Monday 7 November 2016

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI KCMC WALIOPATA MKOPO BATCH 2 2016/2017

kcmuco banner
KUYAONA
Share:

CCM Yatuma Salamu Za Rambi Rambi Kifo Cha Mzee Samwel Sitta

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimepokea kwa majonzi na simanzi kubwa taarifa za kifo cha Mhe. Samuel John Sitta, Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kilichotokea usiku wa jana tarehe 6/11/2016 katika hospitali ya Technical University of Munich nchini Ujerumani alipokuwa akitibiwa.

Mhe. Samuel John Sitta, amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za utumishi katika Chama na Serikali. Alikuwa Katibu wa CCM na Mkuu wa Mkoa, Mkurugenzi Mkuu wa kituo cha uwekezaji, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), Mjumbe wa Kamati Kuu, Mbunge, Waziri na Spika.

Mhe. Sitta alikuwa ni Kiongozi mchapakazi, mwadilifu na aliyejitambulisha kwa utendaji wenye kufuata falsafa yake ya “kasi na viwango”. Ametoa mchango mkubwa katika ujenzi wa Chama na Serikali.

Katibu Mkuu wa CCM Ndg Abdulrahman Kinana amemtumia salamu za rambi rambi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai, familia ya Mhe. Sitta pamoja na Wananchi wa Jimbo la Urambo kufuatia kifo cha Kiongozi huyu. Tunaungana nao katika msiba huu ambao pia ni msiba wetu

Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi, Ameni

Imetolewa na:-
CHRISTOPHER OLE SENDEKA (MNEC)
MSEMAJI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)

07 – 11 – 2016
Share:

TANZIA: Aliyekuwa Spika wa Bunge la tisa, Samwel Sitta afariki dunia





4494_b.jpg
Tunasikitika kuwataarifu kuwa mzee wetu mpendwa Samwel Sitta amefariki dunia katika Hospitali ya Technical University of Munich nchini Ujerumani saa 7:30 kwa muda wa Ujerumani alikokuwa akitibiwa ugonjwa wa Saratani ya Tezi Dume.

0502f3ea-1ffd-4cc2-b748-74e35ff8db86.jpg

Historia yake:

Samuel-Sitta.jpg
Samuel John Sitta alizaliwa Desemba 18, 1942 huko wilayani Urambo Mkoa wa Tabora. Sitta alisoma Shule ya Msingi Urambo kati ya mwaka 1950 – 1953, kisha alikwenda Wilaya ya Sikonge mwaka 1954 - 1957 na kuendelea na masomo ya “Middle School” katika shule ya “Sikonge Middle School”. Baadaye mwaka 1958 – 1963 alianza masomo ya sekondari Shule ya Wavulana Tabora yaani “Tabora Boys” kidato cha I – IV na cha V – VI.

Mara tu baada ya kuhitimu masomo ya sekondari, Sitta alijiunga Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kusomea Shahada ya Sheria (L LB) mwaka 1964 na kuhitimu mwaka 1971.

Sitta amesoma shahada yake kwa miaka 7 kwa sababu mwaka 1966, wakati yuko mwaka wa pili na akiwa kiongozi wa wanafunzi UDSM, wanafunzi waligoma na kuandamana kupinga kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na kukatwa mishahara yao baada ya JKT. Hoja ya wanafunzi ilikuwa na mantiki kubwa, kwamba mbona vigogo wa serikali na wanasiasa wanalipwa mishahara minono na marupurupu makubwa?

Baada ya shinikizo hilo la wanafunzi Mwalimu Julius Nyerere alikubali kupunguza mshahara wake wa Sh4,000 bila kodi akaagiza pia mishahara ya mawaziri ipunguzwe kwa asilimia mbili. Miezi miwili baadaye akatangaza Azimio la Arusha (Februari 5, 1967) kuyapa uzito malalamiko ya wanafunzi hao.

Watukutu wawili – Sitta na Wilfred Mwabulambo (Wote sasa marehemu) na wengine kadhaa – waliojitia wazimu na kutetea kile walichokiita haki zao, (haki za wakulima na wafanyakazi), walimshutumu Mwalimu Nyerere kwa maneno makali wakidai “…ni heri wakati wa ukoloni kuliko utawala wa Mwalimu”.

Mwalimu Nyerere alikasirika na kuwafukuza chuo wanafunzi wote 400 kwa kile alichokiita “kwenda kufunzwa adabu majumbani mwao”. Miezi kumi baadaye, baada ya Nyerere kushawishiwa na hasira kutulia akaamua kuwarudisha chuoni wanafunzi 392. Viongozi wa mgomo; Sitta na wenzake 7 walitiliwa ngumu, hawakurejeshwa chuoni.

Busara za viongozi wa chuo zilifanya Mwalimu aliliwe zaidi na kuandikiwa barua mbili maalumu na chuo zenye Kumb. Na. C3/Sa.13 ya 2/3/1967 na C3/Ss.13 ya 9/07/1967. Mwalimu alikubali kilio hicho na kuwaruhusu vijana hao wanane warudi kwa sharti kwamba wale watukutu wawili (Sitta na Mwabulambo) watandikwe viboko na “Mwalimu Nyerere” mwenyewe. Hii ndiyo ilikuwa pona ya Sitta ambaye alirejea UDSM na kuendelea na masomo kwa miaka kadhaa hadi alipohitimu mwaka 1971.

Wakati Sitta anarudi chuoni tayari alikuwa mwajiriwa wa Kampuni ya Mafuta ya “CALTEX OIL” kama Meneja wa Tawi (1967 – 1969) na mwaka 1969 – 1975 aliajiriwa na Shirika la Maendeleo la Taifa kama Katibu na Mkurugenzi wa Utawala.

Baadaye mwaka 1976 Sitta aliamua kujiendeleza kielimu katika masuala ya Usimamizi nchini Uswisi kwenye Chuo Kikuu cha IMEDE ambako alihitimu Stashahada ya Juu ya Usimamizi mwaka huohuo 1976.

Chini ya mfumo wa chama kimoja, Sitta alikuwa kiongozi wa juu wa CCM na serikali akiwa mbunge, mkuu wa mkoa na Waziri katika nyakati tofauti na ameendelea kuwa mbunge na waziri katika mfumo wa vyama vingi.

Sitta alimuoa Margareth Simwanza Sitta

Mbio za ubunge

Enzi za chama kimoja 1975 - 1995 Sitta alikuwa mbunge wa Jimbo la Urambo (kabla halijagawanywa na kuwa Urambo Magharibi na Mashariki) na pia alifanikiwa kuwa waziri kwa nyakati tofauti. Kwa mfano wakati wa kipindi cha mwisho cha Mzee Mwinyi, Sitta alikuwa Waziri za Katiba na Sheria.

Mwaka 1995 Sitta aliingia kwenye mapambano mapya ya siasa za vyama vingi na kwa bahati mbaya akawa mmoja wa vigogo walioangushwa na wabunge wa NCCR. Mshindani wake mkuu alikuwa Msina Jacob Abraham. Msina alishinda kwa kura 10,788 dhidi ya 9,497 za Sitta.

Sitta alirudi tena kwenye jukwaa la siasa mwaka 2005 kwenye uchaguzi mkuu na aliwashinda wapinzani wake wakuu Lumatiliza Yotamu Lubungila wa NCCR na Wilson George Ntakamulenga wa CUF. Sitta alipata kura 28,660 (72.3%) na kurejesha heshima yake jimboni Urambo Mashariki. Kurudi kwa nguvu kulimpa nafasi ya kuwania na kuteuliwa na CCM kugombea uspika wa Bunge la Tanzania na akaliongoza Bunge la Tisa aliloliita bunge la Viwango Na Kasi "Speed and Standards" kwa mafanikio na changamoto nyingi.

Mwaka 2010 Sitta alishiriki tena uchaguzi Urambo Mashariki akawashinda wapinzani wake wakuu Msafiri Abdulrahmani Mtemelwa (CHADEMA) na Zombwe Lotto Edward (CUF) kwa kupata kura 19,947 (70.47%). Baada ya ushindi huo, Sitta alijaribu tena kuwania uspika bila mafanikio; utendaji wake wa kuiuma serikali na wakati mwingine kuipuliza kwenye Bunge la Tisa ulimfanya achukiwe na serikali.

Ilipoonekana ana nguvu akatengenezewa “chui wa karatasi” (mshindani), Andrew Chenge. Chenge naye akachukua fomu ya uspika ghafla, likatengenezwa ‘zengwe’ kuwa wagombea wote wana nguvu, hapo CCM ikapata mwanya wa kutamka kuwa haiwataki wote ili kuondoa mvutano. Sitta akapoteza ndoto za uspika na ukahamia kwa mwanamama Anne Makinda.

Rais Jakaya Kikwete alipotangaza Baraza la Mawaziri mwaka 2010 alimpa Sitta Wizara ya Afrika Mashariki kama Waziri,vilevile alihamishiwa Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi.

Mbio za urais

Samuel John Sitta alianza mbio za urais “kimyakimya” tangu alipokuwa Spika wa Bunge la Tisa (2005 – 2010). Kuna nyakati alikuwa akitoa kauli zinazoashiria kuwa nchi inayumba na haina uongozi thabiti huku akionyesha kuwa nchi ina viongozi thabiti na hawajapewa uongozi mkuu wa nchi, akiwemo yeye.

Hata alipoliongoza Bunge la Katiba mwaka 2014, mara nyingi Sitta alionekana kama mtu mwenye shauku kubwa na urais na alipohojiwa, mara kwa mara, juu ya urais alionyesha ana ndoto hizo. Mara kadhaa, alilalamika kuwa wala rushwa wakubwa wanampiga vita kwa sababu ni msafi.

Katika Uchaguzi wa 2015, Sitta alitangaza nia ya kuwania Urais na alichukua fomu ya kugombea urais kupita chama cha Mapinduzi ambapo baada ya uchaguzi wa ndani chama, John Magufuli ndo jina lililofanikiwa kupenya na kuteuliwa na chama kugombea Urais wa Tanzania.

Mungu Ailaze Roho Ya Marehemu Mahali Pema Peponi Amen.
Share:

Waliokula Fedha za Mikopo Elimu ya Juu Kitanzini,Sheria Yarekebishwa Kuwabana Zaidi


Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Sheria Mbalimbali Namba 3 wa Mwaka 2016 unatarajiwa kuwasilishwa bungeni leo, ukigusa sheria tisa ikiwemo ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu ambapo sasa mnufaika wa mkopo aliyejiajiri atalipa kiasi kisichopungua Sh 120,000 au asilimia 15 ya kipato chake, huku taasisi za umma, bodi, wakala na tume zimebanwa zisirekebishe au kuwianisha mishahara, posho na marupurupu kwa watumishi.

Kwa mujibu wa muswada huo, kwenye Sheria ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu, waajiri wanaoshindwa kuwasilisha marejesho ya mwezi baada ya makato wataadhibiwa, ambapo mwajiri atawajibika kuitaarifu Bodi ya Mikopo kuhusu ajira ya mtu yeyote ambaye ana shahada au stashahada na kukata makato ya mwezi kutoka kwenye mshahara wa mnufaika wa mkopo.

Kifungu hicho kinapendekeza kufanya marejesho ya mkopo kuwa ya kisheria na kupewa nafasi ya awali katika orodha ya makato na kinapendekeza kupunguzwa idadi ya wajumbe wa Bodi ya Mikopo na kufikia saba kwa lengo la kupunguza gharama za uendeshaji.

Kwenye marekebisho ya Sheria ya Utumishi wa Umma, Kifungu cha 8 kinapendekeza kufanyiwa marekebisho ili kumpa mamlaka Katibu Mkuu (Utumishi) kurekebisha na kuwianisha mishahara, posho na marupurupu mengine kwa watumishi wa umma.

Inapendekezwa kumuondolea Katibu mamlaka ya kuteua watumishi wa umma wanaounda baraza la majadiliano ya pamoja ya watumishi wa umma na sasa waziri atateua katibu kutoka wizara yenye dhamana na kada husika ya watumishi.

Pia inapendekezwa kufuta kifungu cha 11 ili kuondoa masharti yanayokataza Baraza la majadiliano ya pamoja ya watumishi na baraza la pamoja la watumishi wa umma kutoa mapendekezo kuhusu ujira.

Kwa upande wa marekebisho ya Sheria ya Leseni na Usafirishaji, Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) kutaongezwa kifungu ili kuweka masharti yanayoruhusu ulipwaji wa faini pale mkosaji anapokiri kosa, badala ya kila kosa kufuata taratibu za kimahakama.

Muswada huo una marekebisho kwenye Sheria ya Mazingira ambako kutawekwa mwongozo wa namna ya kupima urefu wa mita 60 kwenye kingo za bahari, ziwa, mto au bwawa la maji kinachozuiliwa kufanyia shughuli zozote za binadamu. Upimaji utapimwa kuanzia kwenye kingo za maeneo hayo.

Sheria nyingine zitakazofanyiwa marekebisho kwenye Mkutano wa Tano wa Bunge la 11 ni ya Usafiri wa Anga, Sheria ya Msajili wa Hazina na Sheria ya Vipimo.

Spika Job Ndugai wakati akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Tano wa Bunge wiki iliyopita, alieleza kuwa kwa wiki hii Bunge litapokea taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali(CAG) ya mwaka 2014/2015 kisha kujadili na kuishauri serikali kuhusu Mkataba wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Jumuiya ya Ulaya (EU) na Afrika Mashariki (EPA-EU) na kisha taarifa ya kamati ndogo kuhusu uchambuzi wa sheria ndogo.
Share:

Sunday 6 November 2016

Fourth Batch of Students Selected to Join Various Undergraduate programmes at Main Campus and Mbeya Campus College for Academic Year 2016/2017

CONGRATULATIONS AND WELCOME TO MZUMBE UNIVERSITY
The following applicants have been selected to join various undergraduate programmes (Diploma & Certificate) at Mzumbe University in the the 2016/2017 academic year. Candidates are advised to observe all instructions.
Share:

SELECTED CANDIDATES TO JOIN VARIOUS UNDERGRADUATE AND NON DEGREE PROGRAMMES ACADEMIC YEAR 2016/17

Share:

TAARIFA MUHIMU KWA WANAFUNZI WA SPECIAL DIPLOMA UDOM 2016

 Logo
ALL STUDENTS WHO WERE SELECTED TO RESUME STUDIES IN SPECIAL DIPLOMA IN EDUCATION- SCIENCE, MATHEMATICS AND ICT AT THE UNIVERSITY OF DODOMA, ARE INFORMED TO REPORT AS CONTINUING STUDENTS TO THE COLLEGE OF EDUCATION (5-6TH  NOVEMBER, 2016),   READY TO RESUME STUDIES ON 7TH NOVEMBER 2016.
ISSUED BY THE DIRECTORATE OF UNDERGRADUATE STUDIES
Share:

Official VIDEO | Rayvanny – SUGU | Watch/Download


13691
Share:

Official VIDEO | Fid Q – SUMU | Watch/Download


sumu-video-702x336
Share:

Official VIDEO | Ommy Dimpoz X Alikiba – Kajiandae | Watch/Download

kajiandae
djmwanga2bdownload2blogo
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBER TAREHE 6.11.2016




Share:

Saturday 5 November 2016

Breaking News:WIZARA YA AFYA INATANGAZA NAFASI ZA KUSOMESHA/UFADHILI WA WANAFUNZI WA AFYA WALIOCHAGULIWA CHETI NA DIPLOMA 2016/2017

Image result for serikali ya tanzania 

KUSOMA TANGAZO HILO 
Share:

HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU ST.JOHN UNIVERSITY -SJUT 2016/2017 6TH ROUND

KUONA MAJINA 
Share:

HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA CHUO KIKUU MARIAN UNIVERSITY-MARUCO 5TH ROUND 2016/2017

KUONA MAJINA
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI NOVEMBER 5 2016



Share:

Marekebisho saba Yafanyika Muswada wa sheria ya huduma za habari

Serikali jana imewasilisha bungeni muswada wa sheria ya huduma za habari mwaka 2016, huku ikitaja marekebisho saba katika muswada huo.
Share:

Majibu ya JPM kwa wanahabari kuhusu muswada wa Sheria ya Huduma za Habari 2016


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger