Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Wednesday 24 April 2024

WADAU WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA KILIMO IKOLOJIA HAI


Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Kilimo, Obadia Nyagiro,akizungumza wakati wa kikao cha wadau wa Kilimo Ikolojia hai kilichoratibiwa chini ya mwamvuli wa Taasisi za Kilimo Hai Tanzania (TOAM) kilichofanyika jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa TOAM, Dk.Mwatima Juma,akizungumza wakati wa kikao cha wadau wa Kilimo Ikolojia hai kilichoratibiwa chini ya mwamvuli wa Taasisi za Kilimo Hai Tanzania (TOAM) kilichofanyika jijini Dodoma.

Paul Holmbeck kutoka Shirika la Biovision Foundation,akizungumza wakati wa kikao cha wadau wa Kilimo Ikolojia hai kilichoratibiwa chini ya mwamvuli wa Taasisi za Kilimo Hai Tanzania (TOAM) kilichofanyika jijini Dodoma.


Baadhi ywa wadau wa Kilimo Ikolojia hai wakifatilia majadiliano mbalimbali wakati wa kikao hicho kilichoratibiwa chini ya mwamvuli wa Taasisi za Kilimo Hai Tanzania (TOAM) kilichofanyika jijini Dodoma.


Na.Alex Sonna-DODOMA

WADAU wa kilimo ikolojia hai wamekutana jijini Dodoma kutengeneza mpango kazi wa mwaka 2024/25 kwa ajili ya utekelezaji vipaumbele vya Mkakati wa kitaifa wa kilimo hai wa ikolojia wa 2023-2030 (NEOAS) utakaoleta mageuzi ya kilimo nchini.

Akizungumza kwenye kikao hicho kilichoratibiwa chini ya mwamvuli wa Taasisi za Kilimo Hai Tanzania (TOAM), Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Kilimo, Obadia Nyagiro, alisema kilimo hicho ni muhimu kwa watanzania kwa kuwa kitaleta tija kiuchumi, kulinda afya za walaji, afya ya udongo na kuongeza kipato.

Alisema mkakati huo unatokana na Sera ya kilimo kuelekeza masuala ya kuweka mfumo wa uzalishaji, upatikanaji wa masoko na kutambua bidhaa za kilimo hai.

“Mkakati wenyewe ulizinduliwa mwishoni mwa mwaka jana na upo tayari kwa utekelezaji, kilichotufanya tukutane ni namna ya kutekeleza mkakati huu kwa kuandaa mpango kazi kila mwaka kwa muda wa miaka saba ya huu mkakati wa kitaifa, kama tulivyowashirikisha kwenye maandalizi yake lazima tushiriki sisi wadau kwa kuweka malengo ya utekelezaji wake kila mwaka,”alisema.

Alisema serikali itaendelea kutoa ushirikiano ili kufanikisha uandaaji wa mpango huo kwa kuwa ni muhimu wadau kushiriki katika kilimo himilivu na endelevu kwa mazingira na afya ili kuleta tija kwenye sekta ya kilimo.

Alizitaka asasi za kiraia na sekta binafsi kuchangamkia fursa ya uwekezaji katika kilimo hicho kwa kuwa kina tija kubwa.

“Nihimize sekta binafsi na asasi za kiraia mpitie na kuona fursa ya kuwekeza katika eneo hili kwa kuwa tija yake ni kubwa ikiwamo kuongezeka kwa mapato, mkipitia nchi nyingine mtaona waliowekeza kwenye kilimo hiki na tija yake na ni muhimu mipango yetu izingatie kilimo himilivu kinachozingatia mabadiliko ya tabia nchini,”alisema.

Naye, Mwenyekiti wa TOAM, Dk.Mwatima Juma alisema kilimo hicho kinalenga kuwa na uzalishaji wa kutosheleza, kulinda afya na udongo kwa kuondokana na matumizi ya kemikali.

“Kilimo cha kutumia kemikali kilianza miaka 100 iliyopita baada ya kuisha kwa vita kuu ya pili ya dunia ambapo utengenezaji wa mbolea za kemikali, viuatilifu vya kemikali ilionekana itatusaidia kuzalisha chakula zaidi, tulihamasika kuwa kutumika kemikali ndo ukisasa na kwa bahati mbaya tuliacha kilimo chetu cha asili ambacho mtu alikuwa akilima kahawa ndani yake ana kunde,maharage, mtama vyote vinazalishika vizuri na ana ng’ombe anatupia mbolea shambani kwake.”

“Tukahamasisha tuwe na mashamba makubwa tulime zao moja, tupulize dawa miaka imekwenda na tulipofika mimi binafsi nasema tuwaombe radhi wakulima kwa maeneo tuliyowapeleka hasa wakulima wadogo hapafai, kuna aina ya ukulima wanaweza kulima bila kupunguza uzalishaji, bila kupata shida kwenye chakula na kuuza kwenye masoko ya ndani na nje,”alisema.

Alibainisha kuwa kilimo hicho kitasaidia watanzania kuondokana na maradhi mbalimbali ikiwamo uzazi, saratani kwa kuwa yanatokana na matumizi ya kemikali kwenye kilimo.

Naye, Paul Holmbeck kutoka Shirika la Biovision Foundation akizungumzia mataifa mengine namna yanavyotekeleza kilimo hicho, alisema wanasayansi na mashirika ya kimataifa ya masuala ya kilimo yanahimiza kilimo hicho kwa usalama wa chakula na kuna tija kiuchumi ambapo serikali za nchi ambazo zinatekeleza kilimo hicho zinaweka malengo yake.
Share:

RC MACHA AFUNGUA RASMI SEMINA YA FAMILIA,MALEZI,BIASHARA NA HUDUMA ZA AFYA KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO

 



Na Marco Maduhu,SHINYANGA
MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Anamringi Macha,amefungua Rasmi Semina ya Familia,Malezi,Biashara na huduma za Afya, ambayo inaendeshwa na Kanisa la Waadventista Wasabato Ukanda wa dhahabu Nyanza Gold Belt Field NGBF.

Semina hiyo imeanza kutolewa Aprili 2,2024 ambayo itakwenda hadi Aprili 27 mwaka huu Siku ya Jumamosi,imekutanisha watu mbalimbali ambayo inafanyika katika ukumbi wa Makindo.
Macha akizugumza wakati wa kufungua Semina hiyo, imelipongeza Kanisa la Waadventista Wasabato kwa kuendesha Semina hiyo ambayo inathamani kubwa kwa taifa, kwa kutoa masomo ya Familia na Makuzi,Afya pamoja na Biashara.

“Nalipongeza sana Kanisa la Waadventista Wasabato,ni Kanisa ambalo lenye Mahaghaiko makubwa katika kuhakikisha Makuzi ya Vijana yanakuwa kwenye Maadili mema, sababu sasa hivi hapa nchini kuna Janga la Mmomonyoko wa Maadili ya Vijana, na Taifa bora linajengwa na Malezi bora na Makuzi,”amesema Macha.
“Masomo haya ya Familia yanakumbusha wazazi kulea watoto wao katika Maadili Mema, na siyo kuwaacha wakijilea wenyewe na hatimaye kusababisha watoto kuwa na Maadili Mabovu,”ameongeza Macha.

Amesema kwa upande wa Masomo ya Afya, ameitaka jamii kuzingatia lishe bora, sababu Magonjwa mengine hasa yasiyo ya kuambukiza husababishwa na Mtindo Mbovu wa Maisha, na kwamba kupitia Mafunzo hayo yanaijenga jamii yenye Afya Bora.
Aidha, amesema kupitia Masomo ya Biashara,amewataka Wafanyabiashara wawe na hofu ya Mungu, na kufanya biashara zao kwa haki bila ya kuchakachua bidhaa, pamoja na kulipa Kodi ya Serikali.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa, ametoa wito kwa viongozi wa dini kuendelea kuliombea Taifa Amani, pamoja na Rais Samia na wasaidizi wake,ili awe na maono mazuri ya kuiongoza Nchi katika kweli na haki, sababu Nchi ikiwa na Amani itakuwa na Maendeleo.
Naye Askofu wa Jimbo la Ukanda wa dhahabu (NGBF) Kanisa la Waadventista Wasabato Enock Sando, amesema Kanisa hilo limeendelea kujipambanua katika ulimwengu kote na kugusa jamii, kuisaidia kujitegemea kupitia Semina za Biashara ili wawe na Fikra Chanya ya kujikwamua kiuchumi sababu Mungu hapendezwi na Umaskini.

Amesema Kanisa hilo pia lina amini katika Afya, sababu bila Afya hakuna Maendeleo, ndiyo maana katika Semina hiyo mafunzo ya Afya yanatolewa, pamoja na Masomo ya Kaya na Familia ili kuwe na Taifa lenye Umoja,Mshikamano na Mahusiano Mazuri.

TAZAMA PICHA HAPA CHINI👇👇
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Anamringi Macha akizungumza wakati akifungua Semina hiyo.
Askofu wa Jimbo la Ukanda wa dhahabu (NGBF) Kanisa la Waadventista Wasabato Enock Sando.
Awali Mchungaji Mstaafu Wilbert Nfumbusa akitoa Somo la Kaya na Familia.
Awali Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Mkoa wa Shinyanga (TCCIA) Jonathani Manyama akitoa Somo la Biashara kwenye Semina hiyo.
Awali Afisa Muuguzi Sherida Madanka akitoa Somo la Lishe kwenye Semina hiyo.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Kwaya ya Lubaga Mara Nassa ikiimba kwenye Semina hiyo.
Kwaya ya SAC ikiimba kwenye Semina hiyo.
Kwaya ya Lubaga Mara Nassa ikiimba kwenye Semina hiyo.
Kwaya ya SAC ikiimba kwenye Semina hiyo.
Kamati ya Maandalizi ya Semina hiyo ikiimba kwenye Semina.
Picha ya pamoja ikipigwa kwenye Semina hiyo.
Picha ya pamoja ikipigwa ikipigwa Semina hiyo.
Share:

Tuesday 23 April 2024

MULEBA WAOMBEA TAIFA LA TANZANIA KUELEKEA MIAKA 60 YA MUUNGANO..DC DKT. NYAMAHANGA ASISITIZA ,AMANI , UMOJA NA MSHIKAMANO

Wananchi,watumishi na viongozi wa dini wakiwa kwenye ibada maalum ya kuliombea Taifa,Viongozi wa Kitaifa ikiwa ni maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano
Mwinjilisti wa kanisa  la Kiinjili la Kirutheri Tanzania Felician Mathias wakati akiomba katika ibada maalum ya kuliombea Taifa
Mkuu wa wilaya ya Muleba Dkt Abel Nyamahanga akizungumza na wanachi,Viongozi wa dini na watumishi wa halmashauri ya wilaya hiyo wakati wa ibada maalum ya kuliombea Taifa
Sheikh Nurani Amri akiomba wakati wa ibada maalum ya kuliombea Taifa,Viongozi wa Kitaifa ikiwa ni maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano

Na Mariam Kagenda _Kagera

Katika kuadhimisha miaka 60 ya Muungano wananchi wilayani Muleba mkoani Kagera wamehimizwa kuendelea   kudumisha mila, desturi, umoja na mshikamano kwa mustakabali wa nchi ya Tanzania.



Mkuu wa wilaya ya Muleba Dkt
 Abel Nyamahanga amesema hayo leo wakati wa ibada maalum  ya kuliombea  Taifa na viongozi sambamba na maadhimisho ya miaka 60 ya muungano kati ya  Tanganyika na Zanzibar iliyofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Muleba .



Dkt Nyamahanga amesema kila mwananchi anatakiwa  kuendelea kuuheshimu Muungano huo kwa kudumisha amani iliyopo kwani viongozi waliohasisi jambo hilo waliamini kuwa umoja ni Nguvu .


Amesema kuwa jambo lililofanywa na viongozi  Katika kuchanganya udongo wa pande mbili tafsiri yake ilikuwa ni kuunganisha watanzania hivyo hakuna mtu atakayeweza kuwatenganisha kwa namna yoyote  kila mmoja anatakiwa kuendelea kuuheshimu Muungano ili uweze kudumu .


Ameongeza kuwa Muungano huo ndiyo unawapa heshima watanzania,unawapa heshima ya uhuru Watanzania na unayapa hadhi mapinduzi matukufu ya Zanzibar kwamba wote ni familia moja  kwani ukienda Zanzibar unawakuta Watanzania wanafanya Biashara na ukija Tanzania unamkuta Mzanzibar anafanya biashara na hayo ndiyo mafanikio ya Muungano.


Kwa upande wao baadhi ya viongozi walioongoza ibada hiyo Shekhe Nurani Amri pamoja na Mwinjilisiti kutoka kanisa la Kiinjiri la Kirutheri Tanzania wilaya ya Muleba Felician Mathias wamewahimiza Watanzania kuendelea kuwaombea viongozi waliopo madarakani wakati wote wanapopata nafasi ya kuomba ili waweze kuendelea kuwaongoza katika misingi inayompendeza mwenyezi Mungu.


Kabla ya ibada hiyo viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Muleba , Watumishi pamoja na wananchi wa wilaya hiyo waliungana kwa pamoja kufanya usafi katika kituo cha afya Kaigara kilichopo wilayani humo ambapo kesho watashiriki katika michezo mbalimbali.

Share:

Taasisi ya Internet Society yaja na suluhisho la gharama za bando

Taasisi ya Internet Society Tanzania imewahimiza wananchi kutumia fursa ya huduma ya Internet kujiletea maendeleo, badala ya kufuatilia mambo yasiyo ya msingi na kupoteza muda na gharama za bando.

Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Nasar Kirama wakati akitoa semina kwa wadau wa Internet wakiwemo waalimu, viongozi wa dini, viongozi wa serikali za mitaa, wajasiriamali na mashirika yasiyo ya serikali katika wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.

Kirama alisema huduma ya Internet ikitumika vyema inaweza kubadili maisha ya wananchi ikizingatiwa mwelekeo uliopo sasa ni uchumi wa kidijitali na hivyo kuwahimiza wananchi kutumia fursa hiyo kimaendeleo.

Hata hivyo Kirama alisema baadhi ya maeneo hususani ya pembezoni huduma ya Internet haijawafikia wananchi huku waliofikiwa na huduma hiyo wakitatizwa na gharama za bando na hivyo kueleza kuwa taasisi yake imekuja na suluhisho ambapo wanajamii sasa wanaweza kuungana pamoja na kuchangia upatikanaji wa Internet yenye kasi na kwa gharama nafuu.

Alisema tayari majaribio ya huduma ya wananchi kuchangia Internet (Communit Network) yameleta mafanikio makubwa katika wilaya ya Kigamboni jijini Dar es salaam na hivyo kutoa rai kwa wakazi wa Mwanza kuichangamkia.

Mmoja wa mdau wa Internet ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la MIBOS, Hassan Rangi alisema miundombinu ya mfano iliyofungwa na taasisi ya Internet Society Tanzania katika shirika hilo imesaidia upatikanaji wa huduma ya uhakika na kwa gharama nafuu.

Naye Mratibu wa shirika la GWEITA, Hadija Ferooz alisema huduma ya mtandao wa jamii (Community Network), itasaidia jamii kupata uhakika wa internet na kuondokana na matumizi makubwa ya gharama za bando.
Na George Binagi- GB Pazzo, Mwanza
Wadau wa mtandao wa Internet wakiwemo waalimu, viongozi wa Serikali za Mitaa, wajasiriamali na mashirika yasiyo ya kiserikali katika Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza wakijifunza kuhusu Mtandao wa Jamii (Community Network) iliyofungwa katika ofisi za shirika la MIBOS zilizopo Kiloleli wilayani Ilemela.
Mkurugenzi wa taasisi ya Internet Society Tanzania, Nasar Kirama (kulia) akiwasilisha mada kwa wadau wilayani Ilemela mkoani Mwanza kuhusu Mtandao wa Jamii (Community Network) unaotoa fursa kwa wanajamii kuungana pamoja na kuchangia upatikanaji wa huduma ya Internet yenye kasi na kwa gharama nafuu.
Wadau wa Internet wilayani Ilemela wakifuatilia mada wakati wa semina ya kuwajengea uelewa kuhusu Mtandao wa Jamii (Communituy Networt) iliyotolewa na taasisi ya Internet Society Tanzania yenye makao yake makuu jijini Dar es salaam.
Wadau wa Internet wilayani Ilemela wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kujengewa uelewa kuhusu Mtandao wa Jamii (Communituy Networt) na taasisi ya Internet Society Tanzania.
Tazama Video hapa chini
SOMA PIA>>> HABARI ZAIDI HAPA
Share:

TAKUKURU RAFIKI YASAIDIA KUTATUA KERO ZA ARDHI SHINYANGA.. MLEPA, NDALA WAPEWA NAMBA ZA VIWANJA

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Donasian Kessy akizungumza na waandishi wa habari


Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog

Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Shinyanga (TAKUKURU) kupitia Program ya TAKUKURU RAFIKI imesaidia kutatua kero za wananchi mkoani Shinyanga.

Akitoa akitoa taarifa ya utekelezaji wa kazi za TAKUKURU kwa kipindi cha robo ya tatu ya Januari hadi Machi 2024 leo Jumanne Aprili 23,2024 Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Donasian Kessy amesema Programu ya TAKUKURU imefanya ufuatiliaji wa majibu ya kero ya kutopimwa maeneo ya makazi kwa wananchi wa kata ya Ndala Mtaa wa Ndala tangu mwaka 2018.


“Awali wananchi zaidi ya 246 walichanga kiasi cha shilingi 12,396,000/= na kulipa Manispaa ya Shinyanga kwa ajili ya zoezi la upimaji ardhi. Pia wananchi 1150 wa mtaa wa Mlepa waliokuwa wamechanga fedha kwa ajili ya kupimiwa na kurasimishiwa maeneo yao lakini walikuwa bado hawajapatiwa namba za upimaji wa viwanja vyao tangu mwaka 2023 walipopimiwa”,amesema Kessy.


“Wananchi wa mtaa wa Ndala walitoa keto yao kutopimiwa na kurasimishiwa maeneo yao pamoja na kuwa walikwishachangia huduma hiyo tangu mwaka 2018. Vilevile wananchi wa mtaa wa Mlepa kero yao ilikuwa kupatiwa namba za viwanja vyao tangu walipopimiwa mwaka 2023”,ameeleza.

Amesema hali hiyo ilikuwa inapelekea migogoro ya mipaka, kuwanyima fursa ya kupata mikopo katika taasisi za kifedha kwa kutumia ardhi kama dhamana lakini pia viwanja kutoongezeka thamani kwa kukosa utambuzi rasmi.


“Baada ya kupokea kero hiyo, TAKUKURU iliwasilisha Manispaa ya Shinyanga bango kitita lenye kero kusika na mikakati ya utatuzi wa kero hiyo. Halmashauri ya Manispaa Idara ya ardhi walishughulikia kero hiyo ambapo katika mtaa wa Mlepa zoezi la kugawa namba za viwanja lilianza na hadi sasa namba za viwanja 412 zimeanza kugawiwa tangu mwezi Januari na zoezi bado linaendelea”,amefafanua Kessy.

“Mwezi Februari Manispaa ya Shinyanga ilifanya zoezi la upimaji katika mtaa wa Ndala na kwa sasa Manispaa ipo kwenye mchakato wa ukamilishaji wa utengenezaji wa ramani kwa ajili ya kusajiriwa Wizarani na baada ya hapo kupata namba za viwanja hivyo 246 vya wananchi wa mtaa wa Ndala”,ameongeza.


Mkuu huyo wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga amesema TAKUKURU inaendelea kufuatilia ugawaji wa namba za viwanja vilivyopimwa katika mtaa wa Mlepa mpaka litakapokamilika lakini pia kufuatilia zoezi la ukamilishaji wa uandaaji wa namba za viwanja za mtaa wa Ndala na ugawaji wake.

Hali kadhalika TAKUKURU inaendelea kufanya vikao vya utambuzi wa kero katika kata 14 kutoka kata za Mwenge, Mwawaza, Kolandoto, Lyabukande, Puni, Nyida, Mhongoloi, Majengo, Nyasubi, Ulowa, Bulungwa, Mpunze, Bupigi na Bubiki.

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Donasian Kessy akizungumza na waandishi wa habari

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger