Friday 23 September 2016
Mhadhiri chuo kikuu mbaroni kwa kumkashfu Rais Magufuli
Idadi
ya watu wanaokamatwa kwa tuhuma za kumkashfu Rais John Magufuli kupitia
mitandao ya kijamii imezidi kuongezeka baada ya polisi kumkamata
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu cha Mkwawa (Muce), Dk Oscar
Magava (48).
Dk
Magava amekuwa mtu wa kumi kukamatwa na polisi katika kampeni za jeshi
hilo kudhibiti uhalifu chini ya sheria ya uhalifu wa mtandaoni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Julius Mjengi alisema Dk Magava alikamatwa akiwa Sumbawanga na alirudishwa mkoani Iringa.
Mjengi
alisema Septemba 15, mwaka huu walipata taarifa kuwa mhadhiri huyo
anatumia mitandao ya kijamii kumkashfu Rais. Alisema waliamua kumsaka na
walipopata taarifa kuwa Dk Magava amekwenda Sumbawanga waliwasiliana na
polisi wa huko wakamkamata na kumrudisha Iringa.
Hata
hivyo, Kamanda Mjengi hakuyataja maneno aliyotumia Dk Magava kumkashfu
Rais kwa madai kuwa bado wanaendelea na uchunguzi na kwamba ukikamilika
atafikishwa mahakamani.
Kamanda
Mjengi aliwatahadharisha wananchi kuwa makini na matumizi ya mitandao
ya kijamii kwa kuitumia kwa ajili ya maendeleo na si kutukana wala
kukashfu viongozi au watu wengine.
Watu mbalimbali wamekuwa wakikamatwa na kufikishwa mahakamani kwa kosa la kumkashifu Rais au jeshi la polisi.
BAADA YA TCU KUSHUSHA VIWANGO,BODI YA MIKOPO IMEGOMA KUONGEZA MDA WA KUTUMA MAOMBI 2016/2017
BODI
ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imesema haiwezi kutoa
mikopo kwa waombaji wapya walioomba baada ya Tume ya Vyuo Vikuu (TCU)
kushusha viwango vya udahili.
Wiki iliyopita, TCU ilitangaza kushusha viwango vya udahili bila kueleza sababu za kufanya hivyo.
Mkurugenzi
Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa HESLB, Cosmas Mwaisobwa,
amesema tume hiyo haiwezi kuongeza muda kwa wanafunzi wapya kwa ajili
ya kuomba mkopo kutokana na mchakato huo kufungwa.
Amesema
tofauti na tume ya vyuo vikuu ambayo inaweza kufungua udahili na kutoa
majina ya wale waliopata nafasi ndani ya siku tatu, HESLB huhitaji muda
mrefu kupitia taarifa za waombaji hadi kutoa matokeo.
Kuhusu
marejesho ya mikopo kwa wahitimu wa elimu ya juu waliokopeshwa na bodi
hiyo, Mwaisobwa amesema idadi kubwa ya wadaiwa na waajiri wamejitokeza
kulipa madeni yao na kuhakiki taarifa za madeni yao.
“Idadi
kubwa ya wadaiwa wamejitokeza kulipa na kuhakiki taarifa zao, pia hata
waajiri wengi wamejitokeza na kuthibitisha hili ni kwamba mapato
tuliyokusanya yameongezeka kwa kiasi kikubwa” amesema Mwaisobwa.
Amesema
wanaokaidi kulipa, watambue kuna sheria zitakazowabana, ikiwa ni pamoja
na vifungo na penati, lakini hilo halitangulizwi bali mpaka mkopaji
aonekane kukaidi.
Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa TTC,Amteua Bw. Waziri Waziri Kindamba Kuchukua Nafasi Hiyo
Kufuatia
hatua ya Serikali kununua hisa zote za Bharti Airtel ambaye alikuwa
mbia mwenza wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) na hivyo Serikali
kumiliki hisa za Kampuni hiyo kwa asilimia 100, Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemteua Bw. Waziri
Waziri Kindamba kuwa Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL.
Bw. Waziri Waziri Kindamba ameteuliwa kushika nafasi hiyo kuanzia leo tarehe 23 Septemba, 2016.
Kufuatia uteuzi huo, aliyekuwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Dkt. Kamugisha Kazaura atapangiwa kazi nyingine.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
23 Septemba, 2016
Serikali yaonya dhidi ya kampuni za ajira Zinazotapeli Watu
WIZARA ya Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu imetaka wananchi kuepuka
kampuni za uwakala wa ajira nchini ambazo hutangaza nafasi za ajira huku
zikiwataka waombaji kulipia ili kusailiwa.
Msemaji wa Wizara hiyo, Ridhiwan Wema jana alisema kampuni za namna
hiyo hawazitambui na hivyo hazina usajili wa kufanya shughuli hiyo
nchini.
“Hizi kampuni sisi hatuzitambui, mtafuta kazi hatakiwi kutozwa fedha isipokuwa kampuni inaingia makubaliano na mwajiri ambaye amempa kazi ya kumtafutia wafanyakazi,” alisema Wema.
Alitaka wananchi wawe makini na wasikurupuke kutuma maombi kabla ya kujiridhisha kama kampuni zimesajiliwa na ili kupata taarifa sahihi, mwombaji anaweza kufika Wizara ya Kazi na kuuliza, kwa kuwa wao ndio wasajili pia wakibaini uwepo wa kampuni hizo watoe taarifa wizarani na Polisi ili hatua za kisheria zichukuliwe.
Aidha, aliwasihi wananchi hususan vijana, wasiwe wepesi kulipia gharama, kwa sababu huduma ya ajira haipaswi kutozwa fedha kwa kuwa si haki kutoa kazi kwa masharti ya kulipwa, hali ambayo inaashiria vitendo vya rushwa.
Wema alibainisha kuwa kampuni zinazofanya shughuli za uwakala wa ajira nchini zimesajiliwa na Wizara ambapo moja ya masharti yanayotakiwa kuzingatiwa ni pamoja na kutowatoza waombaji wa nafasi za ajira zinazotangazwa.
Alisema kuna vigezo vingine pia vinavyozingatiwa, ili kukidhi usajili ambapo huainishwa kwa majina na taarifa za mahali pa kudumu zilipo ofisi za kampuni na kufahamu kama zimesajiliwa kwenye mamlaka husika, mfano Brela, hayo yote ni kwa ajili ya kufanya urahisi wa kizifuatilia pindi kunapozuka utata.
Aliongeza kwamba vigezo vingine ni kujiridhisha kama ina wataalamu wa kutosha kwenye masuala ya ajira, ambapo baada ya kujiridhisha husajiliwa na kuzitangaza kwenye vyombo vya habari.
Wema alitaka wananchi watambue kuwa kampuni zinazotangaza nafasi za ajira huku zikitaka waombaji walipie fedha kwa ajili ya usaili si salama kwao, hivyo wanatakiwa kuepukana nazo na kutoa taarifa.
Nuh Yusuf ambaye ni Ofisa wa kampuni ya Zoom ambayo ni wakala wa ajira nchini, alisema sababu kubwa ya kuendelea kwa utapeli wa mtandao ni kukosekana kwa ushikiano wa karibu na vyombo vya sheria hususan Jeshi la Polisi katika kudhibiti suala hilo.
“Tumejaribu kufuatilia suala hilo TCRA kitengo cha TZ-CERT, tukashauriwa twende Polisi na mmoja ambaye alipatwa na hilo tatizo, tulipofika kituo cha Polisi cha Oysterbay hawakuonesha ushirikiano wowote,” alisema Yusuf.
“Hizi kampuni sisi hatuzitambui, mtafuta kazi hatakiwi kutozwa fedha isipokuwa kampuni inaingia makubaliano na mwajiri ambaye amempa kazi ya kumtafutia wafanyakazi,” alisema Wema.
Alitaka wananchi wawe makini na wasikurupuke kutuma maombi kabla ya kujiridhisha kama kampuni zimesajiliwa na ili kupata taarifa sahihi, mwombaji anaweza kufika Wizara ya Kazi na kuuliza, kwa kuwa wao ndio wasajili pia wakibaini uwepo wa kampuni hizo watoe taarifa wizarani na Polisi ili hatua za kisheria zichukuliwe.
Aidha, aliwasihi wananchi hususan vijana, wasiwe wepesi kulipia gharama, kwa sababu huduma ya ajira haipaswi kutozwa fedha kwa kuwa si haki kutoa kazi kwa masharti ya kulipwa, hali ambayo inaashiria vitendo vya rushwa.
Wema alibainisha kuwa kampuni zinazofanya shughuli za uwakala wa ajira nchini zimesajiliwa na Wizara ambapo moja ya masharti yanayotakiwa kuzingatiwa ni pamoja na kutowatoza waombaji wa nafasi za ajira zinazotangazwa.
Alisema kuna vigezo vingine pia vinavyozingatiwa, ili kukidhi usajili ambapo huainishwa kwa majina na taarifa za mahali pa kudumu zilipo ofisi za kampuni na kufahamu kama zimesajiliwa kwenye mamlaka husika, mfano Brela, hayo yote ni kwa ajili ya kufanya urahisi wa kizifuatilia pindi kunapozuka utata.
Aliongeza kwamba vigezo vingine ni kujiridhisha kama ina wataalamu wa kutosha kwenye masuala ya ajira, ambapo baada ya kujiridhisha husajiliwa na kuzitangaza kwenye vyombo vya habari.
Wema alitaka wananchi watambue kuwa kampuni zinazotangaza nafasi za ajira huku zikitaka waombaji walipie fedha kwa ajili ya usaili si salama kwao, hivyo wanatakiwa kuepukana nazo na kutoa taarifa.
Nuh Yusuf ambaye ni Ofisa wa kampuni ya Zoom ambayo ni wakala wa ajira nchini, alisema sababu kubwa ya kuendelea kwa utapeli wa mtandao ni kukosekana kwa ushikiano wa karibu na vyombo vya sheria hususan Jeshi la Polisi katika kudhibiti suala hilo.
“Tumejaribu kufuatilia suala hilo TCRA kitengo cha TZ-CERT, tukashauriwa twende Polisi na mmoja ambaye alipatwa na hilo tatizo, tulipofika kituo cha Polisi cha Oysterbay hawakuonesha ushirikiano wowote,” alisema Yusuf.
Thursday 22 September 2016
UDOM:APPLICANTS SELECTED FOR ADMISSION INTO PhD DEGREE PROGRAMMES
APPLICANTS SELECTED FOR ADMISSION INTO PhD DEGREE PROGRAMMES
APPLICANTS SELECTED FOR ADMISSION INTO PhD DEGREE PROGRAMMES
The University of Dodoma (UDOM) wishes to announce the names of
candidates selected for admission into various PhD programmes for the
academic year 2016/17.
Admission letters for successful candidates are available in UDOM Graduate studies offices at the main administration building, Office No. 124, Third Floor.
For enquiries please visit UDOM Graduate studies offices at the main administration building, Office No. 131,Third Floor or send email through udomgsce@yahoo.com
List of Successful PhD Applicants 2016-2017 BATCH II
Admission letters for successful candidates are available in UDOM Graduate studies offices at the main administration building, Office No. 124, Third Floor.
For enquiries please visit UDOM Graduate studies offices at the main administration building, Office No. 131,Third Floor or send email through udomgsce@yahoo.com
List of Successful PhD Applicants 2016-2017 BATCH II