Saturday, 6 December 2025

“MAWAKILI MNA NAFASI KUBWA YA KUONDOA CHANGAMOTO MBALIMBALI ZA KISHERIA KATIKA TAIFA HILI” – NAIBU MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI


Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Samwel M. Maneno amemuwakilisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza S. Johari katika sherehe za kupokelewa na kukubaliwa Mawakili wapya wa Kujitegemea zilizofanyika tarehe 5 Desemba, 2025 Jijini Dodoma.

Akizungumza katika sherehe hizo za kuwapokea na kuwakubali Mawakili wapya wa Kujitegemea, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali amewakumbusha Mawakili hao kuwa wana nafasi kubwa katika kuondoa changamoto za Kisheria zinazowakabili wananchi katika maeneo mbalimbali nchini.

“Naomba nitumie siku hii adhimu kuwaelezea Mawakili wapya kuwa, mna nafasi kubwa sana ya kuondoa changamoto mbalimbali za kisheria katika Taifa hili." Amesema Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Aidha, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali amewakumbusha Mawakili wa Serikali juu ya umuhimu wa kuzingatia weledi katika utendaji wa haki kwa wananchi, ambapo ameeleza kuwa Mawakili ni kiungo muhimu sana baina ya wananchi na Mahakama katika kuichambua na kuitafsiri haki na sheria.

“Nitumie nafasi hii kuwaeleza Mawakili mliokubaliwa leo kuwa, mna nafasi kubwa katika kuhakikisha jukumu la utoaji haki linatekelezwa kwa ufanisi na Mahakama. Mnapaswa kuisaidia Mahakama itende haki na kuhakikisha wananchi wanapatiwa haki zao wanapokwenda Mahakamani au kwenye vyombo vingine vya kisheria”. Amesema Mhe. Maneno.

Katika hatua nyingine, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali amesema Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali itaendelea kuunga mkono Serikali na taasisi mbalimbali zinazotoa huduma za msaada wa kisheria nchini ambapo Ofisi imeanzisha Kamati za Ushauri wa Kisheria katika ngazi ya Mikoa na Wilaya pamoja na kuendesha Kliniki za msaada wa kisheria katika maeneo mbalimbali nchini.

“Napenda kuwasisitizia pia Mawakili wote ikiwa ni pamoja na Mawakili mlioapishwa siku ya leo kuwa mnapaswa kushiriki katika Wiki ya Sheria na Kampeni mbalimbali za kutoa misaada ya kisheria na kutoa elimu ya sheria kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini.” Amesema Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Vilevile Mhe. Maneno amewasihi Mawakili wapya kuwa nidhamu na kuzingatia Kanuni za Maadili ya taaluma ya sheria, huku akiwakumbusha kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ataendelea kudhibiti nidhamu ya Mawakili wa Kujitegemea kwa kuzingatia mamlaka aliyopewa kupitia Sheria ya Mawakili, Sura ya 341.

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Jaji George M. Masaju amewataka Mawakili hao wapya waliopokelewa na kukubaliwa kufanya kazi kwa kuzingatia uadilifu kwa kufuata Katiba na Sheria za Tanzania ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi mkubwa

.“Mnapokwenda kutekeleza majukumu yenu ni muhimu mkafanye kazi kwa uadilifu mkubwa na kuzingatia miongozo mbalimbali ikiwemo Katiba, Sheria na Kanuni mbalimbali.” Amesema Jaji Mkuu.

Sambamba na hilo, Jaji Mkuu wa Tanzania amewaeleza Mawakili hao kuhakikisha wanatenda haki kwa wananchi, kwa kusimamia misingi ya sheria , kanuni na taratibu, huku wakiwa sehemu ya kuendelea kulinda amani ya Taifa.

“Niwaombe Mawakili mliokubaliwa na kupokelewa leo mkatende haki kwa wananchi, mkazingatie utawala wa sheria unafuatwa, pia ninyi ni sehemu ya kuilinda na kuitetea Amani ya Taifa hili.” Amesema Jaji Mkuu.

Sherehe hizo za 73 za kuwapokea na kuwakubaki Mawakili wapya Kujitegemea zimehusisha jumla ya wahitimu 774.
Share:

Friday, 5 December 2025

MBUNGE MUTASINGWA AKUTANA NA WAANDISHI WA HABARI CHAKULA CHA PAMOJA, AHAMASISHA KALAMU ITUMIKE KULINDA JAMII


Mh. Mbunge wa Jimbo la Bukoba Johnston Johansen Mutasingwa akizungumza na waandishi wa habari 
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Bukoba Mh Acton Jasson Lwankomezi akizungumza na waandishi wa habari 

Na Mbuke Shilagi Kagera.

Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mkoani Kagera Mh.Jonston Johansen Mutasingwa amewataka waandishi wa habari kutumia kalamu zao kuandika mambo yanayosaidia jamii lakini pia ambayo yatailinda jamii.

Akizungumza na waandishi wa habari katika chakula cha mchana leo Desemba 5,2025 katika ukumbi wa St. Teresa uliopo Manispaa ya Bukoba alichowaandalia waandishi wa habari kwa kuwashukuru kwa kazi waliyoifanya wakati wa kampeni Mh. Mutasingwa amesema kuwa waandishi wa habari pia ni wasimamizi wa miradi inayotekelezwa kwa kuandika habari za mwendelezo kwa kila hatua ya miradi inayotekelezwa.

Mh. Mutasingwa ameongeza kwa kusema kuwa kalamu ya mwandishi wa habari inaweza kusababisha upepo kuwa mzuri ama hata kuwa mbaya hivyo amewataka kuwa makini na taarifa wanazozitoa kwa kulinda amani ya nchi.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Bukoba amesema kuwa lengo ilikuwa kukutana na kula chakula pamoja na kufahamiana huku akiongeza kuwa nguvu ya habari ni kubwa kwa kuwataka kushirikiana katika kuhakikisha wanatumia kalamu zao kwa usahihi.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA DESEMBA 5,2025

 

Magazeti

         

          

Share:

NDOTO MBAYA ZAFIKIA MWISHO: AMOS ASIMULIA MASAIBU YAKE


Kwa miaka mingi, maisha yangu, Amos, mwanakijiji wa makamo kutoka Kijiji kidogo cha Sokoine, yalikosa amani. Sikuwa mgonjwa kimwili, lakini ndani ya roho yangu kulikuwa na mateso makubwa. Usiku ulikuwa adui yangu mkubwa. 

Kila nilipolala, nilikumbana na jinamizi lisiloelezeka—ndoto za ajabu, za kufisha moyo, ambazo zilinifanya niamke nikiwa nimechoka, nikiwa na hofu, na nimekata tamaa. Watu wengi waliniona kama mtu niliyepatwa na mikosi isiyokuwa ya kawaida, nilitafuta usaidizi kila kona  bila kupata afadhali. Maisha yangu ya kila siku yalikuwa yameathirika sana kwa kukosa usingizi bora.


Mwezi mmoja uliopita, nilikuwa nimekaa kwenye kibaraza changu, nikivinjari mitandao ya kijamii, kujaribu kusahau uchovu wa mchana. Ghafla, jicho langu likatua kwenye tangazo la ajabu. Ilikuwa ni kuhusu Daktari Magongo, mganga wa asili maarufu kwa kusaidia watu waliokuwa wamekwama katika matatizo mbalimbali ya kiroho na kimwili. Jambo lililonivutia zaidi ni shuhuda nyingi zilizoelezea jinsi alivyomaliza matatizo ya usingizi na ndoto mbaya kwa wengine. Mwanzoni, nilisita, nikijua tayari nilitumia kiasi kikubwa cha pesa bila mafanikio. Lakini kutokana na ukweli kwamba nimekosa amani kwa muda mrefu, niliamua kujipa nafasi nyingine.


Nilituma ujumbe mfupi moja kwa moja kwa Daktari Magongo, nikieleza shida yangu kwa urefu. Alinijibu haraka sana kwa ukarimu na utulivu ulionipa tumaini jipya. Alinielekeza jinsi ya kufuata maelekezo machache, ambayo yote yaliendana na desturi na mila zetu. Sikulazimika kuondoka kijijini kwangu—utaratibu wote ulikuwa rahisi na wa kipekee.


Siku chache baada ya kuanza utaratibu wake, nilihisi tofauti. Mara ya kwanza, ndoto za ajabu zilipungua. Baadaye, zilibadilika na kuwa ndoto za kawaida. Ndani ya wiki mbili tu, jinamizi lilikuwa limeisha kabisa! Sasa ninaweza kulala fofofo, nikiwa na amani kamili usiku kucha. Ninaamka nikiwa na nguvu na furaha ya kuanza siku. Maisha yangu yamebadilika; uhusiano wangu na familia umekuwa mzuri, na kazi yangu inaendelea vizuri.


Siwezi kuelezea kwa maneno jinsi ninavyoshukuru kwa msaada wa Daktari Magongo. Magongo alinirudishia uhai na amani yangu. Kama wewe, ndugu yangu, unateseka kwa namna yoyote ile, iwe ni ndoto, bahati mbaya, au matatizo ya maisha, nakuhimiza sana umtafute Daktari Magongo. Yeye ni daktari wa asili anayeaminika na mwenye uwezo wa kusaidia wengi.

Share:

Thursday, 4 December 2025

WABEBA ZEGE WAYAKATAA MAANDAMANO YA DISEMBA 09, "TUMECHOKA"



Na mwandishi wetu,Dar

WAKATI joto la maandamano ya Disemba 09 likizidi kupanda, mjadala wa kuyapinga na kuyakataa maandamano hayo umeendelea Kila Kona, huku vijana, wazee na wanawake wakieleza kuwa wasingependa kilichotokea Oktoba 29 kijirudie tena.

Hawa hapa ni Vijana waliokuwa katika Shughuli zao za Kujitafutia mkate wa kila siku kama ambavyo inaonekana kwenye Video hii maongezi yao yaliyonaswa hapa ni kuhusu kupinga vikali kujihusisha na masuala ya maandamano huku wakilinganisha athari ambazo wamezipata Oktoba 29.

"Tumechoka na maandamano tumekaa ndani siku tatu tunachokula chamaana hakuna hiyo Tarehe 09 hatuyawezi tumechoka maandamano " Mwananchi wa Dar es Salaam.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger