Wednesday, 26 May 2021

Makatibu Wakuu Afya/ Sheria Na Katiba Kuhakikisha Mfumo Wa Haki Kwa Makosa Ya Ukatili Unaimarika


 Na Mwandishi wetu, Momba
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Profesa Sifuni Mchome wamewataka watendaji wote wanaohusika na upatikanaji wa haki za makosa ya jinai kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ili kuhakikisha haki inapatikana hasa kwa waathirika wa ukatili.

Wameyasema hayo wakati wa ziara yao ya pamoja Wilayani Momba, Mkoa wa Songwe yenye lengo la kuona namna sekta mbalimbali zinavyoshirikiana katika utoaji wa haki hususani kwa watoto waliokinzana na sheria.

Akizungumza na watendaji wa Mahakama, Magereza pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Mpango wa Taifa wa kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) ya Halmashauri ya Mji Tunduma kwa nyakati tofauti, Dkt. Jingu amesema watoto wanaokinzana na sheria wana haki ya kupatiwa huduma muhimu wanazostahili.

"Watoto wanatakiwa watendewe tofauti kwa sababu wao ni tofauti, tuendelee kufanya kazi, kumekuwa na changamoto sana hasa kwenye eneo la ushahidi, wanajamii wanatakiwa kuona umuhimu wa kushirikiana na vyombo vyetu ili haki iweze kutendeka ili iwe ni fundisho kwa wengine wanaofanya vitendo kama hivyo" alisema Dkt. Jingu.

Jingu pia amesema Jamii ina nafasi kubwa ya kumaliza changamoto mbalimbali hasa migogoro kwa kutumia mifumo yao hivyo kuna umuhimu wa kuimarisha mifumo ya kijamii ambayo itasaidia kupunguza misongamano katika vyombo vingine vya utoaji wa haki.

Dkt. Jingu amesema pia Wazee ni kundi muhimu katika mchakato wa utoaji haki kwenye jamii hivyo wana nafasi kubwa ya kumaliza migogoro iwapo wakitumika vizuri.

Katika hatua nyingine, Dkt. Jingu amezitaka Kamati za MTAKUWWA kuhakikisha wanafanya kazi ya kubadili fikra potofu katika jamii ikiwemo za baadhi ya wazazi kuona ni mzigo kusomesha watoto wao.

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Mchome amezitaka Mahakama kufanya jitihada za kutumia adhabu mbadala ikiwemo njia za kijamii ili kupunguza idadi ya mahabusu magerezani.

"Kwa sasa hivi takwimu zinaonesha kwamba hali ya mahabusu ni zaidi ya wafungwa ambapo wengi wao ni wale wenye makosa makubwa" alisema Prof. Mchome.

Kwa upande wake Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Momba Timothy Lyon amesema katika Wilaya hiyo kesi za watoto ni chache na wana utaratibu maalumu wa kuzishughulikia ili kulinda haki za watoto japokuwa kuna changamoto ya ukosefu wa mahabusu ya watoto na shule ya maadilisho.

Nao baadhi ya wajumbe wa Kamati ya MTAKUWWA Halmashauri ya Mji Tunduma wameishukuru Serikali hasa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo  Regina Bieda kwa kuwawezesha kutekeleza majukumu yao hivyo jamii  imeelimika na watoto wanaweza kutoa taarifa za matukio ya ukatili kwa wakati.

Makatibu Wakuu hao wametembelea pia na kujionea ujenzi wa Jengo la Mahakama ya Mkazi Songwe pamoja na kuzungumza na wafungwa wa Gereza la Songwe linalohudumia Wilaya za Mbozi na Momba.

MWISHO


Share:

KAMPUNI YA ASFA HOSE SERVICE YATUA KWA KISHINDO KWENYE MAONESHO YA WAJASIRIAMALI NA WAWEKEZAJI KAHAMA

Share:

WANANCHI TUNDURU WATAKIWA KUTUMIA VYEMA UJUZI WA KUKABILIANA NA TEMBO

Afisa Wanyamapori Wilaya ya Meatu, Revocatus Menei akitoa maelekezo ya namna ya kutumia tochi maalum kufukuza tembo kwa baadhi ya wanakijiji cha Jakika Wilaya ya Tunduru katika mafunzo kwa vitendo yaliyofanyika jana kijijini hapo.

Mratibu wa Shirika la Kimataifa la Uhifadhi wa Mazingira na Wanyamapori (WWF) Kanda ya Kusini, Richard Katombo akionesha namna ya kutumia mizinga ya nyuki kufukuza tembo aliyevamia makazi ya watu, onyesho lililofanyika katika kijiji cha Jakika Wilayani Tunduru jana.

Mtafiti wa Wanyamapori kutoka Taasisi ya Utafiti ya Wanyamapori (TAWIRI), Dkt. Emmanuel Masenga akionesha namna ya kuchanganya pilipili na oili chafu itakayotumika kumfukuza tembo aliyevamia makazi ya watu,onesho lililofanyika kijiji cha Jakika Wilayani Tunduru.

Mtafiti wa Wanyamapori kutoka Taasisi ya Utafiti ya Wanyamapori (TAWIRI), Dkt. Emmanuel Masenga akionesha namna ya kutumia fataki kumfukuza tembo aliyevamia makazi ya watu,onesho lililofanyika kijiji cha Jakika Wilayani Tunduru. Wanaoshuhudia ni ni Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti ya Wanyamapori (TAWIRI), Dkt. Janemary Ntalwila (kushoto) na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Wanyamapori, Wizara ya Maliasili na Utalii, Silvanus Okudo (wa pili kutoka kushoto).

Wahitimu wa mafunzo ya kupunguza migogoro baina ya binadamu na wanyama waharibifu kama tembo wakionyesha wanavijiji kwa vitendo namna ya kutumia honi kuwafukuza tembo katika kijiji cha Jakika Wilayani Tunduru jana. Wa kwanza kulia ni Afisa Wanyamapori Wilaya ya Meatu, Revocatus Menei.

Baadhi ya wanakijiji cha Jakika Wilaya ya Tunduru wakionyesha kwa vitendo namna ya kutengeneza bomu la pilipili linalotumika kumfukuza tembo mara baada ya kupewa mafunzo hayo na Watendaji kutoka Taasisi ya Utafiti ya Wanyamapori (TAWIRI), jana kijijini hapo.

Wananchi waliopewa mafunzo ya kukabiliana na tembo wakionyesha kwa vitendo namna ya kutumia wigo wa pilipili na oili chafu ili kumfukuza tembo aliyevamia makazi ya watu onesho lililofanyika katika kijiji cha Jakika Wilayani Tunduru jana.

*************************

Na Happiness Shayo -TUNDURU

Wananchi 20 kutoka vijiji vya Wilaya ya Namtumbo na Tunduru waliopewa mafunzo ya ulinzi wa wanyamapori na namna ya kukabiliana na wanyama wakali na waharibifu kama tembo wametakiwa kuhakikisha wanautumia vizuri ujuzi huo ili kuilinda jamii inayokabiliwa na tatizo la kuvamiwa na tembo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mhe. Julius Mtatiro wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya kupunguza migogoro baina ya binadamu na wanyama waharibifu kama tembo yaliyofanyika katika ukumbi wa Klasta Wilayani Tunduru jana.

“ Ndugu zangu ambao mmekuja kwenye haya mafunzo msiende kuyaweka kabatini, muende mkayafanyie kazi na mkatoe elimu kwa wananchi na mtumie mafunzo haya kuwadhibiti wanyama waharibifu ” Mhe. Mtatiro amefafanua.

Aidha, amewaasa wakufunzi hao kuwa wepesi kutoa taarifa za uvamizi wa wanyamapori waharibifu katika makazi ya watu pindi inapotokea.

“Nimewakamata wenyeviti kadhaa wanaochukua rushwa na kuruhusu ng’ombe kuingia hifadhini, lakini hii haitasaidia isipokuwa tu pale ambapo mtaamua kutoa taarifa kwa watendaji wa vijiji na ofisi ya mkuu wa wilaya mnapoona makundi ya ng’ombe hifadhini” Mhe. Mtatiro amesema.

Mhe. Mtatiro amewaagiza wakufunzi hao kuhakikisha wanawaelimisha wananchi wengine juu ya mbinu mbalimbali walizojifunza za namna ya kukabiliana na wanyama wakali na waharibifu na pia kuzalisha watu wengi kwenye maeneo yao ambao wana weledi wa udhibiti wa wanyamapori wakali na waharibifu ili jamii ibaki salama.

Akizungumza kwa Niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti ya Wanyamapori (TAWIRI), Dkt. Janemary Ntalwila amesema kuwa mafunzo hayo yamejikita katika kuelezea njia rafiki za kukabiliana na uvamizi wa tembo.

“ Njia zitakazotumika ni njia rafiki na za gharama nafuu kwa mfano matumizi ya mabomu ya pilipili , tochi maalum za kufukuzia tembo, fataki, honi, mizinga ya nyuki, uzio wa vitambaa vilivyolowekwa kwenye mchanganyiko wa oili chafu na pilipili ” Dkt. Ntalwila ameongeza.

Dkt. Ntalwila amesisitiza kuwa, njia hizo zikitumika ipasavyo zitasaidia kuboresha maisha ya wananchi kwa kusaidia kuongeza kipato akitolea mfano matumizi ya njia ya mizinga ya nyuki ambayo ina uwezo wa kufukuza tembo na pia kutoa asali, nta na gundi ya nyuki.

Naye, Kaimu Mkurugenzi wa Wanyamapori kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii Silvanus Okudo amesema mafunzo hayo yatasaidia kupunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la uvamizi wa tembo.

”Nia ya Serikali ni kuisaidia jamii kupunguza au kuondokana kabisa na tatizo hili la kuvamiwa na wanyama wakali na waharibifu na tunaamini kuwa wakufunzi hawa watajitahidi kuzuia changamoto hiyo kabla haijajitokeza” amesema Bw. Okudo.

Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, Amiri Abeid ambaye ni Mkazi wa Kijiji cha Libangu Wilaya ya Namtumbo amesema kuwa mafunzo hayo yatawawezesha wanavijiji kuwadhibiti wanyama wakali na waharibifu pindi wanapovamia makazi yao.

“Lengo la mafunzo haya ni kutuwezesha namna ya kuishi na kukabiliana wanyama wakali na waharibifu kama tembo lakini pia kuchukua ujuzi na kwenda kuwafundisha wanavijiji wengine” amesema Bw. Abeid.

Mafunzo ya kudhibiti wanyama wakali na waharibifu yamehudhuriwa na wakufunzi ishirini kutoka vijiji vya Wilaya ya Namtumbo na Tunduru na yameandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori (TAWIRI) kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii, Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) na Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA).

Share:

Project Manager: Agriculture at Vodacom

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Full Time / Part Time:  Full Time Contract Type:  Permanent At Vodacom, we’re working hard to build a better future. A more connected, inclusive and sustainable world. As a dynamic global community, it’s our human spirit, together with technology, that empowers us to achieve this. We challenge and innovate in order to connect people, businesses, and communities […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Senior Procurement Specialist & Procurement Hub Coordinator at World Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job #: req12088 Organization: World Bank Sector: Procurement Grade: GG Term Duration: 3 years 0 months Recruitment Type: International Recruitment Location: Dar Es Salaam,Tanzania Required Language(s): English Preferred Language(s): Closing Date: 6/15/2021 (MM/DD/YYYY) at 11:59pm UTC Description Do you want to build a career that is truly worthwhile? Working at the World Bank Group provides […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Specialist Underground Infrastructure Engineer at AngloGold Ashanti

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

The Underground infrastructure engineer is responsible for overseeing and coordinating all engineering infrastructure activities and plans relating to engineering services required for underground mining operations at Geita Gold mine Tanzania. The role provides direct output in the design and project management of all infrastructure to support Life of Mine production plans.  This includes managing, overseeing and […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi amefanya uteuzi wa Mkuu wa Skuli ya Sheria Zanzibar.



Share:

SHE Manager at Unilever

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

SHE MANAGER MAIN JOB PURPOSE: The Safety & Environment Manager has the responsibility for managing safety and environment improvement activities to achieve excellence within all site in Unilever Tea Tanzania. The jobholder works with all operation units and departmental teams to develop the local Safety and Environment Strategy and improvement plans to achieve sustainable Safety, […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

INTERNSHIPS at Railway Children Africa

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Railway Children Africa (RCA) is Non-Governmental Organisation (NGO) registered in Tanzania NO. 1563, and affiliate of our parent company Railway Children UK With over ten years working in Africa, we are committed to safeguarding and promoting the welfare of children and young people living and working in street. Additionally, we are also committed to provide […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Various Jobs at Tindwa medical and health service

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Tindwa medical and health service is local registered company dealing with providing Emergency Medical Services, Waste and Environmental Management, Occupation Health and safety both local and international and Medical Supplies Services. Currently, it is looking for a position below… TMHS POLYCLINIC – MIKOCHENI JOB VACANCIES We are looking for highly skilled professionals in the following […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Monitoring & Evaluation Officer 3 at RTI International

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

RTI International is the prime implementor of the USAID Jifunze Uelewe activity focused on sustainably improving literacy and numeracy outcomes of “all learners” from pre-primary through Standard 4 in five regions of Tanzania. For the purpose of this program, “all learners” includes, but is not limited to, marginalized and vulnerable girls and boys, learners with […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Child Protection in Emergency Manager at Plan International

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Location: Nyarugusu Kigoma, Tanzania Company: Plan International The Organisation   Plan International is an independent development and humanitarian organisation that advances children’s rights and equality for girls. We believe in the power and potential of every child. But this is often suppressed by poverty, violence, exclusion and discrimination. And it’s girls who are most affected. Working together […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Technical Lead Education at Plan International

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Location: Geita, Tanzania Company: Plan International The Organisation Plan International is an independent development and humanitarian organisation that advances children’s rights and equality for girls. We believe in the power and potential of every child. But this is often suppressed by poverty, violence, exclusion and discrimination. And it’s girls who are most affected.   Working together with […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Monitoring Evaluation Research and Learning Advisor at Plan International

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Location: Geita, Tanzania Company: Plan International The Organisation Plan International is an independent development and humanitarian organisation that advances children’s rights and equality for girls. We believe in the power and potential of every child. But this is often suppressed by poverty, violence, exclusion and discrimination. And it’s girls who are most affected.   Working together with […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Program Director at Plan International

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Location: Geita, Tanzania Company: Plan International The Organisation Plan International is an independent development and humanitarian organisation that advances children’s rights and equality for girls. We believe in the power and potential of every child. But this is often suppressed by poverty, violence, exclusion and discrimination. And it’s girls who are most affected. Working together with children, […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO MEI 26,2021

















Share:

Tuesday, 25 May 2021

TAGCO CHAMPA TUZO DKT ABBASI KWA KUTAMBUA MCHANGO WAKE

 

  Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi, akitunukiwa Tuzo ya Shukrani kutoka kwa viongozi na wanachama wa Chama cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini (TAGCO) kwa mchango wake aliotukuka kwenye kuleta mageuzi katika sekta ya habari nchini.



a.Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi (katikati) akiongoza kikao kazi cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini Jijini Mbeya, kushoto ni Naibu wake Dkt. Ally Possi, kulia ni Katibu Mkuu -TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe

Na John Mapepele, Mbeya

 

Katibu Mkuu wa Habari wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi ametunukiwa tuzo na Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali (TAGCO) kwa kutambua mchango na mageuzi makubwa aliyoyafanya kwenye Sekta ya Habari hapa nchini.

Akikabidhi tuzo hiyo kwa Dkt. Hassan Abbasi, Mwenyekiti wa TAGCO, Paschal Shelutete wakati wa kikao cha 16 cha TAGCO kilichofanyika Jijini Mbeya Mei 24,2021 amesema Dkt. Abbasi ametoa mchango mkubwa akiwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari- MAELEZO na Mkuu wa Serikali tofauti na hapo awali.

“Ni katika kipindi hiki ambapo miradi ya kimkakati ya Serikali ilisemewa vizuri zaidi na kufahamika na watu wengi hivyo kuwafanya wananchi kuipenda Serikali yao” Amefafanua Shelutete.

Ameongeza kwamba Dkt. Abbasi amefanikiwa kusimamia tasnia ya Habari na uboresha mahusiano ya kikazi miongoni mwa wadau wote wa Sekta ya Habari.

kwa upande wake Dkt. Abbasi amewashukuru Waandishi kwa kumpa tuzo hiyo na kuahidi kuendelea kuwapa ushirikiano ili waweze kuendelea kutekeleza majukumu wao kikamilifu kwa nafasi yake ya sasa ya Katibu Mkuu. Wizara ya Habari, Utamadunim Sanaa na Michezo.

“Tuendelee kushirikiana katika cheo hiki kipya cha Katibu Mkuu katika Wizara yetu ambayo ni Wizara muhimu inayogusa umma kwa nyanja ya burudani na huzuni kutokana na Sekta zake” Ameongeza Dkt. Abbasi.

Amewataka Waandishi  kuzingatia weledi wakati wote wa undaji wao wa kazi ambapo amesisitiza kwamba Serikali inatambua mchango wa waandishi na kwamba  itaendelea  kuhakikisha sekta inaboreka  na kuchangia kwenye  uchumi wa Taifa.

Aidha amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kumwamini na kumrejesha  tena kwenye nafasi ya Katibu Mkuu  na kuahidi kufanya kazi kwa weledi na  bidi ili kutekelea Ilani ya Chama cha Mapinduzi na maelekezo ya Mheshimiwa Rais Samia.

Kikao hiki kimefunguliwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Innocent Bashungwa kimehudhuriwa na Naibu wa Wizara hiyo, Katibu Mkuu -TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe ambaye ametoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya kiutumishi kwa maafisa Habari kutoka halmashauri zote nchini,na viongozi mbalimbali wa Serikali na Maafisa Habari, Mawasiliano  na Uhusiano wa Serikali zaidi ya 270.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger