Sunday 27 March 2016

Magazeti Ya Leo Jumapili Ya March 27, 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Share:

Saturday 26 March 2016

New AUDIO | Yemia Alade Ft. Sauti Sol - Africa | Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
DOWNLOAD via HULKSHARE
http://old.hulkshare.com/dl/9tsxwhj0qdq8/Yemia_Alade_ft_Sauti_Sol_-_Africa.mp3?d=1
Share:

NACTE;HIZI NDIO SIFA ZA KUJIUNGA NA KOZI MBALIMBALI ZITOLEWAZO NA VYUO VILIVYO CHINI YA NACTE 2016/2017

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

PUBLIC NOTICE - MINIMUM ENTRY REQUIREMENTS FOR ACADEMIC YEAR 2016/17

 
THE NATIONAL COUNCIL FOR TECHNICAL EDUCATION
(NACTE)
PUBLIC NOTICE
MINIMUM ENTRY REQUIREMENTS

The National Council for Technical Education (NACTE), would like to inform the Public and other Education stakeholders on the minimum entry requirements to join Basic Technician Certificate (NTA Level 4), which will eventually lead to Ordinary Diploma (NTA Level 6) for successful Candidates.
An applicant should possess secondary certificate from National Examinations Council of Tanzania (NECTA) with a minimum of four passes (Four D’s) excluding religious subjects. Holders of foreign certificates should submit to NECTA for equivalence of their awards to Tanzania awards system to enable them to Apply.
It should be noted that, the entire process of admission is done via Central Admission System (CAS). For more information about registration status for Institutions and programmes/ courses offered, kindly visit our website at www.nacte.go.tz.

ISSUED BY;
THE OFFICE OF EXECUTIVE SECRETARY
THE NATIONAL COUNCIL FOR TECHNICAL EDUCATION
24th March, 2016
Share:

Majambazi Waua Watu Wawili na Kujeruhi Saba Jijini Mwanza

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Watu wawili wameuawa Jijini Mwanza kwa kupigwa risasi na Majambazi, huku Wengine saba wakijeruhiwa katika tukio la uvamizi wa duka lililokuwa likitoa huduma mbalimbali za kifedha.

Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, Justus Kamugisha, amesema kuwa tukio hilo lilitokea jana majira ya saa mbili usiku katika eneo la Bugarika Sokoni, baada ya watu watatu wanaosadikika kuwa ni majambazi waliokuwa na bunduki aina ya SMG kuvamia katika duka la mfanyabiashara na mkazi wa eneo hilo aitwae Daniel Marwa (30).

Kamanda Kamugisha amewataja waliouawa kuwa ni Julius Wankaba (30) ambae ni dereva bodaboda, pamoja na mfanyabiashara mmoja mwenye duka katika eneo hilo aliefahamika kwa jina la Mama Yuni (35).

Amewataja waliojeruhiwa kuwa ni Magesa Mungari (38), Simioni Charles (26) ambao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando huku wengine wakiwa ni Mwita Ryoba (30), Frank Willium (19), Saumu Said (20), Masumbuko Kanduru (38) pamoja na Emmanuel Francis ambao wanapata matibabu katika Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure.

Baadhi ya Mashuhuda wa tukio hilo, akiwemo mmiliki wa duka lililovamiwa, wanasema majambazi hao walipofika eneo la tukio walianza kufyatua risasi ovyo ili kuwatawanya wananchi waliokuwa wamekusanyika katika eneo hilo wakiangalia taarifa ya habari na wengine wakinywa kahawa,  na hivyo kusababisha wananchi kutawanyika jambo lililosababisha vifo na majeruhi hao.

Katika tukio hilo, Majambazi hao walifanikiwa kupora fedha taslimu kiasi cha Shilingi Milioni Mbili, Vocha za simu za mitandao mbalimbali zinazokadiliwa kuwa za shilingi Laki Nane pamoja na simu sita za wateja.

Kamanda Kamugisha amesema Jeshi la polisi Mkoani Mwanza limeanzisha msako mkali ili kuwakamata waliohusika na tukio hilo, huku likiahidi zawadi ya fedha kiasi cha shilingi Milioni Moja kwa yeyote atakaesaidia kufanikiwa kukamatwa kwa watuhumiwa hao.

Wakati huo huo, Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza linaendelea kumsaka mtu aliehusika na wizi wa mtoto mwenye umri wa siku moja katika Hospitali ya Wilaya ya Magu, ambapo tukio hilo limetokea Machi 23 mwaka huu, majira ya saa nane mchana baada ya mtu mmoja asiefahamika mwenye jinsia ya kike, kufika katika wodi ya wazazi na kumuiba mtoto huyo wakati mama yake amelala.

Aidha katika katika kusherehekea Sikukuu ya Pasaka, Jeshi hilo limepiga marufuku watoto kwenda kuogelea katika fukweni (Beach) pamoja na uwepo wa disko toto Jijini Mwanza.
Share:

New AUDIO | Shery Zuu Ft. Msaga Sumu - Babu Uyo | Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
http://old.hulkshare.com/dl/xe5p61m1hn28/Shery_Zuu_Ft_Msaga_Sumu_-_Babu_Uyo.mp3?d=1
Share:

NAFASI ZA MASOMO BUGANDO UNIVERSITY 2016/2017 NGAZI ZA YA DIPLOMA NA POSTGRADUATE,HIZI NDIO SIFA ZA KUJIUNGA BUGANDO

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Application and Medical Forms Downloads 



MODE OF APPLICATION FOR UNDERGRADUATE PROGRAMMES

Applicants with the appropriate “A” Levels passes (Direct Entrants) and Diploma Holders (Equivalent qualification) seeking admission at CUHAS into the Bachelor of Medical Lab Sciences (Code CU001), Bachelor of Science in Nursing Education (Code CU002), the Bachelor of Pharmacy (Code CU003), Doctor of Medicine (Code CU004) and Bachelor of Science in Nursing (CU005) are required to apply through the CENTRAL ADMISSION SYSTEM with the Tanzania Commission for Universities (TCU) using the guidelines provided by TCU as detailed in pages 35,36,37.

    Undergraduate Courses:


  • DOCTOR OF MEDICINE (MD) – 5 YEARS
  • Direct Entrants (Form Six)
    Holders of Principal pass at “C” grade or higher in Chemistry, Biology or Physics, provided that the other two passes are not below “D” at ADVANCED level. Preference will be given to applicants with "C" grade or higher in Chemistry or Biology in that order.Consideration will also be given to applicants with Principal passes at C grade on higher in Chemistry and a ‘D’ grade or higher in Biology or Physics. [C, D (5 points from 2 subjects)]

    Equivalent Qualifications
    Holders of B. Sc. Degrees from recognized institutions, majoring in BIOLOGY or CHEMISTRY. Holders of a Diploma in Clinical Medicine with principal passes at any level in Chemistry, Biology or Physics, in the ADVANCED certificate examinations.

  • BACHELOR OF MEDICAL LAB SCIENCE BMLS) – 3 YEARS
  • Direct Entrants (Form Six)
    Direct Entrants (Form Six) Holders of three Principal passes in Biology, Chemistry or Physics/Geography; provided 2 principal passes are at D level or higher [D,D,E(minimum 5 points from three subjects)] Consideration will also be given to applicants with two principal passes in Physics, Chemistry or Biology provided that one of them is at C grade or higher [C,E (4 points from 2 subjects)]

    Equivalent Qualifications
    Holder of an appropriate Diploma/Advanced Diploma with three Principal passes at any grade in Physics, Chemistry and Biology at “A” level. Appropriate Diploma/Advanced Diploma with at least three credit passes at any grade in Physics, Chemistry, Biology, Mathematics and English at “O” level and has passed Diploma/Advanced Diploma with an average of B grade or above. Preference will be given to students who have attempted “A” level.

  • BACELOR OF PHARMACY (B.PHARM) -
  • Direct Entrants (Form Six)
    Principal pass at C grade or higher in Chemistry, Biology or Physics provided that the other two subjects are NOT below D at (“A”) level. Preference will be given to applicants with “C” grade or above in CHEMISTRY or BIOLOGY in that order. Consideration will also be given to applicants with Principal passes at C grade on higher in Chemistry and a ‘D’ grade higher in Biology or Physics [C, D (5 points from 2 subjects)].

    Equivalent Qualifications
    A Diploma in Pharmacy from a recognized and accredited Institution with passes at a minimum of “B” grade in all Diploma subjects with three principal passes at E grade in Physics/Geography and Chemistry and Biology at “A” Level provided a minimum pass of C in Biology and D in Chemistry was obtained at “O” Level.

  • BACHELOR OF SCIENCE IN NURSING EDUCATION
  • Direct Entrants (Form Six)
    Holder of form-six certificate with THREE Advanced level passes in Physics, Chemistry and Biology; at least TWO passes are at “D” or higher.

    Equivalent Qualifications (3 Year Programme)
    Holder of Diploma in nursing with at least THREE credits in the following subjects: Biology, Chemistry, Physics, Mathematics and English. They should have a working experience of at least 2 years. Preference will be given for those who have attempted “A” Level.

    Equivalent Qualifications (2 Year Conversion Programme)
    Holder of Advanced Diploma in Nursing Education with at least THREE credits in the following subjects of “O” Level secondary certificate: Biology, Chemistry, Physics, Mathematics and English.
Share:

Kificho Ang’oka Uspika

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Pandu Ameir Kificho
ALIYEKUWA Spika wa Baraza la Wawakilishi kwa zaidi ya miaka 20 sasa, Pandu Ameir Kificho, ameng’olewa katika nafasi hiyo baada ya kushindwa katika kura za kuwania awamu nyingine ya uongozi wa baraza hilo.

Badala yake wajumbe wateule wa Baraza la Wawakilishi, wamemchagua Zubeir Ali Maulid, kuwa Spika mteule wa baraza hilo, baada ya kupata kura 55 na kumuacha kwa mbali Kificho aliyeambulia kura 11 katika uchaguzi uliofanyika jana katika Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui, Zanzibar.

Aidha katika uchaguzi huo ambao wawakilishi 72 walipiga kura, Janeth Nora Sekihola ambaye ni hakimu mstaafu akipata kura 4 wakati kura mbili ziliharibika.

Hata hivyo, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuangushwa katika uchaguzi huo, Kificho alisema amekubali kushindwa na yupo tayari kutoa ushirikiano akitakiwa kufanya hivyo.

“Hiyo ndiyo demokrasia, nimekubali kushindwa na nipo tayari kutoa ushirikiano mkubwa nikitakiwa kufanya hivyo kwa sababu ni ukweli kwamba ninao uzoefu mkubwa katika nafasi hiyo kwa zaidi ya miaka 20,” alisema.

Naye Spika mteule wa baraza hilo, Maulid alisema anakabiliwa na changamoto kubwa ya kuleta maendeleo na mabadiliko makubwa katika chombo hicho ambacho ni moja ya mihimili ya dola katika utekelezaji wa majukumu yake.

Amesema atatumia uzoefu alioupata kufanya kazi katika taasisi za kutunga sheria, kwa ajili ya kuleta mabadiliko hayo kwa kuhakikisha kwamba Baraza la Wawakilishi linafanya kazi inayotakiwa ya kuisimamia Serikali kwa mujibu wa Katiba.

“Nimekuwa Mwakilishi Shauri Moyo na Waziri mwaka 2000, pia nimekuwa Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa miaka miwili na nusu kwa hivyo uwezo wa kufanya kazi katika mabunge ya Jumuiya ya Madola ninao mkubwa,” alisema.

Aliwaomba wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wateule kumpa kila aina ya ushirikiano utakaomwezesha kutekeleza na kutimiza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba, kwani chombo hicho ni moja ya mihimili ya dola.

Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waliozungumza na gazeti hili, wamesema kwamba mabadiliko hayo ni ishara na ujumbe tosha kwa Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kwamba wawakilishi wanataka mabadiliko makubwa kwa Serikali kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.

“Mabadiliko makubwa tuliyoyafanya sisi wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa kumchagua Zubeir Ali Maulidi kuwa Spika mteule mpya, ni dalili tosha kwamba sasa tunataka mabadiliko makubwa ndani ya Serikali kwa kuwa na viongozi watakaowatumikia wananchi moja kwa moja,” alisema Rashid Ali Juma mwakilishi mteule wa jimbo la Amani.

Kificho ameweka historia kuwa Spika wa Kwanza katika Baraza la Wawakilishi la mfumo wa vyama vingi kuanzia mwaka 1995, ambapo kabla ya kuchaguliwa kushika wadhifa huo, alikuwa mwakilishi wa Jimbo la Makunduchi kuanzia 1988.

Zubeir Ali Maulid mwaka 2000 alichaguliwa kuwa Mwakilishi wa Shauri Moyo kwa tiketi ya CCM na kuteuliwa kuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, chini ya Serikali ya Rais mstaafu Amani Abeid Karume, ambapo alidumu katika wadhifa huo kwa miaka mitatu.

Mwaka 2005, Zubeir alichaguliwa kuwa Mbunge wa Kwamtipura kwa tiketi ya CCM ambapo akiwa bungeni katika kipindi cha miaka miwili na nusu, alikuwa Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na kuongoza vikao mbali mbali kwa kusaidiana na spika na naibu spika.

Katika hatua nyingine, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein, amemteua Said Hassan Said, kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). Uteuzi huo ndio wa kwanza kufanyika, tangu Rais Shein alipokula kiapo cha kuongoza Zanzibar kwa miaka mitano ijayo Alhamisi ya wiki hii.
Share:

Viongozi wa Dini Wakumbusha Kutenda Haki

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY



Askofu Msaidizi, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Eusebius Nzigilwa.

WAKATI Rais John Magufuli, Baraza la Mawaziri na viongozi wengine wakiombewa ili kufanya kazi vizuri katika ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika jana, viongozi mbalimbali wamekumbushwa kutimiza wajibu wao wa kuwatumikia wananchi kwa haki bila kushinikizwa.

Akihubiri katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Maxmillian Maria Kolbe, Mwenge jijini Dar es Salaam, Askofu Msaidizi, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Eusebius Nzigilwa, alisema ni vyema viongozi katika jamii wakumbuke wamepewa dhamana ya kuangalia wengine na kuongoza kwa haki na kuacha tabia ya ubinafsi na maamuzi ya kushinikizwa.

“Sisi tuliopewa dhamana tuamue kwa haki na kamwe tusiamue kwa shinikizo, kwa sababu ni heri kufa shahidi kuliko kuangamiza damu za watu wasio na hatia,” alisema Askofu Nzigilwa katika Ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika kitaifa kanisani hapo.

Aliwataka waumini kutumia Ibada ya Ijumaa Kuu kuwa kiele- lezo cha upendo kwa wengine na kamwe usaliti usiwepo kwa kuwa ni jambo baya lin- aloleta uharibifu. Alisema usaliti uliofanywa na Yuda Iskariote wa kumbusu Yesu Kristo, ni jambo gumu linalotakiwa kuepukwa na wanadamu kwa sababu ni sumu inayoua.

“Matendo ya unafiki na usaliti ni mabaya, kwa sababu mtu au watu wanaofanya huyafanya dhidi ya wengine huku mkichekeana, lakini kwa ndani unamuua, tafadhali tusiwe na sura mbili, kama ni ndiyo iwe ndiyo na sio iwe sio,” alisema Askofu Nzigilwa.

Naye Askofu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Dar es Salaam, Dk Valentino Mokiwa, amewataka Watanzania hasa waumini wa dini ya Kikristo kuachana na dhambi na kuishi katika uadilifu unaompendeza Mungu.

Akizungumza baada ya misa ya Ijumaa Kuu katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Albano, Askofu Mokiwa alisema, kuna kila haja ya watu kubadilika na kuachana na maisha ya dhambi kwa kuwa hayampendezi Mungu.

Naye Padre Nicholaus Masamba wa katika Kanisa Kuu Katoliki la Mtakatifu Joseph, aliwataka Watanzania kutekeleza wajibu wao katika mambo mbalimbali ili kuhakikisha familia zinakua na maadili mazuri.

“Wazazi wanatakiwa kuhakikisha watoto wanalelewa katika malezi bora ili kuendana na tafakari ya Yesu iliyosema yametia wakati anakata roho baada ya kutimiza wajibu wake,” alisema.

Katika Kanisa la Kiinjili la Kiletheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Azania Front, Mchungaji wa kanisa hilo, Charles Mzinga, aliwataka Wakristo kumtegemea Mungu katika kila jambo wanalopitia na kulifanya kwa kuwa ndio nguzo muhimu katika maisha ya binadamu.

Alisema ibada hiyo inawakumbusha mateso na kifo cha Yesu hivyo kila mmoja anapaswa kumpokea na kumtegea katika maisha yake.

Magufuli aombewa

Katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kipawa Kigango cha Stakishari, Mlezi na Mhadhiri wa Seminari Kuu ya Mtakatifu Karoli Lwanga, Segerea, Padre Peter Msafiri, aliwataka Wakristo kuombea Serikali inayoongozwa na Rais Magufuli.

Aliwataka pia kuwaombea mawaziri, makatibu wakuu na wakuu wote wa vitengo serikalini, ili Mungu awaongeze kwenye utendaji kazi wao.

Wakati katika Kigango cha Stakishari wakifanya sala maalumu ya kumuombea Rais Magufuli na Serikali yake, Rais Magufuli pamoja na mke wake, Janeth Magufuli, walishiriki ibada ya Ijumaa Kuu katika Kanisa la Mtakatifu Petro, jijini Dar es Salaam.

Katika ibada hiyo, mbali na Rais Magufuli na mke wake, viongozi wengine waliohudhuria ni pamoja na mke wa Waziri Mkuu, mawaziri na wabunge.

Mkoani Morogoro, Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro, Telesphor Mkude juzi katika ibada ya Alhamisi Kuu, aliwaasa waumini kuonesha dhamira ya kujishusha na kuhudumia wadogo.

Mkude alisema Yesu Kristu anataka unyenyekevu huo katika jumuiya, katika familia na jamii nzima kwa ujumla ambapo alisema kuwa wanapaswa kutoa sadaka ya kuhudumiana.

Uchaguzi Zanzibar

Nako huko Dodoma Msaidizi wa Askofu wa Kanisa la Kiinjili Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Dodoma, Mchungaji Samwel Mshana ameshauri vyama ambavyo havikushiriki uchaguzi wa Zanzibar kuingizwa katika serikali ya Umoja wa Kitaifa, kwani nao wana nafasi kubwa ya kujenga uchumi amani na ustawi wa Zanzibar.

Katika mahubiri yake pia aliwakumbusha waumini kuiona Pasaka hiyo kama sehemu ya kujihoji kwenye matendo wanayoyafanya kama kuna mahusiano yoyote na Mungu badala ya kuichukulia kuwa ni sikukuu kama zingine.

Naye Askofu mstaafu wa kanisa la Anglikana Dayosisi ya Tabora, Francis Ntiruka alishauri serikali ya Unguja kuachana na siasa na badala yake iwatumikie wananchi. Askofu huyo aidha amemtaka Rais wa Zanzibar kujali na kuwatimizia mahitaji wananchi wote kama alivyoahidi bila kujali kama kuna vyama ambavyo vilisusia uchaguzi huo.

Aidha amewataka Wakristo kuhakikisha wanaitumia Pasaka kwa kutenda mema na kuonesha upendo kwa vitendo huku wakijiepusha matendo yasiyofaa kama vile ulevi uasherati wizi ikiwemo na matumizi ya madawa ya kulevya.

Imeandikwa na Ikunda Erick, Regina Kumba, Theopista Nsanzugwanko na Katuma Masamba Dar, Agnes Haule, Morogoro na Sifa Lubasi, Dodoma.
Share:

Magazeti Ya Leo Jumamosi ya March 26,2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

























Share:

Friday 25 March 2016

download Jose Chameleone Ft. Bob Junior - BAKI NAE | Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

DOWNLOAD via HULKSHARE
http://old.hulkshare.com/dl/6yy4h4yd4bk0/Jose_Chameleone_Ft._Bob_Junior_-_BAKI_NAE.mp3?d=1
Share:

Harry Redknapp aiongoza Jordan kushinda goli 8 – 0, Australia nayo yapiga 7 – 0

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Kocha wa zamani wa Tottenham, Harry Redknapp ameiongoza timu ya taifa ya Jordan ambayo ndiyo anayoifundisha kwa sasa, kupata ushindi wa goli 8 – 0 dhidi ya timu ya taifa ya Bangladesh.

Katika mchezo huo wa kutafuta nafasi ya kufuzu kombe la Dunia 2018 Urusi, magoli ya Jordan yalifungwa na Hamza Aldaradreh aliyefunga magoli matatu dk. 23, 29 na 40, Abdallah Deeb dk. 29, Yusef Al Rawashdeh dk. 32, Baha Faisal dk. 62, Atiqur Rahman Meshu dk. 71, Yousef Al Naber dk. 81, Karim Rezaul dk. 83 na Ahmed Samir dk. 90.

Mchezo mwingine ulikuwa kati ya Australia na Tajikistan ambapo Australia imeibuka na ushindi wa goli saba kwa bila.

Baada ya matokeo hayo, Australia inaongoza kundi B ikiwa na alama 18 huku nafasi ya pili ikishikwa na Jordan iliyo na alama 16 na nafasi ya mwisho ikikamatiliwa na Bangladesh iliyo na alama moja. 
Share:

Watumishi hewa 169 wagundulika Kigoma.....Mkuu wa Mkoa awataka wakurugenzi kubainisha kiasi walicholipwa mwaka mzima.

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Brigedia Jenerali Emanuel Maganga amewataka wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wote waliopo katika halmashauri zote kutaja kiasi cha fedha kilichotumika kuwalipa mishahara watumishi hewa 169 kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Akiongea na waandishi wa habari, Brigedia Jenerali Emanuel Maganga alisema kuwa agizo hilo ni kufuatia agizo la Mheshimwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli la kufanya uhakiki wa watumishi katika halmashauri zote ili kuwabaini watumishi hewa wanaolipwa mishahara kinyume na utaratibu za utumishi.

Alisema katika hao watumishi hewa 169 waliowabainika wapo ambao walishafukuzwa kazi, wapo ambao wameshafariki na wengine hawana sifa za kuwa watumishi wa umma.

Mhe. Maganga alisema kuwa suala la kuwa na wafanyakazi hewa ni wizi ambao hauwezi kuvumilika na wizi wa kuibia wanyonge hauwezi kuvumilika.

"Hakuna anayeweza kuvumilia wizi wa waziwazi kiasi hiki unaofanywa na baadhi ya watumishi wasiowaaminifu, wale wote watakaobainika wajiandae kwani hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao"Alisema Maganga.

Alisema kuwa fedha walizokuwa wakilipwa watumishi hao hewa kwaajili ya mishahara zinatakiwa kurudi zote, pia wakurugenzi wawafute watumishi hao hewa kwenye orodha ya malipo.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa sasa hivi katika serekali hii ya awamu ya tano hakuna kufanya kazi kwa mazoea.

Alizitaja halmashauri zenye watumishi hewa kuwa ni halmashauri ya kasulu watumishi 78,halmashauri ya Kigoma 23,Manispaa ya Kigoma Ujiji 29,halmashauri ya Buhigwe 11,Uvinza 19,kibondo 5,ofisi ya Mkuu wa Mkoa 4 na halmashauri ya Kakonko hakuna mtumishi hewa.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger