Friday, 8 February 2019

JAMAA AMUUA MCHEPUKO WA MKEWE BAADA YA KUWANASA WAKIFANYA MAPENZI KITANDANI KWAKE


Jamaa mmoja mwenyeji wa eneo la Bandari, Kisumu nchini Kenya anasakwa na maafisa wa polisi kwa tuhuma ya kumuua mchepuko wa mkewe baada ya kuwanasa 'live' wakihondomola tendo la ndoa 'wakifanya mapenzi' kwenye kitanda chake.


Majirani wameeleza kuwa jamaa huyo ambaye ni Mwendesha boda boda alirudi nyumbani kutoka kwa mkewe mwingine usiku wa manane Februari 7,2019 na baada ya kuingia ndani alishangaa kuona simu asiyoijua pamoja na nguo zikiwa kwenye kiti.

Alichukua mwendesha bodaboda huyo baada ya  kuona vitu hivyo aliingia moja kwa moja hadi chumba cha kulalia ili kushuhudia ni nini kilichokuwa kikiendelea. 

Alikasirika baada ya kumuona jamaa huyo/mgoni akimmchovya mkewe kitandani akachukua kisu na kumdunga mara kadhaa na kumuua papo hapo.

"Alinaswa akiwa uchi, nguo zilikuwa kwenye kiti na simu yake ilikuwa mezani. Mumewe aliingia chumbani na kumpata mume huyo amemlalia mkewe. Mlango haukuwa umefungwa,’’ jirani moja alisimulia.

Hata hivyo, mkewe huyo aliweza kuponyoka akiwa uchi na kujinusuru ili kuepusha balaa zaidi kutokana na fumanizi hilo. 

Inadaiwa kuwa muuaji huyo alichukua nafasi na kusafisha kisu chake kwa kutumia chupi ya jamaa huyo pole pole kabla ya kutoroka.

 Polisi walifika eneo hilo na kuchukua mwili wa marehemu huku msako ukianzishwa kumkamata mume huyo muuaji.

Share:

HABARI KUBWA KWENYE MAGAZETI YA TANZANIA LEO FEBRUARI 8,2019.

Fahamu yote yaliyojiri katika Magazeti ya Tanzania leo Februari 8, 2019. Hapa unapata habari zote zilizopewa uzito katika kurasa za mbele na kurasa za nyuma za habari za michezo na burudani.

Source

Share:

Thursday, 7 February 2019

SIMBA SC YAREJEA TATU BORA LIGI KUU KWA KISHINDO BAADA YA KUICHAPA MWADUI FC 3-0


Simba SC imerejea ndani ya tatu bora kwenye Ligi Kuu ya soka ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 3-0 usiku wa leo dhidi ya Mwadui FC ya Shinyanga Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam.

Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi 36 sawa na Lipuli FC baada ya kucheza mechi 15, lakini inapanda nafasi ya tatu kwa wastani wake mzuri wa mabao kuliko timu ya Iringa ambayo pia imecheza mechi tisa zaidi.

Yanga SC inaendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi zake 55 za mechi 22, ikifuatiwa na Azam FC yenye pointi 48 za mechi 21. 

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Alfred Vitalis wa Kilimanjaro aliyesaidiwa na washika vibendera, John Kanyenye wa Mbeya na Leonard Mkumbo wa Manyara hadi mapumziko tayari Simba SC walikuwa mbele kwa mabao 3-0. 

Mshambuliaji wa kimataifa wa Rwanda mwenye asili ya Uganda, Meddie Kagere alianza kuifungia Simba bao la kwanza dakika ya 21 kwa kichwa akimalizia krosi ya Mzambia, Clatous Chama aliyenzishiwa kona fupi na kiungo mwenzake, Mnyarwanda, Haruna Niyonzima.

Kiungo Muzamil Yassin akaifungia Simba SC bao la pili dakika ya 25 kwa shuti kali baada ya pasi ya Nahodha John Raphael Bocco kufuatia krosi ya beki Zana Coulibally kutoka Burkina Faso.

Mshambuliaji na Nahodha John Raphael Bocco akaifungia Simba SC bao la tatu dakika ya 29 kwa kichwa akimalizia krosi nzuri ya Niyonzima.

Kipindi cha pili, Simba ilipata pigo baada ya kiungo wake Muzamil Yassin kuumia na kushindwa kuendelea na mchezo, nafasi yake ikichukuliwa na Jonas Mkude.

Mechi iliyotangulia jioni ya leo, Coastal Union ililazimishwa sare ya kufungana 1-1 na Ruvu Shooting Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga, wageni wakitangulia kwa bao la William Patrick dakika ya 37 kabla ya wenyeji kusawazisha kupitia kwa Raizin Hafidh dakika ya 65.

Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Aishi Manula, Zana Coulibally, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Paul Bukaba, Pascal Wawa, James Kotei, Muzamil Yassin/Jonas Mkude dk60, Haruna Niyonzima, John Bocco, Meddie Kagere/Adam Salamba dk78 na Clatous Chama/Emmanuel Okwi dk70.

Mwadui FC: Mussa Mbisa, Revocatus Richard, Emanuel Kichiba, Frank Magingi, Joram Mgeveke, Iddy Mobby, Wallace Kiango, Abdallah Seseme, Fabian Gwanse/Ibrahim Irakoze dk87, Ditram Nchimbi na Gerard Mdamu/Salimu Aiyee dk46.

Via>>Binzubeiry blog
Share:

PESA ZA MBUNGE ROSE TWEVE ZAGEUKA LULU KWA AKINA MAMA WA KATA YA NZIHI IRINGA


Baadhi ya wajumbe wa kikundi cha Rose Tweve kilichopo kata ya Nzihi mkoaniri Iringa wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kikao chao cha kikatiba 
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rose Tweve ameendelea kuitunisha mifuko ya wanawake wa UWT mkoa wa Iringa kwa kukuza mtaji walipewa awali na mbunge huyo.

Akizungumza na blog hii mwenyekiti wa kikundi cha Rose Tweve, Aulelia Mbembe amesema mbunge wa viti maalum Rose Tweve aliwapa mtaji wa shilingi laki tano(500,000/=) kwa kuanzia lakini waliunda kikundi na kukiita Rose Tweve kwa lengo la kumuuezi mbunge huyo kwa mchango wake kwa wanawake wa UWT kata ya Nzihi mkoani Iringa.

“Mbunge alitupa mtaji lakini tulijiongeza kwa kukopeshana kwa riba ndogo ambayo tulijipangia sisi wenyewe kwa kukopeshana na kukutana kwa mwezi mara moja kwa ajili ya kununua hisa pamoja na kubadilisha mawazo kwa lengo la kukuza mitaji na kufanya maendeleo yetu binafsi” ,alisema Mbembe. 

Mbembe alisema mtaji wa kikundi cha Rose Tweve kimefanikiwa kukuza mtaji kutoka shilingi laki tano 500,000/=) hadi kufikia kiasi cha shilingi milioni kumi laki moja na nusu (10,150,000/=) kwa kipindi cha miaka mitatu kutoka mwaka 2017 hadi hii leo hapo ndio utajua kuwa ukimwezesha mwanamke unakuwa umeikomboa jamii.

‘’Kama kikundi tunategemea kuja kuwa na miradi yetu mikubwa itakayokuwa inaingiza faida kwetu na taifa kwa ujumla kupitia kulipa kodi kwa miradi hiyo ,lakini tunategemea kutembelea na kusaidia vikundi vya watu maalumu kama vile walemavu ,yatima ,wazee wasiojiweza,na waathirika wa vvu,yote haya ni mchango na matunda ya Mbunge Rose Tweve ,kwa kweli shukrani nyingi zifike kwake ,na viongozi wengine wachukue mfano wa mbunge dada Rose Tweve kwa kusaidia jamii kama Rose Tweve alivyotusaidia sisi kikundi cha akiba cha wanawake(UWT) Rose Tweve Nzihi”, alisema Aulilelia Mbembe mwenyekiti wa kikundi hicho.

“Hebu angalia ndugu mwandishi wa habari jinsi gani wanawake wa UWT kata ya Nzihi tulivyoweza kutumia vizuri fursa tuliyoipata kutoka kwa mbunge Rose Tweve kwa kutusaidia kubadilisha maisha yetu kwa kuweza kujikimu kimaisha tofauti na ilivyokuwa hapo awali hivyo tunamshukuru sana mbunge Rose Tweve”, alisema Mbembe.

Mery Msigara ni moja wa wajumbe wa kikundi cha akiba cha Rose Tweve alisema kuwa alikuwa anashinda nyumbani kwa kumtegemea mume wake kwa kila kitu lakini baada ya kujiunga kwenye kikukidi cha Rose Tweve amekuwa mjasiriamali anayeweza kufanya biashara ndogondogo na kupata faida kila kukicha huku familia yake ikipata maendeleo ukilinganisha na awali,yote haya ni matunda ya mbunge Rose Tweve.

Wajumbe katika kikundi hicho wameonekana kuwa na malengo makubwa katika kufanikiwa huku wakisema kwa mwanga waliooneshwa na mbunge Rose Tweve wanaamini watafikia malengo yao ya mbali kimafanikio kupitia kikundi hicho cha akiba cha Rose Tweve .

Hadi sasa mbunge Rose Tweve amefakiwa kuvifikia na kuvitembea jumla ya vikundi 92 vya mkoani iringa na kuviwezesha kama ilivyo kwa hiki kikundi cha kata ya Nzihi. 

Na Fredy Mgunda - Iringa 
Share:

SIMBA YAANZA NA MWADAUI YAICHAPA 3-0

Na Shabani Rapwi. Klabu ya Simba SC imeibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mwadui katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) ulipigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Ushindi huo unaifanya Simba SC kufikisha jumla ya alama 36 katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ikiwa na michezo 6 mkononi, ikizidiwa alama 19 na kinara wa Ligi Yanga SC aliyefikisha alama 55 katika michezo 22. Mabao ya Simba katika mchezo huo yamefungwa na Meddie Kagera dakika ya 21′, Mzamiru Yassin dakika ya 26′ na John…

Source

Share:

WALIOBAINIKA MAUAJI YA WATOTO NJOMBE KUANZA KUBURUZWA MAHAKAMANI

Na.Amiri kilagalila Serikali mkoani Njombe inategemea kuanza kuwaburuza mahakamani siku ya kesho wale wote waliouhusika na mauaji ya watoto wadogo mkoani Njombe kutokana na upelelezi kukamilika kwa baadhi ya kesi Mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher olesendeka aliyasema hayo hii leo mbele ya makamu mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM Tanzania bara Philip Mangula katika mkutanao na mabalozi wa halmashauri ya mji mdogo wa makambako pamoja na viongozi wa chama hicho mkoa uliofanyika katika ukumbi wa shule ya secondari makambako mjini humo. “Tulijipanga vizuri tuliomba nguvu ya ziada kutoka makao…

Source

Share:

CHADEMA WAMJIBU NDUGAI KAULI YAKE YA KUTAKA KUSITISHA MSHAHARA TUNDU LISSU


Tundu Lissu

CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KAULI YA SPIKA WA BUNGE JOB NDUGAI KUTAKA KUSITISHA MSHAHARA WA MBUNGE TUNDU LISSU

Leo tarehe 07.02.2019 tumeisikia kauli nyingine tena ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa anasitisha mshahara na malipo yote ambayo Mhe.Tundu Lissu anastahili kulipwa kwa mujibu wa Katiba na sheria zetu.

Spika ametoa tangazo hilo siku chache tangu alipotoa matangazo mengine mawili kuwa anafikiria kumfuta Ubunge na alishamlipa fedha za matibabu kiasi cha shillingi milioni 250, jambo ambalo ilikuja kuthibitika Kuwa ni uongo na Spika alisema amenukuliwa kimakosa!

Spika wa Bunge ametoa kauli hizi katika kipindi ambacho anapambana kuonyesha kuwa Bunge analoliongoza sio 'Dhaifu' kama ambavyo alinukuliwa akisema CAG na ambaye aliitwa kwenye kamati ya Bunge ili akathibitishe kauli yake kuwa 'Bunge ni dhaifu' na tangu alipoenda mbele ya Kamati Spika hajawahi kuelezea UMMA kama kamati ililubaliana na hoja za CAG kuwa Bunge ni dhaifu ama laa!

Tunapenda kumkumbusha Spika wa Bunge kuwa 'taasisi' isiyofuata Sheria na Kanuni ambazo imejiwekea na badala yake ikafuata kauli na matamko ya mtu yaliyo kinyume na sheria na kanuni za taasisi katika kujiendesha ni taasisi dhaifu Sana.

Tunamkumbusha Spika wa Bunge kuwa wapo wabunge wengi kwenye historia ya Bunge letu ambao wamewahi na wengine wapo kwenye matibabu na haijawahi kutokea tukashuhudia kiwango kikubwa cha chuki dhidi yao kama ambavyo sasa tunashuhudia kwa Mhe.Lissu ambaye jaribio la mauaji lilishindikana kwa miujiza ya Mungu.

Tunamtaka Spika wa Bunge ajue kuwa wabunge kama Prof. Mwandosya, Dr. Mwakyembe, Job Ndugai na Sasa Tundu Lissu na Nimrod Mkono ni miongoni mwa wabunge ambao wamelazwa hospitalini kwa kipindi kirefu na katika historia ya Bunge hatujawahi Kuona kauli za chuki kama ambavyo zinatolewa dhidi ya Mhe.Lissu.

Chadema tunasikitishwa Sana na kauli hizi kwani ni uthibitisho wa wazi kuwa Bunge lilipokataa kulipia matibabu ya Lissu walikuwa wana nia Mbaya dhidi ya maisha yake na walipoona watanzania wameendelea kulipia matibabu yake imewaumiza !

Chadema tunamtaka Spika wa Bunge asimamie sheria na kanuni za Bunge na ajue kuwa wabunge wana haki ambazo zipo kwa mujibu wa Sheria na hawafanyi kazi zao kwa kutegemea fadhila.

Tunawaomba Wanachama wetu wamuombee Spika pamoja na wabunge ili waachane na 'roho za chuki' dhidi ya mbunge !ambaye Mungu alimuokoa baada ya kupigwa risasi 16 zilizoingia ndani ya mwili wake.

Tunapenda kumkumbusha Spika Ndugai kuwa haki huinua Taifa.

Imetolewa na;

John Mrema

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje

07 Februari, 2019
Share:

Ulimbukeni Mtandaoni : MUME AUAWA BAADA YA MKE KUCHUKUA MABUNDA YAKE YA PESA NA KUJIGAMBA NAYO FACEBOOK

Bwana mmoja raia wa Nigeria aitwaye Enango Gelsthorpe Sege ameuawa kwa kupigwa na majambazi waliojihami kwa silaha baada ya mke wake kujigamba mtandaoni /facebook akiwa na mabunda ya pesa zake. 

Mtu anayedai kuwa kaka yake marehemu, kwa masikitiko makubwa alisema alipokea taarifa kuhusu kifo hicho Jumanne, Februari 5,2019.

 Enango Gelsthorpe Sege aliuawa kwa kupigwa risasi na majambazi baada ya mke wake kujigamba mtandaoni akiwa na mabunda ya pesa. 

 Ibomo Rafeal Seimiengha, ambaye ni kaka ya marehemu alisema kwamba, Enango alishambuliwa na majambazi hao na hatimaye kupigwa risasi.

 "Nilipata habari hizi za kutisha jana. Kaka yangu alipigwa risasi nyumbani kwake na watu wasiojulikana waliokuwa wamejihami kwa silaha. Ni makosa ya mke. Mke alichapisha picha Facebook akiwa na mabunda ya pesa. Kaka yangu alikuwa amelipwa na kampuni yake. Lala Salama Enango Gelsthorpe Sege.",alieleza.

Inaelezwa kuwa marehemu aliuawa akiwa nyumbani kwake na majambazi hao walivunja na kuingia bila ya yeye na mke wake kufahamu.

 Kabla ya kifo chake, Enango alikuwa amelipwa na mwajiri wake na aliamua kwenda na mabunda ya noti nyumbani kwake. 

Kisha mke wake aliyekuwa na furaha mpwitompwito alijipiga picha akiwa na mabunda ya noti hizo mkononi na kuzianika mtandaoni.

 Katika picha hizo, ilikuwa bayana kwamba, mke wake Enango aliutaka ulimwengu mzima kuona jinsi walivyokuwa na utajiri wa pesa lakini mwisho ukawa mbaya sana. 

Share:

SIMBA NA YANGA ZATUPWA NAFASI ZA SITA NA SABA


Hatimaye bodi ya ligi (TPLB) imeweka wazi kuwa moja ya tatizo kubwa linaliosababisha kubadilishwa kwa ratiba ya ligi kuu ni timu kutokuwa na viwanja vyake ambapo katika timu 20 za ligi kuu zinazomiliki viwanja ni tano pekee na Yanga na Simba si miongoni mwao.

Akiongea kwenye mahojiano maalum na www.eatv.tv, Mtendaji mkuu wa Bodi ya ligi Boniface Wambura amesema tangu kuanza kwa msimu wa 2018/19 ni viwanja vitano pekee ambavyo havijabadilishiwa mechi.

''Suala la ligi kubadilika lipo tu na sio kwa matakwa yetu muda mwingine ni changamoto ya matumizi ya viwanja ambapo mnaweza kupanga vizuri ratiba lakini uwanja ukabadilishiwa matumizi na kwakuwa klabu haikumiliki lazima ikubali kupisha'', amesema.

Aidha Wambura amezitaja timu 5 zinazomiliki viwanja kuwa ni Azam FC (Azam Complex), Mtibwa Sugar (Manungu), Mwadui FC (Mwadui Complex), Ruvu Shooting (Mabatini) na JKT Tanzania (JKT Mbweni).

Wambura amesema kama timu zitamiliki viwanja vyake itapunguza ratiba kubadilika mara kwa mara tofauti na sasa ambapo mechi moja tu ikibadilika inakuwa na athari za moja kwa moja kwenye michezo mingine.
Chanzo - EATV
Share:

MBUNGE ATAKA MASHINE KUPIMA WABUNGE WENYE MKONO WA SWETA

Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Jackline Ngonyani ametaka wabunge ambao hawajafanyiwa tohara kuchunguzwa na wakibainika wafanyiwe, akibainisha kuwa hiyo ni mbinu mojawapo kupambana na maambukizi ya Ukimwi.

Jackline ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Februari 7, 2019 bungeni jijini Dodoma katika mjadala wa taarifa ya kamati ya Bunge ya masuala ya Ukimwi.

Amesema kwa utafiti ambao umefanyika unaonyesha wanaume ambao hawajatahiriwa wamekuwa wakiambukiza magonjwa mbalimbali, ukiwemo Ukimwi kwa asilimia 60.

Mbunge huyo alikatishwa na mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini aliyempa taarifa kwamba hata Bunge la Kenya liliweka wataalam mbele ya mlango wa Bunge, wale waliobainika hawajatahiriwa walipata tiba.

“Ni sahihi kabisa Spika unaweza kuchukua utaratibu huo ili kuepuka maambukizi ya Ukimwi,” amesema Selasini.

Baada ya taarifa hiyo, Jackline aliendelea kuzungumza akibainisha kuwa zoezi hilo ni vyema lianzie kwa wabunge na watakaobainika hawajatahiriwa wafanyiwe tohara mara moja.

Amesema pia wasiofanyiwa tohara wamekuwa wakiambukiza kansa ya kizazi kwa wanawake.

Mbunge wa Mtwara Vijijini (CCM), Hawa Ghasia alimpa taarifa Jackline kuwa wakati akitoa hoja ya wabunge wanaume wapimwe mikono sweta, hawakuwepo ndani ya ukumbi wa Bunge ili waweze kuunga mkono hoja hiyo.

Ghasia amesema jambo la kusikitisha wasiofanyiwa tohara wanakwenda kuambukiza magonjwa wanawake.

Hata hivyo, mbunge wa Geita (CCM), Joseph Kasheku ‘Musukuma’ alitoa taarifa akisema si jambo jema kutaka wabunge wasiofanyiwa tohara waweze kutambulika na kufanyiwa.

“Lakini pia takwimu zinaonesha kuwa hata wanawake waliokeketwa pia wanachangia maambikizi ya Ukimwi. Hivyo tuwekewe mashine ili wakati tunapima wanaume wasiotahiriwa basi tupime na wanawake waliokeketwa,” amesema.

Na Sharon Sauwa, Mwananchi
Share:

WAJASIRIAMALI DODOMA WAIPA SIKU 14 HALMASHAURI KUZUIA MAGARI YA MIZIGO SOKONI

Umoja wa wafanya Biashara wa Masoko Rasmi ya matunda, mboga mboga na samaki wabichi wametoa siku 14 kwa halmashauri ya jiji la dodoma kuhakikisha wanafanyia kazi matamko na matangazo ambayo yamekuwa yakitolewa na mamlaka hiyo kuhusu kutoruhusu magari ya mizigo na wauzaji jumla wa bidhaa hizo kuhakikisha wanashusha bidhaa hizo kwenye soko rasmi la bonanza na sio mahali pengine Akitoa tamko hilo la umoja huo wa wafanyabiashara saidi muumba katibu wa soko la tambukareli amesema kuwa tangu mwaka 2009 halmashauri ya jiji la dodoma lilizuia magari yakushusha bidhaa za samaki…

Source

Share:

KAULI YA WAZIRI MKUU KUHUSU ONGEZEKO LA MISHAHARA KWA WATUMISHI WA UMMA TANZANIA


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa, amewataka watumishi wa umma kuwa na subira kwa sababu Serikali inaendelea na mchakato wa kuwatambua watumishi wa umma halali na kufanya ulinganifu wa mishahara katika kada mbalimbali ili watumishi hao waanze kulipwa mishahara stahiki.

Waziri Mkuu Majaliwa ameyazungumza hayo leo Jijini Dodoma wakati alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Mbozi, Mhe Pascal Haonga, lililohoji juu ya ongezeko la mishahara kwa watumishi wa umma chini ya Sheria ya Utumishi wa Umma.

Mhe. Majaliwa amefafanua kuwa mwanzoni nchi ilikuwa na idadi kubwa ya wafanyakazi hewa ambapo wote kwa pamoja walikuwa wakilipwa mishahara na posho mbalimbali hivyo, ili kuwatambua watumishi halali Serikali iliamua kufanya uchunguzi na kuwagundua watumishi hao hewa.

Pia, Serikali ilifanya uchunguzi mwingine wa kuwatambua watumishi wenye vyeti stahiki vya kufanya kazi mbalimbali Serikalini kwa mujibu wa Kanuni za Utumishi wa Umma.

Mhe. Majaliwa ameongeza kuwa baada ya kumaliza utambuzi wa watumishi halali, Rais Dkt. Magufuli aliunda Tume ya Mishahara na Motisha kwa ajili ya kufanya mapitio ya kada zote za Utumishi wa Umma na viwango vya mishahara ili kutambua ulinganifu kati ya stahiki ya mshahara na kada husika.

"Lengo la Rais Magufuli kuunda tume hiyo ni kufanya tathmini nzuri ili kutambua weledi wa kazi, uwajibikaji na tija inayopatikana mahala pa kazi, hivyo baada ya kukamilika Serikali itatoa taarifa," alisema Mhe. Majaliwa.

Aidha, Mhe. Majaliwa ametoa rai kwa Watumishi wa Umma kuendelea kuiamini serikali kwani ina nia ya dhati kuhakikisha watumishi wote wanapata haki zao stahiki vile vile mpaka sasa mjadala kati ya Serikali na Vyama vya Wafanyakazi unaendelea vizuri.
Na Jacquiline Mrisho - MAELEZO
Share:

WATUMISHI WA TFS WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA SHERIA

Mkurugenzi wa Huduma za Misitu Emanuel Wilfred (pichani) amewataka watumishi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kuhakikisha wanafanya kazi kwa uadilifu na kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Umma na kujiepusha na kutenda kinyume kwenye utekelezaji wa majukumu yao.

Akizungumza katika mkutano na wafanyakazi wa amakao makuu ya TFS jijini Dar es Salaam mapema hivi leo, Wilfred amesema TFS katika kutekeleza majukumu yake ya msingi ya kuhakikisha inasimamia rasilimali za misitu ili zisaidie katika uchumi wa taifa kwa kizazi cha sasa na kijacho, imebaini kuwepo kwa ukiukwaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu miongoni mwa watumishi wake.

Amesema katika siku za hivi karibuni kumeibuka wimbi kubwa la watumishi wenye utendaji usioridhisha na wanaokiuka maadili ya utumishi wa umma waliopo makao makuu na hata mikoani. 

“Sijawahi shuhudia watumishi wengi wakichukuliwa hatua za nidhamu kama mwaka huu. Watu wanafanya mambo yasiyovumilika yani utakuta mtumishi anatoweka tu kazini bila kutoa taarifa wala kuomba ruhusa! Mtumishi kutokuwepo kazini kwa siku tano bila ruhusa wala sababu za msingi adhabu yake ni kufukuzwa kazi. Sasa nawatangazia mtumishi yoyote atakayekosekana katika kituo chake cha kazi huku mwajiri wake hajui, atachukuliwa hatua” ,amesema.

Hata hivyo, Mkurugenzi huyo aliwataka watumishi ambao hawajaenda kwenye mafunzo ya Jeshi Usu kujiandaa kisaikologia kutokana na TFS kubadiri rasmi muundo wake na kuwa Jeshi Usu ambapo tayari watumiashi wa makao makuu wameanza utekelezaji wake.

Aidha, Mkurugenzi huyo aliwaeleza watumishi hao kuwa sambamba na mabadiriko hayo kuna marekebisho ya mishahara yanayoendelea ambapo tayari kuna baadhi wamepata mshahara mpya huku wengine wakiendelea kuhakikiwa ili wapate mshahara huo.

“Watu msiwe na wasiswasi najua wengine mshapata mishahara mipya huku wengine wakiwa hawajapata, waendelee kuwa wavumilivu taratibu za uhakiki zinaendelea na kwa miezi ambayo itakuwa hamjapata mtajaza fomu za madai ili kupata haki yenu,” alisema Mkurugenzi.
Mkurugenzi wa Huduma za Misitu Emanuel Wilfred (aliyesimama) akiwasisitizia watumishi wa TFS makao makuu (hawapo pichani) kufanya kazi kwa weredi kwenye utekelezaji wa majukumu yao leo 7 Februari 2019. Aliyekaa ni Mkurugenzi wa Rasilimali Misitu, Zawadi Mbwambo akifuatilia mkutano huo.
Wengine ni wafanyakazi wa TFS makao makuu wakifuatilia mkutano huo.
Share:

SIMAI : TAMASHA LA SAUTI ZA BUSARA NI LA WAZANZIBAR WOTE


Mwakilishi wa Balozi wa Norway nchini na Mkuu wa Idara ya Ushirikiano, Trygve Bendiksby akizungumza katika tukio na waandishi wa habari leo kwa waandishi wa habari mjini Unguja, Zanzibar. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Bodi ya Busara Promotions, Simai Mohammed Said, akifuatiwa na Balozi wa Uswisi nchini Tanzania, Bi. Tinguely Mattli mwishoni kulia ni Mkurugenzi wa Busara Promotions, Mahmoud Yusuf, kushoto ni Meneja wa tamasha hilo, Ramadhani Journey leo 7 Februari 2019.(Picha zote na Andrew Chale)
Kikundi cha Mwiduka kutoka Mkoani Mbeya kikitoa burudani katika tukio hilo la mkutano wa utambulisho kwa vyombo vya Habari, Zanzibar.
Kikundi cha Mwiduka kutoka Mkoani Mbeya kikitoa burudani katika tukio hilo la mkutano wa utambulisho kwa vyombo vya Habari, Zanzibar.


Na Andrew Chale - Zanzibar 

Wafanyabiashara na wananchi wote wa Zanzibar, wametakiwa kuwa kifua mbele kila msimu wa uwepo wa tamasha kubwa la Kimataifa la muziki la Sauti za Busara kwa kuwa tamasha hilo linabeba taswira chanya ya maendeleo ya Wanzibar wote.

Ambapo pia amewataka kuchangamkia fursa ya uwepo wake kila mwaka kwani limekuwa likileta wageni wengi wanaokuja nchini kuhudhuria tukio hilo kubwa lenye kuvutia watu mbalimbali duniani kote.

Akizungumza katika mkutano na Waandishi wa Habari mjini hapa, Mwenyekiti wa Bodi ya Busara Promotions, Simai Mohammed Said, amesema tamasha hilo la siku nne ni kichocheo cha uchumi kwani watu wanafika mbali na kulishuhudia lakini pia wanafanya manunuzi na matumizi ndani ya Visiwa hivyo na kuongeza pato la serikali.

“Kuanzia leo tutashudia burudani ya muziki kutoka kwa wasanii mbalimbali wa ndani na nje, wanamuziki hao wataonesha nyimbo za tamaduni za nchi zao huku pamoja na kutoa burudani na mafunzo kwa watu wote.

Muziki ni biashara, muziki ni kazi na ni kazi kubwa hivyo ili kuwaunga mkono wasanii hawa ni kujitokeza kushuhudia tamasha hili ambapo pia tumetoa ofa ya punguzo kubwa kwa wenyeji.” alisema Simai.

Aidha, Simai alisema viongozi wa Busara Promotions ambao ni waasisi na waandaaji wa tamasha hilo, wamekuwa wakifanya kila aina ya mbinu kuhakikisha linaandaliwa na kufanyika kwa ubora uliokusudiwa hivyo ni juu ya wananchi haswa wazanzibar kulikubali na kulithamini ili kuinua hadhi ya Zanzibar kimataifa.

“Ili tamasha ni la kwenu Wazanzibar. Tuliinue tulipendemilango ipo wazi kwa wafanyabiashara kujitokeza kwa wingi kulidhamini kwa aina yoyote ile ya udhamini utapokelewa. Tunahitaji liweze kuwa thamani zaidi na tulienzi kwa kiwango cha juu” alisema Simai ambapo amesisitiza kuwa uwepo wa tamasha hilo si kwa ajili ya kuvutia watalii pekee bali kwa watu wote kwenye nyanja za Utamaduni, mila na desturi za mwafrika kupitia njia ya muziki.

Simai pia amesisitiza kwa vyombo vya habari na wataalamu wa teknolojia ya habari Nchini kuendelea kuwaunga mkono katika kutangaza taarifa za habari za tamasha hilo ikiwemo mandhari ya mji wa Zanzibar ili lionekane duniani kote na kuwatia hamu wale ambao hawajawahi kufika Zanzibar kuamua kwenda kushuhudia.

Kwa upande wao Mabalozi wa Uswis na Norway wanaoziwakilisha nchini zao hapa Tanzania, wamewapongeza Busara Promotions kwa namna wanavyoendesha tamasha hilo ikiwemo kukuza tamaduni za Mwafrika kupitia njia za Sanaa.

Balozi wa Uswisi nchini Tanzania, Bi. Tinguely Mattli amesema wanaamini tamasha hilo ni moja ya njia ya kufikisha ujumbe kwa wananchi kupitia wasanii ambao wamekuwa ni kioo cha jamii.

Nae Mwakilishi wa Balozi wa Norway nchini na Mkuu wa Idara ya Ushirikiano, Trygve Bendiksby alisema kupitia kauli mbiu ya mapambano dhdi ya rushwa ujumbe utafika kwa wakati na haraka kupitia wasanii ambao jamii imekuwa ikiwafuatilia kwa ukaribu hivyo wataendelea kudhamini tamasha hilo kwa kipindi kingine.

“Tunaungana na Busara Promotions kwenye tamasha ili kubwa na tutaendelea kulidhamini tamasha kwa kipindi kipindi cha miaka mitatu mingine”, alisema Bendiksby.

Ubalozi huo wa Norway na Busara Promotions wanatarajia kutiliana saini ya udhamini wa miaka mitatu mingine hapo baadae. Tayari Norway imeweza kulidhamini tamasha hilo kwa muda wa miaka tisa (9) kwa kipindi tofautitofauti.

Naye Mkurugenzi wa Busara Promotions, Mahmoud Yusuf amesema kuwa, wamekuwa wakipokea maombi mengi ya wasanii ndani na nje ambapo walio na sifa ndio wenye kuchaguliwa kila mwaka ambapo kwa mwaka huu karibu wote waliochaguliwa ni wa kiwango cha juu.

“Watu ni wengi na karibu hoteli zote zenye hadhi ya nyota nne na tano hususan maeneo ya Mji Mkongwe zimejaa na maeneo mengine watu wamejiandaa kwa ajili ya tamasha ili kubwa visiwani hapa”, alisema Yusuf.

Yusuf alisema, wenyeji wamepewa nafasi ya kipekee ya kushuhudia tamasha hilo kwa bei ya ofa maalum kwa siku tsh. 10,000 huku kwa siku zote nne akitakiwa kulipa tsh. 20,000 huku akitaka pia wawe mfano wa kuigwa kwa kuonesha ukarimu na upendo kwa wageni kuanzia vyombo vya usafiri maeneo ya mitaa na manunuzi ili wajisikie wapo na wenyeji wenye moyo wa kupokea wageni.

Naye Meneja waTamasha hilo, Ramadhan Journey alisema kuwa, kwa mwaka huu ni la 16 vikundi 44, vinatarajia kuonesha burudani kwa siku nne kwenye majukwaa matatu tofauti ya katika ukumbi wa kihistoria wa ‘Old Fort’ mjini Stone Town, Zanzibar.

Aidha, Journey ametaja baadhi ya orodha ya Wasanii kwa mwaka huu ni akiwemo: Fid Q kutoka Tanzania Bara, Wasanii wengine na Nchi zao kwenye mabano ni pamoja na: Mokoomba (Zimbabwe), Afrigo Band (Uganda), Fadhilee Itulya (Kenya), Ifrikya Spirit (Algeria), Rajab Suleiman & Kithara ( Zanzibar), Tune Recreation Committee, (Afrika Kusini), Ithrene (Algeria). Hoba Hoba Spirit (Morocco).

Pia wamo: M'Toro Chamou (Mayotte/Reunion), Trio Kazanchis +2 (Ethiopia/Switzerland), Faith Mussa (Malawi), Shamsi Music (Kenya), Sofaz (Reunion), Dago Roots( Reunion), Lydol (Cameroun), Jackie Akello (Uganda), S Kide & Wakupeti Band (Tanzania), Tausi Women's Taarab (Zanzibar), Mkubwa na Wanawe Crew (Tanzania), Damian Soul (Tanzania) na Wamwiduka Band (Tanzania) na wengineo.
Share:

BALOZI WA TANZANIA MAREKANI AMJIBU TUNDU LISSU,AKANUSHA TUHUMA DHIDI YA SERIKALI

Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu na Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Wilson Masilingi jana usiku walihojiwa katika kipindi cha Straight Talk Africa kinachorushwa na kituo cha televisheni cha Sauti ya Marekani (VOA), huku kila mmoja akipangua hoja za mwenzake.

Masilingi amekuwa balozi wa pili kumjibu Lissu baada ya siku tano zilizopita Balozi  wa Tanzania nchini Ujerumani, Dk Abdallah Possi kumjibu Lissu baada ya mbunge huyo kueleza madai mbalimbali kuhusu Serikali na jinsi alivyoshambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 Septemba 7, 2017 wakati akihojiwa na kituo cha televisheni cha Deutsche Welle cha nchini humo.

Katika kipindi cha jana kilichoongozwa na mtangazaji maarufu, Shaka Ssali kilichokuwa na mada ya ‘Haki ya Uhuru wa kujieleza’, kilikuwa na wanajopo wengine ambao ni Jon Temin kutoka taasisi ya Freedom House na mwanasiasa wa upinzani wa Uganda, Robert Chagulani maarufu kama Bobi Wine.

Akijibu maswali ya mtangazaji huyo kuhusu uhuru wa kujieleza na sababu ya Lissu kushambuliwa kwa risasi, Balozi Masilingi amesema licha ya eneo aliloshambuliwa kuwa ni la nyumba za Serikali lakini halina uhusiano na kubanwa kwa uhuru wa kujieleza.


Kwa upande wake Tundu Lissu alipinga hoja inayotolewa na serikali kuwa yeye anazuia uchunguzi kufanyika baada ya shambulizi la risasi lililofanywa na watu wasiojulikana dhidi yake na dereva wake nchini Tanzania.

“Kama ningelikufa na dereva wangu angelikufa kusingekuwa na uchunguzi?” alihoji Lissu.

Akijibu shutuma zilizotolewa na Lissu, Balozi wa Tanzania, Marekani kwanza alikosoa lugha anayotumia Lissu na kusema kuwa anasikitishwa na kitendo chake cha kutotambua kwake kazi nzuri ya serikali.

“Kutotambua kazi nzuri ya serikali ukazunguka dunia nzima unamtukana rais wako, vyombo vya dola, na kuwaambia watanzania kwamba hamna haki nchini kwenu sio sawa,” alisema Balozi huyo na kungeza;

“Kitendo cha Lissu kuzunguka dunia nzima hakisaidii. BBC, Radio Ujerumani -DW, Sauti ya Amerika -VOA, sio mahakama. Unachofanya ni kutuchafua na kutuvunjia heshima na kujichafua yeye mwenyewe.”

Lissu alipoulizwa dhana hasi juu ya kutembea kwake nchi za nje akieleza hali ya taifa la Tanzania na vitendo vya mashambulizi alivyofanyiwa kuwa ni kitendo cha kulichafuwa taifa au yeye kuwa ni adui wa Tanzania, alieleza:

“Lazima tutofautishe kati ya serikali na taifa. Serikali sio taifa. Serikali inatakiwa kuongozwa na katiba, na katiba yetu imeweka wazi mipaka ya mamlaka. Sisi raia ambao ndio taifa tunahaki ya kuwakosoa viongozi wetu” alieleza Tundu Lissu

“Kwa hivyo tunapoeleza juu ya matendo mabaya iwe tuko ndani ya Tanzania, au nje ya Tanzania au mahali popote tunatimiza wajibu wetu kama raia,” alisisitiza Lissu.

Akijibu hoja hiyo ya Lissu, Balozi alisahihisha kwa kusema kuwa nafasi ya rais na amiri jeshi mkuu wa nchi, ni nembo ya taifa na hivyo (raia) hutakiwi kumtukana rais.

“Unazungumza vitu ambavyo havipo na unapaswa uniheshimu kwa sababu mimi ni kaka yako,” Alisema Balozi  na kuongeza;

“Mimi kama Balozi nimekuja hapa kutetea heshima ya Tanzania, kwa kuwa wewe umekuwa ukitukana nchi yako,”

Balozi alimkumbusha Tundu Lissu kuwa kama kuna sababu zozote za kiushahidi, Tanzania ina Katiba ,inasheria, inamahakama huru na inabunge.

Katika majibu yake Lissu alisema, “Nilishambuliwa kwenye nyumba za Serikali, nilipigwa mara 16 na nimefanyiwa operesheni 22. Swali la kujiuliza, nani aliyetoa agizo la kuondoa ulinzi katika nyumba za Serikali?”

“Pili, hilo eneo linalindwa na CCTV (kamera) ziliondolewa siku moja kabla ya tukio. Hakuna anayejua zilikopelekwa kwa sababu polisi hawasemi zilipelekwa wapi. Ninazungumza na watu, hakuna mtu aliyehojiwa.”

Hata hivyo Balozi alimjibu Tundu  Lissu akisema: "Wewe ulikuwa hospitalini mwaka na nusu unaletewa taarifa za kukuchonganisha na serikali na unazikubali kama zilivyo. Wewe kama mwanasheria huwezi ukachukua ushahidi wa kuambiwa.

"Kama mnadhamira ya dhati ya kutaka uchunguzi ufanyike, kwa nini hutaki kurudi nyumbani ukatoe ushahidi wewe na dereva wako na badala yake unazunguka kutukana na kuichafua nchi"
Share:

NDUGAI ASEMA KUNA HAJA YA KUSIMAMISHA MSHAHARA WA TUNDU LISSU

Spika wa Bunge, Job Ndugai (Mb) amesema kuna haja ya kusimamisha mshahara wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kwa sababu hayupo bungeni, jimboni kwake wala hospitalini, na hajapewa taarifa zozote na daktari.

Spika Ndugai ametoa taarifa hiyo Bungeni wakati akijibu Muongozo wa Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Msukuma ambapo amesema Mbunge huyo hayupo Hosipitali,Hayupo Bungeni na hayupo Tanzania wala hajulikani anafanya kitu gani huko aliko hivyo hana sababu ya kuendelea kulipwa.

Tundu Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, yupo katika ziara ya siku 10 nchini Marekani baada ya kufanya hivyo kwenye nchi za Ujerumani na Uingereza.
Share:

KIUMBE CHA AJABU CHAZUA TAHARUKI SHULENI..CHURA SI CHURA,BINADAMU SI BINADAMU...


Jeshi la Polisi mkoani Rukwa limethibitisha uwepo wa tukio la uwepo wa kiumbe cha ajabu katika maeneo ya shule ya Msingi Kalalasi iliyopo Wilaya ya Kalambo, mkoani Rukwa, hali iliyozua taharuki kwa wanafunzi na walimu.

Kimwonekano, kiumbe hicho kinafananishwa na binadamu ila tu tofauti ni kuwa ni kidogo na kina urefu kati ya sentimita 12-15 tu.

Akizungumza na Daily News Digital leo asubuhi, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Rukwa, George Kyando amekiri kutokea kwa tukio hilo Jumanne wiki hii (Februari 5, 2019).

Kamanda ameeleza kuwa hadi sasa haijajulikana asili ya kiumbe hicho japo wakazi wa maeneo ya jirani na shule hiyo wameanza kulihusisha tukio hilo na ushirikina.

“Wengi wanahusisha na imani za kishirikina lakini sisi kama Jeshi la Polisi bado tunachunguza tujue kama ni binadamu au ni kitu gani maana kimofolojia ni kama mtu kina umbo la binadamu lakini sio binadamu wa kawaida.

“Kwa hiyo tumekikabidhi kwa wataalamu wa afya ili waweze kukifanyia kiumbe hiki utafiti kama huyu ni binadamu au ni kitu gani,” amesema Kamanda Kyando.


Kwa Upande wake shuhuda wa tukio hilo aliyefahamika kwa jina la Nicodemus Kapele amesema kuwa kiumbe huyo alionekana maeneo ya shule hiyo nyakati za asubuhi na kuzua taharuki miongoni mwa wanafunzi na walimu shuleni hapo hali iliyopelekea wanafunzi kuanza kukishambulia kiumbe hicho kwa mawe na kufanikiwa kukiua.

Mwalimu aliyekuwa zamu siku hiyo, Thomas Stephano ambaye alikuwa zamu siku hiyo alieleza kuwa siku ya tukio (Jumanne) alishangaa kuona kuwa muda wa mapumziko umekiwisha (saa 4:30 asubuhi) ila cha kushangaza wanafunzi bado walikuwa nje kwenye kikundi.

“Ilibidi niwafuate kuona nini kilikuwa kinafanyika kufika tu nikakuta wakikiua kiumbe hicho. Tulikimwagia maji tukione vizuri maana niliwaambia usikute ni chura…wao wakasema ni binadamu. Kweli, baada ya kumwagiwa maji, kiumbe huyo ana umbile la binadamu,” ameeleza mwalimu huyo ambaye amefundisha shule ya Msingi Kalabasi kwa miaka minne sasa. 


Naye Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Billy Philipo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ila hakuwa tayari kutoa maelezo zaidi kwa kile alichodai kuwa hawezi kuzungumzia suala hilo kwa kina kwa kuwa uchunguzi unaendelea.


Na Ombeni Utembele - Habarileo
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger