Wednesday, 31 December 2025

MALUNDE 1 BLOG INAKUTAKIA HERI YA MWAKA MPYA 2026!


 
Share:

WANANCHI FUONI WAJITOKEZA KUPIGA KURA KUCHAGUA MBUNGE WAO

Share:

Tuesday, 30 December 2025

MAKAVAZI YA MUUNGANO: SILAHA MPYA DHIDI YA UPOTOSHAJI NA CHUKI ZINAZOLENGA KUIVUNJA TANZANIA

 Serikali imetangaza kuwa ujenzi wa Makavazi ya Muungano sasa umefika ukingoni, huku ikibainishwa kuwa vituo hivyo vitakuwa "darasa la kudumu" la kukabiliana na mawimbi ya upotoshaji wa historia yanayopandikizwa na baadhi ya wanaharakati na watu wenye nia ovu ya kutaka kuuvunja Muungano wa Tanzania.

Akizungumza Desemba 28, 2025, visiwani Unguja, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, amesema ujenzi huo ni utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inayolenga kuziba mwanya wa kutokuelewa mambo unaotumiwa na maadui wa umoja wa kitaifa.

 Kukabiliana na "Wanaharakati wa Uongo"

Waziri Masauni amefafanua kuwa katika miaka ya hivi karibuni, kumeibuka kundi la watu wanaojiita wanaharakati ambao wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii na majukwaa mengine kupotosha ukweli kuhusu makubaliano ya mwaka 1964. Amesema kutokuwepo kwa kituo kimoja chenye ushahidi wa nyaraka kumesababisha baadhi ya vijana kuyumbishwa na hoja za chuki zinazolenga kuleta mfarakano kati ya Tanganyika na Zanzibar.

"Makavazi haya yatakuwa jibu kwa wale wote wanaotaka kuivunja nchi kwa kutumia historia ya uongo. Kijana akitaka kujua kwanini tulitoka huko na kwanini tuko hapa, hatasikiliza maneno ya mitaani ya watu wenye ajenda zao, bali atakuja makavazi kuona nyaraka, picha, na sauti za waasisi wetu," alisisitiza Mhe. Masauni.

Kuziba Pengo la Maarifa kwa Vijana

Hafla hiyo ya uwekaji jiwe la msingi la jengo la Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar, iliyoongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, imetumika kusisitiza kuwa vijana ndio walengwa wakuu. Serikali imebaini kuwa kutokana na kutopata elimu sahihi ya historia mashuleni na kwenye vyanzo rasmi, vijana wengi wamekuwa wepesi kuamini "propaganda" zinazochochea ubaguzi na utengano.

Makavazi kama Kituo cha Elimu na Ushahidi

Mhandisi Masauni amebainisha kuwa makavazi hayo yaliyopo Dodoma, Dar es Salaam (katika Ukumbi wa Karimjee kwa muda), na Zanzibar, hayatakuwa tu majengo ya kuhifadhi vitu vya kale, bali vituo vya kimkakati vitakavyohusisha:

Uhifadhi wa Nyaraka za Asili: Ili kuthibitisha uhalali na faida za Muungano tangu asili yake.

Kumbi za Mikutano na Kusomea: Maeneo ambayo watafiti na wanafunzi wanaweza kuchimba ukweli na kujadiliana kwa msingi wa data, si hisia.

Teknolojia ya Kisasa: Matumizi ya mifumo ya kidijitali kuonyesha safari ya Tanzania ili kuwavutia vijana na kuwapa ukweli usiopingika.

Utekelezaji wa Ahadi ya Rais Dkt. Samia

Waziri Masauni amekumbusha kuwa mradi huu ni kielelezo cha maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa tangu akiwa kwenye kampeni za uchaguzi. Rais aliona mapema hitaji la kulinda amani ya nchi kwa kuimarisha "kinga ya kifikra" kupitia elimu ya historia ya nchi.

Kupitia shamrashamra hizi za miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Serikali imetoa onyo kwa wale wanaotumia ujinga wa historia kama silaha ya kubomoa nchi, ikiahidi kuwa makavazi hayo yatakuwa suluhisho la kudumu la kuunganisha Watanzania kupitia ukweli.

Share:

DC NKINDA AANZA KUTATUA CHANGAMOTO YA BARABARA YA SHUNU–ZONGOMELA, KAHAMA

 


Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mhe. Frank Nkinda, ameanza utekelezaji wa ahadi yake ya kutatua changamoto ya barabara iliyowasilishwa na mwananchi wa Shunu ambaye pia ni Kiongozi wa Chama cha ACT–Wazalendo wilayani Kahama, Abas Omari, wakati alipokutana na vijana katika sherehe za Krismasi maarufu kama Pilau la Wana.


Katika sherehe hizo, DC Nkinda aliahidi kutembelea eneo husika ili kujionea ukubwa wa tatizo na kuchukua hatua stahiki, Leo, ametimiza ahadi hiyo kwa kutembelea barabara yenye changamoto katika Mtaa wa Hongwa, Kata ya Nyahanga, wilayani Kahama mkoani Shinyanga, inayounganisha eneo la Shunu na eneo la viwanda la Zongomela maarufu Dodoma.


Akiwa katika ziara hiyo, DC Nkinda amejionea adha inayowakabili wananchi wanaoutumia barabara hiyo, hususan wafanyabiashara na wafanyakazi wa viwanda vidogo vidogo zongonela, Kutokana na umuhimu wake kiuchumi, ameagiza mkandarasi anayetekeleza mradi huo Prinax investment limited kuhakikisha anakamilisha ujenzi kwa wakati uliopangwa ili kuondoa kero kwa wananchi na kurahisisha shughuli za uzalishaji na biashara.


Akizungumza kuhusu hatua za utekelezaji wa mradi, Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA), mhandisi Juma Masola, ameahidi kumsimamia kwa ukaribu mkandarasi anayetekeleza mradi huo ili kuhakikisha unakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa, hivyo kuwezesha shughuli za kiuchumi kuendelea bila vikwazo.


Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Nyahanga, Mheshimiwa Josephina Kilimba, amwtaja barabara nyingine korofi zinazohitaji matengenezo ya dharura, ikiwemo barabara ya Vatikani iliyopo Mtaa wa Lugela huku akisisitiza umuhimu wa hatua za haraka ili kuboresha miundombinu na kuongeza ustawi wa wananchi.


Wananchi wa eneo hilo wamepongeza jitihada za Serikali ya Wilaya ya Kahama kwa kuanza kuchukua hatua za vitendo katika kutatua changamoto za barabara, wakieleza matumaini kuwa maboresho hayo yataongeza fursa za kiuchumi na kuboresha maisha yao kwa ujumla.




Share:

Monday, 29 December 2025

Video Mpya : CHIEF MAKER - MWAMBA

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU DESEMBA 29,2025



Magazeti
Share:

Sunday, 28 December 2025

VIJANA WASHAURIWA KUKUZA BIASHARA KWA HATUA STAHIKI



Na Sifa Lubasi, Dodoma

VIJANA wametakiwa kufuata hatua zinazotakiwa katika ukuaji biashara pasipo kuwa na matamanio na mafanikio ya haraka.

Akizungumza wakatii wa mahojiamo jana, Kaimu Meneja wa SIDO mkoa wa Dodoma Crispin Kapinga alisema kuwa biashara kabla hazijaanza zina kanuni na taratibu za kufuata ili ziwe endelevu.

Amesema kuwa biashara nyingi hasa za vijana hazifanyiwi tathimini za kutosha juu ya hali halisi, masoko, kutunza mahesabu na hivyo kukosa uendelevu

"Miradi mingi ya vijana inayoendelea ni wale waliokubali kufuata hatua zinazotakiwa za ukuaji biashara pasipo kuwa na matamanio na mafanikio ya haraka, biashara ni kama mtoto haikui tu," amesema

Amesema kuwa biashara ina hatua ya kuzaliwa na wazo la unataka kufanya nini.

"Unatakiwa kuanza na wazo, kulitekeleza, hatua ya kukua ni muhimu kwani hapo wateja wanaongezeka,kila kitu kinaongezeka,pia unapofanya biashara unajifunza tabia za binadamu,"amesema

Amesema kuwa hatua muhimu ni kufanyia tathimini biashara kabla ya kuanza lakini changamoto kubwa wengi wanaanzisha biashara na kusema watajifunza mbele ya safari.

"Biashara yoyote inalenga kundi fulani. Usitangaze tu mtandaoni kuwa bidhaa inapendwa,Je inapendwa kwa kiwango gani lazima ifanyike tathimini ya kutosha na ufahamu walioko sokoni ni akina nani," amesema

Aidha amesema kumekuwa na swali ambalo wengi wamekuwa wakijiuliza kwa nini biashara nyingi zinakufa.

"Kwenye biashara lazima kuwe na wateja wenye uwezo wa kununua hizo bidhaa,, kundi la wateja." amesema

"Hakuna biashara mpya lazima ufanye tathimini ya kufahamu zile zilizo sokoni zina mipango gani,ni nani anakuwa na soko kubwa," amesema

Alisema kuwa vijana wengi wana makundi ya wateja wa mdomoni si halisia na hawana chaguo la pili hali inayopelekea biashara kukosa faida na hatimaye kufa.

Pia alisema unapomuuliza kijana uhalisia wa mtaji wengi huwa hawana majibu,wanakata tamaa

Kapinga alisema kuwa SIDO imekuwa ikishughulika na biashara ndogo ndogo,viwanda vidogo na vya kati ni vyema vijana wakawa wadadisi na kufuatilia fursa zilizopo kwenye taasisi mbalimbali.

"Fursa kama maembe mabichi,kipindi unasubiri yaive sisi tunapopoa tunakula na chumvi, kumbuka kwamba maisha yako yako mikononi mwako," alisema

Alisema kuwa vijana wengine wamekuwa wakikatisha tamaa wenzao ili wakose wote.

"SIDO inatoa ushauri wa kibiashara,kiufundi bure, ushauri wa kifedha wa namna ya kutumia na kutunza fedha, Pia kuwaunganisha na Taasisi za kifedha na Taasisi mbalimbali bila gharama yoyote.," alisema

Pia alisema SIDO wamekuwa wakishighulika na kutoa malezi na kutenga uelewa.

"Vijana wanatakiwa kutumia fursa zilizopo wajasiriamali wengi wanahitaji watu wa masoko na 'branding ',wengi wanahitaji kutangaza bidhaa kutumia mitandao ya kijamii,taarifa za fursa hawazitafuti,mwisho wa siku wao ndio wanalalamika," alisema

Aliwataka vijana kubadilika kwani kwani maisha yao yako mikononi mwao.

" Serikali kazi yake ni kutengeneza' mazingira rafiki jinsi ya vijana kufanya biashara,wakiulizwa mikopo ya Halmashuri kwa nini wanaogopa kwenda wanasema imekuwa lkitolewa kwa udugu tu je uliwahi kuomba au jus unasikia tu maneno,? alihoji.

Share:

Saturday, 27 December 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI DESEMBA 28,2025


Magazeti ya leo
Magazeti ya leo

Magazeti ya leo

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger