Tuesday 26 April 2016

MAGAZETI YA LEO JUMANNE APRIL TAREHE 26.4.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Share:

Monday 25 April 2016

MBOWE ATISHWA ZIGO

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
BARAZA la Mawaziri Kivuli la Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, jana lilikutana kwa saa kadhaa mjini Dodoma kujadiliana mambo mbalimbali, huku likimtwisha mzigo  
Kiongozi wao, Freeman Mbowe.
Moja ya ajenda kubwa iliyotawala kikao hicho  ni jinsi gani mawaziri vivuli hao watakavyokabiliana na mawaziri wa Rais Dk. John Magufuli ndani ya Bunge kuhusiana na hoja nzito zitakazoibuka.
Mawaziri   vivuli wanatokana na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ambavyo ni Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi.
Kikao hicho   kilifanyika kuanzia saa  8.00 mchana hadi 11:30 jioni huku  mawaziri vivuli hao wakijadili   mwenendo wa Bunge kwa sasa, maandalizi ya bajeti za Kambi ya Upinzani na wajibu wao.
Chanzo cha uhakika kutoka ndani ya kikao hicho kiliiambia MTANZANIA kuwa  mawaziri wamemtaka Mbowe kusimama kidete na  kuhakikisha anasimama imara na kutoa kauli kuhusu mambo yanayoendelea ndani ya Bunge.
“Kikao chetu kilikuwa cha kawaida, tulikuwa tunakumbusha wajibu wetu kama mawaziri vivuli na mambo ya kusimamia ndani ya Bunge.
“Tumejadili kwa kina kuhusu mwenendo wa Bunge na namna waandishi wa wanavyopata shida kutimiza wajibu wao, tumemwomba Mbowe atoe msimamo wetu.
“Pia  suala la maandalizi ya bajeti yetu  tumeliangazia kwa kina, hasa upande wa kambi yetu na namna ya kujipanga zaidi… maana Bunge limekuwa kama kibogoyo.
“Serikali imekuwa inaliendesha, jambo hili linatisha,” kilisema chanzo chetu cha habari.
Juhudi za kumpata Mbowe  kuzungumzia majukumu aliyopewa hazikuzaa matunda kwa vile kwa  muda mwingi  simu yake ya kiganjani haikuwa hewani.
Mwishoni wa wiki iliyopita, Mbowe  aligoma kuwasilisha maoni ya kambi  hiyo kuhusiana na Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, huku akitaka maelezo ya muundo wa Serikali ya Rais Dk. John Magufuli akisema haujaundwa kihalali.
Alisema Rais Magufuli ameshindwa kutekeleza sheria ya utekelezaji wa majukumu ya mawaziri ya mwaka 1980  ambayo hutolewa katika gazeti la Serikali kila linapotaka kuundwa Baraza la Mawaziri.
Badala yake  kazi zimekuwa zikifanyika kwa maagizo, alisema.

Mbowe alisema mpaka sasa Serikali inafanya kazi bila kuwa na mwongozo wa utendaji kazi kwa wizara mbalimbali.
Alisema  hiyo  ina maana  Serikali inafanya kazi kwa kauli za Rais na mawaziri bila kufuata mwongozo wowote wenye msingi na uhalali wa  sheria, jambo ambalo Kambi ya Upinzani haiwezi kushiriki kwa vile ni  uvunjaji wa Katiba.
“Sheria ya utekelezaji wa majukumu ya mawaziri ya mwaka 1980, kifungu cha 5(1) kinaweka masharti kwa Rais kutengeneza mwongozo wa muundo na utekelezaji wa majukumu ya Serikali yake.
“Mpaka sasa mwongozo wa utendaji wa Serikali kwa kila wizara unaotumika ni ule uliochapishwa kwenye Gazeti la Serikali namba 494A la tarehe 17/12/2010.
“Mheshimiwa Spika, kitendo cha Serikali hii kuendesha kazi zake kwa Mwongozo wa 2010 inamaanisha kwamba majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu bado ni yale yale yaliyochapishwa mwaka 2010, kwa sababu gazeti hilo la Serikali halijafutwa,” alisema Mbowe huku akishangiliwa na wabunge wa upinzani.
Akiwasilisha hoja ya pili, Mbowe  alisema kuna uvunjwaji wa Katiba na sheria za nchi kuhusiana na bajeti unaofanywa na Serikali.
Alisema Bunge la Bajeti   kwa mujibu wa ibara ya 63(3)(b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, limepewa mamlaka ya kujadili  utekelezaji wa kila wizara wakati wa Mkutano wa Bunge wa kila mwaka wa Bajeti kwa madhumuni ya kujadili na kuidhinisha Bajeti ya Serikali.
Mbowe alisema ikiwa fedha zilizoidhinishwa na Bunge hazikutosha kutekeleza majukumu ya Serikali, kifungu cha 41(1) cha  Sheria ya Bajeti ya mwaka 2015  kinaelekeza kwa Serikali itawasilisha bungeni kwa idhini, bajeti ya nyongeza ya fedha zilizotumika ambazo zimezidi kiwango kilichoidhinishwa na Bunge au kwa madhumuni ya kugharamia mahitaji ambayo hayakupangwa.
“Mheshimiwa Spika utaratibu huu unatiliwa nguvu na Sheria ya Fedha za Umma  wa mwaka 2001(Public Finacne Act, 2001) ambako kifungu cha 18 (3) na (4) kinaitaka Serikali kuleta Bungeni bajeti ya nyongeza (mini-budget) kwa ajili ya kupata idhini ya Bunge ikiwa fedha zilizoidhinishwa awali hazikutosha.
“Utaratibu huo wa  sheria  umekuwa ukivunjwa na Serikali kwa  kufanya matumizi ya fedha ambazo hazikuidhinishwa na Bunge jambo ambalo linaua dhana ya madaraka ya Bunge ya kuisimamia na kuishauri Serikali.

“Ili kuthibitisha jambo hilo, kwa mfano, bajeti ya maendeleo iliyokuwa imeidhinishwa na Bunge kwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa mwaka wa fedha 2015/16  ilikuwa ni Sh  bilioni 883.8 na katika   fedha hizo,  fedha za ndani zilikuwa ni Sh bilioni 191.6,” alisema.
Alisema jambo la kushangaza hadi kufikia Machi mwaka huu, wizara hiyo ilikuwa imepokea kutoka Hazina Sh bilioni  607.4 kama fedha za ndani.
Source: Mtanzania
Share:

Nafasi Mbalimbali za Kazi Toka Benki ya NMB....Mwisho wa Kutuma Maombi ni Tarehe 4 Mwezi wa 5

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Jedwali  hapo chini linaonyesha nafasi mbalimbali toka Benki ya  NMB.

Kwa maelezo zaidi kuhusiana na nafasi hizo  <<  BOFYA  HAPA>  ili  uipakue PDF  yenye maelezo  ya  kina
 
Share:

Bomba la Mafuta Kutoka Uganda kuingiza Bilioni 4.8 Kila Siku

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amesema kuwa mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga ukikamilika utaliingizia Taifa Sh4.8 bilioni kila siku.

Amesema fedha hizo zitatokana na usafirishaji wa mapipa 200,000 kila siku yatakayotozwa dola 12.2 (zaidi ya Sh24,000) kila moja. 
Profesa Muhongo alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasili nchini akitokea Kampala ambako Rais wa Uganda, Yoweri Museveni juzi alitangaza kuwa bomba hilo la mafuta ghafi kutoka Hoima, Ziwa Albert litapita katika ardhi ya Tanzania kwenda Bandari ya Tanga.

Alisema katika kujipanga kwa ajili ya mradi huo, tayari Serikali imetoa kibali kwa wanafunzi 22 ambao wamepelekwa nje ya nchi kusomea masuala ya mafuta na gesi katika ngazi ya Shahada ya Uzamili na Uzamivu. 
“Bomba litakamilika Juni 2020 na itakuwa ni zawadi kwa Rais John Magufuli kabla hajarudisha fomu ya kuomba tena kugombea awamu ya pili ya urais.Lakini tutajitahidi likamilike kabla ya muda huo,” alisema Profesa Muhongo.
Alisema utakapokamilika, yatahitajika magari 100,000 ya kutolea mizigo katika Bandari ya Tanga.
Juzi, taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa ilieleza kuwa Serikali ya Uganda imetangaza rasmi uamuzi wa kutumia Bandari ya Tanga.

Rais Museveni alitangaza uamuzi huo wakati wa mkutano wa 13 wa Ushoroba wa Kaskazini uliomalizika jijini Kampala juzi na kuhudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Dk Augustine Mahiga na Profesa Muhongo.
Share:

TAKUKURU Yaanza Kuchunguza Mabilioni ya Kikwete

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imeanza kuchunguza fedha za uwezeshaji maarufu kama ‘Mabilioni ya JK’ ambazo hazikurejeshwa na wakopaji nchi nzima. 
Msemaji wa Takukuru, Tunu Mleli alisema jana kuwa taasisi hiyo imechukua jukumu hilo kwa sababu moja ya majukumu yake ni kuchunguza masuala ya rushwa na kutoa rai kwa mtu mwenye ushahidi au taarifa kuhusu suala hilo kuzitoa kwa taasisi hiyo.

“Takukuru ipo wazi kuzipokea taarifa hizo ili zitusaidie kwenye uchunguzi,” alisema Tunu.

Kati ya Sh50 bilioni zilizotolewa na Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Rais mstaafu, Jakaya Kikwete, ni Sh43 bilioni tu zilizorejeshwa, huku Sh7 bilioni zikidaiwa kutafunwa. 

Fedha hizo zilitolewa na Kikwete kwa ajili ya kuwawezesha kimitaji, wajasiriamali nchi nzima, mikopo ambayo ilipitia benki za CRDB, NMB, Community Bank na Benki ya Posta Tanzania. 
Fedha hizo kutoka Mfuko wa Rais, zilikuwa zikikopeshwa kwa riba ya asilimia 10, ambapo asilimia mbili ilikuwa inaingia serikalini na nane ilikuwa inabaki kwenye benki hizo. 

Hata hivyo, baadhi ya vyama vya Akiba vya Kuweka na Kukopa (Saccos), vilivyopewa fedha hizo, vilitoa mikopo hiyo kiholela, huku baadhi ya viongozi wakidaiwa kutengeneza majina feki na kukopeshana fedha hizo. 

Imedaiwa kuwa Saccos nyingi ambazo zilifuja fedha hizo katika mikoa mbalimbali, viongozi wake wengi walikuwa pia ni viongozi wa kisiasa na wengine wakiwa na nyadhifa serikalini. 

Kwa mujibu wa uchunguzi huo, baadhi ya waliokopeshwa fedha hizo na Saccos mbalimbali, hawakuwa wanachama, bali walichomekwa baada ya kuonekana kuna fursa ya ‘kupiga dili’.

Chanzo kutoka Takukuru, kimedokeza  kuwa makamanda wa taasisi hiyo katika mikoa mbalimbali, wamepewa maelekezo ya kuchunguza mahali yalipo mabilioni hayo na nani waliyafuja.

 “Ni kweli tumepewa maelekezo ya kuchunguza fedha hizo. Unajua hizi ni fedha za umma haziwezi kutafunwa tu hivihivi na Serikali ikakaa kimya,” alidokeza mmoja wa maofisa wa Takukuru. 
Machi mwaka jana, aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji), Christopher Chiza aliagiza kufanyika kwa ukaguzi wa kina wa fedha hizo.

Alitoa agizo hilo wakati wa ziara yake katika Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi (Neec), ambako aliagiza watakaobanika kuhusika na ubadhirifu wa fedha hizo wachukuliwe hatua za kisheria.

“Lazima tuangalie mabilioni ya JK yalipotelea wapi, yalivyofujwa na wahusika wapo wapi ili sheria ichukue mkondo wake. Nimeambiwa kuna zilizobaki tujue ziko wapi,” alikaririwa Chiza akisema. 
Lakini Desemba 24, 2013, mtangulizi wa Chiza, Mary Nagu alikaririwa akisema Sh43 bilioni kati ya Sh50 bilioni za mabilioni ya JK zilizokopeshwa kwa wajasiriamali 74,701 zilikuwa zimerejeshwa. 

Nagu alitoa takwimu hizo alipokuwa akizungumzia mafanikio ya Serikali ya Rais Kikwete katika, utaratibu uliofanywa pia na wizara nyingine. 
Suala la mabilioni hayo ya JK limekuwa likiibuka mara kwa mara bungeni na katika mitandao mbalimbali ya kijamii huku wananchi wakitaka zirejeshwe.
Share:

CAG Kuanika Mafisadi Bungeni Leo Wakati Akiwasilisha Ripoti Yake

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mdhibiti  na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) leo anawasilisha bungeni ripoti ya mwisho ya ukaguzi wa hesabu za serikali ya mwaka 2014/15.

Ingawa haijajulikana rasmi nini kilichomo ndani yake, baadhi ya watu waliohojiwa wanatarajia CAG kubaini mchwa wanaotafuna fedha za umma na namna ya kukabiliana nao.

Aidha wengine wanatarajia taarifa ya hali bora zaidi ya usimamizi wa fedha za umma kuliko kipindi cha nyuma. 

Ripoti hiyo awali ilikuwa imepangwa kuwasilishwa bungeni mwishoni mwa wiki (Aprili 22) kabla ya kuahirishwa hadi leo.

“Ni kweli CAG atawasilisha ripoti kesho (leo) bungeni, ”Naibu Katibu wa Bunge na Utawala, Joel Joel alithibitisha juu ya kuwasilishwa kwa ripoti hiyo leo. 

Miongoni mwa wabunge waliozungumza na mwandishi wa habari hizi, wamesema wanatarajia CAG kuonesha mambo mazuri kwa maana ya taasisi zilizofanya vizuri katika usimamizi wa fedha za umma lakini pia mambo mabaya.

“Lazima ripoti itaibua madudu maana walizoea (watendaji serikali) kana kwamba hapakuwapo na serikali,” alisema Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ally Keissy na kusisitiza kuwa pamoja na wabunge wenzake, watamsaidia Rais John Magufuli kupambana na ubadhirifu serikalini.

Keisy alisema akiwa mbunge, anaamini pamoja na wenzake, wanachosubiri ni kuona ripoti hiyo na kuhakikisha wanaohusika na kuchezea fedha za serikali, kabla ya kufikishwa mahakamani, wanarudisha fedha hizo. 

“Atakachosema CAG sisi tutakuwa tayari kusimama kusaidia Rais aendelee kupambana na ubadhirifu,” alisema.

Kwa upande wake, Mbunge wa Mbinga Vijijini, Martin Msuha, alisema ripoti hiyo ni muhimu katika usimamizi wa serikali na inategemewa kuwa na mambo mazuri na mabaya kwa maana ya majipu ambayo yatapaswa kutumbuliwa.

Mbunge wa Bukoba Vijijini, Jasson Rweikiza alisema matarajio waliyo nayo ni kwamba ubadhirifu na wizi utakaoibuliwa na ripoti hiyo utashughulikiwa mara moja.

 “Kama kuna ubadhirifu, mishahara hewa na wizi vyote vishughulikiwe...kama kuna ubadhirifu na wizi wowote, mwizi mahali pake ni jela,” alisema Rweikiza akishutumu uwapo wafanyakazi hewa katika halmashauri yake.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATATU APRIL TAREHE 25.4.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

Sunday 24 April 2016

DOWNLOAD VIDEO LADY JAY DEE -NDI NDI NDI

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

download Mafikizolo & Diamond Ft. Dj Maphorisa - Colors Of Africa | Mp3 Download [New Song]-VIDEO &MP3

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

wimbo mpya wa diamond platnumz -Mafikizolo & Diamond Ft. Dj Maphorisa - Colors Of Africa | Mp3 Download [New Song]


https://scontent.cdninstagram.com/t51.2885-15/e35/12959992_1555181168109729_309654457_n.jpg?ig_cache_key=MTIzNDk3OTExNzUwMDg2MDc3Mw%3D%3D.2
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI TAREHE 24.4.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger