Wednesday 21 April 2021

WEZI WAVUNJA KANISA NA KUIBA NGUO ZA NDANI ZA PASTA

Waumini wa Kanisa la Makutano PAG eneo la Lurambi, Kakamega nchini Kenya wanahesabu hasara baada ya wezi kuvunja kanisa hilo na kuiba mali yenye thamani isiyojulikana. 

Kiongozi wa akina mama katika kanisa hilo Mama Prisca Orembo amesema walipata habari kuhusu tukio hilo Jumapili, Aprili 18,2021.

 “Tulifahamishwa kwamba kuna tukio kanisani na tulipofika hapo tulithibitisha ni kweli, wezi walivunja mlango wa kanisa na katika makazi ya mchungaji," Mama Prisca Orembo alinukuliwa na Citizen. 

Duru zinaarifu kwamba wezi hao waliiba mali kadhaa ikiwemo nguo za ndani za pasta na chakula chake jikoni.

 “Wezi hata wanaiba nguo za ndani za pasta wanaenda kuuza, hii ni nini?" alisema Wycliffe Sajida, ambaye ndiye pasta wa kanisa hilo.

 Pasta huyo alisema alipoteza kila kitu wakati wa kisa hicho.

“Walichukua suti mbili, mashati matano, viatu, mtungi wa gesi, nguo za kuhubiri na KSh. 2,500,” pasta Wycliffe alisema.

 Waumini wa kanisa hilo sasa wanataka idara ya polisi eneo hilo kuchukuwa hatua na kuwasaka wezi hao. 

CHANZO - TUKO NEWS

Share:

AKAUNTI ZA BENKI ZA MTANDAO WA WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU 'THRDC' ZAFUNGULIWA


Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umesema akaunti za benki za mtandao zilizofungwa kwa takribani miezi minane zimefunguliwa.

THRDC imetoa shukrani kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake unaojali na kuzingatia haki za binadamu na utawala bora.

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumatano Aprili 21, 2021 na bodi ya mtandao huo na kutoa shukrani kwa wahisani, taasisi mbalimbali na wanachama walioshiriki kwa namna mbalimbali kuhakikisha mtandao unaendelea kutekeleza majukumu yake pia kuhakikisha kuwa changamoto husika zinatatuliwa.

Taarifa hili imeeleza kuwa kufunguliwa kwa akaunti hizo kumetokana na maelekezo kutoka kwa mamlaka za Serikali zilizoagiza kufungwa ili uchunguzi wa tuhuma ufanyike na kisha kutoa maelekezo kuwa zifunguliwe.

Via MWANANCHI
Share:

WASANII KUTUMIA BURE AKAUNTI ZAO BINAFSI YOUTUBE ....WATAKIWA KUACHA KIKI

 Na Grace Semfuko, MAELEZO, Dar es Salaam, Aprili 20, 2021

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi amesema Wizara yake, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, pamoja na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), wameshakubaliana kubadilisha Kanuni ili wasanii na wadau wengine wa maudhui yasiyohusisha uchakataji wa habari waweze kurusha kazi zao kwenye akaunti zao binafsi za YouTube bila kufanya usajili na malipo kwa TCRA.

 

Akizungumza na Viongozi wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) na vyama vinavyounda shirikisho hilo Jijini Dar es Salaam leo, Dkt. Abbasi amesema hatua hiyo imekuja kufuatia kuona umuhimu wa kuwanufaisha Wasanii na kukuza Sanaa nchini.

 

 “Tumefanya mazungumzo na wenzetu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari pamoja na TCRA kuhusu maudhui ya Tv  za mtandaoni, tumeona kuna tofauti kubwa sana kati ya Habari na Sanaa, hivyo tutaboresha kanuni, tumeona eneo hili la Wasanii linapaswa kufanya kazi zao bure, sasa nafurahi kuwaambia kuwa kuanzia sasa wasanii wawe wa muziki au filamu changamoto hii imefika mwisho," amesema Dkt Abbasi.

 

Kuhusu maslahi ya kazi za Wasanii zinazorushwa kupitia vyombo mbali mbali vya habari, Dkt. Abbasi amesema, Wizara yake kupitia taasisi zinazosimamia Wasanii ikishirikiana na TCRA wanaendelea kupitia na kuanzisha mfumo wa kuangalia namna ya kazi zao zinavyorushwa kwenye vyombo hivyo ili waweze kulipwa kwa jinsi zinavyorushwa.

 

“Wizara kupitia Taasisi ya Haki Miliki Tanzania (COSOTA) na wenzetu wa TCRA tunaendelea kukamilisha mfumo wa kuangalia namna ya kazi zenu zinavyoenda katika vyombo vya habari, mfumo huu unalenga kuwanufaisha Wasanii na tayari TV na Redio nyingi wamekubaliana na jambo hili,” amebainisha Dkt Abbasi.

 

Aidha aliwataka Wasanii kutumia maeneo na mazingira ya uhalisia wakati wa kurekodi kazi zao ikiwa ni pamoja na kutangaza miradi ya ajenda za kitaifa lengo likiwa ni kutafuta fursa za wageni kutembelea maeneo hayo ili kukuza uchumi wa taifa kupitia utalii.

 

“Tuna miradi mikubwa tunaifanya hapa nchini na kwenye hifadhi zetu za wanyama na kwingineko mnakodhani ni vizuri mkatangaza, tumieni "location" kama zile kutangaza fursa za utalii katika nchi yetu” amesema.

 

Wakati huo huo Dkt. Abbasi amewataka Wasanii ‘kuacha kiki’ na kutumia taaluma zao vizuri katika kutangaza kazi zao badala ya kuchafuana kwenye mitandao ya kijamii na kueleza kuwa kwa kufanya hivyo wanaondoa uaminifu kwa jamii ambao wameujenga kwa gharama kubwa.

 

“Wote mmeona yaliyokuwa yakiendelea kwenye mitandao ya kijamii siku za karibuni, sasa ile inaua sanaa, leo hata makampuni yaliyoanza kuwa na imani kibiashara na wasanii wameanza kusita tena, heshimuni sanaa ni maisha ya wengi na hii itawajengea heshima badala ya kutumia kiki za kuchafuana” ameongeza Dkt. Abbasi.

Share:

Global Risk Manager at Pathfinder International

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Details Description Pathfinder Overview Pathfinder International is driven by the conviction that all people, regardless of where they live, have the right to decide whether and when to have children, to exist free from fear and stigma, and to lead the lives they choose. Since 1957, we have partnered with local governments, communities, and […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Jobs at NGARA District Council

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Various Jobs at NGARA District Council April, 2021. Ngara District is one of the eight districts of the Kagera Region of Tanzania. It is bordered to the north by Karagwe District, to the east by Biharamulo District, to the south by the Kigoma Region, to the northeast by Muleba District and to the we   […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Field Officers (18 Posts) at Ifakara Health Institute

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Summary Position:          Field Officers (18 Posts) Reports to:  Research Officer/Project Leader Work station:    Tanga District (Tanga Municipality), Kaliua District (Tabora) and  Sengerema District (Mwanza) Apply by: April 23rd 2021 Institute overview  Ifakara Health Institute (IHI) is a leading research organization in Africa with a strong track record in developing, testing and validating innovations for health. […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Technology Procurement & Asset Manager at NBC

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Job Summary The role is responsible to ensure that new and existing IT Assets and Services are procured and renewed cost-effectively. It will also ensure […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Programme Finance Assistant at UNCDF

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Eligibility criteriaCandidate age: between 18 and 29 throughout the entire duration of their assignment. Applicants must be nationals of or legal residents in the country of assignment.  Description of task Assist in financial management activities of the office – 25% Support the preparation of the various financial reports based on our reporting calendar. Ensure that […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Senior Finance and Admin Manager at REDESO

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

About REDESO: Relief to Development Society (REDESO) is a Tanzanian National Non-Governmental Organization dully registered under the Society Ordinance of 1954 with registration number S.O. No. 9459. The organization is engaged in Humanitarian and Community Development projects implemented under the humanitarian to development nexus concept. In the areas of our operation, Local Government has been […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Deputy Director Finance at International Rescue Committee

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Requisition ID: req14307 Job Title: Deputy Director Finance Sector: Finance Employment Category: Fixed Term Employment Type: Full-Time Open to Expatriates: Yes Location: Dar es Salaam, Tanzania Job Description The International Rescue Committee responds to the world’s worst humanitarian crises and helps people whose lives and livelihoods are shattered by conflict and disaster to survive, recover and gain control of their future. We […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Inventory and Asset Assistant at ICAP

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job no: 495106 Work type: Regular Full-Time Location: Tanzania – Dar es Salam Categories: Finance/Administration ICAP at Columbia University, a global health leader situated within the Columbia University Mailman School of Public Health in New York City, seeks Inventory and Asset Assistant  to be based in Dar es Salaam, Tanzania. Inventory and Asset Assistant with safety, efficiency and customer […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Information System (IS) Specialist at Médecins Sans Frontières

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

   JOB VACANCY – INFORMATION SYSTEM (IS) SPECIALIST     Médecins Sans Frontières (MSF) is an international, independent, medical humanitarian organisation that delivers emergency aid to people affected by armed conflict, epidemics, natural disasters and exclusion from healthcare. MSF offers assistance to people based on need, irrespective of race, religion, gender or political affiliation. MSF […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Commercial Specialist at U.S. Embassy Dar es Salaam

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

The U.S. Mission in Dar es Salaam is seeking eligible and Qualified applicants for the position below. Position Title: Commercial Specialist Vacancy Number: DaresSalaam-2021 -018   Duties 25% – Trade facilitation through business matchmaking, including identifying potential partners (incl., distributors, agents, etc.) The incumbent identifies potential distributors, representatives, joint venture partners, or other professional contacts […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRILI 21,2021












Share:

Tuesday 20 April 2021

Naibu Waziri Masauni Awataka Vijana Kuchangamkia Fursa Za Uchumi Wa Blue Zanzibar


Na Benny Mwaipaja, Zanzibar
NAIBU Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amewahimiza vijana Visiwani Zanzibar kuchangamkia fursa za uchumi wa blue unaotokana na shughuli za uvuvi na uchakataji wa samaki ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Mhe. Masauni ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni-Zanzibar, ametoa rai hiyo wakati akizungumza na viongozi na baadhi ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi katika Jimbo la Kikwajuni akiwa katika ziara yake ya kikazi visiwani humo.

Amesema kuwa yeye binafsi na Mwakilishi wa Jimbo hilo katika Baraza la Wawakilishi Mhe. Nasor Ali Jazeerah pamoja na viongozi wengine wamejipanga kutoa vifaa vitakavyotumiwa na vijana kwa ajuili ya shughuli za uvuvi katika sekta hiyo ya uchumi wa blue ili waweze kujitegemea kwa kujipatia kipato cha uhakika.

“Tunataka tuangalie uwezekano wa kujenga mazingira mazuri ya kuwatafutia “ndoano” na siyo “samaki” na tumeandaa vitu vikubwa ambavyo sitaki niseme mapema hapa nitaondoa radha, mkawaambie vijana wa Kikwajuni kama hawatatoka kimaisha kipindi hiki hawatatoka maisha” alilisisitiza Mhe. Masauni.

Pamoja na kusisitiza masuala ya kiuchumi, Mhandisi Masauni alisema kuwa mipango mingine iliyowekwa na uongozi katika Jimbo la Kikwajuni ni kuendesha mashindano ya kusoma qoran kwa vijana na kuwataka wazazi kuwahimiza watoto wao kushiriki mashindano hayo.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Jimbo hilo Mhe. Nasor Ali Jazeerah, aliwaahidi wakazi wa Jimbo la Kikwajuni-Zanzibar kwamba ahadi zote zilizoahidiwa wakati wa Uchaguzi Mkuu uliopita zitatekelezwa kikamilifu.

Alitoa wito kwa wakazi wa Jimbo hilo kushikamana, kupendana na kuacha majungu ili mipango ya maendeleo iliyopangwa iweze kutekelezwa kwa kasi zaidi.

Aliwashukuru wananchi kwa kumwombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ili waendelee kuingoza nchi kwa umahili mkubwa.

Mwisho.


Share:

Dkt. Kalemani : Marufuku kuuza mafuta yasiyo na vinasaba


 Na Zuena Msuya Dodoma,
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amepiga marufu uuzaji wa mafuta ya Petroli, Dieseli, na Mafuta ya Taa yasiyo na vinasaba unaofanywa na baadhi ya wafanyabiashara nchini.

Dkt. Kalemani alitoa maagizo hayo Jijini Dodoma wakati wa ziara yake ya kushtukiza ya kukagua vinasaba kwenye mafuta yaliyopo katika vituo vya kuuzia mafuta mkoani humo, iliyofanyika Aprili 20, 2021.

Katika ziara hiyo aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Leonard Masanja, Naibu Katibu Mkuu, Kheri Mahimbali na Kamishna wa Petroli na Gesi, Adam Zuberi wa wizara hiyo, pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka wa Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji nchini( EWURA),Mhandisi Godfrey Chibulunje.

Dkt. Kalemani Alisema kuwa vinasaba vinadhihirisha viwango na ubora wa mafuta nchini.

“Maelekezo yangu kwa wauzaji wa mafua nchini ni lazima muendelee kuuza mafuta yenye vinasaba kwa sasa ili kujiridhisha na kiwango na ubora wa mafuta nchini, na kama mafuta hayana vinasaba ni marufuku kuyachukuwa na kuuza, kuna minong’ono katika baadhi ya maeneo kuwa kuna mafuta yanayouzwa ya aina hiyo, tutakayembaini tutachukua hatua stahiki”, alisema Dkt. Kalemani.

Katika ziara hiyo, hakuna kituo hata kimoja kilichobaininika kuuza mafuta yasiyo na vinasaba.

Alieleza kuwa kwa sasa Shirika la Viwango nchini (TBS), ndiyo llililopewa kazi ya kupima na kuweka vinasaba katika mafuta yote yanayoingia nchini ili kudhibiti ubora na tayari kazi hiyo imeanza kufanyika.

Alisisitiza kuwa kuanzia sasa mafuta yote nchini yatakuwa yakipimwa na kuwekwa vinasaba na TBS na ikibainika kuna mafuta ambayo hana vinasaba hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watendaji husika.

“TBS ni chombo cha serikali, kinachofanya kazi ya kudhibiti ubora na viwango ikiwepo wa mafuta nchini hivyo kuanzia sasa ndiyo kifanya kazi ya kupima na kuweka vinasaba kwenye mafuta yote nchini, endapo atatokea mwingine mtaelekezwa na serikali”, alisisitiza Dkt. Kalemani.

Lengo la serikali kuipa TBS kazi ya kuweka vinasaba katika mafuta yote nchini ili kuokoa fedha za serikali zaidi ya shilingi bilioni tatu kwa mwezi ambazo awali alikuwa akilipwa aliyekuwa akifanya kazi hiyo.

Vilevile ni kuijengea uwezo taasisi hiyo na kuongeza ajira kwa watanzania.

Katika ziara hiyo, aliitoa maelekezo kwa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Wizara ya Maji kuwachukulia hatua waafisa wawili katika idara ya manunuzi wa Mamlaka wa Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji nchini( EWURA), pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Manunuzi wa taasisi hiyo kwa kushindwa kutekeleza maelekezo ya serikali kwa wakati.

Dkt. Kalemani alisema kuwa watumishi hao, hawakutekeleza maagizo ya serikali yaliyotolewa tangu Februari 5, 2021, kwa sababu zao wenyewe, pia wachunguzwe kwa nini hawakutekeleza maagizo hayo, na kusababisha migogoro.


Share:

MGANGA ARUDISHA PESA BAADA YA NDUMBA ZAKE KUFELI KUNASA MCHEPUKO UNAOPAKUA ASALI YA JAMAA


Mganga kutoka Kathwana, Tharaka Nithi nchini Kenya aliyepokea kitita cha KSh 200,000 kutoka kwa jamaa flani ili amtengenezee dawa ya kumkomesha barobaro aliyezoea kuchepuka na mkewe amelazimika kuzirejesha pesa hizo baada ya dawa yake kutofanya kazi. 

Duru zinaarifu kwamba mzee alikuwa amechoka na tabia ya mkewe aliyempenda sana kugawa asali nje.

Kwa mujibu wa Taifa Leo, mzee huyo hakutaka kumkabili jamaa kwa kuwa alikuwa pandikizi la mtu ambaye angempokeza kichapo cha mbwa. 

Badala yake mzee aliamua kwenda kutafuta huduma za mganga ambapo alitoa donge nono la shilingi elfu mia mbili pesa taslimu.

 Inasemekana mganga alistaajabu kwani katika maisha yake ya huduma kwa wateja hajawahi pata kiasi kama hicho cha pesa.

“Mwanangu usiwe na shaka. Hapa ni maskani ya fundi. Hili suala litashughulikiwa kikamilifu. Halipo hata moja moja lilishawahi kunipiga chenga. Huyu lofa wako atakula nyasi. Wewe kamata hii dawa, uipake blanketi ambalo wawili hao hujifunika pindi wawapo kwenye gemu. Nakuhakikishia nyasi atazila,” mganga alijigamba.

 Mzee alirudi nyumbani akiwa mwingi wa matumaini kuwa dawa ya kutuliza mkewe aache kuruka ruka nje ya ndoa.

 Inaarifiwa kwamba pindi tu mama watoto alipoondoka, mzee alichukua dawa hiyo na kuinyunyiza kwenye blanketi na akasubiri kuona matokeo.

Hata hivyo siku iliyofuata nusra mzee azirai alipowafumania mke na mchepuko wake wakibarizi sebuleni baada ya kumaliza raundi tatu za mechi.

 Jamaa hakuingiwa na baridi kwani tayari alikuwa amezoea kupakua asali hata mzee wa nyumba akiwa karibu. 

Mzee aliingia kwenye gari lake moja kwa moja na kufululiza hadi kwa mganga huku akiwa na hasira.

 “Nipe hela zangu sasa. Zitoe hela zangu au nikutoe utumbo,” mzee alimuungurumia mganga. 

Mpiga ramli ambaye alikuwa na mipango ya kujenga nyumba hakuwa na lingine ila kuzitwaa hela hizo alizokuwa amezificha chini ya godoro akamrejeshea mzee.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger