Wednesday, 26 February 2025

WAZIRI SIMBACHAWENE ATOA WITO KWA WANANCHI WA CHIPOGOLO KUSHIRIKI MAENDELEO



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo wakati alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Wananchi wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akiwa ameongozana na wananchi wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo mara baada ya kuwasili katika Kijiji hicho alipofanya ziara iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (aliyevaa miwani) akisisitiza jambo kwa Viongozi wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo wakati Waziri huyo alipofanya ziara iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (aliyenyanyua mikono) akielekeza jambo kwenye korongo linalohitaji kujengwa daraja katika Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo wakati alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akisalimiana na Wananchi na Viongozi mara baada ya kuwasili katika Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo wakati alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Mwenyekiti Mstaafu wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo Bi. Grace Ndogwe akiwasilisha hoja kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati wa ziara ya Waziri huyo iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Wananchi na Viongozi wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akifurahia jambo wakati akisalimiana na Wananchi wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo mara baada ya kuwasili wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Na. Mwandishi Wetu-Chipogolo


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ametoa wito kwa wananchi wa Kijiji cha Chamsisili, Kata ya Chipogolo, Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa kushiriki shughuli za maendeleo katika kijiji hicho.

Mhe. Simbachawene ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kibakwe katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa ametoa kauli hiyo tarehe 25 Februari, 20245 akiwa kwenye ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika Kata hiyo ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi.

Akizungumza na wananchi katika Kijiji cha Chamsisili, Mhe Simbachawene amewasisitiza wananchi wa Kijiji hicho kuweka nguvu kazi kubwa kwenye daraja wanalokusudia kujenga kufuatia korongo kubwa lililoko sehemu ya Kijiji hicho.

Naomba mshiriki maendeleo katika Kata yenu, adha tunayoipata kwa kutokushiriki maendeleo ni kubwa, hivyo tujitahidi kutumia nguvu zetu wakati Serikali inatafuta namna ya kufanya kupitia taasisi yake ya Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA). Amesisitiza Waziri Simbachawene.

Katika kuhakikisha ujenzi wa daraja hilo unatekelezwa kwa haraka, Waziri Simbachawene ameahidi kuchangia mifuko 300 ya saruji.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Chipogolo, Mhe. Kayanda Mwanika amemshukuru Waziri Simbachawene kwa kufanya ziara hiyo ambayo italeta chachu kwa maendeleo ya Kata hiyo.

Vilevile Mhe. Mwanika amempongeza Waziri Simbachawene kwa ahadi ya mifuko 300 ya saruji itakayoongeza nguvu kubwa katika kukamilisha daraja hilo na kuahidi kushirikiana nae pamoja na wananchi wa Kijiji hicho kwa lengo la kuleta maendeleo.
Share:

TUMIENI VYAKULA VYA ASILI ILI KUDHIBITI UDUMAVU

 






Na mwandishi wetu Muleba


Wadau wa lishe Wilayani Muleba Mkoani Kagera wametakiwa kushirikiana na Serikali kuhamasisha wananchi kula vyakula vya asili ambavyo vipo kwenye maeneo yao ili kuweza kudhibiti udumavu dhidi ya watoto katika Wilaya hiyo.


Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Bi. Edina Kabyazi ametoa  kauli hiyo  kwenye kikao cha kamati jumuishi ya lishe ngazi ya Wilaya cha robo ya pili ya Oktoba hadi Desemba mwaka 2024/2025 ambacho kimefanyika Februari 25, 2025  katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.


Bi. Edna Kabyazi amesema kuwa jukumu la uhamasishaji wa ulaji wa vyakula vyenye lishe sio la Watalaam wa afya pekee bali ni jukumu la kila mdau wa maendeleo kwani panahitajika nguvu ya ziada na kutokata tamaa lengo likiwa ni kuhakikisha kila kaya inakuwa na lishe bora.


Awali akiwasilisha taarifa ya lishe Afisa lishe Wilaya ya Muleba Dkt. Robson Tigererwa amesema kuwa wameweza kufanya kampeni ya ugawaji wa matone ya vitamin A na dawa za minyoo ambapo walilenga kuwapatia watoto 119,737 na wameweza kuwapatia watoto 119,440 sawa na asilimia 99.


Dkt. Tigererwa amesema kuwa pia pamefanyika upimaji wa hali ya lishe kwa watoto 53,881 wenye umri wa miezi sita hadi 59 ambapo watoto wenye hali nzuri ya lishe ni 50,649 sawa na asilimia 94, wenye hali hafifu ya lishe ni 3,017 sawa na asilimia 5.6 huku watoto wenye hali mbaya ya lishe wakiwa ni 216 sawa na asilimia 0.4.


Aidha amesema kuwa bado kuna changamoto ya baadhi ya wazazi kugoma kuwapeleka watoto kwenye zoezi la chakula dawa pamoja na ushiriki mdogo wa wanaume kwenye masuala ya lishe hasa kwenye mafunzo na mikutano.


Nao baadhi ya washiriki ambao ni Johanes Mtoka na Gaudini Gration wameshauri kuwepo kwa mashamba darasa kwenye shule za msingi na Sekondari ili kuondoa changamto ya  wa uhaba wa chakula shuleni ambao umekuwa ukipelekea baadhi ya wanafunzi kuwa na udumavu kutokana na kushinda njaa siku nzima.

Share:

Tuesday, 25 February 2025

NGEZE AMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUPAMBANIA AFYA YAKE



Na Lydia Lugakila - Bukoba

Mwenyekiti wa Alat Taifa,Diwani wa kata ya Rukoma Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Mkoani Kagera Mhe, Murshid Hashimu Ngeze amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu hassan kwa namna alivyosimama katika kugharamia matibabu  yake alipopata ajali Mwaka 2022 iliyopelekea kukatwa mguu wake mmoja.

Mhe, Ngeze ametoa kauli hiyo katika dua Maalum ya Kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumnusuru katika ajali mbaya ambayo imeenda sambamba kuliombea taifa hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi mkuu ujao iliyofanyika kata Rukoma Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Mkoani Kagera  ikiongozwa na viongozi mbali mbali wa dini na madhehebu.

"Namshukuru Rais Samia pamoja na wasaidizi wake kwa juhudi zao za kugharamia matibu yangu ndani na nje ya Nchi tangu nilipopata ajali iliyopelekea kuvunjika mguu  mmoja hadi kupelekea kukatwa" ,amesema Mwenyekiti  Alat Taifa.

Ngeze amesema Rais Samia ana upendo anajali anasikiliza na sio kwamba anaangalia miradi tu bali anaangalia Afya za Watanzania.

Ngeze amesema kupona kwake kuliimarika siku tatu alipokuja Makamu wa Rais wa Tanzania kumuona Hospitalini kwa maelekezo ya Rais Samia aliyemtaka aeleze nini anataka kufanyiwa ili Afya ikae sawa.

Aidha kiongozi huyo amewashukuru Madaktari waliohusika katika kutoa huduma ya matibabu bila kuchoka, Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya Taifa na Mkoa, taasisi za kifedha viongozi mbali mbali wa kiserikali pamoja na mtu mmoja mmoja ikiwemo familia yake  kwa namna walivyoshirikiana kutoa huduma mbali mbali katika kipindi hicho kigumu.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Privatus Mwoleka,  akizungumza kwa niaba ya Madiwani wa Halmashauri hiyo amesema wanamshukuru Mungu kwa uhai wa kiongozi huyo lakini pia wanampongeza Rais Samia kwa matibabu aliyoyapata nje na ndani ya Nchi kwani Rais Samia amegharamikia matibabu ya Ngeze kwa  asilimia 80.

Mkuu wa Wilaya Bukoba Erasto Sima aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa Kagera, Hajjat Fatma Mwassa amesema Kata ya Rukoma imekuwa mfano katika shughuli mbalimbali za maendeleo kupitia Mwenyekiti Ngeze, ambaye amekuwa chachu ya kusimamia miradi inatekelezwa kwenye halmashauri hiyo yenye vijiji 94 kata 29.

Baadhi ya Viongozi wa dini waliongoza dua hiyo ni pamoja na Mchungaji Mathias Buberwa wa Kanisa la KKKT Dayosisi Kaskazini Magharibi, Padre Achileus Rugemalia wa Poroko Ichwandimi pamoja na Sheikh Twahir Said wa Wilaya Bukoba.

Kwa pamoja wameliombea Taifa la Tanzania liendelee kuwa na amani umoja na mshikamano, ili viongozi wake wajaliwe rehema na busara katika kutekeleza majukumu yao kuanzia vitongoji hadi taifa na kuliepusha na migogoro mbalimbali.
Share:

TPA YAELEZA MAFANIKIO YAKE KWA KIPINDI CHA MIAKA MINNE



Na Dotto Kwilasa, Dodoma

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imesema tangu Serikali ya awamu ya Sita iingie madarakani,mapato ya mamlaka hiyo yameongezeka kutoka shilingi trilion 1.1 Mwaka wa Fedha 2021/22 hadi shilingi trilion 1.475 Mwaka wa Fedha 2023/24.

Hayo yameelezwa leo jijini hapa February 24,2025 na Mkurugenzi Mkuu wa TPA Plasduce M. Mbossa wakati akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya Mamlaka hiyo (2021/22 – 2023/24) ikiwa ni mafanikio ya Mamlaka hiyo tangu Serikali ya awamu Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan iingie madarakani.

Amesema katika mwaka wa fedha wa 2022/23 mchango wa sekta ya bandari ulikuwa Shilingi trilioni 10.8 sawa na asilimia 7.3 ya pato la Taifa lililokuwa Shilingi trilioni 148.3.

"Ongezeko hili la mapato limetokana na:Mapato ya matumizi ya bandari kuongezeka kutokana na ongezeko la shehena iliyohudumiwa bandarini
Mapato ya kuhudumia meli ambayo yameongezaka kutokana na ongezeko la idadi ya meli na ukubwa wa meli,Mapato ya mrabaha kwa tani au kasha linalohudumiwa na Kampuni ya DPW Dar es Salaam na Tanzania East Africa Gateway Terminal Limited (TEGTL) pamoja na tozo la pango (Lease Rent) la maeneo ya bandari iliyolipwa na kampuni hizo kwenda Serikalini kupitia TPA, "amesema

Akizungumzia kuhusu utendaji wa kipindi cha Julai-Desemba, 2024
Katika kipindi cha miezi sita ya Mwaka wa Fedha 2024/25 (Julai-Desemba, 2024)amesema jumla ya Shehena iliyohudumiwa na Bandari za TPA ni tani milioni 15.49 ambayo imezidi lengo lililowekwa la kuhudumia tani milioni 14.60 kwa asilimia 6.1, ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 11.1 ikilinganishwa na tani milioni 13.94 iliyohudumiwa kipindi kama hiki mwaka uliopita (Julai-Desemba, 2023).

Amesema jumla ya Shehena ya Makasha iliyohudumiwa na Bandari za TPA ni Makasha TEUS 565,361, ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 4.9 ikilinganishwa na shehena ya Makasha TEUS 539,013 iliyohudumiwa kipindi kama hiki mwaka uliopita (Julai-Desemba, 2023).

Mkurugenzi huyo pia amesema kuwa mamlaka hiyo ikiwa na dhamana ya kutangaza Bandari kimasoko (Promote),
Kusimamia Ulinzi na Usalama wa Bandari (Safety and Security),
Kushirikisha na kusimamia Sekta Binafsi katika uendeshaji wa shughuli za Bandari (Landlord)kwa sasa ina simamia Bandari rasmi 131 zilizoko katika Bahari ya Hindi na Maziwa Makuu.

Akizungumzia hali ya utendaji wa TPA amesema imeboreka ambapo
Jumla ya Shehena iliyohudumiwa
Katika kipindi hiki jumla ya shehena iliyohudumiwa na TPA imekuwa ikiongezeka kwa wastani wa asilimia 15.23 kwa mwaka kutoka tani milioni 20.78 Mwaka wa Fedha 2021/22 hadi tani milioni 27.55 Mwaka wa Fedha 2023/2024.

"Jumla ya shehena iliyohudumiwa katika Bandari ya DSM iliongezeka kwa wastani wa asilimia 13.38 kwa mwaka kutoka tani milioni 18.67 Mwaka wa Fedha 2021/22 hadi tani milioni 23.98 Mwaka wa Fedha 2023/2024,ongezeko la shehena limetokea baada ya Serikali ya Awamu ya Sita kukamilisha miradi mbalimbali ya ujenzi na maboresho ya miundombinu ya Bandari nchini ikiwa ni pamoja na kukamilisha mradi wa maboresho na uendelezaji wa Bandari ya Dar es Salaam ,"amefafanua

Mbossa amesema Shehena ya Makasha Jumla ya shehena ya Makasha (Containers) iliyohudumiwa imeongezeka kwa wastani wa asilimia 12.9 kwa mwaka kutoka makasha (TEUs) 823,404 Mwaka wa Fedha 2021/22 hadi makasha (TEUs) 1,050,486 Mwaka wa Fedha 2023/2024.

Aidha, jumla ya Shehena ya Makasha iliyohudumiwa katika Bandari ya DSM imeongezeka kwa wastani wa asilimia 10.7 kwa mwaka kutoka makasha (TEUs) 816,368 Mwaka wa Fedha 2021/22 hadi makasha (TEUs) 998,872 Mwaka wa Fedha 2023/2024.

Amesema ongezeko la makasha katika Bandari ya Dar es Salaam limetokana na maboresho ya uendeshaji wa vitengo vya makasha vya Bandari ya Dar es Salaam kwa kuviweka chini ya uendeshaji wa Sekta Binafsi wa Kampuni ya DP World Dar es Salaam na Tanzania East Africa Gateway Terminal Limited (TEAGTL) ambazo zimewekeza kwa kufunga mitambo ya kisasa ya kuhudumia shehena pamoja na mifumo ya kisasa ya TEHAMA ya uingizaji na uondoshaji wa makasha bandarini.

Amesema ili kuongeza maboresho zaidi,Serikali kupitia TPA iliingia mikataba ya ushirikishaji na usimamizi wa sekta binafsi kwa ajili ya kuendesha Bandari ya Dar es Salaam ili kuongeza ufanisi katika bandari hiyo.

"Shughuli za uendeshaji wa Kitengo Na. 1 cha Bandari ya Dar es Salaam gati
Shughuli katika kitengo hiki zilianza kukabidhiwa kwa awamu kwa Kampuni ya DP World Dar es Salaam mwezi Aprili 2024,Kampuni ya DP World Dar es Salaam inaendelea na utekelezaji wa Mpango wa Uwekezaji ambao unakusudiwa kugharimu kiasi cha Dola za Marekani (USD) 250 Milioni (sawa na shilingi za Tanzania Bilioni 675) kwa kipindi cha awali cha Mkataba cha Miaka mitano, "amesema

Amesema hadi sasa, Kampuni ya DP World imefanya uwekezaji wa awali katika maeneo mbalimbali ya uendeshaji ili kuboresha na kuongeza ufanisi wa huduma za bandari ambalo ni dhumuni kuu la kuingiwa kwa Mikataba kama ilivyoelezwa hapo awali.

Pia amesema Uwekezaji wa awali uliogharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 214.42 umefanywa katika maeneo mbalimbali ikiwemo ununuzi na usimikaji wa mitambo krini za kisasa za kuhudumiwa shehena ya makasha uliogharimu Shilingi Bilioni 115.80 na Ununuzi na usimikaji wa mitambo nane inayotambulika kama “Rubber Tyred Gantry Crane-RTG” katika Gati Na. 1 la makasha la Bandari ya Dar es Salaam iliogharimu kiasi cha shilingi bilioni 96;

Ununuzi wa ‘terminal tractors’ ishirini (20) ambazo hutumika katika kuhamisha na kusafirisha shehena kutoka eneo moja la bandari kwenda eneo jingine .

Vilevile amesema Serikali ya Awamu ya Sita kupitia TPA inaendelea kutekeleza mapendekezo ya mpango kabambe ya maendeleo ya bandari nchini (2020 – 2045) na programu ya uboreshaji na uendeshaji wa bandari ambao ni mpango wa kitaifa (National Projects Management Information System – NPMIS) ambayo ilisajiliwa Oktoba, 2023 kwa jina la Tanzania Ports Development and Management Programme na kupewa namba ya mradi 4300.

"Katika Programu hiyo Serikali kupitia TPA itaenda kutekeleza miradi 10 ya kimkakati ikiwemo ya kupokelea na kuhifadhia mafuta SRT ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 17 na unagharimu dola za kimarekani million 265,Mradi huu ukikamilika utapunguza siku za kuhudumia meli zenye ujazo wa 150,000 DWT kutoka siku kumi (10) mpaka tatu (3),"amesema.

Ametaja miradi mingine kuwa ni ujenzi wa kituo cha reli na mtandao wake ndani ya bandari ya Dar es Salaam na unagharimu dola za kimarekani million 119.955 na kwamba ukikamilika utapunguza kiwango cha asilimia 98 cha shehena inayotoka bandarini kwa kutumia njia ya barabara na kupelekea kutatua tatizo la msongamano wa malori ndani na nje ya bandari.




Share:

NHC YAAGIZWA KUTOA GAWIO LA BILIONI 10 KWA SERIKALI

 


 ****

Na Mwandishi wetu 

Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amelitaka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kuweka lengo la kutoa gawio serikalini la bilioni 10 kwa mwaka Ujao wa fedha. 

Kauli hiyo ameitoa katika kikao cha baraza la wafanyakazi wa NHC kilichofanyika mkoani Pwani mapema leo.

Akizungumza katika kikao hicho, Mchechu awakumbusha wafanyakazi wa NHC kuwa umoja, upendo, na mshikamano katika utendaji wao wa kazi ni muhimu kwa maendeleo ya taasisi hiyo. 

Amesema kuwa, bila kushirikiana, taasisi hiyo itakuwa ngumu kufikia malengo yake ya kiuchumi.

"Miradi inayotekelezwa na NHC katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Mtwara, Lindi, na Iringa inakaribia kukamilika, na italeta manufaa makubwa kwa taifa. Hivyo, ni muhimu wafanyakazi wa NHC kufanya kazi kwa bidii, kwa uwajibikaji na kwa umoja ili kufanikisha malengo haya," amesema Mchechu.

Mchechu ameongeza kuwa, wafanyakazi wa NHC wanapaswa kutokuwepo na majivuno na kutokuwa na utovu wa nidhamu katika kazi. 

Amesema kuwa maisha ni mafupi, na hivyo ni vyema wafanyakazi wa NHC kupendana na kufanya kazi kwa kujituma ili taasisi iweze kufikia malengo yake.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Ahmad Abdallah, amewakumbusha wafanyakazi kuhusu umuhimu wa kufanya kazi kwa uwadilifu na katika muda uliotakiwa. 

Amesisitiza kuwa, ili taasisi iweze kufikia malengo ya kifedha yaliyowekwa, kila mfanyakazi anapaswa kuchangia kwa kiwango cha juu.

NHC imejipanga kutekeleza miradi mikubwa ya ujenzi wa nyumba na miundombinu katika mikoa mbalimbali, na Mchechu amesema kuwa, kama miradi hii itafanikiwa, itachangia kwa kiasi kikubwa katika maendeleo ya kiuchumi ya taifa.








Share:

Monday, 24 February 2025

Video Mpya : ROGETI Ft. JINASA MADEBE - MJINI

Share:

AFARIKI KWA KUPIGWA NA SHOTI YA UMEME AKIJARIBU KUIBA NYAYA ZA TRANSFOMA SHINYANGA



Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog

Kijana aliyejulikana kwa jina la Daniel Mussa Mageni (27) mkazi wa Kitangili Manispaa ya Shinyanga amefariki dunia kwa kukosa hewa baada ya kupigwa na shoti ya umeme wakati akijaribu kuiba nyaya katika Transfoma iliyopo katika kitongoji cha Isenegeja Kijiji cha Isela kata ya Samuye Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Mashuhuda wanasema kuwa Daniel mkazi wa Kitangili Shinyanga Mjini aliyezaliwa Kilulu wilaya ya Bariadi Mkoa wa Shinyanga amekutwa amefariki katika Transfoma iliyopo jirani na Zahanati ya Isela kata ya Samuye leo asubuhi Februari 24,2025, huku baiskeli aliyotumia kusafiria na vifaa alivyokuwa akivitumia kukata nyaya vikiwa eneo la tukio. 
Sehemu ya waya uliokuwa tayari umekatwa 

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Isegeneja, bi. Amina Hamis Bwire amesema mwanaume huyo amebainika kupoteza maisha dunia majira ya saa mbili asubuhi baada ya kupigwa na shoti ya umeme wakati akijaribu kujuhumu miundombinu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Mhandisi Mwandamizi wa TANESCO Mkoa wa wa Shinyanga, Anthony Tarimo akizungumza kwa niaba ya Meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga amesema kijana huyo amefariki dunia wakati akiingilia njia ya umeme mkubwa katika Transfoma hiyo.

“Kitaalamu ameingilia njia ya umeme mkubwa, ameingilia usalama wa Transfoma akapata ajali hiyo. Alikuwa anajaribu kuiba nyaya za shaba zinazolinda usalama wa Transfoma”,ameeleza Mhandisi Tarimo.
Mhandisi Anthony Tarimo

Mhandisi Tarimo amewataka wananchi kuwa waangalifu na kuacha vitendo vya kuhujumu miundombinu ya umeme, akisisitiza kuwa ulinzi wa miundombinu hiyo ni jukumu la kila mmoja. 

“Ulinzi wa miundombinu ya umeme ni jukumu letu sote, toeni taarifa kuhusu wanaohujumu. Pia wananchi epukeni kusogea kwenye Transfoma na njia za umeme kwani ni hatari. Ukiangalia hata hapa kwenye hii Transfoma kuna onyo kabisa kwamba ni HATARI”,amesema Mhandisi Tarimo.

Amewahimiza wananchi kutoa taarifa pale wanapobaini uhujumu na uharibifu wa miundombinu na kuepuka kukaribia maeneo ya Transfoma, kwani ni hatari kwa maisha.

“Kwa upande wa usalama, miundombinu ya umeme ni hatari na tunapaswa kuepuka kujihusisha nayo kwa namna yoyote ile. Tunaomba wananchi wawasiliane na mamlaka husika pale wanapobaini watu wanaohujumu miundombinu,” ameongeza.

Jeshi la Polisi na Madaktari wamefika kwenye eneo la tukio kwa uchunguzi wa awali na mwili wa marehemu ulichukuliwa na kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti kwa uchunguzi zaidi.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga SACP Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Wakazi wa Isela kata ya Samuye Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga wakiangalia mwili wa Daniel Mussa Mageni (27) aliyefariki dunia baada ya kupigwa na shoti ya umeme alipojaribu kuiba nyaya katika Transfoma.
Wakazi wa Isela kata ya Samuye Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga wakiangalia mwili wa Daniel Mussa Mageni (27) aliyefariki dunia baada ya kupigwa na shoti ya umeme alipojaribu kuiba nyaya katika Transfoma.
Wakazi wa Isela kata ya Samuye Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga wakiangalia mwili wa Daniel Mussa Mageni (27) aliyefariki dunia baada ya kupigwa na shoti ya umeme alipojaribu kuiba nyaya katika Transfoma.
Muonekano wa sehemu ya Transfoma katika kitongoji cha Isenegeja Kijiji cha Isela kata ya Samuye Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
Muonekano wa sehemu ya Transfoma katika kitongoji cha Isenegeja Kijiji cha Isela kata ya Samuye Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga

Muonekano wa sehemu ya Transfoma katika kitongoji cha Isenegeja Kijiji cha Isela kata ya Samuye Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
Muonekano wa sehemu ya Transfoma katika kitongoji cha Isenegeja Kijiji cha Isela kata ya Samuye Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
Muonekano wa sehemu ya Transfoma katika kitongoji cha Isenegeja Kijiji cha Isela kata ya Samuye Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
Share:

MITENDEWAWA YABAHATIKA KUPATA MRADI MKUBWA WA UMEME

Kaimu Afisa Habari wa Huduma kwa Wateja TANESCO Ruvuma Emma Ulendo akizungumza na wananchi wa Mitendewawa
 
Afisa Habari na Uhusiano Tanesco Mkoani Ruvuma Allan Njiro akizungumzia namna ya kulinda miundombinu ya umeme katika kijiji cha Mitendewawa

Wananchi waliojitokeza kupata elimu ya jinsi ya kupata fomu ya maombi ya kupata umeme Mitendewawa



Na Regina Ndumbaro - Ruvuma

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoani Ruvuma limeendelea na ziara yake ya kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kutunza miundombinu ya umeme. 

Ziara hiyo imefanyika katika kijiji cha Mitendewawa, kata ya Mshangano, ambako wananchi walipata fursa ya kufahamu hatua mbalimbali za kuhakikisha wanapata na kutumia umeme kwa usahihi.

Afisa Habari na Uhusiano wa TANESCO mkoani Ruvuma, Allan Njiro, amesema kuwa mradi mkubwa wa umeme umefanikiwa kutekelezwa katika kijiji cha Mitendewawa.

 Hata hivyo, mradi huo ulipitia changamoto mbalimbali, ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa vifaa maalum, hali iliyopelekea ucheleweshaji wa kukamilika kwa wakati uliotarajiwa. 

Pamoja na hayo, amewashukuru wananchi wa Mitendewawa kwa kuwa wavumilivu wakati wa utekelezaji wa mradi huo.

Njiro ameongeza kuwa katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora ya umeme, kijiji cha Mitendewawa kimebahatika kufungiwa transfoma mbili kwa ajili ya matumizi ya wananchi. 

Ameeleza kuwa kwa wale ambao bado hawajapata huduma ya umeme, mpango wa kuendelea na mradi mwingine upo na unatarajiwa kutekelezwa ifikapo mwezi Julai.

Aidha, amewakumbusha wananchi kuwa ni jukumu lao kuhakikisha miundombinu ya umeme inatunzwa vizuri ili kuepusha hasara kubwa inayoweza kutokea. 

Amewataka kuepuka ukataji miti kiholela karibu na nyaya za umeme na kuwa makini na matapeli wanaoweza kuwalaghai katika upatikanaji wa huduma hiyo. 

Pia, ameonya kuwa uharibifu wa miundombinu ya umeme husababisha hasara kubwa kwa serikali na kuwanyima wananchi huduma ya umeme.

Kwa upande wake, Kaimu Afisa Habari wa Huduma kwa Wateja TANESCO Ruvuma, Emma Ulendo, amewashauri wananchi kuhakikisha wanafanya wiring kwa kutumia vifaa bora. 

Ameeleza kuwa maombi ya kuunganishiwa umeme yanaweza kufanywa kupitia ofisi za TANESCO Ruvuma au kwa njia ya mtandao kwa kutumia mfumo wa "NIKONEKTI" unaorahisisha ujazaji wa fomu. Pia, amesisitiza umuhimu wa kulipa ada za umeme kupitia benki au simu ili kuepuka udanganyifu.

Ulendo ameongeza kuwa wale ambao bado hawajafanya wiring wanapaswa kutuma maombi haraka ili waweze kufanikisha upatikanaji wa huduma hiyo. 

Ameeleza kuwa umeme una faida nyingi, ikiwa ni pamoja na kuongeza thamani ya ardhi na kurahisisha shughuli za biashara na maendeleo mengine ya kiuchumi.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Mshangano, Samweli Mbano, ameishukuru TANESCO mkoani Ruvuma kwa jitihada zao za kutoa elimu kwa wananchi juu ya matumizi sahihi ya umeme. 

Ameeleza kuwa elimu hiyo itawasaidia wananchi kuutumia umeme kwa usalama na kuhakikisha miundombinu inatunzwa ipasavyo.

Mbano pia ameishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuhakikisha wananchi wa maeneo ya vijijini wanapata huduma ya umeme. 

Ameeleza kuwa hatua hiyo ni muhimu kwa maendeleo ya wananchi na uchumi wa taifa kwa ujumla.
Share:

KATAMBI AANZA ZIARA YAKE KATA KWA KATA SHINYANGA MJINI…WAJUMBE WA CCM WAKUMBUSHWA KUTETEA CHAMA NA VIONGOZI WAO


Na Mwandishi wetu - Malunde 1 blog

Wajumbe na wanachama wa Chama cha Mapinduzi jimbo la Shinyanga Mjini wametakiwa kutetea na kuyasemea mazuri yanayofanywa na viongozi wa chama chao ili waweze kuendelea kutekeleza ilani ya chama hicho.

Hayo yamebainishwa leo Februari 23, 2025 wakati wa ziara ya kata kwa kata ya Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na watu wenye ulemavu ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi yenye lengo la kukijenga chama na kusikiliza kero za wananchi ndani ya jimbo hilo.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Hamisa Chacha amewahimiza wajumbe hao kuendelea kuhamasisha wananchi kujiunga na Chama Cha Mapinduzi na kuwakumbusha wajibu wao katika kuyasema mazuri yaliyofanywa na viongozi wa chama hicho na kuwatetea kwenye majukwaa dhidi ya watu wanaowakashifu.

"Tuendelee kuwahamasisha wasio wanachama kujiunga na chama chetu ili ifikapo Oktoba tuweze kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uchaguzi wa kuwachagua viongozi wetu, lakini pia twendeni tukayaseme yale waliyofanya viongozi wetu ikiwemo wabunge, madiwani na Rais wetu kupitia majukwaa mbalimbali. Yanayosemwa juu ya viongozi wetu tuwe mstari wa mbele kuwatetea ili kuwapa moyo wa kuendelea kukitumikia", amesema Hamisa Chacha.

Diwani wa kata ya Kizumbi Mhe. Ruben Kitinya ameeleza ukuaji wa kasi wa kata hiyo kwenye sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu, umeme na maji na kumshukuru Mbunge Katambi kwa kuwapigania wananchi na kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kipindi cha miaka minne huku akimuomba Mheshimiwa Mbunge kuwashika mkono katika ukamilishaji wa jengo la zahanati ya Bugayambelele ambalo ujenzi wake umeanzishwa na wananchi.


Akizungumza wakati wa ziara hiyo Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na watu wenye ulemavu ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi amesema kwa sasa Shinyanga imepiga hatua kubwa katika maendeleo sambamba na ukusanyaji wa mapato kupitia vyanzo vyake vya mapato na kufikia bilioni 5 hadi 6 na kuweka wazi miradi iliyotekelezwa kwa kipindi cha miaka 4 ndani ya jimbo la Shinyanga kwenye sekta zote.

"Ahadi nyingi zilizoahidiwa na ilani ya Chama Cha Mapindizi zimeendelea kutekelezwa, tumejenga shule mpya 10 za msingi na sekondari ndani ya miaka 4 lengo ni kutoa elimu ya uhakika, fursa na ajira kwa vijana, lakini pia ujenzi wa vyuo vikuu na vya kati, uhimalishaji wa huduma za afya nao pia umeendelea kuimarishwa",


"Ni lazima tuwe na miundombinu bora ili kufanya manispaa ya Shinyanga kuwa Jiji, tunazidi kuiba serikali kufanya ukarabati wa miundombinu yetu iliyoharibiwa na mvua, dhamira yetu ni kusambaza mtandao wa barabara za lami utakaounganisha kata zetu sambamba na ujenzi wa uwanja wa ndege lengo ni kuongeza mapato na shughuli za uzalishaji ndani ya manispaa ya Shinyanga ili kupiga hatua na kuwa Jiji na haya yote yanafanywa na serikali ya awamu ya sita kupitia Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ", ameongeza Katambi.

Nao baadhi ya wananchi walimpongeza Mbunge Katambi kwa kazi kubwa ambayo ameifanya, huku akimuomba awatatulie changamoto ya ubovu wa miundombinu ya barabara ambayo iliharibiwa na mvua,kufikisha umeme kwenye maeneo ambayo bado, pamoja na umaliziaji wa maboma ya Zahanati yaliyosalia.

Mganga Mkuu wa Manispaa ya Shinyanga Dk. Elisha Robert akijibu swali la ukamilishaji wa Zahanati kwenye Mkutano wa hadhara kata ya Kizumbi amesema kwanza anamshukuru Mheshimiwa Rais Samia pamoja na Mbunge Katambi, kwa kupunguza idadi ya maboma ya vituo na zahanati ambayo yalikuwa bado hayajakamilika kuliwa na Maboma 16,lakini 6 yamekamilishwa na yanatoa huduma, huku Zahanati mbili ya Mwagala na Mwamagunguli zipo hatua za mwisho za ukamilishaji.

Mheshimiwa Mbunge Patrobas Katambi Februari 24,2025 anaendelea na ziara yake Katika Kata ya Mwamalili na Oldshinyanga ambapo leo ameanza ziara hiyo kwenye kata ya Kizumbi na Ibinzamata,

Katibu mwenezi wa CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Said Bwanga akizungumza wakati wa ziara hiyo.Diwani wa kata ya Kizumbi Mhe. Ruben Kitinya akizungumza wakati wa ziara hiyo.
Diwani wa kata ya Ibinzamata Mhe. Ezekiel Sabo akizungumza wakati wa ziara hiyo.
Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Hamisa Chacha akizungumza wakati wa ziara hiyo ya kata kwa kata.



Miongoni mwa wananchi akiwasilisha kero kwenye mkutano wa hadhara kata ya Kizumbi.
Miongoni mwa wananchi akiwasilisha kero kwenye mkutano wa hadhara kata ya Kizumbi.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na watu wenye ulemavu ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi akijibu kero za wananchi kwenye mkutano wa hadhara kata ya Kizumbi.Baadhi ya wajumbe wakiwa kwenye Mkutano kata ya Ibinzamata.
Baadhi ya wajumbe waliohudhuria Mkutano katika kata ya Ibinzamata.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger