Sunday, 22 February 2026

Picha : KATAMBI AFANYA MKUTANO MKUBWA KUWASHUKURU WANANCHI SHINYANGA MJINI, ASISITIZA AMANI


Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi, akihutubia wananchi wa Shinyanga katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru kwa imani yao ya kumchagua kuwa Mbunge pamoja na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa CCM. - Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Mabala Mlolwa kwenye mkutano wa hadhara wa kuwashukuru kwa imani yao ya kumchagua kuwa Mbunge pamoja na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa CCM.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi, amefanya mkutano mkubwa wa hadhara kuwashukuru wananchi kwa imani kubwa waliyoionesha katika Uchaguzi Mkuu kwa kumchagua kuwa Mbunge wa Jimbo la Shinyanga, kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na kuwachagua madiwani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mkutano huo wa kihistoria umefanyika leo, Jumapili Februari 22, 2026, katika viwanja vya Zimamoto Mjini Shinyanga, ukihudhuriwa na maelfu ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Shinyanga, jambo lililoakisi mshikamano mkubwa wa wananchi na imani yao kwa uongozi wa CCM.

Akizungumza mbele ya umati huo, Mhe. Katambi ameeleza shukrani zake za dhati kwa wananchi wa Shinyanga kwa kuendelea kuiamini CCM na Serikali yake, akisisitiza kuwa ushindi huo si wa mtu mmoja bali ni ushindi wa wananchi wote wanaotamani maendeleo, ustawi na amani ya taifa.

Aidha, ameahidi kuendelea kutekeleza Ilani ya CCM kwa vitendo kwa kusimamia miradi ya maendeleo katika sekta za miundombinu, maji, afya, elimu na ajira kwa vijana, huku akieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi na kijamii yanayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja.

Katika kusisitiza suala la amani, Mhe. Katambi ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, amewahimiza wananchi kuendelea kulinda na kudumisha amani, umoja na utulivu wa nchi, akieleza kuwa bila amani hakuna maendeleo. 

Amebainisha kuwa Serikali itaendelea kuimarisha usalama wa raia na mali zao ili kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji na ukuaji wa uchumi.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Mabala Mlolwa kwenye mkutano wa hadhara wa kuwashukuru kwa imani yao ya kumchagua kuwa Mbunge pamoja na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa CCM. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog 

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi, akihutubia maelfu ya wananchi katika mkutano mkubwa wa hadhara Mjini Shinyanga, akitoa shukrani kwa imani waliyoionesha katika Uchaguzi Mkuu kwa kumchagua kuwa Mbunge, kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na kuwachagua madiwani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).  
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi, akihutubia wananchi wa Shinyanga katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru kwa imani yao ya kumchagua kuwa Mbunge pamoja na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa CCM.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi, akihutubia wananchi wa Shinyanga katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru kwa imani yao ya kumchagua kuwa Mbunge pamoja na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa CCM.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi, akihutubia wananchi wa Shinyanga katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru kwa imani yao ya kumchagua kuwa Mbunge pamoja na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa CCM.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi, akihutubia wananchi wa Shinyanga katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru kwa imani yao ya kumchagua kuwa Mbunge pamoja na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa CCM.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi, akihutubia wananchi wa Shinyanga katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru kwa imani yao ya kumchagua kuwa Mbunge pamoja na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa CCM.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi, akihutubia wananchi wa Shinyanga katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru kwa imani yao ya kumchagua kuwa Mbunge pamoja na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa CCM.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi, akihutubia wananchi wa Shinyanga katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru kwa imani yao ya kumchagua kuwa Mbunge pamoja na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa CCM.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi, akihutubia wananchi wa Shinyanga katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru kwa imani yao ya kumchagua kuwa Mbunge pamoja na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa CCM.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi, akihutubia wananchi wa Shinyanga katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru kwa imani yao ya kumchagua kuwa Mbunge pamoja na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa CCM.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi, akihutubia wananchi wa Shinyanga katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru kwa imani yao ya kumchagua kuwa Mbunge pamoja na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa CCM.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Patrobas Katambi, akihutubia wananchi wa Shinyanga katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru kwa imani yao ya kumchagua kuwa Mbunge pamoja na kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na madiwani wa CCM.





Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

Redefining mobile gaming with SportPesa Tanzania Casino USSD

 

A revolution is underway in the casino industry in Tanzania, and it is not being fueled by fancy apps or extensive internet usage. It is fueled by a simple dialing code. Players in the country can now access casino games directly without the need for internet data or app downloads. A technology revolutionizing the way millions of people can access mobile gaming.

In a country where internet connectivity is not stable and access to smartphones is not widespread, SportPesa has started Casino USSD access all over again. The emphasis is on functionality. No app, no 4G, no updates. Simply dial *150*87#, spin, and win.

The rise of Casino USSD in Tanzania

The casino gaming industry in SportPesa Tanzania is on the verge of a smarter revolution. Rather than depending solely on internet-based platforms, many gamers are now turning to Casino USSD Tanzania. It integrates well with their normal mobile phone activities.

Gamers only need to dial *150*87# to log in. Deposit money into their wallet using mobile money, view the casino menu, and begin playing in seconds. The service directly addresses gamers looking for a mobile casino that does not require internet access.

Designed for every phone, every region

One of the greatest benefits of the SportPesa Casino is that it is inclusive. Whether one has a smartphone or a simple feature phone, the platform operates in the same manner. It makes players experience the USSD gaming platform in every region.

Why players prefer the USSD experience

For Tanzanians, reliability is more important than looks. USSD does not have loading screens, buffering, or background updates. The menus are quick to load, even when the signal is low.

For players who are interested in accessing Casino using USSD, the process is very simple. They need to dial the code and follow the instructions. Players who are interested in learning more about the service can check the USSD menu or the website.

A smarter future for Casino gaming

The introduction of Casino USSD in Tanzania proves that innovation can be simple and effective. The brand has broken the internet dependency barrier, and the result is an expanded brand with the same level of security and convenience. The future of casino gaming in Tanzania is not about complexity, it is about accessibility, inclusivity, and smarter technology that works for all.

Enhancing responsible mobile gaming

Accessibility is not a substitute for responsible gaming. The platform is further enhancing responsible mobile gaming practices on all its platforms. Players are encouraged to budget, set personal limits, and consider casino gaming purely as entertainment. By striking a balance between excitement and control, the platform remains the most trusted gaming platform in Tanzania.

Conclusion

The Casino USSD service by SportPesa Tanzania is not only an innovation but a game-changer in the mobile gaming industry in Tanzania. The service has made it possible for all players to enjoy casino entertainment without the need for internet or app downloads. It makes the service not only faster but also builds trust and loyalty across the country. For Tanzanians, it provides accessibility, security, and fun for all.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI FEBRUARI 22,2026



 Magazeti



Share:

Saturday, 21 February 2026

WADAAWA WA KIIRAQW WAPATA NAFASI YA KUSIKILIZWA KWA LUGHA YAO, BARAZA LA ARDHI DODOMA LATOA TUMAINI LA HAKI SAWA


Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya, Mkoa wa Dodoma limewasikiliza wananchi wa jamii ya Kiiraqw waliofika katika Baraza hilo kuwasilisha hoja na ushahidi wao katika mgogoro wa ardhi, wakidai kumiliki kihalali shamba lenye ukubwa wa ekari nane lililopo Wilaya ya Chamwino, Mkoa wa Dodoma.

Hatua hiyo imekuja kufuatia maombi ya wadaawa hao ambao ni pande mbili zinazohusika katika shauri hilo, kubainisha kuwa wanakabiliwa na changamoto ya lugha, hali iliyokuwa ikiathiri uwezo wao wa kujitetea na kueleza kwa uwazi hoja zao mbele ya Mwenyekiti wa Baraza hilo, Mhe. Omary Mbega.

Kutokana na hilo, Baraza lilitoa huduma ya ukalimani kupitia mkalimani, Ndg. Simon Tlatlaa Emmay, ambaye alitafsiri maelezo yao na kuwawezesha wadaawa hao kufafanua kwa kina madai yao, kuwasilisha ushahidi pamoja na vielelezo muhimu bila kikwazo cha lugha.

Shauri hilo ni Shauri la Ardhi Na. 92 la mwaka 2025, linalomhusu Ekaristi Ngu’nda kama Mleta Maombi dhidi ya Lolote Nanacha na Martin Lolo Nanacha, ambao ni Wajibu Maombi. Mgogoro huo unahusu umiliki wa shamba lenye ukubwa wa ekari nane lililopo Kitongoji cha Msunjirire, Kijiji cha Zajilwa, Kata ya Zajilwa, Wilaya ya Chamwino, Mkoa wa Dodoma.

Katika madai yake, Mleta Maombi anadai kuwa ndiye mmiliki halali wa eneo hilo la ardhi, akieleza kuwa ekari hizo ziliuzwa na Wajibu Maombi kwa utaratibu unaozua mgogoro wa kisheria.

Akizungumza mara baada ya kusikilizwa kwa shauri hilo, mmoja wa Wajibu Maombi, Ndg. Lolo Nanacha, alisema uwepo wa mkalimani umeimarisha imani yake katika mfumo wa utoaji haki.

“Leo nimejisikia huru kueleza ukweli wangu. Nimeeleweka vizuri, na ninaamini haki itatendeka,” alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza hilo, Mhe. Omary Mbega, alisisitiza kuwa huduma ya ukalimani ni sehemu muhimu ya kuhakikisha kila mwananchi anapata haki sawa bila kujali tofauti ya lugha au asili yake.

Shauri hilo limeahirishwa hadi tarehe 15 Aprili 2026, ambapo mashahidi zaidi watasikilizwa kabla ya kutolewa uamuzi wa mwisho.

Share:

Friday, 20 February 2026

Breaking News : KARDINALI PENGO AFARIKI DUNIA, RAIS SAMIA ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI

 

Askofu Mkuu wa Dar-es-Salaam Thaddeus Ruwa’ichi kwa masikitiko makubwa ametangaza kifo cha Mwadhama Polycarp Cardinal Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo kuu la Dar-es-Salaam.

Kifo cha Cardinal Pengo kimetokea akiwa katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Dar-es-Salaam.



Share:

BAADA YA MIAKA YA KUJARIBU BILA MATOKEO, HATIMAYE NILIPATA KAZI YA NDOTO SERIKALINI



Miaka mingi ya kuomba, kushindana na wagombea wengine, na kukabili masharti magumu ya kazi serikalini yalinifanya nihisi kuchoka na kukata tamaa.

Kila mwaka nilijaribu tena, lakini kila barua yangu ya maombi ilirudi ikiwa na jibu hasi au bila jibu kabisa. Nilijikuta nikikosa matumaini, nikihisi kama ndoto yangu ya kuwa na kazi ya heshima na yenye uthibitisho ingekufa.

Familia na marafiki walinijulisha kuwa ni lazima nisubiri nafasi nyingine au nitafute kazi nyingine. Lakini kwa moyo wangu, nilijua hilo si mwisho wangu.

Share:

PROGRAM JUMUISHI YA MALEZI,MAKUZI NA MAENDELEO YA AWALI YA MTOTO YAENDELEA KUIMARIKA KISHAPU

Na Sumai Salum- Kishapu
Afisa Ustawi wa Jamii wilayani Kishapu mkoani Shinyanga  Mwajuma Abeid akizungumza wakati akifungua kikao cha utekelezaji wa PJT-MMMAM mwezi Oktoba-Disemba 2025, kwa niaba ya Mganga Mkuu wilayani humo chenye lengo la kupata uelewa wa kadi alama ya tathmini ya maendeleo ya awali ya Mtoto (ECD), Changamoto zilizotambuliwa na njia za kutatua changamoto hizo zinazoikabili programu hiyo Februari 19,2026

Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga imeendelea kutekeleza Programu Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT–MMMAM) kwa lengo la kuhakikisha watoto wanapata malezi bora tangu wakiwa katika hatua za awali za maisha. 


Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa programu hiyo kwa kipindi cha Oktoba hadi Desemba 2025 Mratibu wa PJT–MMMAM wilayani humo,Paul Lupolaso, kwenye kikoa chenye lengo la kupata uelewa wa kadi alama ya tathmini ya maendeleo ya awali ya Mtoto (ECD), Changamoto zilizotambuliwa na njia za kutatua changamoto hizo Februari 19,2026.


Katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2025/2026, Halmashauri imeendelea kutekeleza shughuli mbalimbali zikiwemo utoaji wa elimu ya afya na lishe kwa jamii, kampeni za kupunguza vifo vya wajawazito na watoto wachanga, jitihada za kukabiliana na udumavu, pamoja na utoaji wa elimu ya kuzuia ukatili dhidi ya watoto. 

"Katika kipindi hiki tumeweza kutoa vidonge vya madini chuma kwa wanawake wajawzito na kufikia 91%, elimu ya kinamama kujifungulia vituo vya afya 90%, Watoto kunyonya maziwa ya mama pekee wenye umri wa miezi 0 mpaka miezi 6 kwa 98%" ameongeza Lupolaso

Aidha,  ameongeza kuwa elimu ya usalama wa mtoto imeendelea kutolewa katika shule za msingi 128 zilizopo ndani ya Wilaya ya Kishapu. Hata hivyo, amebainisha kuwa utekelezaji wa programu hiyo umekumbana na changamoto kadhaa ikiwemo upungufu wa watumishi katika kitengo cha lishe, ushiriki mdogo wa wanaume katika masuala ya afya na lishe ya familia, pamoja na uhitaji wa kuimarisha usimamizi elekezi katika vituo vya kutolea huduma za afya. 

Kutokana na changamoto hizo, Halmashauri imeweka mikakati ya kuimarisha utekelezaji wake kwa kufanya kikao cha Kamati ya Lishe kwa kushirikiana na Watendaji wa Kata, kuhimiza maadhimisho ya Siku ya Afya na Lishe (SaLiki), kufanya usimamizi elekezi katika vituo vya afya na zahanati, kuongeza uhamasishaji wa jamii kuhusu usafi wa mazingira na umuhimu wa kinamama kujifungulia katika vituo vya afya, pamoja na kutoa mafunzo kazini kwa watoa huduma kuhusu huduma za dharura kwa mama na mtoto. 

Baada ya uwasilishaji wa taarifa hiyo, wajumbe walitoa maoni mbalimbali ya kuboresha programu hiyo, wakisisitiza umuhimu wa kuongeza mikakati ya kuwahusisha wanaume katika kliniki za wajawazito na masuala ya lishe ili kuimarisha uwajibikaji wa familia, kuanzisha vikundi vya wazazi katika ngazi ya jamii vitakavyosaidia kutoa elimu ya malezi chanya, pamoja na kuimarisha ukusanyaji wa takwimu sahihi zitakazosaidia katika upangaji na utekelezaji wa shughuli za maendeleo ya mtoto. 

Sambamba na hayo, Halmashauri pia imeendelea kutoa shukrani kwa wadau wanaoiunga mkono katika utekelezaji wa programu hiyo wakiwemo World Vision, THPS, Marie Stopes, AMREF, Kivulini na REDESO kwa mchango wao katika kuboresha ustawi wa watoto na jamii kwa ujumla.

Ikumbukwe kuwa Serikali ilizindua rasmi programu hiyo mwezi Desemba 2021 ikiwa na dhamira ya kuimarisha mfumo jumuishi wa malezi ya mtoto unaojikita katika maeneo ya afya bora, lishe, malezi yenye mwitikio, fursa za ujifunzaji wa awali pamoja na ulinzi na usalama wa mtoto.
Mratibu wa PJT–MMMAM wilayani humo,Paul Lupolaso akizungumza kwenye kikao cha utekelezaji wa PJT-MMMAM mwezi Oktoba-Disemba 2025, chenye lengo la kupata uelewa wa kadi alama ya tathmini ya maendeleo ya awali ya Mtoto (ECD), mafanikio yaliyopatikana pamoja na changamoto zinazoikabili programu hiyo na ku Februari 19,2026
















 
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger