Sunday 28 February 2021

MBUNGE KEMBAKI :HATA TUKIVAA BARAKOA KAMA MUNGU HAYUPO PAMOJA NA SISI NI BURE


Aliyenyoosha mkono ni Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato mtaa wa Majengo wilayani Tarime akifanya maombi maalumu kumwombea Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini Michael Kembaki (aliyevaa tai nyekundu). Picha na Dinna Maningo
Aliyenyoosha mkono ni Mchungaji wa kanisa la Waadventista Wasabato mtaa wa Majengo wilayani Tarime akifanya maombi maalumu kumwombea Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini Michael Kembaki (aliyevaa tai nyekundu).
Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini Michael Kembakiakizungumza na waumini wa kanisa la Waadventista Wasabato mtaa wa Majengo wilayani Tarime 
Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini Michael Kembaki akizungumza na waumini wa kanisa la Waadventista Wasabato mtaa wa Majengo wilayani Tarime 
Walioketi mbele katikati ni Mbunge wa jimbo la Tarime Mjini Michael Kembaki, wa kwanza kulia ni katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Tarime Marema Sollo na wa kwanza kushoto ni Diwani wa Kata ya Kenyamanyori Farida Joel wakiwa kwenye ibada katika kanisa la Waadventista Wasabato Nkende ambapo walishiriki pia katika harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa
Wa Kwanza kulia ni Mbunge wa jimbo la Tarime mjini Michael Kembaki,anayemfuatia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji Tarime Thobias Ghati na wa tatu kulia ni Diwani wa Kata ya Turwa Chacha Marwa wakiwa kwenye ibada Kanisa la Waadventista Wasabato Majengo.

***
Na Dinna Maningo, Tarime
Mbunge wa Jimbo la Tarime mjini Michael kembaki amesema kuwa Mungu ndiye tumaini la Watanzania hata watu wakivaa barakoa kama Mungu hayupo pamoja nao ni kazi bure na kwamba ni vyema kuzidi kuombeana na kuliombea Taifa ili mwenyezi Mungu aepushe janga la Corona.

Kembaki aliyasema hayo wakati akichangia sh. milioni mbili ya ujenzi wa nyumba ya Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato mtaa wa Majengo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi yake huku akiwa ameambatana na Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Marema Sollo, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji Tarime ambaye pia ni Diwani wa kata ya Nyamisangura Thobias Ghati na Diwani wa kata ya Turwa Chacha Marwa.

Mbunge huyo aliwaomba waumini hao kuzidi kuliombea taifa dhidi ya janga la Corona ambalo limesababisha hofu kwa wananchi huku akiwapongeza waumini hao kwa kutovaa barakoa na kuweka tumaini lao kwa Mungu.

"Nawashukuru sana kwa jinsi mnavyoliombea taifa Mungu ndiye tumaini letu bwana asipoulinda mji yeye aulindaye akesha bure, hata tukivaa barakoa kama Mungu hayupo pamoja na sisi ni bure, nimefurahi sijaona muumini hata mmoja aliyevaa barakoa.

"Kuna kanisa nilienda nikakuta asilimia 80 wamevaa barakoa na mimi nilikuwa sina barakoa ilinipa hofu sana, Mungu ndiye tumaini letu tuzidi kuliombea taifa letu ili lipite kwa ushindi katika janga hili ,mungu aliyetuepusha na janga hili wakati ule ndiye huyo huyo atatuokoa na janga hili",alisema Kembaki.

Mzee wa Kanisa la Majengo Simon Andrea alimshukuru mbunge kwa kutekeleza ahadi na kusema kuwa mtaa wa Majengo hauna nyumba ya mchungaji hivyo fedha hizo zitasaidia kuanza kujenga msingi kwa kuwa tayari wameshanunua uwanja.

"Mbunge katimiza ahadi yake mungu ambariki kuna watu wanatoa ahadi lakini hawatimizi, Mchungaji wetu anaishi nyumba ya kupanga kwa fedha hizi zitatusaidia kwenye hatua ya ujenzi nikuombe tutakapokuomba tena msaada tusikie na tusaidie", alisema Andrea.

Baada ya Mbunge huyo kuzungumza na waumini mchungaji wa mtaa wa Majengo Kumba Kihiri alifanya maombi maalumu kwa mbunge huyo ili mwenyezi mungu amuongoze katika kazi zake za kuwatumikia wananchi na familia yake pamoja na kumpatia afya njema.

Wakati huo huo, Mbunge Kembaki amechangia milioni 2.5 katika harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa la Nkende ambapo mgeni rasmi katika harambee hiyo alikuwa mbunge wa viti maalumu Ghati Chomete aliyechangia sh.milioni mbili na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mara Samwel Keboye (Namba tatu) akichangia mifuko 50 ya saruji.

Baadhi ya viongozi wengine waliochangia fedha na saruji ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji Tarime ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Nkende Daniel Komote alichangia sh.500.000,Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Thobias Ghati alichangia 100,000 na Marema Sollo akichangia mifuko mitano ya Saruji.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mara Samwel Keboye aliwapongeza wabunge hao Madiwani na wana CCM kwa kujitolea kusaidia shughuli za kanisa, aliwaomba kuendelea kusaidia makanisa na misikiti mbalimbali pale kunapohitajika msaada Kwani kwakufanya hivyo Mungu atabariki na akawakumbusha waumini kuliombea Taifa lililokumbwa na Janga la Corona.
Share:

SHIRIKA LA GCI LATOA ELIMU YA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO KWA WANAUME WANYWA KAHAWA SHINYANGA MJINI


Meneja Mradi wa Sauti ya Mwanamke na Mtoto wa Shirika la GCI, Victoria Emmanuel (kulia) akizungumza wakati akitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika eneo la Nguzo Nane Mjini Shinyanga.

Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog
Shirika la Green Community Initiatives (GCI) linalojihusisha na utetezi wa Haki za Wanawake na Watoto, Vijana, Wazee, Watu wenye ulemavu naWanaoishi na Maambukizi ya Virusi vya Ukimwi limetoa elimu ya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto kwa Wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Nguzo Nane Mjini Shinyanga.

Shirika hilo lenye makao yake makuu Mjlimetoa elimu ya Ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa Jumamosi Februari 27,2021 kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Machi 8,2021 na utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa kutokomeza Ukatili dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWWA).

Meneja Mradi wa Sauti ya Mwanamke na Mtoto wa Shirika la GCI, Victoria Emmanuel alisema wanatoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume kwani ni kundi linalolaumiwa kutenda ukatili kwa watoto na wanawake na kwamba pia watayafikia makundi ya wanawake na mikusanyiko ya kijamii ili wananchi wahamasike kushiriki kutokomeza vitendo vya ukatili.

“Kuelekea Siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo Mwezi Machi 8 lakini pia sisi GCI kama miongoni mwa watekelezaji wa Mpango Mkakati wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto, tunaendelea kutoa elimu ya masuala ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto “,alieleza Victoria.

Alieleza kuwa shirika la GCI limeanzisha kampeni ya Sauti ya Mwanamke na Mtoto likitumia kauli mbiu ya 'Tokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto' kwa lengo la kuelimisha jamii kuhusu madhara yatokanayo na vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto mkoani Shinyanga ambao ni miongoni mwa mikoa vinara wa matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Aliyataja matukio ya ukatili kuwa ni pamoja na ndoa za utotoni,mimba za utotoni,utekelezaji wa familia,malezi duni ya watoto, watoto kuchomwa moto,kunyimwa chakula,kubakwa,kulawitiwa,kutelekezwa,kuitwa majina mabaya na ukatili wa kiuchumi,vipigo kwa wanawake na watoto kutoka kwa watu wao wa karibu mfano mume,mjomba,baba n.k.

Wakichangia mada ya ‘Nani alaumiwe kuwa chanzo cha ukatili dhidi ya wanawake na watoto’, wanaume hao waliokuwa katika Kijiwe cha Kahawa cha bwana Athumani Ibrahim kilichopo Mkabala na Zahanati ya Miti Mirefu Nguzo Nane Mjini Shinyanga, wanaume hao walisema migogoro ndani ya familia ni chanzo kikubwa cha vitendo vya ukatili.

Deogratius Moya alisema kutoelewana ndani ya familia ni chanzo kikubwa cha vitendo vya ukatili hali inasababisha wanaume wasiopenda maneno maneno huamua kuchelewa kurudi nyumbani, kutelekeza familia na kuendelea na maisha mengine hali inayosababisha watoto kukosa haki za msingi.

“Malezi ni changamoto kubwa, mfumo wa kuiga maisha kwa wanawake na watoto umetuletea balaa. Wanakuwa na tamaa ya kuiga maisha ya watu wengine na kupenda vitu vidogo vidogo. Vitu vya rahisi rahisi vinasumbua watoto wetu matokeo yake wanaambulia kupewa mimba na kukatishwa masomo yao”,alisema.

“Ndoa ni chanzo kikubwa cha ukatili. Wanaoana tu hawafanyi uchunguzi ndiyo maana tunaona leo harusi kubwa lakini baada ya siku chache ndoa chalii au mwanaume anabadilika,anaanza kupiga mke wake au unashangaa tu amepata mke mdogo anatekeleza mke wa kwanza,watoto na mke wanaanza kuteseka”,aliongeza.

Katika hatua nyingine aliwatupia lawama wanawake watumishi wa umma na wafanyabiashara kuwa chanzo cha matukio ya ukatili dhidi ya watoto kutokana na kuwa na muda wa kukaa na watoto badala yake wanawaachia wafanyakazi wa ndani kuhudumia watoto.

Elisha Philipo alisema baadhi ya wanawake wanawatumikisha watoto kwa kuwapa kazi ya kuuza vitafunwa,chai na kuokota chupa/makopo ya maji nyakati za masomo.

Naye Alex Elias na Adam Hussein walisema kitendo cha kukurupuka kuoa au kuolewa ni tatizo jingine kwani wanaoana kutokana na tama za kimwili, bila kuchunguzana tabia kwa kina matokeo yake wakioana migogoro inaanza,ndoa inavunjika watoto wanakosa uelekeo na kujikuta wakifanyiwa ukatili.

Kwa upande wake, Stephen Wilson alisema Utandawazi ni janga jingine ambapo sasa wanawake wengine hawataki kuwaheshimu waume zao wakidai haki sawa ambapo wanaume wasiopenda ugomvi huamua kutelekeza familia.

"Utandawazi unachangia sana wanawake kujiona wapo juu zaidi ya wanaume, wanadai haki sawa kwa kila kitu hawataki kuulizwa na waume zao. Hizi ganji zinasababisha ukatili, mwanaume akiacha pesa za mahitaji nyumbani hayanunuliwi, akimuuliza mke wake kulikoni hujawanunulia chakula watoto wakati wakati pesa nimekuachia mwanamke anapanda juu,ukimpiga makofi anakimbilia polisi anaonewa. Ndiyo maana wanaume wasiopenda ujinga/ugomvi wanaamua kuendelea na maisha mengine wanaacha familia au kuongeza mke",alieleza. 

Adam Hussein alisema mavazi yasiyofaa kwa wanawake ‘yakionesha maumbo yao’ yanachochea vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa kuwaingiza wanaume katika tamaa ya kimapenzi ,hakuna ndoa tena na matokeo yake kuwapa ujauzito na kutelekeza mimba na watoto.

Kwa upande wake, Shaban Martin aliiomba serikali kukataza mavazi yasiyofaa kwani sasa baadhi ya wanawake wanavaa mavazi yanayoonesha viungo vyao na kuchochea vitendo vya kingono huku Adam Hussein akisisitiza watoto wafundishwe maadili.

Wanaume hao pia waliomba serikali mkoani Shinyanga kuchukua hatua dhidi ya wanawake wanaofanya biashara ya ngono katika baadhi ya maeneo kwani inamomonyoa maadili.

Mwakilishi wa Dawati la Jinsia na Watoto kutoka Jeshi la Polisi wilaya ya Shinyanga, Bryson John aliwataka wazazi kuacha tabia ya kuwalaza watoto chumba kimoja na wageni kwani baadhi yao siyo wema wamekuwa wakiwafanyia vitendo vya ukatili ikiwemo kuwalawiti na kuwabaka.

Aidha aliwasihi wanandoa kupendana na kuhakikisha wanaepuka migogoro huku akiwasisitiza wanaume wanaofanyiwa ukatili watoe taarifa kwenye dawati la jinsia na watoto.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Meneja Mradi wa Sauti ya Mwanamke na Mtoto wa Shirika la GCI, Victoria Emmanuel akizungumza wakati akitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Athumani Ibrahimu kilichopo mkabala na Zanahati ya Miti Mirefu Nguzo Nane Mjini Shinyanga Jumamosi Februari 27,2021. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Meneja Mradi wa Sauti ya Mwanamke na Mtoto wa Shirika la GCI, Victoria Emmanuel akizungumza wakati akitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Athumani Ibrahimu kilichopo mkabala na Zanahati ya Miti Mirefu Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Muonekano wa kijiwe cha Kahawa cha bwana Athumani Ibrahim kilichopo Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Wanaume wakiwa katika Kijiwe cha Kahawa cha Athumani Ibrahim Nguzo Nane Mjini Shinyanga wakipata elimu ya madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Wanaume wakiwa katika Kijiwe cha Kahawa cha Athumani Ibrahim Nguzo Nane Mjini Shinyanga wakipata elimu ya madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Meneja Mradi wa Sauti ya Mwanamke na Mtoto wa Shirika la GCI, Victoria Emmanuel (kulia) akitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Athumani Ibrahimu Nguzo Nane Mjini Shinyanga. Katikati ni Mhasibu wa shirika la GCI Mongo akiwa na mfanyakazi mwenzake, Elizabeth Samson
Mhasibu wa Shirika la GCI, Victoria Emmanuel akitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Athumani Ibrahimu kilichopo mkabala na Zanahati ya Miti Mirefu Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Mfanyakazi wa Shirika la GCI, Elizabeth Samsonakitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Athumani Ibrahimu kilichopo mkabala na Zanahati ya Miti Mirefu Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Mwakilishi wa Dawati la Jinsia na Watoto wilaya ya Shinyanga, Bryson John akitoa elimu kuhusu ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Athumani Ibrahimu Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Mwakilishi wa Dawati la Jinsia na Watoto wilaya ya Shinyanga, Bryson John akitoa elimu kuhusu ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Athumani Ibrahimu Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Deogratius Moya akichangia hoja kuhusu vyanzo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na nini kifanyike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii wakati Shirika la GCI lilikitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume katika Kijiwe cha Kahawa Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Alex Elias akichangia hoja kuhusu vyanzo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na nini kifanyike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii wakati Shirika la GCI lilikitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume katika Kijiwe cha Kahawa Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Wadau wakiendelea kupata huduma ya kahawa na kusikiliza maoni kuhusu masuala ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto
Stephen Wilson akichangia hoja kuhusu vyanzo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na nini kifanyike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii wakati Shirika la GCI lilikitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume katika Kijiwe cha Kahawa Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Shaban Martin akichangia hoja kuhusu vyanzo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na nini kifanyike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii wakati Shirika la GCI lilikitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume katika Kijiwe cha Kahawa Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Elisha Philipo akichangia hoja kuhusu vyanzo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na nini kifanyike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii wakati Shirika la GCI lilikitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume katika Kijiwe cha Kahawa Nguzo Nane Mjini Shinyanga
John George akichangia hoja kuhusu vyanzo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na nini kifanyike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii wakati Shirika la GCI lilikitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume katika Kijiwe cha Kahawa Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Wadau wakiwa katika kijiwe cha Kahawa
Adam Hussein akichangia hoja kuhusu vyanzo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na nini kifanyike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii wakati Shirika la GCI lilikitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume katika Kijiwe cha Kahawa Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Wadau wa kahawa wakifuatilia majadiliano yaliyokuwa yanaendelea kuhusu masuala ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto
Wafanyakazi wa Shirika la GCI wakifuatilia mjadala kuhusu masuala ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto
Huduma ya kahawa ikiendelea
Wadau wakiwa katika kijiwe cha Kahawa Nguzo nane Mjini Shinyanga
Mwakilishi wa Dawati la Jinsia na Watoto wilaya ya Shinyanga, Bryson John na wafanyakazi wa Shirika la GCI katika Kijiwe cha Kahawa cha Athumani Ibrahimu kilichopo Nguzo Nane Mjini Shinyanga.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

NAIBU WAZIRI MARY PRISCA ATOA ONYO KWA MENEJA WA RUWASA CHATO

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) ametoa onyo kwa Meneja wa Wakala wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Chato Mhandisi Andrew Kilembe kwa kushindwa kutatua kwa wakati kero ya ubovu wa mita za maji zilizowekwa katika mradi wa maji wa Imalabupina Inchwankima na kusababisha wananchi wa eneo hilo kukosa maji kwa siku kadhaa. 

Ametoa onyo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wakati akikagua mradi huo unahohudumia wakazi wa vijiji hivyo. 

Amesema wananchi wanakosa huduma ya maji kwa sababu ya viongozi kufanya kazi kwa mazoea na kushindwa kutatua kero zinazojitokeza kwa wakati. 

“Natoa onyo na naomba fuatilieni hilo tatizo linalosababisha wananchi wasipate maji kwa wakati maeneo mengine yanatoa maji, na hakikisheni hizo mita zinazosumbua zinabadilishwa haraka ili kuondoa kero hiyo na wananchi hawa wapate maji”, amesema Mhandisi Mahundi na kusisitiza kezo zote ikiwemo matatizo ya umeme yasisubiri viongozi.
 
Aidha, amempongeza Meneja huyo wa RUWASA Chato kwa kuamua kutumia shilingi milioni 311 kukarabati miundombinu ya mradi wa maji Kasenga ambao ulichakaa na kuacha kutoa maji kwa muda mrefu. 

Katika ziara yake ya kukagua miradi ya maji mkoani Geita Naibu Waziri alikagua pia mradi wa maji wa Katoro Buseresere ambao utekelezaji wake unaendele vizuri na mradi huo ukikamilika utahudumia wananchi 20,000 wa kata ya Buseresere, Katoro, Ludete na Nyamigota.

Share:

Bible Teacher at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Bible Teacher   Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions are open for […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Accounting & Business Teacher at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Accounting & Business Teacher     Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions are […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Math Teacher – Middle School at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Math Teacher – Middle School     Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

ART Teacher – Primary & Secondary at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

ART Teacher – Primary & Secondary     Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Music Teacher at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Music Teacher     Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions are open for […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Library and Media Specialist at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Library and Media Specialist    Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions are […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Special Needs Coordinator at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Special Needs Coordinator     Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions are open […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

IT Teacher / Google App Specialist at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

IT Teacher / Google App Specialist    Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Senior School Principal at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Senior School Principal    Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions are open […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Geography/History Teacher at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Geography/History Teacher     Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions are open for […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

NAIBU WAZIRI MARYPRISCA ATOA SIKU 7 PAMPU YA MAJI ILIYOCHUKULIWA NA MKANDARASI IRUDISHWE GEITA

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi MaryPrisca Mahundi (Mb) amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Geita Mhandisi Frank Changawa kuhakikisha mkandarasi wa awali aliyekuwa anatekeleza mradi wa Nyamtukuza Petty and Company (Ltd), kurejesha pampu ya mradi huo aliyorudishiwa kwa ajili ya matengenezo madogo ili iweze kufungwa na wananchi waendee kupata huduma ya maji safi na salama.

Ametoa kauli hiyo alipokuwa anakagua utekelezaji wa mradi huo ambao umechukua muda mrefu kukamilika kutokana na wakandarasi kushindwa kukamilisha mradi kwa wakati hadi mkataba ulipovunjwa na kazi ya utekelezaji kuchukuliwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Geita (GEUWASA).

“Ninawapa siku saba (GEUWASA) kuhakikisha pampu iliyochukuliwa na Mkandarasi kwa ajili ya matengenezo inarejeshwa haraka ili ije ifungwe kwenye mradi kama mchoro wa awali unavyoonesha kufunga pampu mbili ili moja ikipata hitilafu, basi nyingine iendelee kufanya kazi, wananchi waendelee kupata huduma ya maji”, amesema Mhandisi Mahundi, na kusisitiza kuwa ndani ya siku hizo saba kupatiwa ripoti ya pampu hiyo kama imerejeshwa.

Amesema wananchi wengi nchini hususani wa maeneo ya vijijini wanahitaji maji na hivyo kuwataka watekelezaji wa miradi hiyo kukamilisha kwa wakati unaotakiwa ili wananchi wapate huduma wanayostahiki.

Aidha, amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Geita (GEUWASA) na watendaji wake kwa kuweza kutekeleza mradi huu ambao hapo awali ulikuwa kati ya miradi kichefuchefu kwa kutokamilika kwa wakati na sasa mradi umefikia hatua za mwisho na baadhi ya wananchi wa Nyamtukuza wameanza kupata huduma ya majisafi. salama na yenye kutosheleza.

Mradi wa Nyamtukuza kwa sasa unatekelezwa na GEUWASA kwa kutumia wataalam wa ndani (Force Account) na umegharimu shilingi bilioni 11 ambapo kwa kutumia watalaam hao wa ndani serikali imeweza kuokoa shilingi bilioni 4 na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Machi, 2021.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI FEBRUARI 28,2021














Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger