Monday, 23 March 2020

Waziri Mkuu:tutahakikisha Corona Haisambai Zaidi Nchini

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali inaendelea kufanya tathmini ili kuhakikisha inazuia ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona (COVID-19) isiweze kusambaa kwa kiasi kikubwa nchini.

Pia, Waziri Mkuu amevishukuru vyombo vya habari nchini kwa ushirikiano wanaoutoa kwa Serikali katika kuelimisha umma namna ya kujikinga na virusi vya corona.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumatatu, Machi 23, 2020) wakati akizungumza na Mawaziri na Makati Wakuu katika Kikao Kazi kilichofanyika kwenye ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma.

Imeelezwa kuwa kinga dhidi ya virusi vya corona liwe ni jambo la kimkakati zaidi kuliko kusubiri kutibu, hivyo kwa sasa Serikali imeweka mkazo kwenye kuwahamasisha wananchi kujikinga na virusi hivyo.

“…Mawaziri hakikisheni katika kipindi hiki ziara za kwenda kukagua miradi zielekezwe kwa Wakurugenzi ikibidi kwa Makatibu Wakuu, Mawaziri mnatakiwa mjikite katika kukinga Taifa na corona.”

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amesema Serikali imeunda kamati tatu kwa ajili ya kukabiliana na homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi ya corona (COVID-19). Kamati hizo ni ya Kitaifa ambayo itaongozwa na Waziri Mkuu na itahusisha baadhi ya Mawaziri, Makatibu Wakuu na Msemaji Mkuu wa Serikali.

Kamati ya pili ni ya Makatibu Wakuu  kutoka sekta husika na itaongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi na kamati ya tatu ni ya Kikosi Kazi cha Taifa ambacho kitaongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto huku wajumbe wake wakiwa ni wataalamu akiwemo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Awali,Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema katika kipindi cha saa 24 jumla ya watu 292,142 duniani walibainika kuwa na virusi vya corona kati yao watu 12,784 walifariki.

Pia, katika Bara la Afrika watu 736 walibainika kuwa na virusi vya corona na kati yake watu 20 walifariki katika kipindi cha saa 24.

Akizungumzia kwa upande wa Tanzania, Waziri Ummy alisema jumla ya watu 12 walibainika kuwa na virusi vya corona tangu mgonjwa wa kwanza alivyogundulika nchini na kwamba wagonjwa wote hali zao ni nzuri na mmoja amepimwa zaidi ya mara mbili na kubainika kuwa hana virusi.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,



Share:

Human Resources Officer Job Opportunity at Save the Children Tanzania

Human Resources Officer Job Opportunity at Save the Children Tanzania Job Description Human Resources Officer – (200001SE) TITLE: Human Resources Officer TEAM/PROGRAMME: Human Resources and Administration LOCATION: Dar es salaam GRADE: 4 CONTRACT TYPE: National Child Safeguarding: Level 3: the role holder will have contact with children and/or young people either frequently (e.g. once a week or more)… Read More »

The post Human Resources Officer Job Opportunity at Save the Children Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Career Opportunities: Project Leader / Deputy Chief of Party – Tanzania

Organization Overview The International Development Division focuses on improving the lives and economic well-being of people in lower and middle-income countries. We command technical expertise in health, agriculture, climate change, food security and governance—as well as in international evaluation. Our multi-layered health portfolio includes policy, health promotion and disease prevention, health finance, and health systems management. In partnership… Read More »

The post Career Opportunities: Project Leader / Deputy Chief of Party – Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Lodge Assistant Manager (Tanzanian National) at Four Seasons Hotels and Resorts

Lodge Assistant Manager (Tanzanian National) Company Name: Four Seasons Hotels and Resorts Company Location:  Arusha, TZ   This position is for a local Tanzanian, If you are not Tanzanian we can not consider your application. The Ideal candidate should have luxury hotel / lode experience and previous management experience. BASIC PURPOSE: Oversees the Front Desk operations and acts… Read More »

The post Lodge Assistant Manager (Tanzanian National) at Four Seasons Hotels and Resorts appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Inter-University Council of East Africa  (IUCEA)  Job opportunities March 2020

Inter-University Council of East Africa  (IUCEA) Vacancies for the posts of Principal Innovations and Outreach Officer (P3), Senior Administrative Officer (P2) and Senior Qualifications Framework Officer (P2) at IUCEA Secretariat See attachment below for more details  Attachment: 20200319_065752_UDSM_IUCEA JOB OPPORTUNITIES.pdf Inter-University Council of East Africa  (IUCEA)  “Quality Education for Development”  Vacancies for the posts of Principal Innovations and Outreach… Read More »

The post Inter-University Council of East Africa  (IUCEA)  Job opportunities March 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

JAMHANGA & SHOMARI - CORONA

Huu hapa wimbo mpya wa Jamhanga na Shomari unitwa Corona.
Sikiliza Hapa chini
Share:

Wizara Ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Yatekeleza Agizo La Rais Magufuli Kabla Ya Siku 7

Waziri  wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe, amezindua rasmi magari kupita katika daraja la Kiyegeya la mchepuko lililopo Wilaya ya Kilosa katika barabara ya Morogoro- Dodoma kabla ya siku saba zilizoagizwa na Rais John Magufuli.

Agizo la Rais Magufuli lilitolewa Machi 16 mwaka huu, wakati akiwa kwenye daraja hilo na kubaini kuwapo kwa uzembe katika usimamizi wa ujenzi wake na kutoa siku saba kwa waziri na watendaji wake kukamilisha daraja la mchepuko na magari kupita haraka, huku akisisitiza asisikie magari yamekwama katika eneo hilo.

Kukamilika kwa muda mwafaka kwa ujenzi wa daraja hilo umechangiwa na uamuzi wa wizara hiyo kununua makalvati makubwa 120 ya zege kutoka Kampuni ya Yapi Merkezi ya Uturuki inayojenga mradi wa reli ya kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam -Makutupora.

Akizungumza wakati wa kuanza kupita kwa magari ya kwanza ya majaribio, Waziri Kamwelwe alisema daraja hilo la mchepuko lina upana wa mita tisa, ambalo lina uwezo wa kupitisha magari makubwa mawili.

“Niliamua kuitumia gari langu liwe ofisi ya muda, tulikaa mimi mwenyewe, Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Elius Mwakalinga na Mtendaji Mkuu wa Tanroads, Mhandisi Patrick Mfugale na kuja na mwafaka wa kununua makalvati makubwa ya zege 120 kutoka Reli ya SGR,” alisema Waziri Kamwelwe.

Alisema daraja hilo kuwa na uwezo huo wa kupitisha magari hayo mawili kwa mara moja, lakini kwa sehemu iliyozinduliwa litaruhusiwa kupita gari moja kwa zamu ili kuruhusu kuendelea ujenzi mwingine wa kuunganisha daraja lingine lenye upana kama huo liendelee.

“Kama mlivyosikia mimi na wenzangu tulipewa siku saba na Rais Dk. Magufuli tuwe tumekamilisha kujenga daraja la muda la mchepuko, na wizara imekamilisha ujenzi wa daraja hilo ndani ya muda wa siku sita, na hivi sasa nazindua rasmi kuanza kupita magari,” alisema Waziri Kamwelwe.

Akizungumzia kuhusu ujenzi wa daraja lingine ambalo lina upana kama huo litakalounganishwa na lilokamilika, alisema lengo lake litakapokamilika kuwezesha kupita magari hayo kwa nafasi zaidi kila upande katika daraja hilo.

Hata hivyo, Waziri huyo hakuwa tayari kutaja gharama ya ununuzi wa makalvati hayo, na kueleza kila kalvati moja lina urefu wa mita mbili na uzito wa tani 13 na mpaka kukamilika hatua ya pili yatatumika jumla makalvati 120.

“Njia hii ya mchepuko sasa itakuwa ni ya kudumu kwa magari kupita pande zote mbili bila ya kusubiri kwa zamu,” alisema Waziri Kamwelwe.


Share:

Kilomita 39 za Lami Zaanza Kujengwa Mji wa Serikali Mtumba Dodoma

Na Mwandishi Wetu
Ujenzi wa barabara za lami katika mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma  waanza kwa kasi ili kuimarisha mawasiliano na huduma kwa wananchi.
 
Akizungumza leo Machi 20, 2020 katika mahojiano maalum, Katibu wa Kikosi Kazi cha Taifa cha Kuratibu Mpango wa Serikali kuhamia Dodoma Bw. Meshack  Bandawe amesema kuwa ujenzi huo  unahusisha barabara zenye urefu wa kilomita 39 ndani ya mji huo.
 
“Serikali inaimarisha miundombinu ndani ya mji wa Serikali ikiwemo ujenzi wa barabara  za njia mbili zenye urefu wa kilomita 28 na zenye njia 4 kilomita 11, ujenzi huu unaenda sambamba na kujengwa kwa miundombinu mingine kama TEHAMA, Afya, Makazi na Sehemu za Biashara”, Alisisitiza Bandawe
 
Akifafanua  Bandawe amesema kuwa  ujenzi wa miundombinu katika mji wa Serikali unaenda sambamba kujengwa kwa majengo ya gorofa kwa ajili ya matumizi ya Ofisi za Wizara 22.
 
Mji wa Serikali ulizinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli mwezi Machi 2019.


Share:

Ajali Ya Teni Yaua Watumishi Watano

Uongozi wa Shirika la Reli Tanzania -TEC unatangaza taarifa za Vifo vya watumishi 5 wa TRC.Vifo hivyo vimesababishwa na ajali ya Treni ya uokoaji kugongana na Kiberenge No.HDT-3 katika maeneo yaliyopo kati ya stesheni za Mwakinyumbi na Gendagenda tarehe 22.3.2020.

Eneo hili lipo katika Reli inayotoka Ruvu Junction  mpaka Mruanzi Junction.
 
Watumishi wa TRC walikua sita, Watumishi wanne wamefariki pale pale  katika eneo la ajari na majeruhi wawili walifikishwa katika Hospitali  ya Wilaya ya(magunga) Korogwe kwa huduma za Kitabibu.

Mpaka  ilipofikia saa tano usiku (23:00) tarehe 22.3.2020 majeruhi mmoja alifariki na kufikia jumla ya  watumishi wa TRC watano wamefariki.

Watumishi hao ni :
1.Ramadhani Gumbo-DTM Tanga
2.Eng.Fabiola Moshi DME DSM
3.Joseph Komba - ATM DSM
4.Philip Kajuna -Safety Technical
5.George Urio - Dereva wa trolley

Mpaka sasa majeruhi mmoja anaendelea na matibabu ni Guard wa treni Elizabeth Bona.

Poleni sana familia ya Reli kwa tukio hili la kusikitisha sana.
Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi kuhusu maandalizi ya kuhifadhi miili ya wapendwa wetu.

Aidha uchunguzi wa kujumuisha taasisi zingine utafanywa kubaini chanzo cha ajali hii mbaya.

Bwana ametwaa na Bwana ametoa, Jina lake lihidimiwe🙏🙏


Share:

TANZIA: Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Ilala Dk Makongoro Mahanga afariki dunia

Aliewahi kuwa Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, kabla ya kuhama CCM na kwenda CHADEMA ambako alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Ilala,Dk.Makongoro Mahanga amefariki Dunia.

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa chama hicho, Tumaini Makene, amethibitisha kutokea kwa msiba huo.

"Ni kweli aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama Ilala na Mjumbe wa Baraza Kuu la Chama amefariki asubuhi ya leo, alikuwa amelazwa tangu juzi Muhimbili, taarifa za kina zaidi tutazitoa baadaye" amesema Makene.



Share:

Nyumba (pagala) limeshuka bei tena: Mapinga jirani na Bunju

Nyumba (pagala) limeshuka bei tena: Mapinga jirani na Bunju

Pagala la vyumba 3 na kiwanja cha sqm 416 (mita 16/26) linauzwa kwa bei ya kutupwa. Huduma za umeme na maji zipo na lipo mtaa wa maana. Lipo umbali wa km 2 kutoka main road.

Wiki iliyopita bei ilikuwa milion 11, sasa imeshuka  mpaka milion 9.5
Mhitaji awahi kulipia, alipaue na kuhamia.

Kwa taarifa zaidi call 0758603077


Share:

Wenye Virusi Vya Corona Nchini Kenya Wafika 15

Waziri wa Afya wa Kenya Mutahi Kagwe ametangaza kuwa, watu wengine wanane wamethibitishwa kuwa na ugonjwa wa Corona nchini humo. Ongezeko hilo sasa linafikisha idadi ya watu 15 walioambukizwa virusi hivyo hatari nchini Kenya.

Kwa mujibu wa Waziri Mutahi Kagwe, walioambukizwa ni Wakenya watano na raia watatu wa kigeni walio na umri wa kati ya miaka 20 hadi 57.

Aidha amebainisha kuwa, Wanane hao waliingia nchini kupitia uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Jomo Kenyatta kati ya Machi 4 na 17.

Serikali kwa sasa inafanya juhudi ya kuwatafuta watu 363 walioambatana nao ili kudhibiti maambukizi.

''Inasikitisha kwamba baadhi ya Wakenya wanapuuza maagizo tuliyoweka kukabiliana na ugonjwa huu'' alisema Waziri Kagwe.

Akizungumza na vyombo vya habari Waziri wa Afya wa Kenya amesisitiza umuhimu wa Wakenya kuzingatia hatua zilizowekwa ili kuepusha maafa.

''Huu ugonjwa sio mzaha'' aliongeza kusema. Kenya inasisitiza kuwa wiki mbili zijazo zitakuwa hatari zaidi endapo hali ya maambukizi haitadhibitiwa.

Hatua za dharura zilizochukuliwa kuanzia usiku wa jana  Jumapili, baa zote zitafungwa na wenye hoteli wataruhusiwa kuuza chakula cha kubeba na kwenda kula nyumbani.

Ibada za Kanisa na Swala za pamoja Misikitini zimesitishwa huku mazishi yakiruhusiwa kuhudhuriwa na familia ya marehemu pekee. Sherehe za harusi pia zimepigwa marufuku.


Share:

Serikali ya Awamu ya Tano Yawezesha Upatikanaji wa Huduma bora za Afya Mkoa wa Morogoro

Na; Mwandishi Wetu
Shilingi Bilioni 4.5 zimetumika kujenga Hospitali za Wilaya Mkoani Morogoro ikiwa ni jitihada za Serikali kuhakikisha kuwa huduma za afya zinawafikia wananchi wote.
 
Akizungumza katika kipindi cha ‘TUNATEKELEZA’ Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bw.  Loata Ole Sanare amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imewezesha wananchi kufikiwa na huduma bora za fya katika maeneo yao.
 
“Mkoa wetu kwa sasa una Hospitali za Wilaya katika Wilaya zote baada ya Serikali kutuwezesha kujenga katika Wilaya 3 ambazo hazikuwa na Hospitali za Wilaya”, Alisisitiza Sanare
 
Akifafanua zaidi, Mhe.  Sanare  amesema kuwa Hospitali hizo zimejengwa katika Wilaya za Malinyi, Morogoro Vijijini na  Gairo  ili kuwezesha wananchi kupata huduma bora za afya. 
 
Aliongeza kuwa dhamira ya Serikali ya kuwawezesha wananchi kupitia huduma bora imeendelea kutekelezwa kupitia ujenzi wa vituo vya afya na zahanati katika Wilaya zote za mkoa huo hivyo kusogeza huduma kwa wananchi.
 
Aidha,  Serikali imewezesha Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro mjini kujenga soko lenye thamani ya shilingi Bilioni 18 ili kuimarisha upatikanaji wa huduma  kwa wananchi mjini humo na maeneo ya jirani.
 
Kipindi cha TUNATEKELEZA kinarushwa kila alhamisi kikishirikisha Wakuu wa Mikoa katika awamu hii ili waweze kueleza utekelezaji katika mikoa yao.


Share:

Iran yakata msaada wa Marekani

Kiongozi mkuu wa kidini nchini Iran, Ayatollah Ali Khamenei amesema Iran haitopokea msaada wowote kutoka Marekani, katika kubadili hali ilivyo kutokana na wimbi la maambukizi ya virusi vya corona nchini mwake. 

Katika taarifa yake hiyo Khamenei alirejea kuizungumzia dhana ya kwamba virusi hivyo ni silaha iliyoundwa na Marekani dhidi ya maadui zake.

Katika hotuba yake iliyorushwa moja kwa moja kupitia televisheni kiongozi huyo amesikika akisema wana maadui wengi lakini, mkubwa kuliko wote ni Marekani.. na sasa anataka kuwasaidia. Ni vyema taifa hilo likajikita katika kuwasaidia wananchi wake. 

Iran limekuwa eneo tete la usambaaji wa virusi vya corona, ambavyo vilianzia China mwishoni mwa mwaka uliopita. 

Hata hivyo usambaaji wa visa hivyo ulianza kuingia Marekani wiki iliyopita. 

Marekani inakabiliwa na mamia ya vifo vyenye kuhusishwa na virusi hivyo, wakati Iran vifo vyake vinapindukia watu 1000. 

Katika hatua hiyo ya kukataa msaada, Khamenei aligusia nadharia ya kwamba virusi hivyo viliundwa na Marekani kwa lengo la kuyadhoofisha mataifa adui kama China na Iran. 

-DW


Share:

Atiwa Mbaroni Kwa Tuhuma za Kumuua Mpenzi Wake

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia FESTO MADUHU [28 -30] Mbeba Mizigo @ Kuli na Mkazi wa Mtaa wa Benki Kabwe Jijini Mbeya kwa tuhuma za kumuua mpenzi wake na kisha yeye mwenyewe kujaribu kujiua kwa kisu.

Ni kwamba mnamo tarehe 22/03/2020 majira ya saa 09:00 Asubuhi huko katika nyumba ya kulala wageni iitwayo “NEGERO” iliyopo Mtaa wa Ilolo, Kata ya Ruanda, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya katika chumba namba 111 @ Victoria, Mwanamke mmoja aitwaye JESCA MICHAEL @ KUNGULU [28] Mhudumu wa Nyumba ya Kulala Wageni na Baa na Mkazi wa Ilolo Jijini Mbeya aligundulika kuuawa kwa kukabwa shingo na kupigwa sehemu za usoni na mtuhumiwa FESTO MADUHU ambaye ni mpenzi wake.

Kiini cha tukio hili ni wivu wa kimapenzi kwani mtuhumiwa alikuwa anamtuhumu marehemu kuwa alikuwa na mahusiano na mwanaume mwingine ambaye jina linahifadhiwa kwa sababu za kiupelelezi na ufuatiliaji.

Katika ufuatiliaji wa kumkamata mtuhumiwa mara baada ya tukio hilo, mtuhumiwa alikutwa akiwa amejifungia nyumbani kwake na baada ya askari kuvunja mlango wa nyumba hiyo alikutwa akiwa anaendelea kujichinja koromeo lake kwa kutumia kisu ambapo askari Polisi walimuokoa na kumpeleka Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya kwa matibabu.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya kwa uchunguzi zaidi wa kitabibu. Aidha mtuhumiwa anaendelea kupatiwa matibabu kitengo cha dharura Hospitalini hapo akiwa chini ya ulinzi na mara apatapo nafuu atahojiwa na kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma za Mauaji na kujaribu kujiua.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi ULRICH MATEI anatoa wito kwa jamii kuacha kujichukulia sheria mkononi. Aidha anatoa wito kwa jamii kuacha tabia ya kupuuzia migogoro ya aina yoyote baina ya mtu na mtu au kikundi cha watu na badala yake watoe taarifa mapema sehemu husika likiwemo Jeshi la Polisi kwa hatua zaidi za kisheria.

Imetolewa na:
[ULRICH O. MATEI -SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.


Share:

Waziri Ummy Mwalimu Akutana Na Taasisi Ya Sekta Binafsi- TPSF kujadili namna ya kukabiliana na ugonjwa wa Corona

Na WAMJW-DSM
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu jana amekutana na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) na kujadili namna ya kukabiliana na ugonjwa wa Corona (COVID-19) nchini.

Katika kikao hicho, Waziri Ummy Mwalimu ameshukuru baraza hilo kwa kushirikiana na Sekta ya afya katika mapambano ya ugonjwa huo.

”Mchango wa sekta binafsi mkiwamo nyie wafanyabiashara ni muhimu kwani mtaleta manufaa makubwa katika mapambano haya,” amesema Waziri Ummy Mwalimu.

Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa TPSF, Bi. Angelina Ngalula amesema watahakikisha vifaa kinga vinavyohitajika vinasambazwa kila mkoa na wilaya nchini ili kukabiliana na ugonjwa wa homa ya Corona.

Katika kuhakikisha kwamba sekta hiyo inakabiliana na maambukizi ya homa ya Corona, TPSF imekubaliana na wamiliki nchini kuwapatia madereva na wasaidizi wao vifaa kinga.

“Sisi kama sekta binafsi tutahakikisha kwamba tunalinda ajira za watumishi wetu kwa gharama zote,” amesema Bi. Ngalula.

Naye Mwenyekiti Kamati ya TPSF Inayosimamia Jitihada za Kukabiliana na Maambukizi ya Homa ya Corona, Bw. Abdulsamad Abdulrahim amesema sekta binafsi imebainisha maeneo 26 katika Mkoa wa Dar es Salaam ambayo ni hatarishi kwa maambukizi ya homa ya Corona na kwamba vijana waelekea mikoani kwa ajili ya kubaini maeneo mengine.

Bw. Abdulrahim amesema katika upande wa elimu ya afya nyakati za dharura na majanga, wamewasiliana na kampuni za   simu na kwamba tayari zimeanza kusambaza ujumbe kuhusu elimu ya kijikinga na maambukizi ya homa ya Corona.

“Tumewatafuta wadau wanaomiliki mabango barabarani nchi nzima na wameweka ujumbe wa kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa huu. Mheshimiwa Waziri hivi tunavyozungumza, tayari jumbe mbalimbali zimeshawekwa kwenye mabango ya barabarani,” amesema Bw. Abdulrahim.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu March 23























Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger