Tuesday 5 July 2016

Magazeti Ya Leo Jumanne ya July 5, 2016


Share:

Monday 4 July 2016

New AUDIO | Lady JayDee - Sawa na wao | Download

Share:

Official VIDEO | Harmonize - MATATIZO | Watch/Download


https://youtu.be/VMyRIff0OJg
Share:

New Audio | Raymond (Rayvanny) - Jikatae | Download MP3

Share:

PICHA: Watu 29 wapoteza maisha katika ajali ya mabasi ya City Boy, Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi

IMG-20160704-WA0026 IMG-20160704-WA0028 IMG-20160704-WA0029 IMG-20160704-WA0031 IMG-20160704-WA0033 IMG-20160704-WA0036 IMG-20160704-WA0038
IMG-20160704-WA0027
.
Ajali mbaya imeyohusisha mabasi mawili ya kampuni ya City Boy imetokea katika kijiji cha Maweni wilaya ya Manyoni, Singida na kusababisha watu 29 kupoteza maisha papo hapo huku chanzo cha ajali kikitajwa kuwa ni mwendo kasi.

Mabasi hayo yenye namba za usajili T531 DCE na T247 DCD, moja lilikuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Kahama na lingine likitokea Kahama kuelekea Dar es Salaam.

Moja ya mashuhuda wa ajali hiyo amesema kuwa madereva wa mabasi yote walikuwa katika mwendo kasi na wakati ajali inatokea walikuwa wakisalimiana kwa kunyosheana mikono kisha basi moja kupoteza mwelekeo na kuingia upande wa basi lingine na ndipo yakakutana uso kwa uso na kusababisha ajali hiyo.

Kamanda wa Polisi Singida, Thobias Sedoyeka tayari amethibittisha kutokea ajali hiyo na uchunguzi zaidi unaendelea kufanyika.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli ametuma salamu za rambirambi na kueleza kuwa amepokea taarifa hiyo kwa mshtuko na amesikitishwa na ajali hiyo ambayo imechukua maisha ya watanzania.
Share:

Kesi za Mafisadi Kutozidi miezi 9

JAJI Mkuu, Mohammed Chande Othman, amesema Mahakama Maalumu ya Uhujumu Uchumi na Ufisadi itaamua kesi kwa muda usiozidi miezi tisa na kwamba itaanza na majaji 14.

Aidha, wameandaa kozi maalumu kwa majaji 14 watakaofanya kazi katika mahakama hiyo itakayoanza Julai 11 hadi 15, mwaka huu, kwenye Chuo cha Mahakama Lushoto mkoani Tanga, ili kupeana mwongozo juu ya uendeshaji wa mahakama hiyo.

Jaji Mkuu alisema, kesi zitakazoendeshwa katika mahakama hiyo ni zile ambazo upelelezi wake umekamilika ili uamuzi utolewe mapema. Kwa mujibu wa Jaji Mkuu, dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kupambana na uhalifu huo.

Aliyasema hayo jana wakati alipotembelea Maonesho ya 40 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo katika Barabara ya Kilwa, ambayo alisema yamezidi kuwa bora kuliko miaka mingine. 
Alisema baada ya sheria hiyo ya uhujumu uchumi kupitishwa na Bunge, imekuwa na marekebisho mengi na kuboreshwa kwa kiasi kikubwa.

Jaji Mkuu alisema pia, hatua inayofuata ni Rais kutoa idhini ya sheria hiyo na baadaye kupitishwa kwa kutangazwa katika Gazeti la Serikali ili ianze kutumika.

Alieleza kuwa baada ya kutangazwa katika Gazeti hilo la Serikali, Jaji anatakiwa kutunga kanuni mbalimbali, mojawapo ikiwa ya kulinda mashahidi kutokana na kuwa sheria hiyo inahusu makosa makubwa na hatari ya ugaidi, rushwa na uhujumu uchumi.

“Tuko mbioni kutunga kanuni hizo na kuhakikisha mashahidi wanalindwa. Jengo la mahakama hii litakuwa katika Chuo cha Sheria karibu na Mlimani City na tayari tumepeleka wasajili watendaji,” alisema.

Mwishoni mwa wiki, Jaji Mkuu huyo alisema kuwa majengo ya mahakama hiyo yatakabidhiwa leo. Kutokana na maelezo yake, Mahakama iko tayari kuendesha divisheni hiyo, baada ya kukabidhiwa majengo hayo.

Alisema wataanza kutoa semina kwa majaji na watumishi wengine wa mahakama hiyo juu ya namna divisheni hiyo itakavyoendesha shughuli zake. 
Aidha, aliweka wazi kuwa hadi sasa hakuna kesi hata moja iliyokwishatambuliwa kwamba itashughulikiwa na mahakama hiyo.
Share:

Bwawa Nyumba ya Mungu Lafungwa kwa Miezi 12

SERIKALI za mikoa ya Kilimanjaro na Manyara zimelifunga Bwawa la Nyumba ya Mungu kwa kipindi cha mwaka mmoja ili kuepusha kutoweka kwa viumbe hai wakiwamo samaki kutokana na kushamiri kwa uvuvi haramu.

Aidha, wakuu wa wilaya za Moshi, Mwanga na Simanjiro wametakiwa kusimamia maamuzi hayo na kuchukua hatua kali za kisheria kwa watakaokaidi agizo hilo.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Mecky Sadiki alisema hayo wakati wa hafla maalumu ya kuwaapisha wakuu wapya wa wilaya mkoani Kilimanjaro iliyofanyika mjini Moshi, juzi.

Alisema uamuzi huo ulifikiwa katika kikao cha ujirani mwema baina ya mikoa hiyo kupitia wilaya tatu zinazolizunguka bwawa hilo na kwamba utekelezaji wa agizo hilo umeanza rasmi Julai Mosi mwaka huu.

“Hali ya uvuvi haramu katika Bwawa la Nyumba ya Mungu ni mbaya sana, mazingira yameharibiwa, kuna athari nyingi zinajitokeza ikiwamo ya kupungua kwa maji katika bwawa hilo na hii huenda ikaathiri uzalishaji umeme na kutoweka kwa viumbe hai....kama serikali hatuwezi kuvumilia tena,” alisema Sadiki.

Pamoja na bwawa hilo, Sadiki alitaka wakuu wa wilaya kusimamia agizo la Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC), kupiga marufuku misumeno ya mnyororo, kwani imebaini ni adui mkubwa wa misitu.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa aliwakabidhi wakuu hao wa wilaya migogoro mikubwa mitano iliyopo katika hatua mbalimbali za utatuzi wake kupitia viongozi waliowatangulia na kutaka kufuata sheria katika kuishughulikia.

Miongoni mwa migogoro aliyoitaja ni unaohusisha jamii ya wafugaji wanaozunguka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) na kampuni inayohudumia uwanja huo ya KADCO kuhusu umiliki wa eneo la ardhi.

Mgogoro mwingine ni wananchi wa wilaya ya Longido mkoani Arusha na mwekezaji wa eneo la utalii la Ndarakwai uliowahi kusababisha kuchomwa moto kwa eneo hilo.
Share:

Siku 72 za Vita ya UKAWA na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson

Kukamilika kwa siku 72 za mkutano wa Bunge la Bajeti kumeacha rekodi mpya ya wabunge wa upinzani kususia vikao vya Bunge kwa muda mrefu zaidi kutokana na madai ya kutoridhishwa na utendaji wa Naibu Spika, Dk Tulia Ackson katika chombo hicho cha uwakilishi nchini.

Wapinzani chini ya mwavuli wao wa Ukawa, wamejikuta kwa mara ya kwanza, 12 kati yao wakisimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kwa nyakati tofauti baada ya kutiwa hatiani na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge inayoongozwa na Mbunge wa Newala (CCM), George Mkuchika kwa kukiuka maadili. Wachambuzi wa siasa wameeleza kuwa hali hiyo imefanya Bunge kuongozwa kwa mgogoro ulioathiri mijadala na mikakati ya ndani na nje ya bajeti hiyo.

Hata hivyo, uamuzi wa Ukawa kususia vikao vinavyoongozwa na Dk Tulia kuliwafanya wabunge wa CCM kupoteza wastani wa dakika tatu kati ya 10 ambazo hupatiwa kujadili hoja, kwani walikuta wakitumia dakika za mwanzo kwenye mizaha, kebehi na vioja dhidi ya wapinzani badala ya mijadala.

Baadhi ya wabunge ambao walioongoza kumwaga vijembe ni Livingstone Lusinde (Mtera), Goodluck Mlinga (Ulanga Mashariki), Juliana Shonza (Viti Maalumu) na Abdallah Ulega (Mkuranga).

Ulega katika moja ya michango yake alifikia uamuzi wa kumpatia mtoto wake mchanga jina la Tulia kama ishara ya “kumuenzi Dk Tulia kwa uendeshaji wa Bunge unaofuata kanuni.”

“Dk Tulia umekuwa mvumilivu licha ya wabunge wa upinzani kususia vikao vinavyoendeshwa na wewe. Mke wangu naye amekuwa mvumilivu kama wewe na nitampatia mtoto wangu jina la Tulia,”alisema Ulega kabla ya siku chache Dk Tulia kutembela Hospitali ya Taifa Muhimbili kumuona mtoto huyo.

Mlinga alijikuta akiingia kwenye orodha ya wabunge waliotoa vioja bungeni wakati akichangia bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria aliposema wanawake wa vyama vya upinzani ni lazima waitwe ‘baby’ ili wapate ubunge wa viti maalumu.

Kauli nyingine iliyoibua mjadala ni ile aliyoitoa kwenye mjadala wa bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kutaka Sanamu ya Askari iliyopo Mtaa wa Samora Jijini Dar es Salaam ibadilishwe na kuwekwa ya mwanamuziki wa kizazi kipya, Diamond Platinumz kutokana na kuipaisha nchi kimataifa.

Wabunge 12 wasimamishwa 
Katika adhabu za awali, kambi ya upinzani ilishuhudia wabunge saba wakisimamishwa kushiriki vikao vya Bunge baada ya kutiwa hatiani na Kamati ya Maadili kuhusika na vurugu zilizotokea bungeni Januari 27, mwaka huu wakati wakipinga kusitisha matangazo ya moja kwa moja ya Bunge.

Wabunge wawili wa Chadema Esther Bulaya (Bunda Mjini) na Tundu Lissu wa Singida Mashariki, walisimamishwa kuhudhuria vikao vyote vya Bunge la Bajeti lililomalizika wiki iliyopita na mkutano utakaoanza Septemba.

Wengine wa Chadema Pauline Gekul (Babati Mjini), Godbless Lema (Arusha Mjini), Halima Mdee (Kawe) na Kabwe Zitto, Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia ACT–Wazalendo walisimamishwa kuhudhuria vikao vyote vya bajeti.

Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche (Chadema) alipigwa marufuku kuhudhuria vikao 10 mfululizo. Juni 17 mwaka huu wabunge wawili wa viti maalumu pia kutoka Chadema, Suzan Lyimo na Anatropia Theonest walisimamishwa kwa kudaiwa kusema uongo bungeni.

Suzan alisimamishwa vikao vitano wakati Anatropia alisimamishwa vikao vitatu na kukatwa nusu mshahara na posho.

Kama hiyo haitoshi, wabunge wengine watatu, Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini), James Ole Millya (Simanjiro) na Saed Kubenea wa Ubungo walisimamishwa vikao vya Bunge kuanzia siku hiyo na kumalizia adhabu vikao vya Septemba.

Mbilinyi alisimamishwa vikao 10 kwa kudharau mamlaka ya spika kwa kuonyesha kidole cha kati juu cha mkono wa kulia, ishara ambayo inatafsiriwa ni matusi.

Kubenea na Ole Millya walisimamishwa vikao vitano kwa kudaiwa kusema uongo baada ya kushindwa kuthibitisha madai yao. 

Upinzani wasusa 
Ukilinganisha na mabunge yaliyopita, ukiacha Bunge la Katiba, wabunge wa upinzani walikuwa wakipinga jambo bungeni bila kutoka katika mkutano, lakini safari hii walikuja na staili mpya ya kususia vikao vyote vinavyoendeshwa na Dk Tulia na kusababisha kutochangia bajeti kuu.

Wabunge hao walisusa pia kushirikiana na wabunge wa CCM katika kutumia kantini ya Bunge, michezo na mitandao ya kijamii, mbaya zaidi wamekuwa hawawasalimu.

“Wao wameamua kuanza kututenga wenyewe, Dk Tulia anaona kiongozi wa upinzani anatukanwa, anacheza tu, lakini mbunge wa upinzani anapelekwa kwenye Kamati ya Maadili. Ngoja na sisi tujitenge,” alisema Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, James Mbatia.

Ingawa kuna wenyeviti wanne ambao kwa kawaida Spika hupokezana nao, katika mikutano yote iliyotangulia kiongozi huyo aliacha kiti mara moja tu kwa Andrew Chenge, lakini siku nyingine alikaa mwenyewe na kufanya wabunge wa Ukawa kuondoka ukumbini kila anapoongoza. 

Mbunge CCM akerwa
Hata hivyo, Mbunge wa Kasulu Mjini, Daniel Nsanzugwako (CCM), ingawa alipingwa na wabunge wengi wa CCM, alisema bado anaamini katika kukaa kwa pamoja kati ya wabunge wa upinzani na Dk Tulia ili kumaliza tofauti zao.

Dk Tulia aliwataka wabunge hao kufuata utaratibu wa kikanuni wa kufikisha malalamiko yao kuhusu kiti cha Spika, licha ya kwamba hata yale yaliyofikishwa dhidi yake hayakutolewa maamuzi yoyote. 
Hoja zilizosisimua 
Unapozungumza hoja zilizosisimua katika mkutano huo wa tatu, huwezi kuacha suala la kiinua mgongo cha wabunge kukatwa kodi kwani wabunge karibu wote waliopata nafasi ya kuchangia bajeti kuu waliibuka na hoja hiyo kuipinga, lakini waliambulia patupu.

Hoja hiyo ilihitimishwa baada ya Rais Dk John Magufuli kukubali kukatwa kodi katika kiinua mgongo chake pamoja na Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya.

Wabunge wa CCM walimshukia Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango wakidai kuwa kitendo cha kukata kodi za kiinua mgongo cha wabunge ni mtego wa kuwachonganisha na wananchi.

“Kwanini muwaache Rais, mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na majaji?” alihoji mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe wakati akichangia mjadala huo kabla ya viongozi hao kujumuishwa.

Mbunge wa viti maalumu (CCM), Jacqueline Msongozi alisema Dk Mpango amegusa pabaya kwa kukata kiinua mgongo kwa kuwa tayari kila mwezi hukatwa Sh1.3 milioni ya kodi na kwa miaka mitano watakayokaa bungeni watakuwa wamekatwa Sh50 milioni.

Hoja nyingine iliyojadiliwa kwa kila wizara ni bajeti iliyopitishwa na Bunge kutopelekwa yote ambapo Mbunge wa Tarime Mjini, Easter Matiko (Chadema), alisema katika miaka yote aliyokuwa bungeni hajawahi kuona Serikali ikileta bajeti bungeni inayotekelezeka.

Hata hivyo, Mbunge wa Lulindi Jerome Bwanausi (CCM) alisema usimamizi wa karibu wa Bunge katika kuhakikisha wanachopanga Serikali inatekeleza unaanza mwaka huu kwa kamati ya Bajeti kukutana kila baada ya miezi mitatu ili kujadili utekelezaji wa bajeti na kutoa ushauri.

Kubana matumizi 
Miongoni mwa mambo yalitajwa sana ni kubana matumizi kukidhi sera ya Rais Magufuli, ambapo Mbunge wa Sengerema-CCM, William Ngeleja alisema ni moja ya mambo mema yaliyo kwenye mkutano huo.

“Uchungu wa bajeti hii ni mafisadi na wala rushwa. Walizoea kufanya kazi kwa mazoea wataumia sana. Fedha za matumizi ya kawaida zimepunguzwa kwa kiasi kikubwa, uadilifu ndio utatawala matendo ya watumishi,” alisema Ngeleja.

Katika wizara mbalimbali matumizi ya kawaida ikiwemo bajeti zilizokuwa zikitolewa kwa ajili ya viburudisho imepunguzwa kwa kiasi kikubwa huku ofisi na wizara zikiagizwa kutumia kumbi za Serikali wakati wanapofanya mikutano, makongamano na warsha.
Share:

Chadema: Maandalizi ya Kuuzuia Mkutano wa CCM Yameanza



KATIKA kutekeleza tamko la Baraza la Vijana wa Chadema (Bavicha) la kufika Dodoma kusaidiana na Jeshi la Polisi kuzuia Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bavicha Dodoma wameanza maandalizi ya kupokea vijana zaidi ya 2000.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana Malambaya Manyanya, Mwenyekiti wa Bavicha Mkoa wa Dodoma alisema, kwa sasa viongozi wa mkoa wameanza maadalizi ya kuwapokea wageni wao ambao wanatarajiwa kuanza kuwasili tarehe 21 na 22 Julai mwaka huu.

Alisema, maadalizi hayo ni ya kuwapokea vijana ambao watatoka katika mikoa yote ya Tanzania kwa lengo la kutimiza tamko la Bavicha taifa la kushirikiana na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma kuzuia mikutano na vikao vya CCM.

Alisema, kwa sasa mkoa tayari umeunda kikosi cha kufanya kazi ya maadalizi ya ugeni huo ambapo kwa nia njema utafika mjini Dodoma kutekeleza kauli ya Rais John Magufuli ya kuzuia vikao vyote na mikutano ya vyama vya siasa.

Alisema, maadalizi hayo ya kuwapokea vijana hao ni pamoja na viongozi wa kitaifa wa Bavicha kwa maana ya kutafuta mahali pa kulala na maandalizi ya chakula.

“Wapo watu ambao wanadhani Bavicha wana mpango wa kufanya fujo, sisi tunataka kurejesha Demokrasia nchini na kutekeleza kauli ya mkuu wa nchi.

“Tumekuwa tukiona jinsi mikutano ya Chadema inavyozuiliwa, na sasa msimamo wa Bavicha ni  kuzuia mkutano ya CCM unaotarajiwa kufanyika Julai 23 kwa lengo la kubadilishana uongozi kati ya mwenyekiti wa sasa wa CCM na rais msitaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete na Rais John Magufuli.

“Tumeandaa vijana takribani 2000 kutoka mikoa yote nchini watakaokuja Dodoma kusaidiana na Jeshi la Polisi kutawanya mkutano usio halali wa CCM.

“Kwa sababau mkuu wa nchi ametoa tamko la kuzuia mikutano yote ya siasa ikiwa ni pamoja na vikao vya ndani na mikutano ya hadhara hadi 2020.” Alisema Malambaya.

Alisema, Jeshi la Polisi lilizuia mikutano ya vyama vya siasa vya upinzani na mahafali ya Jumuiya ya Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Chadema (CHASO) na kuwa, sasa wanashirikiana na polisi kuhakikisha mikutano ya CCM haitafanyika.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger