Friday, 15 April 2016
Thursday, 14 April 2016
HABARI NJEMA KWA WALIMU WANAOSUBIRIA AJIRA
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Selemani Jafo, amewatoa hofu wahitimu wa Kozi ya Ualimu ambao wamekuwa wakisubiri ajira kwa muda mrefu.
Akizungumza leo (JANA) Jijini Dsm Naibu Waziri Jafo amewataka wahitimu hao kuwa na subira kwani ajira hizo zitatangazwa muda wowote kutoka hivi sasa, huku akiwahakikishia kuwa wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu wamejipanga kuhakiki idadi ya walimu wanaohitajika.
Ameongeza kuwa licha ya uhakiki huo pia wizara yake inamalizia takwimu za walimu waliostaafu kazi pamoja na waliohama kutoka shule binafsi ili serikali iweze kujua idadi halisi ya nafasi zinazoitajika.
Jafo ameiambia Mtandao huu kuwa mwaka huu serikali inampango wa kuongeza idadi ya ajira za Walimu hadi kufikia Walimu 40,000 katika ngazi za Shule za Msingi na Sekondari.
Kuhusu ajira hizo Jafo, amefafanua kuwa mikoa ya Kigoma, Mara, Tabora na Rukwa ndio itapewa kipaumbele kwani ndio inaongoza kwa kuwa na idadi ndogo ya Walimu na hii itapunguza kasumba ya wahitimu kozi ya ualimu kupenda kuajiriwa mjini.
Selemani Jafo, amewatoa hofu wahitimu wa Kozi ya Ualimu ambao wamekuwa wakisubiri ajira kwa muda mrefu.
Akizungumza leo (JANA) Jijini Dsm Naibu Waziri Jafo amewataka wahitimu hao kuwa na subira kwani ajira hizo zitatangazwa muda wowote kutoka hivi sasa, huku akiwahakikishia kuwa wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu wamejipanga kuhakiki idadi ya walimu wanaohitajika.
Ameongeza kuwa licha ya uhakiki huo pia wizara yake inamalizia takwimu za walimu waliostaafu kazi pamoja na waliohama kutoka shule binafsi ili serikali iweze kujua idadi halisi ya nafasi zinazoitajika.
Jafo ameiambia Mtandao huu kuwa mwaka huu serikali inampango wa kuongeza idadi ya ajira za Walimu hadi kufikia Walimu 40,000 katika ngazi za Shule za Msingi na Sekondari.
Kuhusu ajira hizo Jafo, amefafanua kuwa mikoa ya Kigoma, Mara, Tabora na Rukwa ndio itapewa kipaumbele kwani ndio inaongoza kwa kuwa na idadi ndogo ya Walimu na hii itapunguza kasumba ya wahitimu kozi ya ualimu kupenda kuajiriwa mjini.
NAFASI ZA MAOMBI ZA KUJIUNGA NA VYUO VYA KILIMO DIPLOMA NA CHETI MWAKA WA MASOMO 2016/2017
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
APPLICATION FOR ADMISSION INTO DIPLOMA AND CERTIFICATE PROGRAMMES FOR
THE ACADEMIC YEAR 2016/2017
The Permanent Secretary Ministry of Agriculture Livestock and Fisheries (Agriculture)
in collaboration with National Council for Technical Education (NACTE) are officially
announcing applications for admission into diploma and certificate programmes
offered at the Ministry of Agriculture Training Institutes (MATIs) registered by NACTE
for the academic year 2016/2017. Applicants who meet the minimum entry
qualifications are invited to apply for admission by 31st May, 2016. The following are
the programmes offered at MATIs: More details
Polisi watatu Wafikishwa Mahakamani Wakituhumiwa Kupokea Rushwa
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Polisi watatu wa wilayani Urambo, Mkoa wa Tabora wamefikishwa mahakamani kwa mashitaka ya kuomba na kupokea rushwa.
Taasisi
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Tabora, iliwafikisha
askari hao jana katika Mahakama ya Wilaya ya Urambo huku mwingine
akidaiwa kukimbia.
Askari hao waliofukuzwa kazi kabla ya kufikishwa mahakamani ni John Okinda, Kabila Pius na Patrick Robart.
Anayedaiwa kukimbia ni Elisha ambaye polisi inaendelea kumtafuta.
Mbele
ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Urambo, Hassan Momba,
Wakili wa Takukuru, Edsoni Mapalala alidai washitakiwa walitenda makosa
hayo Machi 7 mwaka huu.
Mapalala
alidai siku hiyo katika kijiji cha Mkirigi, Kata ya Ilege, Wilaya ya
Kaliua, washitakiwa hao wakiwa waajiriwa wa jeshi la polisi, waliomba
rushwa ya Sh milioni tatu kutoka kwa Dotto Gandulanye ili wasimchukulie
hatua za kisheria baada ya kumkuta akiwa na bangi.
Wabunge Waiponda Bajeti Ya Viwanda
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Wajumbe wa Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira wamekerwa na kiwango
cha bajeti ya Sh95. 6 bilioni zilizotengwa kwa ajili ya Wizara ya
Viwanda, Biashara na Uwekezaji, wakisema haionyeshi malengo ya Tanzania
kuelekea kuwa nchi ya viwanda.
Wabunge walisema hayo baada ya
Waziri Charles Mwijage kuwasilisha taarifa ya makadirio ya mapato na
matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa 2016/17 mbele ya kamati.
Waziri
Mwijage alisema kati ya fedha hizo, Sh 53.5 bilioni (sawa na asilimia
56), zimetengwa kwa matumizi ya kawaida wakati Sh42.1 bilioni (asilimia
44) ni kwa ajili ya maendeleo.
Mbunge wa viti maalumu (Chadema),
Hawa Subira alisema wakati wa kujadili taarifa hiyo kuwa kiwango hicho
kinaonyesha wazi jinsi Serikali isivyo na nia ya kufufua viwanda kama
alivyoahidi Rais John Magufuli.
“Homa ya Magufuli inawaogopesha.
Nakuonea huruma waziri (kwa kuwa) unaonyesha kabisa kuwa una nia njema,
lakini kwa mtindo huu lazima uumwe,” alisema Subira.
“Tafuteni
panadol tuwasaidieni. Tunataka nchi hii kweli iwe ya viwanda. Hatuwezi
kufanya kazi namna hii watu mmejaa uoga hata kupanga bajeti ya kueleweka
mnashindwa au mkikaa mnaogopa kurekodiwa,” alisema.
Mbunge wa
Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema alisema nchi kuwa ya viwanda na
biashara inawezekana, lakini Serikali inapaswa kudhihirisha kwa vitendo
badala ya maneno kwa kuwa wizara hiyo ilipaswa kutengewa fedha za
kutosha kuonyesha njia ya kuelekea kwenye malengo yaliyokusudiwa, kama
kuruhusu safari za nje ya nchi kwa maofisa wa wizara kwa nia njema.
“Lakini
kuna mambo yamekuwa yakifanyika ya ajabu. Mimi naweka mambo ya siasa
pembeni. Serikali iangalie upya hii bajeti, lakini pia huo mradi wa
China Logistics Centre hauna msaada kwa nchi badala yake utaua hata
viwanda vidogo vidogo vilivyopaswa kusaidiwa kuinuka. Hatuwezi kuifanya
Dar kuwa Dubai wakati viwanda vya ndani havijaimarishwa,” alisema.
Kwa
upande wake mbunge wa Nkenge(CCM), Dk Diodorus Kamala alisema wakati
mwingine Serikali imekuwa ikiwapa wapinzani kauli kutokana na mambo
inayofanya.
Alisema kiwango hicho cha fedha hakiendani hata na taarifa
aliyoiyoa Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango hivi karibuni
alipowasilisha mapendekezo ya mpango wa bajeti.
“Fedha ni ndogo
wakati tunatakiwa tujikomboe kwa kupiga hatua za kimaendeleo kutoka hapo
tulipo. Mfano naona wizara imeridhika kuwa pale kwenye jengo la Water
Front, badala ya bajeti hii kueleza mpango wake wa kujenga ofisi ya
kujitegemea ili kusaidia hata kupunguza matumizi,” alisema.
Akijibu
hoja hizo, Mwijage alisema haoni tatizo kwa kiwango cha bajeti
alichotengewa kwa kuwa malengo ya wizara yake kwa mwaka huu wa fedha
pamoja na mambo mengine ni kuboresha mazingira ya viwanda vilivyopo
kisha mwaka ujao ndipo watajikita kujenga vipya.
“Ninachokiona
hapa ni kwamba wengi wanataka kuona nchi inakuwa hivyo leo, kumbe
tunatakiwa kuanzia kwa kuboresha mazingira ya hivi vilivyopo kwani vingi
vinazalisha chini ya asilimia 50 kutokana na vikwazo mbalimbali ikiwamo
miundombinu duni,” alisema.
Katika mapendekezo ya mpango wa
bajeti ya 2016/17, Serikali imeweka fedha nyingi katika kuboresha
miundombinu ya usafiri kama reli, barabara na viwanja vya ndege,
uzalishaji wa nishati ya uhakika, hasa umeme unaotokana na gesi na makaa
ya mawe na kuboresha rasilimali watu kwa ajili ya kuweka mazingira
wezeshi ya kukua kwa viwanda.
ACT-Wazalendo Waishambulia CHADEMA
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
CHAMA
cha ACT-Wazalendo Wilaya ya Shinyanga Mjini kimetamba kuwa kwenye
uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, ndicho kitakuwa mpinzani mkubwa wa CCM
badala ya Chadema.
Katibu
wa ACT-Wazalendo, Wilaya ya Shinyanga, Melkyoli Sebastian alisema hayo
baada ya kumuingiza kwenye chama hicho, kada wa Chadema, Ibrahimu
Mbogoma.
Mbogoma alikuwa mwenyekiti wa baraza la wazee kata ya Masekelo manispaa ya Shinyanga.
Sebastian
alisema chama chao kimeanza kuaminiwa na wananchi kutokana na sera zake
za kiujamaa ambazo zimelenga kumkomboa mwananchi wa hali ya chini bila
ya kubagua dini, kabila wala rangi.
Alisema
kutokana na sera hizo, ndiyo maana wanachama wa Chadema wameanza
kujiunga na chama chao baada ya kusoma alama za nyakati.
“Kujiunga
kwa kada huyo aliyekuwa Chadema ni salamu tosha kuwa Chadema inaelekea
kufa kiupinzani, nina imani wapo wanachama wengi wa vyama vya upinzani
watakuja kujiunga na ACT Wazalendo.
"Sisi tunawakaribisha waje kwa wingi ili tukijenge chama kuelekea Ikulu 2020,” alisema Sebastian.
Akieleza
sababu za kuhama Chadema, Mbogoma, alisema ameamua hivyo kutokana na
kuchoshwa na migogoro ndani ya Chadema pamoja na kuongozwa na viongozi
wasiojua majukumu yao.
Mbogoma
alisema tangu alipojiunga na Chadema mwaka 2010 hajaona mafanikio
yoyote licha ya kushika nyadhifa mbalimbali. Alisema amekuwa akikumbana
na migogoro ya mara kwa mara. Alisema anaamini ACT-Wazalendo ndicho
kitaipindua CCM.
Katibu
wa Chadema wilaya ya Shinyanga Mjini, George Kitalama alisema alikuwa
hajapata taarifa rasmi za kiofisi za kuhama kwa mwanachama wake huyo.
Hata hivyo, alisema kila mtu ana haki ya kwenda kujiunga kwenye chama anachokitaka kwa mujibu wa Sheria za nchi.
Ombaomba Waanza Kuondolewa Jijini Dar
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Agizo
la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda limeanza kufanyiwa kazi
baada ya karandinga kuanza kuwasomba ombaomba waliojaa katika maeneo
mengi jijini hapa.
Makonda
alitangaza kuanza kuwaondoa ombaomba hao juzi, huku akipiga marufuku
wananchi kuwapa pesa kwa kuwa ndicho chanzo cha kuwapo kwao jijini hapa.
Zoezi hilo la kuwaondoa watu hao lilianza juzi usiku katika maeneo ya Mnazi Mmoja, Samora na Kariakoo.
Jana maeneo mbalimbali ambayo aghalabu ombaomba hupenda kukaa yalikuwa tupu.
Maeneo hayo ikiwamo barabara ya Morocco, Magomeni Usalama, Fire na Baridi hayakuwa na watu wa kundi hilo.
Mmoja
wa ombaomba aliyekuwa na watoto wawili alipomuona mwandishi wa habari
hizi katika maeneo ya Fire, alitimua mbio na kujificha pembeni mwa
barabara, huku akisema: “Tumetoka Dodoma, hatutaki kurudi.”
Kadhalika,
operesheni hiyo licha ya timuatimua kuwakumba ombaomba, wapigadebe nao
wameunganishwa katika kundi hilo kwa kuanza kuondolewa kwenye vituo vya
mabasi.
Baadhi
ya wapigadebe hao wamedai ni vigumu kwa Makonda kuwaondoa kwa kuwa
wanachofanya ni kwa manufaa ya maisha yao na hawana pa kwenda.
Agizo
la kutaka ombaomba wakamatwe na kuondokana na vitendo hivyo liliwahi
kutolewa pia na waliowahi kuwa wakuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Yusuf
Makamba, Abbas Kandoro na Said Mecky Sadiki.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRIL TAREHE 15-4-2016


MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRIL 15 2016


















MAGAZETI YA LEO ALHAMIS APRIL TAREHE 14-4-2016







