Monday, 14 March 2016

TCU:Students undertaking a five-year Bachelor of Science in Education at ST.JOSEPH UNIVERSITY

Share:

Tamko la CUF Kuhusiana na Hali ya Kisiasa Zanzibar

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa tareh 25 Oktoba 2015, usalama wa raia wa Zanzibar na mali zao umekuwa katika hali tete. 


Hali hii inatokana na kushuhudiwa kushamiri kwa matukio ya kuogopesha wananchi na kufurutu ada ukiukwaji wa HAKI ZA BINAADAMU miongoni mwa wananchi kunakofanywa na vyombo vilivyopewa dhamana ya kuhakikisha ulinzi na usalama wa nchi yetu raia wake na mali zao.

Katika siku za hivi kadribuni, hususan baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Sali Jecha, kutangaza kinyume na katiba ya nchi, kufuta uchaguzi wa 25 Oktoba 2015 na matokeo yake, Zanzibar imeshuhudia uingizwaji na uingiaji mkubwa wa askari, vifaa na zana nzito za kivita katika visiwa vya Unguja na Pemba.

Sambamba na hayo kumekuwepo kwa askari wengi wa JWTZ wanaorandaranda mitaani wakiwa na silaha nzito za kivita na operasheni isiyo rasmi ya kuwakamata na kuwabambikizia kesi wananchi wasio na hatia na hatimaye kuwaweka katika vituo mbali mbali vya polisi na kuwanyima dhamana hata kwa makosa ambayo kisheria yanapaswa kudhaminiwa.

Katika mwezi wa February 2016 huko kengeja wafuasi wa CUF walikamatwa na polisi na kuwekwa ndani kwa tuhuma ya kuchoma tawi la CCM la eneo hilo. Polisi walichukuwa hatua hiyo mara tu tukio hilo liliporipotiwa kwao. Aidha katika mwezi huu wa Machi baadhi ya matawi ya CUF na Baraza za CUF zilichomwa moto na kuteketea tikitiki.

Taarifa ya uhalifu huu zlipripotiwa katika vituo vya polisi na RB kuandikwa, hata hivyo hadi hii leo hakuna yoyote aliyekamatwa kwa tuhuma ya uhalifu huo. Matukio ya uchomwaji moto na uharibifu wa mali za CUF umetokea mahala mwingi Unguja na Pemba kama vile Kisauni ambapo ofisi mpya ya CUF jimbo la Dimani zilizogharimu zaidi ya sh 90m zilichomwa moto tarehe 24/03/2015 na kuteketea. Kwa makusudi kabisa, hata baada ya polisi kupata taarifa hiyo na kulikagua eneo husika hakuna yeyote aliyetuhumiwa na kukamatwa.

Mtakumbuka kwamba tabia hii ya wananchi ambao kwa asilimia kubwa huwa ni CCM au vyombo vya serikali vilikuwa vikihujumu kwa makusudi mali ya CUF na hata mali ya serikali kama vile shule, zahanati, visima vya maji nk. Tukio la Shengajuu la 1996 ambapo watu waliofanya tukio la kcuhoma moto shule, kutia kinyesi visima walikamatwa wakiwa na petrol, bunduki, mapanga, madoo ya kinyesi vyote vikiwa usoni ya gari la idara ya usalama wa Taifa lenye namba za usajili ZNZ 1296).

Baada ya tukio hilo la kufedhehesha serikali na mapambamo yaliyofuata baina ya wafuasi wa CUF na wahalifu (usalama wa Taifa), serikali iliwaadhibu kwa kuwapiga, kuwaibia mali zao, kuwafanyia vitendo vya kinyama na kuwaweka ndani kwa zaidi ya miezi 9 wananchi wasio na hatia. Hivyo haya yanayoendelea hivi sasa huko Pemba si mambo mageni hasa katika kipindi hiki ambapo SMZ imechukia sana kwanini CUF wamegomea kushiriki uchaguzi batili wa madrudio wa 20/03/2016.

Sisi CUF tunaamini pasipo na shaka yeyote kwamba matukio ya kuchomwa moto kwa masikani na matawi ya CCM huko Pemba ama baadhi ya nyumba za watu binafsi na mali za serikali ni mwendelezo tu wa siasa chafu za chuki zinazoendelezwa na serikali dhidi ya wananchi wasio na hatia. CUF imesikitishwa sana na vitendo hivi vya kihuni na visivyoonyesha siasa za kistaarabu na inalaani vikali na kwa nguvu zote uhalifu huu ambao unarejesha nyuma ‘spirit’ ya kushindana bila kupigana.

Kwa upande mwengine, CUF imepokea taarifa kwamba zaidi ya wananchi 30 wengi wakiwa wafuasi, viongozi na wanachama wa CUF wamekamatwa na polisi na wameshikiliwa katika vituo mbali mbali vya polisi huko pemba. Utendaji huu wa Jeshi la polisi umeipelekea Zanzibar kugawika vipande vipande na kuwa chanzo cha siasa za chuki, uhasama na kusababisha nchi yetu kushindwa kutekeleza shughuli zake za kimaendeleo.

Kwa mfano amri ya Mkuu wa Mkoa kaskazini Pemba kupiga marufuku watu wasitembee baada ya saa mbili za usiku na kwamba atakayevunja amri hiyo atakamatwa na kushtakiwa kwa kosa la uzembe na uzururaji ni hatua nyengine ya SMZ ya kuwahalalilisha na kuwaweka wananchi wa mkoa wa Kaskazini Pemba katika hali ngumu ya maisha. Amri hii inazuwia hata sala za Isha na Alfajiri jambo ambalo waumini wa Kiislamu hawatakubaliana nalo.

CUF inamtaka Mkuu wa Mkoa uliotajwa hapo juu awache ukereketwa na aendeshe mkoa kwa hekima, busara, na weledi. Kuongoza watu kwa amri za kidikteta kumepitwa na wakati. Asome alama za nyakati, aache kutoa amri zinazopingana na hata haki za binaadamu.

Chama Cha Wananchi CUF kinaamini kuwa kutokea kwa matukio haya ni mwendelezo wa njama za CCM zinazoratibiwa na kutekelezwa kimkakati kwa malengo mahususi ya kuamsha hamasa na kupandisha joto la jazba miongoni mwa wananchi ili kuhalalisha mpango maalum na kutoa fursa kwa vyombo vya ulinzi na usalama kutumika kutisha, kukamata, kupiga na kufungulia mashtaka wananchi wasio na hatia.

Kutokana na unyeti wake matukio ya uvunjifu wa amani na hatua za ukiukwaji wa HAKI ZA BINAADAMU, hayapaswi kupuuzwa kwani yanaweza kupelekea kufanikiwa kwa dhamira mbaya waliyonayo baadhi ya watu katika nchi yetu wasioitakia mema Zanzibar na kwa hivyo kuathiri umoja wa kimataifa uliopo uliopatikana kwa gharama kubwa ya jasho la viongozi wazalendo, Mheshimiwa Rais mstaafu wa Zanzibar Dr. Amani Karume na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad na uhai wa wananchi wanyonge. Kwa hivyo sisi katika CUF:

• Tunavinasihi vyombo vya ulinzi na usalama wa nchi yetu kukataa katakata kuingia katika mtego wa mipango miovu ya wanasiasa waliofilisika wenye lengo la kuleta taharuki miongoni mwa wananchi na kuamsha hamasa na kupandisha jazba na ghamidha zitakazopelekea kuchafuka kwa hali ya amani ya nchi yetu. CUF inatoa wito kwa kwa vyombo vyote vya Ulinzi na Usalama hapa nchini kusimamia amani na utulivu pasi na kuegemea upande wowote wa kisiasa.

Ni muhimu vyombo hivyo vikajipambanua na kujijengea heshima na kulinda imani ya wananchi waliyonayo kwao. Kinyume na haya, vyombo vyetu vya ulinzi na usalama hasa jeshi la polisi na jeshi la wananchi wa Tanzania JWTZ, ambalo katika siku za hivi karibuni limeonekana kutumika vibaya, kufahamu kuwa mustakbali wa utu wa raia, mali zao na amani ya nchi yetu imo mikononi mwao na watakuwa wa mwanzo kuwajibika endapo jahazi la amani yetu litakwenda mrama.

• Tunaziomba Taasisi za kiraia za ndani kuacha woga na badala yake kupaza sauti zao masikioni mwa viongozi madhalimu kukemea unyanyasaji na ukandamizaji wa haki za binadamu. Aidha, CUF inaziomba jumuiya za kimataifa kuendelea kuitazama Zanzibar kwa umakini wa hali ya juu kufuatilia mwenendo na matukio na kuweka kumbukumbu kwa hatua za baadae kwa kila anaeonekana kushtadi kuonea wananchi wanyonge kutokana na nafasi yake katika utumishi wa umma.

• Tunatoa wito kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa, John Magufuli, kuchukua dhamana ya uongozi kukataa kuhadaiwa na wasaidizi wake na kukomesha matumizi mabaya ya vyombo vya ulinzi na usalama vilivyo chini ya amri yake na kudhibiti uhuni wa kisiasa wa baadhi ya watendaji wa vikosi vya Idara Maalum ya Zanzibar kama Amiri Jeshi Mkuu wa Tanzania. Kwa la zanzibar, Rais Magufuli hana pa kupenyea na kwamba atawajibika kutokana na mfumo wa Katiba, sheria na utaratibu wa kuongoza nchi tuliojiwekea.

• Tunatambua usumbufu, idhilali na mateso makubwa yanayowapata wananchi wa visiwa vyote vya zanzibar kufuatla maamuzi yao ya tarehe 25 Oktoba 2015 ya kuikataa CCM na kuamua kufanya mabadiliko katika uongfozi wa nchi. CUF inawaomba wananchi wote kuendelea na kujipamba na mavazi ya subira na kuamini kuwa hizi ni hatua za mwisho za CCM kuelekea kufutika katika nyoyo za wazanzibari na kwamba wananchi wote wausiane katika kuvumilia na kukataa kuchokozeka kwa lengo la kutunza amani ya nchi yetu na kufikia malengo yetu ya muda mrefu ya kukamata hatamu za dola ya zanzibar bila kuathiri wanachi wetu.

• CUF inawahakikishia wananchi wote kuwa haitarudi nyuma katika mapambano ya kudai haki ya wananchi na kwamba maamuzi yao ya tarehe 25 Oktoba 2015 yatazingatiwa, kuheshimiwa na hatimaye haki kutamalaki katika visiwa vya zanzibar. Ni wajibu kwa wazanzibari wote kutambua kuwa giza nene hufuatiwa na miale ya nuru inayotoa faraja kwa kila mwanandamu.
……………………………….
HAMAD MASOUD HAMAD
KAIMU MKURUGENZI WA HABARI, UENEZI NA
MAWASILIANO KWA UMMA
Share:

Picha: Wafuasi wa CHADEMA Wafurika Mahakamani Kufuatilia Kesi ya Ezekiel Wenje,mabomu yarindima mwanza

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Mamia ya wafuasi wa CHADEMA  wakiongozwa  na  Mwenyekiti  wao Freeman Mbowe leo  wamefurika mahakama  kuu  jijini  Mwanza katika kesi ya  mbunge wa zamani wa Nyamagana, Ezekiel Wenje (CHADEMA)  anayepinga  matokeo  ya  Stanslaus Mabula (CCM). 

Polisi  wametumia  nguvu  ya  ziada  kuhakikisha  ulinzi  unaimarika  mahakamani  hapo
Ezekia Wenje akiwa  Mahakamani
Mbunge wa Nyamagana Stanslaus Mabula akiwa mahakamani
Ezekiel Wenje akisubiri kutoa ushahidi
Freeman Mbowe na  Ezekiel Wenje wakiwa mahakamani
Share:

Official VIDEO | UDZM QS BAND - Nishukie wapi?

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Share:

Video Mpya: ‘My Life’ ya Dogo Janja Imeachiwa Tayari

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Baada ya kimya cha muda mrefu Dogo Janja kutoka Tip Top Connection 2016 aliachia hit single yake ya ‘My Life’, ngoma hiyo Dogo Janja amebadili ni tofauti na tulivyomzoea katika ngoma zake za nyuma. March 14 Dogo Janja kaachia rasmi video ya hit Single ya ‘My Life’ enjoy mtu wangu.
TAZAMA HAPA:

Share:

Sunday, 13 March 2016

RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI WA WAKUU WA MIKOA 26 KATI YAO 13 NI WAPYA 7 WAMEBAKIZWA NA 5 WAMEHAMISHWA.TAZAMA HAPA MAJINA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara, ambapo kati yao 13 ni wapya, 7 wamebakizwa katika vituo vyao vya kazi, 5 wamehamishwa vituo vya kazi na 1 amepangiwa Mkoa Mpya wa Songwe.
Uteuzi huo umetangazwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Mussa Ibrahim Iyombe leo tarehe 13 Machi, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam.
 
Wakuu wa Mikoa walioteuliwa ni kama ifuatavyo;
  1. Mh. Paul Makonda - Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam.
  2. Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga - Mkuu wa Mkoa wa Geita.
  3. Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu - Mkuu wa Mkoa wa Kagera.
  4. Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga - Mkuu wa Mkoa wa Katavi.
  5. Brigedia Jeneral Mstaafu Emmanuel Maganga - Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.
  6. Mh. Godfrey Zambi - Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
  7. Dkt. Steven Kebwe - Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
  8. Kamishna Mstaafu wa Polisi Zerote Steven - Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.
  9. Mh. Anna Malecela Kilango - Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
  10. Mhandisi Methew Mtigumwe - Mkuu wa Mkoa wa Singida.
  11. Mh. Antony Mataka - Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.
  12. Mh. Aggrey Mwanri - Mkuu wa Mkoa wa Tabora.
  13. Mh. Martine Shigela - Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
  14. Mh. Jordan Mungire Rugimbana - Mkuu wa Mkoa Dodoma.
  15. Mh. Said Meck Sadick - Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.
  16. Mh. Magesa Mulongo - Mkuu wa Mkoa Mara.
  17. Mh. Amos Gabriel Makalla - Mkuu wa Mkoa Mbeya.
  18. Mh. John Vianey Mongella - Mkuu wa Mkoa Mwanza.
  19. Mh. Daudi Felix Ntibenda - Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
  20. Mh. Amina Juma Masenza - Mkuu wa Mkoa wa Iringa.
  21. Mh. Joel Nkaya Bendera - Mkuu wa Mkoa wa Manyara.
  22. Mh. Halima Omary Dendegu - Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.
  23. Dkt. Rehema Nchimbi - Mkuu wa Mkoa wa Njombe.
  24. Mhandisi Evarist Ndikilo - Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
  25. Mh. Said Thabit Mwambungu - Mkuu wa Mkoa Ruvuma.
  26. Luteni Mstaafu Chiku Galawa - Mkuu wa Mkoa wa Songwe (Mkoa mpya).
Wakuu wote wa Mikoa walioteuliwa, wataapishwa Jumanne tarehe 15 Machi, 2016 saa 3:30 Asubuhi Ikulu, Jijini Dar es salaam.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
13 Machi, 2016
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MARCH 13 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

Saturday, 12 March 2016

SOMA HAPA HISTORIA NA WASIFU WA KATIBU MKUU WA CHADEMA DR.VINCENT B MASHINJI

INNOCENT-THE BLOGGER BOY  
Wasifi (CV) ya Katibu Mkuu wa Chadema Tanzania kamanda Dr. Vincent B. Mashinji
Professional experience

Clinical Advisor & TB/HIV lead

UMSOM-IHV

July 2008 - Present

ART Program Doctor/IMA team lead

IMA Worldhealth

August 2006 - June 2008 (1 year 10 months)

Medical Officer/Anaesthesiology

Regency Medical Centre

October 2005 - August 2006 (10 months)

Medical Officer

Muhimbili National Hospital

August 2003 - October 2005 (2 years 2 months)

Research Assistant

Freelance

November 2002 - August 2003 (9 months)

Intern Docor

Muhimbili National Hospital

September 2001 - October 2002 (1 year 1 month)

Education history

Open University of Tanzania

PhD

August 2010 - Present

AMREF/UCLA Anderson School

MDI Certificate

April 2010 - April 2010

Blekinge Institute of Technology

MBA

September 2007 - March 2010 (2 years 6 months)

UMSOM-IHV

IPEP Certificate

May 2008 - May 2008

Evin School of Management

Certificate in CSR

October 2005 - October 2005

Muhimbili University College of Health Sciences

MMed/Anaesthesiology

September 2003 - April 2005 (1 year 7 months)

Muhimbili University College of Health Sciences

Certificate in Research Methodology

September 2004 - September 2004

Makerere University

MBChB

October 1995 - July 2001 (5 years 9 months)

Mzumbe High School

ACSEE

July 1992 - June 1994 (1 year 11 months)

St. Pius X Seminary, Makoko

GCSEE

January 1988 - October 1991 (3 years 9 months)

Iligamba Primary School

Leaving Certificate/Primary School

January 1981 - October 1987 (6 years 9 months) 

Share:

Katibu Mkuu wa CHADEMA ni Dr Vicent Mashinji ,Kuchukua Mikoba ya Dr Slaa

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimemteua Dr Vicent Mashinji  usiku  huu  kuwa katibu mkuu mpya wa chama hicho kuchukua  nafasi iliyoachwa wazi na Dr Slaa ambaye alijiuzulu wadhifa  huo mwaka  jana.
Share:

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUAJIRI WAHITIMU WA VYUO VYA KILIMO WALIOSOMA KOZI MAALUM 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
 

Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi inautangazaia umma kuwa wahitimu mahiri 10,629 waliofuzu Vyuo vya Kilimo vya Inyala, Mtwara, Horti Tengeru, Igurusi, Katrin, Ukiriguru, Maruku, Uyole, KTC Moshi, Mlingano, Tumbi, Ilonga, NSI Kidatu na Mubondo, wanaweza wakatumiwa kwa lengo la kuongeza uzalishaji na tija katika kilimo.
Jumla ya wahitimu 7,525 wamefaulu katika ngazi ya Astashaada kati ya hao, wanawake ni 2,557 na wanaume ni 4,968. Wahitimu 3,104 wameafaulu katika ngazi ya Stashahada (Diploma) ambapo wanawake ni 774 na wanaume 2,370.
Wahitimu hawa ni mahiri katika michepuo ya Stashahada ya fani ya kilimo cha mboga matunda na maua (Horticultural Crops), Zana za Kilimo, Uzalishaji wa Mazao, Umwagiliaji na Huduma za Kiufundi, Mipango na Matumizi Bora ya Ardhi ya Kilimo na Chakula na Lishe.
Aidha, Wahitimu hao wanauwezo wa kiutendaji katika kuanzisha na kutunza bustani za mimea, mboga na matunda, kushauri wakulima kwa kutumia teknolojia mbalimbali ikiwemo TEHAMA, kusimamia kazi zote zinazohusu matumizi ya Zana za Kilimo na kuzifanyia matengenezo kila itapohitajika, kujenga miundombinu ya shamba ikiwemo maghala, vihenge na mabanda ya wanyama mbalimbali.
Pia wanauwezo wa kuzalisha mazao makuu ya chakula na biashara yanayolimwa nchini, kusaidia tafiti na kukusanya takwimu za utafiti wa mazao, kusimamia ujenzi wa miradi midogo ya umwagiliaji na kuandaa michoro ya miradi hiyo.
Wahitimu hao pia wanao uwezo wa kuandaa mazao baada ya kuvunwa, kuchakata na kufungasha, kufanya tathmini ya lishe na mahitaji ya chakula katika jamii, kuandaa mipango na kutoa ushauri kwa jamii kuhusu masuala ya lishe.
Serikali inawafahamisha Wadau wa maendeleo ya kilimo na mifugo, Wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi na yeyote mwenye mahitaji yanayoweza kutekelezwa na wataalam hawa kuwa wanayo fursa ya kuwaajiri, wahitimu hao ili kupata ufanisi katika shughuli zao za kilimo.

Imetolewa na;
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
WIZARA YA KILIMO MIFUGO NA UVUVI

  
source:www.kilimo.go.tz
Share:

HII HAPA LIST YENYE MAJINA YA WANAFUNZI WA ST.JOSEPH AMBAO TAARIFA ZAO ZINAMISS

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger