Tuesday, 7 May 2019

Mbunge Chadema akamatwa na polisi Dodoma

...
Mbunge wa Mbozi, Pascal Haonga (Chadema), amekamatwa na Jeshi la Polisi jijini Dodoma leo Jumatatu Mei 6, wakati akitoka kuhudhuria vikao vya Bunge vinavyoendelea.
 
Akizungumzia tukio hilo, Katibu wa wabunge wa Chadema, David Silinde amesema hawajapata taarifa rasmi kwanini mbunge huyo amekamatwa.

“Huu ni mwendelezo wa matukio ya viongozi wetu kukamatwa, licha kwamba walitakiwa kuujulisha uongozi wa bunge,” amesema Silinde.

Alipoulizwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto amesema hana taarifa za kukamatwa kwa mbunge huyo.

"Niko Gairo sijapata taarifa zozote za  kukamatwa kwa mbunge huyo," amesema Muroto.


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger