Wednesday, 19 May 2021

Investment Specialist at Mr Kuku Farmers Limited

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

INVESTMENT SPECIALIST JOB PURPOSE DUTIES AND ACCOUNTABILITIES The ideal candidate will have a successful track record of closing and supervising transactions, including in our developing markets, typically as a banker or developer, and ideally with both debt and equity experience. Furthermore, specific responsibilities include, but are not limited to:   PROJECT ORIGINATION Assist in the […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Chief Finance and Administration Officer at Swiss TPH

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

The Swiss Tropical and Public Health Institute (Swiss TPH) is a world-leading institute in global health with a particular focus on low- and middle-income countries. Associated with the University of Basel, Swiss TPH combines research, services, and education and training at the local, national and international level. About 850 people from more than 80 nations […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

National Technical Advisor at Enabel

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Category:  National Location:   Kigoma, Tanzania, United Republic of Reference:  14262 The Belgian development agency, Enabel, mobilises its resources and its expertise to eliminate poverty in the world. Enabel contributes to the efforts of the international community and works towards a society that provides present and future generations with sufficient resources to build a sustainable and fair world. […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo May 19



Share:

Tuesday, 18 May 2021

WAZIRI KALEMANI ATOA SIKU 10 WAKANDARASI KUANZA UTEKELEZAJI MRADI WA KUMALIZIA VIJIJI VISIVYO NA UMEME

Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Medard Kalemani ametoa muda wa siku 10 kwa wakandarasi walioshinda zabuni za kutekeleza Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili kuanza kazi ya ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme. 

 

Waziri Kalemani alitoa agizo hilo tarehe 17/05/2021 wakati akizndua Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili katika Kijiji cha Mpakali kilichopo Wilaya ya Mbogwe katika Mkoa wa Geita.

 Dkt. Kalemani alisema Serikali imetenga Shilingi bilioni 75.6 kwa ajili ya kupeleka umeme katika vijiji 97 ambavyo havina umeme katika Mkoa wa Geita.

 “Vijiji vyenye umeme ni 377 kati ya vijiji 474 n katika Wilaya ya Mbogwe vijiji visivyo na umeme ni 33 na tumewaletea mkandarasi atakayekamilisha kazi ya kupeleka umeme katika vijiji hivyo” alisema. 

Aidha, alisisitiza kuwa Serikali imetoa muda wa miezi 18 kwa wakandarasi wanaotekeleza miradi ya kusambaza miundombinu ya umeme vijijini na kuwa muda huo hautaongezwa. 

Aliwataka REA kuwasimamia wakandarasi wakamilishe miradi kwa wakati kwa mujibu wa mikataba.

 Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe Martha Mkupasi alisema kuwa Umeme ni nishati muhimu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi na kuwa itasaidia katika kuboresha utoaji wa huduma za kijamii kama vile afya na elimu. 

Naye Mbunge wa Jimbo la Mbogwe, Mhe. Nicodemus Maganga alisema kuwa upatikanaji wa nishati ya umeme katika jimbo hilo utafungua fursa ya uwekezaji wa viwanda vya kusindika mpunga, dengu na karanga ambazo zinalimwa ukanda huo.

Share:

Yaliyojiri wakati Mhe. Rais Samia alipofungua kiwanda cha ushonaji cha Jeshi la Polisi kilichopo Kurasini Mkoani Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 18 Mei, 2021 amefungua kiwanda cha ushonaji bohari kuu ya Jeshi la Polisi kilichopo Kurasini Mkoani Dar es Salaam.


Kiwanda hicho kimejengwa kwa utaratibu wa nguvu kazi (force account) kwa gharama ya shilingi Milioni 666.4 badala ya shilingi Bilioni 1.4 kama kingejengwa kwa utaratibu wa zabuni.


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IJP Simon Sirro amesema ujenzi wa kiwanda hicho umepanua uwezo wa kiwanda kutoka vyerehani 70 hadi 130 vyenye uwezo wa kushona sare 125,000 za Askari kwa mwaka.


IJP Sirro amemshukuru Mhe. Rais Samia kwa kufungua kiwanda hicho na amesema Jeshi la Polisi linapanga kuanzisha shirika la uzalishaji litakaloendesha miradi mbalimbali kikiwemo kiwanda cha ushonaji, kiwanda cha kuzalisha maji na usindikizaji wa fedha.


Pia, IJP Sirro amemshukuru Mhe. Rais Samia kwa Serikali kutoa shilingi Bilioni 6 kwa ajili ya kuwalipa wastaafu wa Jeshi la Polisi ambao wameanza kulipwa.


Akizungumza na Maafisa wa Polisi, Askari na viongozi mbalimbali katika uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini, Mhe. Rais Samia amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kujenga kiwanda hicho kwa kutumia mapato yake ya ndani na kwa kutumia nguvukazi iliyotumia kiasi kidogo cha fedha ikilinganishwa na endapo lingetumia wazabuni.


Mhe. Rais Samia ameelezea kufarijika kwake kukifungua kiwanda hicho ambacho kiliwekwa jiwe la Msingi na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli na amesema kukamilika kwa kiwanda hicho ni uthibitisho wa kumuenzi Hayati Dkt. Magufuli.


Ameelekeza Majeshi mengine kushona sare zao katika kiwanda hicho na pia kujielekeza kushona sare nyingine kama vile viatu badala ya kila Jeshi kushona aina ileile ya sare zinazoshonwa na Jeshi lingine ili kudhibiti uagizaji wa sare za Askari kutoka nje ya nchi. 


Aidha, Mhe. Rais Samia amelitaka Jeshi la Polisi kujielekeza kudhibiti matukio ya uhalifu na uvunjaji wa sheria ikiwemo makosa ya usalama barabarani badala ya kujikita katika kutoa adhabu ama kuwa kitega uchumi.


Amelitaka jeshi hilo kuongeza juhudi katika kukabiliana na vitendo vya uhalifu ambavyo vimeanza kujitokeza na ameonya kuwa katika upandishaji wa vyeo, uteuzi na kutengua uteuzi wa Maafisa wakiwemo Makamanda wa Polisi wa Mikoa kipimo cha juhudi za udhibiti wa matukio ya uhalifu hasa ujambazi kitatumika.


Mhe. Rais Samia amelitaka Jeshi la Polisi kuweka mfumo utakaowezesha kutambuliwa kwa wavunja sheria za usalama barabarani popote walipo hapa nchini ili ikitokea dereva kafanya makosa katika mkoa mmoja aonekane katika mkoa mwingine na achukuliwe adhabu stahiki ikiwemo kufutiwa leseni.


Amelitaka Jeshi la Polisi kuendelea kupunguza msongamano wa Mahabusu waliokamatwa kutokana na makosa mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwaachia wenye kesi za kubambikizwa kama ambavyo imefanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambayo imefuta kesi 147 za rushwa za kubambikizwa.


Mhe. Rais Samia ameagiza sheria inayolazimu majeruhi kuwa na fomu ya PF3 ndipo wapatiwe matibabu katika vituo vya tiba irekebishwe ili majeruhi wasikoseshwe matibabu pale wanapokuwa hawana fomu hiyo.


Mhe. Rais Samia ameahidi kufanyia kazi changamoto mbalimbali za Jeshi la Polisi kadiri Serikali itakavyokuwa na uwezo wa kifedha.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
18 Mei, 2021




Share:

Waziri wa Mambo ya Nje Balozi Mulamula Akutana Na Kufanya Mazungumzo Na Balozi Wa Poland, Uswisi


Na Mwandishi wetu, Dar
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Poland nchini, Mhe. Krzystof Buzalski pamoja na Balozi wa Uswisi nchini Mhe. Didier Chassot katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Waziri Mulamula amesema kuwa mazungumzo yake na mabalozi hao yalilenga kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano wa uwili (bilateral cooperation) baina ya Tanzania na nchi hizo katika sekta za afya, elimu, utalii pamoja na biashara na uwekezaji.

Akiongelea uhusiano baina ya Tanzania na Poland Balozi Mulamula amesema kuwa wapoland walikuja kwa kasi katika uwekezaji ambapo wana kampuni zao zinazozalisha matreka Kibaha, na kuanzisha miradi katika sekta ya maji, miradi katika uwekezaji wa nafaka pamoja na kutoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wa kitanzania nchini Poland.

“Sasa hivi Balozi amenijulisha kuwa fursa hizo za watanzania kusoma Poland na kutuhamasisha kuzichangamkia fursa hizo, lakini pia tumeongelea jinsi ya kukuza biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Poland,” Amesema Balozi Mulamula

Akiongelea kuhusu ushirikiano wa Tanzania na Uswisi Mhe. Mulamula amesema kuwa ushirikiano wa Tanzania na Uswisi umekuwa ni wa muda mrefu na wamekuwa wakisaidia sana Tanzania katika sekta ya Afya hasa katika kupambana na Malaria.

“……..Uswisi imekuwa ikisaidia mikopo mbalimbali lakini pia ni mwenyekiti mwenza katika kuunganisha Tanzania na nchi wadau/zinzaotoa misaada, pamoja na mambo mengine, madhumuni ya kukutana leo ni kuangalia jinsi gani ya kukuza sekta ya uwekezaji na biashara,” Amesema Balozi Mulamula

Kwa upande wake Balozi wa Poland nchini, mhe. Krzystof Buzalski amesema kuwa wamekubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya Poland na Tanzania katika sekta ya uchumi, maendeleo, utalii na siasa.

“Leo tumekubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya Poland na Tanzania katika sekta ya uchumi, maendeleo, utalii pamoja na siasa kati ya Poland na Tanzania,” amesema Balozi Buzalski.

Nae balozi wa Uswisi Mhe. amesema kuwa Uswisi na Tanzania zimekuwa na ushirikiano wa siku nyingi kwa zaidi ya miaka 40 na viongozi hawa wamejadili masuala mbalimbali ya ushirikiano wa uwili (Bilateral cooperation) katika masuala ya kiuchumi na kisiasa.

“Mimi na Mhe. Waziri tumekubaliana kuendeleza ushirkiano baina ya nchi zetu mbili katika sekta ya afya; elimu; biashara; uwekezaji pamoja na maliasili na utalii,” amesema Balozi Chassot.



Share:

Marekani Yaahidi Kuendeleza Ushirikiano Na Zanzibar Katika Kuimarisha Afya Za Wananchi Wake


 Na Ramadhani Ali – Maelezo
Balozi wa Marekani nchini Tanzania Donald Wright ameahidi Serikali ya nchi yake itaendelea kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha afya za wananchi.

Ameeleza kuridhishwa na hatua kubwa iliyofikiwa katika mapambano dhidi ya maradhi ya Maleria na kusema kuwa Marekani itaendeleza mkakati utakaohakikisha maradhi hayo yanamalizika kabisa.

Balozi Donald ameeleza hayo alipofanya mazungumzo na Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto Nassor Ahmed Mazrui Ofisini kwake Mnazimmoja.

Balozi wa Marekani amemueleza Waziri wa Afya kuwa Serikali ya nchi yake imetenga fedha maalumu kwa ajili ya kupambana na maradhi ya Ukimwi nchini Tanzania.

Ameahidi kuwa nchi hiyo ipo tayari kusaidia masuala ya chanjo ya Covid 19 ili Zanzibar iendelee kuwa salama na maradhi hayo ambayo yamekuwa tatizo kubwa katika nchi nyingi duniani.

Aidha Balozi Donald ameeleza suala la Wafanyabiashara wa Marekani kuja kuwekeza vitega uchumi Zanzibar ili kuwapatia vijana wengi ajira na kuimarisha uchumi wan chi.

Amesema vijana ndio nguvu kazi ya nchi na iwapo watapatiwa ajira za uhakika wataweza kusaidia maendeleo ya nchi yao kwa kiwango kikubwa na kuipunguzia Serikali gharama zisizokuwa na ulazima.

Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto Nassor Ahmed Mazrui amemueleza Balozi Donald kuwa maradhi ya Maleria yapo kwa asilimia moja hivi sasa na Wizara ya Afya huchukuwa hatua za dharura sehemu ambayo atapatikana mgonjwa wa maradhi hayo.

Akizungumzia maradhi ya Covid 19 Waziri Mazurui amesema kwa kipindi cha mwezi mmoja sasa Zanzibar hajapatikana mgonjwa wa maradhi hayo na  tahadhari kubwa inaendelea kuchukuliwa kwa wenyeji na wageni wanaoingia nchini.

Amesema Zanzibar haijaweka vizuizi kwa watu kuingia na kutoka lakini milango mikuu yote ya kuingilia kumewekwa mashine maalumu za kufanyia uchunguzi ili kuhakikisha maradhi hayo hayaingia nchini.


Share:

FAMILIA YAPATA MSHTUKO WASIOJULIKANA KUWEKA JENEZA LENYE MAKOROKORO MLANGONI

 Familia katika kijiji cha Ebunyang'anyi kata ya Bunyala, Kakamega nchini Kenya imepatwa na mshtuko baada ya kuamka na kupata jeneza lililokuwa na misalaba mitatu likiwa limewekwa mlangoni  nje ya mlango wa nyumba ya Peter Wekondi, mzee mkongwe ambaye pia ni mgonjwa.

Mmoja wa walioshuhudia kisa hicho cha kushangaza kilichotokea leo asubuhi, Janepher Masika amesema kuwa jeneza hilo lilikuwa limefungwa kwenye kitambaa cheupe huku nzi wakiwa wamejaa juu yake.

 "Leo asubuhi nilipokuwa nikienda shambani niliona jeneza nje ya nyumba ya majirani zangu na nikawaamsha kuwaarifu. Nilishtuka kwa sababu sijawahi kuona kitu kama hicho maishani," amesema Masika.

Kwa muda mfupi, tukio hilo lilikuwa limevuta umati mkubwa uliokusanyika katika boma hilo kushuhudia kisa hicho kilichowaacha midomo wazi.

Watu wasiojulikana walikuwa wameacha jeneza hilo nje ya mlango wa nyumba ya Peter Wekondi, mzee mkongwe ambaye pia ni mgonjwa .

Baada ya kufungua jeneza hilo wenyeji hao waliachwa na mshtuko baada ya kupata mchanga na vifaa vingine visivyojulikana. Baadhi yao walikihusisha kisa hicho na ushirikina ambao walisema huenda mhusika alichukua hatua hiyo kutokana na wivu. 

Jotham Makokha, mzee wa 'nyumba kumi' alitoa wito kwa wenyeji kupendana na kuishi kwa amani na uwiano. 

"Ninawarai watu wetu waachane na njia za kitamaduni zilizopitwa na wakati na kuleta hofu miongoni mwa wengi. Hatuishi tena kama enzi zile za mababu zetu", alisema Makokha.

 Familia ya waliotendewa kisha hicho yake Jackline Oteng'o sasa inaishi kwa hofu kubwa na sasa imetoa wito kwa yeyote aliye na habari kuhusu tukio hilo, kusaidia kutegua kitendawili kabla ya familia yake kuanza kushuhudia misururu ya maafa. 

Chanzo - Tuko News

Share:

RAIS SAMIA AFUNGUA KIWANDA CHA USHONAJI CHA JESHI LA POLISI TANZANIA -KURASINI



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akivuta utepe kufungua Kiwanda cha Ushonaji cha Jeshi la Polisi Tanzania kilichopo Kurasini mkoani Dar es Salaam leo tarehe 18 Mei, 2021. Kushoto ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Khamis Hamza Khamis pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimpongeza Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro mara baada ya kufungua Kiwanda cha Ushonaji cha Jeshi la Polisi Tanzania kilichopo Kurasini mkoani Dar es Salaam leo tarehe 18 Mei, 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akipiga makofi na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Khamis Hamza Khamis pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro mara baada ya kukata utepe kuashiria ufunguzi wa Kiwanda cha Ushonaji cha Jeshi la Polisi Tanzania kilichopo Kurasini mkoani Dar es Salaam leo tarehe 18 Mei, 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akikagua kazi mbalimbali zinazofanywa katika kiwanda hicho cha ushonaji cha Jeshi la Polisi Tanzania kilichopo Kurasini mkoani Dar es Salaam mara baada ya kukifungua leo tarehe 18 Mei, 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akikagua kazi za upimaji na ukataji wa vitambaa vinavyotumika katika kushona sare za Jeshi la Polisi katika Kiwanda cha Ushonaji Nguo cha Jeshi la Polisi Tanzania kilichopo Kurasini mkoani Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride la Heshima lililoandaliwa na Jeshi la Polisi Kurasini mkoani Dar es Salaam mara baada ya kufungua Kiwanda hicho cha Ushonaji
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizungumza na Askari pamoja na Maafisa mbalimbali wa Jeshi la Polisi pamoja na Wageni wengine Kurasini mkoani Dar es Salaam mara baada ya kufungua Kiwanda cha Ushonaji cha Jeshi la Polisi Tanzania.

PICHA NA IKULU
Share:

Electrical Technician Mwanza at Serengeti Breweries Limited

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Description  About us From Arthur Guinness to Johnnie Walker, our business was founded on people of great character, and in 250 years, nothing’s changed. We’re the world’s leading premium alcohol company. Our brands are industry icons. And our success is thanks to the strength of our people, in every role. It’s why we trust […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Rais Samia: Makosa Yasitumike Kama Kitega Uchumi

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amelitaka jeshi la polisi kujielekeza zaidi kutoa elimu badala ya kutumia sheria zao kutoza faini. .

Rais Samia amesema hayo leo Mei 18, 2021 wakati akizindua kiwanda cha ushonaji cha jeshi la polisi kilichopo kilichopo katika Bohari Kuu ya Jeshi la Polisi Kurasini jijini Dar es Salaam.

“Takwimu zinasema kuna upungufu wa makosa na upungufu wa makusanyo ya pesa kutokana na upungufu wa makosa, nataka nielekeze kwamba kazi ya Jeshi la Polisi ni kudhibiti makosa, tusijielekeze sana kwenye kipengele cha makosa na adhabu kwamba ni kitega uchumi, zaidi zitumike kudhibiti kuliko ukusanyaji wa faini na tozo nyingine. Nihimize suala la elimu kwa raia, naona vipindi vyenu kwenye TV lakini naomba muongeze zaidi.

Kuhusu hali ya usalama nchini, Rais Samia Suluhu Hassan amempongeza Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Simon Sirro kwa kutekeleza agizo lake alilolitoa hivi karibuni la kutaka kudhibitiwa kwa vitendo vya uhalifu ambavyo vimekuwa vikijitokeza katika maeneo mbalimbali nchini.


Hata hivyo, ametaka kudhibitiwa kwa  wale wote wanaolijaribu Jeshi la Polisi kwa kuendeleza vitendo vya uhalifu.

“Baada ya kutoa ile kauli yangu kuhusu wahalifu IGP ulifanya mkutano na kuweka mikakati, lakini tunasikia bado kuna wanaojaribu kina cha maji, wanabonyeza bonyeza, nawaomba mjipange, wakibonyeza pasibonyezeke, kama mliweza huko nyuma hamuwezi kushindwa sasa. " Amesema

Rais Samia  ameongeza kuwa kuanzia sasa miongoni mwa vigezo atakavyotumia katika kuwapandisha vyeo Makamanda wa polisi  ni namna ambavyo wamekuwa wakikabiliana na vitendo vya uhalifu katika maeneo yao.

“Hii sio kwa Dar es Salaam tu, bali nchi nzima, miongoni mwa vigezo tutakavyovitumia kuteua au kutengua Makamanda wa Polisi wa Mikoa ni kasi ya kudhibiti vitendo vya uhalifu, kwahiyo mkajitahidi kudhibiti vitendo vya ujambazi,” amesema Rais Samia.



Share:

IGP Simon Sirro asema hali ya usalama nchini ni shwari na hakuna matukio ya kutisha.


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Simon Sirro amesema hali ya usalama nchini ni shwari, na hakuna matukio ya kutisha.

IGP Sirro ametoa kauli hiyo katika Chuo Cha Taaluma ya Polisi Dar es salaam,  baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzindua kiwanda cha ushonaji cha Jeshi la Polisi.

Amesema kuna matukio madogo ya uhalifu ambayo yamekuwa yakitokea katika maeneo mbalimbali nchini, ambayo Jeshi la Polisi nchini limekuwa likikabiliana nayo.

Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi nchini amesema matukio ya uhalifu nchini yameendelea kupungua, na kutolea mfano katika kipindi cha mwezi Januari hadi Aprili mwaka huu yamepungua kwa zaidi ya asilimia 13 tofauti na ilivyokuwa katika kipindi kama hicho mwaka 2020.

Amesema katika kipindi hicho hicho, pia ajali za barabarani zimepungua kwa asilimia 29.1.

Kwa mujibu wa IGP Sirro, Jeshi la Polisi nchini kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ndani na nje ya nchi, linaendelea kupambana na vitendo vya ugadi na biashara ya dawa za kulevya.

Kuhusu nidhani ndani ya Jeshi la Polisi, IGP Sirro amesema ni ya kuridhisha na askari ambao wamekuwa wakikiuka sheria wanachukuliwa hatua za kinidhamu.



Share:

Senior Manager – Advisory at PwC

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Description & Summary At PwC, our purpose is to build trust in society and solve important problems. We are a network of firms in 157 countries with more than 276,000 people who are committed to delivering quality in Assurance, Tax and Advisory services. In Africa, we are the largest provider of professional services with […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

National Consultant at International Organization for Migration

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Terms of Reference REF: IOM/DAR/007/2021 Assignment Title: National Consultant Duty Station : Home Based. Type of Appointment : Consultancy Contract Estimated start date: June 2021 Established in 1951, IOM is a Related Organization of the United Nations, and  as the leading UN agency in the field of migration, works closely with governmental, intergovernmental and non- […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

CHIEF EXECUTIVE OFFICER at TEMESA

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST CHIEF EXECUTIVE OFFICER – 1 POST POST CATEGORY(S) BANKING, ECONOMICS AND FINANCIAL SERVICES ENGINEERING AND CONSTRUCTION MARKETING,MEDIA AND BRAND TRADES AND SERVICES EMPLOYER Tanzania Electrical,Mechanical and Electronics Services Agency (TEMESA) APPLICATION TIMELINE: 2021-05-17 2021-05-30 JOB SUMMARY The Chief Executive Officer is responsible for the overall management of the TEMESA by ensuring that the Agency […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Wash Technical Assistant-Sanitation at Norwegian Refugee Council

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Description All NRC employees are expected to work in accordance with the organization’s core values: dedication, innovation, inclusivity and accountability. These attitudes and believes shall guide our actions and relationships. Job Description Adhere to NRC policies, tools, handbooks and guidelines Assist with the implementation of the support function portfolio according to plan of action […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger