Monday, 30 December 2024

SERA YA MADINI NGUZO MUHIMU KUIMARISHA SEKTA YA MADINI – MBIBO


⚪  Yasaidia Ukusanyaji wa Mapato ya Serikali zaidi ya Trilioni 1.93 kati ya 2021 na 2024

 📍 Morogoro, 

Imeelezwa kuwa Sera ya Madini ya 2009 imekuwa nguzo muhimu katika kuimarisha Sekta ya Madini, japokuwa kuna haja ya kuhuisha sera hiyo ili kuendana na mabadiliko ya sasa pamoja na matarajio ya baadaye katika maendeleo ya Sekta ya Madini na maendeleo ya kiuchumi kwa ujumla.

Hayo yameelezwa leo, Desemba 30, 2024 na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini Msafiri Mbibo wakati akiongoza Kikao cha Mapitio ya Sera ya Madini ya mwaka 2009, kilichofanyika katika Ofisi ya Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Morogoro na kuhudhuriwa Wataalam wa Sera, na Wawakilishi wa taasisi mbalimbali za Serikali ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa lengo la kufanya mapitio ya Sera hiyo na kuandaa mapendekezo ya maboresho.

Amesema kuwa mchakato mapitio ya Sera ya Madini ya mwaka 2009 katika kuhakikisha Sekta ya Madini inakuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi nchini. 

“Lengo letu ni kuhakikisha tunakuwa na Sera ya Madini inayoendana na viwango vya kitaifa na mahitaji ya sasa ya kiuchumi na kijamii. Tunahitaji sera itakayotoa mwongozo thabiti wa usimamizi endelevu wa rasilimali za madini kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho,” amesema Mbibo.

Mbibo ameongeza kuwa, Wizara ya Madini hivisasa inaongozwa na Sera ya Madini ya Mwaka 2009 ambayo inalenga masuala mahsusi yakiwemo kuimarisha ushirikiano wa Sekta ya Madini na sekta nyingine za uchumi; kuboresha mazingira ya kiuchumi kwa uwekezaji; kuongeza faida kutokana na uchimbaji madini; kuboresha masuala ya kisheria; kuendeleza wachimbaji wadogo; pamoja na kuimarisha usimamizi wa mazingira.

Akitoa wasilisho kuhusu Manufaa ya Sera ya Madini 2009, Mkurugenzi Msaidizi wa Sera na Mipango Wizara ya Madini Angelo Haule, amesema kuwa, ukuaji wa Sekta ya Madini umeimarika na Mchango wake kwa Taifa umeongezeka ambako kati ya Machi 2021 na Mei 2024, Tume ya Madini ilikusanya shilingi trilioni 1.93 kama Mapato ya Serikali, ikionyesha ufanisi mkubwa wa usimamizi wa sekta hiyo.

“Ukuaji wa sekta uliongezeka kwa kiwango cha asilimia 7.3 hadi 10.9 kati ya mwaka 2020 na 2022, huku mchango wake kwenye Pato la Taifa ukiongezeka kutoka asilimia 6.7 mwaka 2020 hadi asilimia 9.1 mwaka 2022. Aidha, masoko 42 na vituo 100 vya ununuzi wa madini vimeanzishwa, na kusaidia mauzo ya madini zenye thamani kubwa ikiwa ni pamoja na dhahabu, almasi, na tanzanite” amesema Haule

Haule amesisitiza kuwa, kwa upande wa ununuzi wa bidhaa na huduma, Kampuni za Kitanzania zilishiriki kwa asilimia 82 mwaka 2021 na asilimia 86 mwaka 2023, ikidhihirisha ongezeko la mchango wa wazawa kwenye sekta hiyo kwa kutoa huduma na kusambaza bidhaa migodini.

Ameongeza kuwa, zaidi ya leseni 23,924 za Uchimbaji Madini ya aina mbalimbali zilitolewa kati ya Mwaka 2021 na 2024, hatua inayolenga kuimarisha uwekezaji na ufanisi wa Sekta ya Madini nchini.

Share:

NYOTA MPYA YA TANZANIA: RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA MAGEUZI YA KIUCHUMI

Tanzania, ambayo kwa muda mrefu imeonekana kama moja ya nchi zenye viwango vya juu vya kiuchumi katika Afrika Mashariki, sasa inavuma kwa uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan. Tangu kuchukua madaraka mnamo Machi 2021, Rais Samia amejitokeza kama mtu wa mageuzi, akiiongoza nchi kuelekea utulivu, usawa, na ukuaji wa kiuchumi. Uongozi wake haujatu tu kuamsha matumaini ndani ya nchi, bali pia kuipa Tanzania nafasi muhimu katika mazingira ya kiuchumi ya kanda hii.  

Zama Mpya ya Uongozi  

Rais Samia Suluhu Hassan alifanya historia kwa kuwa rais wa kwanza mwanamke wa Tanzania, akivunja vikwazo katika eneo la kisiasa ambalo kwa muda mrefu limekuwa likiongozwa na wanaume. Kuongozwa kwake kulifuata baada ya kifo cha ghafla cha mtangulizi wake, John Magufuli, ambaye wakati wa uongozi wake ulionyesha maendeleo makubwa ya miundombinu lakini pia sera zinazozua mabishano. Hata hivyo, mtindo wa uongozi wa Samia umekuwa unaojulikana kwa uhalisi, mazungumzo, na juhudi za kukuza umoja.  

Mtazamo wake umeonekana hasa katika juhudi zake za kurekebisha uhusiano wa kidiplomasia na kuvutia uwekezaji wa kigeni. Tofauti na sera za mtangulizi wake zilizokuwa za kujitenga, Samia amekubali msimamo wa wazi na wa kushirikiana, akishirikiana na washirika wa kimataifa na majirani wa kanda ili kuimarisha matarajio ya kiuchumi ya Tanzania.  

Mageuzi ya Kiuchumi na Ukuaji  

Chini ya uongozi wa Rais Samia, Tanzania imeona mwelekeo mpya wa kuzingatia mageuzi ya kiuchumi na utofautishaji. Uchumi wa nchi, ambao kwa muda mrefu umetegemea kilimo, sasa unaona ukuaji katika sekta kama vile madini, utalii, na nishati. Uwiano wa kimkakati wa Tanzania, rasilimali asilia nyingi, na miundombinu inayoboreshwa vimeifanya kuwa mahali pazuri pa wawekezaji wanaotafuta fursa katika Afrika Mashariki.  

Moja ya mafanikio makubwa ya Samia imekuwa uwezo wake wa kurejesha imani katika mazingira ya biashara ya Tanzania. Serikali yake imeweka kipaumbele uwazi, kurahisisha michakato ya kiserikali, na kutekeleza sera zilizolenga kuvutia uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni (FDI). Juhudi hizi hazijaenda bila kutambuliwa, huku waangalizi wa kimataifa wakisifia mwelekeo mzuri wa kiuchumi wa Tanzania.  

Miundombinu na Ushirikiano wa Kanda  

Maendeleo ya miundombinu ya Tanzania yamekuwa msingi wa mkakati wake wa kiuchumi. Bandari za nchi, hasa Bandari ya Dar es Salaam, hutumika kama milango muhimu kwa nchi zisizo na pwani kama vile Zambia, Malawi, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Chini ya uongozi wa Samia, uboreshaji unaoendelea wa bandari na mitandao mingine ya usafiri unaimarisha jukumu la Tanzania kama kitovu cha biashara ya kanda.  

Zaidi ya hayo, ushiriki wa Tanzania katika Eneo la Biashara huru la Afrika (AfCFTA) unaonyesha juhudi zake za kushirikiana kiuchumi na nchi jirani. Kwa kukuza uhusiano wa karibu wa kiuchumi na nchi jirani, Tanzania iko tayari kufaidika na fursa kubwa zinazotolewa na soko la watumiaji linalokua la Afrika.  

Maendeleo ya Kijamii na Ushirikiano  

Rais Samia pia amechangia maendeleo ya kijamii, akisisitiza umuhimu wa ushirikiano na usawa wa kijinsia. Serikali yamechukua hatua za kushughulikia masuala kama vile elimu, afya, na uwezeshaji wa wanawake, kwa kutambua kuwa maendeleo endelevu hayawezi kufikiwa bila kuwekeza katika mtaji wa binadamu.  

Uongozi wake umewahimiza kizazi kipya cha Watanzania, hasa wanawake na wasichana, ambao wanamwona kama kioo cha matumaini na ushahidi wa uwezekano wa kuvunja vikwazo vya kijamii.  

Changamoto na Njia 

Licha ya maendeleo, changamoto bado zipo. Tanzania bado inakabiliana na masuala kama vile umaskini, ukosefu wa ajira, na hitaji la kuendelea na utofautishaji wa kiuchumi. Zaidi ya hayo, kupungua kwa uchumi wa kimataifa na athari za mabaki ya janga la COVID-19 vinaweza kuwa hatari kwa mwelekeo wa ukuaji wa nchi.  

Hata hivyo, mtazamo wa Rais Samia wa kimazoea na wa kutazamia mbele umejenga matumaini miongoni mwa Watanzania na waangalizi wa kimataifa. Uwezo wake wa kusuluhisha changamoto ngumu huku akizingatia maendeleo ya muda mrefu unaashiria mwendo mzuri wa Tanzania.  

Kimulimuli cha Matumaini Afrika Mashariki  

Tanzania inapoendelea na safari yake ya kuwa nguvu ya kiuchumi katika Afrika Mashariki, Rais Samia Suluhu Hassan anajitokeza kama kimulimuli cha matumaini na maendeleo. Uongozi wake haujatu kuibadilisha Tanzania ndani ya nchi, bali pia kuimarisha nafasi yake kama mchezaji muhimu katika kanda hii.  

Kwa mtazamo wazi, juhudi za kushirikisha wote, na mwelekeo wa maendeleo endelevu, Rais Samia anapisha njia kwa mustakabali mkavu wa Tanzania na watu wake. Nchi inapoendelea kuinuka, dunia inatazama, na hadithi ya mageuzi ya Tanzania chini ya uongozi wake bado haijakwisha.

Share:

Sunday, 29 December 2024

KUNYWA FURAHA GINGER LIFE SWEET - KINYWAJI CHA MAAJABU! , FURAHA TANGAWIZI IPO PALE PALE!!


Furaha Ginger Life Sweet: Kinywaji kilichojaa furaha, afya, na nguvu.

Furaha Limited maarufu kwa utengenezaji wa Kinywaji  Furaha Tangawizi imekuletea kinywaji kingine cha asili Furaha Ginger Life Sweet  ambapo pia kina nguvu ya Tangawizi (Ginger)  kukufanya ujivunie afya bora na nguvu za asili.

Kinywaji kipya cha Furaha Ginger Life Sweet ni kinywaji cha asili kilichojazwa nguvu za ginger (Tangawizi), na manufaa mengi kwa afya yako. 

Ongeza Nguvu na Kuondoa Uchovu: Furaha Ginger Life Sweet inakuwezesha kutawala siku yako bila uchovu! Huupatia mwili wako nguvu ya asili.

Kinga ya Mwili Imara: Imarisha kinga yako dhidi ya magonjwa ili upate afya bora kila wakati.

Tengeneza Tumbo Lako: Furaha Ginger Life Sweet ni msaidizi mzuri katika mmeng’enyo wa chakula, kuondoa gesi tumboni na kuzuia sumu mwilini.

Afya Bora ya Magoti (Joint): Ikiwa unakutana na maumivu ya goti, Furaha Ginger Life Sweet itakusaidia kuondoa maumivu haya na kuimarisha afya ya viungo vyako.

Furaha Ginger Life Sweet

Kunywa furaha, pata afya! 🌱🍃

Tupigie 
0627460413 - Kahama
0757485153 - Mwanza
0713217634 - Dar es salaam
0713773001- Suppliers

Pia Kunywa Furaha Tangawizi kwa ajili ya Afya ya Asili kwa Mwili Wako!

👉 Inasaidia Mmeng'enyo wa Chakula
Furaha Tangawizi husaidia kuboresha utendaji wa mmeng’enyo wa chakula na kuondoa maumivu ya tumbo.

👉 Inaondoa Sumuvu Mwilini
Husaidia kuondoa sumu mwilini, ukiacha mwili wako ukiwa safi na wenye afya.

👉 Inaimarisha Kinga ya Mwili
Inasaidia kuimarisha kinga yako dhidi ya magonjwa, ikikufanya kuwa na afya bora kila wakati.

👉 Inasaidia Kupunguza Uzito
Furaha Tangawizi ni nzuri kwa wale wanaotaka kupunguza uzito, huku ikichoma mafuta kwa asili.

👉 Inakata Shinikizo la Damu na Magonjwa ya Moyo
Husaidia kupunguza shinikizo la damu na inazuia magonjwa ya moyo kwa njia ya asili.

👉 Inazuia Saratani
Furaha Tangawizi ni nzuri kwa kuzuia saratani kwa asili.

👉 Anti-Aging 100%
Furaha Tangawizi inasaidia kupambana na dalili za kuzeeka na kukuacha ukiwa na ngozi nyororo na afya nzuri.

Tupigie 
0627460413 - Kahama
0757485153 - Mwanza
0713217634 - Dar es salaam
0713773001- Suppliers




Share:

UWT YAKEMEA TABIA ZINAZOKWAMISHA WATOTO KUENDELEA NA MASOMO




📍28 DISEMBA, 2024 - IRINGA

Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg Mary Pius Chatanda (MCC) amewataka wazazi kuacha mara moja tabia ya kuozesha watoto wakiwa na umri mdogo au kuwasafirisha mikoani kwenda kufanya kazi za ndani.

Akizungumza na wananchi wa Igowole mkoa Iringa, Chatanda amesema;
"Rais Samia ametengeneza na kuboresha miundombinu mizuri ya shule, ameajiri walimu wa kutosha na kuongeza vifaa ikiwemo vitabu kwasababu anataka watoto wasome katika mazingira mazuri ili waweze kufaulu, waweze kuajirika na kuajiriwa na waweze kujitegemea kiuchumi. Mkiwaozesha watoto wadogo au kuwapeleka kufanya kazi za ndani, mnakosea sana"

Chatanda amepiga marufuku tabia hii kwani inawanyima watoto haki ya kupata elimu na inakwamisha jitihada za kuwainua kiuchumi Watanzania wote ususani watoto wakike zinazofanywa na Serikali ya CCM kupitia Ilani yake ya Uchaguzi 2020/2025.







Share:

Saturday, 28 December 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI DESEMBA 29,2024

 

Magazeti ya Jumapili
 

   
Share:

THE BLESSED PRAISE AND WORSHIP TEAM KUFANYA MAAJABU KAGERA KUFUNGA MWAKA 2024!

 

Na Lydia Lugakila -Bukoba.

Tamasha  kubwa na la aina yake linataraji kunguruma Desemba 29,2024 saa nane mchana katika Viwanja vya Bukoba Sekondari lengo likiwa ni kumsifu Mungu na Kumwabudu na Kumshukuru kwa ajili ya mwaka huu 2024.

Akizungumza na Malunde 1 blog mmoja wa  walezi wa kikundi hicho Pastor Agape kutoka kanisa la Kinabii  ECG Taifa la Yesu mjini Bukoba alisema kuwa kikundi cha The Blessed Praise and Worship kitakuwa kinatambulisha nyimbo zao kadhaa katika ibada hiyo ya fungua malango ya Mbinguni ambapo ametumia fursa hiyo kuwaomba wazazi kuwapeleka watoto wao kujifunza namna ya kumwabudu na kumsifu Mungu kupitia uimbaji.

Kiongozi wa Kikundi hicho Elgibo Emmanuel ametumia fursa hiyo pia kuwakaribisha Wananchi wote wa Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera na kuwa watu wote watamwabudu na kumsifu Mungu kwa pamoja ikiwa ni pamoja kupokea muujiza mkubwa.

Amesema hakika kila mtu atabarikiwa sana atakapoingia mwaka 2025 kwa kumwabudu na kumsifu aliye juu maana malango ya Mbinguni yatamfungukia kwa ajili mambo makubwa yenye utakatifu wa Mungu yaliyo mbele yao.

Hata hivyo amesema atatumia fursa hiyo kutoa kuwanoa watoto ili wajue kumuomba na kumwabudu Muumba wao.

Share:

BUGANDIKA DAY YAFANA.. WANAFUNZI WA KIKE BUGANDIKA SEKONDARI KUFUTWA MACHOZI

Na Lydia Lugakila _ Misenyi.

Wadau mbalimbali wa maendeleo ambao ni wazawa wa kata ya Bugandika na waishio nje ya Bugandika  wameamua kwa pamoja kuchangia maendeleo ya kata hiyo kwa kujenga bweni la shule ambalo ujenzi wake unaendelea ikiwa ni hatua ya kuwanusuru wanafunzi wa kike wa shule ya Sekondari Bugandika kutokana na kutembea umbali   kilometa 8 kwenda na kurudi kufuata huduma ya elimu ambapo wamekuwa wakikutana na changamoto mbalimbali njiani.

Katika risala iliyosomwa na mtendaji wa kata ya Bugandika Nassoro Mswadiko katika sherehe za Bugandika day amesema siku hiyo maalum ya kuchangia maendeleo  ya kata Bugandika(Bugandika Day) wameamua kuchangia maendeleo ya kata ikiwa ni pamoja na kuanza kuwanusuru watoto wa kike wanaopitia changamoto wawapo njiani kwani hukumbana na vishawishi vingi vinavyoweza kuleta madhara makubwa ikiwemo kupata mimba.

"Utoro,kukosa muda wa kujisomea na  kushindwa kutimiza ndoto zao ni mambo yaliyokuwa yakiumiza roho zetu hivyo kwa kuanza tutaweza bweni litabeba watoto 120 wa kike tutakuwa tumesaidia pakubwa" ,amesema Mswadiko.

Ameongeza kuwa wanalazimika kujenga bweni ili kuwasaidia wanafunzi  kuboresha ufaulu wao na kuchochea nidhamu bora,kujitegemea na kujiamini.

Naye Diwani wa kata ya Bugandika Amudi Migeyo alisema kuwa shule ya Sekondari Bugandika ilianzishwa mwaka 2007 ambapo licha ya Wananchi kujitoa kujenga vyumba vya kutosha vya shule changamoto kubwa ilikuwa ni bweni la shule.

Migeyo amesema wana Bugandika waishio nje ya Bugandika wamekuwa chachu kubwa ya kuleta maendeleo ndani ya shule hiyo.

"Bugandika Day iliyoanzishwa ilikuwa inahusisha kanisa (Bugandika Parish) ambapo sisi tumeomba tuwe na Bugandika Day yah pamoja ndani ya vijiji 7 tayari Wananchi wamejitoa kwa nguvu kubwa", amesema diwani huyo.

Naye Mgeni rasmi katika sherehe hiyo ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Nkenge Frolent Kyombo amewapongeza wadau hao kwa nguvu zao kwani wamewezesha kupatikana kwa kiasi cha ya shilingi milioni 20.6 ikiwemo ahadi na taslimu kupitia harambee ya kuchangia ujenzi wa shule hiyo.

Naye Profesa Hosea Rwegoshora akitoa neno la hamasa amewapongeza waasisi wa Bugandika day kwa wazo hilo la muda mrefu ambalo limeanza kwa hatua kubwa huku akiomba mshikamano ili kusonga mbele.

Naye Naibu Kamishina wa Polisi mstaafu Adrian Rweikiza Magayane kutoka Wilayani Misenyi amesema kuwa baadhi ya watu ambao wanakuwa hawachangii maendeleo wanakuwa hawapapendi nyumbani kwao hivyo wao wamerudi kwa kuunga mkono juhudi za Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Hajat Fatma Mwassa za Ijuka Omuka.

Mwenyekiti wa bodi ya shule Bugandika Harun Said amewashukuru wadau hao na kuwa suala la kuanzisha bweni linahitaji mshikamano, nguvu huku akiomba vijana na wazee kuchangamka kwani shule ni yao na watoto ni wao hivyo wajivunie maendeleo ya Bugandika kwa kujitoa kwa moyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi Steven Ndyakoa amesema kupitia kikundi cha Whatsapp  cha Bugandika mpya fukuto la maendeleo lilianzia hapo hadi wakafikia hatua ya kupendekeza na kushauri Desemba 26 iwe siku maalum ya Bugandika ili kukutana na kufahamiana kwa waishio ndani na nje ya jamii huku akiwapongeza Wananchi na Serikali kwa kuzidi kujitoa kwa ajili ya maendeleo.

Aidha amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Nkenge Wilayani Misenyi mkoani kagera Florent Kyombo kwa kutoa Mamilioni ya pesa kuijenga kata hiyo.

Hata hivyo Mbunge wa jimbo la Nkenge Florent Kyombo amesema wataendelea kuboresha kila wakati ili Bugandika day iweze  kufana zaidi ya hiyo iliyofanyika.

"Niwapongeze kwa nguvu nyingi mfuko wa Mbunge imeishatanguliza Milioni 2 kwa ajili ya ujenzi wa bweni leo Ofisi ya Mbunge tutaongeza milioni 3 ambapo Desemba 30 Mwaka huu tutaidhinisha fedha hizo ambazo ni jumla ya shilingi milioni 5.


Hata naye Dr. Auson Simeon Rwehumbiza ambaye ni Mwenyekiti wa Bugandika Mpya alisema miaka miwili iliyopita walianzisha kusomba mawe eneo la mradi ambayo gharama yake ni Shilingi milioni 2.3 hivyo chimbuko la Bugandika Mpya limefanya Bugandika day hivyo ushirikiano mshikamano uendelee ambapo ametumia fursa hiyo kuwahamasisha wadau mbali mbali wa maendeleo kuweka nguvu ili Bugandika iwe na manufaa kwa wote huku akiwaomba Wananchi kuilinda miundo mbinu inayotolewa na wadau.


Ikumbukwe kuwa kata ya Bugandika ndiyo kata yenye mtaji mkubwa kuliko kata nyingine zote ikilinganishwa na kata Kasambya kutokana na wingi wa kuwa na vijiji 7 ambapo kata Bugandika ina wasomi wakubwa ikiwa ni pamoja na kuwepo Maprofesa 4  ndani ya kata hiyo na Maprofesa 2 wanaotokea katika familia moja.

Share:

FDH YAANZA UTEKELEZAJI WA KUWAJENGEA UWEZO WANAWAKE WENYE ULEMAVU


Na Dotto Kwilasa, Dodoma

Taasisi ya Foundation For Disabilities Hope (FDH) imeanza kuteleza mradi wa mwaka mmoja wa kuwajengea uwezo wanawake wenye ulemavu kushiriki masuala ya uongozi pamoja na ujasiriamali ili kuwainua kiuchumi.

Mradi huo wa mwaka mmoja unalenga kuwafikia wanawake wenye ulemavu zaidi ya 300, katika kata mbalimbali za Halmshauri ya wilaya ya Kondoa.

Mkurugenzi Mtendaji wa FDH, Maiko Salali, akizungumza wakati wa utoaji wa mafunzo
wilayani kondoa, amesema mradi huo wa mwaka mmoja umejikita kusaidia watu wenye ulemavu kukamata fursa za kiongozi pamoja na ujasiriamali.
Amesema takwimu zinaonyesha ushiriki wa watu wenye ulemavu kwenye masuala ya uchanguzi mbalimbali nchini bado ni hafifu hali ambayo inahitaji jitihada za pekee kuibadili.

“Hata katika uchaguzi uliopita wa serikali za mitaa hivi karibuni takwimu zinaonyesha kuwa ushiriki wa wa watu wenye ulemavu ulikuwa mdogo sana lakini pia hata ushiriki wa wanawake ulikuwa hafifu sana hivyo ipo haja kwa wadau pamoja na serikali kuweka jitihada kubadili hali hii.

“Tutakua hapa kwa kipindi cha mwaka mmoja ili kuwaelimisha na kuwajengea uwezo wanawake wenye ulemavu waweze kushiriki kikamilifu katika michakato mbalimbali ya kiuongozi niwashukuru sana Abilis Foundation kwa kufadhili mradi huu ili kuongeza elimu na uelewa kuhusu masuala ya watu wenye ulemavu ili kuwa na jamii jumuishi”amesema

Aidha, alisema wanaishukuru wilaya ya Kondoa kwa kutupatia ushirikianao ili kuwafikia na kuwajengea uwezo watu wenye ulemavu ili mtu mwenye ulemavu asonge mbele.
Ofisa Maendeleo ya Jamii wilaya ya Kondoa Jafari Haji, alisema mradi huo umekuja wakati mwafaka kwani watu wenye ulemavu bado wanakabiliwa na chanamoto mbalimbali ikiwemo ushiriki wa masula ya uongozi.

“Mafunzo ambayo yanayotolewa kupitia mradi huu yatasaidia watu wenye ulemavu kushiriki kwenye masula mbalimbali yakiwemo ya kiungozi pamoja na ujasiriamali”amesema

Salma Ramadhani, mkazi wa Kondoa alishauri wazazi kuacha kuacha tabia ya kuficha watoto wenye ulemavu bali wawatoe ili wapate haki zao za msingi ikiwemo elimu.






Share:

AJALI YA GARI YAUA WATU SITA NYASA, WAMO WALIMU WANNE



Na Regina Ndumbaro- Ruvuma

Watu sita wamefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea katika Wilaya ya Nyasa, Mkoani Ruvuma. 

Ajali hiyo imetokea leo, tarehe 28 Desemba 2024, wakati wa safari kutoka kijiji cha Lumalu kilichopo katika Kata ya Upolo kuelekea makao makuu ya wilaya.

Akizungumza kwa njia ya simu, Mkuu wa Wilaya ya Nyasa, Mheshimiwa Peres Magiri, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, ambayo imesababisha vifo vya wafanyakazi wanne wa Serikali, wakiwa ni walimu wa Shule ya Msingi Lumalu.

 Watu wawili wengine, wakiwemo dereva wa gari hilo na raia mmoja, pia amepoteza maisha.

Gari lililohusika katika ajali hiyo ni la aina ya Predo T 647 CVR, mali ya Vincent Alel Milinga kutoka kijiji cha Lumalu, Kata ya Upolo, Wilaya ya Nyasa.

Walimu waliopoteza maisha ni Damas Damasi Nambombe (Mwalimu),Domenica Abeat Ndau (Mwalimu),Judith Joseph Nyoni (Mwalimu),na John Silvester Mtuhi (Mwalimu).

Raia mwingine aliyefariki duni ni Boniface Bosco Mapunda pamoja na dereva wa gari hilo ambaye ni Vincent Alel Milinga.

Share:

Friday, 27 December 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI DESEMBA 28,2024

 

Magazetini
 
       
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger