Monday, 29 September 2025

WITO WATOLEWA KWA WADAU KUENDELEA KUUNGA MKONO JITIHADA ZA KUPAMBANA NA CHANGAMOTO ZA LISHE NCHINI




NA. MWANDISHI WETU - DAR ES SALAAM
Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Chakula na Lishe Dkt. Germana Leyna ametoa wito kwa wadu wa masuala ya lishe nchini kuendelea kuunga mkono jitihada za kupambana na changamoto zinazokabili masuala ya Lishe huku akisema kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kukabili changamoto hizo kwa kuwa na mikakati madhubuti.


Wito huo umetolewa leo 29 Septemba, 2025 kwenye mahojiano maalumu katika kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Jijini Dar es Salaam katika kuelekea kwenye Mkutano Mkuu wa 11 wa Wadau wa Masuala ya Lishe.

"Serikali imeendelea kuweka mikakati mbalimabli ikiwemo kuendelea kutoa elimu kwa umma na kuhakikisha jamii inakuwa na uelewa wa masuala ya lishe ili kuendelea kuwa na Taifa lenye watu wenye lishe bora na niseme apa kuwa wadau waje tunganishe nguvu katika kupambana na changamoto za maswala ya Lishe" amesema Dkt Germana Leyna.


Pia ameongoza kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha inawafikia wazalishaji hasa wakulima wawapo katika shughuli zao za kilimo na kuhakikisha wanapata elimu ya lishe bora na umuhimu wa kutunza chakula cha matumizi ya nyumbani badala ya kuuza chote.

Ametumia fursa hiyo kutoa rai kwa wadau kuendelea kujitokeza na kuendelea kuweka chachu katika masuala ya lishe nchini.



=MWISHO=
Share:

TAEC YATOA ELIMU YA MIONZI KWA WANAFUNZI 9,391 WA SEKONDARI MKOANI TANGA


Na Mwandishi Wetu, Tanga

Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) imeendesha kampeni maalum ya kutoa elimu ya mionzi kwa wanafunzi 9,391 wa shule 10 za sekondari mkoani Tanga, ikiwa ni hatua ya kuondoa dhana potofu kuhusu teknolojia ya nyuklia na kuhamasisha kizazi kipya kuelekea sayansi.

Kampeni hiyo ilifanyika kuanzia Septemba 22 hadi 26, 2025 katika shule za Chumbageni, Galanosi, Kiomoni, Mikanjuni, Mkwakwani, Usagara, Nguvumali, Pongwe, Mabokweni na Msambweni.

Kupitia mafunzo ya vitendo, mijadala ya papo kwa papo na maonesho ya vifaa vya mionzi, wanafunzi walipata uelewa wa matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia katika sekta za afya, kilimo, viwanda na mazingira.

TAEC wamesema elimu hiyo inalenga kuondoa hofu kwa jamii, kuandaa wataalamu wa baadaye na kuchangia mapambano dhidi ya saratani kupitia tiba ya mionzi (radiotherapy).

“Tunataka vijana wetu waelewe kuwa mionzi siyo silaha pekee, bali pia ni tiba, chakula bora na usalama wa mazingira. Wanafunzi hawa ndio wataalamu wa kesho,” walisema wataalamu hao.

TAEC pia imesisitiza kuwa elimu hii ni mchango katika kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), hususan afya bora, elimu bora, nishati na viwanda pamoja na ulinzi wa mazingira.

Kwa kuwahamasisha wanafunzi kuchukua masomo ya sayansi, TAEC inalenga kuongeza idadi ya wataalamu katika fani za fizikia tiba, uhandisi wa nyuklia na usalama wa mionzi.

Kampeni hiyo ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu wa tume hiyo kuhakikisha taifa linakuwa na kizazi chenye maarifa ya sayansi ya nyuklia kwa maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi.
Share:

Sunday, 28 September 2025

MATHIAS CANAL AONGOZA UPATIKANAJI MIL 85 UJENZI WA KANISA KIOMBOI-IRAMBA


Mwanzilishi na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya WAZOHURU MEDIA Ndg Mathias Canal amewaongoza Viongozi wa dini, Wadau wa maendeleo na Waumini kwenye harambee ya ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania-KKKT Usharika wa St George Kiomboi Wilaya ya Iramba Mkoani Singida.

Katika harambee hiyo iliyofanyika leo tarehe 28 Septemba 2025 katika eneo la Ujenzi wa Kanisa Mtaa wa Lulumba, Mgeni huyo rasmi amesimamia upatikanaji wa fedha taslimu Tsh 79,407,000 ambapo ahadi ni Shilingi Milioni 4,010,000 na jumla ya fedha zote zilizopatikana ni Shilingi Milioni 85,017,000.

Mgeni rasmi Ndg Mathias Canal pamoja na marafiki zake waliomuunga mkono amechangia jumla ya Tsh milioni 3,835,000 na mifuko 10 ya Saruji.

Akizungumza katika harambee hiyo Mathias amesema kuwa Kanisa ni nguzo muhimu ya maisha ya kiroho, kijamii na hata kiuchumi. Kupitia kanisa waumini wanajifunza misingi ya upendo, mshikamano, uadilifu na ujenzi imara wa taifa.

"Ujenzi wa kanisa si kwa ajili ya kizazi cha leo pekee, bali ni urithi wa vizazi vijavyo. Tunaposhiriki katika harambee hii, tunakuwa sehemu ya historia ya imani na mshikamano wa Kikristo, Mradi huu wa ujenzi wa kanisa la kisasa ni mfano wa kujitegemea kama kanisa, uzalendo, na dira ya maendeleo ya KKKT kwa ujumla Usharika wa St George, Jimbo la kati, na Dayosisi ya kati" Amesisitiza

Amewasihi waumini kuchangia ujenzi wa kanisa hilo kwani litakapokamilika litakuwa kanisa bora linalozingatia mahitaji ya sasa na baadaye yakiwemo ya watu wenye uhitaji maalumu na wanajamii ya Kiomboi. Kanisa linalojengwa lina uwezo wa kuhudumia waumini 2500, ukumbi wa mikutano wenye uwezo wa kuhudumia watu 300, ofisi 6 za viongozi, stoo ya vifaa vya meza ya Bwana, Duka la vitabu, sehemu ya kusomea, ukumbi mdogo wa chakula na vinywaji baridi kwa wakati moja.

Ujenzi huo wa kanisa upo katika awamu ya pili ya ukamilishaji wa ujenzi wa ukuta na kuanza kumwaga zege ya juu (Slab) ikiwa ni sehemu muhimu ya ujenzi katika zile awamu nne ambazo ni (1) Kujenga msingi, (2) Kujenga ukuta, (3) Kupaua jengo, na (4) kupaka rangi na umaliziaji.

Mathias ameongeza kuwa Ujenzi wa kanisa hilo unahitaji mshikamano wa dhati kati ya waumini, viongozi na wadau wote wa maendeleo hivyo amewasihi waumini kushikamana kwa moyo wa kujitolea; kwani inapojengwa nyumba ya Mungu, ni kujijengea wao na familia zao baraka zisizopimika.
Share:

MAHAFALI YA 19 YA KIDATO CHA NNE SHULE YA SEKONDARI RWEPAS

Share:

RAIS SAMIA ANATHAMINI MCHANGO WA WAONGOZA WATALII NCHINI


Na Mwandishi Wetu- Karatu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anathamini na kujua kazi na mchango wa waongoza watalii nchini Tanzania.

Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi ameyasema hayo katika tukio la Fainali ya Safari Field Challenge Toleo la 10, likiambatana na maadhimisho ya Miaka 10 ya mashindano haya, sambamba na Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani lililofanyika kwenye ukumbi wa Oasis Wilayani Karatu, Arusha usiku wa Septemba 27,2025.

“Rais Samia anafahamu tunafanya tuzo hapa leo na ameangalia challenge zote mlizofanya na amekubali na akasema anawapenda sana na anawaelewa sana na ndio maana alifanya filamu ya Tanzania the Royal Tour, alikwenda Pemba akavua Samaki” amesema Dkt. Abbasi.

Aidha, Dkt. Abbasi ametumia fursa hiyo kuwahimiza waongoza watalii kushiriki katika tuzo za utalii na uhifadhi zinazotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2025.

“Tumezindua tuzo za utalii na uhifadhi, ni tuzo za ushindani watu watashindanishwa kwenye kategoria mbalimbali hivyo mshiriki katika kupambania kategoria mbalimbali ikiwemo ya safari guide, mountain guide n.k” amesema Dkt. Abbasi.

Amesema kuanzi tarehe 10 mwezi Oktoba tuzo zitafunguliwa na zitakuwa na kategoria saba zenye tuzo zaidi ya 56, na tarehe 19 itakuwa ni usiku wa tuzo.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI SEPTEMBA 28,2025

Magazeti






 





Share:

Saturday, 27 September 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI SEPTEMBA 27,2025




Magazeti
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger