi na wenyeji wa eneo hilo kushauriwa waondoke, shirika la habari la Reuters liliripoti.

Jeshi la Israel linasema kuwa linalenga wanamgambo mjini Gaza kujibu shambulio la awali la roketi.

Watu 31 wameuawa baadhi yao katika ghasia mbaya zaidi zilizowahi kushuhudiwa katika miaka ya hivi karibuni.

Jamii ya kimataifa imetoa wito kwa pande zote mbili kukomesha mapigano, yaliyofuatiwa na siku kadhaa za ghasia mjini Jerusalem.

Wanamgambo walikuwa tayari wafyatua mamia ya maroketi kuelekea upande wa Jerusalem na maeneo mengine.

Watu watatu wameuawa katika maeneo ya Israeli huku Wapalestina 28 wakiuawa kwa makomboro ya Israel.

Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu awali ailisema kundi kubwa la wanamgambo, Hamas, “limevuka mpaka” kwa kurusha maroketi kuelekea Jerusalem kwa mara ya kwanza ndani ya miaka kadhaa.

Hamas, ambayo inadhibiti Gaza, inasema imechukua hatua hiyo kulinda msikiti wa al-Aqsa mjini Jerusalem dhidi ya “ dhalimu na ugaidi” wa Israel baada ya eneo hilo, takatifu kwa Waislamu na Wayahudi, kukumbwa na makabiliano kati ya polisi wa Israeil na Wapalestina siku ya Jumatatu na kusbabisha mamia kujeruhiwa.

 

Credit:BBC



Share:

Branch Manager – Stone Town, Zanzibar at KCB

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Summary: The role holder is responsible for overall leadership of the branch to achieve growth, profitability and customer service excellence whilst ensuring implementation of an effective risk management framework through efficient utilization of resources. Job Details: Key Responsibilities Achieve profitability targets through revenue maximisation and prudent cost management. Grow and monitor branch’s liability and […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Training Centre Administrator at Sustainable Agriculture Tanzania

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Training Centre Administrator alias Hotel Manager We are looking for an experienced Training Centre Administrator with experience in Hotel Management. As our Training Centre Administrator, you will oversee the daily operations of our Centre and provide strategic direction. You will plan and supervise the activities of an extensive and diverse workforce to ensure the smooth and […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Construction Supervisor at Sustainable Agriculture Tanzania

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Description We are looking for an experienced, driven Construction Supervisor with construction experience. To ensure success, the ideal candidate should be comfortable splitting their hours between the office, on-site visits and engaging the communities. The Construction Supervisor plans and oversees the construction site. They lead crews, ensure safety regulations and health codes are observed, […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Technical Operator-Brewing at Serengeti Breweries

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

About us From Arthur Guinness to Johnnie Walker, our business was founded on people of great character, and in 250 years, nothing’s changed. We’re the world’s leading premium alcohol company. Our brands are industry icons. And our success is thanks to the strength of our people, in every role. It’s why we trust them with […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Cash and Trade Specialist at Citi Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Overview Acting as the functional heart of our business, Operations makes everything work on time and on target, in a world that demands lightning-fast transaction speeds, pinpoints execution accuracy and full visibility. It ensures global transactions flow smoothly around the clock, wherever we do business. Without it, the daily clearance, settlement and execution of a […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Junior Process Engineer/ CCR Operator at dangote

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Description · Monitor various sections of the production line from the Central Control Room (CCR) To ensure precision and adherence to standards in the cement production process. · Provide relevant information and direction to patrollers and operators in the production line based on monitored operations in liaison with the shift coordination · Assist in implementing […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Senior Mechanical Engineer at dangote

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Description Operation & maintenance expert for pertaining to the mechanical equipment for production of cement like vertical roller mills and reclaimers. Lead the team of engineers for supervision of maintenance and timely completion of maintenance activity. To ensure the standard of quality standard are followed during maintenance work. Planning and implementing preventive & breakdown maintenance […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

KAMPUNI YATANGAZA NAFASI ZA KAZI ZA KULALA

Kampuni moja nchini Marekani ambayo hutoa vidokezo vya usingizi imetangaza nafasi za kazi ya weledi wa usingizi sawa na takribani shilingi Milioni 3.3. za Tanzania.

Kampuni ya Eachnight imesema inawatafuta watu wa kujiunga na kikosi cha utafiti kama weledi wa kulala kubaini umuhimu wa usingizi na hasara yake. 

"Kwa sasa tunaajiri kikosi cha watu watano ambao watakuwa weledi wa usingizi na kulipwa kulala! Pia hatufanyi matani," ilisema kampuni hiyo kwenye tovuti yake. 

Kampuni hiyo iliwaomba wale ambao wangelipenda kuwa sehemu ya utafiti huo kuwasilisha maombi yao mtandaoni kabla ya Mei 31, 2021. 

Watakaofaulu kupata kazi hiyo watalipwa KSh 159,000 na wataanza punde baada ya kuchaguliwa kwa kipindi cha siku 30 za utafiti huo. Watakaotuma maombi ni lazima walale pekee yao wakati wa kipindi hicho ili kuhakikisha kuwa usingizi wao haukatizwi.

Wakati wa utafiti huo, watafiti watabaini muda mwafaka wa kulala na athari za kulala sana hadi kuchoka. 

Mambo mengi watakayozingatia ni athari za usingizi kwa kumbukumbu, motisha na tija Kama sehemu ya utafiti na kufaulu kwake, kutakuwa na simu za video baada na wakati wa utafiti na kuulizwa maswali ya moja kwa moja ambapo weledi wa usingizi wataelezea ushuhuda wao.

CHANZO - TUKO NEWS


Share:

Junior Instrumentation Engineer at dangote

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Description Job Summary Installation, Testing, Operation & Maintenance, Trouble shooting of Instrumentation equipment’s. Responsible for trouble free operation of assigned area to achieve optimum reliability and availability of equipment’s. Job planning and execution. Maintains the maintenance records of equipment. Implementation of safety measures and compliance of safety guide lines. Material management of assigned area for […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

TEAM LEADER PACKAGING at Coca-Cola Kwanza

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Reference Number CCB210511-1 Job Title TEAM LEADER PACKAGING Function Manufacturing Company Coca-Cola Kwanza (Tanzania) Job Type Permanent Location – Country Tanzania Location – Province Not Applicable Location – Town / City Dar es Salaam Job Description Coca-Cola Kwanza Ltd has an exciting opportunity in Manufacturing Department. We are looking for a talented individual with the […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

MWANACHAMA WA USHIRIKA ANUFAIKE NA MIRADI YA USHIRIKA- MRAJIS

 

Mrajis na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt. Benson Ndiege (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa chama cha Ushirika Mahenge Amcos Julius Mbunda (kushoto) kuhusu mradi wa Shule unaojengwa na Chama hicho wengine pichani ni Afisa Ushirika pamoja na viongozi wa Chama Kikuu cha Ushirika MBIFACU, Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma hivi karibuni

Mrajis na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt. Benson Ndiege (katikati) akipata maelezo kutoka kwa katibu wa chama cha Ushirika Kimuli Amcos Ernest Komba (kushoto) kuhusu mtambo wa kuchakata kahawa kulia ni Mrajis Msaidizi wa Mkoa wa Ruvuma Bumi Masuba, Mbinga Mkoani Ruvuma

Mrajis Msaidizi wa Mkoa Bumi Masuba akieleza jambo wakati wa mafunzo elekezi ya Ushirika kwa Viongozi wapya wa Vyama vya Ushirika wa vinavyosimamiwa na Chama Kikuu cha Ushirika MBIFACU, mafunzo yaliyofanyika Mbinga Mkoani Ruvuma



Washiriki wa mafunzo elekezi ya Ushirika kwa Viongozi wapya wa Vyama vya Ushirika wa vinavyosimamiwa na Chama Kikuu cha Ushirika MBIFACU wakifuatilia mada na majadiliano ya mafunzo, Mbinga Mkoani Ruvuma.


Na.Mwaandishi Wetu,Mbinga, Ruvuma

Vyama vya Ushirika vimepewa wito wa kuendesha Miradi na mali za Vyama vya Ushirika kwa maslahi ya wanachama wa Vyama vya Ushirika ili wanachama waweze kunufaika na miradi hiyo kwa lengo la kuendeleza na kuimarisha umoja wa wanaushirika.

Wito huo umetolewa na Mrajis wa Vyama vya Ushirika na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt. Benson Ndiege Mei 11, 2021 wakati alipotembelea miradi ya mbalimbali ya Chama Kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Kahawa cha Mbinga (MBIFACU) ikiwemo Mbicu hoteli, mashamba ya kahawa, pamoja na miradi ya shule na maghala ya vyama vya msingi vya MBIFACU wilayani Mbinga, mkoani Ruvuma

Mrajis ameeleza kuwa ni muhimu wanachama kuwa na uhusiano wa moja kwa moja na miradi inayoendeshwa na Vyama vyao vya Ushirika kuanzia ile miradi inayoendeshwa na Vyama vya msingi pamoja na vyama vikuu ili kuhakikisha wanachama wanakuwa na umiliki wa miradi hiyo pamoja na kupata faida zitokanazo na miradi hiyo.

“Ni lazima Vyama Vikuu na Vyama vya Msingi vyote vihakikishe kuwa vinaendesha na kuendeleza miradi hii kwa maslahi ya wanachama wake ili mwanachama anufaike na uwekezaji unaofanywa na chama chake na mwanachama awe ni sehemu ya mradi wa huo,” alisisitiza Mrajis

Akielezea umuhimu huo Mrajis alibainisha kuwa mwanachama anaweza kuwa na umiliki na miradi kupitia njia ya hisa za miradi ya hoteli, mashamba, viwanda zinazoweza kuuzwa na Vyama vya Ushirika kwa wanachama wake ambapo wanachama watakuwa wanapata gawio la faida zinazopatikana na miradi hivyo mwanachama kunufaika na miradi ya vyama. 

Pamoja na kuangalia uwezekano wa faida za miradi kupunguza gharama za uendeshaji za vyama ili kutoa nafuu ya huduma kwa wanachama wake.

Akiongeza kuwa vyama viangalie hata katika miradi ya Shule vyama vinaweza kuweka viwango nafuu vya ada kwa watoto wa mwanachama. 

Jambo ambalo litafanya Jamii kuwa sehemu ya mradi na pia kuvutia wengi zaidi kuwa wanaushirika. 

Hivyo, amevitaka vyama vya Ushirika kwa kushirikiana na wadau kuongeza ubunifu huduma za Ushirika na kueleza Serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa Vyama katika hatua mbalimbali za kuboresha na kuimarisha huduma bora kwa wanachama wa Ushirika.

“Ili mwanachama wa Ushirika aweze kujivunia chama chake lazima kuwe na huduma za ziada anaweza kuzipata katika chama chake hii ni pamoja na masoko, pembejeo, bima za afya, pensheni kwa kufanya hivyo mwanachama atakuwa mlinzi wa kwanza wa mali na miradi ya chama,” alisema Mrajis

Pamoja na mambo mengine Mrajis amevitaka Vyama vya Ushirika kuwa na mipango ya uwekezaji inayotoa dira na kuelekeza shughuli za miradi ya maendeleo ya Vyama ya muda mfupi na muda mrefu ili kuhakikisha chama kinaendeshwa kwa utaratibu maalum uliopangwa na kuridhiwa na wanachama wake kupitia mikutano mikuu ya wanachama.

Katika hatua nyingine, Mrajis amewataka viongozi na wajumbe wa Bodi wapya wa Vyama vya msingi vya vinavyosimamiwa na Mbifacu waliokuwa wakipata mafunzo elekezi ya uendeshaji wa Vyama vya Ushirika yaliyokuwa yakiendeshwa na Tume ya Maendeleo ya Ushirika kuhakikisha kuwa wanafikisha elimu ya ushirika kwa wanachama wao.

 Akisisitiza lazima viongozi wa Ushirika kujiwekea mipango ya mafunzo kwa wanachama wanaporudi kwenye vyama vyao.

Mafunzo hayo yalihusisha wadau mbalimbali wanaoshirikiana kwa karibu na Sekta ya Ushirika ikiwemo Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Shirika la Ukaguzi wa Vyama vya Ushirika (COASCO), Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mada zilizoelezwa kutolewa ni masuala ya misingi ya Ushirika, uandishi sahihi wa vitabu, uandaaji wa makisio, maadili na uadilifu katika uendeshaji wa Vyama.

Kwa upande wake mshiriki wa mafunzo hayo Winfrida Kapinga amesema mafunzo elekezi yanaenda kuongeza tija katika utendaji wao kama viongozi hasa kwa kuzingatia misingi ya Ushirika, uadilifu na maelekezo ya wataalamu ili kuepusha migogoro katika Vyama. 

Akizungumzia katika vyama vya Ushirika, Winfrida ameeleza kuwa atatumia fursa hiyo kama kiongozi kwenda kuwaelimisha na kuhamasisha wanawake kushiriki katika nafasi za uongozi zinazojitokeza katika vyama pamoja na shughuli za uzalishaji mali wa vyama vya ushirika ili kuondoa utegemezi na umasikini

Share:

UBALOZI WA PALESTINA NCHINI TANZANIA UNAANGAZIA UHALIFU WA ISRAELI DHIDI YA WATU WA PALESTINA


 
Ubalozi wa Palestina nchini Tanzania unaangazia uhalifu wa Israeli dhidi ya watu wa Palestina katika Yerusalem ya Mashariki iliyoko chini ya ukoloni na ukalizi wa Israeli.

Yerusalemu ya Mashariki ni sehemu muhimu ya nchi ya Palestina. Tangu kukaliwa kwake na ardhi kuporwa kutoka kwa Wapalestina kinyume na sheria za kimataifa mnamo mwaka 1967, Israeli imeweka lengo na utaratibu wa kubadilisha hali ya kisheria ya jiji, kudhibiti na kubadilisha muundo wa idadi ya watu waishio hapo.

Kupitia sera za kibaguzi na kwa kukiuka sheria Za Kimataifa kama ilivyoelezewa na ripoti ya Haki za Binadamu, iliyotoka hivi karibuni; Israeli ina nia ya kuunda kwa makusudi, ukweli mpya juu ya ardhi ya Wapalestina. Kuwezesha hilo, Israel imekuwa ikihamisha maelfu ya mamia ya watu wa Palestina kwa nguvu na kuwaondosha katika makazi yao ya miaka mirefu na kisha kuikabidhi kwa walowezi wa Israeli. Zaidi ya walowezi 200,000 wanaishi katika makazi haramu mjini humo, Mashariki ya Yerusalem. Israel yaendelea na upanuzi wa makazi haya katika ardhi ya Wapalestina kama ilivo sasa katika mtaa wa Sheikh Jerrah huko mjini Yerusalemu ya Mashariki ampapo famia saba za Wapalestina zalazimishwa kuondoka katika makazi yao.

HalikadhalikaIsraeli katika harakati zake kuufanya mji wa Yerusalemu kuwa mji wa Kiyahudi hufanya mashambulio yake ya kimfumo dhidi ya waumini wa Palestina wa dini za Kikristo na Kiislamu. Jeshi la Israeli limekuwa likivamia na kushambulia waamini wa Kikristo na Kiislamu hasa katika sherehe zao za dini mjini Yerusalemu mashariki. Wanajeshi wa Israeli mara kwa mara huzuia waumini wa Kiislamu wa Palestina kuingia ndani ya msikiti wa Al – Aqsa kwa ajili ya sala

Kulingana na ripoti ya Human Rights Watch ambayo ilichapishwa mnamo mwezi Aprili mwaka huu, Israeli inaendelea kuonyesha ukandamizaji na vitendo visivyo vya kibinadamu dhidi ya watu wa Palestina kwa nia ya kudumisha utawala wa kikabila unaowapa ukuu Wayahudi juu ya Wapalestina.

Ripoti hiyo ilihitimisha kwa kusema kuwa, Israeli inatekeleza utawala katili wa ubaguzi wa rangi ambao umesababisha miaka 54 ya ukoloni na makazi haramu katika ardhi ya Palestina na hivyobasi kukiuka sheria na maazimio ya Umoja wa Mataifa.

Ubalozi wa Palestina nchini Tanzania unaangazia msimamo wa serikali ya Palestina kuhusu unyama huu unaofanywa na Israeli dhidi ya Wapalestina.

Akiongea na waandishi wa habari hivi leo, Balozi wa Palestina nchini Mh. Hamdi Mansour AbuAli ameitaka jumuiya ya kimataifa kutokaa kimya mbele ya uhasama na ukatili huu unaotendeka dhidi ya Wapalestina katika ardhi yao. Balozi amesema kuwa huu ni wakati muafaka kwa hatua ya kimataifa kutumia njia na hatua zinazoelezwa na sheria za kimataifa na hatimaye kuifanya Israeli na mashirika ya walowezi kuwajibika kwa ukiukaji wao na uhalifu dhidi ya watu wa Palestina.
Share:

Tuesday 11 May 2021

WAZIRI AOMBA RADHI...SASA MECHI YA SIMBA SC Vs YANGA KUPANGWA UPYA...MASHABIKI KUPEWA TIKETI UPYA

Hatimaye Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kutoa taarifa za kina juu ya sakata hilo, imeweka wazi taarifa rasmi kuhusu sakata la kuahirishwa kwa mechi namba 208 ya Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL) kati ya Watani wa Jadi Simba na Yanga iliyotakiwa kuchezwa Mei 8 katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa, amezitaka mamlaka za serikali zinazohusika na masuala ya tiketi kuhakikisha zinawapatia tiketi upya mashabiki takribani 43,000 waliokuwa wamekata tiketi.

Aidha ameagiza mamlaka za soka ikiwemo Bodi ya Ligi na TFF, kupanga upya tarehe ya mechi ya Simba SC vs Yanga.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger