Wednesday, 26 February 2025
WAZIRI SIMBACHAWENE ATOA WITO KWA WANANCHI WA CHIPOGOLO KUSHIRIKI MAENDELEO
TUMIENI VYAKULA VYA ASILI ILI KUDHIBITI UDUMAVU
Na mwandishi wetu Muleba
Wadau wa lishe Wilayani Muleba Mkoani Kagera wametakiwa kushirikiana na Serikali kuhamasisha wananchi kula vyakula vya asili ambavyo vipo kwenye maeneo yao ili kuweza kudhibiti udumavu dhidi ya watoto katika Wilaya hiyo.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Bi. Edina Kabyazi ametoa kauli hiyo kwenye kikao cha kamati jumuishi ya lishe ngazi ya Wilaya cha robo ya pili ya Oktoba hadi Desemba mwaka 2024/2025 ambacho kimefanyika Februari 25, 2025 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.
Bi. Edna Kabyazi amesema kuwa jukumu la uhamasishaji wa ulaji wa vyakula vyenye lishe sio la Watalaam wa afya pekee bali ni jukumu la kila mdau wa maendeleo kwani panahitajika nguvu ya ziada na kutokata tamaa lengo likiwa ni kuhakikisha kila kaya inakuwa na lishe bora.
Awali akiwasilisha taarifa ya lishe Afisa lishe Wilaya ya Muleba Dkt. Robson Tigererwa amesema kuwa wameweza kufanya kampeni ya ugawaji wa matone ya vitamin A na dawa za minyoo ambapo walilenga kuwapatia watoto 119,737 na wameweza kuwapatia watoto 119,440 sawa na asilimia 99.
Dkt. Tigererwa amesema kuwa pia pamefanyika upimaji wa hali ya lishe kwa watoto 53,881 wenye umri wa miezi sita hadi 59 ambapo watoto wenye hali nzuri ya lishe ni 50,649 sawa na asilimia 94, wenye hali hafifu ya lishe ni 3,017 sawa na asilimia 5.6 huku watoto wenye hali mbaya ya lishe wakiwa ni 216 sawa na asilimia 0.4.
Aidha amesema kuwa bado kuna changamoto ya baadhi ya wazazi kugoma kuwapeleka watoto kwenye zoezi la chakula dawa pamoja na ushiriki mdogo wa wanaume kwenye masuala ya lishe hasa kwenye mafunzo na mikutano.
Nao baadhi ya washiriki ambao ni Johanes Mtoka na Gaudini Gration wameshauri kuwepo kwa mashamba darasa kwenye shule za msingi na Sekondari ili kuondoa changamto ya wa uhaba wa chakula shuleni ambao umekuwa ukipelekea baadhi ya wanafunzi kuwa na udumavu kutokana na kushinda njaa siku nzima.
Tuesday, 25 February 2025
NGEZE AMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUPAMBANIA AFYA YAKE

TPA YAELEZA MAFANIKIO YAKE KWA KIPINDI CHA MIAKA MINNE
NHC YAAGIZWA KUTOA GAWIO LA BILIONI 10 KWA SERIKALI
Na Mwandishi wetu
Kauli hiyo ameitoa katika kikao cha baraza la wafanyakazi wa NHC kilichofanyika mkoani Pwani mapema leo.
Akizungumza katika kikao hicho, Mchechu awakumbusha wafanyakazi wa NHC kuwa umoja, upendo, na mshikamano katika utendaji wao wa kazi ni muhimu kwa maendeleo ya taasisi hiyo.
Amesema kuwa, bila kushirikiana, taasisi hiyo itakuwa ngumu kufikia malengo yake ya kiuchumi.
"Miradi inayotekelezwa na NHC katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Mtwara, Lindi, na Iringa inakaribia kukamilika, na italeta manufaa makubwa kwa taifa. Hivyo, ni muhimu wafanyakazi wa NHC kufanya kazi kwa bidii, kwa uwajibikaji na kwa umoja ili kufanikisha malengo haya," amesema Mchechu.
Mchechu ameongeza kuwa, wafanyakazi wa NHC wanapaswa kutokuwepo na majivuno na kutokuwa na utovu wa nidhamu katika kazi.
Amesema kuwa maisha ni mafupi, na hivyo ni vyema wafanyakazi wa NHC kupendana na kufanya kazi kwa kujituma ili taasisi iweze kufikia malengo yake.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Ahmad Abdallah, amewakumbusha wafanyakazi kuhusu umuhimu wa kufanya kazi kwa uwadilifu na katika muda uliotakiwa.
Amesisitiza kuwa, ili taasisi iweze kufikia malengo ya kifedha yaliyowekwa, kila mfanyakazi anapaswa kuchangia kwa kiwango cha juu.
NHC imejipanga kutekeleza miradi mikubwa ya ujenzi wa nyumba na miundombinu katika mikoa mbalimbali, na Mchechu amesema kuwa, kama miradi hii itafanikiwa, itachangia kwa kiasi kikubwa katika maendeleo ya kiuchumi ya taifa.
Monday, 24 February 2025
AFARIKI KWA KUPIGWA NA SHOTI YA UMEME AKIJARIBU KUIBA NYAYA ZA TRANSFOMA SHINYANGA



MITENDEWAWA YABAHATIKA KUPATA MRADI MKUBWA WA UMEME

Afisa Habari na Uhusiano Tanesco Mkoani Ruvuma Allan Njiro akizungumzia namna ya kulinda miundombinu ya umeme katika kijiji cha Mitendewawa

Wananchi waliojitokeza kupata elimu ya jinsi ya kupata fomu ya maombi ya kupata umeme Mitendewawa

KATAMBI AANZA ZIARA YAKE KATA KWA KATA SHINYANGA MJINI…WAJUMBE WA CCM WAKUMBUSHWA KUTETEA CHAMA NA VIONGOZI WAO

Katibu mwenezi wa CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Said Bwanga akizungumza wakati wa ziara hiyo.
Diwani wa kata ya Kizumbi Mhe. Ruben Kitinya akizungumza wakati wa ziara hiyo.
Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Hamisa Chacha akizungumza wakati wa ziara hiyo ya kata kwa kata.













































